bioto
JF-Expert Member
- Oct 1, 2017
- 1,261
- 2,099
Riwaya:MACHO YA AJABU
Na:Humph de throne
WhatsApp:0629314605
Sehemu ya kwanza
Yapata karne kadhaa zimepita toka kipindi ambacho himaya kubwa ya mfalme Sangu akiwa kama mtawala mwenye nguvu Katika makabila mbalimbali yaliyokuwa yanaizunguka himaya yake, kabla ya kuwa na ngome hii isiyoingilika kirahisi kulikuwa na vita kubwa isiyoelezeka kati ya makabila haya yanayopatikana ukanda huo.
Mfalme Sangu alipoona hali ni tete ndipo aliamua kuwaita waganga wake wote ili afahamu wataisaidiaje himaya yao kwa kutumia nguvu hizo walizo nazo, walijitokeza waganga wengi wenye uwezo tofauti tofauti.
Mfalme Sangu alikuwa ni mtu mwenye akili sana alichokifanya ni kuwaambia kuwa "nataka wote muungane mjadili ni jinsi gani mtaikomboa himaya hii kwa njia yoyote ile mtakayoona inafaa"
Hilo lilikuwa agizo la mfalme kwahiyo haikuwa rahisi mtu awaye yote kupinga hivyo jopo hilo lilikaa chini na kuanza kutafakari, wa kwanza alinyoosha mkono kuashiria ana wazo, mwenyekiti wa kikao alimruhusu aongee "Mimi nafikiri ngome yote hii izindikwe haswaa ili iwe vigumu kwa maadui kuingia"
Mwenyekiti "asante kwa hoja naomba wanao kubaliana nae wanyooshe mikono" walijitokeza wengi kasoro mtu mmoja tu ambaye alionekana hajaafikiana nae
Mwenyekiti "Nashukuru kwa kumuunga mkono lakini bwana Mpao hapo nadhani unajambo lingine tofauti na wazo la mwenzio unaweza kutudokeza tafadhali?"
"Aaaaa! Ni kweli Mwenyekiti Mimi sipingi kwani ni wazo zuri tu ila mapendekezo yangu ningeomba tutengeneze kitu ambacho kinaweza kututabiria matukio yajayo nadhani hii inaweza kutusaidia kutambua udhaifu wa maadui zetu"
Mwenyekiti "ndugu zangu nafikiri mmemsikia bwana Mpao sasa ni wangapi wanakubaliana nae?"
Wote walinyoosha mikono kuashiria wamekubaliana lakini swali likawa ni kitu gani kitengenezwe, kimya kilitawala kwa dakika kadhaa ndipo mikono miwili iliibuka Mwenyekiti akamruhusu wa kwanza kisha atamalizia wa mwisho
"Ahsante ndugu Mwenyekiti kwa kunipa nafasi hii mimi napendelea tutengeneze hirizi ambayo mfalme ataifunga mkononi"
Mwenyekiti "wanaomuunga mkono tafadhali"
Wachache walinyoosha mikono ndipo alipomruhusu Mzee Mandevu nae atoe hoja yake "Kwa upande wangu mwenyekiti natazamia tuunde macho ya ajabu hii itakuwa hivi macho hayo yatakuwa hayaonekani kwa mtu wa kawaida na mvaaji wa macho hayo atakuwa kawaida kama awali hiyo itamsaidia kutambua tukio baya litakalotokea mda wowote ule"
Mwenyekiti "wangapi wanaungana na hoja ya mzee Mandevu"
Wote walikubali kwa kunyoosha mikono,Mwenyekiti akamkabidhi uongozi Mzee Mandevu katika hilo zoezi ambalo lilitakiwa kuanza kesho yake baada ya maandalizi.
Asubuhi na mapema shughuli ilianza chini ya mzee Mandevu na ilipofika jioni zana yao ilikuwa imekamilika ilikuwa na mng'ao kama wa dhahabu iliyo katika mtindo unaofanana na macho. Alikabidhiwa mfalme,alipoishika na kuanza kuikagua ghafla ikamrukia machoni mwanga mkali ukatokea eneo lote hilo ikawa kama maajabu mfalme alitetemeka kwa woga na hali ilipotulia alikuwa kama awali japo alijihisi tofauti na mwenye nguvu zaidi kuliko awali.
Mfalme akiwa amelala aliota maadui wanakuja kuivamia himaya yake alionyeshwa njia zote watakazopitia alipostuka kutoka usingizini alienda moja kwa moja kwa mkuu wa majeshi akamuelezea ambaye aliagiza vikosi vingi sana kuelekea sehemu alizoonyeshwa na mfalme katika ramani yao hivyo ndivyo himaya yake ilivyozidi kupanuka.
Baada ya kuja wakoloni mfalme Sangu aliuawa macho yale ya ajabu yalifichwa na wazee wenye busara katika mapango yenye michoro ya kale ili yasijekufikia katika mikono ya watu wabaya.
********Karne ya leo********
Tulikuwa katika safari ya kishule kutazama michoroya mapangoni tukijifunza kutokana na somo la historia linavyoelezea Mimi Humph na wanafunzi wenzangu katika kutembea tembea humo tukielezewa mambo mbalimbali Mimi niliona pembeni yangu kuna kama kapango kadogo halafu kuna giza lakini kulikuwa na kitu kinawaka waka.
Kwakuwa nilikuwa mbovu wa macho,miwani yangu ikiwa imeshika vyema katika paji la uso nikapuuzia, moyo uligoma kabisa kulipotezea hilo suala nikaamua kwenda,haikuniwia vigumu kuondoka katika kikundi chetu kwasababu nilikuwa wa mwishoni, nilisogea mpaka pale panapong'aa kama dhahabu nilipotaka kushika ili nijue ni kitu gani nilistukia kimenirukia machoni nikapiga kelele za kuomba msaada mwanga mkali ukasambaa kila kona katika hiyo sehemu ukitokea machoni mwangu,popo wengi waliruka wakanifanya
nizidi kupiga kelele kwa uoga....
Na:Humph de throne
WhatsApp:0629314605
Sehemu ya kwanza
Yapata karne kadhaa zimepita toka kipindi ambacho himaya kubwa ya mfalme Sangu akiwa kama mtawala mwenye nguvu Katika makabila mbalimbali yaliyokuwa yanaizunguka himaya yake, kabla ya kuwa na ngome hii isiyoingilika kirahisi kulikuwa na vita kubwa isiyoelezeka kati ya makabila haya yanayopatikana ukanda huo.
Mfalme Sangu alipoona hali ni tete ndipo aliamua kuwaita waganga wake wote ili afahamu wataisaidiaje himaya yao kwa kutumia nguvu hizo walizo nazo, walijitokeza waganga wengi wenye uwezo tofauti tofauti.
Mfalme Sangu alikuwa ni mtu mwenye akili sana alichokifanya ni kuwaambia kuwa "nataka wote muungane mjadili ni jinsi gani mtaikomboa himaya hii kwa njia yoyote ile mtakayoona inafaa"
Hilo lilikuwa agizo la mfalme kwahiyo haikuwa rahisi mtu awaye yote kupinga hivyo jopo hilo lilikaa chini na kuanza kutafakari, wa kwanza alinyoosha mkono kuashiria ana wazo, mwenyekiti wa kikao alimruhusu aongee "Mimi nafikiri ngome yote hii izindikwe haswaa ili iwe vigumu kwa maadui kuingia"
Mwenyekiti "asante kwa hoja naomba wanao kubaliana nae wanyooshe mikono" walijitokeza wengi kasoro mtu mmoja tu ambaye alionekana hajaafikiana nae
Mwenyekiti "Nashukuru kwa kumuunga mkono lakini bwana Mpao hapo nadhani unajambo lingine tofauti na wazo la mwenzio unaweza kutudokeza tafadhali?"
"Aaaaa! Ni kweli Mwenyekiti Mimi sipingi kwani ni wazo zuri tu ila mapendekezo yangu ningeomba tutengeneze kitu ambacho kinaweza kututabiria matukio yajayo nadhani hii inaweza kutusaidia kutambua udhaifu wa maadui zetu"
Mwenyekiti "ndugu zangu nafikiri mmemsikia bwana Mpao sasa ni wangapi wanakubaliana nae?"
Wote walinyoosha mikono kuashiria wamekubaliana lakini swali likawa ni kitu gani kitengenezwe, kimya kilitawala kwa dakika kadhaa ndipo mikono miwili iliibuka Mwenyekiti akamruhusu wa kwanza kisha atamalizia wa mwisho
"Ahsante ndugu Mwenyekiti kwa kunipa nafasi hii mimi napendelea tutengeneze hirizi ambayo mfalme ataifunga mkononi"
Mwenyekiti "wanaomuunga mkono tafadhali"
Wachache walinyoosha mikono ndipo alipomruhusu Mzee Mandevu nae atoe hoja yake "Kwa upande wangu mwenyekiti natazamia tuunde macho ya ajabu hii itakuwa hivi macho hayo yatakuwa hayaonekani kwa mtu wa kawaida na mvaaji wa macho hayo atakuwa kawaida kama awali hiyo itamsaidia kutambua tukio baya litakalotokea mda wowote ule"
Mwenyekiti "wangapi wanaungana na hoja ya mzee Mandevu"
Wote walikubali kwa kunyoosha mikono,Mwenyekiti akamkabidhi uongozi Mzee Mandevu katika hilo zoezi ambalo lilitakiwa kuanza kesho yake baada ya maandalizi.
Asubuhi na mapema shughuli ilianza chini ya mzee Mandevu na ilipofika jioni zana yao ilikuwa imekamilika ilikuwa na mng'ao kama wa dhahabu iliyo katika mtindo unaofanana na macho. Alikabidhiwa mfalme,alipoishika na kuanza kuikagua ghafla ikamrukia machoni mwanga mkali ukatokea eneo lote hilo ikawa kama maajabu mfalme alitetemeka kwa woga na hali ilipotulia alikuwa kama awali japo alijihisi tofauti na mwenye nguvu zaidi kuliko awali.
Mfalme akiwa amelala aliota maadui wanakuja kuivamia himaya yake alionyeshwa njia zote watakazopitia alipostuka kutoka usingizini alienda moja kwa moja kwa mkuu wa majeshi akamuelezea ambaye aliagiza vikosi vingi sana kuelekea sehemu alizoonyeshwa na mfalme katika ramani yao hivyo ndivyo himaya yake ilivyozidi kupanuka.
Baada ya kuja wakoloni mfalme Sangu aliuawa macho yale ya ajabu yalifichwa na wazee wenye busara katika mapango yenye michoro ya kale ili yasijekufikia katika mikono ya watu wabaya.
********Karne ya leo********
Tulikuwa katika safari ya kishule kutazama michoroya mapangoni tukijifunza kutokana na somo la historia linavyoelezea Mimi Humph na wanafunzi wenzangu katika kutembea tembea humo tukielezewa mambo mbalimbali Mimi niliona pembeni yangu kuna kama kapango kadogo halafu kuna giza lakini kulikuwa na kitu kinawaka waka.
Kwakuwa nilikuwa mbovu wa macho,miwani yangu ikiwa imeshika vyema katika paji la uso nikapuuzia, moyo uligoma kabisa kulipotezea hilo suala nikaamua kwenda,haikuniwia vigumu kuondoka katika kikundi chetu kwasababu nilikuwa wa mwishoni, nilisogea mpaka pale panapong'aa kama dhahabu nilipotaka kushika ili nijue ni kitu gani nilistukia kimenirukia machoni nikapiga kelele za kuomba msaada mwanga mkali ukasambaa kila kona katika hiyo sehemu ukitokea machoni mwangu,popo wengi waliruka wakanifanya
nizidi kupiga kelele kwa uoga....