Simulizi: Kwanini Mimi? 01

Simulizi: Kwanini Mimi? 01

gilbert35

JF-Expert Member
Joined
Nov 20, 2021
Posts
253
Reaction score
476
SIMULIZI YA MAISHA: KWANINI MIMI? 01
MWANDISHI : MIKA AUTHOR
MSAMBAZAJI: Simulizi za Gilbert
MAWASILIANO: +255621249611

Kuna kitu kisichokuwa cha kawaida kilikuwa kwenye maisha yao.Maisha yao yote,Baba tatu na mama tatu walikuwa wakitafutiana wapenzi wa pembeni,yaani mume ambaye ni baba tatu alikuwa akimtafutie mke wake wanaume,na mke ambaye ni mama tatu alikuwa anamtafutia mume wake wanawake.Kuna siri nzito iliyojificha nyuma yao.Kuijua siri iyo na mengine mengi ungana nami katika simulizi hii.

" Mume wangu jifiche.Akikuona ataogopa.Ingia jikoni ujifiche" mama tatu alimwambia mumewe.Na mumewe bila iyana aliingia jikoni kujificha.Baada ya kuona mumewe amejificha ,haraka sana mama tatu alimfata hans aliyekuwa naye chumbani na kutokana naye nje.

Wakati wanapita jikoni mama tatu alitoa macho kuangalia pale jikoni.Wakati anaangalia macho yake yalikutana na macho ya mumewe ambaye alikuwa anawachungulia .Alimbinyia jicho kisha atatoka na hans hadi nje .

" mmmmh ,aya mambo kuyafanyia nyumbani kwako ni hatari sana.Kwanza hata raha yenyewe inakuwa haipo.Siku nyingine tusikutania hapa" aliongea hans.

" Acha uwoga.Mbona mimi nimeenjoy tu" alijibu mama tatu.

" Basi ngoja mimi niende.Asije akatokea mume wako hapa halafu ikawa balaa" aliongea hans kisha akamkumbatia mama tatu na kumkiss .Kabla hajaondoka mama tatu alifungua pochi na kutoa elfu hamsini akamkabizi hans.

" shika hii itakusaidia kwa nauli" aliongea mama tatu.

Baada ya hans kuondoka.Mama tatu alirudi ndani na kumkuta mumewe bado yuko jikoni. " Ameshaondoka.Toka huko jikoni" aliongea mama tatu.

" ok sawa.Lakini kijamaa chako chenyewe mbona kinaonekana kioga sana" aliongea baba tatu.

" kibanadamu kawaida ,lazima awe mwoga" alijibu mama tatu.

" Halafu nimekumiss sana mke wangu." aliongea baba tatu huku akimshika mkono mkewe.

" mmmh! Unachotaka leo haiwezekani mume wangu.Huyu jamaa kanichosha sana.Kukutana na wewe tena kwa leo haiwezekani.Hapa inabidi nikaoga halafu nipumzike.Maaana shughuli ya yule kijana sio mchezo"

" Sawa mke wangu usijali.Kama amekufurahisha na kukurizisha kabisa mimi sina neno.Ninachotaka ni wewe ufurahi" aliongea baba tatu.

" Asante kwakunielewa.Lakini kama unahamu sana ,si uende kwa yule dada niliyemdanganya kuwa wewe ni kaka yangu.Maana nilikutongozea akakubali.Kilichobaki ni wewe tu"

" Lakini yule si anakaa na wazazi wake?"

" Ndio bado anakaa kwa wazazi wake."

" Daaah ,sasa kama bado anakaa kwa wazazi wake mbona ni tatizo"

" aaah! Tatizo kivipi mume wangu?"

" Hawa mabinti wanaokaa kwa wazazi wao kwenda nao lodge ni hatari sana ?"

"haina haja ya kwenda lodge mume wangu.Wewe wasiliana naye uje naye hapa hapa nyumbani"

" mmmh! Sasa mama tatu,Akija hapa nyumbani na kuona nguo zako hizi chumbani si atajua wewe ni mke wangu? Huoni kama mambo yataharibika"

" usijali hawezi kujua.Nguo zangu zote humu chumbani nazitoa.Zinabaki za kwako tu.Na kila kitu nakiweka vizuri.Akija hawezi kujua kama una mke"

" sawa,lakini saiz usiku.Nikimpigia simu akija wewe utaenda wapi?"

" Nitaenda wapi kivipi.Mimi nitajifungia chumba cha wageni.Hivyo hataniona.Na hata kama ikatokea akaniona sio tatizo kwasababu anajua wewe ni kaka yangu.Hivyo kuwa na amani baba tatu wangu."

" ok sawa mke wangu lakini yule mwanamke umejua kunichagulia aisee.Ni mzuri kweli kweli yaaani"

" kwani siku nyingine nakuchaguliaga wabaya.Mbona siku zote uwa nakutongozea wanawake wazuri tu.ila wewe sema wanaume unaoniunganishia wengine wanakuwa sio."

" wanakuwa sio kivipi mke wangu?"

" aaah! Wengine wanakuwa wachafu sana.Yaani hadi hamu ya tendo lenyewe inapungua.Yaani unakuta kwa nje msafi lakini kwa ndani ni mchafu balaa.Kitendo cha kuvua tu nguo ,unakuta boxer zinaanza kutoa harufu"

" aaaah! Mimi sijawahi kukuunganishia mwanaume mchafu bana.Huyo mchafu labda ulimtafuta mwenyewe"

" hujawahi wapi.Unamkumbuka fred yule kinyozi wa pale saloon"

" Ndio namkumbuka."

" sasa yule namba yake si ulinipa wewe. Sasa kwa taarifa yako yule kaka ni mchafu hakuna tena.Nilijuta kukutana naye"

"Duuuh! Basi nisamehe kwa ilo mke wangu.Leo wakati narudi nimekutana na jamaaa mzuri kinoma.Kwanza ni mrefu halafu amejazia jazia"

" kweli mume wangu?"

" Ndio ni kweli."

" ulivyomuona anasixpack?"

" Ndio anazo.Ni handsome balaaa"

" duuuh! Ulifanikiwa kuchukua namba yake.Maana inavyoonekana nitaenjoy sana kwake"

" usijali namba yake nilichukua,yaani nilivyomuona tu.Nilikufikiria wewe.Nilijua ukimpata yule utaenjoy sana.Namba yake hii hapa .Mpigie muongee" aliongea baba tatu huku akimuonyesha mke wake namba ya simu.Mke wake aliinakiri namba kwenye simu yake na kisha akatuma message.

" sasa mke wangu huyo jamaa utachati naye siku nyingine.Naomba kwasasa katoe nguo zako chumbani ili yule dada akija ajuwe sina mke ." aliongea baba tatu.Mama tatu alisimama na kwenda chumbani kwao kutoa nguo zake zote .Alitoa nguo zake na kukiweka chumba vizuri.Kwa jinsi alivyokifanya ,mwanamke yeyote ambaye angekuja lazima angejua baba tatu hakuwa na mke.

..........

Monica akiwa nyumbani kwake.Sms iliingia kwenye simu yake.Alipoifungua alikuwa ni baba tatu. " tuonane basi mke wangu mtarajiwa"ilisomeka ile sms kwenye simu yake.Monica moyo wake ulishaanza kumpenda baba tatu.Kilichomfanya ampende zaidi ni kitendo cha mama tatu kumpigia simu mara nyingi na kumuita wifi.

" Huyu mbaba atakuwa ananipenda sana.Yaani kawaambia hadi ndugu zake.Dada yake karibu kila siku ananitumia sms.Huyu hataki kunichezea anataka kunioa tu" aliwaza monica.Alichukua simu yake na kumjibu " haina shida baby,sema tu wapi tuonane" alijibu monica.

Sms ile ilimfurahisha baba tatu akaisoma kisha akampa na mke wake aisome.Baada ya hapo akamjibu kuwa ajiandae atamtuma dereva yebo akamchukue na kumleta nyumbani kwake.Baada ya kumwambia hivyo alimgeukia mke wake na kumwambia." aisee yule dada anakuja.Naomba toa nguo zako chumbani haraka na uondoke au ukakae chumba kingine" aliongea baba tatu.

....,.....

Wakati ayo yanaendelea .Kwenye kijiwe cha boda boda madereva bodaboda walikuwa wanazungumzia matendo ya baba tatu na mama tatu.

" Nyie wale watu sio bure.Lazima kuna kitu kilichojificha.Haiwezekani mume amtafutie mke wake michepuko ,na mke pia eti anamtafutia mumewe wanawake.Wale sio bure lazima kunakitu kilichojificha" aliongea mussa na kuungwa mkono na wenzake.

" aisee kweli mussa ,pale lazima kutakuwa na kitu .Sio bure" alijibu ally

............

Wakati ayo yanaendelea.Hans kijana aliyetoka kufanya mapenzi na mama tatu,Mwili wake haukuwa sawa.Alihisi kama amepungukiwa na kitu. " mmmh! Mbona mwili wangu haupo kawaida.Mbona kama nimepungukiwa na kitu flan" aliwaza Hans.

=== kuna nini? Kwanini hans anajihisi tofauti? Kitu gani kimetokea kwenye mwili wake? ,kujua ayo na mengine mengi tukutane sehemu inayofata====
received_305920581416448.jpg
 
Kwanini Mimi ep
SIMULIZI YA MAISHA: KWANINI MIMI? 02
MWANDISHI : MIKA AUTHOR
MSAMBAZAJI: Simulizi za Gilbert
MAWASILIANO: +255621249611

Tulipoishia - Wakati ayo yanaendelea.Hans kijana aliyetoka kufanya mapenzi na mama tatu,Mwili wake haukuwa sawa.Alihisi kama amepungukiwa na kitu. " mmmh! Mbona mwili wangu haupo kawaida.Mbona kama nimepungukiwa na kitu flan" aliwaza Hans.

Endelea nayo.

" Kwanini mwili wangu upo hivi? Kuna kauzito flan nakasikia , pamoja na uzito ninao usikia lakini kuna kitu kama kimepungua kwenye mwili wangu" aliwaza Hans. Aliendelea kujiuliza lakini hakupata majibu.

" mmmh! Au ni uchovu unaotokana na kufanya mapenzi? ,Ngoja nikaoge kwanza labda ninaweza kuwa sawa" aliwaza john huku akifungua mlango wa nyumbani kwake na kuingia ndani.

......

Twende kwa mama tatu na mumewe.

Mama tatu alitoa nguo zake chumbani kwao na akaweka mazingira sawa.Baada ya kuona kila kitu kipo sawa.Alimuaga mumewe.

" baba tatu mume wangu?"

" Niambie mke wangu"

" kila kitu nimekiweka sawa.Mimi naondoka nakuacha .Sitaki monica anikute hapa "

" sasa unaenda wapi?"

"Naenda kwa mama nasra pale kupiga story"

" ok poa. Mimi ngoja nimsubiri huyu mrembo.Ameniambia ameshapanda pikipiki."

" Ok sawa,me naondoka basi"

" poa" .Mama tatu aliondoka kuelekea kwa shoga yake aitwae mama nasra.Haukupita muda monica akawa amefika.Baba tatu alimfungulia geti akaingia ndani.Monica alishangaa uzuri wa ile nyumba.

" mmmh! Unataka kusema unaishi bila mke kwenye hii nyumba nzuri hivi?" aliuliza monica.Tamaa ya kuwa mama mwenye nyumba ilimuingia.Hakuwahi kamwe kufikiria kama atakuja kuingia kwenye nyumba kama ile.

" Siishi peke yangu.Naishi na mdogo wangu ambaye unawasiliana naye mara nyingi." alijibu baba tatu.Nyumba yao ilikuwa ni kubwa na ya kifahari. Ilikuwa ina fensi matata sana.Baba tatu aliongozana na monica hadi ndani.Walipiga story mbili tatu kisha wakaelekea moja kwa moja chumbani.

......

Kwa upande wa mama tatu alikuwa kwa shoga yake akipiga story. ." mmmh shoga yangu unajua maisha yenu mimi siyaelewi?,japokuwa mnajaribu kufanya siri,lakini saizi hakuna siri.Watu wengi wameshajua.Na kila aliyejua anajiuliza kwanini mnafanya hivi?" aliuliza mama nasra.

"Mmmmh! Mama nasra na wewe umesheanza.Tunafanya hivi kivipi?,sisi hatuna sababu yeyote zaidi ya upendo.Nampenda mume wangu na ninapenda aburudike,na Ndio mana nikiona msichana mzuri namtongozea "

" mmmmmmh!"

," acha kuguna.Ngoja nikuulize swali?"

" uliza tu?"

" Hivi kumpenda mtu maana yake si unataka uyo mtu aishi vizuri na ajisikie burudani?"

" Ndio ,iyo ndo maana yake"

" Sasa kama iyo ndo maana yake. Kwanini nyinyi mnatushangaa sisi.Sisi tunapendana ,na tunataka kila mmoja wetu afurahie maisha.Ndio mana tunafanya hivi"

" Mmmmh! Siyo kweli shoga.Kwenye mapenzi ayo mambo hayapo.Halafu ujue siku hizi magonjwa ni mengi sana.Hamjui mnaweza kuwa mnajitafutia magonjwa?"

" aaaah! Magonjwa hayawez kutupata sisi" aliongea kwakujiamini mama tatu.

" Shauri yenu.Halafu mtaani watu wameanza kusema mna ukimwi hivyo,mnausambaza makusudi? Wanasema mnafanya hivi kwasababu mnaukimwi ndio mana"

," sio kweli shoga .Hatuna ukimwi wala nini"

" Sasa kama hamna ukimwi.Kwanini mnafanya hivi?

" ilo mbona nilishakujibu.Ni upendo tu.Hakuna lingine" alijibu mama tatu.

Mama tatu na shoga yake , waliendelea kupiga story kwa muda mrefu sana.Mama nasra alikuwa anajaribu kumdodosa mama tatu ili amwambie sababu ya wao kufanya vile.Kila alipomdodosa alipewa majibu ambayo hakuridhika nayo.

.........

Monica na baba tatu baada ya kufanya yao,Monica alinogewa.Hakutaka kuondoka .Alitaka alale pale pale.Baba tatu alijaribu kumshawishi aondoke lakini monica alikuwa mbishi.

" sikiliza baby.Hatukukubaliana wewe ulale hapa leo.Kama unataka kulala hapa,inabidi uniambie mapema ili nijipange."

"Mmm!h! Hujipange nini mpenzi.Yaani mimi kuja kulala hapa tu mpaka ujipange,Hapana bana.Leo mimi siondoki hapa.Leo nalala hapa hapa" alijibu monica.

Kitendo cha monica kungangania kulala pale kilimkera baba tatu.Alimwangalia monica kwa jicho kali sana.". Kama tabia yako ndo hiii,mapenzi yenyewe mimi na wewe yatakuwa ndio basi.Haiwezekani yaani tumekutana siku moja tu halafu ukangangania kulala hapa hapa"

" mmmmh! Yaani ndio umekasirika "

" ndio umenikera.Hatukupanga wewe kuja kulala hapa.Kwanini unganganie "

" basi mpenzi.Sitaki kukuuzi.Ngoja niondoke." aliongea monica huku akisimama na kuvaa nguo zake.Alivaa nguo na kujiweka sawa tayari kwa kuondoka. ." mimi nipo tayari mpenzi wangu" aliongea monica.

" Sawa.Basi shika hii itakusaidia." aliongea baba tatu ,huku akimpa monica noti nne za elfu kumi kumi.

" asante mpenzi" alijibu monica.Baba tatu alimpigia simu dereva boda boda aje kumchukua monica.Alimsindikiza hadi getini nje.Haikuchukua muda dereva boda boda akawa amefika na kumchukua.Monica alipanda kwenye boda na kuondoka.Wakati anaondoka aliiangalia nyumba ya baba tatu kwa uchu sana " nitafanya kila niwezalo nije kuishi katika hii nyumba" aliwaza monica.

Lakini akiwa njiani monica alihisi mwili wake kama umepungua kitu flan." mmmmh! Mbona siko sawa. Kuna nini? Mbona kama mwili wangu unatatizo flan! Au janaba la ngono linanisumbua?" aliwaza monica.Haikuchukua muda akawa amefika nyumbani kwao.Alishuka kwenye piki piki na kuingia ndani.

Lakini wakati anashuka kwenye pikipiki mama yake alimuona.

" mmmmh! Monica.Tabia ya kuletwa na mapikipiki usiku imeanza lini?"

" mama saizi nimekuwa mtu mzima.kwanza nimepata mchumba.Siku sio nyingi nitaolewa" alijibu monica huku akiingia ndani.

"Sasa mwanangu kama umepata mchumba si inabidi umlete kwanza tumuone." aliongea mama yake monica.Wakati anaongea ayo monica hakumsikia alikuwa ameshaingia ndani.

BAaada ya monica kuondoka.Baba tatu alichukua simu na kumpigia mkewe .

" Njoo bana.Kazi imeshaisha huku" aliongea baba tatu.

" mmmmh! Mara hii.Mapenzi gani ayo ya kufanya haraka haraka ivyo. vipi umeenjoy lakini?

" Ndio,sema tatizo mwanamke mwenyewe kinganganizi huyo.Eti alitaka alale hapa hapa"

"Aaah! Yaani kuja leo tu anataka kuhamia kabisa?"

" Ndiyo ivyo,ila nimemlia ngumu.Nimemuondoa kwa lazima."

" ok safi,nakuja basi mume wangu?" alijibu mama tatu,kisha akamuaga shoga yake mama nasra na kuondoka.

.............

Majira ya saa tisa usiku.Mama tatu alimuamsha mumewe .

" baba tatu,baba tatu.Amka muda umefika.Amka" aliongea mama tatu huku akimtikisa mumewe .

" mmmmh! Niache nipumzike kidogo"

," upumzike wapi? Utaleta matatizo wewe? Muda umefika mume wangu amka" aliongea mama tatu huku akiendelea kumtikisa mumewe.Baba tatu aliamka kisha wote wawili wakaelekea bafuni kuoga.

Baada ya kuoga ,Mama tatu na baba tatu walifungua mlango na kuingia kwenye chumba chao maalum.Mama tatu alivua nguo zote na kujilaza kwenye meza ya chuma iliyokuwa mle ndani.

= kuna nini? Baba tatu na mama tatu wanafanya nini kwenye chumba chao cha siri?, kwanini walale kwenye meza ya chuma? =
Full vipande vyote 27 vinapatikana kwa buku tu kupitia WhatsApp namba 0621249611
Namba ya Malipo ni HALOPESA NAMBA 0621249611
 
Hii simulizi cjaipenda inachochea ugaidi!
 
SIMULIZI YA MAISHA: KWANINI MIMI? 03
MWANDISHI : MIKA AUTHOR
MSAMBAZAJI: Simulizi za Gilbert
MAWASILIANO: +255621249611

Tulipoishia -
Baada ya kuoga ,Mama tatu na baba tatu walifungua mlango na kuingia kwenye chumba chao maalum.Mama tatu alivua nguo zote na kujilaza kwenye meza ya chuma iliyokuwa mle ndani.

Endelea nayo.

Akiwa amelala kwenye ile meza ya chuma alianza kulalamika huku akirusha rusha miguu kama mwanamke anayetaka kuzaa.Wakati mama tatu anafanya ayo,baba tatu na yeye alikuwa amekaa kwenye kiti cha chuma akiwa uchi wa mnyama.Yeye alikuwa akilalamika na kujipiga piga.Wote wawili walikuwa kana kwamba wanapata maumivu makali sana.Machozi na jasho viliwatoka.Wote wawili kila walipokuwa wanalalamika ,vitu ambavyo vilikuwa havieleweki ni nini,Vilikuwa vinatoka kwenye sehemu zao za siri.

..........

Wakati ayo yanendelea ,Juma majira ya saa tisa usiku alikuwa barabarani na mke wake wakielekea hospitali. Uchungu wa kujifungua ulikuwa umemshika mke wake. Juma Aliwapigia madereva wote anaowajua waje kumchukua lakini hakuna hata mmoja aliyepokea simu.Baada ya kuona mkewe anazidi kulalamika na hakuna dereva aliyepokea simu yake juma aliamua kutembea kwa mguu na mke wake kuelekea hospitali.

" jikaze mke wangu.Hakuna nji nyingine .Tutafika tu,"

" jamani juma,jaribu kuwapigia tena waje kutuchukua"

" Nimewapigia sasa hivi hawajapokea simu.Naomba vumilia kidogo hapo mbele tuta pata gari "

Waliendelea kujikongoja kwa umbali mrefu bila pikipiki wala gari kutokea.Hali ya mkewe ilizidi kuwa mbaya." nafanyaje sasa?,daaah umasikini mbaya sana.Ningekuwa na pikipiki au gari aya yote yasingetokea" aliwaza juma.

"Vumilia kidogo mke wangu.Sasa hivi tutapata usafir" aliongea juma.

" mmmmh! Jamani mme wangu! Kwanini ukumwandaa dereva mapema.Ona sasa mkeo napata shida hivi"

" nisamehe mke wangu.ila usijali kila kitu kitakuwa sawa"

" Nahisi chupa imepasuka.Mtoto anataka kutoka"

Maneno ya mkewe yalimpasua kichwa juma.Aliangalia kushoto na kulia hakuona kitu.Alitamani aruke lakini haikuwezekana.Wakati akiwa amechanganyikiwa hajui afanye nini,gafla walitokea vijana watatu wakiwa na mapanga mikononi.

" oya usiku huu mnafanya nini kwenye maeneo yetu" aliongea kijana mmoja.

" aisee mke wangu ameshikwa na uchungu,inabidi nimuwaishe hospital"

" ayo sisi hayatuhusu.Kwakuwa mmepita mitaa yetu itabidi mlipie"

" aaah! Nilipie nini ?"

" ulipie nini ?,hujui kama huu ni mtaa wa mamafia.Hapa ukipita ni lazima ulipie"

Maneno yale yalimchanganya juma.Mfukoni alikuwa na hela ndogo kwa ajili ya mkewe hospital.

" jamani mimi sina kitu chochote.Hapa nilipo nina elfu kumi tu kwaajili ya mke wangu kujifungua"

" Tupe iyo elfu kumi" aliongea kijana mmoja.Alipoona juma hamjibu kitu alimpiga na bapa la panga kichwani." oya usitupotezee muda.Au unataka hadi tuwakate mapanga ndio mtupe vitu mlivyokuwa navyo"

" Hapana sio ivyo........" kabla hajamaliza kuongea vizuri alikatwa mtama. Akaanguka chini.Alipojaribu kusimama alipigwa teke la tumbo." kaa hapo hapo chini.Unajua sisi tupo kazini halafu wewe unatuletea habari zako sio." aliongea kijana aitwae buti kubwa ambae ni kiongozi wa wale vibaka.

Walimsachi juma na kuchukua elfu kumi aliyokuwa nayo.

"Daaah! Washikaji nioneeni huruma.Hela niliyokuwa nayo ni iyo iyo.Naombeni mnionee huruma"

" unataka tukuonee huruma? Basi chagu moja. Tumbake mke wako au tuchukue hii elfu kumi na hiki kimkoba chenu?"

" aaah! Kumbaka tena? Si mnaona hali yake ilivyo.Anaenda kujifungua huyu? Mtambakaje?"

" kwenda kujifungua sio ishu.Burudani ipo pale pale.Swala ni wewe kuamua kama mtuachie hii hela na mkoba au tumbake mkeo kwa zamu halafu tuwaache muende"

" Daaah! Washikaji kwanini tunafanyiana hivi? Mjue sisi sote ni wanaume.Leo kwangu kesho kwenu.Naomba msinifanyie ivyo.Naomba mniache na mke wangu niende"

Wakati majibizano yanaendelea rose mke wa juma uchungu ulikuwa umemshika kweli kweli.Maumivu aliyokuwa anayasikia yalikuwa makali sana.

"Sikiliza wewe jamaa,sisi hatujasema kuwa hautaenda.Tumekuambia uchague moja.Tupe hela na mkoba au turuhusu tumbake mke wako" aliongea buti kubwa.

Juma alishikwa na hasira.Alitamani awavamie awapige lakini ubongo wake ulimkatalia.Akili yake ilimwambia kufanya ivyo ni kujitafutia kifo kwakuwa wenzake wapo wengi.

" aisee hela niliyokuwa nayo ni elfu kumi tu ambayo mmeichukua.Sina chochote kingine".

Baaada ya kuambiwa ivyo walimnyanga dishi na mkoba ambao ulikuwa na nguo kwa ajili ya kujifungulia.Juma alisimama pale chini na kumshika mkewe wakawa wanaondoka.Lakini kabla hawajapiga hatua nyingi walisimamishwa.

" nani amewaambia muondoke?,bado hatujamalizana"

" Lakini mlichotaka si nimeshawapa.Naombeni mniache nimuwaishe mke wangu hospitali"

" kuna mtu amekwambia ukichelewa utaikuta hospitali imehama? Hospital ipo muda wote.Njooni hapa haraka"

Bila ubishi juma alirudi hadi pale walipo." nimefika kaka," aliongea juma kiupole japo moyo wake ulikuwa ukivuja damu kwa hasira."

" vua suruali na viatu weka pale"

" daah! Jamani nikuvua nitaendaje hospitali?,nawaombeni sana .mimi ni kijana mwenzenu.Naombeni mniache kwa leo"

" aaah! Wewe jamaa boya sana,yaani mimi nakuambia halafu wewe unaleta story" aliongea buti kubwa ,kisha akachukua panga na kumpiga nalo juma mgongoni. " nikileta mzaha naweza kufa hapa" aliwaza juma kisha akaamua kuvua nguo na viatu kuwakabizi.

" sasa mambo si ayo.Aya mwambie na mke wako avue nguo aliyovaa"

" aaah! Yaani na mke wangu tena?"

" Ndio mwambie atupe nguo haraka"

Juma alifikiria aliona haina jinsi alimvata mke wake na kumwambia avue nguo aliyovaa.Bila ubishi akaivua na kuwakabidhi.Juma na mkewe walibaki na nguo za ndani tu.

" ayaaa poteeeni haraka" aliongea buti kubwa.Juma alimshika mkewe taratibu wakawa wanaenda.Lakini wakiwa wapo hatua kadhaa mbele.Katika wale vibaka,kibaka mmoja alimsogelea buti kubwa na kumuambia.

" broo yule mwanamake ni dili,pale alipo ameshikwa na uchungu.Kuna mganga wangu aliwahi kuniambia ukifanya mapenzi na mwanamke aliyekuwa anakaribia kujifungua unaondoka mikosi yote ,na pia unavutia utajiri"

" aaah! Kweli ?"

== kuna mengi ya kujua .Je mke wa juma atabakwa?,lakini pia je,juma na mke wake wanauhusiano gani na baba tatu pamoja na mkewe mama tatu?, kujua ayo na mengine mengi endelea kuifatilia===
 
SIMULIZI YA MAISHA: KWANINI MIMI? 03
MWANDISHI : MIKA AUTHOR
MSAMBAZAJI: Simulizi za Gilbert
MAWASILIANO: +255621249611

Tulipoishia -
Baada ya kuoga ,Mama tatu na baba tatu walifungua mlango na kuingia kwenye chumba chao maalum.Mama tatu alivua nguo zote na kujilaza kwenye meza ya chuma iliyokuwa mle ndani.

Endelea nayo.

Akiwa amelala kwenye ile meza ya chuma alianza kulalamika huku akirusha rusha miguu kama mwanamke anayetaka kuzaa.Wakati mama tatu anafanya ayo,baba tatu na yeye alikuwa amekaa kwenye kiti cha chuma akiwa uchi wa mnyama.Yeye alikuwa akilalamika na kujipiga piga.Wote wawili walikuwa kana kwamba wanapata maumivu makali sana.Machozi na jasho viliwatoka.Wote wawili kila walipokuwa wanalalamika ,vitu ambavyo vilikuwa havieleweki ni nini,Vilikuwa vinatoka kwenye sehemu zao za siri.

..........

Wakati ayo yanendelea ,Juma majira ya saa tisa usiku alikuwa barabarani na mke wake wakielekea hospitali. Uchungu wa kujifungua ulikuwa umemshika mke wake. Juma Aliwapigia madereva wote anaowajua waje kumchukua lakini hakuna hata mmoja aliyepokea simu.Baada ya kuona mkewe anazidi kulalamika na hakuna dereva aliyepokea simu yake juma aliamua kutembea kwa mguu na mke wake kuelekea hospitali.

" jikaze mke wangu.Hakuna nji nyingine .Tutafika tu,"

" jamani juma,jaribu kuwapigia tena waje kutuchukua"

" Nimewapigia sasa hivi hawajapokea simu.Naomba vumilia kidogo hapo mbele tuta pata gari "

Waliendelea kujikongoja kwa umbali mrefu bila pikipiki wala gari kutokea.Hali ya mkewe ilizidi kuwa mbaya." nafanyaje sasa?,daaah umasikini mbaya sana.Ningekuwa na pikipiki au gari aya yote yasingetokea" aliwaza juma.

"Vumilia kidogo mke wangu.Sasa hivi tutapata usafir" aliongea juma.

" mmmmh! Jamani mme wangu! Kwanini ukumwandaa dereva mapema.Ona sasa mkeo napata shida hivi"

" nisamehe mke wangu.ila usijali kila kitu kitakuwa sawa"

" Nahisi chupa imepasuka.Mtoto anataka kutoka"

Maneno ya mkewe yalimpasua kichwa juma.Aliangalia kushoto na kulia hakuona kitu.Alitamani aruke lakini haikuwezekana.Wakati akiwa amechanganyikiwa hajui afanye nini,gafla walitokea vijana watatu wakiwa na mapanga mikononi.

" oya usiku huu mnafanya nini kwenye maeneo yetu" aliongea kijana mmoja.

" aisee mke wangu ameshikwa na uchungu,inabidi nimuwaishe hospital"

" ayo sisi hayatuhusu.Kwakuwa mmepita mitaa yetu itabidi mlipie"

" aaah! Nilipie nini ?"

" ulipie nini ?,hujui kama huu ni mtaa wa mamafia.Hapa ukipita ni lazima ulipie"

Maneno yale yalimchanganya juma.Mfukoni alikuwa na hela ndogo kwa ajili ya mkewe hospital.

" jamani mimi sina kitu chochote.Hapa nilipo nina elfu kumi tu kwaajili ya mke wangu kujifungua"

" Tupe iyo elfu kumi" aliongea kijana mmoja.Alipoona juma hamjibu kitu alimpiga na bapa la panga kichwani." oya usitupotezee muda.Au unataka hadi tuwakate mapanga ndio mtupe vitu mlivyokuwa navyo"

" Hapana sio ivyo........" kabla hajamaliza kuongea vizuri alikatwa mtama. Akaanguka chini.Alipojaribu kusimama alipigwa teke la tumbo." kaa hapo hapo chini.Unajua sisi tupo kazini halafu wewe unatuletea habari zako sio." aliongea kijana aitwae buti kubwa ambae ni kiongozi wa wale vibaka.

Walimsachi juma na kuchukua elfu kumi aliyokuwa nayo.

"Daaah! Washikaji nioneeni huruma.Hela niliyokuwa nayo ni iyo iyo.Naombeni mnionee huruma"

" unataka tukuonee huruma? Basi chagu moja. Tumbake mke wako au tuchukue hii elfu kumi na hiki kimkoba chenu?"

" aaah! Kumbaka tena? Si mnaona hali yake ilivyo.Anaenda kujifungua huyu? Mtambakaje?"

" kwenda kujifungua sio ishu.Burudani ipo pale pale.Swala ni wewe kuamua kama mtuachie hii hela na mkoba au tumbake mkeo kwa zamu halafu tuwaache muende"

" Daaah! Washikaji kwanini tunafanyiana hivi? Mjue sisi sote ni wanaume.Leo kwangu kesho kwenu.Naomba msinifanyie ivyo.Naomba mniache na mke wangu niende"

Wakati majibizano yanaendelea rose mke wa juma uchungu ulikuwa umemshika kweli kweli.Maumivu aliyokuwa anayasikia yalikuwa makali sana.

"Sikiliza wewe jamaa,sisi hatujasema kuwa hautaenda.Tumekuambia uchague moja.Tupe hela na mkoba au turuhusu tumbake mke wako" aliongea buti kubwa.

Juma alishikwa na hasira.Alitamani awavamie awapige lakini ubongo wake ulimkatalia.Akili yake ilimwambia kufanya ivyo ni kujitafutia kifo kwakuwa wenzake wapo wengi.

" aisee hela niliyokuwa nayo ni elfu kumi tu ambayo mmeichukua.Sina chochote kingine".

Baaada ya kuambiwa ivyo walimnyanga dishi na mkoba ambao ulikuwa na nguo kwa ajili ya kujifungulia.Juma alisimama pale chini na kumshika mkewe wakawa wanaondoka.Lakini kabla hawajapiga hatua nyingi walisimamishwa.

" nani amewaambia muondoke?,bado hatujamalizana"

" Lakini mlichotaka si nimeshawapa.Naombeni mniache nimuwaishe mke wangu hospitali"

" kuna mtu amekwambia ukichelewa utaikuta hospitali imehama? Hospital ipo muda wote.Njooni hapa haraka"

Bila ubishi juma alirudi hadi pale walipo." nimefika kaka," aliongea juma kiupole japo moyo wake ulikuwa ukivuja damu kwa hasira."

" vua suruali na viatu weka pale"

" daah! Jamani nikuvua nitaendaje hospitali?,nawaombeni sana .mimi ni kijana mwenzenu.Naombeni mniache kwa leo"

" aaah! Wewe jamaa boya sana,yaani mimi nakuambia halafu wewe unaleta story" aliongea buti kubwa ,kisha akachukua panga na kumpiga nalo juma mgongoni. " nikileta mzaha naweza kufa hapa" aliwaza juma kisha akaamua kuvua nguo na viatu kuwakabizi.

" sasa mambo si ayo.Aya mwambie na mke wako avue nguo aliyovaa"

" aaah! Yaani na mke wangu tena?"

" Ndio mwambie atupe nguo haraka"

Juma alifikiria aliona haina jinsi alimvata mke wake na kumwambia avue nguo aliyovaa.Bila ubishi akaivua na kuwakabidhi.Juma na mkewe walibaki na nguo za ndani tu.

" ayaaa poteeeni haraka" aliongea buti kubwa.Juma alimshika mkewe taratibu wakawa wanaenda.Lakini wakiwa wapo hatua kadhaa mbele.Katika wale vibaka,kibaka mmoja alimsogelea buti kubwa na kumuambia.

" broo yule mwanamake ni dili,pale alipo ameshikwa na uchungu.Kuna mganga wangu aliwahi kuniambia ukifanya mapenzi na mwanamke aliyekuwa anakaribia kujifungua unaondoka mikosi yote ,na pia unavutia utajiri"

" aaah! Kweli ?"

== kuna mengi ya kujua .Je mke wa juma atabakwa?,lakini pia je,juma na mke wake wanauhusiano gani na baba tatu pamoja na mkewe mama tatu?, kujua ayo na mengine mengi endelea kuifatilia===
shusha vitu
 
SIMULIZI YA MAISHA: KWANINI MIMI? 04
MWANDISHI : MIKA AUTHOR
MSAMBAZAJI: Simulizi za Gilbert
MAWASILIANO: +255621249611



Tulipoishia - broo yule mwanamake ni dili,pale alipo ameshikwa na uchungu.Kuna mganga wangu aliwahi kuniambia ukifanya mapenzi na mwanamke aliyekuwa anakaribia kujifungua unaondoka mikosi yote ,na pia unavutia utajiri"

" aaah! Kweli ?"

Endelea nayo.

" ndio ni kweli kiongozi.Yule mama tusimwache.Tumbake tuondoe mikosi"

" mmmh! Wazuieni basi"

" oya simameni hapo hapo"

" daaah . hawa jamaa wananitafuta nini mimi.Kila walichotaka nimewapa.Kwanini lakini bado wananisumbua sumbua?" aliwaza juma.

Waliwasogelea mpaka pale.Vijana wawili walimvamia juma na kumfunga kamba.Buti kubwa alienda akamshika mke wa juma.

" sikiliza dada.aya mambo hayataki hasira.Ukileta purukushani utamzuru mtoto aliyekuwa tumboni .Mimi situmii nguvu.Taratibu tu naondoa mkosi wangu halafu nawaacha muondoke.

Maneno yake hayakuingia kwenye akilini ya mke wa juma.Hakujua jamaa alikuwa anamaanisha nini kusema vile.Huku akiwa anaugulia maumivu makali ya uchungu alimuuliza .

" unatakaje?" aliongea mke wa juma huku akikaa chini.

" ok safi kaa hapo hapo chini .Kwanza hapo chini mambo yataenda vizuri" aliongea buti kubwa.

Juma alijaribu kujitutumua kutoka kwa wale vijana lakini ilikuwa ngumu walikuwa wamemkamata kwa nguvu kweli kweli.

" aisee mwache mke wangu. Unataka kumfanya nini mke wangu. Nitakuua nakuambia ,nitakuua " aliongea juma huku akilia kwa uchungu.

Baada ya mke wa juma kukaa chini.Buti kubwa akawa anamlazimisha alale chini.Kutokana na uchovu na kutingwa na uchungu wa mimba ,mke wa juma akalala bila matatizo.

"Ok safi.Lala ivyo ivyo" aliongea buti kubwa huku akipereka mkono kiunoni kujaribu kumvua chupi.Aliishika na kuivuta.Kitendo kile kilimshtua mke wa juma ." aaah unataka kufanya nini?" aliongea mke wa juma huku akilia.

" usijali dada nataka nikusaidie ujifungue haraka" aliongea buti kubwa na kuivua kabisa chupi .Juma kuona vile alijua kinachotaka kuendelea.Alipiga kelele za uchungu,alijaribu kuwasukuma wale vibaka.Wale vibaka walipoona juma anawasumbua walimpiga panga la kichwa pale pale alianguka chini na kupoteza fahamu.

Baada ya juma kuanguka chini na kupoteza fahamu walienda alipo buti kubwa pamoja na mke wa juma.Kufika pale walimshika mikono mke wa juma ili asilete fujo.Buti kubwa alimnyanyua miguu mke wa juma na kujiweka sawa ili ambake.

Lakini kabla hajafanikiwa kumuingia.Lilitokea defender la jeshi na kupaki karibu yao.Kitendo cha kuliona defender la jeshi kiliwafanya buti kubwa na wenzake wasimame na kukimbia. Kwenye ile defender alishuka kijana mmoja na kwenda kumuangalia mke wa juma ambaye alikuwa analia kama mtoto.

" mmmh! Hawa washenzi walikuwa wanataka kukufanya nini? Na usiku huu peke yako unaenda wapi " aliongea alex ambaye ni dereva wa lile defender.Alex alikuwa anakaa karibu na pale.Na siku ile kutokana na mjukumu ya kikazi alishindwa kurudi nyumbani kwa muda muafaka.

Alimnyanyua na kwenda kumuingiza kwenye gari.Alipanda na yeye kisha akawasha gari na kutaka kuondoka." mume wangu ,tumemuacha mume wangu" aliongea mke wa juma.

" aaah! Kumbe upo na mume wako? ,yupo wapi? " aliuliza alex kisha akasimamisha gari na kwenda kumchukua juma ambaye alikuwa amepoteza fahamu huku akivuja damu kichwani .Alimpakiza nyuma ya gari kisha akaenda kuwasha gari na kuondoka.

" mmmmh! Kwa kesi ilivyo inabidi kwanza twende polisi tukajaze fomu ya pf3" aliongea alex.Mke wa juma hakumjibu,kwani uchungu ulikuwa mkubwa na muda wote alikuwa akiangaika angaika.

" Lakini hapana,nikienda polisi saiz nitapoteza muda.Ngoja tu niwawahishe hospitali .Nikifika pale nitajua chakufanya" aliongea alex huku akiongeza mwendo wa gari.

Ndani ya muda mfupi wakawa wamefika hospital.Mke wa juma alipokelewa .Juma kabla yakuanza kutibiwa, daktari akitaka apewe pf3. " aisee hapana.Huyu amejeruhiwa.Siwezi kumtibu mpaka nipate pf3" aliongea daktari.

" sikiliza daktari.Wewe anza kumtibu.Mimi nafatilia pf3,sasa hivi naileta hapa" aliongea alex.

" utanisamehe ndugu.Bila pf3 siwezi kumtibu.Mtu amejeruhiwa huko sijui kama ni jambazi au la.Naanzaje kumtibu kienyeji hivi? Wewe unataka kunipa mimi matatizo sio bure"

" nakupa matatizo gani.Huyu sio jambazi.kavamiwa na vibaka njiani wakati anakuja hospitali"

"Hata kama sio jambazi.utaratibu ni lazima pf3 ijazwe ndio nianze kumtibu"

" duuuuh! Hivi wewe ni daktari kweli?.Yaani umuonei huruma kijana wa watu kabisa.Hujui kama anaweza kufa kama hautachukua hatua za haraka?"

" Najua anaweza kufa ila sasa mimi nifanyaje? Utaratibu ndio huo.Lazima pf3 ipatikane kwanza."

" mmmmh,aisee wewe ni kichwa maji sana" alifoka alex huku akitoka pale hospital.Aliingia kwenye gari na kwenda polisi.Kufika polisi alikuta polisi amesinzia pale kaunta kutokana na uchovu.

" oya oyaa " aliongea alex huku akimtikisa yule askari wa kaunta.Yule askari alishtuka na kumkodolea macho alex. " usiku huu umefata nini?"aliuliza yule askari

" Nahitaji pf3 kuna mgonjwa nimemuokota amekatwa na panga yupo hospital"

" mmmh! Sio kibaka uyo kapigwa mapanga baada ya kuiba"

" aaaah kwani akiwa kibaka hatibiwi.Kisheria awe mwizi au asiwe mwizi matibabu ni haki yake."

" mmmmh sawa,yuko wapi huyo mtu"

" yupo hospitali"

" aaaah nitatoje pf3 kwa mtu ambaye simuoni.utaratibu ni kuwa uyo majeruhi ilibidi uje naye hapa"

" daaaah! Aiseee izi taratibu zitanishinda.Sasa fanya hivi,twende hospital ukamuone"

" niende hospital halafu kituo nimuachie nani?"

" sasa unanisaidiaje? ,kijana wawatu atakufa ujue?"

"Chakukusaidia ni hiki.Chukua hii namba yangu,nenda nayo hospital.ukifika mwambie daktari aongee na mimi" aliongea yule askari huku akiandika namba kwenye karatasi.Baada ya kuandika alimkabizi. Alex alichukua namba na kuondoka.

Moyoni mwake alishaanza kujutia uamuzi wake wa kuwasaidia watu asiowajua." daaah! Huu usumbufu sio.Yaani mtu mwenyewe nimemuokota tu barabarani." aliwaza alex.

Alifika hospital akafanya kama alivyofanya .Daktari aliongea na yule polisi kwa simu kisha akaanza kumtibu juma.

...........

Majira ya saa kumi na mbili asubuhi.Baba tatu na mama tatu walitoka kwenye kile chumba chao.Waliingia bafuni kwa pamoja walioga na kutoka.Walijifuta maji kisha wakavaa nguo za gharama tayari kwa kutoka.Baba tatu alifungua droo akatoa vitita vyenye noti nyingi za elfu kumi kumi,kisha akaviweka kwenye begi.

" leo unaelekea wapi mume wangu? "

" aiseee leo naenda maeneo ya chuo pale.Wanawake wazuri wapo wengi pale. Vipi wewe unaelekea wapi?"

" mmmh! Hata sielewi ,ila sio ishu naenda nje ya mji kabisa .Kuna baa moja nzuri sana,najua pale lazima nitapata kijana tu.Si unajua vijana wanataka kulelewa siku hizi"

" ok sawa" alijibu baba tatu kisha wakaongozana kutoka nje.Kufika nje kila mmoja aliingia kwenye gari lake.Kwa jinsi walivyokuwa ,kama ungebahatika kuwaona ungejua wanafanya kazi kwenye ofisi za juu sana au ni wafanya biashara.Ila ukweli ni kuwa walikuwa hawana kazi yeyote ya maana zaidi ya kuwatafuta watu wa kushirikia nao ngono.

...........

Turudi hospital.

Majira ya saaa tatu asubuhi uchungu ulikuwa mkali sana kwa mke wa juma.Taratibu mtoto akaanza kutoka.Nesi na daktari walikuwa karibu wakimsaidia.Haikuchukua muda mtoto akawa anatoka.Baada ya kumuona mtoto akitoka ,Nesi na daktari waliyokuwa wanamuhudumia walirudi nyuma na kutaka kukimbia.

" aaah! Mungu wangu hiki ni nini?" aliongea daktari huku akirudi nyuma.

=== je daktari ameona nini? Kuna nini? Kwanini daktari ashtuke na kurudi nyuma? ,kuna nini? endelea kufatilia===

Ukivihitaji vipande vyote leo mcheki mwandishi whatsapp kwa namba 0621249611
Lipia Tshs 1000 tu kwa namba 0621249611 au M-PESA 0765824715
Jina lisomeke Gilbert Evarist
 
SIMULIZI YA MAISHA: KWANINI MIMI? 05
MWANDISHI : MIKA AUTHOR
MSAMBAZAJI: Simulizi za Gilbert
MAWASILIANO: +255621249611


Tulipoishia - Majira ya saaa tatu asubuhi uchungu ulikuwa mkali sana kwa mke wa juma.Taratibu mtoto akaanza kutoka.Nesi na daktari walikuwa karibu wakimsaidia.Haikuchukua muda mtoto akawa anatoka.Nesi na daktari waliyokuwa wanamuhudumia walirudi nyuma na kutaka kukimbia baada ya kuona mtoto akiyekuwa anatoka.

Endelea nayo

" Mungu wangu hiki ni nini?." aliongea daktari huku akirudi nyuma . Daktari alirudi nyuma hatua kazaa ,kisha Haraka sana akawahi kwenda kumdaka mtoto ambaye alikuwa anamalizia kutoka .Baada ya mtoto kutoka ,mke wa juma alizimia na kupoteza fahamu.Nesi kwa uwoga alikimbia na kutoka mle ndani.

" nesiiii,nesiiiii" aliita daktari .

" Tangu nianze hii kazi sijawahi kukutana na kitu kama hiki.Hiii ni laana au ni nini?,aaaah mtoto anamkia na sura ya ajabu hivi" aliwaza daktari.

Mtoto aliyezaliwa alikuwa na mkia.Wakati anatoka daktari na yule nesi walirudi nyuma walijua ule mkia ni nyoka,ndio maana walitaka kukimbia kwa uwoga.Daktari alimchukua yule mtoto na kwenda kumuweka sehemu wanayohifadhia watoto.

Taarifa ile ilisambaa pale hospitali kama upepo.Kila mmoja aliongea lake." mmmh! Mwenzangu uoga ulinishika nikaaona nitoke nduki" aliongea yule nesi aliyekimbia.

"Lakini inawezekana vipi binadamu mzima kabisa akazaa mtoto asiyeeleweka.Tena mwenye mkia" aliuliza mwenzake.

" aiseee mimi mwenyewe sielewi.Nimeshangaa sana kuona ile hali.Yaani ilibaki kidogo tu nizimie" aliongea yule nesi.

" wewe daktari anakuita kule.Amekasirika huyo.Hebu nenda haraka" aliongea mwenzake.Yule nesi aligeuka nyuma na kumuona daktari akiwa kakasirika sana.Hofu ilimwingia na taratibu akamfata daktari pale aliposimama.

" Hivi ndio tabia gani iyo? Hujui kama unavunja miiko ya kazi.unaanzaje kutoa taarifa za mtoto nje bila ruhusa." alifoka yule daktari.

" mmmh sijasema mimi"

" Hujasema wewe? sasa kasema nani? Mbona hospitali nzima wanajua kuhusu mtoto."

" mimi sielewi wamejuaje"

" Huelewi vipi wakati mle ndani tulikuwa mimi na wewe tu.Uoni kama unavunja taratibu.Halafu mbaya zaidi unajifanya kukataa kila kitu.Yaaani upumbavu umefanya wewe halafu saizi unakataa kuwa sio wewe'

Maneno yale yalimwingia nesi .Akawa mpole.Alijua kosa lake. " samahani daktari naomba nisamehe.Naomba unifichie siri watu wasijue kama mimi ndiye niliyesambaza habari"

" halafu kingine.kwanini ulikimbia mle ndani.Kwanini uliondoka wakati mimi nakuhitaji.Mgonjwa yupo kwenye hali mbaya wewe unakimbia"

' aaah mimi niliogopa.Nilijuwa nyoka"

" Wewe hufai kabisa kuwa nesi.Na hili nitaliandikia taarifa" alifoka daktari na kuondoka.

Baada ya masaa kazaa kupita .Mke wa juma fahamu zilikuwa zimemrejea.Kitu cha kwanza alichoongea baada ya fahamu kumrejea ni kumtaka mwanae." mwanangu yuko wapi? ,nataka kumuona mwanangu"

" mmmh! Hivi anajua kuwa mwanae yupo tofauti sana?" nesi alimuuliza mwenzake.

" Hatajuaje wakati alizimia?"

" Daaah! Mbona kama hivyo ni mtihani mkubwa.Kwahiyo tunafanyaje tukamletee ivyo ivyo au ?"

" Aisee mimi nashauri twende tukamuulize daktari kwanza.Daktari atatuambia tufanye nini?" walishauriana manesi, wakatoka kwenda kuongea na daktari.Baada ya kushauriana na daktari .Daktari aliamua yeye mwenyewe ndiye akampe mtoto na kumuweka sawa kisaikolojia.

Daktari aliongozana na wale wauguzi wakamchukua mtoto na kumpelekea mke wa juma.Mke wa juma baada ya kuonyeshwa mwanae alimkataa kata kata kuwa yule sie mwanae.

" mmenibadirishia mwanangu.Namtaka mwanangu.Huyo sio mwanangu" aliongea mke wa juma huku akilia kwa uchungu.Daktari alitumia saikolojia kubwa hadi mke wa juma akatulia.

....

Kwa upande wa juma fahamu zilimrejea.Alitibiwa akakaa sawa.Lile panga alilopigwa lilikuwa halijamwingia kisawa sawa.Baada ya fahamu kurejea na kupewa matibabu.Alitaka kumuona mke wake.Ndugu yake aliyefika asubuhi kumuona alimsaidia kutembea mpaka kwenye wodi aliyokuwa mke wake.

Alimkuta mke wake akiwa ameshika mtoto huku akilia.Kwa haraka haraka juma alivyomuona mkewe analia akajuwa analia kwa furaha kutokana na changamoto walizokutana nazo njiani wakati wanafika hospital.

" usilie mke wangu.Yale yote yameshapita.Lamsingi ni kumshukuru mungu,umajifungua salama.Namwomba mwanangu nimshike" aliongea john huku akimsogelea mkewe.

" aaaah vipi mbona mtoto yuko hivi?" alishtuka john baada ya kumuona mwanae.Mkewe aliendelea kulia bila kujibu chochote.

" Mbona hunijibu.Mbona sielewi!,tatizo nini? Mbona yupo hivi? Au huyu sio mtoto wangu? Lakini kwanini umemshika wewe?" aliuliza maswali mfululIzo .Daktari baada ya kuona taharuki ya Juma alimshika mkono na kumwwambia waende ofisini." Twende ofisini kijana" aliongea daktari huku akimshika mkono juma.

" ofisini nikafanye nini? Nataka nimwone mwanangu.Mwanangu yuko wapi?"

" Mwanao yupi? Mwanao si huyo hapo kashikwa na mke wako"

" Hapana huyu sio mwanangu ,hapana huyu sio mwanangu .hapana ,hapana" alipiga kelele juma.Aliutupa mkono ambao daktari alimshika kisha akamsogelea mke wake na kumuuliza.

" nimekukosea nini mke wangu?,kosa lipi? Huyu sio mtoto wangu?,sio kabisa mtoto wangu" aliongea juma huku akimtikisa mke wake.

Haukupita muda waandishi wa habari wakafika kuripoti tukio la mke wa juma kuzaa mtoto wa ajabu, ambaye anamkia.

...........

Baba tatu baada ya kutoka nyumbani alienda maeneo ya chuo kikuu .Alipaki gari lake la gharama na kuingia kwenye mgahawa mmoja.Alienda kaunta akaagiza chakula na kutoa shilingi elfu kumi.Muhudumu alipotaka kumrudishia chenji aliikataa na kumwambia abaki nayo.Alienda kukaa kwenye meza akaletewa chakula .

Macho yake yalikuwa yanaangaza kushoto na kulia kuwaangalia mabinti wa chuo.Katika angalia angalia yake macho yake yalikwama kwa mary. Ambaye ni Mwanafunzi wa mwaka wa pili pale chuo.Alimpungia mkono na kumuita.Mary alienda bila hiyana.

" habari yako binti?"

" Nzuri ,shikamoo"

" marahaba.Sasa naomba nikuagize mara moja.Nimesahau fedha ya malipo kwenye gari.Naomba kanichukulie binti yangu.Ukifungua mlango na kuingia kwenye gari,utakuta kibegi kipo kwenye siti .Kifungue utakuta hela kidogo,naomba chota kiasi niletee"

" mmmmmh!" mary aliguna.Lakini baada ya kufikiri akaona sio shida wacha aende.

" mlango nimeegesha tu,sijafunga na funguo" aliongea baba tatu.Mary alitoka moja kwa moja mpaka nje kwenye gari la baba tatu.Alifungua mlango na kuingia ndani.Alifungua mkoba alioukuta kwenye gari na kukuta noti kibao za elfu kumi kumi.

" daaah! Aisee kuna watu wanahela.Hela zote hizi.Halafu hata haogopi kuibiwa. daaaah.Ukimpata mzee kama huyu awe danga lako mbona raha sana" aliwaza mary.

=== vipi baba tatu atafanikiwa kumpata mary? Lakini swali la msingi ni kwanini anafanya hivi?====
 
SIMULIZI YA MAISHA: KWANINI MIMI? 06
MWANDISHI : MIKA AUTHOR
MSAMBAZAJI: Simulizi za Gilbert
MAWASILIANO: +255621249611

Tulipoishia - " mlango nimeegesha tu,sijafunga na funguo" aliongea baba tatu.Mary alitoka moja kwa moja mpaka nje kwenye gari la baba tatu.Alifungua mlango na kuingia ndani.Alifungua mkoba alioukuta kwenye gari na kukuta noti kibao za elfu kumi kumi.

" daaah! Aisee kuna watu wanahela.Hela zote hizi.Halafu hata aogopi kuibiwa daaaah.Ukimpata mzee kama huyu awe danga lako mbona raha sana" aliwaza mary.

Endelea nayo.

Mary alichota hela kidogo kama alivyoambiwa na kumpelekea baba tatu.Alifika ndani na kumkabidhi baba tatu.Baba tatu alizipokea na kuzihesabu.

" aaah! Mbona umeleta kidogo.Sasa hapa wewe nitakupa nini?"

" mmmh! Kwani kwenda kuchukua hela lazima unilipe mzee wangu"

" lazima nikupe kiasi bana.Kusoma ni kazi ngumu sana,inabidi uwe na hela ya kutosha ya matumizi"

" usijali mzee wangu"

" Hapana" alijibu baba tatu ,kisha akasimama kwenye kiti na kumshika mkono mary." twende kwenye gari nikakupe kiasi .Haiwezekani nikutume halafu nishindwe kukuripa" aliongea baba tatu.

Kitendo cha baba tatu kumshika mkono mary ,kilimshtua alfani ambaye ni mpenzi wa mary.Yote ayo wakati yanatokea alfani alikuwa kwa mbali akiyaangalia.Kitendo cha baba tatu kumshika mkono kilimfanya asimame na kutaka kwenda.Mary alijua mpenzi wake amechukia kwa kile kitendo.Alimbinyia jicho na kumwambia atulie.Alfani akatulia kama mary alivyomkonyeza.

Mary aliongozana na baba tatu mpaka kwenye gari.Baba tatu alifungua mlango wa gari na kuingia ndani. " ingia mbona umesimama hapo" aliongea baba tatu.Mary aliangalia kushoto na kulia kisha akaingia.

" nikulipe sh ngapi kwa kazi uliyoifanya"

" mmmh! Kazi gani? Mbona sijafanya kazi yeyote.Kukuchukulia tu hela, ile sio kazi nilikusaidia tu."

" mmmh! Kwahiyo hutaki malipo"

" ndio"

" Kama hutaki mimi nakupa tu.Niambie kwenye masomo yako nini kinakutatiza?"

" aisee shida inayonisumbua ni moja tu."

" ipi iyo?"

" sina computer mpakato ,yaani napata shida kweli kuhusu ilo.Nikitaka kuchapa kazi mbaka nimuombe mwenzangu.Na yeye akiwa anaitumia ndo ivyo nashindwa kufanya kazi zangu"

" aaah ilo tu.iyo computer mpakato inauzwa shilingi ngapi?"

" hata sifahamu,ila zipo hadi za laki tatu"

" za laki tatu izo zitakuwa used,twende nikakununulie saiz.Au unaratiba nyingine?"

" Hapana ,twende" aliongea mary.Moyoni mwake alianza kujiona mshindi.Siku zote alikuwa anatamani kupata mtu wa kumlea pale chuo.Mpenzi wake alfani alikuwa anashindwa kumuhudumia vile atakavyo.Fedha alizoziona kwenye begi na uzuri wa gari la baba tatu vilimchanganya.

Waliondoka moja kwa moja hadi kwenye maduka yanayouza komputer.Alichagua aliyokuwa anaitaka na bila shida baba tatu alilipa.Computer aliyoichagua ni aina ya dell toleo mpya,ambayo ilikuwa inauzwa laki nane.

Baada ya kununua ile computer waliingia kwenye gari." sasa mrembo tunafanyaje.Bila shaka mpaka sasa utakuwa umeshaelewa kuwa kwako mimi nimeoza.Nimevutiwa sana na wewe,ndio mana hata hela natoa bila kufikiria." aliongea baba tatu.

" Nitampa mapenzi moto moto mpaka hamsahau mke wake.Hii nafasi nitaitumia vilivyo" aliwaza moyoni Mary.

" mimi mwenyewe nilishakupenda tangu kule chuoni,ila namuogopa tu mke wako" aliongea kwa mahaba mary.

" kuhusu mke usijali.Mimi sina mke .Naishi peke yangu,kama utanifurahisha nitakuoa wewe au"

" mmmmmh! Kweli"

" ndio kwanini isiwe kweli.Nikutanie ili iweje"

Waliongea mawili matatu,baba tatu akageuza gari na kuelekea kwenye hotel moja maarufu iliyokuwa nje ya mji .Walichukua chumba na kujifungia ndani.Mary moyoni mwake alikuwa amempania baba tatu kweli kweli.Alipanga kumpa mapenzi moto moto mpaka hamsahau mkewe.

Bila kusubiri na bila maelezo baada ya kufika ndani mary alivua nguo zote na kumvamia baba tatu.Baba tatu akabaki kutoa macho kwa mshangao.Vitu alivyokuwa anafanyiwa na mary hakuwahi kufanyiwa.

" mmmh huyu chuo anasomea uhasibu au anasomea mapenzi" Aliwaza baba tatu moyoni.Wakati baba tatu anawaza ayo ,mary yeye aliwaza yake,Akili yake ilikuwa ni kumpa mapenzi moto baba tatu ili kumteka kabisa.

" nampa mapenzi moto mbaka achanganyikiwe,akichanganyikiwa najua atatangaza ndoa.Akinioa tu habari yake imekwisha,nitamuua ili nirithi mali zake zote" aliwaza mary.

Muda ulienda wakafanya waliyoyafanya.Baada ya kumaliza baba tatu alichukua begi lake na kumkabidhi mary lakin tatu." sasa mary shika hii,itakusaidia katika matumizi madogo madogo" aliongea baba tatu.

"Asante nashukuru" alijibu mary.

Walitoka pale hotelini na kuondoka.Baba tatu alimpeleka mary mpaka karibu na chuo ,akamuacha aende hostel.Mary alishuka kwenye gari na kuelekea chuoni.

" kama danga nimepata ,aaah yaani siku ya kwanza tu ameninulia laptop na kunipa laki tatu za matumizi.Danga nimepata" alijisemeha moyoni mary.Lakini wakati akipiga hatua mbele alijihishi tofauti.Aliona mwili wake haupo sawa kabisa.

" mmmh! Mbona kama mwili wangu unamatatizo? Mbona kama nimepungukiwa na kitu flani? Au ni uchovu uliotokana na kufanya mapenzi na yule mzee" aliwaza mary.

Baba tatu baada ya kumshusha mary alichukua simu na kumpigia mke wake.Simu iliita kisha ikapokelewa.

" upo wapi mama tatu?"

" nimesharudi nyumbani "

" aaaah! Mbona mapema ivyo au leo hujafanikiwa"

" Sijafanikiwa wapi? Nimefanikiwa.Leo nimekutana na kidume kweli kweli,alichonifanya ni balaa.Sina hamu naye tena"

" mmmh! Pole"

" vipi na wewe umefanikiwa?"

" Ndio nimefanikiwa.Nimekutana na mwanachuo ,anajua mambo balaaa,nimeenjoy sana kwakweli"

"Njooo basi unisimulie" aliongea mama tatu.Baba tatu alikata simu na kuelekea nyumbani kwake.

..........
Turudi kwa juma na mkewe.

Baada ya siku mbili juma na mkewe waliruhusiwa kutoka hospitali.Juma mwanzoni alikuwa anamkataa mtoto kuwa sio wake ila baada ya kupewa ushauri na madaktari alimkubali japo kwa shingo upande.

Mkewe muda wote alikuwa analia."unalia nini mke wangu? Jikaze na uvumilie ivyo ivyo.MUNGU anakusudi lake katika ili" aliongea juma kumpooza mke wake.

Ndugu wa juma walimkataa kabisa mtoto kuwa sio wa kwao.Tangu walivyotoka hospital kumuona, hawakwenda nyumbani kwa juma.

"Mmmh yule mwanamke anabalaaa kweli.Yaani mtoto wa kwanza anatuzaliwa kituko kile.Hivi kwanza yule ni mtoto au ni ndondocha?" aliuliza mama yake mzazi juma.

" mama yule mtoto atakuwa sio wa kaka juma.Yule mwanamke lazima atakuwa amezaa na mwanaume mwingine.Ukute alikuwa na mimba ya mwanaume mwingine halafu akawa anakutana na kaka, ndio maana MUNGU kamlaani vile" aliongea mdogo wake juma.

" kesho nitaenda kumuona "

" mmmh mama si ulisema hautakanyaga kwake "

" Siendi kumuona mtoto.Naenda kumuona juma.Nataka nikamwambie achague moja,achague sisi au yule mwanamke wake "

" mmmh kaka juma alivyompenda yule mwanamke ,mbona atamchagua mke wake"

" amempenda wapi? Juma yule mwanamke hajampenda wala nini. Sema madawa yanamchanganya.Yule mwanamke kamkorogea madawa ."

" inamaana unataka kusema kaka kapewa limbwata?"

" ndio we uoni ,mtu kamletea mkosi. Kamzalia mtoto asiyeeleweka baada ya kumfukuza bado anaendelea kukaa naye" aliongea mama juma huku akisimama na kuingia ndani.

..........

Kutokana na mawazo na kukosa hamu na mtoto wake.Mke wa juma alimchukua mwanae na kwenda kumuweka chumbani kisha yeye akabaki barazani.Alikaa barazani kwa muda mrefu akiwaza nini afanye.Muda huo mumewe alikuwa hayupo.

Majira ya saa tatu usiku mumewe alikuwa amesharudi ." mke wangu huyu mtoto mbona umemuweka ndani peke yake .Hebu nenda kamuangalie basi" aliongea juma.

Mkewe bila ubishi alisimama kuelekea chumbani alikomuweka mtoto.Alifungua mlango na kuingia ndani.Alitoa neti kitandani na kutoa nguo ambazo zilikuwa zimemfunika mtoto. Baada ya kumfunua nguo na kumuanglia mwanae ,mke wa juma Alishtuka na kurudi nyuma huku akisema " aaah baba tatuu,baba tatuu,baba tatu"

=== kuna nini? Kwanini mke wa nyuma ashtuke? Mtoto wake amekuwaje? na kwanini amtaje baba tatu mtu ambaye hayupo pale? ==
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom