Simulizi: Makaburi ya wasio na hatia

Hili jama senge kweli, sasa kwanini umeleta hadithi yako wakati huna vocha..
 
Hii hadithi mwisho.si Kwa mauza uza hayo.ila nzuri mpaka inakufanya hata ukiumwa na kichwa utaona umechezewa
 
Hii hadithi mwisho.si Kwa mauza uza hayo.ila nzuri mpaka inakufanya hata ukiumwa na kichwa utaona umechezewa
kwakweli waeza jikuta ,huishi kwa amani...
Ndio maana Mungu hakutupa uwezo huo wa kuona haya mambo maana waeza Changanyikiwa.
 
Hadidhi za humu tatizo lake ni hili. Zinaanza vizuri halafu hazimalizwi.ni chache huwa zinafikia mwisho.sasa huwa mnatudodisha? Tatizo ni nini? Bora mseme kuanzia mwanzo. Kuliko kutufanyia hivi
 
SEHEMU YA 46:

ILIPOISHIA:
Tangu nizaliwe, sikuwahi kuchinja hata kuku tu, achilia mbali ndege tuliokuwa tukiwawinda kule kijijini kwetu lakini sasa eti nilikuwa natakiwa nimchinje binadamu, mtoto asiye na hatia yoyote ili nifaulu mtihani na kuwa mwanachama kamili, nilijikuta nikitetemeka kuliko kawaida.
Nilikichomoa kisu pale kiunoni nilipokiweka, mikono ikawa inatetemeka kuliko kawaida, nikawa namtazama mtoto yule usoni, nilijikuta nikiingiwa na huruma isiyo ya kawaida.
SASA ENDELEA…
Kisu kikadondoka na kwenda kujikita kwenye udongo. Nikamuona Mkuu akinikata jicho la ukali, akatembea kwa hatua zenye vishindo vizito mpaka pale nilipokuwa nimesimama, akainama kwa tabu na kukichomoa kile kisu, akanishikisha mkononi.
Baada ya hapo aliingiza mkono kwenye kimkoba chake kidogo cha ngozi, akatoa kichupa kilichokuwa na ungaunga mweusi, akamimina kwenye viganja vya mikono yake kisha akanipulizia usoni bila kusema chochote, nikapiga chafya mbili mfululizo kisha nikaanza kuona kama akili zangu zinabadilika jinsi ya ufanyaji kazi wake.
Hata sijui nini kiliendelea lakini baadaye akili zangu zilipokuja kukaa sawa, nilikuwa nimeshika kisu kwa nguvu huku mwili wangu ukiwa umetapakaa damu, watu wote wakawa wanashangilia kwa nguvu.
Yule mtoto hakuwepo tena pale kwenye kile kitanda cha miti, nadhani alishaondolewa maana niliwaona watu wengine kadhaa wakiwa wamezunguka pale ambapo jana yake palikuwa na furushi la nyama, wakawa ni kama kuna kazi wanaifanya, hakuna hata aliyegeuka nyuma.
>>>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Mkuu alinisogelea huku uso wake ukiwa na tabasamu pana, sikuwahi kumuona akiwa na furaha kama aliyokuwa nayo, akaja na kunishika kichwani kama mtoto anavyomsalimia mkubwa wake, akanishika pia kifuani kisha akainama na kunishika vidole gumba vya miguu.
Alipoinuka, alifungua kimkoba chake, akatoa hirizi nyeusi na kunifunga kwenye mkono wa kushoto, akaniambia kwamba hicho ndiyo kitambulisho na silaha yangu na kwamba maelekezo mengine nitapewa na watu walionizidi, watu wote wakapiga makofi kwa nguvu na kuanza kuimba nyimbo za ajabuajabu huku wakicheza kwa mtindo ambao hata sikuuelewa.
Nilimuona baba akija mpaka pale katikati, akatoa salamu kwa Mkuu kisha akanikumbatia kwa nguvu. Hakujali zile damu nilizokuwa nazo, akakichukua kile kisu na kukifuta damu kisha akakichomesha kwenye mshipi wake kiunoni, akanishika mkono huku akiendelea kucheza sawa na wale watu wengine, akanipeleka mpaka sehemu aliyokuwa amekaa yeye na baba yake Rahma.
Sauti ya pembe la ng’ombe ilisikika kisha watu mbalimbali wakaanza kuja pale nilipokuwa pamoja na baba na baba yake Rahma, wakawa wananisogelea kisha wanainamisha vichwa vyao kama ishara ya heshima.
Baba aliniambia kwamba hiyo ni ishara ya kukaribishwa kwenye ulimwengu wao na kila mwanachama mpya anayetimiza masharti, huwa anafanyiwa hivyo. Waliendelea kuja kwa wingi lakini wengi sura zao zilikuwa ngeni kabisa kwangu.
Kulikuwa na wazee, watu wa makamo, vijana kama mimi na watoto wadogo, wanaume kwa wanawake. Wengine walikuwa ni wasichana wazuri tu ambao wala usingeweza kudhania kwamba nao wanahusika na yale mambo. Wengine walikuwa ni watu wazima wenye heshima zao.
Unajua watu wengi huwa wakisikia neno ‘mchawi’, tafsiri ambayo wanaijenga vichwani mwao, ni mtu fulani wa ajabuajabu, anayetisha, aliyezeeka au aliyedhoofika mwili. Ukweli ni kwamba mchawi hana alama, mwingine unaweza kuwa unamuona kama bosi fulani, au mwingine unamuona kama msichana mrembo, mzee wa heshima au mtoto mdogo lakini kumbe akawa anahusika na mambo hayo.
>>>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Wakati wakiendelea kuja, mara nilimuona Isri akitokezea, akanitazama na mimi nikamtazama, tukatazamana kwa sekunde kadhaa, tukio ambalo baba aliliona ‘mubashara’, akanigeukia na kunitazama usoni, nikaacha kumtazama Isri na kumtazama baba kisha harakaharaka nikakwepesha macho yangu.
Isri alisogea mbele kisha akainamisha kichwa kama wale wengine wote kisha tararibu akaondoka na kutoa nafasi kwa watu wengine kuendelea na zoezi hilo. Zoezi likaendelea na baadaye, nilishtuka kuziona sura za watu ambao niliwakumbuka vizuri.
Wa kwanza alikuwa ni yule bibi kizee aliyenizabua kibao siku nilipokuwa mahabusu, usiku walioingia na kuanza kuwanga ndani ya chumba cha mahabusu. Nakumbuka siku aliponipiga na kunisababisha maumivu makali, nilijiapiza kwamba siku nitakayokutana naye lazima nilipize kisasi.
Wakati akinisogelea, nilitazama kushoto na kulia, baba akawa ameshajua ninachotaka kukifanya, akanionesha ishara kwamba sitakiwi kufanya chochote. Yule bibi naye ni kama alinikumbuka, aliponitazama vizuri usoni akawa ni kama ameshtuka, akasogea kwa kujihami na kutoa ishara kwangu huku akinitazama kwa macho ya kuibia, moyoni nikajiapiza kwamba ipo siku yake lazima nilipe kisasi.
Nyuma yake alikuwa ameongozana na wale watu wote alioingia nao siku ile mahabusu, wote wakawa wananitazama kwa macho yenye ujumbe fulani, mwisho akatokeza yule ambaye nilisababisha akanasa ndani ya mahabusu kisha mimi nikatoka kimiujiza.
Tofauti na wenzake wote, huyu alionesha kuwa na hasira na mimi maana jicho alilonikata, mpaka nilijishtukia, baba na baba yake Rahma wakawa wanacheka. Ni kama walikuwa wanajua kila kitu kinachoendelea. Basi pilikapilika ziliendelea kama kawaida, ukafika muda wa chakula ambapo sikuogopa sana kama siku ya kwanza.
Baada ya hapo, ulifika muda wa kucheza ngoma za kienyeji na baadaye tulitawanyika, sikujua nimefikaje nyumbani lakini nilichokuwa nakikumbuka ni kwamba baba na baba yake rahma walinishika mikono, wakawa wanaagana na wenzao na muda mfupi baadaye, nilijikuta nikiwa kwenye kona ya chumba nilichokuwa nalala.
Ni hapo ndipo nilipopata muda wa kutosha kuanza kutafakari kilichotokea, nilijihisi kuwa na hatia kubwa ndani ya moyo wangu na nikajiapiza kwamba lazima asubuhi niende Kibaha kufuatilia taarifa za ile ajali na kuona nini hasa ambacho watu wengine watakiona.
Sikupata hata lepe la usingizi, nikawa najiuliza maswali mengi yasiyo na majibu, mara kwa mara nikawa naitazama ile hirizi niliyopewa na Mkuu na kuvalishwa kwenye mkono wangu. Ilikuwa nyeusi tii, ikiwa imefungwa kwa kamba nyekundu.
Kwa kuwa muda ulikuwa umeenda sana, muda mfupi baadaye kulianza kupambazuka, kwa kuwa sikuwa nimelala kabisa, nilienda bafuni kutaka kujimwagia maji kupunguza uchovu lakini ghafla nilikumbuka kwamba baba aliniambia sitakiwi kugusa maji kwa muda wa siku saba.
Ikabidi nijifutefute tu usoni na miguuni na kwenye yale madoa ya damu kisha nikarudi chumbani kwangu, nikaanza kujiandaa kuelekea Kibaha. Sikuwa na nauli na sikutaka kumuaga mtu yeyote, nilitaka kwenda kujionea nini hasa kilichotokea.
Wakati natoka kwa kunyata, nilipitia sebuleni, nikafungua droo ambayo wenyeji wetu huwa wanaweza chenji zinazobaki kwenye manunuzi yao, niliijua kwa sababu mara kadhaa nilimuona Rahma akichukua fedha, nikachukua noti mbili za shilingi elfu mojamoja, nikanyata na kutoka mpaka nje.
Tofauti ambayo niliiona dhahiri, safari hii nilikuwa najiamini sana, sikuwa Togo yule wa saa chache zilizopita, mara kwa mara nikawa najishika pale mkononi kuhakikisha kinga yangu ipo sehemu yake.
Nilipofika mita kadhaa kutoka kwenye geti kubwa, nilimuona yule kijana aliyekuwa akinicheka mara kwa mara kwamba eti mimi ni muuaji. Nilikumbuka maneno aliyoyatoa jioni iliyopita wakati nikiwa na baba na baba Rahma tukielekea kule eneo la tukio, nikaona huo ndiyo muda muafaka wa kumaliza hasira zangu.
“Broo vipi unaenda?” alisema huku akisimamisha Bajaj yake jirani kabisa na pale nilipokuwa nimesimama, nadhani kwa sababu ya kigiza kile cha alfajiri hakuwa ameniona vizuri, aliniponisemesha na mimi kumtazama usoni, niliona jinsi alivyoshtuka, akataka kuondoa Bajaj yake haraka lakini alishachelewa.
Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 47:

ILIPOISHIA:
“Broo vipi unaenda?” alisema huku akisimamisha Bajaj yake jirani kabisa na pale nilipokuwa nimesimama, nadhani kwa sababu ya kigiza kile cha alfajiri hakuwa ameniona vizuri, aliniponisemesha na mimi kumtazama usoni, niliona jinsi alivyoshtuka, akataka kuondoa Bajaj yake haraka lakini alishachelewa.
SASA ENDELEA…
Nilishika bomba la Bajaj yake na kuingia, nikakaa siti ya nyuma, akawa ni kama amepagawa maana hakujua kama akimbie na Bajaj au aiache akimbie kwa miguu.
“Simama kwa usalama wako,” niliongea kwa sauti ya mamlaka, nikamuona jinsi alivyokuwa akihangaika, kijasho chembamba. Hakuwa tayari kusimama, inaonesha alikuwa akiniogopa sana, nilichoamua kukifanya ilikuwa ni kumtumia kutimiza mahitaji yangu.
Nilivuta pumzi ndefu na kuzibana kama baba alivyonielekeza, nikaweka utulivu kidogo kisha nikamuamrisha kunipeleka Ubungo. Nilifanya hivyo kwa kuzungumza moyoni maana ndivyo nilivyoelekezwa, nikamuona akizidi kuichochea Bajaj yake.
Hata hivyo, njia aliyokuwa anapita, ilikuwa ni ileile tuliyoipita jana wake wakati tukielekea Ubungo kupanda magari ya kwenda Kibaha. Alizidi kuongeza kasi, akawa anakimbia kama mshale, mwenyewe alidhani ananikimbia lakini kumbe tayari nilishaingia ndani ya akili yake.
Huwa si kawaida ya Bajaj kukimbia spidi kubwa na kuyapita magari lakini siku hiyo iliwezekana. Baada ya dakika kadhaa za kukimbia kwa kasi kubwa kwenye lami, hatimaye tuliwasili Ubungo, nikavuta tena pumzi na kumpa amri ya kusimama kwenye kituo cha mafuta.
Kilichonishangaza hata mimi, kweli alipunguza mwendo bila mimi kusema kitu chochote, akaiacha barabara kubwa ya lami na kuingia kwenye kituo cha mafuta, nikapeleka mkono wangu kwenye ile hirizi niliyokuwa nimevaa mkononi, nikanuiza maneno kwamba sitaki kuonekana.
“Jamani msaada! Nisaidieni washkajiii,” nilishangaa yule dereva Bajaj akipaza sauti, akazima Bajaj na kushuka huku akikimbia, akaenda kujichanganya na madereva Bajaj wenzake wanaopaki Ubungo, akawa ni kama anawaelekeza kitu fulani huku akihema kwa nguvu.
>>>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Sikutaka kupoteza muda, kwa sababu nilishakuwa na uhakika kwamba hakuna mtu anayeniona baada ya kufuata maelezo yale niliyofundishwa, niliteremka kwenye Bajaj na kusimama pembeni nikitaka kuona nini kitatokea.
Vijana kama kumi hivi waliongozana naye mpaka pale kweye Bajaj kuja kujionea kuna nini kimetokea.
“Yuko wapi?”
“Alikuwa amekaa siti ya nyuma.”
“Siti gani ya nyuma?”
“Hee! Au ameshuka nini?”
“Nani ameshuka? Mbona sisi muda wote tunakuangalia tangu umefika na kuanza kupiga kelele za kuomba msaada hatujaona mtu yeyot akiteremka kwenye Bajaj?” alisema kijana mwingine ambaye alikuwa amesimama jirani kabisa na pale mimi nilipokuwa nimesimama.
Mjadala mkali ukazuka, yule dereva Bajaj akikazania kwamba ni kweli kuna mtu alikuwa amembeba kwenye Bajaj yake na alikuwa akitaka kumuua, wenzake wakawa wanamshikia bango amuoneshe huyo mtu.
“Hizo bangi mnazovuta bila kula ndiyo matatizo yake haya!” alisema dereva mwingine na kusababisha wenzake wacheke, wakaanza kutawanyika huku kila mmoja akionesha kumpuuzia. Nilikuwa na uhakika kwamba hakuna mtu yeyote aliyeniona na ndiyo maana hata pale nilipokuwa nimesimama, watu walikuwa wakinipita tu bila kuonesha dalili yoyote kwamba wameniona.
Nilishangazwa sana na kilalichokifanya yule dereva Bajaj, kwa tafsiri nyepesi, kama kweli wale watu wangenikuta kwenye Bajaj ile, nini kingetokea? Bila shaka wangenidhuru wakiamini mimi ni mhalifu, nikaamua kumkomesha zaidi.
Nilisubiri aingie kwenye Bajaj yake, akaiwasha huku mara kwa mara akigeuka nyuma, na mimi nikaingia lakini nikiwa bado nimeishika ile hirizi ya mkononi, kwa hiyo nikawa sionekani. Alipotoka na kuingia barabarani tu, niliachia ile hirizi, akageuka na kushtuka kuona nimekaa palepale kwenye siti ya nyuma, akaanza kuchachawa.
Nilivuta pumzi ndefu na kuzishikilia kisha nikamuamuru kunipeleka Kibaha, nikashangaa akikata kona kali katikati ya barabara, magari mengine yakawa yanapiga honi kwa nguvu an kufunga breki, akavuka kwenye taa za kuongozea magari kwa kasi kubwa, almanusura tugongwe na magari yaliyokuwa yameruhusiwa na taa. Kila mtu alibaki amepigwa na butwaa kwa jinsi Bajaj ilivyovuka kwenye taa zile, akawa anakimbia kwa kasi kubwa kuliko kawaida. Kila alipokuwa akigeuka na kuniona nimetulia kwenye ile siti, ndivyo alivyokuwa akizidi kuongeza kasi.
>>>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Ikafika mahali Bajaj ikaisha mafuta, nilichoamua ilikuwa ni kumtesa tu, akapaki Bajaj yake pembeni ya barabara, mimi nikashika ile hirizi yangu, nikawa sionekani tena, akashuka na kwenda kusimama mbali kabisa, akionesha dhahiri kuwa na hofu kubwa ndani ya moyo wake.
Niliamua kushuka kwenye Bajaj yake lakini nikajiapiza kwamba bado hatujamalizana, nilitembea kwenda mbele kidogo kwenye kituo cha daladala, tayari kulishaanza kupambazuka. Nikaiachia ile hirizi yangu, nikajichanganya na abiria wengine. Muda mfupi baadaye, gari lilikuja, nikawa wa kwanza kupanda, abiria wengine nao wakapanda.
Tukiwa ndani ya gari safari ikiendelea, mjadala kuhusu ajali iliyotokea usiku, ambayo ndiyo hasa iliyonifanya nifunge safari ile bila kumwambia mtu yeyote ilianza. Abiria mmoja aliamnza kusimua kwamba usiku yeye alikuwa akisafiri kutoka Mlandizi kuelekea jijini Dar es Salaam alipokuta ajali hiyo mbaya na ya kutisha, akaendelea kueleza kwamba aliyepata ajali alikuwa jirani yake, Mlandizi.
Mpaka hapo nilishapata sehemu ya kuanzia kwa sababu nilitaka nifike eneo la ajali lakini pia niende mpaka msibani nikajionee hali halisi. Alieleza jinsi ajali yemnyewe ilivyokuwa ya kutatanisha hukuakieleza kwamba mtoto alikufa palepale huku maiti yake ikiharibika vibaya kiasi cha kutotambulika na mama yake alikuwa amelazwa kwenye Hospitali ya Tumbi, hali yake ikiwa mbaya.
Nilizidi kupata taarifa nyingi zaidi, lakini moyoni nikawa najiuliza hiyomaiti wanayosemaimeharibika vibaya ni ipi wakati nakumbuka mimi ndiye niliyeenda kuweka mgomba pale kwenye siti aliyokuwa amekaa yulemtoto na kuweka kipande cha mgomba?
Mjadala uliendelea, kila mtu akawa anasema lake lakini kikubwa walichokuwa wakikizungumza wengi, ni kwamba eneo ilipotokea ajali hiyo limekuwa na mauzauza mengi katika siku za karibuni, kwani hakuna mlima, mteremko wala korongo lakini magari yanap[ata ajali za kustaajabisha.
“Naskia kuna mtumishi wa Mungu kutoka Nigeria anakuja wiki ijayo na atafika pale kufanya maombi,” alisema dereva, abiria wote wakawa wanaunga mkono hoja hiyo. Nilichopanga kichwani, ni kuchukua maelekezo vizuri kwa yule mtu aliyesema marehemu ni jirani yake kisha kwenda kwanza mpaka eneo la ajali na baada ya hapo, nitakwenda Tumbi kujionea hali ya mgonjwa na hiyo maiti kama nitapata nafasi. Nilikuwa na shauku kubwa ya kujua kila kitu maana moyo wangu ulikuwa na hatia kugbwa, hasa kutokana na jinsi taarifa za ajali ile zilivyowaumiza mioyo abiria wengi.
Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 48:


ILIPOISHIA:
Nilichopanga kichwani, ni kuchukua maelekezo vizuri kwa yule mtu aliyesema marehemu ni jirani yake kisha kwenda kwanza mpaka eneo la ajali na baada ya hapo, nitakwenda Tumbi kujionea hali ya mgonjwa na hiyo maiti kama nitapata nafasi. Nilikuwa na shauku kubwa ya kujua kila kitu maana moyo wangu ulikuwa na hatia kubwa, hasa kutokana na jinsi taarifa za ajali ile zilivyowaumiza mioyo abiria wengi.
SASA ENDELEA…
Safari iliendelea na hatimaye tukawasili Kibaha, gari liliposimama tu, nilimuwahi yule abiria aliyekuwa akisimulia kuhusu ile ajali, nikamsalimu na kumuomba anielekeze ulipo msiba kwa sababu aliyefariki ni ndugu yangu.
“Ni Mlandizi, ukishuka tu pale kituoni, uliza mtu yeyote eti kwenye msiba wa mtoto aliyekufa kwenye ajali ni wapi? Huwezi kupoteza, mtoto alikuwa anafahamika sana yule kutokana na jinsi alivyokuwa na heshima,” alisema yule abiria, nikamshukuru.
Nilipoachana naye, nilimfuata dereva ili anielekeze sehemu gari lilipopata ajali kwani kuna muda nilimsikia akisema kwamba eneo hilo ni baya sana, ajali huwa zinatokea mara kwa mara. Eneo lenyewe nilikuwa nalifahamu lakini sikujua naweza kufikaje.
“Siyo mbali sana kutoka hapa, hata kwa miguu unaweza kufika, panaitwa machinjioni,” alisema yule dereva, nikamshukuru na kuanza kutembea kuelekea eneo la tukio. Tayari kulishaanza kupambazuka na lile giza la afajiri lilianza kupungua na kumezwa na nuru ya alfajiri.
Kila nilipokuwa napita, wafanyabiashara na wasafiri walikuwa wakizungumzia ajali iliyotokea usiku wa siku hiyo. Kila mtu alikuwa akizungumza lake lakini kama baba alivyoniambia usiku, eneo hilo huwa linatumiwa sana na wachawi, hasa waliopo mafunzoni kama mimi kusababisha ajali.
>>>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Kila mtu alikuwa anashauri eneo hilo watafutwe waganga waliobobea au wachungaji wakaliombee kwani kulikuwa na nguvu za giza au ‘nyoka chunusi’ anayesababisha ajali. Njiani sikuwa peke yangu, baadhi ya watu nao waliposikia kuhusu ajali hiyo, walitaka kwenda kujionea wenyewe.
Niliongozana na vijana kadhaa, tukawa tunatembea pembeni ya barabara na dakika kadhaa baadaye, tulifika eneo ajali hiyo ilipotokea. Nilipofika eneo hilo, nilishangaa nywele zikianza kusisimka kuliko kawaida huku harufu ya damu ikitawala kwenye pua zangu. Gari lililopata ajali bado lilikuwa eneo la tukio, pembeni ya barabara, yaani kwa jinsi lilivyokuwa limeharibika, kila mmoja alibaki kushika kichwa.
Mjadala uliotawala kwa wote waliokuwa wamefika kushuhudia ajali hiyo, ulikuwa ni nini kilichosababisha ajali hiyo. Kwa sababu kulishapambazuka, niliweza kuliona vizuri eneo hilo, lilikuwa ni tambarare kabisa, hakukuwa na kona wala mteremko, achilia mbali mlima wa kuweza kusababisha ajali mbaya kiasi kile.
Nilitazama kule tulikokuwa tumekaa na baba na baba yake Rahma, ambako baada ya kuuchukua ule mwili wa yule mtoto niliupeleka, nikashangaa kuona kwamba eneo lote lilikuwa jeupe kabisa kiasi kwamba ungeweza kuona umbali wa karibu mita mia tano.
Hakukuwa na miti wala vichaka, eneo lote lilikuwa jeupe kabisa. Nikawa najiuliza pale kwenye migomba tulipokuwa tumekaa ni wapi? Ule mgomba uliokatwa kisha nikapewa ulitoka wapi? Nikahisi labda nimechanganya upande, nikageukia upande wa pili wa barabara, nako kulikuwa kweupe kabisa, nikawa ni kama nimechanganyikiwa.
“Vipi kijana, mbona unaonesha kutotulia? Unatafuta nini?” niligeuka baada ya kusikia sauti hiyo, nikamtazama aliyekuwa akinisemesha. Alikuwa ni mzee mmoja mwenye ndevu nyingi zilizofunika mdomo wote. Mkononi alikuwa na mkongojo na kwa jinsi alivyokuwa amevaa, ilionesha haishi mbali na eneo hilo.
“Aah! Hamna kitu, nashangaa tu jinsi hii ajali ilivyotokea.”
“Mh! Hebu nitazame usoni,” alisema, nikamtazama na yeye akanitazama. Kitendo cha kutazama naye tu, nilihisi ile hirizi niliyoivaa mkononi ikinibana. Maelezo aliyonipa baba, ni kwamba nikiona inanibana ghafla, lazima kutakuwa na mtu eneo hilohilo mwenye nguvu za giza anajaribu kunipima.
Akaniambia nikishaona hali hiyo, haraka sana nizibe kucha ya mkono wa kushoto kwa kutumia kidole gumba cha mkono huohuo, jambo ambalo nililifanya bila yule mzee kunishtukia. Nikashangaa ameanza kupiga chafya mfululizo, tena kwa nguvu. Alipiga chafya kama kumi hivi, kamasi na machozi vikawa vinamtoka kwa wingi, mpaka watu wengine waliokuwa eneo hili wakawa wanamshangaa.
>>>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
“Mtoto mbaya sana wewe, mtazame bichwa lake,” alisema mzee huyo kwa hasira, akawa anaondoka huku akiendelea kunitukana na kupiga chafya.
“Hivi vizee ndiyo vichawi vyenyewe, unakiona kile kibabu kilivyokuwa kinapiga chafya, inaonesha kimenogewa na harufu ya damu,” alisema mmoja kati ya watu waliokuwa eneo lile, wengine wakacheka huku wengine wakiendelea kusikitika.
“Mbona yule mzee anakutukana, kwani umemfanya nini?”
“Mzee gani?”
“Yule aliyekuwa anapiga chafya?” mwanamke mmoja wa makamo aliniuliza, kumbe alikuwa ameshuhudia kila kitu, nikaamua kuvunga maana kuendelea kuzungumza kungefanya watu waanze kunitazama kwa makini, jambo ambalo sikuwa tayari kuona likitokea.
“Mh! Labda umeangalia vibaya, mbona mimi simfahamu na wala sijaongea naye chochote?” nilijibu huku nikigeuka na kumpa mgongo yule mwanamke, nikaona bado ananifuata kwa manenomaneno.
“Itakuwa kuna jambo baya umemfanyia, haiwezekani mzee kama yule aanze tu kukutukana, nataka uniambie, unajua yule ni nani kwangu,” alisema mwanamke huyo huku akizidi kunisogelea mwilini. Kitendo cha kunisogelea tu, nilishtukia ile hirizi ikianza tena kunibana, safari hii kwa nguvu kuliko mwanzo.
Ikabidi nikae chonjo kwa sababu ubanaji wake ulikuwa wa nguvu na baba alishaniambia kwamba ukiona inabana kwa nguvu, ujue upo jirani na mtu mwenye nguvu kubwa ambaye usipokuwa makini anaweza kukudhalilisha mbele za watu.
Haraka niliibana kucha ya kidole kidogo kwa kidole gumba changu na safari hii, nilitumia mikono yote miwili. Kwa mtu asiyejua, angeweza kudhani labda nachezea tu vidole vya mikono yangu kumbe nilikuwa na shughuli nyingine kabisa.
Kitendo hicho kilisababisha mwanamke yule awe ni kama amepandwa na mashetani, akaanza kukimbia huku na kule huku akiongea maneno yasiyoeleweka, akawa anasema kwamba eti pale eneo la tukio pamejaa wachawi na yeye ni miongoni mwa hao wachawi.
Kila mtu alibaki kumshangaa, ikabidi niachie vidole haraka maana kwa jinsi alivyokuwa akiongeaongea huku mara kwa mara akinigeukia na kunitazama kwa macho ya woga, angeweza kunisababishia kizaazaa.
Nilipoachia tu vidole vyangu, alidondoka chini na kuzimia, wanawake wengine wawili ambao inaonesha ni kama alikuja nao, wakawa wanampepea huku wakinitazama kwa macho mabaya. Kwa hali ilivyokuwa, ilibidi tu nianze kuangalia utaratibu wa kuondoka eneo hilo maana hali ilishaanza kuwa tete na sikutaka akizinduka anikute bado nipo eneo hilo.
Nilizugazuga kisha nikajichanganya na watu waliokuwa wakielekea kule upande wa stendi, tayari kulishapambazuka na kijua cha asubuhi kilishachomoza. Kilichonishangaza, ni kugundua kwamba licha ya ajali yenyewe kutokea katika mazingira ya kishirikina, bado kulikuwa na wachawi miongoni mwa watu waliokuwa wakishuhudia kilichotokea.
Nilipanga niende kwanza msibani kisha nikiwa narudi ndiyo nipitie kule Hospitali ya Tumbi kwenda kumwangalia majeruhi wa ajali ile na kama ikiwezekana nikaione na maiti ya huyo mtoto maana ukweli ni kwamba mimi ndiye niliyemchukua kutoka eneo la tukio na sehemu yake nikaweka kipande cha mgomba.
>>>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Nilikuwa na shauku kubwa sana ya kutaka kujua mambo mengi ambayo kwangu yalikuwa mageni kabisa. Nilipofika stendi, sikuwa na muda wa kupoteza, nilipanda kwenye gari linaloenda Mlandizi ambalo nalo ilikuwa ni lazima lipite pale eneo la ajali.
Safari ilianza, tulipokaribia eneo hilo, nilitoa kichwa nje ili nichungulie tena, nikamuona yule mwanamke aliyekuwa akinichokoza akiwa amekaa kitako chini kuonesha kwamba fahamu zimemrudia, ndugu zake wakawa wanajaribu kumuinua. Nilijikuta nikitabasamu huku moyoni nikijisikia fahari kubwa kuwashikisha adabu waliokuwa wakitaka kunichokoza.
Baada ya muda, gari liliwasili Mlandizi, hiyo ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kukanyaga ardhi ya eneo hilo. Niliposhuka, niliwauliza wenyeji mahali kulikokuwa na msiba ambapo bila hiyana walinionesha. Tayari watu wengi walikuwa wamekusanyika nje ya nyumba moja nzuri na ya kisasa, huku wengine wakihangaika kuweka maturubai.
Nilipofika, na mimi nilijifanya ni mwombolezaji wa kawaida tu, nikawasalimia baadhi ya watu kisha nikajichanganya na waombolezaji wengine. Ghafla nilishtuka baada ya kuona kitu ambacho sikukitarajia, nikahisi kijasho chembamba kikianza kunitoka, mara hirizi yangu ikaanza kunibana kwa nguvu, kufumba na kufumbua kamba yake ikakatika, ikadondoka chini!
Je, nini kitafuatia?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom