Simulizi: Makaburi ya wasio na hatia

SEHEMU YA 26:



ILIPOISHIA:
Nilipomtazama, macho yangu na yake yaligongana, akanikazia macho, ikabidi nikwepeshe macho yangu, safari ya kurudi nyumbani ikaanza huku mara kwa mara baba akichomoza kichwa na kunitazama, jambo ambalo sikulifurahia.
SASA ENDELEA…
Bado nilikuwa na maswali mengi kuhusu huyu msichana, sikuwa najua ndani ya ile bahasha kuna nini na kwa sababu gani anaonekana kunijali kiasi hicho. Baada ya dakika kadhaa, tukawa tumeshawasili nyumbani.
Magari yaliposimama tu, baba alishuka haraka na kunifuata, kabla hata dereva hajanisaidia kufungua mkanda, baba alifika na kunitazama kwa macho ya ukali, safari hii nikaona kama ananionea, na mimi nikamkazia macho, tukawa tunatazamana kama majogoo yanayotaka kupigana, huku nikiificha ile bahasha asiione maana angeweza kunipokonya kama alivyofanya kwenye simu.
“Kwa nini unakuwa huelewi unapoonywa jambo? Unataka mpaka nini kitokee ndiyo ujue kwamba yule msichana ni mtu hatari kwako na kwetu sisi sote?”
Magari yaliposimama tu, baba alishuka haraka na kunifuata, kabla hata dereva hajanisaidia kufungua mkanda, baba alifika na kunitazama kwa macho ya ukali, safari hii nikaona kama ananionea, na mimi nikamkazia macho, tukawa tunatazamana kama majogoo yanayotaka kupigana, huku nikiificha ile bahasha asiione maana angeweza kunipokonya kama alivyofanya kwenye simu.
“Kwa nini unakuwa huelewi unapoonywa jambo? Unataka mpaka nini kitokee ndiyo ujue kwamba yule msichana ni mtu hatari kwako na kwetu sisi sote?”
“Sasa baba, unajua mimi kuna mambo mengi sana sielewi, halafu nikikuuliza hata hunipi majibu ya kuridhisha.”
“Hilo siyo jibu, umeanza kuwa na kiburi,” alisema baba kwa sauti ya chini lakini akionesha kama alikuwa amepania kuniadhibu. Sikumjibu chochote, akauma meno kwa hasira na kuelekea pale alipokuwa amesimama baba yake rahma, wakawa wanazungumza jambo. Nadhani walikuwa wananijadili.
Kiukweli, uhusiano wangu na baba ulikuwa umeingia doa kubwa na sababu ya yote, ni mambo ya ajabu yaliyokuwa yakinitokea ambayo yeye alionesha kwamba anajua kila kitu na pengine ndiyo chanzo cha yote. Bado nilikuwa na maswali mengi ambayo alipaswa kunijibu.
Swali la kwanza, nilitaka aniambie kwa nini wanakijiji wenzake kule kijijini kwetu, Chunya walikuwa wakimtuhumu kwamba ni mchawi na ndiye aliyeshiriki kwenye vifo vya watu wawili katika mazingira ya kutatanisha. Kwa macho yangu nilishuhudia akipambana na watu hao kabla ya baadaye kubainika kwamba wamekufa vifo vya ghafla.
Nilitaka aniambie ukweli, yeye ni mganga kama mwenyewe alivyokuwa akijinadi au alikuwa ni mchawi? Nilitaka pia anieleze, aliwezaje kusafiri kutoka Chunya mpaka Dar es Salaam bila kuwemo kwenye basi tulilokuwa tumepanda lakini muda wote akawa anatoke apale panapotokea tatizo, kama alivyotusaidia kuepukana na ajali mbaya zilizotaka kutokea wakati tukisafiri kutoka Chunya kuja Dar, ya kwanza ikiwa ni kwenye eneo hatari la Mlima Nyoka na la pili likiwa ni kwenye Mlima Kitonga.
Nilitaka anieleze vizuri aliwezaje kuniokoa nisigongwe na gari, lakini wakati huohuo watu wengine wote wakawa hawamuoni wala kumsikia zaidi yangu. Nilitaka aniambie, ile dawa aliyonipa niwe namnyunyizia dereva, ilikuwa na maana gani na iliwezaje kutuepusha na ajali?
*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
“Nataka kujua nini kimetokea hapa kwa akina Rahma maana nasikia kabla sisi hatujafika walikuwa wakiishi kwa amani, mbona tangu tuingie, japo ni muda mfupi tu lakini tayari kuna mambo mengi ya ajabu yametokea? Kwa nini naona mambo ambayo watu wengine hawayaoni?”
“Mbona unaongea peke yako Togo?” sauti ya Rahma ndiyo iliyonizindua kutoka kwenye dimbwi la mawazo machungu, nikashtuka sana kugundua kwamba kumbe nilikuwa nikizungumza kwa sauti huku mwenyewe nikidhani nawaza.
“Umesikia nini kwani?” nilimuuliza huku mapigo ya moyo wangu yakinienda mbio sana. Kwa bahati nzuri, kumbe sikuwa nimetamka kwa sauti mambo mengi zaidi ya kujiuliza kwa nini tangu tufike nyumbani kwa akina Rahma mambo mengi ya ajabu yalikuwa yakitokea.
“Kwani unafikiri ujio wenu ndiyo chanzo cha haya yote?” aliniuliza Rahma kwa upole huku akinishika mkono na kunielekeza tuelekee ndani maana nilikuwa nimesimama, nikiwa nimepoteza kabisa mwelekeo.
“Sisi ndiyo chanzo na pengine mimi ndiyo chanzo hasa,” nilisema kwa sauti ya unyonge, Rahma akaniambia kuna jambo zuri anataka tukazungumze chumbani kwake. Nilimkubalia, tulipoingia ndani tulipitiliza mpaka chumbani kwake.
Akina mama ilibidi waanze kuchakarika kwa sababu hata chakula cha usiku hakikuwa kimepikwa siku hiyo kwa sababu ya majanga yaliyonitokea ambapo baada ya kupata taarifa kwamba nipo hospitali nikiwa sijitambui, ilibidi nyumba nzima ije kunijulia hali. Waliingia jikoni huku ndugu zangu na wadogo zake Rahma wakikaa sebuleni kutazama runinga.
Baba na baba Rahma, kama kawaida yao wao walibaki nje wakiendelea na mazungumzo yao.
“Unataka kuniambia nini Rahma,” nilimuuliza kwa upole baada ya kumuona akifunga mlango wa chumbani kwake kwa komeo. Hakujibu kitu zaidi ya kuvua blauzi yake kisha ‘bra’, akanisogelea na kunikumbatia kwa nguvu.
*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
Japokuwa mwili wangu haukuwa na nguvu, nilijikuta nikisisimka mno. Rahma alikuwa amejaliwa kifua kizuri mno, ambacho kwa mwanaume yeyote aliyekamilika, ilikuwa ni lazima atokwe na udenda kama fisi aliyeona mfupa.
Rahma aliendelea kunikumbatia huku akinibusu sehemu mbalimbali za mwili wangu kimahaba, hali ambayo ilinichanganya kabisa kichwa changu. Taratibu alinirudisha nyuma mpaka tulipofika kwenye uwanja wa fundi seremala, akanisukumia juu yake kisha akamalizia na za chini zilizokuwa zimesalia.
Akionesha kuwa na papara za hali ya juu, alihamia kwangu na kuitoa ya juu, nikabaki kifua wazi, akahamia na ile ya chini na muda mfupi baadaye, tulikuwa ‘saresare’ maua. Bado mwili wangu haukuwa na nguvu kwa hiyo nilimuachia yeye ndiye awe ‘dairekta’ wa filamu ile ya kusisimua na kweli alikitendea haki cheo nilichompa.
Kwa ufanisi wa hali ya juu, Rahma aliitii kiu yangu, mpaka anashuka kutoka juu ya mnazi, alikuwa ameshaangua madafu kadhaa, akajitupa upande wa pili huku akinishukuru, na mimi nikawa namshukuru. Hatukuchukua raundi, kila mmoja akapitiwa na usingizi mzito.
Nadhani wangu ulikuwa mzito zaidi kwa sababu kuichwa changu kilikuwa kimebeba mambo mazito mno na alichonipa rahma ilikuwa sawa na dawa ya usingizi. Tulikuja kushtuka baadaye baada ya kusikia mlango wa chumba cha Rahma ukigongwa. Mimi ndiye niliyekuwa wa kwanza kuzinduka, nikamuamsha Rahma ambaye aliamka kichovu na kusogea karibu na mlango.
Safari hii hatukuwa na hofu tena kwani tulikuwa na ruhusa ya kukaa pamoja karibu, mimi kazi yangu ikiwa ni kuhakikisha rahma harudii tena kujaribu kuyakatisha maisha yake na Rahma kuhakikisha ananisaidia mimi mgonjwa.
“Unasemaje?”
*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
“Mama anauliza kama mtakula na sisi au mletewe chakula chenu huku.”
‘Ngoja nakuja mwenyewe,” alijibu Rahma wakati akizungumza na mdogo wake aliyetumwa na mama yao kuwaulizia.
‘Eti mpenzi wangu, we unapenda tukakae sebuleni au tulie hukuhuku chumbani.”
‘Utakavbyosema wewe hamna shida ila napenda zaidi tukikaa peke yetu,” nilimjibu, akanitazama kwa macho yake ambayo yalikuwa yameelemewa na usingizi kisha akaachia tabasamu la kichovu.
“Ngoja nikaonge kwanza,” alisema na kuchukua kitenge, akaelekea bafuni na muda mfupi baadaye, alirudi akiwa amechangamka kidogo. Ilibidi na mimi niende kuoga wakati yeye akihangaikia chakula.
Niliporudi kutoka bafuni, tayari rahma alikuwa ameleta chakula kizuri kule chumbani. Tofauti ya vyakula tulivyozoea kula kijijini na mjini ilikuwa kubwa mno. Chakula kilipikwa vizuri, yaani kwa kukitazama tu ilikuwa ni lazima mate yakutoke. Tulinawa vizuri lakini nilipotaka kuanza kula, Rahma alinikatazana na kusema anataka anilishe kidogo.
Yalikuwa ni mambo mageni kabisa, nilizoea kuona watoto wadogo au wagonjwa ambao wako mahtuti ndiyo wanalishwa, lakini eti dume mimi nilishwe? Hata hivyo sikumkatalia. Akaanza kunilisha kwa upole, huku mara kwa mara akinitazama machoni. Sijui nini kilimtokea Rahma lakini alionesha kunipenda sana, tena sana.
*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
Mara kwa mara alikuwa akinibusu na kuniambia kwamba ananipenda sana, mpaka nikawa najisikia aibu. Sikuwa najua kabisa mambo ya kikubwa na wala sikuwa na uelewa wowote wa mahaba. Nilikuwa nikisikiasikia kwamba watu wa pwani ndiyo wataalamu wa hayo mambo.
Japo Rahma alikuwa akinilisha matonge madogo tofauti na niliyozoea lakini kiukweli nikiri kwamba nilijisikia raha ya ajabu ndani ya moyo wangu. Tulipomaliza kula, alitoa vyombo, akaja kufanya usafi kisha akafunga tena mlango.
“Itabidi mimi nikalale chumbani kwangu,” nilimwambia Rahma lakini akakataa katakata, akaniambia tutalala wote humo chumbani kwake na tutajifunika shuka moja. Japokuwa kwa nje nilikuwa navunga, ukweli ni kwamba hata mimi nilikuwa napenda sana kuwa karibu na Rahma hasa kutokana na mapenzi ya dhati aliyokuwa ananionesha.
Ile tofauti ya umri kati yetu sikuiona tena, namimi nikawa najiona mkubwa kama yeye, hata ile harufu ya undugu kati yetu nayo ilitoweka kabisa, ndani ya muda mfupi tu tuliokaa pamoja ikawa utafikiri tumeishi pamoja kwa miaka mingi tangu zamani.
Tulipiga stori za hapa na pale, baadaye muda wa kulala ulipofika, kama ilivyokuwa mara ya kwanza, Rahma aliniganda kama ruba, tukapeana tende na halua kwa mara nyingine kabla ya kupitiwa na usingizi mzito, akiwa ameniganda kifuani kama ruba.
Nilikuja kuzinduka usiku wa manane baada ya kuhisi hali isiyo ya kawaida. Kilichoniamsha, zilikuwa ni kelele za paka waliokuwa wakipigana juu ya paa, huku wakitoa milio ya ajabu kama watoto wachanga.
Sikutaka kumuamsha Rahma, nilimtoa kifuani kwangu taratibu kisha nikashusha miguu chini, nikawa nimekaa huku nikitazama huku na kule. Sikuweza kuona chochote kutokana na giza lililokuwa limetanda usiku huo. Mara nikasikia kishindo kizito kama cha kitu kilichodondoka kutoka darini mpaka sakafuni, mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio kuliko kawaida.
Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 26:



ILIPOISHIA:
Nilipomtazama, macho yangu na yake yaligongana, akanikazia macho, ikabidi nikwepeshe macho yangu, safari ya kurudi nyumbani ikaanza huku mara kwa mara baba akichomoza kichwa na kunitazama, jambo ambalo sikulifurahia.
SASA ENDELEA…
Bado nilikuwa na maswali mengi kuhusu huyu msichana, sikuwa najua ndani ya ile bahasha kuna nini na kwa sababu gani anaonekana kunijali kiasi hicho. Baada ya dakika kadhaa, tukawa tumeshawasili nyumbani.
Magari yaliposimama tu, baba alishuka haraka na kunifuata, kabla hata dereva hajanisaidia kufungua mkanda, baba alifika na kunitazama kwa macho ya ukali, safari hii nikaona kama ananionea, na mimi nikamkazia macho, tukawa tunatazamana kama majogoo yanayotaka kupigana, huku nikiificha ile bahasha asiione maana angeweza kunipokonya kama alivyofanya kwenye simu.
“Kwa nini unakuwa huelewi unapoonywa jambo? Unataka mpaka nini kitokee ndiyo ujue kwamba yule msichana ni mtu hatari kwako na kwetu sisi sote?”
Magari yaliposimama tu, baba alishuka haraka na kunifuata, kabla hata dereva hajanisaidia kufungua mkanda, baba alifika na kunitazama kwa macho ya ukali, safari hii nikaona kama ananionea, na mimi nikamkazia macho, tukawa tunatazamana kama majogoo yanayotaka kupigana, huku nikiificha ile bahasha asiione maana angeweza kunipokonya kama alivyofanya kwenye simu.
“Kwa nini unakuwa huelewi unapoonywa jambo? Unataka mpaka nini kitokee ndiyo ujue kwamba yule msichana ni mtu hatari kwako na kwetu sisi sote?”
“Sasa baba, unajua mimi kuna mambo mengi sana sielewi, halafu nikikuuliza hata hunipi majibu ya kuridhisha.”
“Hilo siyo jibu, umeanza kuwa na kiburi,” alisema baba kwa sauti ya chini lakini akionesha kama alikuwa amepania kuniadhibu. Sikumjibu chochote, akauma meno kwa hasira na kuelekea pale alipokuwa amesimama baba yake rahma, wakawa wanazungumza jambo. Nadhani walikuwa wananijadili.
Kiukweli, uhusiano wangu na baba ulikuwa umeingia doa kubwa na sababu ya yote, ni mambo ya ajabu yaliyokuwa yakinitokea ambayo yeye alionesha kwamba anajua kila kitu na pengine ndiyo chanzo cha yote. Bado nilikuwa na maswali mengi ambayo alipaswa kunijibu.
Swali la kwanza, nilitaka aniambie kwa nini wanakijiji wenzake kule kijijini kwetu, Chunya walikuwa wakimtuhumu kwamba ni mchawi na ndiye aliyeshiriki kwenye vifo vya watu wawili katika mazingira ya kutatanisha. Kwa macho yangu nilishuhudia akipambana na watu hao kabla ya baadaye kubainika kwamba wamekufa vifo vya ghafla.
Nilitaka aniambie ukweli, yeye ni mganga kama mwenyewe alivyokuwa akijinadi au alikuwa ni mchawi? Nilitaka pia anieleze, aliwezaje kusafiri kutoka Chunya mpaka Dar es Salaam bila kuwemo kwenye basi tulilokuwa tumepanda lakini muda wote akawa anatoke apale panapotokea tatizo, kama alivyotusaidia kuepukana na ajali mbaya zilizotaka kutokea wakati tukisafiri kutoka Chunya kuja Dar, ya kwanza ikiwa ni kwenye eneo hatari la Mlima Nyoka na la pili likiwa ni kwenye Mlima Kitonga.
Nilitaka anieleze vizuri aliwezaje kuniokoa nisigongwe na gari, lakini wakati huohuo watu wengine wote wakawa hawamuoni wala kumsikia zaidi yangu. Nilitaka aniambie, ile dawa aliyonipa niwe namnyunyizia dereva, ilikuwa na maana gani na iliwezaje kutuepusha na ajali?
*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
“Nataka kujua nini kimetokea hapa kwa akina Rahma maana nasikia kabla sisi hatujafika walikuwa wakiishi kwa amani, mbona tangu tuingie, japo ni muda mfupi tu lakini tayari kuna mambo mengi ya ajabu yametokea? Kwa nini naona mambo ambayo watu wengine hawayaoni?”
“Mbona unaongea peke yako Togo?” sauti ya Rahma ndiyo iliyonizindua kutoka kwenye dimbwi la mawazo machungu, nikashtuka sana kugundua kwamba kumbe nilikuwa nikizungumza kwa sauti huku mwenyewe nikidhani nawaza.
“Umesikia nini kwani?” nilimuuliza huku mapigo ya moyo wangu yakinienda mbio sana. Kwa bahati nzuri, kumbe sikuwa nimetamka kwa sauti mambo mengi zaidi ya kujiuliza kwa nini tangu tufike nyumbani kwa akina Rahma mambo mengi ya ajabu yalikuwa yakitokea.
“Kwani unafikiri ujio wenu ndiyo chanzo cha haya yote?” aliniuliza Rahma kwa upole huku akinishika mkono na kunielekeza tuelekee ndani maana nilikuwa nimesimama, nikiwa nimepoteza kabisa mwelekeo.
“Sisi ndiyo chanzo na pengine mimi ndiyo chanzo hasa,” nilisema kwa sauti ya unyonge, Rahma akaniambia kuna jambo zuri anataka tukazungumze chumbani kwake. Nilimkubalia, tulipoingia ndani tulipitiliza mpaka chumbani kwake.
Akina mama ilibidi waanze kuchakarika kwa sababu hata chakula cha usiku hakikuwa kimepikwa siku hiyo kwa sababu ya majanga yaliyonitokea ambapo baada ya kupata taarifa kwamba nipo hospitali nikiwa sijitambui, ilibidi nyumba nzima ije kunijulia hali. Waliingia jikoni huku ndugu zangu na wadogo zake Rahma wakikaa sebuleni kutazama runinga.
Baba na baba Rahma, kama kawaida yao wao walibaki nje wakiendelea na mazungumzo yao.
“Unataka kuniambia nini Rahma,” nilimuuliza kwa upole baada ya kumuona akifunga mlango wa chumbani kwake kwa komeo. Hakujibu kitu zaidi ya kuvua blauzi yake kisha ‘bra’, akanisogelea na kunikumbatia kwa nguvu.
*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
Japokuwa mwili wangu haukuwa na nguvu, nilijikuta nikisisimka mno. Rahma alikuwa amejaliwa kifua kizuri mno, ambacho kwa mwanaume yeyote aliyekamilika, ilikuwa ni lazima atokwe na udenda kama fisi aliyeona mfupa.
Rahma aliendelea kunikumbatia huku akinibusu sehemu mbalimbali za mwili wangu kimahaba, hali ambayo ilinichanganya kabisa kichwa changu. Taratibu alinirudisha nyuma mpaka tulipofika kwenye uwanja wa fundi seremala, akanisukumia juu yake kisha akamalizia na za chini zilizokuwa zimesalia.
Akionesha kuwa na papara za hali ya juu, alihamia kwangu na kuitoa ya juu, nikabaki kifua wazi, akahamia na ile ya chini na muda mfupi baadaye, tulikuwa ‘saresare’ maua. Bado mwili wangu haukuwa na nguvu kwa hiyo nilimuachia yeye ndiye awe ‘dairekta’ wa filamu ile ya kusisimua na kweli alikitendea haki cheo nilichompa.
Kwa ufanisi wa hali ya juu, Rahma aliitii kiu yangu, mpaka anashuka kutoka juu ya mnazi, alikuwa ameshaangua madafu kadhaa, akajitupa upande wa pili huku akinishukuru, na mimi nikawa namshukuru. Hatukuchukua raundi, kila mmoja akapitiwa na usingizi mzito.
Nadhani wangu ulikuwa mzito zaidi kwa sababu kuichwa changu kilikuwa kimebeba mambo mazito mno na alichonipa rahma ilikuwa sawa na dawa ya usingizi. Tulikuja kushtuka baadaye baada ya kusikia mlango wa chumba cha Rahma ukigongwa. Mimi ndiye niliyekuwa wa kwanza kuzinduka, nikamuamsha Rahma ambaye aliamka kichovu na kusogea karibu na mlango.
Safari hii hatukuwa na hofu tena kwani tulikuwa na ruhusa ya kukaa pamoja karibu, mimi kazi yangu ikiwa ni kuhakikisha rahma harudii tena kujaribu kuyakatisha maisha yake na Rahma kuhakikisha ananisaidia mimi mgonjwa.
“Unasemaje?”
*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
“Mama anauliza kama mtakula na sisi au mletewe chakula chenu huku.”
‘Ngoja nakuja mwenyewe,” alijibu Rahma wakati akizungumza na mdogo wake aliyetumwa na mama yao kuwaulizia.
‘Eti mpenzi wangu, we unapenda tukakae sebuleni au tulie hukuhuku chumbani.”
‘Utakavbyosema wewe hamna shida ila napenda zaidi tukikaa peke yetu,” nilimjibu, akanitazama kwa macho yake ambayo yalikuwa yameelemewa na usingizi kisha akaachia tabasamu la kichovu.
“Ngoja nikaonge kwanza,” alisema na kuchukua kitenge, akaelekea bafuni na muda mfupi baadaye, alirudi akiwa amechangamka kidogo. Ilibidi na mimi niende kuoga wakati yeye akihangaikia chakula.
Niliporudi kutoka bafuni, tayari rahma alikuwa ameleta chakula kizuri kule chumbani. Tofauti ya vyakula tulivyozoea kula kijijini na mjini ilikuwa kubwa mno. Chakula kilipikwa vizuri, yaani kwa kukitazama tu ilikuwa ni lazima mate yakutoke. Tulinawa vizuri lakini nilipotaka kuanza kula, Rahma alinikatazana na kusema anataka anilishe kidogo.
Yalikuwa ni mambo mageni kabisa, nilizoea kuona watoto wadogo au wagonjwa ambao wako mahtuti ndiyo wanalishwa, lakini eti dume mimi nilishwe? Hata hivyo sikumkatalia. Akaanza kunilisha kwa upole, huku mara kwa mara akinitazama machoni. Sijui nini kilimtokea Rahma lakini alionesha kunipenda sana, tena sana.
*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
Mara kwa mara alikuwa akinibusu na kuniambia kwamba ananipenda sana, mpaka nikawa najisikia aibu. Sikuwa najua kabisa mambo ya kikubwa na wala sikuwa na uelewa wowote wa mahaba. Nilikuwa nikisikiasikia kwamba watu wa pwani ndiyo wataalamu wa hayo mambo.
Japo Rahma alikuwa akinilisha matonge madogo tofauti na niliyozoea lakini kiukweli nikiri kwamba nilijisikia raha ya ajabu ndani ya moyo wangu. Tulipomaliza kula, alitoa vyombo, akaja kufanya usafi kisha akafunga tena mlango.
“Itabidi mimi nikalale chumbani kwangu,” nilimwambia Rahma lakini akakataa katakata, akaniambia tutalala wote humo chumbani kwake na tutajifunika shuka moja. Japokuwa kwa nje nilikuwa navunga, ukweli ni kwamba hata mimi nilikuwa napenda sana kuwa karibu na Rahma hasa kutokana na mapenzi ya dhati aliyokuwa ananionesha.
Ile tofauti ya umri kati yetu sikuiona tena, namimi nikawa najiona mkubwa kama yeye, hata ile harufu ya undugu kati yetu nayo ilitoweka kabisa, ndani ya muda mfupi tu tuliokaa pamoja ikawa utafikiri tumeishi pamoja kwa miaka mingi tangu zamani.
Tulipiga stori za hapa na pale, baadaye muda wa kulala ulipofika, kama ilivyokuwa mara ya kwanza, Rahma aliniganda kama ruba, tukapeana tende na halua kwa mara nyingine kabla ya kupitiwa na usingizi mzito, akiwa ameniganda kifuani kama ruba.
Nilikuja kuzinduka usiku wa manane baada ya kuhisi hali isiyo ya kawaida. Kilichoniamsha, zilikuwa ni kelele za paka waliokuwa wakipigana juu ya paa, huku wakitoa milio ya ajabu kama watoto wachanga.
Sikutaka kumuamsha Rahma, nilimtoa kifuani kwangu taratibu kisha nikashusha miguu chini, nikawa nimekaa huku nikitazama huku na kule. Sikuweza kuona chochote kutokana na giza lililokuwa limetanda usiku huo. Mara nikasikia kishindo kizito kama cha kitu kilichodondoka kutoka darini mpaka sakafuni, mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio kuliko kawaida.
Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 27:



ILIPOISHIA:
Sikutaka kumuamsha Rahma, nilimtoa kifuani kwangu taratibu kisha nikashusha miguu chini, nikawa nimekaa huku nikitazama huku na kule. Sikuweza kuona chochote kutokana na giza lililokuwa limetanda usiku huo. Mara nikasikia kishindo kizito kama cha kitu kilichodondoka kutoka darini mpaka sakafuni, mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio kuliko kawaida.
SASA ENDELEA…
Nilikaza macho kwenye giza kujaribu kuangalia ni kitu gani hicho kilichodondoka, kwa mbali nikaanza kuona kama mtu amepiga magoti kwenye kona ya chumba hicho, taratibu akaanza kuinuka, nikazidi kumkazia macho na kadiri muda ulivyokuwa ukizonga ndivyo nilivyozidi kuiona vizuri taswira yake.
Nilimtambua kwamba ni mwanamke kutokana na maumbile yake ingawa alionesha kuwa ni mzee kwani niliweza kuiona ngozi yake ilivyokuwa imekunjamana, nikamkazia macho usoni nikitaka niione sura yake. Hata hivyo eneo la usoni lilikuwa na giza sana, nikamuona akiinua mikono juu kama anayetoa ishara fulani, akageuka na kuanza kujisugua makalio yake ukutani.
Mara nilisikia kishindo kingine, hofu ikazidi kutanda ndani ya moyo wangu, kijasho chembamba kikawa kinanitoka huku nikiwa nimekodoa macho kwa nguvu zote.
*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
Nilitamani niamke nikawashe taa lakini ujasiri huo sikuwa nao, nilitamani niingie chini ya kitanda lakini mwili wote haukuwa na nguvu, nilitamani kupiga kelele kuwaamsha nyumba nzima lakini sikuwa na uwezo huo, nikawa natetemeka kuliko kawaida.
Nilipotazama kwa makini pale chini, nilimuona mtu mwingine kama yule wa kwanza naye akiinuka taratibu lakini tofauti yake, huyu alikuwa mwanaume kutokana na jinsi mwili wake ulivyokuwa na alionesha pia kuwa mzee zaidi maana mpaka mgongo wake ulikuwa umepinda.
Alipoinuka, naye alisogea ukutani na kuanza ‘kusonta’ ukutani kwa kutumia makalio yake kisha akasogea mbele na kushikama mikono na yule mwanamke wa kwanza, wakaiinua juu na kutoa ishara ambayo sikuielewa, mara nikasikia vishindo mfululizo.
Vilisikika vishindo kama sita hivi, ikimaanisha kwamba watu wengine sita walikuwa wameingia, uzalendo ukanishinda. Sijui nilipata wapi ujasiri, nikasimama wima kisha nikapaza sauti, ‘tokeni hapa washenzi nyie, hata mimi baba yangu ni mchawi vilevile’.
Kauli yangu ni kama iliwashtua watu wale wa ajabu ambao hata sielewi niwaelezeeje, wote wakashtuka na kunitazama, nikazidi kushtuka baada ya kuona wote macho yao yalikuwa yakiwaka kama mnyama mkali gizani.
Kwa wale ambao wameishi maeneo ya maporini watakuwa wananielewa kwamba mida ya usiku, wanyama kama simba, chui, mbwa mwitu au hata mbwa wa kawaida na paka, wakiwa kwenye giza totoro kisha wakakukodolea macho yao, huwa yanatoa mwanga fulani wa kutisha.
Kwa jinsi walivyonitazama, hofu ilinizidi maradufu lakini nikaona hakuna kingine cha kufanya zaidi ya kuendelea ‘kugangamala’. Sikuwa najua kama wakinigeukia nitafanya nini, sikuwa najua mbinu zozote za kupambana nao na eti nilijikuta nikijilaumu kwa nini baba hakunifundisha au hakunipa mbinu yoyote ya kukabiliana na wachawi.
*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
Yule mwanamke aliyekuwa wa kwanza kuingia mle ndani, nilimuona akinisogelea huku akionesha kutokuwa na hata chembe ya woga. Nilihisi haja ndogo ikitaka kunitoka lakini nilijikaza kiume na kusema liwalo na liwe, akanisogelea jirani kabisa huku akiendelea kunitazama kwa macho yake makali, cha ajabu, licha ya kunisogelea, sikuweza kabisa kuitambua sura yake.
Nimewahi kusikia kwamba wachawi wana kawaida ya kula nyama za watu, nikahisi na mimi usiku huo nakwenda kuliwa huku nikijiona. Niliujutia uamuzi wangu wa kusimama na kuwafokea watu hao, nikiwa bado natetemeka, nilisikia kofi moja zito likitua kwenye shavu langu la kushoto, maumivui niliyoyasikia yalikuwa hayaelezeki, nikapiga kelele kwa nguvu nikimuita baba.
Sikumbuki kama nimewahi kutoa sauti kubwa kama hiyo maishani mwangu, mara mlango ukaanza kugongwa kwa nguvu nje, nikasikia kibao kingine kikitua kwenye shavu la upande wa pili, likafuatiwa na misonyo mingi kisha wale watu wakayeyuka wote na kupotea kama moshi upoteavyo angani.
“Togo! Nini kimetokea?” alisema baba baada ya kuwa amefanikiwa kufungua mlango na kuwasha taa. Jambo la aibu ni kwamba baada ya ule mchezo wa kikubwa niliocheza na Rahma, hakuna aliyekumbuka tena kuvaa nguo zake kwa hiyo nilikuwa kama nilivyozaliwa, baba akanitazama kwa mshangao.
Najua alishangazwa na mambo mengi kwa wakati mmoja, kwanza kwa nini nilikuwa chumbani kwa Rahma mpaka usiku huo wakati makubaliano yalikuwa ni kwamba kila mmoja atalala kwake, kwa maana kwamba baada ya c hakula ilitakiwa mimi nitoke na kwenda kwenye chumba nilichopangiwa lakini sikufanya hivyo. Yote tisa, kumi ni kwamba nilikuwa kama nilivyozaliwa, na Rahma naye ambaye bado alikuwa kwenye usingizi mzito, akikoroma bila kujua chochote kilichokuwa kinaendelea, hakuwa na chochote mwilini, nikamuona baba akishusha pumzi ndefu na kunipa ishara kwamba nivae kwanza nguo, akatoka na kuurudisha mlango.
*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
Kumbe sekeseke hilo lilisababisha nitokwe na haja ndogo bila kujua, ikabidi nichukue tambara la kufanyia usafi na kufuta harakaharaka huku nikigeuka kumtazama Rahma asije kuwa ameamka na kuona nilichokifanya. Nilipomaliza kufuta, harakaharaka nilivaa nguo zangu huku nikitetemeka kuliko kawaida.
Baba alikuwa pale mlangoni akinisubiri, nilipomaliza aliingia na kunionesha ishara kwamba nisizungumze kwa sauti ya juu, akaniuliza nini kilichotokea.
“Wachawi baba, wachawi wengi wamekuja, angalia walivyonifanya,” nilisema huku nikimuonesha mashavu yangu ambayo nilikuwa nahisi kama yanawaka moto. Awali niliona baba hataki kuamini kama ambavyo imekuwa kawaida yake mara kwa mara ninapotokewa na mambo kama hayo lakini nashukuru safari hii kulikuwa na ushahidi wa moja kwa moja.
“Mungu wangu, umefanya nini?”
“Wamenipiga,” nilisema huku nikianza kutokwa na machozi.
“Hebu niambie ukweli, umefanya tena mapenzi na Rahma?”
“Ndiyo.”
“Lakini si tumeshawakataza nyie na kuwasisitiza kwamba msirudie ujinga wenu?” baba alizungumza kwa hasira lakini kwa sauti ya chini. Sikujua kwa nini alikuwa akizungumza kwa sauti ya chini, akanishika mkono na kufungua mlango, akatazama huku na kule na alipojiridhisha, alinipeleka mpaka kwenye chumba ambacho ndicho nilichotakiwa kulala.
“Hutakiwi kumwambia yeyote kuhusu hiki kilichotokea, umenielewa?” baba aliniambia, nikatingisha kichwa lakini nilijiuliza, kama yeye ameweza kusikia zile kelele nilizopiga, si ina maana nyumba nzima wamesikia? Na kama wamesikia, kwa nini wengine wote hawakuamka isipokuwa yeye tu?
“Lakini kwa nini haya yanatokea?” utajua tu lakini unachoniudhi ni kwamba ukiambiwa jambo fulani usilifanye, wewe ndiyo unalifanya. Hukuwa na mambo ya wanawake kabisa lakini tangu tumefika hapa ndiyo umekuwa mchezo wako… utasababisha vifo vya wasio na hatia kwa nini unakuwa mgumu kuelewa?” baba alisema, safari hii siyo kwa ukali bali kwa hisia za ndano kabisa, kauli yake ikanishtua mno.
Yaani mimi ndiyo nisababishe vifo vya wasio na hatia? Kivipi? Halafu kulikuwa na uhusiano gani wa mimi kulala na Rahma na hayo yaliyokuwa yanatokea? Katika yote, jambo ambalo nilijiapiza, ni kwamba kamwe sitamuacha Rahma maana alikuwa amenionesha dunia ya tofauti mno.
Baba alitoa kichupa kilichokuwa na unga mweusi lakini kabla hajafanya chochote, aliniambia nikajitazame kwenye kioo kilichokuwa humo chumbani.
“Mungu wangu,” nilisema kwa mshtuko usio wa kawaida.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue
 
SEHEMU YA 27:



ILIPOISHIA:
Sikutaka kumuamsha Rahma, nilimtoa kifuani kwangu taratibu kisha nikashusha miguu chini, nikawa nimekaa huku nikitazama huku na kule. Sikuweza kuona chochote kutokana na giza lililokuwa limetanda usiku huo. Mara nikasikia kishindo kizito kama cha kitu kilichodondoka kutoka darini mpaka sakafuni, mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio kuliko kawaida.
SASA ENDELEA…
Nilikaza macho kwenye giza kujaribu kuangalia ni kitu gani hicho kilichodondoka, kwa mbali nikaanza kuona kama mtu amepiga magoti kwenye kona ya chumba hicho, taratibu akaanza kuinuka, nikazidi kumkazia macho na kadiri muda ulivyokuwa ukizonga ndivyo nilivyozidi kuiona vizuri taswira yake.
Nilimtambua kwamba ni mwanamke kutokana na maumbile yake ingawa alionesha kuwa ni mzee kwani niliweza kuiona ngozi yake ilivyokuwa imekunjamana, nikamkazia macho usoni nikitaka niione sura yake. Hata hivyo eneo la usoni lilikuwa na giza sana, nikamuona akiinua mikono juu kama anayetoa ishara fulani, akageuka na kuanza kujisugua makalio yake ukutani.
Mara nilisikia kishindo kingine, hofu ikazidi kutanda ndani ya moyo wangu, kijasho chembamba kikawa kinanitoka huku nikiwa nimekodoa macho kwa nguvu zote.
*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
Nilitamani niamke nikawashe taa lakini ujasiri huo sikuwa nao, nilitamani niingie chini ya kitanda lakini mwili wote haukuwa na nguvu, nilitamani kupiga kelele kuwaamsha nyumba nzima lakini sikuwa na uwezo huo, nikawa natetemeka kuliko kawaida.
Nilipotazama kwa makini pale chini, nilimuona mtu mwingine kama yule wa kwanza naye akiinuka taratibu lakini tofauti yake, huyu alikuwa mwanaume kutokana na jinsi mwili wake ulivyokuwa na alionesha pia kuwa mzee zaidi maana mpaka mgongo wake ulikuwa umepinda.
Alipoinuka, naye alisogea ukutani na kuanza ‘kusonta’ ukutani kwa kutumia makalio yake kisha akasogea mbele na kushikama mikono na yule mwanamke wa kwanza, wakaiinua juu na kutoa ishara ambayo sikuielewa, mara nikasikia vishindo mfululizo.
Vilisikika vishindo kama sita hivi, ikimaanisha kwamba watu wengine sita walikuwa wameingia, uzalendo ukanishinda. Sijui nilipata wapi ujasiri, nikasimama wima kisha nikapaza sauti, ‘tokeni hapa washenzi nyie, hata mimi baba yangu ni mchawi vilevile’.
Kauli yangu ni kama iliwashtua watu wale wa ajabu ambao hata sielewi niwaelezeeje, wote wakashtuka na kunitazama, nikazidi kushtuka baada ya kuona wote macho yao yalikuwa yakiwaka kama mnyama mkali gizani.
Kwa wale ambao wameishi maeneo ya maporini watakuwa wananielewa kwamba mida ya usiku, wanyama kama simba, chui, mbwa mwitu au hata mbwa wa kawaida na paka, wakiwa kwenye giza totoro kisha wakakukodolea macho yao, huwa yanatoa mwanga fulani wa kutisha.
Kwa jinsi walivyonitazama, hofu ilinizidi maradufu lakini nikaona hakuna kingine cha kufanya zaidi ya kuendelea ‘kugangamala’. Sikuwa najua kama wakinigeukia nitafanya nini, sikuwa najua mbinu zozote za kupambana nao na eti nilijikuta nikijilaumu kwa nini baba hakunifundisha au hakunipa mbinu yoyote ya kukabiliana na wachawi.
*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
Yule mwanamke aliyekuwa wa kwanza kuingia mle ndani, nilimuona akinisogelea huku akionesha kutokuwa na hata chembe ya woga. Nilihisi haja ndogo ikitaka kunitoka lakini nilijikaza kiume na kusema liwalo na liwe, akanisogelea jirani kabisa huku akiendelea kunitazama kwa macho yake makali, cha ajabu, licha ya kunisogelea, sikuweza kabisa kuitambua sura yake.
Nimewahi kusikia kwamba wachawi wana kawaida ya kula nyama za watu, nikahisi na mimi usiku huo nakwenda kuliwa huku nikijiona. Niliujutia uamuzi wangu wa kusimama na kuwafokea watu hao, nikiwa bado natetemeka, nilisikia kofi moja zito likitua kwenye shavu langu la kushoto, maumivui niliyoyasikia yalikuwa hayaelezeki, nikapiga kelele kwa nguvu nikimuita baba.
Sikumbuki kama nimewahi kutoa sauti kubwa kama hiyo maishani mwangu, mara mlango ukaanza kugongwa kwa nguvu nje, nikasikia kibao kingine kikitua kwenye shavu la upande wa pili, likafuatiwa na misonyo mingi kisha wale watu wakayeyuka wote na kupotea kama moshi upoteavyo angani.
“Togo! Nini kimetokea?” alisema baba baada ya kuwa amefanikiwa kufungua mlango na kuwasha taa. Jambo la aibu ni kwamba baada ya ule mchezo wa kikubwa niliocheza na Rahma, hakuna aliyekumbuka tena kuvaa nguo zake kwa hiyo nilikuwa kama nilivyozaliwa, baba akanitazama kwa mshangao.
Najua alishangazwa na mambo mengi kwa wakati mmoja, kwanza kwa nini nilikuwa chumbani kwa Rahma mpaka usiku huo wakati makubaliano yalikuwa ni kwamba kila mmoja atalala kwake, kwa maana kwamba baada ya c hakula ilitakiwa mimi nitoke na kwenda kwenye chumba nilichopangiwa lakini sikufanya hivyo. Yote tisa, kumi ni kwamba nilikuwa kama nilivyozaliwa, na Rahma naye ambaye bado alikuwa kwenye usingizi mzito, akikoroma bila kujua chochote kilichokuwa kinaendelea, hakuwa na chochote mwilini, nikamuona baba akishusha pumzi ndefu na kunipa ishara kwamba nivae kwanza nguo, akatoka na kuurudisha mlango.
*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
Kumbe sekeseke hilo lilisababisha nitokwe na haja ndogo bila kujua, ikabidi nichukue tambara la kufanyia usafi na kufuta harakaharaka huku nikigeuka kumtazama Rahma asije kuwa ameamka na kuona nilichokifanya. Nilipomaliza kufuta, harakaharaka nilivaa nguo zangu huku nikitetemeka kuliko kawaida.
Baba alikuwa pale mlangoni akinisubiri, nilipomaliza aliingia na kunionesha ishara kwamba nisizungumze kwa sauti ya juu, akaniuliza nini kilichotokea.
“Wachawi baba, wachawi wengi wamekuja, angalia walivyonifanya,” nilisema huku nikimuonesha mashavu yangu ambayo nilikuwa nahisi kama yanawaka moto. Awali niliona baba hataki kuamini kama ambavyo imekuwa kawaida yake mara kwa mara ninapotokewa na mambo kama hayo lakini nashukuru safari hii kulikuwa na ushahidi wa moja kwa moja.
“Mungu wangu, umefanya nini?”
“Wamenipiga,” nilisema huku nikianza kutokwa na machozi.
“Hebu niambie ukweli, umefanya tena mapenzi na Rahma?”
“Ndiyo.”
“Lakini si tumeshawakataza nyie na kuwasisitiza kwamba msirudie ujinga wenu?” baba alizungumza kwa hasira lakini kwa sauti ya chini. Sikujua kwa nini alikuwa akizungumza kwa sauti ya chini, akanishika mkono na kufungua mlango, akatazama huku na kule na alipojiridhisha, alinipeleka mpaka kwenye chumba ambacho ndicho nilichotakiwa kulala.
“Hutakiwi kumwambia yeyote kuhusu hiki kilichotokea, umenielewa?” baba aliniambia, nikatingisha kichwa lakini nilijiuliza, kama yeye ameweza kusikia zile kelele nilizopiga, si ina maana nyumba nzima wamesikia? Na kama wamesikia, kwa nini wengine wote hawakuamka isipokuwa yeye tu?
“Lakini kwa nini haya yanatokea?” utajua tu lakini unachoniudhi ni kwamba ukiambiwa jambo fulani usilifanye, wewe ndiyo unalifanya. Hukuwa na mambo ya wanawake kabisa lakini tangu tumefika hapa ndiyo umekuwa mchezo wako… utasababisha vifo vya wasio na hatia kwa nini unakuwa mgumu kuelewa?” baba alisema, safari hii siyo kwa ukali bali kwa hisia za ndano kabisa, kauli yake ikanishtua mno.
Yaani mimi ndiyo nisababishe vifo vya wasio na hatia? Kivipi? Halafu kulikuwa na uhusiano gani wa mimi kulala na Rahma na hayo yaliyokuwa yanatokea? Katika yote, jambo ambalo nilijiapiza, ni kwamba kamwe sitamuacha Rahma maana alikuwa amenionesha dunia ya tofauti mno.
Baba alitoa kichupa kilichokuwa na unga mweusi lakini kabla hajafanya chochote, aliniambia nikajitazame kwenye kioo kilichokuwa humo chumbani.
“Mungu wangu,” nilisema kwa mshtuko usio wa kawaida.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue
 
SEHEMU YA 28



ILIPOISHIA:
Nikiwa bado naendelea kuugulia, nilisikia ndugu yangu mmoja akiniita kutokea dirishani, nikafunua pazia na kuchungulia nje. Sikuyaamini macho yangu baada ya kumuona akiwa na yule msichana tuliyesafiri naye, harakaharaka nikafungua dirisha huku tabasamu pana likiwa limechanua kwenye uso wangu.
SASA ENDELEA…
“Mambo Togo?”
“Safi, karibu,” nilisema huku nikitazama huku nakule. Yule ndugu yangu alikuwa amesimama pembeni akikutazama kwa zamuzamu.
“Samahani nina maongezi kidogo na wewe,” alisema. Kwa hali niliyokuwa nayo, nilikuwa nikifikiria jambo moja tu kutokakwake, mapenzi.
“Nisubiri kwa kule mbele,” nilimuelekeza huku harakaharaka nikitoka na kuelekea bafuni. Nilijimwagia maji ya baridi kwa wingi ili angalau nitulie kisha nikarudi chumbani na kuvaa nguo.
Nilijitazama tena kwenye kioo, bado nilikuwa na alama za kuvilia damu usoni lakini sikujali, akili yangu ilikuwa ikihitaji kitu kimoja tu kwa wakati huo. Nilitoka kimyakimya bila kumuaga mtu yeyote mpaka nje.
Nikamfuata yule ndugu yangu na kumwambia kwamba iwe siri yetu nitampa zawadi, nikamsisitiza kwamba asimwambie mtu yeyote. Alikubali, nikamshukuru nakumfuata yule msichana ambaye alionesha kuwa na shauku kubwa ya kuonana na mimi.
Tulitoka mpaka nje kabisa, sehemu ambayo mtu yeyote aliyekuwa ndani asingeweza kutuona, akanikumbatia kwa nguvu na kunibusu shingoni. Nilijikuta nikisisimka mno, nikawa nachekacheka tu mwenyewe.
Aliniambia kuna mahali anataka rtwende pamoja kwa sababu alikuwa na jambo muhimu lililokuwa likimsumbua ndani ya moyo wake. Nilimuuliza amepata wapi ujasiri wa kuingia mpaka kule ndani? Akaniambia ilikuwa ni muhimu sana kuonana na mimi na ndiyo maana hakujali chochote.
“Huwa unakunywa pombe?” aliniuliza, nikatingisha kichwa kumkatalia. Licha ya kujaribu mara kadhaa kunywa pombe za kienyeji tukiwa Chunya, kiukweli kichwa changu kilikuwa kibovu sana, kiufupi sikuwa na uwezo wa kuhimili pombe. Akacheka sana huku mara kwa mara akinipigapiga begani.
*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
“Chagua sehemu ambayo unadhani inaweza kufaa kwa mazungumzo ya mimi na wewe, twende beach, Mlimani City au tutafute ‘lodge’ yoyote nzuri,” aliniuliza l;akini kati ya sehemu zote alizozitaja, ni moja tu ndiyo niliyokuwa naelewa, beach. Sikuwa najua Mlimani City ndiyo wapi na kupoje wala sikuwa najua huko ‘lodge’ ni wapi na kuna nini cha muhimu. Waliosema ushamba mzigo, hawakukosea.
Ilibidi nimuulize ili anipe ufafanuzi, akacheka sana, akaniambia Mlimani City ni kituo maalum cha kibiashara, mahali ambapo kuna maduka makubwa, mabenki, migahawa ya kisasa ya sehemu mbalimbali za starehe. Akaniambia pia kuwa neno lodge ni la Kiingereza lakini linamaanisha nyumba ya kulala wageni. Nikashtuka!
“Unamaanisha gesti?”
“Ndiyo?” alinijibu huku akinitazama kwa macho yake mazuri, ikabidi nijifanye sitaki nataka kwa sababu kule kwetu kulikuwa na stori kwamba watu wanaoingia gesti wakati hawapo safarini ni wale wahuni walioshindikana. Nikamwambia kwamba Mlimani City atanipeleka siku nyingine, akanitazama tena usoni na kuachia tabasamu pana.
Japo jibu langu halikuwa la moja kwa moja, nadhani alinielewa haraka nilikuwa namaanisha nini. Tuliingia kwenye Bajaj, nikageuka huku na kule na nilipohakikisha hakuna aliyeniona, nilimpa ishara kwamba tuondoke.
Kwa makusudi kabisa, aliniegamia kimahaba huku mara kwa mara akiendelea kuniangushia mabusu ya hapa na pale. Yaani kama angekuwa anajua kilichokuwa ndani ya kichwa changu, kamwe asingethubutu kumwagia petroli kwenye moto.
Hatukwenda mbali sana, Bajaj ikaingia kwenye jengo moja la kisasa, getini likiwa na maandishi yaliyosomeka Sideview Hotel, tukashuka kwenye Bajaj, nikawa nashangaashangaa huku na kule, alinishika mkono bila hata wasiwasi, tukaingia mpaka ndani ambapo alimfuata dada wa mapokezi na kuanza kuzungumza naye.
Alimwambia anahitaji chumba kwa siku nzima mpaka kesho yake. Nilishangaa kwa nini anataka tukae mpaka kesho yake wakati anajua mimi ni mgeni na nilikuwa chini ya wazazi wangu. Hata hivyo, sikutaka kumhoji chochote mpaka nipate nilichokuwa nakitaka.
Alitoa pochi yake na kuhesabu fedha, akampa yule mhudumu, akatoka na funguo na kwenda kutuonesha chumba chenyewe. Kilikuwa chumba kizuri mno, yaani pengine kuliko vyumba vya kwenye majumba ya watu wengi sana. Picha niliyokuwa nimeijenga kichwani mwangu mwanzoni, nilitegemea chumba kitakuwa kama vile vya gesti za kijiji, kitanda kidogo chenye kunguni na kilicholegea, godoro chafu na jembamba sambamba na mashuka makuukuu.
*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
Kitanda kilikuwa kikubwa, juu yake kikiwa kimetandikwa kwa mashuka meupe na mito mikubwa mizuri, chini kikiwa kimepigwa marumaru safi nyeupe, huku taa zenye mwanga fulani mzuri zikizidi kuyapendezesha mandhari ya chumba hicho, nikawa nashangaashangaa.
Sikuwa na habari kwamba mwenzangu bila hata kuzungumza kile alichosema tunataka kuzungumza, ameshaanza kufaanya kazi nyingine. Alikuwa tayari ameshavua blauzi yake na kubaki na bra, akawa anahaha kufungua suruali yake iliyokuwa imembanana kulichora vilivyo umbo lake. Nilijikuta nikitetemeka mwenyewe, hata sijui ni kwa nini, nikampa mgongo.
“Togo! Mimi mwenzio na…ku..pe…” alishindwa kumalizia alichotaka kukisema, akagusanisha mdomo wake na wangu huku mikono yake ikiwa imenibana kisawasawa kwenye kifua chake kilichosheheni. Kwa kuwa rahma alikuwa amenipa ‘twisheni’ ya mambo hayo, na mimi sikutaka kubaki nyuma, nilimpa ushirikiano, tukawa tunaelea kwenye ulimwengu tofauti kabisa.
Ile halai niliyokuwa naisikia mwanzo, safari hii ilizidi mno, yaani nikawa naona kama nachelewa. Tofauti na Rahma, huyu yeye hakuwa na aibu kabisa na kila alichokuwa anakifanya, alikuwa akifanya kwa kujiamini. Akaninyonyoa manyoya yote kama kuku aliyechinjwa huku na yeye akifanya hivyohivyo, muda mfupi baadaye, tukawa ‘saresare’ maua.
“Togoo!” aliniita kwa mshtuko huku akiwa amepigwa na butwaa iliyochanganyikana na furaha.
“Kumbe upo hivi,” alisema huku akinitazama kwa macho yake kama anasikia usingizi, sikuelewa kauli yake hiyo ilikuwa ikimaanisha nini, lakini aliendelea kunimwagia sifa lukuki kwamba siku ya kwanza aliponiona tu aligundua kwamba nina sifa za kipekee ambazo wanaume wengine hawana.
Sikutilia sana maanani kile alichokuwa anakisema, akili yangu ilikuwa ikiwaza jambo moja tu. Muda mfupi baadaye, tuliianza safari huku mimi nikiwa ndiyo kiongozi wa msafara. Unajua kama una kiu kali ya maji, hata ukipewa jagi zima unaweza kulifakamia lote mpaka liishe. Hicho ndicho kilichotokea kwangu.
Ghafla nilishangaa akianza kugeuza macho na kutupatupa mikono na miguu kama mtu anayetaka kukata roho, haraka nikashuka chini na kuanza kumtingisha kwa nguvu huku nikishindwa hata namna ya kumuita maana kiukweli sikuwa nalijua jina lake.
Kadiri nilivyokuwa namtingisha ndivyo alivyozidi kulegea, mara akatulia huku macho yake yakiwa yamegeuka na kutazama upande wa juu. Nilijaribu kusikiliza mapigo ya moyo wake lakini hayakuwa yakipiga na hakuwa akipumua.
“Mungu wangu,” nilisema huku nikianza kutafuta nguo zangu, harakaharaka nikavaa huku kijasho chembamba kikinitoka, nikawa najiuliza nini cha kufanya maana tayari ulishakuwa msala. Hakuna ambaye angeamini kwamba msichana huyo amekufa mwenyewe, wangejua kwamba nimemuua, nilijikuta nikitetemeka mno.
Akili niliyoipata, ilikuwa ni kuondoka haraka hotelini hapo bila mtu yeyote kujua. Nilichukua shuka na kumfunika kisha nikafungua mlango. Nilitazama huku na kule, nilipoona hakuna mtu, nilitoka na kuurudishia mlango, harakaharaka nikawa natembea kuelekea nje.
Kwa bahati nzuri, nilipofika pale mapokezi, yule dada hakuwepo, nikatoka kimyakimya mpaka nje, nikaelekea lilipo geti kubwa huku nikijitahidi kuvaa tabasamu la uongo ili walinzi wa hoteli hiyo wasishtukie chochote.
“Aroo! We kijana… Aroo wewe,” nilisikia sauti ya mlinzi wa nje ya geti la hoteli hiyo akiniita, moyo ukalipuka paah!
Je, nini kitafuatia
 
SEHEMU YA 29:



ILIPOISHIA:
Kwa bahati nzuri, nilipofika pale mapokezi, yule dada hakuwepo, nikatoka kimyakimya mpaka nje, nikaelekea lilipo geti kubwa huku nikijitahidi kuvaa tabasamu la uongo ili walinzi wa hoteli hiyo wasishtukie chochote.
“Aroo! We kijana… Aroo wewe,” nilisikia sauti ya mlinzi wa nje ya geti la hoteli hiyo akiniita, moyo ukalipuka paah!
SASA ENDELEA…
“Unaenda wapi?”
“Naenda dukani afande.”
“Mwenzako umemuacha wapi?”
“Yupo ndani, narudi sasa hivi, naenda kununua kinga.”
“Mbona kama una wasiwasi?” alisema yule mlinzi huku akinisogelea. Licha ya kujaribu kucheza na akili zake, ni kama alishashtukia jambo kwa jinsi nilivyokuwa na hofu. Mtu kukufia chumbani, usifanye mchezo.
Hata kama ulikuwa jasiri vipi, lazima uchanganyikiwe. Hicho ndicho kilichonitokea. Hofu ilishindwa kujificha kwenye macho yangu, nikawa nakwepesha macho kwa sababu niliamini yule mlinzi kwa jinsi alivyonishupalia, angeweza kugundua kitu. Nilitamani kufanya kitu lakini sikuwa na uwezo, harufu ya jela ikaanza kunukia.
“Mkazie macho usoni,” ile sauti ya ajabu ya baba, ilisikika masikioni mwangu, nikageuka huku na kule lakini baba hakuwepo eneo hilo. Kwa kuwa mara zote ilikuwa ikinisaidia, nilifanya kama nilivyoelezwa.
Nilimkazia macho yule mlinzi, na yeye akanitazama. Ghafla nikashangaa anakuwa mpole ghafla, mwanzo alikuwa amekunja sura lakini ghafla alitabasamu. Niliendelea kumkazia macho.
‘Haya nenda, unajua siku hizi kumekuwa na matukio ya ajabu sana kwenye hizi nyumba za kulala wageni kwa hiyo lazima tuwe makini,” alisema huku akichekacheka, akageuka na kurudi getini. Sikuamini kilichotokea.
Kwa tafsiri nyepesi, baba alikuwa anaona kila kinachoendelea kwa sababu asingeweza kuniambia maneno yale tena katika muda muafaka kabisa. Hofu yangu ilikuwa ni je, anajua nilichokifanya kule gesti? Mara kwa mara alikuwa akinikanya lakini kwa ubishi wangu nikaona kama ananibania nisifaidi.
Sikuwa nalijua Jiji la Dar es Salaam wala sikuwa najua ramani ya kunifikisha nyumbani, kitu pekee nilichokumbuka, ni barabara ile tuliyojua, nikawa natembea harakaharaka huku nikitamani kama ningekuwa na uwezo ningepaa kabisa na kutoweka eneo hilo.
Nilinyoosha na barabara na nilipofika mbali, nilianza kukimbia, hofu kubwa ikiwa imetanda kwenye moyo wangu. Kwa bahati mbaya zaidi, sikuwa nakumbuka sehemu ambayo tulikatia kona na kutokezea kwenye barabara hiyo, nikajikuta nikipoteza uelekeo, nikawa nazunguka huku na kule, kijasho chembamba kikinitoka.
Sikuwa na fedha mfukoni kwamba ningezitumia kukodi bodaboda na kuwaelekeza nyumbani. Nikiwa naendelea kuumiza kichwa, hatimaye nilipata akili mpya. Pale nyumbani, kwa nje kulikuwa na kituo cha madereva wa Bajaj na nimewahi kusikia kwamba wenyewe wana umoja wao na wanajiita City Boys wakimaanisha watoto wa mjini.
Kuna Bajaj ilikuwa ikija mbele yangu, nikaipiga mkono, ikapunguza mwendo na hatimaye ikasimama. Nilimfuata dereva na ikabidi niwe mkweli kwake, nikamwambia kwamba nimepotea na ramani pekee iliyopo kichwani mwangu, ni kituo cha Bajaj cha City Boys.
Alicheka kisha akaniambia niingie kwenye Bajaj yake, nikamtahadharisha kwamba sikuwa na fedha, akaniambia atanisaidia.
“Wewe si unakaa pale kwa akina Rahma, mbona mimi nakujua,” alisema yule kijana kwa uchangamfu, nikamshukuru Mungu wangu na kuelewa kwa nini alicheka nilipomueleza kwamba nimepotea.
‘Mimi nakusaidia lakini na wewe nataka unisaidie jambo, unajua mi nampenda sana yule dada Rahma ila naogopa kumwambia ukweli maana muda wote yupo ‘sirias’, nataka unisaidie kufikisha ujumbe, mwambie Zedi dereva teksi, ukifanikisha ntakuwa nakuja kukuchukua nakutembeza viwanja mbalimbali na Bajaj, hata ukitaka pesa ntakuwa nakutoa,” aliniambia yule dereva Bajaj.
Kwa kuwa nilikuwa na shida kwa wakati huo, nilimkubalia kila alichokuwa anakisema. Hakuwa akijua kwamba mimi ndiye mmiliki wa Rahma. Kumbe sikuwa mbali sana na nyumbani, muda mfupi baadaye tukawa tumeshafika, akanishusha getini na kunisisitiza kuhusu ombi lake, nikazidi kumdanganya kwamba asiwe na wasiwasi.
Niliposhuka niliingia moja kwa moja ndani huku bado hofu kubwa ikiwa imetanda kwenye moyo wangu.
“Ulikuwa wapi?” mama aliniuliza kwa ukali mara tu nilipofika sebuleni. Nikakosa cha kujibu kwa muda, nikawa najiumauma, baadaye nikamwambia kwamba kuna rafiki yangu nilikuwa nimemsindikiza.
“Rafiki? Rafiki gani? Una rafiki hapa mjini wewe?” mama alinihoji huku akionesha kutokuwa na hata chembe ya masihara. Ilibidi ninyamaze kimya, nikataka nipitilize kwenda chumbani lakini aliniambia nataakiwa kukaa nao hapohapo sebuleni kwa sababu ninapopewa muda wa kuwa huru nashindwa kuutumia uhuru wangu vizuri.
Huo ulikuwa mtihani mkubwa sana kwangu, ikabidi nimwambie mama kwamba bado sijisikii vizuri, akaniambia nitakapotoka tena bila ruhusa yake au bila kuaga, atanisemea kwa baba aninyooshe. Nilifurahi kwa sababu aliniruhusu niende chumbani kwangu.
Nilipoingia tu, nilijifungia kwa ndani, nikakaa kwenye ukingo wa kitanda na kujiinamia, maswali mengi yakiendelea kupita ndani ya kichwa changu. Sikuwa najua nini itakuwa hatima yangu endapo ukweli utafahamika. Hata hivyo, kwa upande mwingine, nilianza kujiuliza mimi kosa langu ni nini kwa sababu, yeye ndiye aliyenifuata hadi nyumbani na ndugu yangu alikuwa shahidi.
Yeye ndiye aliyenishawishi twende kwenye nyumba ya kulala wageni na hata tulipofika, alionesha wazi kwamba alikuwa akinihitaji na kwa vile na mimi nilikuwa kwenye hali mbaya, tulijikuta tukiangua dhambini.
Nilijaribu kujiuliza kwamba labda kuna kitu kisicho cha kawaida nilimfanyia mpaka yakatokea ya kutokea lakini sikukumbuka chochote. Bado niliendelea kujiuliza maswali mengi yasiyo na majibu.
Nikiwa nimejifungia chumbani, mara nilianza kusikia kelele sebuleni, ndugu zangu wakawa wananiita nikaangalie. Ilibidi nitoke na kwenda mpaka sebuleni. Habari za dharura au Breaking News kama wengi walivyozoea kuita, zilikuwa zikioneshwa runingani moja kwa moja kutoka eneo la tukio.
Zilikuwa ni habari za samaki hatari aina ya papa kuvamia kwenye ufukwe wa bahari ya Hindi na kusababisha vifo vya watu kadhaa, wakiwemo wavuvi na wengine waliokuwa wakiogelea ufukweni huku wengine kadhaa wakijeruhiwa. Nilijikuta moyo wangu ukilipuka kuliko kawaida.
Kilichonishtua ni kwamba, mazingira ya tukio lile, yalikuwa sawa kabisa na kile kilichonitokea nilipoenda ufukweni na Rahma.
Habari zilieleza kwamba wavuvi walaikuwa kwenye boti yao wakivuta nyavu lakini ghafla, samaki huyo aliwashambulia kwa kuvunjavunja boti yao na kuanza kuwala, mmoja baada ya mwingine, hali iliyosababisah maji ya bahari yageuke rangi na kuwa mekundu.
Yaani kilekile nilichokieleza na kila mmoja kuniona kama mwendawazimu, ndicho kilichokuwa kimetokea, taarifa ya habari iliendelea kueleza kwamba polisi na vikosi vya uokoaji, wamefika eneo la tukio na wanahangaika kupambana na samaki huyo mkubwa.
Baada ya habari hiyo kuisha, watu wote pale sebuleni walinigeukia na kunitazama kwa mshangao uliochanganyikana na hofu. Tukiwa bado tunatazamana, mara baba aliingia getini akiwa ameongozana na baba yake Rahma na askari watatu waliokuwa na silaha. Nikajua mwisho wangu umefika, nilishindwa cha kufanya, nikabaki nimesimama palepale, nikitetemeka kuliko kawaida.
Je, nini kitafuatia? Usikose J
 
SEHEMU YA 30:



ILIPOISHIA:
Nikiwa bado naendelea kumtazama kwa jicho baya, mara nilishtuka kusikia vishindo viwili vikubwa juu ya bati, kama vile nilivyokuwa navisikia usiku uliopita, moyo wangu ukapatwa na mshtuko mkubwa mno. Mara nilisikia vishindo vingine vitatu mfululizo, nikawa nimepigwa na butwaa huku macho yangu yote yakiwa juu.
SASA ENDELEA…
Kwa jinsi vishindo hivyo vilivyokuwa vikisikika, ilikuwa ni kama kuna watu wanaruka kutoka angani na kudondokea juu ya bati kwani vilikuwa vizito mno. Safari hii nilitaka kuwa makini kushuhudia je, kile ninachokisikia mimi, kila mtu anasikia hivyohivyo maana nilishahisi kuna kitu hakipo sawa kwangu lakini baba hataki kuniambia ukweli.
Baada ya vishindo vile vya kama watu au vitu kutua juu ya bati, mara vilianza kusikika vishindo vya mtu akitembea juu ya bati.
Unajua haya matukio kama hujawahi kutokewa nayo, huwezi kuelewa ile hofu unayokuwa nayo lakini kiukweli, ni bora tu uwe unasikia lakini yasikutokee. Hakuna hofu inayotesa kama hofu ya matukio kama haya yanapokutokea, hasa usiku kama huo.
Nilijikuta nywele zikisisimka vibaya mno, mapigo ya moyo yakawa yananienda kwa kasi maana sikujua safari hii wanakuja kwa mtindo gani. Vishindo viliendelea kusikika kisha kikasikika kishindo kingine ambacho kwa makadirio yangu ya haraka, kilikuwa ni kwenye sakafu ya mle mahabusu.
Nilishindwa kuelewa, inawezekanaje usikie mtu anatembea juu ya bati, tena kwa nje halafu muda mfupi baadaye umsikie akirukia na kudondokea kwa ndani, tena jirani kabisa na pale ulipo! Inatisha sana.
“Humu ndani kuna wanga eeh! Mbona nywele zinanisisimka? Sasa ole wake mtu aniguse,” mmoja kati ya wale mahabusu tuliokuwa nao mle ndani, aliyekuwa amekaa kwenye kona nyingine, alisikika akiongea kilevilevi, akawa anaporomosha matusi mazitomazito.
Kitendo kile kilinifanya niamini kwamba hatimaye sasa sikuwa peke yangu ambaye nilikuwa nikishuhudia mchezo uliokuwa ukiendelea. Niliamini hivyo kwa sababu kwenye kona aliyokuwa amekaa yule mahabusu ambaye alikuwa akiendelea kutukana, ndiko ambapo makadirio yangu yalinionesha kwamba yule mtu aliyekuwa akitembea juu ya bati alidondokea palepale.
*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
Matusi aliyokuwa akitukana, yalisababisha mahabusu wengine ambao bado hawakuwa wamelala, waanze kucheka kwa nguvu na kumtania kwamba amelewa lakini kelele zote zilizimika ghafla bila mtu yeyote kutoa amri, ikatokea tu kwamba watu wote wapo kimya.
Katika ukimya huo, ulisikika msonyo mkali ambao japokuwa wale mahabusu wengine waliamini kwamba umetolewa na yule mahabusu aliyekuwa akitoa matusi mazito kwa wale aliowaita wanga, mimi nililitazama tukio hilo katika sura nyingine tofauti.
Haikuwa mara ya kwanza kusikia msonyo wa namna hiyo ingawa safari hii ulionekana kutoka kwa mtu tofauti ambaye sijawahi kuisikia sauti yake. Unajua kuna watu wamezaliwa wakiwa na uwezo fulani wa kipekee, sijui niuiteje lakini kwa kifupi mtu anakuwa na uwezo wa kufikiri na kuyaona mambo kwa utofauti na wengine.
Yaani kuna baadhi ya watu, nyie wengine wote mnaweza kuamini kwa mfano ajali iliyotokea barabarani imesababishwa na uzembe wa dereva kukimbia kwa mwendo kasi akiwa hajafunga mkanda, lakini mtu mwingine hapohapo akalitazama tukio na kutoa jibu tofauti kabisa ambalo pengine halikutegemewa.
Baba amewahi kunifundisha kwamba japokuwa watu wa namna hii huwa wanachekwa au kuzomewa na kuonekana wanaishi kwenye ulimwengu wa ndoto, lakini wao ndiyo huwa sahihi kwa sababu wanautazama ulimwengu kwa jicho tofauti na watu wengine wote.
Ndicho kilichotokea mle mahabusu, wakati watu wote wakilichukulia tukio la yule mahabusu kudai kule ndani kuna wachawi kisha akaanza kuporomosha matusi, wengi walimuona kama mlevi tu lakini mimi nilimtazama kwa jicho tofauti.
Hata uliposikika ule msonyo na watu kuanza kumtuhumu kwamba anawavurugia usingizi wao, mimi nilikuwa nikiamini kwamba hakuutoa yeye na alichokuwa akikisema kwamba mle ndani kulikuwa na wanga, ulikuwa ni ukweli mtupu.
“Sikilizeni, sikilizeni,” alisema yule mahabusu, kwa msaada wa mwanga hafifu uliokuwa ukipenya kutokea nje, nilimuona akiinua kichwa chake juu kutazama darini, lakini kelele za mahabusu wengine zikamfanya ashindwe kusikia alichokuwa akitaka kukisikia.
“Au naye ana nguvu kama mimi?” nilijiuliza kwa sababu wakati akiwataka watu wote watulie ili wasikie, ni kweli juu ya bati kuna mtu alikuwa akitembea kwa vishindo kabisa kisha naye akasikika akidondokea ndani ya ile mahabusu.
*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
Baada ya hapo, vilianza kusikika vishindo vya watu wakirukia mle mahabusu mfululizo, nikawa natetemeka nikiwa sijui nini kitatokea maana kama unavyojua, milango ya mahabusu huwa muda wote imefungwa na haiwezekani ikafunguliwa kwa muda ule. Nilichokuwa nakiomba, ni wachawi hao wasije wakawa wamekuja kwa shari kama ilivyotokea kwangu na safari hii, nilijifunza kuufyata mkia, sikutaka kuzungumza chochote zaidi ya kuzidi kukodoa macho yangu gizani kama nitaona kitu chochote.
Nilishangaa mfuko wa suruali yangu ukianza kutetemeka kama ndani kulikuwa na kitu ‘kinacho-vaibreti’, sikukumbuka kama niliweka kitu chochote mfukoni na hata kama ni simu, wala sikuwa nikimiliki baada ya baba kunipokonya ile niliyopewa na yule dada ambaye ndiye aliyesababisha muda huo nikawa nyuma ya nondo.
Kwa hofu kubwa niliingiza mkono mfukoni huku nikiwa bado nimekodoa macho, nikagundua kwamba kulikuwa na kitu kwenye mfuko wangu ambacho sikuwa najua ni kitu gani.
Mbaya zaidi, sikujua ni nani aliyekiweka kwenye mfuko wa nguo yangu kwa sababu wakati naingizwa na wale askari, waliniambia pale kaunta nitoe kitu chochote nilichokuwa nacho mfukoni na wala sikuhitaji kujisachi kwa sababu nilikuwa najua sina chochote.
Cha ajabu, nilipokigusa kitu hicho tu, kiliacha kutetemeka lakini yote tisa, kumi ni kwamba nilianza kuona vitu vya ajabu mno. Japokuwa mle ndani kulikuwa na giza, niliweza kuwaona watu wote vizuri, mpaka sura zao utafikiri ilikuwa mchana, ila tofauti yake ni kwamba hakukuwa na mwanga wenye uangavu kama wa mchana bali ulifanana kwa mbali na nuru ya mbalamwezi.
Kwa wale tuliokulia vijijini nadhani wanaelewa vizuri usiku wa mbalamwezi unavyokuwa, yaani unaweza kusema ni mchana kabisa kwani vitu vyote vinaonekana japo siyo vizuri kama vile nilivyokuwa naona mimi.
Nilianza kuwatazama mahabusu wenzangu mmoja baada ya mwingine maana kama unavyojua, niliingizwa giza likiwa limeshaingia na kwa sababu mle ndani hakukuwa na taa, watu pekee niliowaona vizuri ni wale waliokuwa jirani na mimi.
Cha ajabu, wakati nikiendelea kuwatazama mahabusu hao ambao wengi walishaanza kusinzia kutokana na uchovu, niligundua kwamba kulikuwa na watu wengine wasio wa kawaida mle ndani, nao wakiwa wamejichanganya na mahabusu lakini tofauti yao ilikuwa moja.
Karibu wote walikuwa na macho mekundu sana na walikuwa wakinitazama kama wanaosubiri kuona nitafanya nini lakini kubwa, wote walikuwa watupu kabisa. Nilipopiga jicho harakaharaka na kujaribu kuwahesabu, walikuwa kama saba hivi, tena wengine wawili walikuwa ni wanawake na kama unavyojua mahabusu huwa hawachanganywi wanawake na wanaume.
Wote waliacha kila walichokuwa wanakifanya, wakawa wananitazama kwa macho makali. Sikuelewa nini hasa kimetokea, wakati nikiendelea kuwatazama vizuri kwa mara ya pili, kuna jambo moja lilinishtua mno mpaka nikajikuta nimetoa mkono mfukoni, giza likarudi kama lilivyokuwa mwanzo.
Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 31:


ILIPOISHIA:
Wote waliacha kila walichokuwa wanakifanya, wakawa wananitazama kwa macho makali. Sikuelewa nini hasa kimetokea, wakati nikiendelea kuwatazama vizuri kwa mara ya pili, kuna jambo moja lilinishtua mno mpaka nikajikuta nimetoa mkono mfukoni, giza likarudi kama lilivyokuwa mwanzo.
SASA ENDELEA…
Japokuwa kulikuwa na giza, niliweza kuonamacho ya wale watu yaking’ara kama wanyama wakali wa porini, nikawa najilaumu kwa kile nilichokifanya. Hata sijui nini kilitokea kwani kuanzia mwanzo nilikuwa nimejiapiza kwamba siku hiyo sitaleta ujuaji wowote mbele ya watu hao lakini cha ajabu, ndani ya muda mfupi tu, tayari nilishakuwa nimewekwa mtu kati.
Sikujua safari hii wataniadhibu vipi lakini niliamua kupiga moyo konde, liwalo na liwe. Bado nilikuwa najiuliza maswali mengi kuhusu kile kilichokuwa kwenye mfuko wangu, sikujua ni nini na kilikuwa na uhusiano gani na ule mwanga uliotokeza ghafla mle ndani ya mahabusu.
Sijui nilipata wapi ujasiri lakini nilijikuta nikiingiza tena mkono taratibu mfukoni, nilipokigusa tu kile kitu mle mfukoni, ule mwanga ulirudi tena vilevile, wale watu ambao safari hii walikuwa wamejikusanya na kutengeneza kama nusu duara hivi, waliinua wote shingo zao na kunigeukia tena, nikakishika kile kitu kwa nguvu huku na mimi nikiwa nawatazama.
*Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Katika hali ambayo sikuitegemea, nilishangaa wa kwanza akisimama na kukimbilia kwenye ile kona alipokuwa amekaa yule mahabusu ambaye awali alikuwa akipiga kelele. Safari hii alikuwa amelala, tena kwa kuinamisha kichwa mbele, katikati ya miguu yake.
Nikamuona yule mtu wa kwanza, mikono yake akiwa amejiziba sehemu nyeti, akisogea mpaka kwenye kona, alipoikaribia, aligeuka na kuanza kutembea kinyumenyume, akamkanyaga yule mahabusu kisha nikashangaa akipotelea kwenye ukuta.
Ni hapo ndipo nilipoamini yale maneno niliyowahi kuyasikia kwamba wachawi wanao uwezo wa kuingia na kutoka ndani ya nyumba hata kama milango imefungwa. Nilishindwa kuelewa ni nini hasa kilichofanya iwezekane kwa yule mtu kupotelea kwenye ukuta.
Nikiwa bado nimepigwa na butwaa, nilimuona mwingine naye akiinuka, akaanza kutembea kuelekea kwenye ile kona, wengine nao wakasimama, wakawa wanatembea huku wote wakiwa wananitazama kwa macho mabaya. Ni kama nilikuwa nimewavurugia mipango yao, nikazidi kukishikilia kile kitu mfukoni.
“Hiyo ndiyo nafasi yako ya kutoka mahabusu, hakikisha unamshika mmoja kati yao na kumvua usinga aliovaa shingoni kisha na wewe utatoka kama hao wengine walivyotoka,” nilisikia sauti masikioni mwangu ambayo niliitambua vizuri kwamba ni ya baba.
Bado sikuwa nimeelewa ni mbinu gani anayoitumia baba kuwasiliana na mimi kwa sauti ambayo hakuna mtu mwingine yeyote anayeisikia. Hata hivyo, sikutaka sana kuhoji, nilichokifanyailikuwa ni kufuata maelekezo.
Cha ajabu, wale watu walipoona nawafuata, walianza kukimbia lakini kwa sababu ya nafasi ndogo iliyokuwepo, walishindwa kutoka wote kwa mkupuo, nikafanikiwa kumkamata mmoja ambapo moja kwa moja nilipeleka mkono shingoni ambapo alikuwa amevaa kitu kama kamba nyembamba lakini iliyosokotwa kwa nywele, ikakatika na kubaki mkononi mwangu.
Kitendo hicho kilisababisha alie kwa sauti kubwa lakini cha ajabu sasa, sauti yake ilitoka kama zile sauti zinazotolewa na mapaka yanayolia usiku, akadondoka chini na kuendelea kulia kwa sauti kubwa kama paka.
*Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Cha ajabu, wakati nikiwa nimeshageuka na kuupa mgongo ukuta, tayari kwa kufanya kile baba alichoniambia nikifanye, yule mtu aliinua uso wake huku akionesha ishara kwamba nimsamehe. Kilichonishtua ni kwamba sura yake ilikuwa ikifanana na mimi kwa kila kitu wakati awali hakuwa vile.
Nikiwa bado naendelea kumshangaa, nilisikia sauti ya baba ikinisisitiza kutoka haraka. Sikuwa nimewahi kushiriki uchawi mkubwa kiasi hicho, nikawa natetemeka nikiwa siamini kama kweli naweza kupita ukutani. Nilipiga hatua kurudi nyuma mpaka nilipoufikia ukuta.
Cha ajabu, nilipouegamia ulilainika kama pazia, nikapiga hatua nyingine na kujikuta nusu ya mwili wangu tayari ipo nje, nikapiga hatua nyingine, nikawa nimetoka nje kabisa. Nilibaki nimesimama kwenye maua yaliyopandwa pembezoni mwa ile mahabusu nikiwa bado siamini.
Niligeuka na kutazama huku na kule, hakukuwa na mtu yeyote eneo hilo, harakaharaka nikatembea na kupotelea kwenye kota za askari wa kituo kile, nikawa nazidi kutembea nikiwa sielewi naelekea wapi. Nilizimaliza kota hizo, kwa mbali nikawa nawasikia mbwa wakibweka, nikaongeza mwendo na muda mfupi baadaye, nilitokeza kwenye barabara ya lami.
Siwezi kuficha jinsi nilivyofurahi kutoka mle mahabusu. Hapohapo nikajikuta eti na mimi nikitamani kuwa mchawi ili nipate nafasi ya kufaidi mambo mengi kwenye hii dunia ambayo binadamu wa kawaida hawawezi.
Hebu vuta picha, hata kama ni wewe, yaani ndugu yako yupo gerezani anateseka halafu leo ukiambiwa kuna ujuzi ukifundishwa ndugu yako anaweza kutoka kiulaini, tena bila kutumia nguvu wala fedha, huwezi kutamani kweli?
Labda kamauna imani kali ya dini ndiyo unaweza kuukwepa mtego huo lakini kwangu mimi, siwezi kuficha kwamba nilifurahi sana na kutamani kuwa mchawi, tena niliyebobea. Nilijiapiza kwamba nitakapopata nafasi ya kuzungumza na baba, nitamueleza nia yangu bila kujali atanichukuliaje.
Niliendelea kutembea kufuata ile barabara ya lami huku muda mwingi tabasamu likiwa limechanua kwenye uso wangu. Tafsiri ya kile kilichotokea n kwamba asubuhi polisi wangeingia na kufanya ukaguzi mle mahabusu wangekuwa na imani kwamba bado nipo, labda watashtuka kwa nini sijavaa nguo kwa sababu yule mchawi hakuwa amevaa nguo.
*Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Nilielewa kwa nini baba aliniambia nisitoe maelezo yoyote kwa sababu kama yule mtu niliyebadilishana naye na kumuacha mle ndani mahabusu atahojiwa, maelezo atakayoyatoa yatakuwa hayaungi chochote na tukio lililotokea kwa hiyo uwezekano wa baadaye kuja kuachiwa kwa sababu ya kukosekana ushahidi ulikuwa mkubwa.
Sikujua atasota kwa muda gani mle mahabusu, tena kesi yenyewe ikiwa ni ya mauaji lakini niliona kama anastahili maana ni uchawi wa aina gani watu wanaenda kuufanyia sehemu hatari kama mahabusu? Niliendelea kutembea huku mara kwa mara nikicheka mwenyewe maana nilijiona bonge la mjanja kuukwepa msala ule.
Nikiwa naendelea kutembea nikiwa sijui naelekea wapi kwa sababu kama nilivyoeleza, sikuwa naijua mitaa ya Jiji la Dar es Salaam, nilisikia vishindo vya mtu akija huku akikimbia akitokea nyuma yangu. Baba amewahi kuniambia kwamba ukiwa unatembea usiku, ni mwiko kugeuka nyuma.
Alizidi kunikaribia, nikawa najiuliza kama atakuwa ni mtu mbaya itakuwaje? Niliendelea kujikaza kisabuni, vishindo vikazidi kunikaribia na alipofika usawa wangu, nikasikia akipunguza mwendo. Kilichonifanya niamini kwamba hawezi kuwa mtu mbaya, ni jinsi manukato aliyokuwa amejipulizia mwilini yalivyokuwa yakinukia vizuri.
“Mambo,” sauti ya kike ilisikika, safari hii ikiwa usawa wangu kabisa, ikabidi nisimame, nikageuza shingo yangu upande wa kulia alipokuwepo mtu huyo aliyenisalimu. Muda huo kwa makadirio ilikuwa ni kama saa nane za usiku maana kuna sehemu nilipita nikasikia redio kwa mbali ikitangaza kwamba ni saa nane kasoro za usiku.
“Mbona umeshtuka Togo!” alisema huku akinisogelea. Siwezi kuficha, mshtuko nilioupata nusura nidondoke na kuzimia.
Je, nini kitafuatia? Usikose
 
SEHEMU YA 32;




ILIPOISHIA:
Muda huo kwa makadirio ilikuwa ni kama saa nane za usiku maana kuna sehemu nilipita nikasikia redio kwa mbali ikitangaza kwamba ni saa nane kasoro za usiku.
“Mbona umeshtuka Togo!” alisema huku akinisogelea. Siwezi kuficha, mshtuko nilioupata nusura nidondoke na kuzimia.
SASA ENDELEA…
Alikuwa ni yule msichana ambaye mchana wa siku iliyopita alinifia gesti tukiwa kwenye mechi ya kirafiki na kunisababishia matatizo makubwa mpaka nikapelekwa mahabusu nikikabiliwa na kesi kubwa ya mauaji.
Nilitaka kukimbia nikahisi mwili wangu ukiishiwa nguvu, nilitaka kupiga kelele lakini sauti ikawa haitoki, nikabaki nimesimama palepale nikitetemeka kama mbwa mbele ya chatu, akawa ananishangaa usoni kama anayejiuliza maswali mengi yaliyokosa majibu.
“Wewe si ulikufa wewe?” nilisema huku safari hii miguu yangu ikiwa imeanza kupata nguvu, nikawa narudi nyuma nikiangalia upenyo wa kukimbia. Ni kama alishagundua ninachotaka kukifanya, akacheka na kunisihi nisikimbie bali kuna jambo la muhimu anataka kuniambia.
Maneno yake yaliingilia sikio moja na kutokea la pili, akili yangu ilinifanya niamini kwamba hakuwa yeye bali mzimu wake, akawa anazidi kunisogelea mwilini.
*Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
“Najua unafikiri labda mimi ni mzimu, siyo, nipo hai wala sijafa na leo nitakutajia mpaka jina langu,” aliniambia huku akizidi kunisogelea. Mazungumzo yake hayakuonesha kama alikuwa mzimu au alikuwa na nia mbaya na mimi lakini bado niliendelea kurudi nyuma, naye akawa anazidi kunifuata.
“Jina langu naitwa Isrina au wengi huwa wanapenda kuniita Isri. Nakuomba unipe japo dakika chache nikueleze kilichotokea leo na historia fupi ya maisha yangu, pia nataka nikueleze kitu ambacho hukijui kuhusu wewe ambacho kitakusaidia sana,” alisema kwa sauti ya upole.
Sijui nini kilitokea lakini nilijikuta nikishawishiwa na maneno yake matamu, nikasimama, akazidi kunisogelea mwilini na kunikumbatia kimahaba. Kitendo hicho kilisababisha hofu yote niliyokuwanayo iyeyuke ghafla kwa sababu nimewahi kusikia kwamba tofauti ya mtu na mzimu, ni kwamba mzimu unakuwa na mwili ambao japo unauona, hauwezi kuushika ukashikika.
Nimewahi kusikia kuwa miili ya mizimu inakuwa kwenye mfumo wa hewa, kwamba unamuona mtu lakini ukitaka kumkumbatia anakuwa kama hewa, hashikiki. Ili kuwa na uhakika, na mimi nilimshika kiuno chake, kweli kikashikika vizuri kabisa, tukawa tunatazamana usoni.
Tukiwa bado tunaendelea kutazamana, alinibusu kwenye shavu langu la kushoto, nikajikuta mwili mzima ukisisimka na ndani ya sekunde chache tu, ile hali iliyokuwa inanisumbua sana, ya kuwa na kiu kubwa ya kucheza mchezo wa kikubwa ilinianza tena.
Ni kama Isri alielewa nilichokuwa nakihitaji, alichokifanya ilikuwa ni kuendelea kunitoa hofu huku akiendelea kunichokoza hapa na pale, hali ikazidi kuwa tete kwa upande wangu.
Usiku huo kulikua kimya kabisa, hakukuwa na mtu yeyote aliyekuwa akuipita barabarani, kelele pekee zilizokuwa zinasikika zilikuwa ni za mbwa waliokuwa wakibweka mitaani. Ilibidi tusogee pembeni ya barabara, hakukuwa na muda wa kupoteza, kila mmoja alijiweka kwenye mkao wa kula na kazi ilianza palepale.
Kwa jinsi nilivyokuwa na ‘kiu’, nilimsambaratisha vilivyo Isri mpaka ikabidi aweke mpira kwapani. Hata hivyo, angalau kidogo nilianza kujisikia vizuri, akili yangu sasa ikahamia kwenye kutaka kuujua ukweli kwa sababu nilishahakikisha kwamba Isri hakuwa amekufa.
“Haya niambie kilichotokea.”
*Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
“Kwanza nashukuru,” alisema huku akinikumbatia na kunibusu huku tabasamu pana likiwa limechanua kwenye uso wake.
“Usijali, ahsante na wewe,” nilisema, akazidi kucheka. Alivuta pumzi ndefu na kunitazama usoni, Japokuwa ilikuwa ni usiku, kwa msada wa mbalamwezi niliweza kumtazama vizuri jinsi alivyokuwa ananiangalia kwa macho yaliyojaa ujumbe.
Alishusha tena pumzi ndefu kisha akanikumbatia na kujilaza kifuani kwangu, akaniambia kama sitajali, tutafute sehemu na kukaa kwa sababu alikuwa amechoka sana. Nilimkubalia, tukasogea kwenye nyumba ambayo ilikuwa ikijengwa lakini bado haijakamilika, tukakaa kwenye msingi na kuanza kuzungumza.
Aliniambia kwamba aligundua kwamba nina kitu fulani cha kipekee siku ya kwanza tulipokutana ndani ya basi, wakati tukisafiri kutokea Mbeya kuja Dar es Salaam. Aliniambia kwamba yeye amezaliwa katika ukoo wa kichifu kwani babu yake mzaa baba, alikuwa ni kiongozi wa mila wa Wanyakyusa waliokuwa wakiishi kandokando la Mlima Rungwe na alikuwa akiheshimika sana. Aliniambia kwamba hata babu yake huyo alipofariki, alimrithisha mikoba yake baba yake ambaye licha ya kuwa msomi, akiwa ni daktari kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, pia alikuwa akiendelea na shughuli za kimila na ndiyo maana yeye alikuwa na uwezo wa tofauti na watu wengine kwani ndani kwao yeye ndiye aliyekuwa wa kwanza kuzaliwa.
Maelezo hayo bado hayakuwa yamenisaidia kuelewa chochote, niliona kama ananizungusha tu lakini sikutaka kumkatisha, nikatulia na kuendelea kumsikiliza.
Aliniambia kwamba kwa kuwa yeye ndiye mtoto wa kwanza kwenye familia yao, na kawaida zile kazi za kimila huwa zinarithishwa kwa mtoto wa kwanza, baba yake alikuwa amefanya kitu kimoja kibaya sana kwenye maisha yake ndiyo maana siku aliponiona mimi alifurahi sana.
“Unamaanisha nini?”
“Mimi ni kaburi la wasio na hatia Togo, nimeamua kukueleza ukweli kwa sababu wewe ndiye mwanaume pekee ambaye umeweza kuuvuka mtego wa kifo,” aliniambia, nikawa simuelewi kabisa. Sikuelewa anamaanisha nini anaposema yeye ni kaburi la wasio na hatia na anamaanisha nini anaposema mimi nimeweza kuuvuka mtego wa kifo?
Nikiwa bado na shauku kubwa ya kutaka kumsikiliza alichomaanisha, nilipoinua uso wangu na kutazama upande wa barabarani, nilishtuka sana kuona kulikuwa na watu wengi wamekusanyika, wote wakiwa wanatutazama.
“Mungu wangu,” nilisema kwa mshtuko kwani ilionesha kuna jambo halikuwa sawa kwetu na ndiyo maana walikuwa wakitutazama. Tofauti na mimi, yeye alipowatazama wala hakushtuka, akaniambia ni haki yao kushangaa kwa sababu hatukuwa tukionekana wa kawaida.
*Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
“Unamaanisha nini?”
“Umewahi kusikia stori za majini?” aliniuliza, nikamgeukia na kumtazama usoni kisha nikawatazama tena wale watu, walikuwa wakizidi kuongezeka kwa wingi, safari hii baadhi yao wakawa wanatupiga picha kwa kutumia simu zao. Niliweza kuligundua hilo kwa sababu ya mwanga wa flash uliokuwa ukitumulika.
Nilimtaka tuondoke lakini akasema wala nisiwe na wasiwasi, hawawezi kutufanya jambo lolote na hawana uwezo huo. Alipoona situlii, aliniambia nimpe mkono wangu wa kushoto, nikafanya hivyo, akashika kidole changu cha mwisho kisha akaniambia na mimi nifanye hivyohivyo, nikamshika.
“Nahesabu mpaka tatu, nikifika tatu fumba macho na usifumbue mpaka nitakapokwambia,” alisema, nikatii kile alichoniambia. Alipofikisha tatu, nilifumba macho, nikashtukia ghafla tumehama pale tulipokuwa na kwenda upande wa pili, kule barabarani ambako watu wengi walikuwa wamesimama wakishangaa, tukajichanganya na wale watu.
“Hebu angalia wanachokishangaa,” alisema huku akinitaka nitazame pale tulipokuwa tumekaa awali. Macho yalinitoka nikiwa ni kama siamini.
Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 33:



ILIPOISHIA:
Alipofikisha tatu, nilifumba macho, nikashtukia ghafla tumehama pale tulipokuwa na kwenda upande wa pili, kule barabarani ambako watu wengi walikuwa wamesimama wakishangaa, tukajichanganya na wale watu.
“Hebu angalia wanachokishangaa,” alisema huku akinitaka nitazame pale tulipokuwa tumekaa awali. Macho yalinitoka nikiwa ni kama siamini.
SASA ENDELEA…
Watu wawili, mmoja akionesha kuwa mwanamke na mwingine mwanaume, wakiwa watupu kabisa huku miili yao iking’aa sana, walikuwa wamekaa kwenye msingi wa nyumba, wakiwa wanazungumza. Macho ya kila mmoja yalikuwa yaking’aa sana na nyuso zao zilikuwa na gizagiza fulani ambalo lilifanya iwe vigumu kwa watu kuwatambua sura zao.
“Hivi ndivyo tulivyokuwa tukionekana ndiyo maana unaona hawa watu wote wamekusanyika hapa,” alisema Isri huku akiniegamia.
Nilibaki nimepigwa na butwaa huku nikiwatazama wale watu ambao wala hawakuwa na taarifa kwamba tulikuwa tumeshajichanganya nao. Nilitamani kumuuliza Isri kwamba sasa iweje wale watu wawe wanaendelea kutuona wakati tulishahama na kujichanganya nao? Kabla hata sijamjibu, ni kama alizisoma hisia zangu, akaniambia kile walichokuwa wakiendelea kukiona, ilikuwa ni kiini macho.
Akaniambia kwamba watu wengi hawajui lakini hakuna jambo la hatari kama kusimama usiku na kuanza kutazama vitu usivyovijua au visivyo vya kawaida kwa sababu kama ni watu wenye nia ovu, unapowatazama tu wanajua kwamba unawatazama na wanao uwezo wa kubadilisha kile unachokiona wewe na kukuonesha kitu cha tofauti kabisa.
*Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Akaniambia ndiyo maana baadhi ya watu hupata matatizo makubwa sana baada ya kuona majini usiku, wengine huona watu warefu wenye kwato, wengine huona miti ikibadilika au huona viumbe vya ajabu wakati kiukweli ni kwamba wanakuwa wamewaona wachawi wakiwa kwenye maumbo yao ya kawaida lakini kwa kuwa wachawi nao wanakuwa wameshagundua kwamba wanatazamwa, wanawafanyia kusudi.
“Sijaelewa, kwa hiyo unamaanisha hata mimi na wewe ni wachawi?”
“Sijamaanisha hivyo.”
“Kwani wewe ulijua kwamba wanatutazama?”
“Ndiyo nilijua,” alinijibu Isri na kunifanya nipigwe na mshangao mkubwa. Watu walikuwa wakizidi kuongezeka na wengi walikuwa ni walinzi wa maeneo ya jirani na pale, wengine wakiwa ni Wamasai na wengine wakiwa ni wafanyabiashara wanaodamka alfajiri na mapema kuwahi kuchukua bidhaa zao.
“Sasa mbona wanazidi kuongezeka, itakuwaje? Ina maana hapa hawatusikii wala hawatuoni?” nilimuuliza, akatingisha kichwa kuonesha kukubali, akaniambia ipo namna ya kuwatawanya. Aliposema hivyo tu, mara nilishangaa wale watu ambao watu wote walikuwa wakiwatazama, wakibadilika na kuwa mbwa wawili wakubwa, dume na jike.
Wakaanza kubweka kwa hasira na kuanza kutimua mbio kulifuata lile kundi la watu. Kiukweli kwa jinsi mbwa hao walivyokuwa wakubwa, wenye hasira huku meno yao makali yakiwa yametoka nje, hata mimi mwenyewe nilijikuta nikiogopa mno. Kufumba na kufumbua, kundi lote lilianza kutimua mbio, kila mmoja kivyake.
Na mimi nilitaka kukimbia lakini Isri alinikamata mkono kwa nguvu, wale mbwa wakawa wanazidi kuja kwa kasi, ikabidi nisimame nyuma yake. Watu walizidi kutimua mbio huku wakipiga kelele na ghafla tukasikia breki kali za gari zikifuatiwa na kishindo kikubwa.
“Tayari!” alisema Isri lakini sikumtilia maanani, akili zangu zote zikawa kwa wale mbwa. Cha ajabu, japokuwa sisi tulikuwa tumesimama, walitupita kwa kasi kubwa na kuendelea kuwatimua wale watu.
“Tayari huko,” alisema Isri kwa mara nyingine, ikabidi nimuulize tayari nini? Akaniambia twende tukajionee wenyewe. Yeye alitangulia, mimi nikawa namfuata, tukanyoosha na ile barabara ya lami mpaka mahali palipokuwa na njia panda, akanionesha kwa kidole nitazame mwenyewe.
Gari dogo aina ya Toyota Carina lilikuwa limeacha njia na kugonga kingo za daraja na kuingia mtaroni, huku barabarani kukiwa na mtu amelala huku damu nyingi zikimtoka akionekana amegongwa na gari lile.
“Mungu wangu,” nilisema kwa mshtuko, akaniambia mtu huyo alikuwa miongoni mwa wale waliokuwa pale wakitushangaa na wakati akiwakimbia wale mbwa ndipo akaingia barabarani bila kutazama, hali iliyosababisha agongwe na gari hilo kisha na lenyewe likapoteza mwelekeo na kugonga kingo za barabara.
Yaani kwa jinsi Isri alivyokuwa akizungumza kirahisirahisi, ungeweza kudhani anasimulia stori au anazungumza masihara, alikuwa anarahisisha sana mambo hali ambayo ilinifanya nigeuke na kumtazama usoni.
Nilishtuka sana nilipomtazama usoni, macho yake yalikuwa yamebadilika rangi na kuwa mekundu sana na kung’aa huku kwenye kingo za mdomo wake kukiwa kama na michuruziko ya damu, meno makali kama ya wale mbwa yakiwa yametokea kila upande.
Mshtuko nilioupata ulikuwa hauelezeki, nikahisi na mimi nipo kwenye mtego mbaya wa kifo, sikusubiri chochote, nilikurupuka na kuanza kutimua mbio kwa kasi kubwa nikiwa hata sielewi naelekea wapi.
“Togo! Togo rudi nakwambia, ohooo!” alisema kwa sauti kali ya kutisha lakini wala sikuvijali vitisho vyake. Jambo ambalo najisifia, ni uwezo mkubwa wa kutimua mbio. Unajua maisha ya kule kijijini tuliyokulia, ilikuwa ni lazima tu ujifunze kukimbia kwa kasi kubwa, kwani kinyume na hapo usingeweza kuambulia chochote mnapoenda kuwinda wanyama wa porini.
Nilikimbia kisawasawa, dakika chache baadaye nikawa nimeshafika mbali kabisa, nikatokezea kwenye barabara kubwa ya lami ambayo japokuwa ilikuwa ni usiku, yenyewe ilikuwa na magari mengi yakiendelea kupita, hasa makubwa ya mizigo.
*Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Kiukweli nilikuwa mgeni kabisa na jiji lakini niliona ni bora nipotee kuliko kuendelea kukaa karibu na Isri. Japokuwa alikuwa amenieleza mambo mengi kuhusu yeye, yale mambo aliyoyafanya dakika za mwisho, ikiwemo kuwabadilisha wale watu kuwa mbwa, jinsi alivyokuwa akichekelea ile ajali iliyosababisha maafa makubwa na jinsi alivyobadilika na kuwa kama mnyama mkali wa porini, yalinifanya nimuogope mno.
Nikawa naendelea kukimbia pembezoni mwa barabara nikiwa hata sijui naelekea wapi. Kwa mbali kulianza kupambazuka, nikaanza kuona watu wachache wakifanya mazoezi ya kukimbia pembeni ya barabara.
Niliamini hao ndiyo wanaoweza kunisaidia uelekeo wa kufika nyumbani kabla hakujapambazuka kabisa.
Cha ajabu, kila nilipokuwa nikimkaribia mtu yeyote anayefanya mazoezi, alikuwa akitimua mbio za ajabu kunikwepa, mwingine almanusra agongwe na gari kwani alikuwa akija kwa mbele, na mimi nikawa nakimbia taratibu huku nikionesha dalili za kutaka kusimama ili nimuulize lakini ghafla aliponiona, alipiga kelele na kuvuka barabara kwa kasi kubwa mpaka upande wa pili bila hata kutazama, lori kubwa likapiga honi kali na dereva akakata kona kali kumkwepa.
Ilibidi nisimame na kujitazama mwilini kwa nini watu wananikimbia. Jambo la kwanza ambalo lilinishtua, kumbe kwa muda wote huo nilikuwa nikikimbia kwa kutumia mikono na miguu, hata sijui kwa nini muda wote huo sikujishtukia, harakaharaka nikainuka na kusimama kwa kutumia miguu.
Nilipojitazama mwilini, nilishtuka mno kugundua kwamba kumbe nilikuwa na manyoya mengi kama mnyama wa porini, nilipojitazama mikono, nilizidi kupagawa baada ya kugundua kuwa kumbe mikono yangu ilikuwa imebadilika na kuwa kama ya mbwa.
Mara nilishtukia jiwe kubwa likirushwa na kunikosakosa, kabla sijatulia nikashtukia jiwe lingine likinikosakosa, nikaona naweza kuuawa bure, nikaanza kutimua mbio lakini nilipojaribu kukimbia kwa miguu nilijikuta nikishindwa, ikabidi nijaribu kutumia na mikono, nikaweza na kasi ilikuwa kubwa zaidi. Nilikimbia sana huku nikilia nikiwa sielewi nini itakuwa hatma yangu.
Ni hapo nilipogundua kwamba kumbe Isri alikuwa amenigeuza umbo langu na kuwa kama mbwa mkubwa, nilimlaani sana moyoni mwangu na kujikuta nikiyakumbuka maneno ya baba ambaye mara kwa mara alikuwa akinionya kuhusu msichana huyo.
Nikiwa naendelea kukimbia, nilishtukia mtu mmoja akija kwa kasi kubwa nyuma yangu, nikazidi kuongeza kasi lakini kabla sijafika mbali nilishtukia kamba nene ilipita shingoni mwangu na kunifunga kitanzi, nikadondoka chini kama mzigo.
Nikiwa bado hata sijui nini cha kufanya, nilishtukia nikifungwa mikono na miguu, nikajaribu kukurupuka lakini sikuweza kufanya chochote, ikabidi nitulie na kuanza kumtazama ni nani aliyenifanyia kitendo hicho na alikuwa na lengo gani kwangu maana niliona kifo changu kikiwa kimewadia. Na hata kama ningeuawa, kila mtu angeamini aliyekufa ni mbwa mkubwa.
Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 34:



ILIPOISHIA:
NIKIWA bado hata sijui nini cha kufanya, nilishtukia nikifungwa mikono na miguu, nikajaribu kukurupuka lakini sikuweza kufanya chochote, ikabidi nitulie na kuanza kumtazama ni nani aliyenifanyia kitendo hicho na alikuwa na lengo gani kwangu maana niliona kifo changu kikiwa kimewadia. Na hata kama ningeuawa, kila mtu angeamini aliyekufa ni mbwa mkubwa.
SASA ENDELEA…
“MIMI sipendi mtu mkaidi, siku nyingine nitakuacha uwe mbwa koko, unafikiri unaweza kunikimbia mimi?” alikuwa ni Isri, akiwa anahema huku jasho likimvuja kwa wingi. Nilitaka nimuombe msamaha lakini sauti haikutoka, nikawa naendelea kutokwa na machozi kwa wingi.
Aliniinamia pale chini, akanionyesha ishara nifumbue mdomo, nikafanya hivyo, akaingiza mkono mfukoni na kutoa kichupa kilichokuwa na maji, akayamimina yote mdomoni mwangu. Yalikuwa machungu sana lakini nilivumilia, akanionyesha ishara kwamba niyameze.
Nilifanya hivyo, nikahisi kama mwili wangu wote unawaka moto kwa maumivu lakini kufumba na kufumbua, nilijikuta nikibadilika na kurudi kwenye hali yangu ya kawaida. Alinifungua ile kamba ya shingoni kisha mikononi na miguuni, akaniambia nisimame lakini nilishindwa kufanya hivyo kwani sikuwa na nguo hata moja mwilini, akafungua kimfuko alichobeba mgongoni na kunirushia nguo zangu.
>>>>Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
Yaani kama kuna mtu anabisha uchawi haupo kwenye hii dunia, basi anajidanganya sana, kuna uchawi na wachawi na wengine wana uwezo mkubwa kuliko unavyoweza kufikiri. Sijui hata hizo nguo nilizivua saa ngapi na yeye alizipata wapi, sikutaka kuhoji, harakaharaka nilizivaa huku nikitazama huku na kule kama hakuna mtu yeyote anayetuona.
Bado mwili wangu ulikuwa na harufu ya mbwa-mbwa na mikono ilikuwa imechubuka nadhani ni kwa sababu ya kukimbia kama mbwa.
“Kwa nini unanifanyia hivi Isri? Kosa langu ni nini?”
“Sasa kwani mimi nimekufanyaje? Badala unishukuru unaanza kunilaumu tena.”
“Nikushukuru! Nikushukuru kwa lipi,” nilisema kwa hasira huku nikimsogelea Isri mwilini, mwili wangu ukitetemeka kwa jazba.
“Unataka kufanya nini Togo!”
“Nataka unieleze, kwa nini umenifanyia hivi? Unanijua au unanisikia?” niliwaka kwa jazba. Miongoni mwa vitu ambavyo nilikuwa najivunia na hata wenzangu kule kijijini walikuwa wakiniogopa, ni ubavu niliokuwa nao. Hakukuwahi kutokea ugomvi wowote wa kupigana halafu nikashindwa ingawa ilikuwa si rahisi kunikuta nikipigana mpaka mtu anichokoze sana.
“Mimi ni nani kwako?” Isri aliniuliza swali ambalo kidogo lilizifanya jazba zangu zitulie. Aliniuliza swali hilo kwa mara nyingine, halafu akaniuliza kama naamini yeye anaweza kunifanyia jambo baya kwa makusudi kwa jinsi alivyokuwa ananipenda mpaka kufikia hatua ya kunipa mwili wake wa thamani. Akaniuliza kama nimesahau mapenzi makubwa aliyonionyesha tangu siku ya kwanza ananiona, nikajikuta nikishusha pumzi ndefu na kujiinamia, mwili ukianza kupunguza kutetemeka.
“Twende huku,” alisema huku akinishika mkono, nilitaka kujichomoa lakini moyo ukasita, nikawa mpole kama kondoo anayepelekwa machinjioni, nikamfuata mpaka chini ya mwembe mkubwa uliokuwa jirani na pale tulipokuwa. Akaniambia nimpe mkono wangu wa kushoto, akaugeuza na kuutazama kwa muda kwenye upande wa nyuma wenye kucha.
>>>>Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
“Unauona huu mshipa wa damu,” aliniambia huku akinionyeshea mshipa mkubwa wa damu uliokuwa unaonekana. Akaniambia kwamba nikifika nyumbani, kabla sijaingia ndani, natakiwa kuchukua kitu chenye ncha kali, iwe sindano au wembe na kujitoboa kwenye huo mshipa ili damu itoke.
“Damu ikiwa inatoka, hakikisha unaipakaza kwenye kingo mbili za mlango kisha ndiyo uingie ndani na usitoke mpaka giza liingie,” aliniambia huku akinipa pole kwa yote yaliyotokea, sikumjibu kitu kwani bado sikuwa najua nini itakuwa hatma yangu.
Baada ya hapo, aliniambia nifumbe macho, nikatii alichokisema, akaniambia nisifumbue mpaka atakaponiambia. Ghafla nikaanza kuhisi kama kimbunga kikali kinavuma pale chini ya mwembe tulipokuwa, sikuelewa tena kilichoendelea mpaka niliposikia sauti za watu ninaowafahamu wakilitaja jina langu, akiwemo Isri mwenyewe.
Ikawa ni kama nimetoka kwenye usingizi mzito ambao hata sielewi ulitokea wapi, nilipofumbua macho, nilishtuka mno kujikuta nipo nje ya nyumba ya akina Rahma huku mama na ndugu zangu wakiwa wamenizunguka lakin Isri hakuwepo. Yaani kuna mambo mengine yanatokea hata ukiulizwa yametokeaje, huwezi kuelezea.
“Vipi? Mbona umelala nje?” mama aliniuliza huku akiniinua. Sikutaka kuwa na maelezo marefu maana kila mtu angeniona mwendawazimu kama ningesimulia kila kitu kilichotokea. Kwa bahati nzuri, baba alitoka na kuja hadi pale nilipokuwa, nikiwa bado nimekaa chini kwenye maua.
Akanitazama usoni kwa makini kisha akawaambia ndugu zangu pamoja na mama wakaendelee na usafi kwa sababu ndiyo kwanza walikuwa wametoka kuamka na walikuwa wakifanya usafi wa mazingira na nyumba.
Waliondoka kwa shingo upande, mara kwa mara wakawa wanageuka na kunitazama, wakiwa na maswali mengi yasiyo na majibu. Walichokuwa wanakijua wao ni kwamba nilikuwa nimekamatwa na polisi na kwa jinsi taratibu za kisheria zilivyo, isingekuwa rahisi mimi kutoka bila kuja kuwekewa dhamana na hakukuwa na mtu mwingine wa kufanya hivyo zaidi ya baba na baba yake Rahma.
“Hebu simama,” alisema baba huku akinipa mkono, na mimi nikampa mkono wa kushoto. Wakati akinivuta kuniinua, nilimuona akiukazia macho mshipa wangu wa mkononi, uleule ambao Isri aliniambia nikifika nyumbani, kabla sijaingia ndani niutoboe kisha damu nizipake kwenye kingo za mlango.
“Umefanya nini? Hebu tuone?” alisema baba huku akizidi kuuvutia ule mkono wangu kwake, akautazama ule mshipa kwa sekunde kadhaa kisha nikamuona akiingiza mkono wake mmoja mfukoni, akatoa pochi yake na kuipekuakwa mkono mmoja, huku ule mwingine akiwa bado amenishikilia.
Nikamuona akitoa sindano ya kushonea nguo iliyokuwa na uzi mweusi, nikiwa bado najiuliza anataka kufanya nini, nilishtukia akinitoboa, nikaruka kwa maumivu, damu nyingi ikawa inaruka kwa kasi. Harakaharaka, akiwa bado amenishikilia, nilimuona baba akitoa kichupa kidogo mfukoni, cha ajabu eti akawa anakinga damu ambayo licha ya kutobolewa sehemu ndogo, ilikuwa ikiendelea kuruka kwa nguvu.
Sikuelewa kulikuwa na uhusiano gani kati ya ule mshipa wangu, damu iliyokuwa inanitoka na kile alichokisema Isri. Kile kichupa kidogo kilikaribia kujaa lakini cha ajabu, damu yenyewe ilikuwa nyeusi tii. Ilipopungua kutoka, baba aliniachia, akakifunga kile kikopo na bila kunisemesha kitu aliingia ndani haraka na kuniacha palepale nje.
Ndugu zangu waliokuwa wakiendelea kunitazama kwa macho ya kuibia, walibaki kunishangaa tu. Kwa kuwa baba hakuniambia chochote, na tayari Isri alikuwa amenipa maelezo fulani, nilijifuta ile damu iliyokuwa ikiendelea kunivuja, safari hii ikiwa imepungua, harakaharaka nikasogea mlangoni na kuipaka kwenye kingo za mlango, nikawa nageuka huku na kule kuhakikisha hakuna anayeona ninachokifanya.
Nilipofanya kitendo hicho tu, nilisikia kama masikio yamezibuka hivi, nikawa nasikia sauti za ajabuajabu kama miluzi hivi ambayo awali sikuwa naisikia, nikajikuta nikilazimika kuziba masikio kwa mikono, nikaingia ndani.
>>>>Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
Cha ajabu, nilipoingia ndani tu, ile miluzi ilikoma kusikika, nikarudi kwenye hali yangu ya kawaida ingawa bado damu ilikuwa ikinitoka kidogo.
“Togoooo!” Rahma ambaye ndiyo kwanza alikuwa akitoka chumbani kwake baada ya kuamka, alisema huku akinikimbilia pale koridoni nilipokuwepo, akaja na kunikumbatia kwa nguvu huku akipiga kelele, akasema eti haamini kama ameniona.
“Mbona unatoka damu?”
“Nimeumia,” nilimjibu kwa mkato, akanipa pole sana na kunishika mkono, akawa ananipeleka kule chumbani kwake. Mwili wangu ulikuwa mchafu na nilikuwa nanuka lakini mwenyewe hakujali. Furaha aliyokuwa nayo, iliweza kabisa kuumaliza uchovu wa asubuhi aliokuwa nao, uso wake ukachangamka mno, akawa anatembea kwa madaha huku akijinyonganyonga.
Kabla ya kupatwa na yale matatizo siku iliyopita, hatukuwa tumeonana na Rahma kwa sababu asubuhi aliwahi sana kuamka na kuondoka na mama yake kufuatilia mambo ya chuo, hatukupata muda wa kuwa pamoja.
“Togoo!” nilisikia baba akiniita kwa sauti ya juu akiwa amesimama kwenye mlango wa chumba anacholala na mama.
“Naam baba,” niliitikia huku nikijaribu kumtoa Rahma maana alikuwa amenishika kimahaba, baba akaja mbiombio na kunishika mkono, akamwambia Rahma kuna kazi hatujamaliza kwa hiyo anisubiri, alinishika mkono na kuanza kunivuta kuelekea nje lakini tulipofika kwenye kingo za mlango tu, jambo la ajabu lilitokea.
Je, nini kitafuatia
 
SEHEMU YA 35:


ILIPOISHIA:
“Naam baba,” niliitikia huku nikijaribu kumtoa Rahma maana alikuwa amenishika kimahaba, baba akaja mbiombio na kunishika mkono, akamwambia Rahma kuna kazi hatujamaliza kwa hiyo anisubiri, alinishika mkono na kuanza kunivuta kuelekea nje lakini tulipofika kwenye kingo za mlango tu, jambo la ajabu lilitokea.
SASA ENDELEA…
Kishindo kikubwa kilisikika, nikamuona baba akianza kuyumbayumba kama amelewa, na mimi nikaanza kusikia kizunguzungu kikali huku damu zikianza kututoka wote, mdomoni na puani. Muda huo tulikuwa tumeshavuka kizingiti cha mlango.
Sijui nilipata wapi ujasiri kwani ni muda huo ndipo nilipogundua kwamba kuna kosa nilikuwa nimelifanya, Isri aliniambia kwamba nisitoke nje mpaka giza litakapoingia, jambo ambalo nililikiuka kwa hiyo ili kurekebisha makosa, nilimvuta baba kwa nguvu, wote tukaangukia upande wa ndani wa mlango.
Kilisikika kishindo kingine kisha baba akawa ni kama amezinduka kutoka kwenye usingizi mzito.
“Nini kimetokea?” baba aliniuliza huku na yeye akiwa ni kama amepigwa na butwaa, akainua shingo na kutazama huku na kule, nikamuona akishtuka zaidi baada ya kuona damu zinamtoka mdomoni na puani pale chini.
“Hata mimi sijui,” nilimjibu huku nikisimama, na yeye akasimama kisha akawa anajifuta damu huku akitazama vizuri pale mlangoni. Aliangalia kwa sekunde kadhaa kisha akanigeukia na kunitolea macho ya ukali.
 
SEHEMU YA 36:



“Umeweka nini hapa?” aliniuliza kwa ukali.
“Hakuna kitu.”
“Una uhakika?” aliniuliza huku akinisogelea mwilini. Miongoni mwa sifa za baba, huwa hapendi kabisa mtu muongo, ni bora akikuuliza unyamaze kuliko kutoa majibu ya uongo. Ili kuepusha shari, nilinyamaza na kujiinamia.
“Si naongea na wewe?”
“Wakati naingia nilipakaza damu hapo kwenye mlango,” nilisema, akaonesha kushtuka mno, hakusema kitu zaidi ya kunishika mkono, akawa ananivutia ndani huku akiendelea kujifuta damu.
Tulienda mpaka kwenye kile chumba changu, tukaingia huku baba akiwa makini kuhakikisha hakuna mtu yeyote anayetutazama. Wakati naingia, nilitupia macho kwenye mlango wa chumba cha Rahma, nikamuona akiwa anatuchungulia. Nilimuonesha ishara kwamba anisubiri, akatingisha kichwa kuniitikia.
“Mimi ni nani kwako?”
“Ni baba yangu.”
“Haya nataka unieleze kila kitu, umetokaje mahabusu na nini kimetokea mpaka ukapaka damu kwenye mlango,” alisema baba kwa sauti ya chini, lakini akionesha kutokuwa na hasira na mimi.
Kabla sijamjibu, niliingiza mkono mfukoni na kutoa ile dawa ya ajabu ambayo kwa kiasi kikubwa ilinisaidia sana.
“Hiyo ni mimi nilikuwekea muda ule wakati polisi wanakuchukua, naamini imekusaidia sana,” alisema baba huku akiichukua ile dawa mikononi mwangu na kuiweka kwenye mfuko wa shati. Ni hapo ndipo nilipoanza kupata picha juu ya nini kilichotokea.
>>>>Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
“Sasa baba, unataka nikueleze nini wakati kumbe unajua kila kitu na wewe ndiye uliyenielekeza jinsi ya kutoka mahabusu?”
“Unachokisema ni sawa lakini najua kuna mambo mengi yametokea ukiachilia mbali wewe kutoka mahabusu na ndiyo maana nimekutoboa mkono wako na kukinga damu yako, mimi ni baba yako na hakuna mtu mwenye uchungu na wewe kuliko sisi wazazi wako, ni lazima ujifunze kuniamini na kuwa muwazi kwangu,” alisema.
Kiukweli sikuwahi kumsikia baba akizungumza kwa busara na mimi kiasi hicho, yaani ni kama alikuwa akizungumza na mkubwa mwenzake na hata ule ukali wake wa siku zote, hakuuonesha kabisa.
Nilishusha pumzi na kukaa vizuri, sikuona sababu ya kuendelea kumficha, nilianza kumueleza kila kitu kilichotokea, kuanzia nilipofikishwa kituoni, wale wachawi waliokuja usiku kule mahabusu na jinsi yule mwingine alivyobadilika sura na kufanana na mimi.
Nilipofikia kipengele hicho, baba alinikatisha, akaniambia kwamba dawa aliyokuwa amenipa, ina nguvu kubwa ya kufanya chochote ninachokitaka. Akaniambia kwamba yule mchawi aliyebadilika sura, alishindwa kutoka mpaka asubuhi na askari walipoingia kwa ajili ya kufanya ukaguzi.
“Nasikia wameshtuka sana kumuona, wakadhani ni wewe lakini tofauti ikawa ni kwamba sura mmefanana lakini yeye ni mzee na amekutwa hana nguo hata moja, mtaani kote ndiyo gumzo na hata vyombo vya habari vimeanza kuripoti tukio hilo la ajabu,” alisema baba.
Kauli yake ilinifanya niwe na shauku kubwa ya kutaka kujua nini kimeendelea, akaniambia nisiwe na wasiwasi atanieleza lakini pia akaniambia kwamba anataka kumtumia yule mchawi kama funzo kwa watu wengine wenye tabia ya kufanya uchawi wa kijinga.
Aliposema uchawi wa kijinga, sikumuelewa anamaanisha nini, nikataka kumuuliza tena lakini aliniambia niendelee kumueleza kilichotokea. Nilimueleza kila kitu na jinsi nilivyokutana na yule msichana usiku ule.
“Lakini si nilishakukataza kuwa karibu na Isri?” alisema huku akinitazama usoni, nilishtuka kumsikia baba akimtaja jina. Kwa ilivyoonesha, kumbe baba alikuwa akimfahamu vizuri msichana huyo na hata aliponikataza kuwa naye karibu, alikuwa na maana yake.
“Huyo si ndiye aliyekusababishia matatizo mpaka ukakamatwa kwa tuhuma za mauaji? Ina maana wewe hukushtuka mtu amekufia mchana gesti halafu usiku unakutana naye tena? Akili zako zinafanya kazi sawasawa kweli?” baba alinibadilikia, nikawa nataka kujitetea lakini alinikatisha na kuniambia anaelewa kila kitu kilichotokea kati yetu.
“Hebu hiyo mikono yako,” alisema, nikasita kidogo lakini baadaye nilimpa, akaishika na kuanza kuitazama upande wa mbele kisha akanitazama usoni.
“Na wewe umeshakuwa kama yeye,” alisema huku akiniachia, akaniambia nifumbue mdomo wangu. Nilifanya hivyo, akawa anayatazama meno yangu kwa makini. Bado nilikuwa na maswali mengi kuliko majibu na ilionesha kwamba baba anamfahamu vizuri sana Isri.
Kitendo cha kutazama mikono yangu kisha wakati huohuo akaanza kukagua meno yangu, kilitosha kunifanya nielewe kwamba kumbe anajua jinsi msichana huyo alivyonigeuza na kuwa kiumbe wa ajabu.
“Umewapa ushindi maadui zangu kwa sababu ya mambo yako ya kipumbavu,” alisema baba huku akiinuka, bado damu zilikuwa zikimtoka puani ingawa safari hii haikuwa kwa wingi kama ilivyokuwa mwanzo.
Alipotaka kutoka, nilimuita, akageuka na kunitazama, nikamwambia Isri ameniambia nisitoke nje mpaka giza litakapoingia, akanijibu kwa kifupi kwamba anajua kisha akaondoka zake.
Harakaharaka niliinuka na kukimbilia bafuni kwani nilikuwa najisikia aibu kukutana na Rahma nikiwa na harufu mbaya kiasi kile, nikajifungia na kufungulia maji kwa wingi, nilivua nguo zangu kisha nikaanza kujimwagia maji huku nikijikagua kama hakukuwa na kitu chochote kisicho cha kawaida mwilini mwangu.
Mara nilisikia mlango wa bafu ukigongwa, nikahisi ni Rahma amenifuata, harakaharaka nikaufungua, nikakutana uso kwa uso na baba.
>>>>Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
“Ogea hii,” alisema huku akinipa ile dawa ambayo aliwahi kunipa niogee, ambayo ukiogea mwili unatoa uchafu mweusi kama mkaa. Nilimshukuru na kufunga mlango, nikaendelea kuoga. Maji machafu, meusi tii yalianza kunitoka, safari hii nikawa sina wasiwasi maana nilikuwa naelewa kinachotokea.
Nilioga mpaka uchafu wote ukaniisha mwilini, nikachukua nguo zangu na kuzikung’uta sana kisha nikavaa na kutoka. Rahma alikuwa amesimama kwenye mlango wa chumba chake, akionesha kunisubiri kwa shauku kubwa.
Hakuwa amevaa chochote zaidi ya kujifunga upande wa khanga nyepesi, akawa ananitazama usoni kwa macho yake mazuri, ambayo yalikuwa ni kama yana usingizi kwa jinsi yalivyolegea.
Nilitazama huku na kule, nilipoona hakuna mtu anayetutazama, nilimsogelea, akanikumbatia kwa mahaba kisha akanivutia ndani. Hatukukumbuka hata kufunga mlango, kwa makusudi aliuachia ule upande wa khanga, ukadondoka chini, nikawa kama fisi aliyeona mfupa.
Je, nini kitafuatia? Usikose
 
SEHEMU YA 37:


ILIPOISHIA:
Nilitazama huku na kule, nilipoona hakuna mtu anayetutazama, nilimsogelea, akanikumbatia kwa mahaba kisha akanivutia ndani. Hatukukumbuka hata kufunga mlango, kwa makusudi aliuachia ule upande wa khanga, ukadondoka chini, nikawa kama fisi aliyeona mfupa.
SASA ENDELEA…
Harakaharaka nilichojoa magwanda yangu huku nikiwa na pupa isiyo na mfano, muda mfupi baadaye tulikuwa saresare maua, nikamnyanyua Rahma juujuu na kumbwaga kwenye uwanja wa fundi seremala. Mwenyewe alionesha kufurahia sana, akanibana kwenye kifua chake kilichojaa vizuri, tukagusanisha ndimi zetu.
Hata hivyo, tofauti na mara zote ninapokuwa kwenye mazingira kama hayo, ambapo ‘Togo’ wangu huwa mkali kama nyoka koboko, nilishangaa akiwa kimya kabisa, kama hajui ni nini kilichokuwa kinataka kutokea.
Kama nilivyoeleza tangu mwanzo, sikuwa najua chochote kwenye ulimwengu wa kikubwa na Rahma ndiye aliyekuwa wa kwanza kuniingiza kwenye ulimwengu huo, akifuatiwa na Isri, tena ndani ya siku chache tu. Kwa hiyo, sikuwa mzoefu na hicho kilichotokea, kilikuwa kitu kigeni kabisa kwangu.
Nimewahi kusikia kwamba, kwa mwanaume, hakuna aibu kubwa kama kuwa na mwanamke faragha halafu ukashindwa kazi, nikajikuta nikiwa na wasiwasi mkubwa kweli ndani ya moyo wangu. Sikujua Rahma atanichukuliaje, sikujua atanidharau kwa kiasi gani, nikajikuta kijasho chembamba kikinitoka huku akili ikiwa imehama kabisa.
“Togo, vipi?” aliniuliza Rahma baada ya kubaini mabadiliko niliyokuwa nayo. Swali lake lilinifanya nizidi kujisikia aibu, nilikosa cha kujibu na kiukweli sikuwa na majibu. Alipeleka mkono bondeni yaliko makazi ya ‘Togo’ na kujaribu kumpa hamasa kwa kutumia mikono yake laini lakini ilikuwa sawa na kazi bure.
“Mshukuru sana Mungu wako, ulikuwa unaenda kumuua mtoto wa watu, mshenzi sana wewe,” nilisikia sauti ya baba ikiniongelea sikioni kwa ukali, ikafuatiwa na msonyo mrefu, nikakurupuka kwa hofu kubwa, nikawa namtazama Rahma nikiwa nimekodoa macho, kijasho chembamba kikinitoka.
Nilikumbuka tukio lililonitokea na Isri, nilipokutana naye kwa mara ya kwanza faragha, ambapo tukiwa mchezoni, ghafla ‘alikata roho’ ingawa baadaye nilikutana naye tena akiwa mzima na ndiyo yakatokea yale yaliyotokea usiku uliopita. Alichokisema baba kilinifanya nihisi kwamba huenda kuna kitu kibaya mwilini mwangu ambacho ndiyo chanzo cha yote na nikifanya masihara, kweli Rahma atakufa na kusababisha msiba mzito kwa familia yake.
Nilikumbuka pia kauli ya Isri kwamba mimi ndiye mwanaume pekee niliyeweza kuushinda mtihani wa kifo baada ya kukutana naye kimwili.
“Togo, una nini mpenzi wangu,” alisema Rahma huku akisimama, naye akionesha kushangazwa na kilichotokea. Alinisogelea na kutaka kunikumbatia lakini nilijitoa harakaharaka, nikavaa nguo zangu huku nikiendelea kuhema kwa nguvu, nikamuona Rahma akikaa pembeni ya kitanda na kujiinamia, machozi yakaanza kumtoka.
Niliondoka haraka na kuelekea bafuni, nikajifungia mlango kwa ndani na kujiinamia, nikiwa hata sielewi nini cha kufanya. Ilibidi nijimwagie tena maji, mwili wangu ukapata nguvu, nikatoka na kwenda chumbani kwangu, nikawa nimejilaza huku nikiendelea kutafakari kilichotokea.
Kwa mbali ile kiu kali ya kukutana kimwili na mwanamke ilinianza upya, nikawa najiuliza, inawezekanaje muda mfupi tu uliopita nimeshindwa kabisa kufanya chochote na Rahma na kumuacha akiwa na huzuni kubwa kwenye moyo wake, halafu dakika chache baadaye niwe na hamu kali isiyoelezeka.
Nilipokumbuka ile kauli ya baba, niliona kabisa kinachoenda kutokea ni janga kubwa kwa Rahma kwa sababu muda si mrefu, mimi ningeenda chumbani kwake au yeye angekuja kwangu, tungeanza kubembelezana na mwisho tungeishia kuangukia dhambini, na matokeo yake dhambi ingekomaa na kuzaa mauti kwa Rahma, jambo ambalo lingenifanya niishi na hatia ya kukatisha maisha ya mtu asiye na hatia milele.
Nilichokifanya, harakaharaka niliamka pale kitandani, nikavaa viatu vyangu na kutaka kutoka lakini nilikumbuka kwamba giza halikuwa limeingia kwa hiyo kutoka nje kungemaanisha kwamba ningepata madhara makubwa kama Isri alivyonipa masharti.
Niliamua kwenda kukaa sebuleni, ndugu zangu pamoja na wadogo zake Rahma wakawa wananishangaa. Kwa muda mfupi tu tuliokaa hapo nyumbani, tayari nilishaonesha tabia za ajabu sana. Kila mtu akawa ananitazama kwa macho ya chinichini, haikuwa kawaida yangu kukaa sebuleni.
Nilijikaza kiume, nikakazia macho kwenye runinga, nikawa sina habari na mtu, ukimya ukatanda pale sebuleni. Baba na baba yake Rahma walikuwa wamekaa kwenye sehemu ya kulia chakula, wakiwa wanacheza bao huku mama na mama yake Rahma wenyewe wakiwa jikoni.
Muda mfupi baadaye, Rahma alikuja na kuchungulia pale sebuleni, alipochungulia tu, macho yangu na yake yakagongana, akanionesha ishara ya kuniita kwa mkono kisha nikamsikia akitembea kuelekea chumbani kwake.
“Mungu wangu, sasa itakuwaje?” niliwaza, nikaamua kujikausha kama sijamuona Rahma, nikawa naendelea kukazia macho kwenye runinga imngawa kiukweli wala akili zangu hazikuwa pale na sikuwa najua hata kunaoneshwa nini.
Muda mfupi baadaye, Rahma alikuja tena lakini safari hii, alikuja na kukaa kwenye kochi nililokuwa nimekaa mimi, uso akiwa ameukunja. Nilijua kwamba amekasirika lakini sikuwa na namna zaidi ya kujiepusha naye, nilikuwa nampenda Rahma na sikuwa tayari kuona anapatwa na jambo lolote baya.
Alikuwa amejifunga khanga nyepesi na ndani hakuwa na kitu kabisa, nikazidi kujikuta kwenye wakati mgumu, tukawa tunatazama runinga bila mtu yeyote kumsemesha mwenzake. Hata wale ndugu zetu nadhani nao waligundua kwamba hatupo sawa kwa sababu si kawaida ya mimi na Rahma kukaa sehemu moja bila kusemeshana, tena mara nyingi tulikuwa tukicheka na kufurahi.
Dakika kadhaa baadaye, Rahma alibadili mkao aliokuwa amekaa, akanisogelea halafu akawa ni kama ameniegamia kimtindo, haikuwa rahisi kwa watu wengine kuelewa kilichokuwa kinaendelea lakini kiukweli nilijikuta nikipata msisimko mkubwa sana.
Mwisho niliamua kukata shauri maana na mimi nilikuwa nateseka, nikaamua liwalo na liwe, nikamgeukia Rahma na kumtazama usoni, naye akanigeukia, tukawa tunatazamana machoni, nikampa ishara kwamba atangulie ndani, akaniitikia huku akinitazama kwa macho yenye hisia kali za mapenzi.
Aliinuka na kutembea kwa madoido, nikawa namsindikiza kwa macho, nikawaona watu wote pale sebuleni wakitazamana. Nilishusha pumzi ndefu na kukaa vizuri kwenye kiti, nikawa navutia kasi ili na mimi niinuke na kumfuata Rahma kule ndani, tukatii kiu zetu.
“Togoo,” nilisikia sauti ya baba akiniita, nikaitika na kusimama, ilibidi nijiweke vizuri maana ilikuwa aibu kwa wote waliokuwa pale sebuleni, nikaelekea kule walikokuwa wamekaa baba na baba yake Rahma.
“Wewe sasa hivi una mambo ya kikubwa, hutakiwi kuwa unachanganyikana na wenzako, inabidi uanze kukaa na sisi baba zako, vuta kiti kaa hapa,” alisema baba, akawa ametibua shoo nzima, nilitaka kutoa visingizio lakini hakutaka kusikia chochote kutoka kwangu, ikabidi nikae na kujiinamia, wote wakawa wananitazama.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
 
SEHEMU YA 38:




ILIPOISHIA:
“Wewe sasa hivi una mambo ya kikubwa, hutakiwi kuwa unachanganyikana na wenzako, inabidi uanze kukaa na sisi baba zako, vuta kiti kaa hapa,” alisema baba, akawa ametibua shoo nzima, nilitaka kutoa visingizio lakini hakutaka kusikia chochote kutoka kwangu, ikabidi nikae na kujiinamia, wote wakawa wananitazama.
SASA ENDELEA…
“Una matatizo gani?” baba aliniuliza baada ya kuniona nikiwa nimekaa huku uso wangu nikiwa nimeukunja.
“Unajua hata sisi wote unaotuona hapa, kuna kipindi tulikuwa kama wewe, sote tulikuwa vijana hapa na tulipitia yote unayoyapitia, kwa hiyo usitake kujifanya mjanja, umenisikia?” baba alisema kwa msisitizo.
“Na nyie mlipitia mauzauza kama yangu? Kwa nini kila siku huniambii ukweli mimi ni nani?” kwa mara ya kwanza nilimpandishia baba sauti mbele ya baba yake Rahma, nikaona wameacha kucheza karata, wakawa wanatazamana kisha wote wakanigeukia.
“Sisi ni baba zako, hutakiwi kuzungumza kwa namna hiyo, umesikia mwanangu,” alisema baba yake Rahma huku akinipigapiga begani. Tofauti kati ya baba na baba yake Rahma, yeye alikuwa na busara na mpole lakini baba yeye alizoea kufokafoka tu.
“Hapana mimi nimechoka, kila siku nikimuuliza baba aniambie ukweli hataki, mauzauza yanazidi kunitokea kila siku, mambo ya ajabu yananikumba mimi tu, mbona ndugu zangu hakuna anayepata shida kama mimi,” nilisema kwa uchungu huku machozi yakianza kunilengalenga.
Baada ya kusema ya moyoni, niliegamia meza na kujilaza huku machozi yakinitoka, kiukweli nilikuwa na dukuduku kubwa sana moyoni. Hakuna kitu ambacho kilikuwa kikinikasirisha kama kitendo cha baba kuwa ‘ananikontroo’ kama roboti bila kunieleza ukweli uliokuwa nyuma ya maisha yangu.
“Najua kwamba mimi ni mwanaye, tena anayenipenda kuliko watoto wengine wote lakini kwa nini nipo tofauti? Kwa nini haniambii ukweli?” nilisema kwa kulalama, machozi yakiwa yanaendelea kunitoka.
“Kama anaweza kufikiria haya maana yake ni kwamba ameshapevuka kiakili, nafikiri ni muda muafaka wa yeye kuujua ukweli.”
“Hapana, bado hajakua huyu, ana mambo ya kitoto sana, mimi ndiyo namjua,” baba alisema, kauli ambayo ilinifanya niinuke pale mezani na kumkodolea baba macho. Yaani kumbe alikuwa anashindwa kunieleza ukweli kwa kipindi chote hicho kwa sababu tu alikuwa anahisi kwamba mimi bado nina akili za kitoto?
Kauli ile ilinifanya nijiulize maswali mengi yaliyokosa majibu. Kwa nini baba alikuwa ananiona mimi kama bado mtoto wakati tayari nilishapevuka na kuwa mwanaume kamili? Hata Rahma aliniambia kwamba mimi ni kidume cha mbegu, achilia mbali Isri aliyekuwa akinisifia sana. Na kama ni hivyo, mbona pale aliponiita alisema nimeshakua mkubwa kwa hiyo natakiwa kukaa nao?
“Kwa nini unaniona bado mdogo?”
“Kwa sababu huwezi kuelewa kitu kwa kuelezwa mara moja. Kila unachokatazwa kufanya wewe unafanya,” alisema baba na kurudia kauli yake kwamba hawezi kuniamini kwa asilimia mia moja mpaka nitakapomuonesha ukomavu wangu wa akili.
Kiukweli kwa kipengele hicho baba alikuwa amenishinda kwa pointi na udhaifu wangu mkubwa nilikuwa nimeuonesha kwenye suala zima la mapenzi. Nakumbuka tulianza kutofautiana na baba baada ya kukutana na Isri kwenye basi, akawa ananikataza kuwa naye karibu lakini nikampuuza.
Pia hata tulipofika kwa akina Rahma, mara kadhaa alishagundua kwamba tulikuwa na ukaribu usiofaa na akanikataza kwa msisitizo kwamba nisijaribu kukutana kimwili na Rahma, tena mpaka wakatumia kigezo kwamba sisi tulikuwa ndugu lakini bado tuliangukia dhambini, tena siyo mara moja.
Kubwa zaidi, hata hapo tulipokuwa tukizungumza, licha ya baba kunikataza kwamba endapo nitakutana kimwili tena na Rahma basi atakufa, kama wasingeniita na kunizuia, pengine muda huo ningekuwa ‘nikilitafunilia mbali tunda la mti uliokatazwa’ na Rahma.
Kama kigezo hicho pekee ndicho kilikuwa kinaonesha kwamba mtu amekuwa mkubwa, basi ni kweli nilikuwa nimefeli mtihani uliokuwa mbele yangu, nikawa mdogo kama ‘piriton’.
“Eti ni kweli anachokisema baba yako?” aliniuliza baba yake Rahma, nikakosa cha kujibu.
“Unajua kwa jinsi sisi baba zako tulivyo, na pengine wewe ukija kupata nafasi hiyo, hakuna kitu ambacho kinaheshimika kwenye jamii yetu kama utii. Ukiambiwa jambo ni lazima ufanye vilevile ulivyoambiwa na si vinginevyo, kosa dogo tu linaweza kusababisha matatizo makubwa mno ndiyo maana baba yako anakuwa mkali,” alisema baba yake Rahma.
>>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Kauli hiyo ilinifanya nijiulize maswali mengine mengi zaidi. Aliposema ‘jamii yetu’, baba yake Rahma alikuwa akimaanisha nini? Nilianza kupata picha kwamba huenda naye alikuwa anafahamu kila kitu kinachoendelea na kama alikuwa jamii moja na baba, basi moja kwa moja na yeye alikuwa akishughulika na mambo kama yale ya baba.
Tangu tumefika, baba yake Rahma hakuwahi kutoka kwamba labda anaenda kazini au kwenye biashara zake, muda wote alikuwa nyumbani tu lakini alikuwa na maisha ya hali ya juu sana. Nikiwa bado naendelea kujiuliza maswali mengi, baba yake Rahma alinisogelea.
“Baba yako anasema hakuamini kwa sababu bado una akili za kitoto lakini mimi nikikutazama nakiona kitu kikubwa sana ndani yako, tucheze dili?” aliniuliza kwa sauti ya chini huku akinikonyeza kwa jicho moja. Sikujua ni dili gani ila kwa sababu nilikuwa nataka kujua ukweli wa maisha yangu, nilitingisha kichwa kuonesha kumkubalia.
“Inatakiwa mimi na wewe tukazungumze lakini hatuwezi kuzungumzia humu ndani, inabidi tutoke nje! Lakini hapohapo, baba yako ameniambia kwamba kuna ‘madhambi’ mengine umeyafanya kiasi kwamba wewe na yeye hamuwezi kutoka mpaka giza liingie, ni kweli au si kweli?”
“Ni kweli.”
“Sasa mtihani wa kwanza, unatakiwa ukazivunje hizo nguvu zako za giza ulizozitega pale mlangoni.”
“Mimi sina nguvu zozote za giza wala sijatega chochote…” nilimkatisha lakini alinitazama usoni na kunikumbusha kwamba utii ni jambo muhimu sana, nikaufyata mkia.
“Unauona ule mlango, inatakiwa utembee kinyumenyume mpaka pale, ukiukaribia, unaugeukia lakini unatakiwa kufumba macho, kisha unakojoa mkojo wa kutosha kulowanisha eneo lote la mlango,” alisema baba yake Rahma, macho yakanitoka kama mjusi aliyebanwa na mlango.
“Hakuna kitu kinachoweza kuvunja na kumaliza kabisa nguvu za giza kama mkojo, haya fanya kama nilivyokwambia,” alisema baba yake Rahma. Ama kweli huo ulikuwa mtego mkali sana kwangu, yaani nikakojoe mlangoni, tena mahali ambapo watu wote waliokuwa sebuleni wangeweza kuniona?
Sikujua ndugu zangu watakichukuliaje kitendo hicho, wala sikujua Rahma na wadogo zake nao watanichukuliaje ila kwa sababu nilikuwa na shauku ya kuujua ukweli, nilipiga moyo konde.
>>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Wakati nikijiandaa kwenda, nilimsikia Rahma akiimba huku akitoka koridoni na kwenda kule sebuleni, nadhani alishachoka kusubiri na kuamua kunifuata, mtihani ukazidi kuwa mgumu. Ningemjibu nini Rahma endapo angeniuliza kwa nini nakojoa mlangoni wakati choo kipo, tena siyo kwamba nimelewa au naumwa, nina akili zangu timamu kabisa!
Baba na baba yake Rahma walikuwa wametulia wananitazama huku nikimuona baba uso wake ukionesha ishara kama anayesema ‘hawezi huyu, akili zake bado za kitoto’. Niliamua kujilipua, nikasema liwalo na liwe, nilisogea usawa wa mlango, nikageuka na kuupa mgongo, nikaanza kutembea kinyumenyume kuuelekea kisha nikafumba macho, nilipoukaribia, niligeuka, macho nikiwa nimeyafumba.
Nilifungua zipu kisha nikaanza kufanya kama vile nilivyoelekezwa. Nikiwa naendelea na kitendo kile cha aibu na cha aina yake, nilisikia watu wote waliokuwa sebuleni wakishtuka, nadhani waliniona nilichokuwa nakifanya, sikuwajali, nikaendelea kuumwaga, mara kilisikika kishindo kikubwa ambacho kilinifanya nishindwe kuendelea kufumba macho, nikayafumbua.
“Mungu wangu!” nilisema kwa sauti ya juu.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue
 
SEHEMU YA 38:



ILIPOISHIA:
“Wewe sasa hivi una mambo ya kikubwa, hutakiwi kuwa unachanganyikana na wenzako, inabidi uanze kukaa na sisi baba zako, vuta kiti kaa hapa,” alisema baba, akawa ametibua shoo nzima, nilitaka kutoa visingizio lakini hakutaka kusikia chochote kutoka kwangu, ikabidi nikae na kujiinamia, wote wakawa wananitazama.
SASA ENDELEA…
“Una matatizo gani?” baba aliniuliza baada ya kuniona nikiwa nimekaa huku uso wangu nikiwa nimeukunja.
“Unajua hata sisi wote unaotuona hapa, kuna kipindi tulikuwa kama wewe, sote tulikuwa vijana hapa na tulipitia yote unayoyapitia, kwa hiyo usitake kujifanya mjanja, umenisikia?” baba alisema kwa msisitizo.
“Na nyie mlipitia mauzauza kama yangu? Kwa nini kila siku huniambii ukweli mimi ni nani?” kwa mara ya kwanza nilimpandishia baba sauti mbele ya baba yake Rahma, nikaona wameacha kucheza karata, wakawa wanatazamana kisha wote wakanigeukia.
“Sisi ni baba zako, hutakiwi kuzungumza kwa namna hiyo, umesikia mwanangu,” alisema baba yake Rahma huku akinipigapiga begani. Tofauti kati ya baba na baba yake Rahma, yeye alikuwa na busara na mpole lakini baba yeye alizoea kufokafoka tu.
“Hapana mimi nimechoka, kila siku nikimuuliza baba aniambie ukweli hataki, mauzauza yanazidi kunitokea kila siku, mambo ya ajabu yananikumba mimi tu, mbona ndugu zangu hakuna anayepata shida kama mimi,” nilisema kwa uchungu huku machozi yakianza kunilengalenga.
Baada ya kusema ya moyoni, niliegamia meza na kujilaza huku machozi yakinitoka, kiukweli nilikuwa na dukuduku kubwa sana moyoni. Hakuna kitu ambacho kilikuwa kikinikasirisha kama kitendo cha baba kuwa ‘ananikontroo’ kama roboti bila kunieleza ukweli uliokuwa nyuma ya maisha yangu.
“Najua kwamba mimi ni mwanaye, tena anayenipenda kuliko watoto wengine wote lakini kwa nini nipo tofauti? Kwa nini haniambii ukweli?” nilisema kwa kulalama, machozi yakiwa yanaendelea kunitoka.
“Kama anaweza kufikiria haya maana yake ni kwamba ameshapevuka kiakili, nafikiri ni muda muafaka wa yeye kuujua ukweli.”
“Hapana, bado hajakua huyu, ana mambo ya kitoto sana, mimi ndiyo namjua,” baba alisema, kauli ambayo ilinifanya niinuke pale mezani na kumkodolea baba macho. Yaani kumbe alikuwa anashindwa kunieleza ukweli kwa kipindi chote hicho kwa sababu tu alikuwa anahisi kwamba mimi bado nina akili za kitoto?
Kauli ile ilinifanya nijiulize maswali mengi yaliyokosa majibu. Kwa nini baba alikuwa ananiona mimi kama bado mtoto wakati tayari nilishapevuka na kuwa mwanaume kamili? Hata Rahma aliniambia kwamba mimi ni kidume cha mbegu, achilia mbali Isri aliyekuwa akinisifia sana. Na kama ni hivyo, mbona pale aliponiita alisema nimeshakua mkubwa kwa hiyo natakiwa kukaa nao?
“Kwa nini unaniona bado mdogo?”
“Kwa sababu huwezi kuelewa kitu kwa kuelezwa mara moja. Kila unachokatazwa kufanya wewe unafanya,” alisema baba na kurudia kauli yake kwamba hawezi kuniamini kwa asilimia mia moja mpaka nitakapomuonesha ukomavu wangu wa akili.
Kiukweli kwa kipengele hicho baba alikuwa amenishinda kwa pointi na udhaifu wangu mkubwa nilikuwa nimeuonesha kwenye suala zima la mapenzi. Nakumbuka tulianza kutofautiana na baba baada ya kukutana na Isri kwenye basi, akawa ananikataza kuwa naye karibu lakini nikampuuza.
Pia hata tulipofika kwa akina Rahma, mara kadhaa alishagundua kwamba tulikuwa na ukaribu usiofaa na akanikataza kwa msisitizo kwamba nisijaribu kukutana kimwili na Rahma, tena mpaka wakatumia kigezo kwamba sisi tulikuwa ndugu lakini bado tuliangukia dhambini, tena siyo mara moja.
Kubwa zaidi, hata hapo tulipokuwa tukizungumza, licha ya baba kunikataza kwamba endapo nitakutana kimwili tena na Rahma basi atakufa, kama wasingeniita na kunizuia, pengine muda huo ningekuwa ‘nikilitafunilia mbali tunda la mti uliokatazwa’ na Rahma.
Kama kigezo hicho pekee ndicho kilikuwa kinaonesha kwamba mtu amekuwa mkubwa, basi ni kweli nilikuwa nimefeli mtihani uliokuwa mbele yangu, nikawa mdogo kama ‘piriton’.
“Eti ni kweli anachokisema baba yako?” aliniuliza baba yake Rahma, nikakosa cha kujibu.
“Unajua kwa jinsi sisi baba zako tulivyo, na pengine wewe ukija kupata nafasi hiyo, hakuna kitu ambacho kinaheshimika kwenye jamii yetu kama utii. Ukiambiwa jambo ni lazima ufanye vilevile ulivyoambiwa na si vinginevyo, kosa dogo tu linaweza kusababisha matatizo makubwa mno ndiyo maana baba yako anakuwa mkali,” alisema baba yake Rahma.
>>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Kauli hiyo ilinifanya nijiulize maswali mengine mengi zaidi. Aliposema ‘jamii yetu’, baba yake Rahma alikuwa akimaanisha nini? Nilianza kupata picha kwamba huenda naye alikuwa anafahamu kila kitu kinachoendelea na kama alikuwa jamii moja na baba, basi moja kwa moja na yeye alikuwa akishughulika na mambo kama yale ya baba.
Tangu tumefika, baba yake Rahma hakuwahi kutoka kwamba labda anaenda kazini au kwenye biashara zake, muda wote alikuwa nyumbani tu lakini alikuwa na maisha ya hali ya juu sana. Nikiwa bado naendelea kujiuliza maswali mengi, baba yake Rahma alinisogelea.
“Baba yako anasema hakuamini kwa sababu bado una akili za kitoto lakini mimi nikikutazama nakiona kitu kikubwa sana ndani yako, tucheze dili?” aliniuliza kwa sauti ya chini huku akinikonyeza kwa jicho moja. Sikujua ni dili gani ila kwa sababu nilikuwa nataka kujua ukweli wa maisha yangu, nilitingisha kichwa kuonesha kumkubalia.
“Inatakiwa mimi na wewe tukazungumze lakini hatuwezi kuzungumzia humu ndani, inabidi tutoke nje! Lakini hapohapo, baba yako ameniambia kwamba kuna ‘madhambi’ mengine umeyafanya kiasi kwamba wewe na yeye hamuwezi kutoka mpaka giza liingie, ni kweli au si kweli?”
“Ni kweli.”
“Sasa mtihani wa kwanza, unatakiwa ukazivunje hizo nguvu zako za giza ulizozitega pale mlangoni.”
“Mimi sina nguvu zozote za giza wala sijatega chochote…” nilimkatisha lakini alinitazama usoni na kunikumbusha kwamba utii ni jambo muhimu sana, nikaufyata mkia.
“Unauona ule mlango, inatakiwa utembee kinyumenyume mpaka pale, ukiukaribia, unaugeukia lakini unatakiwa kufumba macho, kisha unakojoa mkojo wa kutosha kulowanisha eneo lote la mlango,” alisema baba yake Rahma, macho yakanitoka kama mjusi aliyebanwa na mlango.
“Hakuna kitu kinachoweza kuvunja na kumaliza kabisa nguvu za giza kama mkojo, haya fanya kama nilivyokwambia,” alisema baba yake Rahma. Ama kweli huo ulikuwa mtego mkali sana kwangu, yaani nikakojoe mlangoni, tena mahali ambapo watu wote waliokuwa sebuleni wangeweza kuniona?
Sikujua ndugu zangu watakichukuliaje kitendo hicho, wala sikujua Rahma na wadogo zake nao watanichukuliaje ila kwa sababu nilikuwa na shauku ya kuujua ukweli, nilipiga moyo konde.
>>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Wakati nikijiandaa kwenda, nilimsikia Rahma akiimba huku akitoka koridoni na kwenda kule sebuleni, nadhani alishachoka kusubiri na kuamua kunifuata, mtihani ukazidi kuwa mgumu. Ningemjibu nini Rahma endapo angeniuliza kwa nini nakojoa mlangoni wakati choo kipo, tena siyo kwamba nimelewa au naumwa, nina akili zangu timamu kabisa!
Baba na baba yake Rahma walikuwa wametulia wananitazama huku nikimuona baba uso wake ukionesha ishara kama anayesema ‘hawezi huyu, akili zake bado za kitoto’. Niliamua kujilipua, nikasema liwalo na liwe, nilisogea usawa wa mlango, nikageuka na kuupa mgongo, nikaanza kutembea kinyumenyume kuuelekea kisha nikafumba macho, nilipoukaribia, niligeuka, macho nikiwa nimeyafumba.
Nilifungua zipu kisha nikaanza kufanya kama vile nilivyoelekezwa. Nikiwa naendelea na kitendo kile cha aibu na cha aina yake, nilisikia watu wote waliokuwa sebuleni wakishtuka, nadhani waliniona nilichokuwa nakifanya, sikuwajali, nikaendelea kuumwaga, mara kilisikika kishindo kikubwa ambacho kilinifanya nishindwe kuendelea kufumba macho, nikayafumbua.
“Mungu wangu!” nilisema kwa sauti ya juu.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue
 
SEHEMU YA 39:




ILIPOISHIA:
Nilifungua zipu kisha nikaanza kufanya kama vile nilivyoelekezwa. Nikiwa naendelea na kitendo kile cha aibu na cha aina yake, nilisikia watu wote waliokuwa sebuleni wakishtuka, nadhani waliniona nilichokuwa nakifanya, sikuwajali, nikaendelea kuumwaga, mara kilisikika kishindo kikubwa ambacho kilinifanya nishindwe kuendelea kufumba macho, nikayafumbua.
“Mungu wangu!” nilisema kwa sauti ya juu.
SASA ENDELEA…
Kile kilichokuwa kikinitoka, hakikuwa haja ndogo kama mwenyewe nilivyokuwa nadhani, ilikuwa ni damu, tena nzito kabisa yenye wekundu uliokolea kisawasawa, na kile kishindo kilichosikika, kilikuwa ni cha dude kubwa lililoanguka kutoka angani.
Sijui niliiteje dude hilo kwa sababu kwanza lilikuwa na miiba kama nungunungu, lakini pia lilikuwa na mabawa yenye kucha kama popo, ukubwa wake ulikuwa kama ng’ombe mdogo.
Usoni lilikuwa na pembe zilizojikunja na sehemu ya macho, kulikuwa kumezibwa kabisa, kwa kifupi halikuwa na macho. Ile damu iliendelea kunitoka, hata pale nilipotaka kuikata haja ndogo, iliendelea kunitoka kwa wingi utafikiri inavutwa na bomba.
Lile dude la ajabu, lilijiburuta chini na kusogea mpaka pale nilipokuwa natolea haja ndogo, kwenye vizingiti vya milango, likafumbua mdomo kidogo na kutoa ulimi mrefu uliokuwa umegawanyika katikati kama wa nyoka, likaanza kulamba kile nilichokuwa nakitoa.
Naomba nieleze vizuri kilichotokea na ambacho huwa kinatokea pale mtu anapokumbwa na nguvu za uchawi. Yaani tukio unaliona, na ile hatari iliyopo mbele yako unaiona kabisa lakini mwili unakufa ganzi, unakuwa huwezi kufanya chochote zaidi ya kile ambacho unakuwa umeshaanza kukifanya na akili zako zinakosa maamuzi, kwa kifupi unakuwa siyo wewe.
>>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Hicho ndicho kilichotokea, sikuwa na uwezo wa kuikatisha ile haja ndogo ya damu, sikuwa na uwezo wa kwenda mbele, wala sikuwa na uwezo wa kurudi nyuma, nilitamani kupiga kelele za kuomba msaada lakini pia sikuweza kufanya hivyo, nikabaki nimeduwaa tu.
Lile dude lililamba ile damu yote pale mlangoni, likaona haitoshi, likafumbua mdomo wake ambao ulikuwa na meno mengi na kukinga ile iliyokuwa ikiendelea kunitoka kupitia haja ndogo, nikasikia kitu kama ganzi ikinipata kwenye maeneo yangu nyeti kisha ile damu ikakata.
Lile dude ambalo ama kwa hakika lilikuwa linatisha, likajilamba na kugeuka, likajikung’uta kwa nguvu kwenye mabawa yake yenye kucha kubwa na kali, likawa kama linataka kuruka kwani lilipigapiga mbawa zake, kufumba na kufumbua, likayeyuka na kupotea.
Lilipopotea tu, nilihisi kichwa kikiwa kizito, nikaanza kuona giza machoni mwangu, nikawa nasikia sauti za ajabuajabu masikioni, nikadondoka chini kama mzigo. Sikuelewa tena kilichoendelea.
***
Nilipokuja kuzinduka, nilijikuta nimelala chini kwenye majani, mwili wangu ukiwa unahisi baridi kali kuliko kawaida. Kilichonizindua zilikuwa ni kelele za ngoma na manyanga na sauti za ajabuajabu za watu wakiimba nyimbo kwa lugha ambayo sikuwa naielewa.
Nilifumbua macho, huku mapigo yangu ya moyo yakiwa yananienda mbio kuliko kawaida, macho yangu yalitazama juu moja kwa moja. Nikawa naziona nyotanyota kwa mbali kuashiria kwamba ni usiku sana, lakini pia upande wangu wa kushoto, kulikuwa kumewashwa moto mkubwa ambao ulipafanya pale nilipolala, pawe na mwanga.
Niligeuza shingo kutazama pale ni wapi, nilishtuka kugundua kwamba kumbe nilikuwa katikati ya duara, watu wengi waliokuwa hawana kitu mwilini zaidi ya kujiziba kidogo na nguo nyeusi au nyekundu kwenye maeneo nyeti walikuwa wamenizunguka. Wengine ambao ni wanawake, walikuwa wamejiziba pia vifuani mwao.
>>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Walikuwa wakiimba na kucheza kwa kuzunguka duara ambalo ndani yake nilikuwa nimelazwa mimi na pia kulikuwa na moto mkubwa jirani kidogo na pale nilipokuwa nimelala. Walikuwa wakiimba na kucheza, huku kila mmoja akionesha kuwa na furaha kubwa.
Nilishtuka mno, nikawa sielewi pale ni wapi na nimefikaje, nilijaribu kuwatazama watu hao kwenye nyuso zao kama kuna yeyote ninayeweza kumtambua lakini macho yangu hayakuwa na nguvu za kutosha kuona. Nilitaka kusimama lakini nilishtuka zaidi kugundua kwamba kumbe nilikuwa nimefungwa mikono na miguu kwa kamba za miti.
Zile purukushani zangu, ziliwafanya wale watu waache kila walichokuwa wanakifanya, wote wakawa wananitazama. Niligeuka huku na kule, wote walikuwa wamenikazia macho. Kilichozidi kunitisha, macho yao yalikuwa yakiwaka kama wanyama wakali wa porini.
Nikamsikia mmoja kati yao akizungumza kwa lugha ambayo sikuwa naielewa, watu wote wakainua mikono juu kisha taratibu wakaishusha chini, wakati wakishusha mikono, nao walishuka mpaka wakapiga magoti, wakapeleka vichwa vyao mpaka chini kisha wakainuka na kusimama kama mwanzo.
Yule mwanaume ambaye sikuwa najua yupo upande gani, aliyarudia tena maneno yale, wakafanya hivyo tena mpaka chini, wakarudia mara tatu kisha wote wakakaa chini na kukunja miguu.
Kizee kimoja kilichokuwa kimepinda mgongo, kiliibuka kutoka kusikojulikana, kikiwa kinatembelea mkongojo. Kikawa kinajikongoja kuja pale nilipokuwa nimefungwa, kadiri kilivyokuwa kinanikaribia ndivyo mapigo ya moyo wangu yalivyokuwa yakizidi kuongezeka.
Sikujua kinataka kunifanya nini, kilisogea mpaka pale nilipokuwa nimefungwa, nikakiona kikitoa kisu kikali, kikaniinamia huku kikiyumbayumba, nikajua nimekwisha. Nimewahi kusikia kwamba wachawi wana mchezo wa kuchinja watu na kuwala nyama, nikajua na mimi ndiyo siku yangu ya kuliwa imewadia.
Tofauti na nilivyotegemea, wala hakunidhuru mwilini, badala yake alikitumia kile kisu kukata kamba nilizofungwa mikononi na miguuni. Kilichonishangaza zaidi, kumbe alikuwa akinijua mpaka jina langu kamili.
“Togolai!”
“Naam, shikamoo babu,” niliitikia kwa kutetemeka. Hakujibu salamu yangu, badala yake alinionesha sehemu ya kukaa, akaniambia kwa ishara nikunje miguu kama watu wengine wote walivyokuwa wamekaa. Nilitii agizo hilo haraka.
Kumbe pembeni ya pale nilipokuwa nimelazwa, kulikuwa na vifaa mbalimbali, nikamuona akichukua kibuyu kimoja, akakitingisha kisha akanipa na kunionesha kwa ishara kwamba ninywe kilichomo ndani.
Huku nikitetemeka, nilikishika kibuyu hicho, nikawa nakipeleka mdomoni huku nikimtazama kwa kina mzee huyo, pamoja na watu wengine waliokuwa wamenizunguka kwa mbali.
“Nwa, ulogoleza shoni, nwa!” aliongea kwa kilugha ambacho sikuwa nakielewa lakini kwa jinsi matamshi yake yalivyokuwa, nilihisi ananiambia, ‘kunywa, unaogopa nini, kunywa’.
Nilipokisogeza kibuyu hicho karibu na pua, nilikumbana na harufu kali kwelikweli, ikabidi nizibe pua, nikanywa huku nikiwa nimefumba macho. Kabla sijameza, nilisikia vitu vikinitembea mdomoni, nilipotazama vizuri kile kibuyu, pale kwenye mdomo wa kunywea, sikuyaamini macho yangu, nikataka kutema lakini tayari nilishachelewa, vitu vyote vilikimbilia tumboni vyenyewe.
Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 40:



ILIPOISHIA:
Nilipokisogeza kibuyu hicho karibu na pua, nilikumbana na harufu kali kwelikweli, ikabidi nizibe pua, nikanywa huku nikiwa nimefumba macho. Kabla sijameza, nilisikia vitu vikinitembea mdomoni, nilipotazama vizuri kile kibuyu, pale kwenye mdomo wa kunywea, sikuyaamini macho yangu, nikataka kutema lakini tayari nilishachelewa, vitu vyote vilikimbilia tumboni vyenyewe.
SASA ENDELEA…
Pale kwenye sehemu ya kunywea, ndipo paliponipa picha kwamba nilichokunywa kilikuwa ni kitu gani. Minyoo mingi ya rangi mbalimbali, ilikuwa imechanganywa na maji machungu yenye harufu mbaya mno. Jambo lile, la kugundua kwamba nilikuwa nimekunywa minyoo, lilinifanya nisisimke sana, nilijaribu kujitapisha lakini ilikuwa sawa mna kazi bure.
Kwa jinsi minyoo yenyewe ilivyokuwa imechangamka, muda mfupi tu baadaye, nilisikia tumbo likianza kutibuka, hofu kubwa ikanitanda ndani ya moyo wangu. Sikujua nini itakuwa hatma yangu.
Yule babu alikichukuaa kibuyo na kukifunga, akakirudisha pale chini, nikamuona akichaguachagua na muda mfupi baadaye, alichukua kibuyu kingine lakini hiki kilikuwa kidogo kuliko kile cha awali. Akawatazama wale watu wengine waliokuwa wamekaa pembeni na kutulia kisha akawapa ishara fulani, nikaona wanaume wawili wakiinuka.
Wakatembea harakaharaka kusogea mpaka pale nilipokuwa nimekalishwa. Sikutaka kuyaamini macho yangu, ilibidi nijifikiche macho nikidhani labda nipo ndotoni.
Haikuwa ndoto, ilikuwa ni kweli kabisa. Mbele yangu walikuwa wamesimama baba na baba yake Rahma. Niliwatazama mmoja baada ya mwingine, bado nikawa siamini. Nao walikuwa wamevaa kama wale watu wengine, walijistiri kidogo tu lakini sehemu kubwa ya miili yao ilikuwa wazi.
Ni hapo ndipo nilipoielewa kauli ya baba yake Rahma aliyoitoa muda mfupi kabla ya yale mauzauza hayajanitokea, kwamba eti utii ni jambo muhimu sana na la lazima kwa jamii yao. Kumbe urafiki au ukaribu wa baba na baba yake rahma ulikuwa zaidi ya vile kila mmoja alivyokuwa akiamini.
>>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Yule mzee alimtazama baba, baba naye akamtazama kisha kichwa chake akakiinamisha kwa utii, yule babu akawa anaongea kwa lugha ambayo hata sikuwa naielewa, baba naye akawa anamfuatisha anachokisema, muda mfupi baadaye baba yake Rahma naye alikuwa akifuatisha walichokuwa wanakisema.
Muda mfupi baadaye, walinizunguka na kutengeneza kama duara jingine hivi, wakawa wanaendelea kuzungumza yale maneno kwa sauti ya juu, muda mfupi baadaye wale watu wengine nao walidakia, wakawa wanawafuatisha. Ilivyoonesha, wote walikuwa wakiielewa vizuri lugha ile maana hakuna aliyekuwa akibabaika.
Baadaye, yule mzee alitoa ishara, watu wote wakanyamaza, akaanza kuzungumza lakini safari hii, alikuwa akiongea Kiswahili japo ilionesha hakuwa akikielewa vizuri. Akawaambia watu wote kwamba anayo furaha kubwa kukutana nao usiku huo na furaha yake iliongezwa zaidi na tukio lililokuwa likifanyika usiku huo.
Aliwaambia watu wote kwamba kulikuwa na utambulisho wa mwanachama mpya, akanitaka nisimame. Nilishtuka sana, mwanachama mpya? Wa nini? Ina maana kile ni chama? Kinahusika na nini? Sikuwa na majibu. Nilimgeukia baba, naye akanigeukia, akanipa ishara kwamba nitulie.
Yule babu alimkabidhi baba kile kibuyu, nikamuona akirudi tena pale palipokuwa na vifaa vingine, akachaguachagua kisha nikamuona akichukua kitambaa cheusi, au wengine wanapenda kuita kaniki. Alimpa baba, akainamisha kichwa chake kama ishara ya utii, kisha yule babu akaendelea kuzungumza na kila mtu.
Alisema hatua ya kwanza natakiwa kukabidhiwa vifaa kwa ajili ya kazi kisha baada ya hapo, nitatawazwa rasmi kuwa mwanachama kamili, watu wote wakalipuka kwa shangwe za kila namna. Zilikuwa ni kelele kubwa sana, kila mtu akionesha kuwa na furaha sana.
Baba aliniinamia, akaongea kwa sauti ya chini akiniambia nivue suruali niliyokuwa nimevaa maana mpaka muda huo nilikuwa kifua wazi. Niliona kama ni jambo lisilowezekana, yaani nivue nguo wakati watu wote wananitazama? Macho yakanitoka.
>>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Ni kama baba alinielewa, alinipa na ile kaniki, akanionesha kwa ishara kwamba nijifunge juu ya suruali kisha ndiyo niiteremshe. Nilifanya hivyo, muda mfupi baadaye, nilikuwa nimeshaivua na kujifunga kaniki. Sasa na mimi nilikuwa nikifanana na wale watu isipokuwa mimi nilijifunga kaniki ndefu wakati wengine wote walikuwa wamejifunika kwa vipande vidogo.
Nilikalishwa chini, yule babu akampa ishara baba, akanisogelea na kupiga magoti, akanikabidhi kile kibuyu kilichokuwa kimevalishwa shanga, kisha akaongea kwa sauti ya chini akinitaka nisiogope chochote na nimthibitishie kwamba kweli nimekuwa mtu mzima na si mtoto kama alivyokuwa akiamini. Nilitingisha kichwa, japokuwa hakuwa ameniambia chochote, tayari nilishaelewa kilichokuwa kinaendelea.
Nilipokabidhiwa kile kibuyu, baba na baba yake Rahma waliondoka na kurudi kwenye sehemu zao, yule babu akaniambia nishike kibuyu hicho kwa mikono miwili kisha nikiinue mbele ya uso wangu.
Nilifanya kama alivyoniambia, nikamuona akichukua karai la chuma lenye maji meusi ndani yake, akanimwagia kichwani kisha kwa kutumia kisu kikali, alianza kuninyoa nywele. Sikuwahi kuona mtu akinyolewa nywele kwa siku, hata kule kijijini kwetu ambako saluni zilikuwa chache, tulikuwa tukinyolewa kwa wembe au mkasi.
Kwa kawaida nywele zangu huwa ni nguvu na wakati wa kunyoa huwa ni shughuli kwelikweli lakini huwezi kuamini, yule babu alipitisha mara kadhaa tu, kichwa kikawa cheupe kabisa. Alichukua dawa kutoka kwenye kichupa kimoja kisha akanisogelea, akarudia kunisisitiza kwamba sitakiwi kuachia kibuyu hicho kwani ndiyo maisha yangu.
Alichokifanya, kwa kutumia kilekile kisu, alianza kunichanja chake, kuanzia kichwani, akaja shingoni upande wa nyuma, akashuka mgongoni mpaka miguuni. Kiukweli maumivu niliyokuwa nayasikia yalikuwa makali sana, yote tisa, kumi ni pale alipoanza kunisugua sehemu alizonichanja kwa kutumia ile dawa iliyokuwa kwenye kile kichupa.
Maumivu ya kuchanjwa ukijumlisha na ukali wa ile dawa, nilishindwa kujizuia, nikawa nalia kwa maumivu.
“Kumbe hujakuwa mrume wewe,” alisema yule babu kwa Kiswahili kibovu lakini ambacho kilinifanya nimuelewe. Alimaanisha kwamba eti bado nilikuwa mtoto ndiyo maana nilikuwa nalia. Hakuna kitu ambacho nilikuwa nakichukia kama kuitwa mtoto. Japokuwa nilikuwa nikijisikia maumivu makali, ilibidi nijikaze, akaendelea kunisugua na ile dawa huku nikigugumia kwa maumivu.
Damu nyingi ilikuwa ikinitoka kwenye majeraha yangu lakini safari hii sikujali, sikutaka kuonekana mtoto, yule babu akaendelea mpaka alipomaliza. Baada ya kumaliza, alinishika mkono na kunisimamisha, akanisogeza kwenye ule moto.
Ni hapo ndipo nilipogundua kwamba kumbe pale kulikuwa na nyama nyingi ya kutosha imewekwa pembeni ya moto. Yule babu aliinama pale kwenye nyama, akatoka na kipande kimoja, akanifuata na kunipa.
Kwa akili yangu nilielewa kwamba ananipa ili niichome kwenye moto ikiiva ndiyo niile, nikashangaa ananiambia eti niile vilevile ikiwa mbichi. Nilishtuka sana maana ilikuwa bado na damudamu kabisa.
Nilitamani kumuuliza kwanza ile ni nyama ya nini lakini nilikumbuka kauli ya baba yake rahma na aliyoniambia baba muda mfupi uliopita kwamba natakiwa kuwa mtiifu, ikabidi nifumbe macho, nikaitia mdomoni na kutaka kuimeza bila kutafuna lakini ilikuwa kubwa, ikabidi nipige moyo konde, nikaanza kuitafuna kisha harakaharaka nikameza.
“Twive umile,” alisema yule mzee huku akinionesha kwa ishara kwamba nifumbue mdomo. Sijui kile ni kilugha alichokuwa akizungumza, nilifanya kama alivyoniambia, nikafumbua mdomo. Nadhani alitaka kuhakikisha kama nimemeza, alipohakikisha, alinishika mkono na kuuinua juu kama wanavyofanya waamuzi wa mapambano ya ndondi wanapomtangaza msshi ulingoni.
Watu wote walishangilia kwa nguvu, wengine nikawaona wakirukaruka kwa furaha, ikabidi na mimi nifurahi ingawa bado nilikuwa gizani. Yule mzee aliniachia mkono na kuanza kuzungumza na wale watu, akiwataka wanipe ushirikiano na kunifundisha yale nisiyoyajua.
Wakati anaongea hayo, sijui nini kilinituma nitazame pale zilipokuwepo zile nyama, nikashtuka kuliko kawaida kuona kuna viungo vya binadamu, viganja vya mikono na miguu. Ile nyama aliyonipa aliichukua palepale, kwa hiyo alikuwa amenipa nyama ya mtu? Macho yalinitoka nikiwa siamini macho yangu.
Nikiwa bado nashangaa, mwili ukiwa unatetemeka kwa hofu, nilishtukia wale watu wakikimbilia pale kwenye moto na kujipanga foleni, yule babu akasogea kwenye zile nyama, akawa anagawa, kila mmoja anapita na kupewa kipande chake kisha anatafuta sehemu ya kwenda kukaa na kuanza kula. Nilihisi kama nipo ndotoni lakini haikuwa hivyo.
“Hongera, umekuwa sasa,” alisema baba huku akinikumbatia, akanishika mkono na kunipeleka kwenye foleni, akaniingiza kwenye foleni.
Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 41:



ILIPOISHIA:
Nikiwa bado nashangaa, mwili ukiwa unatetemeka kwa hofu, nilishtukia wale watu wakikimbilia pale kwenye moto na kujipanga foleni, yule babu akasogea kwenye zile nyama, akawa anagawa, kila mmoja anapita na kupewa kipande chake kisha anatafuta sehemu ya kwenda kukaa na kuanza kula. Nilihisi kama nipo ndotoni lakini haikuwa hivyo.
“Hongera, umekuwa sasa,” alisema baba huku akinikumbatia, akanishika mkono na kunipeleka kwenye foleni, akaniingiza kwenye foleni.
SASA ENDELEA…
“Hapana baba, siwezi! Siwezi…” nilisema huku nikitaka kutoka kwenye foleni lakini baba alinishika mkono kwa nguvu. Nilikuwa natafuta upenyo ili nijitie vidole mdomoni kujitapisha ile nyama lakini ni kama baba alinishtukia.
Hakunipa upenyo hata kidogo, nikawa naendelea kutetemeka kwa hofu kubwa, nikiwa sielewi hatima ya yote yale itakuwa nini. Tofauti na mimi, watu wengine wote waliokuwepo eneo lile, akiwemo baba, baba yake Rahma na wale watu wengine wote, walikuwa na furaha kubwa ndani ya mioyo yao.
Kingine kilichonishangaza na kuniacha na maswali mengi, kila mtu aliyekuwa akifika pale mbele kwa yule babu aliyekuwa akigawa nyama, akikabidhiwa yake alikuwa akifurahi sana na kwenda kukaa pembeni na kuanza kuila bila wasiwasi wowote.
Nimewahi kusikia sana kuhusu stori za watu wanaokula nyama za watu lakini siku zote nilikuwa naona kama ni mambo ya kutunga, iweje mtu amle mwenzake? Ni hapo ndipo nilipoelewa kwamba kumbe siyo stori za kusadikika tu bali ni mambo ambayo yapo na yanafanyika kwa wingi.
Nilijiuliza sana, wale waliokuwa wakiliwa nyama ni akina nani? Walifanya makosa gani mpaka waliwe? Walikuwa wanaishi wapi na nyama zao zilifikishwaje pale? Je, walikuwa wanaume au wanawake, wakubwa au wadogo? Sikuwa na majibu.
Foleni ikawa ikazidi kusogea mbele, mwili wangu ulikuwa na maumivu sehemu mbalimbali, hasa yale maeneo ambayo yule babu alikuwa amenichanja lakini huwezi amini, kwa jinsi nilivyokuwa na hofu, wala sikuwa nasikia chochote.
Foleni iliendelea kusogea mbele, hofu ikazidi kunijaa lakini sikuwa na cha kufanya. Mara nilipata wazo, kwamba nikifika na kupewa nyama yangu, nijifanye naenda pembeni kuila lakini nikifika pembeni niitupe na tukirudi nyumbani, nitoroke na kurudi Chunya maana sikuwa tayari kwa kile kilichokuwa mbele yangu.
>>> Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
Ni kweli mara kadhaa nilijikuta nikitamani kuzijua mbinu mbalimbali za kichawi, kama kuweza kujilinda kwenye nyakati za hatari au kumuadhibu anayekuudhi lakini sikuwa tayari kuona nakuwa sehemu ya jamii hiyo iliyokuwa na mambo ya kutisha kiasi hicho.
Hatimaye zamu yangu iliwadia, yule mzee mgawaji, huku akijitafuna na damudamu zikiwa zimelowanisha mdomo wake, alinitazama usoni huku tabasamu pana likiwa limechanua kwenye uso wake.
Kuna kipande alikuwa amekishika mkononi lakini alipoona ni mimi, nilimuona akikirudisha pale chini palipokuwa na nyama nyingine nyingi, zikiwa zimewekwa juu ya majani ya migomba, akachaguachagua na muda mfupi baadaye, aliibuka na mnofu mkubwa wenye damudamu, akanipa huku akiinamisha kichwa kama ishara ya heshima.
Huku nikitetemeka nilipokea, macho yangu yakiwa hayatulii, nilikuwa nikilichunguza kwa umakini lile rundo la nyama pale chini ambalo sasa lilikuwa limepungua sana. Nilichokiona awali ndicho nilichokiona tena, kulikuwa na miguu iliyokatwa, viganja vya mikono na viungo vingine vya mwili.
Nikiri kwamba moyo wangu haujawahi kupatwa na hofu kama niliyoipata siku hiyo na kilichonitisha zaidi, ni pale nilipogundua kwamba katika rundo lile, kulikuwa na miguu na mikono ya watoto wadogo kabisa. Maskini… hawakuwa na hatia yoyote!
Baba naye alipewa kipande chake, akanishika mkono huku akiniongelesha kwa sauti ya chini. Aliniambia kwamba nina bahati sana kupewa heshima kubwa kama hiyo na mzee huyo ambaye baba aliniambia huwa wanamuita Mkuu kwa sababu ndiye kiongozi wao wa kanda. Akaniambia kwamba kitendo cha yeye kuinamisha kichwa chake tu, ilikuwa ni ishara kwamba amenikubali mno.
Hatukwenda mbali, tulikaa chini huku baba akinielekeza namna ya kukaa. Haukuwa ukaaji wa kawaida, mguu wa kushoto ulikuwa ukitangulia chini, kisha unakuja wa kulia halafu unakaa juu ya vifundo vya miguu yote miwili huku ukiwa umeikunja na kutengeneza alama ya V mbili.
Nilijaribu lakini miguu ikawa inaniuma sana, nilipowatazama watu wengine, wote walikuwa wamekaa kwa mtindo huo na wala hakukuwa na aliyekuwa akibabaika kama mimi, walikuwa wakiendelea kupiga stori za hapa na pale huku wakifurahia ‘kitoweo’, baba akaniambia atanifundisha taratibu.
Lile wazo langu la kwenda kuitupa ile nyama liliyeyuka kutokana na baba alivyonibana, ambapo muda mfupi baadaye, baba yake Rahma naye alikuja na kuungana na sisi pamoja na wanaume wengine watatu ambao sikuwa nawafahamu.
Kwa muda wote huo nilikuwa nikizugazuga tu kwani kiukweli sikuwa tayari kuila ile nyama ambayo ilikuwa ikichuruzika damu, mara kwa mara nilikuwa nikiitazama kwa woga, nikitamani hata niirushe mbali na kupiga kelele kwa hofu lakini haikuwezekana.
“Kula, muda unaenda,” baba aliniambia kwa kunihimiza, wale watu wengine ambao sikuwa nawafahamu, wakawa wanamuuliza baba mimi ni nani.
“Ni mwanangu, hamuoni tunavyofanana,” aliwajibu na wote wakawa wanampongeza kwa hatua ya kunisajili rasmi, wakawa wananipongeza na mimi wakiniambia kwamba sitajuta kujiunga na jamii yao. Kwa kuwa wote sasa walikuwa wakinitazama huku wakiendelea kunisifia, ilibidi nijikaze kiume maana baba alikuwa akinitazama kwa jicho kama la kunidharau hivi au kuonesha kwamba zile sifa nilizokuwa napewa sistahili.
>>> Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
“Umekua sasa si ndiyo?” baba yake Rahma aliniambia huku akinipigapiga begani na mkono wake uliokuwa na damu, mdomoni akiendelea kujitafuna. Nadhani aliongea hivyo kama kunikumbusha kile tulichokuwa tukitofautiana mara kwa mara na baba, akidai kwamba mimi bado nina akili za kitoto.
“Ndiyo,” nilimjibu kwa msisitizo, nikafumba macho na kupeleka ule mnofu mdomoni, nikaziba pua ili nisisikie hata harufu nikaanza kutafuna huku nikijikaza kisawasawa, sikuwa nataka kuonekana bado nina akili za kitoto kwa hiyo nilijikuta nikifanya kitu nisichopenda kukifanya ilimradi tu nimdhihirishie baba na baba yake Rahma kwamba sikuwa mtoto tena.
Mara kadhaa nilikuwa nikitaka kutapika lakini mwisho, hatimaye nilifanikiwa kuitia yote tumboni mwangu na kuufanya mwili wangu usisimke sana.
“Tafuna hii,” alisema baba yake Rahma huku akinipa vitu kama mizizi fulani hivi, nikavitafuna haraka na kuvimeza. Cha ajabu, mpaka muda huo, kumbe mimi ndiye niliyekuwa wa mwisho kumaliza ‘shea’ yangu, watu wote walikuwa wameshamaliza na sasa walikuwa wakipiga stori za hapa na pale.
“Vipi una swali lolote kwa kijana?” baba yake Rahma alimwambia baba kwa kejeli, nilishaelewa kwa nini amesema vile. Kwamba kwa sababu baba alikuwa ananiona kama nina akili za kitoto, je alikuwa na swali lingine lolote baada ya mimi kuonesha kile nilichokionesha pale mbele yao?
“Umenitoa aibu mwanangu, zawadi nitakayokupa hautakuja kuisahau maishani mwako,” aliniambia baba akionesha kuwa na furaha kubwa.
Mara sauti ya kama pembe la ng’ombe lililopulizwa kwa nguvu ilisikika, watu wote wakainuka walipokuwa wamekaa na kuanza kujipanga kwa mtindo wa duara kama ilivyokuwa mwanzo.
“Sasa hivi unaenda kukabidhiwa rasmi nguvu za giza ili uwe kama sisi, naomba ujasiri uliouonesha kwenye kula uuoneshe hapa pia, nenda pale ulipokuwa umekaa mwanzo,” baba aliniambia huku akinipigapiga begani kwa upole.
Kwa akili yangu nilijua kwamba tayari kazi imekwisha, kumbe kulikuwa na kazi nyingine, nikaanza kutetemeka tena huku nikigeuka huku na kule kuwatazama wale watu ambao wote walikuwa na nyuso za furaha. Nilipogeuka upande wa kushoto, nilimuona mtu aliyenifanya nishtuke mno, nilifikicha macho nikiwa ni kama siamini.
Je, nini kitafuatia? Usikose
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom