Simulizi: Makaburi ya wasio na hatia

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 64
ILIPOISHIA:
Tukiwa tunaendelea kuchanja mbuga, baba akiwa mbele na baba yake Rahma akiwa nyuma, mara tulianza kusikia sauti za ajabu kutoka ndani ya pori lile, huku kukiwa na purukushani kubwa, mapigo ya moyo wangu yalilipuka na kuanza kunienda mbio kuliko kawaida.
SASA ENDELEA...
“Nakufaaa! Naku...fa...aa,” sauti ya mwanamke ilisikika, aliporudia mara ya pili kuimba msaada, sauti yake ilikuwa ikikwamakwama na muda mfupi baadaye akaanza kukoroma kuonesha kwamba mtu au watu waliokuwa wakitaka kumdhuru tayari walishafanikisha lengo lao.
Tofauti na hali niliyokuwa nayo mimi, baba na baba yake Rahma hawakuonesha kushtuka chochote, yaani ilikuwa ni kama hakuna kilichotokea na wala hakuna aliyeshughulika kwa chochote.
Muda mfupi baadaye, harufu ya damu mbichi ilitawala eneo lote lile, milio ya bundi na midege mingine ya ajabu ikazidi kuifanya hali iwe ya kutisha mno. Baba aliendelea kupiga hatua ndefundefu, hukumoyo wangu ukiwa umepondwapondwa kwa hofu na mshtuko, na mimi nikawa naongeza mwendo, miguu yangu ikitetemeka kuliko kawaida.
“Unaogopa nini? Hili linaitwa pori la kafara, huku ndiyo watu wanakokuja kutolea makafara ili mambo yao yafanikiwe,” alisema baba yake Rahma huku tukiendelea kusonga mbele, sikumjibu chochote maana bado nilikuwa natetemeka sana.
Jambo ambalo mpaka leo huwa silipatii majibu, ni kwa nini watu wenye imani za giza hawaoni hatari kabisa kuyakatisha maisha ya mtu mwingine? Ni kweli kwamba sote tutakufa na kifo hakiepukiki lakini kwa nini uyakatishe maisha ya mtu mwingine kwa sababu zako binafsi?
Japokuwa na mimi nimefanya sana huo mchezo, natamani kama utokee muujiza nguvu zote za giza zipotee. Ukweli ambao watu wengi hawaujui, katika vifo vinavyotokea kila siku, iwe ni kwa ajali, magonjwa, watu kujinyonga au kuuana, nguvu za giza zinahusika kwa asilimia kubwa sana.
Kuna matukio mengine unaweza kuona kama ni kifo cha kawaida tu lakini mtu mwenye uwezo wa kuona mambo kwa jicho la tatu, anakuwa anaelewa mchezo mzima ulivyotokea. Si kila kifo kinachotokea kipo kama unavyoweza kudhani, humu duniani kuna mambo mengi sana yaliyojificha na kuna watu wanawaonea sana wenzao na kundi kubwa linaloonewa sana, ni wale watu wasio na imani thabiti ndani ya mioyo yao.
Basi tulifika mpaka barabarani, kwa kuwa muda ulikuwa umeenda sana, hakukuwa na magari yoyote yaliyokuwa yakipita, barabara ilikuwa kimya kabisa. Nilitegemea baba atasema tutafute sehemu ya kuondokea kama kawaida yetu maana nilikuwa nimchoka sana lakini safari hii alizungumza kitu cha tofauti.
Alisemakwa sababu tulikuwa tumebeba kitu cha muhimu sana, ilikuwa ni lazima tufike nyumbani kwa njia za kawaida. Aliposema tumebeba kitu muhimu sikumuelewa kwa sababu kiukweli hakuna hata mmoja kati yetu aliyekuwa na mzigo wowote. Tulianza kutembea pembezoni mwa barabara ileile ya lami tuliyojia, huku wote tukiwa kimya kabisa. Utaratibu wetu ulikuwa uleule, baba mbele, mimi katikati na baba Rahma nyuma.
Kwa bahati nzuri, tulipofika mbele kidogo, kuna Fuso lilikuwa likitokea upande wa mashambani, likiwa na shehena ya mananasi, kama ujuavyo tena Bagamoyo kunalimwa sana matunda.
Harakaharaka baba alimpungia mkono dereva, akasimamisha gari kabla hajaingia kwenye barabara ya lami, akamfuata na kuzungumza naye ambapo sekunde chache baadaye, baba alitupa ishara kwamba tupande.
Nadhani walishakubaliana, ikawa ahueni maana nilikuwa nikiiwazia sana ile safari. Gari lilikuwa limejaza mananasi mpaka juu kabisa, ikabidi tupande na kukaa juu ya mabomba na kujishikilia vizuri, dereva akaliingiza gari kwenye barabara ya lami na safari ikaendelea.
Japokuwa kule juu kulikuw ana upepo mkali unaochoma mpaka ndani ya kifua, ilibidi tuvumilie maana ilikuwa bora kuliko kutembea kwa miguu. Baada ya kama dakika hamsini hivi, tuliwasili jijini Dar, tukateremka kwenye kituo cha Mwenge, tukamshukuru sana yule dereva, yeye akaendelea na safari yake na sisi tukaanza kutembea kuelekea nyumbani.
Kitu kingine ambacho nilijifunza lakini nisingependa kukizungumzia sana leo, maduka mengi, hasa yale makubwa, yanakuwa na ulinzi wa nguvu za giza hasa nyakati za usiku ambapo kama una uwezo wa kuona mambo yaliyojificha, unaweza kustaajabu sana.
Hii dunia ina mambo mengi sana yaliyojificha, kama nioivyosema, sitaki kuelezea sana kuhusu hili. Basi tuliendelea na safari yetu mpaka tulipofika nyumbani, tayari ilishagonga saa tisa na nusu.
“Unatakiwa kuwa mtulivu na msiri, hakuna kitu cha ajabu tena kwako, umenielewa,” baba aliniambia kwa kauli ya msisitizo wakati tukiagana kwa ajili ya kila mmoja kwenda kulala lakini sikumuelewa anamaanisha nini.
“Kuanzia leo utakuwa unalala peke yako, chumba chako kinatakiwa kuwa kimefungwa muda wote na usiruhusu watu kuingiaingia, hata awe nani, umenielewa?” alisema baba, baba yake Rahma akawa anatingisha kichwa kuonesha kwamba anaunga mkono kile alichokisema baba.
Bado sikuwa naelewa kwa nini wananiambia vile, baba akahitimisha kwa kuniambia kwamba eti hategemei kunisikia nikifanya jambo lolote la ajabu. Tuliagana, nikaingia chumbani kwangu, kweli yule ndugu yangu niliyekuwa nalala naye siku mojamoja hakuwepo, kwa hiyo nilikuwa peke yangu.
Kwa jinsi nilivyokuwa nimechoka, sikutaka hata kufanya kitu kitu chochote, nikavua nguo zote, nikazima taa na kujilaza kitandani. Mwili wangu ulikuwa na maumivu sehemu mbalimbali, lakini pale yule mwanamke aliponichanja usiku huo palikuwa na maumivu makali zaidi.
Nikiwa bado natafakari mambo chungu nzima yaliyotokea kwa siku nzima, nilisikia kitu kilichonishtua sana. Chini ya kitanda changu kulikuwa kama na purukushani fulani hivi kwa mbali, ikabidi harakaharaka niinuke na kwenda kuwasha taa.
Nikainama chini kwa tahadhari kubwa na kuchungulia uvunguni, katika hali ambayo sikuitegemea kabisa, nilikiona kile kimfuko kilichotengenezwa kwa kipande cha gunia, nilichokionakule kwa yule mtaalamu kikiwa chini ya kitanda changu.
Ni kimfuko hichohicho ndicho yule mtaalamu tuliyetoka kwake usiku huo, alichomuweka yule nyoka mdogo baada ya kumlambisha damu yangu. Kilichonishtua zaidi, kimfuko kilikuwa tupu, kwa akili za harakaharaka nikahisi kwamba lazima zile purukushani nilizokuwa nazisikia, zilikuwa ni za yule nyoka akihangaika kutoka.
Sasa kimfuko kimefikaje chumbani kwangu? Na kama kile nilichokuwa nakihisi ni kweli, yule nyoka alikuwa mle ndani, ningelalaje? Nilijikuta usingizi wote ukiniisha, harakaharaka nikapanda juu ya kitanda na kukaa kwenye uchago wa kitanda ili hata akipanda kitandani, asiweze kunifikia.
Ni hapo ndipo nilipoanza kuelewa kauli za baba zilikuwa na maana gani, kuanzia ile ya kule njiani kwamba ‘tumebeba kitu muhimu sana’, mpaka yale maneno aliyoyazungumza muda mfupi uliopita kabla kila mmoja hajaenda kulala.
Nilijiapiza kwamba sitalala mpaka kupambazuke, na ukizingatia tayari muda ulishaenda sana, niliona isiwe tabu. Lakini waliosema usingizi ndugu yake kifo hawakukosea, hata sijui nini kilitokea, nilipokuja kushtuka baadaye, nilijikuta nimelala kitandani na kibaya zaidi, hata taa ilikuwa imezimwa.
Mshtuko nilioupata ulikuwa hauelezeki, nikafumbua macho na kuyakodoa kama nitaona chochote lakini nilijitahidi nisitingishike hata sehemu moja kwenye mwili wangu. Nikiwa nimejikausha kama gogo, nilihisi hali fulani kwenye ile sehemu yule mwanamke aliponichanja usiku huo.
Nilihisi kama kuna kitu kinanilamba hivi, nikaanza kutetemeka huku nikiendelea kujikausha nisisababishe mtikisiko wa aina yoyote, nilipozidi kuvuta utulivu, nikahisi kuna kitu cha baridi kinatingishikatingisha upande ule niliokuwa nalambwa, mapigo ya moyo yakawa yanadunda kama nimetoka kukimbia mbio za mita mia moja.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
Endelea
 
SEHEMU YA 42:


ILIPOISHIA:
Kwa akili yangu nilijua kwamba tayari kazi imekwisha, kumbe kulikuwa na kazi nyingine, nikaanza kutetemeka tena huku nikigeuka huku na kule kuwatazama wale watu ambao wote walikuwa na nyuso za furaha. Nilipogeuka upande wa kushoto, nilimuona mtu aliyenifanya nishtuke mno, nilifikicha macho nikiwa ni kama siamini.
SASA ENDELEA…
Alikuwa na Isrina, naye akiwa amevaa kama wale watu wengine wote waliokuwepo eneo lile. Alikuwa ametulia akinitazama kwa makini, ilionesha kwamba kumbe naye muda wote wakati yale mambo yakiendelea alikuwepo na alikuwa akinifuatilia hatua kwa hatua.
Nilishtuka kupita kiasi, nikageuka na kumtazama baba, naye akanitazama huku akitingisha kichwa kama ishara ya kuniambia ninachokiona ni kweli. Ni hapo ndipo nilipoelewa kwa nini mara kwa mara baba alikuwa akinikanya kuwa karibu na msichana huyo huku akiniuliza mara kwa mara kama najua ana malengo gani na mimi.
Nilijikuta kama kichwa kikiwa kizito, kwa tafsiri nyepesi, Isrina au Isri kama mwenyewe alivyokuwa akipenda kuitwa, alikuwa akifahamiana vizuri na baba kwa sababu wote walikuwa jamii moja. Bado sikutaka kuamini kama Isrina naye anahusika na hayo mambo, nilijaribu kuvuta kumbukumbu ya siku niliyokutana naye kwa mara ya kwanza.
Bado sikuwa na majibu ilikuwaje mpaka tukapanda basi moja, ilivyoonesha ni kama kukutana kwetu hakukuwa bahati mbaya bali ni jambo ambalo lilipangwa. Sasa kama anafahamiana na baba, kwa nini hataki kabisa niwe karibu naye? Kwa nini anamchukia? Nilijiuliza maswali mengi yasiyo na majibu.
Nikiwa bado naendelea kujiuliza maswali mengi yasiyo na majibu, yule babu ambaye baba aliniambia anaitwa Mkuu, alinishika mkono baada ya kuona nimepigwa na butwaa. Licha ya uzee wake na mwili wake kuchoka, Mkuu alikuwa na nguvu kwelikweli, akanivutia kwake na kuanza kutembea na mimi kuelekea pale katikati nilipokuwa nimelazwa kwa mara ya kwanza.
Mara nilishtuka kuona wanaume wanne, wakitoka kule pembeni na kusogea mpaka pale tulipokuwa, wakiwa wamebeba jeneza. Sikuelewa lile jeneza ni la nini lakini kwa jinsi walivyolibeba, ilionesha kama lipo tupu.
>> Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Walilisogeza mpaka pale jirani na kuliweka chini, wakasimama wakiwa ni kama wanasubiri maagizo kutoka kwa Mkuu huku wote wakinitazama. Niligeuka na kumtazama baba, akawa ni kama ananipa ishara kwamba nisiogope, nikageuka na kumtazama Isri, bado alikuwa amenikazia macho muda wote, nikashusha pumzi ndefu na kumgeukia Mkuu.
Alitoa kichupa kutoka kwenye mkoba wake wa ngozi aliokuwa ameuvaa kiunoni, akakitingisha kisha akakifungua na kunipa ishara kwamba ninuse kilichokuwemo ndani. Nilipofanya hivyo tu, nilianza kupiga chafya mfululizo kutokana na ukali wa ile dawa iliyokuwa mle ndani ya kichupa.
Nikapiga chafya zisizo na idadi, mara nikaanza kuhisi kizunguzungu kikali, nikawa napepesuka, wale wanaume wakanishika ili nisianguke, Mkuu akanisogelea pale nilipokuwa nimeshikwa, akaninusisha tena na safari hii, hakukitoa haraka kile kichupa puani, nikaendelea kupiga chafya nyingi, mwisho giza nene likatanda kwenye uso wangu na mwili wote ukawa ni kama umekufa ganzi.
Licha ya hali hiyo, bado nilikuwa naweza kuelewa kinachoendelea ingawa sikuwa na uwezo wa kufanya chochote, nikasikia wakinilaza chini kisha lile jeneza likagongwagongwa na kitu kizito, nadhani walikuwa wakilifungua.
Nikiwa bado sielewi hatma yangu, nilishtukia wakininyanyua na kunilaza ndani ya jeneza. Sikuwa hata na uwezo wa kufumbua macho ingawa bado nilikuwa na fahamu zangu. Baada ya hapo, nilisikia tena jeneza likigongwagongwa juu yangu, nikajua mimi ndiyo nimewekwa kwenye jeneza.
Mara nilisikia tena lile pembe la ng’ombe likipulizwa kisha Mkuu akapaza sauti na kutamka haraka maneno ambayo sikuyaelewa, wale watu wengine wakaanza kuimba nyimbo kama za maombolezo, nikahisi lile jeneza nililowekwa ndani yake likinyanyuliwa na waliolibeba wakaanza kutembea.
Ilikuwa ni kama nipo kwenye ndoto lakini tofauti yake ni kwamba nilikuwa najielewa. Wale watu waliendelea kuimba huku nao wakionesha kuwafuata wale walionibeba kwenye jeneza. Wakatembea umbali fulani kisha nikahisi jeneza likishushwa chini huku wale watu wakiendelea kuimba.
Nikiwa sielewi nini hatima yangu, nilihisi kama jeneza linahamishwa tena na safari hii, lilikuwa kama linaingizwa kwenye shimo, mara nikashtukia vitu vizito vikianza kuangushiwa juu ya jeneza.
>> Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Kwa jinsi vilivyokuwa vikidondoka kwa vishindo, nilielewa moja kwa moja kwamba ulikuwa ni udongo, nikajiuliza ina maana wamenipeleka makaburini? Ina maana wananizika nikiwa hai? Sikupata majibu.
Vile vishindo viliendelea na muda mfupi baadaye, zile sauti za watu waliokuwa wakiimba nazo zilianza kufifia na baadaye zikatoweka kabisa, ukimya mkubwa ukiwa umetanda kila sehemu. Sikuelewa tena kilichoendelea kwani hata zile fahamu zangu, sasa zilinitoka kabisa.
Nilipokuja kushtuka, ilikuwa tayari kumepambazuka na licha ya yote yaliyotokea, nilijikuta nikiwa kwenye chumba changu, nikiwa nimelala kitandani, mwili wangu ukiwa hauna nguvu kabisa.
“Vipi unajisikiaje?” sauti ya baba ilinishtua, nikageuza shingo na kumtazama, alikuwa amekaa pembeni yangu, mkononi akiwa na bakuli la uji. Hata nguvu za kumjibu sikuwa nazo, pembeni pia alikuwepo baba yake Rahma ambaye uso wake ulikuwa na furaha.
Walisaidiana kuniinua kidogo upande wa shingoni, wakaniwekea mto na baba akaanza kuninywesha ule uji.
“Jitahidi kunywa ili upate nguvu,” alisema baba, nikajilazimisha hivyohivyo, kweli nikamaliza lile bakuli maana ni kweli tumbo nalo lilikuwa tupu kabisa.
“Inabidi uendelee kupumzika, leo hutakiwi kufanya shughuli yoyote mpaka utakapopewa maagizo na Mkuu,” aliniambia baba, nikatingisha kichwa kuashiria kukubaliana na alichokisema ingawa sikuelewa huyo Mkuu atanipaje hayo maagizo. Yaani nilivyokuwa nikijisikia, ni kama mtu aliyeumwa kwa kipindi kirefu sana na kusababisha mwili uishiwe nguvu kabisa kiasi cha kushindwa hata kujigeuza pale kitandani.
Waliinuka na kutoka, mimi nikapitiwa tena na usingizi mzito. Nikiwa usingizini, nilianza kuota ndoto ya kutisha, nilijiona nipo kulekule porini lakini tofauti na mara ya kwanza, safari hii tulikuwa tumebaki wawili tu, mimi na Mkuu. Akawa ananiambia ili nguvu zangu nilizopewa zianze kufanya kazi, ni lazima nitoe kafara na kafara hilo ndiyo utakuwa mtihani wangu wa kwanza.
Aliniambia kwamba wachawi wote, sifa ya kwanza ni lazima wawe na uwezo kuua na kwamba kadiri mtu anavyoua watu wengi zaidi ndivyo anavyopanda ngazi. Alisema maneno hayo kwa msisitizo kisha baada ya kumaliza, alicheka kicheko cha nguvu kilichokuwa kinasikika kama mwangwi kisha akayeyuka.
Kwa jinsi ndoto ile ilivyokuwa inatisha nilijikuta nikishtuka, kutazama nje bado ilikuwa mchana, mapigo ya moyo yakawa yananienda mbio kuliko kawaida. Kumbe pale wakati nashtuka, nilipiga kelele zilizomfanya baba na baba yake Rahma waje haraka kule chumbani kwangu.
Cha ajabu, nilipowahadithia nilichoota, hakuna aliyeonesha kushtuka, sanasana baba akapigilia msumari kwa kusema kwamba ile haikuwa ndoto bali ni Mkuu alikuwa akiwasiliana na mimi.
“Baba!” nilisema kwa mshtuko nikiwa bado palepale kitandani.
“Nini sasa.”
“Mimi niue mtu?” nilipotamka maneno hayo, baba alinionesha ishara kwamba nisipige kelele, wote wakanisogelea pale kitandani na kuniambia kwa sauti ya chini kwamba Mkuu akishatoa maagizo kwa mtu, kinachofuatia huwa ni utekelezaji tu na endapo mtu akishindwa kutekeleza alichoambiwa, anakufa yeye. Nilishtuka mno, nikamtazama baba, nikamtazama baba yake Rahma, wote walionesha kumaanisha kile walichokisema.
“Hapana! Hapanaaa,” nilisema kwa sauti ya juu, ikabidi baba anizibe mdomo maana alihisi naweza kuropoka mambo mengine na kuwafanya wasiohusika wajue.
“Huna haja ya kuogopa, zipo njia za kutimiza hicho ulichoambiwa bila kuonekana kama wewe ndiyo umefanya moja kwa moja, mbona sisi huwa tunafanya sana tu” alisema baba, macho yakanitoka.
Je, nini kitafuatia?
Narudi
 
LIPOISHIA:
Sehemu ya 66

“Mbona unavuja damu nyingi hapo, umepatwa na nini?” alisema Rahma, nilipojitazama pale ubavuni, nilishtuka sana baada ya kuona damu nyingi nzito zikiwa zimenitoka bila mimi mwenyewe kujua chochote na kulowanisha kabisa shati langu.

SASA ENDELEA...

Sikujua nini cha kufanya, nilitamani nirudi haraka ndani kabla mambo hayajazidi kuharibika lakini Rahma akaning’ang’ania, kwanza akitaka kujua kwa nini yule muuzaji alikuwa akinikimbia lakini pili nini kimetokea mpaka shati langu lilowe damu kiasi kile.

Kiukweli sikuwa na majibu, nikawa naendelea kuhangaika kuzuia damu isiendelee kunitoka. Rahma alivua kitenge chake na kunipa, naye akawa ni kama haelewi kilichokuwa kinaendelea.

Tukiwa tunaendelea kuhangaika, mara nilisikia ile hirizi yangu mkononi ikinibana sana, nikajua mambo yameshaharibika. Nilishaambiwa kwamba nikiona inanibana ghafla, ujue mahali nilipo kuna mtu mwenye nguvu za giza na kuna jambo baya anataka kulifanya.


Harakaharaka nilifanya kama nilivyokuwa nimeelekezwa, niliunganisha kidole gumba na kidole kidogo kwenye mkono wa kushoto, nikafanya hivyo kwenye mkono wa kulia, nikaviminya kwa nguvu huku nikigeuka huku na kule kuangalia ni nani atakayeonesha dalili zisizo za kawaida.

Nilifundishwa kwamba kama kuna mtu yeyote anataka kukujaribu kwa nguvu za giza, ukifanya hivyo basi umemkomesha na kama nguvu zake ni ndogo, anaweza kuumbuka hadharani.

“Mmefuata nini hapa?” sauti ya mwanaume ilisikika kutoka kwenye lile duka, wote tukageuka kutazama ni nani aliyekuwa akitusemesha.

“Shikamoo mzee!” Rahma alimsalimu mwanaume mzee aliyekuwa ndani ya duka hilo kwa uchangamfu. Ilionesha wanafahamiana. Badala ya kujibu, yule mzee alimuuliza Rahma mimi ni nani na nimefuata nini pale.

“Ni kaka yangu, anaitwa Togo, tuna mazungumzo ya kifamilia tulitaka tunywe soda huku tukiendelea kuzungumza.”

“Hapana! Hatuuzi soda hapa, ukitaka huduma uje peke yako, siyo na huyo,” alisema mwanaume huyo huku akiwa amenikazia macho, Rahma akashtuka na kunigeukia. Kadiri yule mzee alivyokuwa akizidi kunitazama, na mimi ndivyo nilivyozidi kuminya vidole huku nikiwa nimemkazia macho kwani nilihisi ndiye mbaya wangu mwenyewe.

“Ondokeni! Ondokeni,” alisema mzee huyo kwa kupaza sauti, wateja wengine waliokuwa pembeni wakawa wanashangaa kwa sababu hakukuwa na jambo lolote baya tulilofanya. Rahma aligeuka na kutaka kuondoka huku akishangaa iweje mzee huyo atubadilikie kiasi hicho lakini mimi wala sikutishika kwa sababu nilishaanza kuiona hofu ilivyomjaa ghafla.

Niliendelea kumtazama huku nikiendelea kuminya vidole vyangu kwa nguvu, nikashangaa kumuona akianza kutokwa na jasho jingi huku akitingisha kichwa kama kunipa ishara kwamba niache nilichokuwa nakifanya. Mara alianza kutetemeka, jasho likazidi kumtoka na kufumba na kufumbua, akaanza kutapatapa kama anayetaka kupandwa na kifafa, akadondoka chini kama mzigo, puh!

Kitendo hicho kilinishtua sana kwani alipodondoka tu, ile hirizi nayo iliacha kunibana, sijui nini kilinituma niangalie juu ya mlango wa kuingilia kwenye duka hilo ambalo lilikuwa limejaza vitu vingi vya thamani, nikashtuka mno kuona kitu kama fuvu la mtoto mdogo likiwa limeninginizwa juu ya mlango.

Nikiwa bado nimepigwa na butwaa, nilisikia sauti ya baba kutokea nyuma. Kumbe wakati nikiendelea kuvutana na yule mzee, Rahma alikimbilia nyumbani na kwenda kumuita baba yake pamoja na baba, harakaharaka wakaja.

“Unafanya nini Togo?” baba aliniuliza kwa sauti ya chini, nadhani hakutaka asikike kwa watu ambao walishaanza kukusanyika kwa lengo la kutoa huduma ya kwanza na kutaka kujua nini kimetokea.

“Hamna kitu baba, tulikuwa tunataka kuagiza soda, hakuna kingine,” nilisema huku nikiendelea kukitazama kile kitu kama fuvu.

“Ondoka haraka, hili eneo si salama, fanya haraka,” alisema baba, nikageuka na kukutana ana kwa ana na Rahma ambaye naye alikuwa ananionesha ishara ya kutaka tuondoke haraka eneo hilo maana tayari watu walishajaa.

Nikarudi kinyumenyume, nikajichanganya kwenye umati wa watu waliokuwa wakiendelea kujaa, Rahma akanishika mkono na kuanza kunivuta haraka tuelekee nyumbani.

“Togo, kuna kitu unanificha si ndiyo? Nataka leo unieleze ukweli, ngoja kwanza nikaangalie kinachoendelea, nakuomba usitoke, baba amesema ikibidi nikufungie chumbani kwako na funguo,” Rahma aliniambia huku akipumua kwa kasi, akarudia kunisisitiza kwamba nisitoke kisha harakaharaka akaondoka.

Nilikaa kitandani na kuvua shati ambalo lilikuwa limelowa damu, nikawa najitazama pale damu ilipokuwa inanitoka. Ilikuwa ni kwenye kile kidonda changu, nikawa nashangaa iweje nitokwe na damu nyingi kiasi kile wakati sikuwa nimejitonesha? Nilijiuliza maswali mengi ambayo yote hayakuwa na majibu.

“Ina maana yule ndiyo mmiliki wa lile duka? Kwa nini anatumia uchawi kwenye biashara yake? Kile pale mlangoni ni fuvu kweli? Ina maana alimuua mtoto ili kuvutia wateja kwenye biashara yake?

“Kwa nini yule mdada amekimbia tena kwa mara nyingine, tena akiwa mtupu? Ina maana ndiyo mchezo wake kuuza akiwa hana nguo mwilini?” niliendelea kujiuliza kwa sauti ya chini, maswali yalikuwa mengi sana ndani ya kichwa changu, hata sikujua ni nani atakayenipa majibu.

Dakika kadhaa baadaye, niliwasikia baba na baba yake Rahma wakirejea wakiwa wanazungumza kwa sauti za chinichini. Muda mfupi baadaye, Rahma naye akarejea na kuja moja kwa moja mpaka chumbani kwangu.

“Vipi, nini kimeendelea?” nilimuuliza Rahma huku nikisimama, nikiwa kifua wazi, akashusha pumzi ndefu na kabla hajanijibu chochote, macho yake yakatua kwenye ile hirizi niliyokuwa nimeivaa mkononi, akashtuka kidogo kisha akahamishia macho pale kwenye jeraha dogo ambalo bado lilikuwa likichuruzika damu.

“Hapo umefanya nini?” alisema huku akinisogelea na kuinama kunitazama vizuri, nikarudi nyuma huku nikimuonesha ishara kwamba asiniguse. Akanitazama usoni na kuyagandisha macho yake, tukawa tunatazamana.

“Hizo damu zimetoka wapi?” sauti ya baba ndiyo iliyotuzindua. Kumbe wakati nikipita pale koridoni kuelekea chumbani kwangu, matone ya damu yalikuwa yakidondoka chini mpaka kwenye mlango wangu.

Alipoingia na kunikuta nipo kifua wazi, tukitazamana na Rahma, alinisogelea na kitu cha kwanza, macho yake yalitua pale kwenye jeraha langu, akapatazama kwa sekunde kadhaa kisha akanitazama usoni, naye tukawa tunatazamana.

“Rahma hebu kamuite baba yako haraka,” alisema baba, harakaharaka Rahma akatoka.

“Haya ndiyo mambo niliyokuwa siyataki mimi, umeona huo utajiri unaoutaka ulivyo na mambo magumu? Hutakiwi kutembeatembea mpaka zipite siku saba, siku nyingine utakutana na magwiji watakuua, una bahati yule mzee bado hajakomaa kwenye haya mambo,” alisema baba, akaingiza mkono mfukoni na kutoa karatasi alilokuwa amelikunja, akalifungua na kutoa ungaunga mweusi, akachukua kidogo na kunipaka huku akinitaka kuwa makini.

“Naona na wewe umeanza kuonesha ukidume wako, unawaona watu si ndiyo?” alisema baba huku akiachia tabasamu hafifu. Ilikuwa ni nadra sana kwa baba kutabasamu, akanipigapiga mgongoni huku akiendelea kutabasamu.

Muda mfupi baadaye, baba yake Rahma aliingia, nikashangaa wote wanacheka na kugongesheana mikono, naye akarudia kuniambia kwamba niwe makini na nisiende tena kwenye lile duka, kama nahitaji soda ni bora niagize niletewe nyumbani. Hawakukaa sana, wakatoka na kuniacha mle chumbani, sekunde chache Rahma akaingia tena.

“Nataka uniambie ukweli Togo, nini kinachoendelea?”

“Hujanijibu swali langu kuhusu kilichotokea.”

“Watu wanasema eti yule mzee ni mchawi na biashara zake amekuwa akiziendesha kwa uchawi sasa leo amekutana na kiboko yake, wamempeleka kwa mganga lakini hali yake siyo nzuri,” alisema rahma, nikashusha pumzi ndefu na kukaa vizuri, Rahma akanisogelea huku bado akionesha kuwa na shauku kubwa ndani ya moyo wake.

“Togo wewe ni mchawi?” Rahma aliniuliza swali ambalo lilinishtua mno moyo wangu, nikamtazama, akarudia tena swali lake huku akisisitiza kwamba anataka mimi mwenyewe ndiyo nimweleze ukweli kama kweli nampenda.

Nikashusha pumzi ndefu huku nikijiuliza, nimweleze ukweli? Uamuzi niliofikia, ilikuwa ni kumweleza tu maana hayo ndiyo yalikuwa malengo yangu tangu jana yake, sikutaka kujali ataupokeaje ukweli, nikameza mate na kumtazama.

Je, nini kitaendelea?
 
LIPOISHIA:
Sehemu ya 66

“Mbona unavuja damu nyingi hapo, umepatwa na nini?” alisema Rahma, nilipojitazama pale ubavuni, nilishtuka sana baada ya kuona damu nyingi nzito zikiwa zimenitoka bila mimi mwenyewe kujua chochote na kulowanisha kabisa shati langu.

SASA ENDELEA...

Sikujua nini cha kufanya, nilitamani nirudi haraka ndani kabla mambo hayajazidi kuharibika lakini Rahma akaning’ang’ania, kwanza akitaka kujua kwa nini yule muuzaji alikuwa akinikimbia lakini pili nini kimetokea mpaka shati langu lilowe damu kiasi kile.

Kiukweli sikuwa na majibu, nikawa naendelea kuhangaika kuzuia damu isiendelee kunitoka. Rahma alivua kitenge chake na kunipa, naye akawa ni kama haelewi kilichokuwa kinaendelea.

Tukiwa tunaendelea kuhangaika, mara nilisikia ile hirizi yangu mkononi ikinibana sana, nikajua mambo yameshaharibika. Nilishaambiwa kwamba nikiona inanibana ghafla, ujue mahali nilipo kuna mtu mwenye nguvu za giza na kuna jambo baya anataka kulifanya.


Harakaharaka nilifanya kama nilivyokuwa nimeelekezwa, niliunganisha kidole gumba na kidole kidogo kwenye mkono wa kushoto, nikafanya hivyo kwenye mkono wa kulia, nikaviminya kwa nguvu huku nikigeuka huku na kule kuangalia ni nani atakayeonesha dalili zisizo za kawaida.

Nilifundishwa kwamba kama kuna mtu yeyote anataka kukujaribu kwa nguvu za giza, ukifanya hivyo basi umemkomesha na kama nguvu zake ni ndogo, anaweza kuumbuka hadharani.

“Mmefuata nini hapa?” sauti ya mwanaume ilisikika kutoka kwenye lile duka, wote tukageuka kutazama ni nani aliyekuwa akitusemesha.

“Shikamoo mzee!” Rahma alimsalimu mwanaume mzee aliyekuwa ndani ya duka hilo kwa uchangamfu. Ilionesha wanafahamiana. Badala ya kujibu, yule mzee alimuuliza Rahma mimi ni nani na nimefuata nini pale.

“Ni kaka yangu, anaitwa Togo, tuna mazungumzo ya kifamilia tulitaka tunywe soda huku tukiendelea kuzungumza.”

“Hapana! Hatuuzi soda hapa, ukitaka huduma uje peke yako, siyo na huyo,” alisema mwanaume huyo huku akiwa amenikazia macho, Rahma akashtuka na kunigeukia. Kadiri yule mzee alivyokuwa akizidi kunitazama, na mimi ndivyo nilivyozidi kuminya vidole huku nikiwa nimemkazia macho kwani nilihisi ndiye mbaya wangu mwenyewe.

“Ondokeni! Ondokeni,” alisema mzee huyo kwa kupaza sauti, wateja wengine waliokuwa pembeni wakawa wanashangaa kwa sababu hakukuwa na jambo lolote baya tulilofanya. Rahma aligeuka na kutaka kuondoka huku akishangaa iweje mzee huyo atubadilikie kiasi hicho lakini mimi wala sikutishika kwa sababu nilishaanza kuiona hofu ilivyomjaa ghafla.

Niliendelea kumtazama huku nikiendelea kuminya vidole vyangu kwa nguvu, nikashangaa kumuona akianza kutokwa na jasho jingi huku akitingisha kichwa kama kunipa ishara kwamba niache nilichokuwa nakifanya. Mara alianza kutetemeka, jasho likazidi kumtoka na kufumba na kufumbua, akaanza kutapatapa kama anayetaka kupandwa na kifafa, akadondoka chini kama mzigo, puh!

Kitendo hicho kilinishtua sana kwani alipodondoka tu, ile hirizi nayo iliacha kunibana, sijui nini kilinituma niangalie juu ya mlango wa kuingilia kwenye duka hilo ambalo lilikuwa limejaza vitu vingi vya thamani, nikashtuka mno kuona kitu kama fuvu la mtoto mdogo likiwa limeninginizwa juu ya mlango.

Nikiwa bado nimepigwa na butwaa, nilisikia sauti ya baba kutokea nyuma. Kumbe wakati nikiendelea kuvutana na yule mzee, Rahma alikimbilia nyumbani na kwenda kumuita baba yake pamoja na baba, harakaharaka wakaja.

“Unafanya nini Togo?” baba aliniuliza kwa sauti ya chini, nadhani hakutaka asikike kwa watu ambao walishaanza kukusanyika kwa lengo la kutoa huduma ya kwanza na kutaka kujua nini kimetokea.

“Hamna kitu baba, tulikuwa tunataka kuagiza soda, hakuna kingine,” nilisema huku nikiendelea kukitazama kile kitu kama fuvu.

“Ondoka haraka, hili eneo si salama, fanya haraka,” alisema baba, nikageuka na kukutana ana kwa ana na Rahma ambaye naye alikuwa ananionesha ishara ya kutaka tuondoke haraka eneo hilo maana tayari watu walishajaa.

Nikarudi kinyumenyume, nikajichanganya kwenye umati wa watu waliokuwa wakiendelea kujaa, Rahma akanishika mkono na kuanza kunivuta haraka tuelekee nyumbani.

“Togo, kuna kitu unanificha si ndiyo? Nataka leo unieleze ukweli, ngoja kwanza nikaangalie kinachoendelea, nakuomba usitoke, baba amesema ikibidi nikufungie chumbani kwako na funguo,” Rahma aliniambia huku akipumua kwa kasi, akarudia kunisisitiza kwamba nisitoke kisha harakaharaka akaondoka.

Nilikaa kitandani na kuvua shati ambalo lilikuwa limelowa damu, nikawa najitazama pale damu ilipokuwa inanitoka. Ilikuwa ni kwenye kile kidonda changu, nikawa nashangaa iweje nitokwe na damu nyingi kiasi kile wakati sikuwa nimejitonesha? Nilijiuliza maswali mengi ambayo yote hayakuwa na majibu.

“Ina maana yule ndiyo mmiliki wa lile duka? Kwa nini anatumia uchawi kwenye biashara yake? Kile pale mlangoni ni fuvu kweli? Ina maana alimuua mtoto ili kuvutia wateja kwenye biashara yake?

“Kwa nini yule mdada amekimbia tena kwa mara nyingine, tena akiwa mtupu? Ina maana ndiyo mchezo wake kuuza akiwa hana nguo mwilini?” niliendelea kujiuliza kwa sauti ya chini, maswali yalikuwa mengi sana ndani ya kichwa changu, hata sikujua ni nani atakayenipa majibu.

Dakika kadhaa baadaye, niliwasikia baba na baba yake Rahma wakirejea wakiwa wanazungumza kwa sauti za chinichini. Muda mfupi baadaye, Rahma naye akarejea na kuja moja kwa moja mpaka chumbani kwangu.

“Vipi, nini kimeendelea?” nilimuuliza Rahma huku nikisimama, nikiwa kifua wazi, akashusha pumzi ndefu na kabla hajanijibu chochote, macho yake yakatua kwenye ile hirizi niliyokuwa nimeivaa mkononi, akashtuka kidogo kisha akahamishia macho pale kwenye jeraha dogo ambalo bado lilikuwa likichuruzika damu.

“Hapo umefanya nini?” alisema huku akinisogelea na kuinama kunitazama vizuri, nikarudi nyuma huku nikimuonesha ishara kwamba asiniguse. Akanitazama usoni na kuyagandisha macho yake, tukawa tunatazamana.

“Hizo damu zimetoka wapi?” sauti ya baba ndiyo iliyotuzindua. Kumbe wakati nikipita pale koridoni kuelekea chumbani kwangu, matone ya damu yalikuwa yakidondoka chini mpaka kwenye mlango wangu.

Alipoingia na kunikuta nipo kifua wazi, tukitazamana na Rahma, alinisogelea na kitu cha kwanza, macho yake yalitua pale kwenye jeraha langu, akapatazama kwa sekunde kadhaa kisha akanitazama usoni, naye tukawa tunatazamana.

“Rahma hebu kamuite baba yako haraka,” alisema baba, harakaharaka Rahma akatoka.

“Haya ndiyo mambo niliyokuwa siyataki mimi, umeona huo utajiri unaoutaka ulivyo na mambo magumu? Hutakiwi kutembeatembea mpaka zipite siku saba, siku nyingine utakutana na magwiji watakuua, una bahati yule mzee bado hajakomaa kwenye haya mambo,” alisema baba, akaingiza mkono mfukoni na kutoa karatasi alilokuwa amelikunja, akalifungua na kutoa ungaunga mweusi, akachukua kidogo na kunipaka huku akinitaka kuwa makini.

“Naona na wewe umeanza kuonesha ukidume wako, unawaona watu si ndiyo?” alisema baba huku akiachia tabasamu hafifu. Ilikuwa ni nadra sana kwa baba kutabasamu, akanipigapiga mgongoni huku akiendelea kutabasamu.

Muda mfupi baadaye, baba yake Rahma aliingia, nikashangaa wote wanacheka na kugongesheana mikono, naye akarudia kuniambia kwamba niwe makini na nisiende tena kwenye lile duka, kama nahitaji soda ni bora niagize niletewe nyumbani. Hawakukaa sana, wakatoka na kuniacha mle chumbani, sekunde chache Rahma akaingia tena.

“Nataka uniambie ukweli Togo, nini kinachoendelea?”

“Hujanijibu swali langu kuhusu kilichotokea.”

“Watu wanasema eti yule mzee ni mchawi na biashara zake amekuwa akiziendesha kwa uchawi sasa leo amekutana na kiboko yake, wamempeleka kwa mganga lakini hali yake siyo nzuri,” alisema rahma, nikashusha pumzi ndefu na kukaa vizuri, Rahma akanisogelea huku bado akionesha kuwa na shauku kubwa ndani ya moyo wake.

“Togo wewe ni mchawi?” Rahma aliniuliza swali ambalo lilinishtua mno moyo wangu, nikamtazama, akarudia tena swali lake huku akisisitiza kwamba anataka mimi mwenyewe ndiyo nimweleze ukweli kama kweli nampenda.

Nikashusha pumzi ndefu huku nikijiuliza, nimweleze ukweli? Uamuzi niliofikia, ilikuwa ni kumweleza tu maana hayo ndiyo yalikuwa malengo yangu tangu jana yake, sikutaka kujali ataupokeaje ukweli, nikameza mate na kumtazama.

Je, nini kitaendelea?
Endelea mzee baba
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom