Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,983
- 10,804
Simulizi: Kurudi Kwa Moza
Mwandishi: ATUGANILE MWAKALILE
Imeletwa kwenu na: BURE SERIES
SEHEMU YA 1
Moza alikuwa msichana mrembo ila aliishi maisha ya shida na kumfanya ajaribu kufanya kazi za ndani, na kwa bahati akapata kazi kwenye nyumba ya mama mmoja tajiri, aliyejulikana kwa jina la Rose ila huyu mama mara nyingi alikuwa hadumu na wafanyakazi wa ndani mara nyingi huwa anawafukuza na watu walijua hivyo hakuna aliyejua ukweli kuhusu wafanyakazi wa Rose kwani gafla utakuta wamepotea na ameleta mfanyakazi mpya kwahiyo wengi walihisi huwa anawafukuza.
Siku ya kwanza kumleta Moza nyumbani kwake alimpa onyo kabisa,
"Mambo ya nyumba hii uyaache kama yalivyo, wewe fanya kazi zako tu basi. Usiingilie mambo yasiyokuhusu"
"Sawa mama nimekuelewa, unadhani naweza kuingilia yasiyonihusu? Siwezi kufanya huo ujinga "
"Yani usithubutu kuingilia utaishia kubaya"
"Mbona unanitishia mama?"
"Sikutishii ila nakwambia hali halisi, umbea kwangu sitaki kabisa kama huwezi kazi unaweza umbea useme kabisa uondoke"
"Hapana mama simaanishi kuwa naweza umbea, kwanza binafsi umbea siupendi kabisa kwahiyo hata usijali kuhusu mimi"
Basi huyu mama alimuonyesha kazi zote za ile nyumba na vyumba vyote vya kusafisha, kwakweli nyumba ilikuwa ni kubwa sana lakini alimuonyesha yote, ila kulikuwa na chumba flani kilikuwa na chumba kwa ndani kile chumba kilikuwa kama choo cha ndani ya chumba na vigumu kujua kama kuna chumba ndani ya chumba, yule mama alimwambia Moza
"Hiki chumba ukishasafisha unakifunga halafu funguo unaweka juu ya mlango"
"Na hiko choo je nitakuwa nakishafishaje maana naona kufuli au hakisafishwagi?"
"Wee binti mbona umeanza kunitisha, umekionaje hiko?"
"Nilijikuta nimeangalia tu nyuma ya hilo kabati, nisamehe lakini. Kwani hakisafishwi au?"
"Hiko kilitengenezwa kwa lengo la kuwa choo ila kishazibwa na hakitumiki, nyuma yake kushabomolewa ila hapa mwanzo mlango ulibakia na kufuli, huwa hapafunguliwi maana hakuna choo wala nini na ukitoka ni nje kabisa ndiomana nimeweka kabati kama kuziba. Na wewe uache kuchunguza chunguza, kazi yako kwenye chumba hiki ni kusafisha tu nikikwambia ili kusiwe na vumbi basi ingawa halali mtu lakini panatakiwa kusafishwa."
Wakatoka nje na kumuonyesha sehemu zingine za kusafisha kisha alipomaliza ndipo Moza alianza kazi rasmi kwenye nyumba hiyo.
Moza alianza kumfahamu mtoto mmoja mmoja wa yule mama na hatimaye akamfahamu mume wa yule mama aliyejulikana kwa jina la Mr.Patrick, ila kitu kilichomshangaza Moza ni kuwa huyu baba hakuwa na sauti yoyote kwa mkewe yani chochote kitakachosemwa na mkewe kwake ni sawa, Moza alishangaa sana na kujiuliza,
"Ina maana huyu baba hawezi kuhoji? Au ndio mambo ya mjini ya mume kulelewa na mke wake, hata kama ndio akubali kila kitu. Ila nishaambiwa nisifanye umbea kwenye nyumba hii, ngoja niendelee na kazi zangu mie "
Moza aliendelea na kazi zake ila alijikuta akizoeana sana na mtoto wa kwanza wa yule mama, mtoto huyo alikuwa ni mdada mkubwa na alijulikana kwa jina la Sara, huyu msichana alimpenda Moza sababu Moza alikuwa anamsikiliza mambo yake,
"Unajua kwanini nakufagilia? "
"Sijui, hebu niambie kwanini"
"Sababu wewe unapenda kunisikiliza ninachosema "
"Unajua kila mtu anapenda kusikilizwa, lakini kwanini wewe hupendagi kumsikiliza baba yako?"
"Achana na yule baba bhana utaniudhi, kwanza hana hadhi ya kuwa na mtoto kama mimi. Yule ni bwege la mama tu"
Sara akaondoka zake ila Moza alibaki na maswali mengi sana kuwa kwanini yule Sara aseme vile, inamaana si mtoto wa yule baba? Na watoto wengine je, mbona wote hawamuheshimu yule baba? Moza aliwaza sana lakini badae alijiambia.
"Mambo ya umbea nilishaonywa kwenye nyumba hii"
Muda kidogo akiwa anafanya usafi wa kusafisha dirisha aliwasikia watoto wawili wa kiume wa yule mama Wakiongea, yule mama alikuwa na jumla ya watoto wanne, wa kwanza wakike aliyejulikana kwa jina la Sara, wa pili ni wakiume ambao walikuwa ni mapacha walijulikana kama Kulwa na Doto, wa mwisho alikuwa wakike ila alikuwa sio mkubwa sana na alijulikana kwa jina la Ana. Sasa watoto ambao Moza alitegesha sikio lake kuwasikiliza ni hao mapacha na hata hawakujua kama kuna mtu anawasikiliza, Moza alitulia tu akiwasikiliza:
"Yani mimi nikitaka kuoa nitamwomba sana Mungu nisije pata mke kama mama yetu"
Mwenzie akasikika akacheka kisha akasema,
"Kumbe inakuuma eeehh anavyofanyiwa huyu baba? "
"Yani inaniuma kinoma, sema tu ndio hivyo sio baba yetu hatuna cha kufanya ila inaniuma sana yani sana"
"Lakini moyoni unafurahia maisha ambayo mama anatupa, hivi ushawahi kujiuliza ungekuwa wapi maana baba yetu alishatukataa toka kitambo."
"Mi nadhani alichofanyiwa mama na baba yetu labda ndio kimemfanya awe hivi alivyo, ila nashukuru Mungu tunakula vizuri, tunaishi maisha mazuri tunayoyataka. Ila anayoyafanya mama yetu duh!"
"Mama alishasema tusiwaze sana na anachokifanya, tuwe makini na maisha yetu tu."
"Hata kama, hivi unakumbuka juzi aliku.......... "
Moza gafla alishtuliwa na Ana, na kumfanya ashtuke sana na aache kusikiliza umbea,
"Dada twende ukanitandikie kitanda"
Moza aliondoka na Ana huku akijiuliza maswali mengi sana juu ya yule baba mwenye Nyumba.
Moza alifika chumbani kwa Ana na kumtandikia kisha akamuuliza,
"Hivi mtoto mkubwa kama wewe unashindwaje kujitandikia kitanda"
"Wenzako kama wewe walikuwa na maswali ya kudadisi sana kwangu, kazi ikawashinda na mama akawatokomeza. Wewe umekuja kufanya kazi au kuuliza maswali?"
Ikabidi Moza amuombe msamaha mtoto Ana kisha kuondoka zake kwenda kuendelea na kazi zake huku akijiuliza maswali mengi sana.
Usiku wake Moza alishangaa yule mama akimuita kwa ukali sana,
"Wee Moza wewe"
Moza alishangaa kuitwa kwa ukali vile na kwenda kwa haraka sana, alivyofika pale tu cha kwanza alipigwa kofi hadi chini, akamtazama yule mama aliyeonekana na hasira sana, kisha yule mama akamuuliza Moza,
"Maswali gani ya kijinga hayo unamuuliza mwanangu?"
Moza alikuwa kimya alishindwa kujibu maana hakujua ubaya wa swali lake kwa yule mtoto ukizingatia anaonekana ni binti tayari wa karibia miaka kumi na mbili.
Mwandishi: ATUGANILE MWAKALILE
Imeletwa kwenu na: BURE SERIES
SEHEMU YA 1
Moza alikuwa msichana mrembo ila aliishi maisha ya shida na kumfanya ajaribu kufanya kazi za ndani, na kwa bahati akapata kazi kwenye nyumba ya mama mmoja tajiri, aliyejulikana kwa jina la Rose ila huyu mama mara nyingi alikuwa hadumu na wafanyakazi wa ndani mara nyingi huwa anawafukuza na watu walijua hivyo hakuna aliyejua ukweli kuhusu wafanyakazi wa Rose kwani gafla utakuta wamepotea na ameleta mfanyakazi mpya kwahiyo wengi walihisi huwa anawafukuza.
Siku ya kwanza kumleta Moza nyumbani kwake alimpa onyo kabisa,
"Mambo ya nyumba hii uyaache kama yalivyo, wewe fanya kazi zako tu basi. Usiingilie mambo yasiyokuhusu"
"Sawa mama nimekuelewa, unadhani naweza kuingilia yasiyonihusu? Siwezi kufanya huo ujinga "
"Yani usithubutu kuingilia utaishia kubaya"
"Mbona unanitishia mama?"
"Sikutishii ila nakwambia hali halisi, umbea kwangu sitaki kabisa kama huwezi kazi unaweza umbea useme kabisa uondoke"
"Hapana mama simaanishi kuwa naweza umbea, kwanza binafsi umbea siupendi kabisa kwahiyo hata usijali kuhusu mimi"
Basi huyu mama alimuonyesha kazi zote za ile nyumba na vyumba vyote vya kusafisha, kwakweli nyumba ilikuwa ni kubwa sana lakini alimuonyesha yote, ila kulikuwa na chumba flani kilikuwa na chumba kwa ndani kile chumba kilikuwa kama choo cha ndani ya chumba na vigumu kujua kama kuna chumba ndani ya chumba, yule mama alimwambia Moza
"Hiki chumba ukishasafisha unakifunga halafu funguo unaweka juu ya mlango"
"Na hiko choo je nitakuwa nakishafishaje maana naona kufuli au hakisafishwagi?"
"Wee binti mbona umeanza kunitisha, umekionaje hiko?"
"Nilijikuta nimeangalia tu nyuma ya hilo kabati, nisamehe lakini. Kwani hakisafishwi au?"
"Hiko kilitengenezwa kwa lengo la kuwa choo ila kishazibwa na hakitumiki, nyuma yake kushabomolewa ila hapa mwanzo mlango ulibakia na kufuli, huwa hapafunguliwi maana hakuna choo wala nini na ukitoka ni nje kabisa ndiomana nimeweka kabati kama kuziba. Na wewe uache kuchunguza chunguza, kazi yako kwenye chumba hiki ni kusafisha tu nikikwambia ili kusiwe na vumbi basi ingawa halali mtu lakini panatakiwa kusafishwa."
Wakatoka nje na kumuonyesha sehemu zingine za kusafisha kisha alipomaliza ndipo Moza alianza kazi rasmi kwenye nyumba hiyo.
Moza alianza kumfahamu mtoto mmoja mmoja wa yule mama na hatimaye akamfahamu mume wa yule mama aliyejulikana kwa jina la Mr.Patrick, ila kitu kilichomshangaza Moza ni kuwa huyu baba hakuwa na sauti yoyote kwa mkewe yani chochote kitakachosemwa na mkewe kwake ni sawa, Moza alishangaa sana na kujiuliza,
"Ina maana huyu baba hawezi kuhoji? Au ndio mambo ya mjini ya mume kulelewa na mke wake, hata kama ndio akubali kila kitu. Ila nishaambiwa nisifanye umbea kwenye nyumba hii, ngoja niendelee na kazi zangu mie "
Moza aliendelea na kazi zake ila alijikuta akizoeana sana na mtoto wa kwanza wa yule mama, mtoto huyo alikuwa ni mdada mkubwa na alijulikana kwa jina la Sara, huyu msichana alimpenda Moza sababu Moza alikuwa anamsikiliza mambo yake,
"Unajua kwanini nakufagilia? "
"Sijui, hebu niambie kwanini"
"Sababu wewe unapenda kunisikiliza ninachosema "
"Unajua kila mtu anapenda kusikilizwa, lakini kwanini wewe hupendagi kumsikiliza baba yako?"
"Achana na yule baba bhana utaniudhi, kwanza hana hadhi ya kuwa na mtoto kama mimi. Yule ni bwege la mama tu"
Sara akaondoka zake ila Moza alibaki na maswali mengi sana kuwa kwanini yule Sara aseme vile, inamaana si mtoto wa yule baba? Na watoto wengine je, mbona wote hawamuheshimu yule baba? Moza aliwaza sana lakini badae alijiambia.
"Mambo ya umbea nilishaonywa kwenye nyumba hii"
Muda kidogo akiwa anafanya usafi wa kusafisha dirisha aliwasikia watoto wawili wa kiume wa yule mama Wakiongea, yule mama alikuwa na jumla ya watoto wanne, wa kwanza wakike aliyejulikana kwa jina la Sara, wa pili ni wakiume ambao walikuwa ni mapacha walijulikana kama Kulwa na Doto, wa mwisho alikuwa wakike ila alikuwa sio mkubwa sana na alijulikana kwa jina la Ana. Sasa watoto ambao Moza alitegesha sikio lake kuwasikiliza ni hao mapacha na hata hawakujua kama kuna mtu anawasikiliza, Moza alitulia tu akiwasikiliza:
"Yani mimi nikitaka kuoa nitamwomba sana Mungu nisije pata mke kama mama yetu"
Mwenzie akasikika akacheka kisha akasema,
"Kumbe inakuuma eeehh anavyofanyiwa huyu baba? "
"Yani inaniuma kinoma, sema tu ndio hivyo sio baba yetu hatuna cha kufanya ila inaniuma sana yani sana"
"Lakini moyoni unafurahia maisha ambayo mama anatupa, hivi ushawahi kujiuliza ungekuwa wapi maana baba yetu alishatukataa toka kitambo."
"Mi nadhani alichofanyiwa mama na baba yetu labda ndio kimemfanya awe hivi alivyo, ila nashukuru Mungu tunakula vizuri, tunaishi maisha mazuri tunayoyataka. Ila anayoyafanya mama yetu duh!"
"Mama alishasema tusiwaze sana na anachokifanya, tuwe makini na maisha yetu tu."
"Hata kama, hivi unakumbuka juzi aliku.......... "
Moza gafla alishtuliwa na Ana, na kumfanya ashtuke sana na aache kusikiliza umbea,
"Dada twende ukanitandikie kitanda"
Moza aliondoka na Ana huku akijiuliza maswali mengi sana juu ya yule baba mwenye Nyumba.
Moza alifika chumbani kwa Ana na kumtandikia kisha akamuuliza,
"Hivi mtoto mkubwa kama wewe unashindwaje kujitandikia kitanda"
"Wenzako kama wewe walikuwa na maswali ya kudadisi sana kwangu, kazi ikawashinda na mama akawatokomeza. Wewe umekuja kufanya kazi au kuuliza maswali?"
Ikabidi Moza amuombe msamaha mtoto Ana kisha kuondoka zake kwenda kuendelea na kazi zake huku akijiuliza maswali mengi sana.
Usiku wake Moza alishangaa yule mama akimuita kwa ukali sana,
"Wee Moza wewe"
Moza alishangaa kuitwa kwa ukali vile na kwenda kwa haraka sana, alivyofika pale tu cha kwanza alipigwa kofi hadi chini, akamtazama yule mama aliyeonekana na hasira sana, kisha yule mama akamuuliza Moza,
"Maswali gani ya kijinga hayo unamuuliza mwanangu?"
Moza alikuwa kimya alishindwa kujibu maana hakujua ubaya wa swali lake kwa yule mtoto ukizingatia anaonekana ni binti tayari wa karibia miaka kumi na mbili.