Simulizi -Kitabu kilichojaa majina yote

Boss kuna kigongo kipya hapa kinaendelea kwenye grupu ,inatumwa kila siku vipande vitatu kujiunga ni 2000 tu kwa mwezi ,zipo simulizi zingine pia zinatumwa kila siku simulizi zenyewe ni Book of all names ,Masaa mawili ya kumbukumbu season 2 ,My Freedom ,Waraka wa rais kabla ya kifo.Lipia kwenye namba 0687151346 Airtel Au 0657195492 Tigo Au 0623367345 Halopesa Ukilipa nitumie message ya muamala NAKUKUMBUSHA SIMULIZI NI MPYA INAITWA "NILIMDHANIA NI KAHABA KUMBE BIKRA Leo tunaanza na vipande vitatu hii sio ya kukosa ni nzuri mnp na inasisimua
DEMU%201.jpg
 
Hilo group ukiingia Si inakosa mwanzo wa hadidhi au ni telegram. Maana WhatsApp huwezi ona matukio ya nyuma kabla ya kujiunga
 

SURA YA 21​

Upande wa huku hospitalini yule baba aiekuja na kijana huyu hospitalini , alikuwa katika hali ya wasiwasi sana na hii ni baada ya kumtafuta Hassani kila kona pasipo kumuona , alijikuta akichanganyikiwa na kuogopa kwa wakati mmoja , alihofia Hassani asije akafanya kitendo hatarishi , kwani alikuwa kwenye majonzi.

Mwanadada Lisa alionekana ni mwenye kuguswa sana na tukio lile . hali ile ilimfanya kukosa amani na kujikuta akiomba wenzake ruhusa kwamba anarudi nyumbani walikokuwa wamepanga , kwani walikuwa ndani ya hospitali hii ya Bombo kwa ajili ya mafunzo ya vitendo .

Baada ya kurudi nyumbani alijikuta akikosa raha kabisa , ni kama mtu ambaye alikuwa akikukumbuka matukio ya nyuma ambayo yalimkosesha Amani , baada ya kuona mawazo bado yanamwandama , alitoka ndani na kisha alisogea upande wa barabarani na kuita bodaboda iliompeleka mpaka mtaa wa Raskazoni sehemu ambayo alikuwa akipendelea sana kukaa pindi anapokuwa na mawazo .

Baada ya kushushwa alijikuta akitembea taratibu sana kutafuta sehemu ya kukaa na ile anageuza upande wa kulia alijikuta akimuona yule kijana aliekuwa hospiutalini akilia , Lisa alijikuta akisogelea na kukaa kwenye kile kimbweta alichokuwa amekaa huyu kijana.

“Pole sana”Ni sauti iliosikika kwa mara ya pili kwenye masikio ya kijana Hassani na kujikuta akigeuza macho yake na kumwangalia mtu anaempa pole , maana hakuwa akijua kuwa pembeni yake kulikuwa na mtu aliekuwa amekaa .

Kijana huyu ambae alionekana kuwa na maisha Duni kutokana na maazi yake aliokuwa amevaa , alijikuta akimwangalia mwanadada huyu mwenye uzuri wa ajabu .

Lakini Lissa ni kama alikuwa amefungulia kilio kwa wakati mwingine kwa kijana huyu , kwani alianza kulia tena kwa kwikwi akionyesha alikuwa kwenye machungu makubwa sana.

“Nimemuua baba , sistahili kuonewa huruma”Aliongea kijana huyu jambo ambalo lilimfanya mwanadada huyu kushangaa ni kwanini kijana huyu anatamka neno kama hilo .

“Sio kweli hupaswi kujilaumu , kila kitu hutokea kwasababu ni mipango ya Mungu”Aliongea mwanadada Lisa huku akionekana kumuonea huruma kijana huyu .

“Kifo cha baba nimekisababisha mimi , na wala sio mpango wa Mungu”

“Sio kweli ni mipango ya Mungu usiseme hivyo”

“Kama Mungu amenionyesha hili jambo kabla ya kutokea , huu sio mpango wa Mungu hata kidogo , mimi ndio wa kupaswa kulaumiwa”Aliongea na kisha alinyanyuka na kuondoka .

Hakika maneno haya yalimchanganya sana mwanadada huyu Lisa , hakuelewa ni kwanini kijana huyu anaongea maneno hayo , alitamani sana kujua ni kwasababu ipi kijana huyu alikuwa akisema amemuua baba yake ,jambo ambalo ni mara chache sana kulisikia ,na hata kama ni kweli kwannini kijana huyo alikuwa akili ilihali alimuua baba yake , na hata kama ilikuwa ni nahati mbaya je ilikuwaje , hayo yote yalikuwa ni maswali aliojiuliza Lisa huku akiendelea kuangalia maji ya bahari .

*****

Naam Ndani ya kijiji cha Nkumba wilayani Muheza ndani ya nyumba moja ndogo sana iliokuwa imeezekwa kwa nyasi tofauti na nyumba zote zilizokuwepo ndani ya kijiji hiki , walionekana baadhi ya wanakijiji waliokuwa na hali ya simanzi kwenye nyuso zao , na hii ni mara baada ya kupokea mwili wa Mzee Nyangwe aliekuwa amefariki ndani ya hospitali ya Bombo Tanga .

Licha ya mazingira kuwa finyu ndani ya eneo hilo , lakini watu walionekana kujaa kwelikweli,huku kijana Hassani aliekuwa amejibanza pembeni ya nyumba yao alionekana ni mwenye huzuni kweli , mrafiki zake kutoka shule ya sekondari Nkumba walikuwa wakimpa pole lakini badi hawakuweza kutoa hali ya huzuni aliokuwa nayo kijana huyu .

Baada ya kama masaa manne kupita ndipo mwili wa marehemu ulitolewa nje na Shekhe alianza kuswali dua kwa ajili ya kuombea mwili huo , kitendo ambacho kilifanyika kwa lisaa na baada ya hapo safari ya kuupeleka kwenye nyumba yake ya milele ilianza , vijana walipokezana kubeba mwili huo kwa kujipanga njiani kuelekea lilipo shamba la Mzee Nyangwe sehemu ambayo ndio kaburi lake lilikuwa limechimbwa.

Ni ndani ya masaa kadhaa baada ya kuupeleka mwili wa mzee Nyangwe katika nyumba yake ya ,milele , muda wa saa sita kamili ndani ya nyumba hii ya mzee Nyangwe kulionekana kumepoa kutokana na kwamba maziko yalikuwa yamekwisha kufanyika na hakukuwa na lingine la kufanyika hapo nyumbani , kwani familia mzee nyangwe maisha yake ya hapo kijijini yalikuwa ni ya kimasiikini sana , kiasi kwamba hata kwenye huo msiba hakuna chochote kilichokuwa kimepikwa.

Ni karibu watu watano tu ndio waliiokuwa wamebakia hapo nyumbani mmoja akiwani rafiki yake wa karibu wa Hassani na wengine walikuwa ni family ya mzee Kitasa ambae ni yule aliemsindikiza Hassani Hospitalini.

Wakati hayo yakiendelea mara baada ya dakika chache walionekana vijana kadha wakiingia ndani ya eneo hilo huku wakiwa wameongozana na mwanadada Lisa ambae haikueleweka amefikaje ndani ya kijiji hicho , , watu wengi wa kijiji hicho walimshangaa sana mwanadada huyo , hasa pale alipoeleza kwamba amekuja kwenye msiba wa Mzee Nyangwe Jambo ambalo liliwashangaza wanakijiji hawa , kwani walikuwa wakimjua mzee ?nyangwe hakuwa na ndugu mjini na juu ya yote ni mwanadada huyu kuja akiwa na gari la kifahari . .

Hassani alijikuta akishangaa sana ujio wa mwanadada huyu , kwani katika kumbukumbu zake ni kwamba mara walipoonana kule Raskazoni hawakuongea chochote Zaidi ya Hassani kunyanyuka na kuondoka .

“Pole sana”

Ni neon ambalo kwa mara ya tatu mwanadada huyu analitamka akimwambia Hassani.

“Asante”Aliongea Hassani huku akimwangalia kwa Mshangao wanadada huyu .

“Karibu sana Dokta kiti”Aliongea Mzee Kitasa kwani alikuwa akimkumbuka mwanadada huyu kama moja ya madaktari waliokuwa wamemfanyia mzee Nyangwe upasuaji jambo ambalo lilimshangaza kidogo Hassani.

Lisa alieleza kwamba amekuja kwa ajili ya msiba , lakini pia alieleza kuwa alikuwa amegunswa na maneno ambayo kijana Hassani alikuwa akiyatamka , alitaka kujua ni kwanini kijana huyo alikuwa akisema kwamba yeye ndie aliemuaa baba yake

Na hapo ndipo alipoweza kusimuliwa kisa ambacho kilimsisimua na kumsahangaza sana mwanadada huyu .

*****

Kwa majina yangu halisi naitwa Hassani Hamisi Nyangwe nimezaliwa hapa hapa kijijini kwetu na kukulia hapa hapa , mpaka kufikia umri huu wa miaka kumi na sita nikiishi na baba yangu Nyangwe , kwani mama yangu alifariki punde tu baada ya kunileta duniani.

Maisha yetu kwa ujumla sio mazuri sana na naweza kusema kwamba kwa hapa kijijini ni familia yetu pekee ambayo ilikuwa ni ya umasikini uliokithiri , lakini licha ya hivyo sikuwahi hata mara moja kujilaumu kuzaliwa katika aina hii ya familia , kwani nilichokuwa nikiamini katika maisha yangu ni kwamba Mungu ndio mpaji wa yote.

Licha ya umasikini wetu nilikuwa nikimpenda sana baba yangu mzee Nyangwe na hata yeye ia alikuwa akinipenda sana , naweza kusema kwamba tokea nifikie umri wa kujielewa Mzee Nyangwe kwangu ndio baba ndio mama kwangu na kwangu nilimchukulia kama zawaidi ambayo Mungu amenipa

Maisha yetu hapa kijijini kwa ujumla wake licha ya kuwa masikini , yalikuwa ni ya furaha sana , kwani mimi na baba tuliishi maisha kama washikaji , na tulikuwa tumezoeana sana kiasi kwamba hata baadhi ya wanakijiji walikuwa wakishangaa namna ambavyo nilikuwa nimemzoea mzee .

Lakini licha ya furaha niliokuwa nayo katika maisha yangu , kuna jambo moja tu ambalo lilikuwa likinisumbua sana katika maisha yangu na hili ni jambo ambalo nilizaliwa nalo , sikuwahi kujua uwezo huu ambao nilizaliwa nao ulikuwa ukimaanisha nini katika maisha yangu na siku niliokuja kuanza kujua nina uwezo huu ni kipindi nikiwana miaka kumi.

Ilikuwa ni siku ya ijumaa jioni baada ya kumaliza kujisomea kwani kipindi hicho nilikuwa darasa la pili, kama ilivyokuwa kawaida baada ya kusoma nilipanda kitandani na kuutafuta usingizi , kitanda ambacho nilikuwa nikilala na baba , kwani nyumba yetu ilikuw ani ya vyumba viwili tu yaani jiko na sehemu ya kupikia .

Basi wakati nikiwa kwenye usingizi ilinijia ndoto nikiwa naenda shule asubuhi siku ya jumatatu , siku ambayo kwenye ndoto niliona ni siku ambayo ilikuwa na mvua, na hata mwendo ambao nilikuwa nikitembea ni wa kukimbia ili kuepuka kuloanisha nguo na madaftari , basi wakati nafika shule ya sekondari Nkumba , shule ambayo ilikuwa imepaka na shule ya msingi Nkumba , nilijikuta nikiteleza na kutumbukia kwenye mtaro ambao ulikuwa ndio kama mpaka kati ya shule ya sekondari na ya msingi Nkumba , na kutokana na kwamba siku hio mvua ilikuwa imenyesha sana na ule mtalo ulikuwa umejaa maji machafu , yalinichafua mwili mzima na kufanya wanafunzi wenzangu ambao walikuwa wamesimama kwenye korido za madarasa kunicheka .

Kabla ya ndoto kuisha nilijikuta nikiamshwa na baba .

“Wewe hassani Amka kumekucha tujiandae twende shambani”

Basi niliamka baada ya baba kuniamsha na niliwasha moto na kuchemsha mihogo ambayo kwa kipindi hicho ndio kilikuwa chakula chetu kikubwa , kwani ni zadi ya miezi tisa mvua hazijawahi kunyesha na hata msimu wa kulima mahindi ulikuwa unakaribia kupita , lakini mvua bado haikuwa hata na dalili.

Basi hatimae tulienda shambani na kulima na kurudi nyumbani muda wa jioni huku tukiwa tumechoka sana .

“Hivi Hassani mvua isponyesha sijui maisha yatakuwaje miezi ijayo , maana sio kwa hili jua”Aliongea mzee huku akirusha Jembe chini .

“Nimeota mvua itanyesha Jumatatu”

“Hio ni ndoto tu , sidhani kama itanyesha” Aliongea baba na mimi nikacheka na kupotezea na hata siku hio ilipita na siku pia ya jumapili ilipita na siku ya jumatatu ikafika , siku ambayo nilichelewa sana kuamka kiasi kwamba baba ndie alieniamsha .

“Wewe Hassani amka mvua imepungua uwahi shuleni utachelewa”Aliongea baba ambae alinifanya nikurupuke na kuanza kujiandaa kuelekea shuleni , huku nikiwa nimechelewa kweli halafu wiki hio iliokuwa inaanza ilikuwa ni zamu ya mwalimu Bony , mwalimu ambae alikuwa akiogopeka sana kwa kuchapa , alikuwa ni mkurya na alikuwa na kajimsemo kake akitaka kukuchapa anakwambia “Okoa muda” na hata kwenye meza yake ofisini alikuwa ameandika hilo neno la “Okoa Muda” sasa shuleni ndio tulikuwa tunamuita kwa jina hilo la Mzee wa kuokoa Muda , na siku ukiona mwalimu huyu anakwambia okoa Muda basi jua tu anamaanisha lala ule zako ambapo ukiamka baada ya kichapo wiki nzima utakuwa unakaa kwa maumivu mengi sana darasani na pengine usije kabisa shuleni.

Basi nilijiandaa harakaharaka na kunywa chai isiokuwa na sukari na kisha ninakimbia kuelekea shuleni huku mvua ikiwa inayesha japo sio sana , niliungana na wanafunzi wenzangu na kuendelea na safari , huku nikiwa nimesahau kabisa ndoto niliokuwa nimeota usiku wa kuamkia jumamosi , basi ile nilivyofika katika mtalo nilijikuta nikteleza na kutumbukia mtaloni na kuchafuka mwili mzima , huku wanafunzi wenzangu wakiwa wanazomea na kucheka , hakika ilikuwa ni aibu sana kwangu , nilijiangalia na kujiona sifai kuendelea kubaki hapo shuleni na kugeuza taratibu kurudi nyumbani kwani nisingeweza kuendelea na masomo kwa namna ambavyo nilikuwa nimechafuka na nilikuwa nikitoa harufu.

Sasa wakati narudi ndio nikaanza kukumbuka ile ndoto niliokuwa nimeota , hakika nilishangaa kabisa , kwani kila kitu kilichokuwa kwenye ile ndoto ndio kilichokuwa kimenitokea nilishangaa lakini mwisho wa siku niliipotezea japo pia nilimwambia baba , lakini hata yeye hakuizingatia sana.

Basi siku zilipita na baada ya wiki nilijikuta nikiota ndoto nyingine na hii ilikuwa ni ndoto ambayo nilimuona baba aking`atwa na nyoka , ndoto hii wakati naona ilikuwa ni siku ya jumaanne kuelekea Jumatano na jambo la kushangaza ni kwamba siku hio hio ya Jumatano wakati narudi shuleni nilipokea taarifa kutoka kwa mke wa mzee Kitasa kwamba baba ameng`atwa na nyoka na amepelekwa hospitali ya Teule , taarifa hio ilinishitia mno na kunishangaza kwa wakati mmoja , kwani nilichokuwa nimeota ndio hiko hiko kilichokuwa kimetokea na nilichokuwa nikitaka kuhakikisha ni sehemu ambayo baba alikutwa na janga hilo , na baada ya siku mbili za kutoka hospitali ya Teule ndio nikamwambia baba anionyeshe mahali ambapo alikutwa na mkasa huo wa kung`atwa na nyoka na sehemu alionipeleka ni pale pale ambapo nilipashuhudia ndotoni na hili swala niliamua kumsimulia na baba akaniambia kwamba .

“Hizo ni ndoto tu Hassani hazina maana yoyote “

“Lakini baba hii ni mara ya pili naota kitu kinatokea kweli bahati mbaya haitokeagi mara mbili”

“Basi tufanye hivi kama itatokea umeota mara ya tatu na ikawa kweli nitakupeka kwa mzee Kigo asome nyota yako huenda ukawa Nabii”Aliongea mzee na mimi nikakubaliana nae.

Basi ilipita mwezi namini nilisahau kabisa lile swala na tulikuwa kwenye mfungo wa Ramadhani mwezi wa tano , kipindi ambacho tulikuwa tukielekea kumaliza muhula wa kwanza shuleni ili tufunge shule .

Basi siku moja niliota nyumba ya Mzee Kesi ikiungua na moto huku yeye na familia yake yote wakiwa ndani , na tena ilikuwa ni muda wa usiku kabisa , Mzee kesi alikuwa ni moja ya watu waliokuwa na pesa hapo kijijini , kwani alikuwa akimiliki ‘Chain Saw’(mashine ya kukatia miti na mbao) na kupitia mashine yake hio alikuwa akijipatia pesa nyingi sana kwa kuuza mbao lakini pia kukodisha , mzee huyu alikuwa na familia ya watu saba , mke wake, yeye mwenyewe , Ratifa ambae alikuwa Sekondari Nkumba , Abasi ambaye alikuwa ni mkubwa kabisa ashamaliza shule ila alikuwa akiishi na wazee wake oamoja na wajukuu zake watatu mmoja akiwa ni mtoto wa Abasi aliezaa na mwanamke ambaye alimkimbia na wengine wawili walikuwa ni watoto wa mtoto mkubwa wa mzee Kesi aliekuwa akifahamika kwa jina la Mwantumu ambae alikuwa jijini Dar es salaam.

Basi siku ile kwangu nilikuwa na wasiwasi sana juu ya ile ndoto na mbaya Zaidi sikuwa nyumbani Nkumba siku hii , kwani tulikuwa tumeenda Magila kupasua mawe mimi na baba na Mzee Kitasa , wakati tupo njiani nilimweleza mzee huyu juu ya ndoto hio lakini hakuwa ni mtu wa kuzingatia namimi nikapotezea .

Nakumbuka siku hii tuliweza kurudi muda wa saa moja kasoro hivi na wakati tunafika Nkumba bahati nzuri niliweza kukutana na Ratifa ambae alikuwa amebeba ndoo ya maji akiwa ametangulizana na mtoto wa Abasi aliekuwa akifahamika kwa jina la Adam aliekuwa anasoma Chekechea akiwa na yeye amebeba maji kwenye kigaloni cha lita tatu .

“Dada Rat nimeota ndoto nyumba yenu inaungua”

“Wewe mtoto hebu acha kutuwangia bhna” Aliongea Ratifa kwa dharau na mimi sikumjali sana nikasepa zangu kwani kipindi hiki nilikuwa mtoto na hata ningemwambia mtu asingeniamini. .

Basi nilikuja kuamshwa na vilio vya watu muda huo ilikuwa ni saa Sita za usiku na hata nilipoangalia pembeni baba sikumuona , nilijikuta nikitoka nje na ile natoka tu niliona wingu la moshi likiwa limetanda uelekeo wa nyumba ya Mzee kesi , lakini ile nashangaa sauti za vilio huku nikisia wamam wanaongea kwa sauti ‘Nyumba ya mzee kesi jamani inaungua na wenyewe wapo ndani”

Kusikia hivyo tu nilijikuta nikipatwa kama mshituko wa moyo huku mapigo ya moyo yakienda kwa kasi sana , nilitoka na kuelekea upande huo , sehemu ambayo ulikuwa ukivuka nyumba nne tu unakuwa umefika na ile nafika ni kama vile nipo ndotoni , kwani vile vile moto ulivyokuwa unawaka ndio nilicyo ota , huku watu wakihangaika kuokoa watu waliondani , na maji kumwagwa , lakini ni kama moto ulikuwa ukizidi .

“Bahati nzuri ni kwamba wazee wa kijiji walifanikiwa kutoboa tundu na kuanza kuitia jina la Mzee Kesi wakimwambia atoke lakini tulichoweza kusikia ni neno moja tu kwa mzee Kesi , kwamba hawezi kutoka ilihali familia yake yote imeshateketea kwa moto , wanakijiji walijaribu kumbembeleza mzee Kesi atoke , lakini halikusaidia kwani hakutoka.

Mpaka inafika saa tisa za usiku moto ulikuwa umezima , lakini vilio vilikuwa vya aina yake , sio watoto sio wazee watu walishindwa kujizuia ,kila aliekuwa akiangalia miili iliokuwa imetolewa na kupangwa nje ikiwa imeungua vibaya alijikuta akilia sana , Siku hii pia nililia mno , yaani sana huku nikijiona mkosaji sana .

Tukio hili liliniathiri vibaya sana kisaikolojia kiasi kwamba hata usiku nilikuwa nikiogopa kulala kwa kuhofia kuota jambo baya , na ukiachilia kwamba hiki kipindi bado nilikuwa mtoto ,,Baba nae alijaribu kuniweka sawa , lakini bado niliogopa sana kwa wakati mmoja .

Basi baada ya wiki kupita mzee alinichukua na kunipelka kwa mzee kigo kwa ajili ya nyota yangu kuangaliwa

Mzee kigo alikuwa ni mganga aliekuwa akifahamika sana pale kijijini na kuogopeka sana , alikuwa akifichua wachawi wengi lakini pia kutibu watu wengi wenye shida mbali mbali , na wengi walikuwa wakitoka mpaka mikoani kwa ajili ya kuja kupata huduma kwa mzee Kigo.

Basi nilipokelewa na kuanza kufanyiwa tiba pale , akachukua kioo chake flani hivi alikuwa akikipaka unga flani ambao sikuwa nikiujua halafu anakirusha juu kinatua chini huku anaongea maneno anayoyajua yeye halafu anaangalia tena , na anakirusha tena juu na kinatua chini , , alivyomaliza , alikichukua akaitumbukiza kwenye maji yaliokuwa yamejaa kwenye chungu kikubwa na kisha aliweka unga flani hivi kama majivu na kisha akakitoa kile kioo na kukifuta na kisha akanisogelea na kukiweka kwenye uso wangu , yaani mimi nikiangalia nyuma ya kioo na kisha yeye akiangalia mbele ya kioo.

Baada ya dakika mbili alijikuta akishituka sana na kukidondosha kile kioo na kisha akanza kuniangalia kwa umakini huku akiokota kile kioo na wakati huo baba alikuwa anaangalia tu kinachoendelea .

Baada ya kama dakika kumi hivyo alionekana kumaliza kile alichokuwa anakifanya na kisha alinipa kisu na kuniambia nichukue Jogoo ambae tumekuja nae , maana kwa huyu mzee sheria zake kama unataka kusomewa nyota yako , basi unatakiwa kuja na jogoo mweupe na mchanga wa mlangoni , yaani pale kwenye mlango wa kutokea unachimba chini na unachukua mchanga..

“Tayariii ….. Tayariii …. Hassaniii …” aliongea kwa sauti yake ya kutisha pale na tulikuwa tayari kwa kupokea majibu

SURA YA 22​

“Kijana umezaliwa na bahati kubwa sana kwenye maisha yako , Mababu wa ukoo wako wamekupatia uwezo wa kutambua mambo yatakayokuja”

“Unamaanisha nini Mzee Kigo?”Aliuliza baba

“Hassani ni Mlinzi mkuu wa kijiji hiki , mababu wa koo zote hapa Nkumba wamemchagua kama mlinzi , ilikuwa kosa kubwa sana kuruhusu familia ya mzee Kise kuungua na moto , ulitakiwa kuwaokoa, maana ni jukumu la mababu wa koo waliokupatia na hivi sasa wamekasirika na wanapaswa kutulizwa” aliongea Mzee Kigo na kumfanya Mzee wangu kushituka na kujawa na wasiwasi , kwangu mimi sikuwa na imani sana na mambo ya kiganga tofauti na Mzee ambae yeye alikuwa ni muuminni mzuri tu.

“Kwa hio tunafanyaje mzee Kigo”.

“Kafara ya Mbuzi kwa kila koo inatakiwa kufanyika kwa ajili ya kuwatuliza mababu wa koo”.

Basi kama alivyolekeza tuliweza kutoa kafara ya Mbuzi ambayo tunachinja huko juu milimani kabisa kwenye pango moja , pembeni kabisa na kilipo chanzo cha maji ambayo ndio hutumiwa na watu wa kijijini kwetu kwani kulikuwa kumeunganishwa mabomba .

Basi baada ya hapo niliendelea kuota ndoto za kweli tu na katika kuota ndoto hizo , hakuna siku ambayo hata moja niliweza kuzuia ndoto mbaya kutokutokea , yaani nilichoweza mimi ni kuota tu lakini sikuweza kuzuia kile nilichokuwa nikiota kutokutokean kama ni kibaya , licha ya maneno ya Mzee Kigo kwamba ninatakiwa kuzuia.

Basi baada ya miaka kupita , siku ya ijumaa kuelekea jumamosi , mzee wangu muda wa usiku aliweza kuniambia kuwa siku ya kesho wanaelekea Muheza mjini kwa ajili ya kuuza vitunguu na Mzee Kitasa, huku akiniachia kazi ya kwenda kumwagilia pilipili asubuhi na mimi nilikubali na kisha tukala tukalala , basi usiku niliweza kuota ndoto mzee anagongwa na pikipiki Muheza mjini.,ndoto ambayo nilivyokuja kushituka ilikuwa ni saa kumi na moja kama na nusu hivi asubuhi na nilipoangalia pembeni sikumuona mzee ,nilijikuta nikikurupuka na kutoka nje kumwangalia kama mzee yupo lakini sikumuona , nilichokifanya ni kutulia na kusubiria , kwani mzee aliniambia ni asubuhi na huwaga hana ile tabia ya kuondoka pasipo kuniamsha , nilirudi ndani na kusubiri mpaka saa moja na robo ndipo hofu ilipo nijaa na kujua lazima mzee atakuwa amekwisha kwenda Muheza , niliinuka mbio na kwenda nyumbani kwa Mzee kitasa na nilimkuta mke wake akiwa nje anafagia nilimsalimia na kisha kumuuliza kama mzee alikuwa ashaenda mjini na jibu lake ndio liliniacha hoi kwani aliniambia kuwa walikwisha kwenda toka saa kumi na moja .

Nilijihisi kuchangayikiwa na hilo hata kwa mama Jabu aliliona hilo .

“kwani kuna nini Hassani?”

“Baba atakufa , nimeota anakufa” Niliongea na mama Jabu alijikuta akishituka mno kwani pia hata yeye alikuwa akijua uwezo wangu huo wa kuota vitu vinatokea .

“jamani jamani sasa tunafanyaje ?”

“naenda ,mjini mama Jabu niazime hela kidogo”

Basi mama Jabu alinipatia elfu moja na miatano ya nauli na kisha nikapanda bodaboda kuwahi mjini kumuokoa baba , safari ambayo kama ningejua nisingeenda , kwani ile nafika uwanja wa jitegemee , sijui ilikuwaje , kuna mtoto alikuwa barabarani na sisi tukawa tupo kwenye spidi kali halafu mbele yetu kulikuwa na gari ya Tanesko inakuja , sasa katika harakari za kumkwepa mtoto yule bodaboda alijikuta akichukua uelekeo wa kwenda hopitali ya Teule na hapo ndipo nipokuja kushitukia baba yupo mbele yetu na pikipiki ilikuwa kwenye spidi kali ,na kilichotokea ni kwamba baba tulimgonga na kumrusha upande mwingine na akaenda kuvaa chuma cha mashine ya kupasulia mbao upande wa kushoto na kujigonga kisha akatumbukia mtaloni huku damu zikiwa zimetapakaa .

****

“Pole sana Hassani , sasa hukujiona kwenye hio ndoto ukiwa kwenye pikipiki?”

“Hapana sikujiona nilchoota ni baba kugongwa na pikipiki tu ila sikujua pikipiki hio ndio itakuwa nitakayopanda” Alijibu Hassani huku mwanadada Lisa akiguswa mno na simulizi hio , licha ya kushangaa uwezo aliokuwa nao Hassani wa kuota mambo yanayotokea kweli , lakini swala la ajali ya baba yake kusababishwa na yeye mwenyewe katika harakati za kumuokoa lilimgusa mno , na aliona ni kweli kijana huyu alikuwa na haki ya kutamka yale maneno ya kwamba amemuua baba yake .

“Mimi naamini kuna kitu cha ziada juu yako , labda hujakitambua bado”

“:Sidhani kama kuna kitu kama hicho ,, hii ni laana kwangu , haiwezekani niote vitu ambavyo ni vya kweli ila nishindwe kuzuia matukio mabaya ninayoota”

“Ushawahi kutoa tukio lolote ambalo sio la kutisha ?”

“Sijawahi kuota “

“Basi kunasababu ya kuwa hivyo Hassani , naamini ni uwezo ambao Mungu kakupatia akiwa na sababu zake”

“Siamini hivyo Sister”

Basi mwandda huyu alitoa rambirambi yake na kisha kuaga huku akiahidi kurudi Nkumba akiwa na jibu juu ya uwezo wa Hassani.

Je simulizi hii inauhusiano gani na Book of all names tuendelea tulipoishia

*****

MIEZI MIWILI BAADA YA MAANDALIZI. ,SIKU MOJA KABLA YA SIKU AMBROSE AKISIMULIWA SIMULIZI YA BOOK OF ALL NAMES

WACO –TEXAS


Ni ndani ya shamba moja kubwa lililokuwa likimilikuwa na bwana mmoja aliekuwa akifahamika kwa jina la Hudson , shamba hili lilionekana kujaa mahindi mengi ambayo yalikuwa akikaribia kuvunwa , kwani yalikuwa kwenye hatua za mwisho , ilikuwa ni muda wa mchana , muda ambao bwana Hudsoni akiwa kwenye banda lake kubwa la Ng`ombe alipokea wageni , mmoja akiwa ni mwanamke rangi ya kiafrika mrembo alievalia suruali ya jeans na tisheti ya Puma , na mwingine alikuwa ni mwanaume pia akiwa ni rangi ya kiafrika alievalia jeans na tisheti nyeupe huku akiwa na koti la suti rangi ya ugoro . .

Mabwana hawa walijitambulisha mmoja akiitwa Linda na huyu mwanaume alijitambulisha kama Zakayo , ujio wa watu hawa ndani ya nyumba ya bwana Hudsoni ilikuwa ni kwa ajili ya kukodi Ghala lake moja la kuhifadhia mahindi kwa muda wa wiki moja , jambo ambalo lilimshangaza bwana Hudson kwa watu hao kuomba Ghala lake ambalo ni mwezi uliopita tu alitoka kulisafisha kwa ajili ya kuweka mahindi mapya na kutoa yale ya zamani .

“Mnahitaji ghala langu kwa madhumbuni yapi?”

“Hilo hatuwezi kuliweka wazi Mr Hudson ila tatalipa pesa nyingi sana Zaidi ya mara mbili ya bei utakayotutajia kukodi eneo hilo kwa wiki moja”

Mzee Hudsoni mwenye umri wa miaka 61 alijikuta akishawishika kwa utayari wa watu hawa kutaka kumlipa mara mbili ya pesa ambayo atawatajia , lakini licha ya kushawishika huko hakuwa tayari kutoa Ghala lake , kwani alikuwa na wasiwasi wa kile watu hao watakifanya pale tu atakapo toa hilo Ghala lake ,na maamuzi alioyafanya ni kutaja bei kubwa Zaidi kuliko s thamani ya Ghala lake na hapo watu wale yaani Zakayo na Linda walitabasamu na kuzidisha mara tatu ya hela aliotaja mzee huyu na kisha wakamwambia watampatiakiasi hicho , jambo ambalo liliibua mshangao na matamanio ya kiasi hicho cha pesa kwa mzee Hudson na moja kwa moja alikubali na kuwapeleka watu hawa kwenye Ghala kwa ajili ya kuangalia lakini pia na kuwaachia mlango .

Lakini licha ya hivyo mzee Hudsoni alitaka malipo yake hapo hapo na ilichukua dakika moja tu malipo yaliweza kufanyika na kuingia kwenye akaunti yake ya benki , kitendo ambacho mzee huyu alitoa macho , kwani hakuwahi kuzania kama anaweza kupata kiasi hiko cha pesa kwa muda mfupi na aliona kwa hela hizo zinamtosha kabisa katika uzee wake na hata asipolima tena .

Basi baada ya Linda na Zakayo kukabidhiwa ufunguo wa ghala hili ambalo lilikuwa na umeme , muda wa saa moja kamili iliingia gari nyingine na hii ilikuwa ikiendeshwa na Erick Peter.

“Kazi nzuri sana mmefanya , lakini ninawasiwasi na mzee Hudsoni asije kuta taarifa”.

“Halafu hilo tumeshau ila nitayaweka sawa na mzee huyu na kutokana na pesa tuliompatia nadhani hatafanya jambo kama hilo”Aliongea Zakayo huku wakisaidiana kutoa baadhi ya vitu kama vile tarakishi , mikoba na mazaga mengine na kuyaingiza kwenye hili Ghala , uzuri ni kwamba hili Ghala lilikuwa limejitenga kwa umbali wa mita kadhaa na nyumba aliokuwa akiishhi Mzee Hudsoni na hata kilichokuwa kinaendelea huku hakuwa ni mwenye kuona .

Ndani ya dakika kadhaa tu , ghala hili liligeuka kama ofisi ya kitehama , kwani kulikuwa na tarakishi moja kubwa na baadhi ya vifaa vingine ambavyo sikujua maana yake , lakini pia kulikuwa na meza na viti , lakini pia kulikuwa na kiti kimoja ambacho kilikuwa wazi , lakini kiti hiki pia kikiwa kimeunganishwa na umeme .

Ilikuwa ni muda wa saa nne kamili za jioni gari nyingine aina ya Range iliingia na kwenda kupaki mbele kabisa ya Ghala hilo . na ndani ya dakika kadhaa tu alionekana Janeth akiwa na mzee mmoja wa kizungu ambae alikuwa amezibwa zura yake huku akiwa na pingu kwenye mikono yake iliofungwa kwa nyuma .

Baada ya madakika sekunde kadhaa mzee alikuwa amekarishwa kwenye kile kiti ambacho kilikuwa wazi lakini kilikuwa kimefungwa na kwa kuunganishiwa umeme .

“Bruno lamberk hatimae upo kwenye mikono yangu”Aliongea mwanadada Janeth na kumvua mzee huyu lile kofia walilokuwa wamemvalisha na hapo mzee huyu aliangalia watu waliokuwa mbele yake kwa mshangao huku akichunguza mandhari ya eneo hilo.

“Janeth unachokitaka kukifanya hutofanikiwa , baba yako alijitahidi sana lakini naamini unajua kilichomkuta watu mnaocheza nao ni watu wa hatari sana na huenda wako njiani kuja eneo hili”Aliongea huyu mzee kwa ujasiri amao ulimpandisha hasira sana Janeth , lakini alijizuia na kutabasamu.

“Tutaona kama utakuwa na ujasiri wa kuongea baada ya kuona kinachoendelea ISLAND X” Aliongea janeth na kisha walifunga karatasi nyeupe mbele ya Bruno na kisha walielekeza Projecta kwenye lile karatasi , huku Linda akimpiga gundi ya mdomo mzee huyu .

Wakati huo hayo nayaendelea Erick Upande wa nje alikuwa akirusha Drones ambazo zilikuwa ni kwa ajili ya kuangalia usalama wa eneo hilo .

Baada tu ya kurudi alisogelea tarakishi ile kubwa na kisha alianza kubonyeza batani kwa spidi na ndani ya dakika chache ule upande kulikokuwa na projecta , projecta mbalimbali kulionekana Picha mbalimbali zikionyesha eneo kubwa la kisiwa.

Na ndani ya madakika kadhaa tu , tu picha ilibadilika na kuonesha eneo la nje la Jumba moja kubwa lililokuwa katikati ya Mikoko likiwa limejengwa kwa ustadi mkubwa sana huku mbele kabisa ya jengoo hilo kukiwa na maandishi makubwa yaliosomeka ISLAND X –U-97 ECLUSIVE HEADQURTER .

Ni kitendo kilichokuwa kikionesha kama Movie kwani ndani ya madakika kadhaa tu , picha zilionekana zikionesha ndani kabisa ya jumba hili , huku watu eneo hili likiwa na makachero waliokuwa wakilinda kuanzia juu ya paa , pembezoni mwa ukuta ,getini na ndani ya eneo hili .

Baada ya madakika kadhaa tu video ile ilionesha eneo la nje ya kisiwa hiki mita kadhaa kutoka kwenye hili jumba , eneo hili lilikuwa ni sehemu ya Ndege kutua yaani kulikuwa na kiwanja kikubwa cha ndege ambacho kwa haraka haraka kilionekana kutosha ndege kubwa ya abiria kutua kwenye hili eneo .

Zilipita dakika chache tu chopa moja ilifika ndani ya hili eneo huku ikiwa na wanajeshi ambao walishuka na Kamba na kuimarisha ulinzi wa hili eneo , hakika ilikuwa ni jambo la kushangaza na ilikuwa ni kama kwenye Muvi .

Yote haya wakati yanaendelea , Janeth ,Linda , Erick pamoja na Zakayo walikuwa wakifatilia kwa ukaribu kabisa , lakini hilo pia kwa upande wa Bruno pia alikuwa akiangalia kile kilichokuwa kinaendelea huku akionekana ni mwenye kuwa na wasiwasi mkubwa.

Baada ya dakika kadhaa za ulinzi kuimarishwa hatimae ndege moja kubwa ya saizi ya kati ilionekana kutua eneo hili na baada ya kama nusu saa hivi , walionekana wanaume na wanawake waliotoka katika hili ndege wakiwa na mavazi yaliokuwa kama yale ya Majaji wanayovaa , na baada ya watu hawa kutoka , walifuatia watu wanne waliovalia nguo nyeusi wakiwa wamebeba kitu kama jeneza , lakini hili halikuwa jeneza ,ni mfano wake tu lakini likiwa la kioo huku watu wale wakiwa wanabeba kwa umakini mkubwa sana .

Baada ya jeneza hilo kushushwa hatimae alionekana , kijana Ambrose alietoka akiwa amevalia Suti akiwa ndani ya hili eneo na wakati haya yote yanafanyika ilikuwa ni mchana kweupe na jambo hili lilidhihirisha kwamba eneo walilokuwepo hao watu ni bara linguine kutokana na utofauti wa muda..

Basi baada ya ya kijana Ambrose kutoka na kuelekea kwenye Gari hatimae alitoka mtu ambae alimfanya Janeth ageuze Macho na kumwangalia Bruno kwa hasira .

Huyu hakuwa mwingine bali alikuwa ni mwanaume ambae alikuwa anafanana kwa kila kitu na mwanaume aliekuwa amefungwa kwenye kiti alichokuwa amekalia Bruno , jambo hili lilimfanya mzee huyu afurukute kwenye kiti chake , jambo ambalo lilimfanya Janeth kutabasamu.

“huu ndio mwisho wa U-97 kuwa na nguvu duniani , tunakwenda kusambaratisha kila kitu mlichokiandaa karne na karne wewe pamoja na hao mashetani wenzako”Aliongea janeth akimwagnalia Bruno na kumfanya mwanaume huyu azidi kufurukuta kwani hakuwa na uwezo wa kuongea neno lolote kwani alikuwa amefungwa na gundi mdomoni.

“Operesheni Island X inaanza kuanzia sasa na nataka wote muwe makini , kwani hili ndio jambo ambalo tulikuwa tukilisubiria kwa muda mrefu na hakutakiwa kuwa na makossa ya aina yoyote ile” Aliongea kijana huyu kwa kujiamini huku akiendelea kuchezesha cidole vyake kwenye komputa .

Naam nini kilitokea mpaka kufikia hatua hii ???????.....

SURA YA 23​

BAADA YA MIEZI MIWILI YA DAMIANI KUINGIA NCHINI MAREKANI , LAKINI PIA KUANZIA SIKU AMBAYO PROFESA MIKE ALAN ANAPOKEA MAAGIZO YA KUMUANDAA AMBROSE

FRORIDA –MAREKANI

Ni siku kadhaa tokea Rania kurudi nchi Australia akitokea Tanzania , sehemu ambayo alienda kwa ajili ya kumtambulisha Erick kwa baba yake , zoezi ambalo halikufanikiwa kutokana na hali ya Peter kupoteza kumbukumbu na kutomkumbuka kabisa Rania .

Siku hii ya Jumatano saa tisa za alasiri ndani ya shule ya North Broward ndani kabisa ya eneo la mgahawa wa shule hii sehemu ambayo wazazi wa watoto mara nyingi hufikia ,wanapokuja kuwatembelea watoto wao walionekana wanaume wawili , mmoja akiwa ni kijana wa makamo alkekuwa amevaa nguo zilizompendezesha na mwingine alikuwa ni mwanaume wa miaka kati ya therathi na tano kwenda juu aliekuwa amevalia suti ya rangi ya zambarau , hawa hawakuwa wengine bali walikuwa ni Erick akiwa pamoja na Joseph...

“Mzee hakikisha akili yako inakuwa na utulivu kama unataka kumuokoa mwanao katika hatari ambayo ipo mbele yake”Aliongea kijana Erick akiwa katika hali ya kirafiki kabisa akimweleza mzee huyu ambae alionekana kuwa katika hali ya wasiwasi mno.

“Nimekuelewa”Aliongea Peter au Joseph akionekana ni mwenye kuvuta pumzi akijiweka sawa , kwani alionekana kutokuwa sawa kabisa.

Baada kama nusu saa hivi ya kukaa pale huku wakiwa wanapata kahawa mara alikuja mwanamama wa kizungu aliekuwa amevalia tisheti yenye nembo ya shule hio.

“Nipo hapa kwa ajili ya kuonana na mwanangu , anafahamika kwa jina la Ambrose Joseph”Aliongea mzee huyu mara baada ya mwanamama kujitambulisha kama Matron.,.

“Okey na huyu mwingine ni nani kwa Ambrose?”

“Huyu ni kaka yake” aliongea mzee huyu na kumfanya Erick kutabasabu .

“Okey ngoja nifanye mawasiliano na uongozi ili mpate utaratibu maalumu wa kuonana nae” Aliongea huyu mzungu kwa Lugha ya kingereza na kisha aliondoka na hazikupita dakika tano alirudi akiwa ameongozana na mwalimu mwingine , huyu hakuwa mwingine bali alikuwa ni mwalimu Nick Jonas , mwalimu aliekuw andani ya shule hio kwa ajili ya kazi maalumu , kazi ya kumfanya Ambrose kupenda mambo ya kale.

Baada ya mwalimu huyu kufika mbele ya meza hii ya mzee Peter alimwamuru yule mama kumuacha sasa aendeelee kuanzia hapo jambo ambalo kidogo lilimshangaza Peter kwani aliekuwa akitarajia kuonana nae hakua huyo kijana bali alikuwa ni mtoto wake Ambrose .

“Naitwa Nick Jonas ni mwalimu na mlezi wa Ambrose “

“Naitwa joseph ni baba wa mtoto Ambrose , nipo hapa kwa ajili ya kuonana na mwanangu”

“Nafurahi sana kuonana na wew Mr Joseph” Aliongea mwalimu Nick huku akiweka tabasamu ambalo kwa Erick aliona taasamu hilo ni la kinafiki huku akiwa amenyoosha mkono kumpatia Joseph.

“Nafurahi pia , lakini sipo hapa kwa ajili ya kuonana na wewe Mr Nick nipo kwa ajili ya kuonana na mwanangu”Jibu hili ni kama lilimfikirisha kidogo Mwalimu Nick na kisha akatabasamu.

“Ambrose hayupo hapa bali yupo katika safari ya kimasomo itakayo chukua muda wa miezi miwili , nipo hapa kw ajili ya kukufahamisha hilo lakini pia kukutoa wasiwasi kuwa mtoto wako yupo kwenye mikono salama”.

Mzee huyu alimwangalia Erick kwanza na kisha Erick alimwangalia Peter na kisha na kumpa ishara ya kukubali.

“Basi sawa mwalimu , nitafika hapa baada ya miezi miwili kwa ajili ya kuonana na Ambrose”..

Basi wawili hawa baada ya kupata jibu hilo kutoka kwa Mwalimu Nick walitoka na kuingia kwenye gari yao huku Joseph akionesha waswasi wa waziwazi .

“Mr Erick kipi kinafuata mpaka hapa naamini mtoto wangu hayupo salama kabisa”

“Punguza wasiwasi mzee , kila kitu kitakuwa katika mpangilio wake kama tu utafata kile ninachokuambia , mwanao yupo kwenye mikono hatarishi na hakuna serikali yoyote duniani itakayokusaidia Zaidi yangu , unachotakiwa ni kufata kile ninachokuambia”

“Kwa hayo nishakubali , ninachotaka ni kujua mpango wako kama unamafanikio yoyote ya kumpata mwanangu”.

Aliongea mzee huyu akiwa ni mwenye wasiwasi , lakini kwa Erick hakuonekana mwenye wasiwasi /tena alichukua simu yake na kisha aliangalia ujumbe ulioingia ambao juu kabisa ya kioo hiko cha simu kuna jina lililokuwa likisomeka STUPID BOSS.

“UNA MIEZI MIWILI TU KULIJUA SOMO LA SIRI”yalikuwa ni maandishi yaliokuwa yameandikwa kwa maneno ya kodi lakini yalioeleweka kwenye kichwa cha Erick , kwani alijua kuwa yalikuwa yakimaanisha kuwa alikuwa na ana miezi miwili tu iliobaki kukamilisha misheni ya kujua simulizi ya Book of all names

Baada ya Erick kusoma ujumbe huu aliweka simu yake mfukoni na kisha akamgeukia mzee Joseph .

“Sikia mpango uliopo hapa ni kuonana na Ambrose na kumshawishi juu ya hatari iliopo mbele yake, lakini ili niweze kumshawishi nitahitaji msaada wako katika hilo”

Aliongea kijana huyu pasipo wasiwasi huku akitoa simu yake na kupiga jina ambalo limesomeka kwene kioo chake kama Damiani.

“Nataka kwenda kuonana na Ambrose kwani kwasasa haifahamiki sehemu alipo na ili kufanikisha hilo nataka kwenda kama Profesa Mike nataka kutumia Advanced full body mask technology(A-FBM).

****


Hakuna kitu ambacho kilimpagawisha kijana Ambrose kama pale alipopata taarifa kutoka kwa mwalimu Nick kwamba anakwenda kuambiwa siri juu ya ufunguo ambao utamfanya kuwa na uwezo wa kufanya kila kitu ndani ya ya dunia , hakika hili lilikuwa ni jambo kubwa nyuma ya juhudi zake za kujituma katika kuijua historia ya kale , kwani aliaminni njia moja tu ya kutimiza malengo yake ni kuhakikisha anashikilia ufunguo uliokuwa unafungua kila mlango wa mafanikio ndani ya dunia hii , na ili kutimiza ile ndoto yake ya kuweka kumbukumbu ambayo itakuja kukumbukwa na vizazi na vizazi.

Ilikuwa ni siku ya Ijumaa siku ambayo kijana /ambrose alikuja kutolewa ndani ya shule hii ya North Broward na maafisa usalama wa UMOJA NAMBA TISINI NA SABA , Ambrose baada ya kuambiwa na mwalimu Nick kwamba watu hao watamfikisha kwa mtu ambae anasiri juu ya ufunguo unaoweza kushikilia kila kitu katika dunia hii hakuwa na wasiwasi Zaidi ya kufatishana na wanasalama hao.

Ni ndani ya dakika chache tu kijana huyu alikuwa ndani ya uwanja wa ndegea wa Frorida International Ariport , sehemu ambayo alipitishwa na wanausalama hawa pasipo hata kufata sheria za hapo uwanjani kwani alikuwa amepitishwa kupitia mlango wa VIP , yaani mlango ambao ulikuwa ukitumiwa na viongozi kupita kama vile maraisi .

Ilikuwa ni ndege moja kubwa ya wastani ya kampuni ya Boeng iliokuwa ndani ya eneo hili la uwanja wa ndege ambayo ilikuwa ni Dhahiri kabisa , kijana Ambrose ndio aliokuwa akitarajia kupanda kuelekea mahali ambapo alikuwa anamamini anakwenda kuonana na mtu ambaye atampatia siri ya namna ya kupata ufunguo utakao fungua kila mlango ndani ya dunia hii.

Naam baada ya madakika kadhaa ndege aliokuwa amepanda kijana Ambrose ilikuja kusimama ndani ya kisiwa kimoja kilichokuwa kinamaandishi yaliokuwa yanasomeka kwa jina la ISLAND Y WORLD TOP SECRET ARCHIVES

Hiki ni kisiwa ambacho hakikueleweka uelekeo wake , japo ni kisiwa ambacho kilikuwa ndani ya nchi ya Marekani , lakini jimbo halikufahamika , na hio yote ilikuwa ni kuhakikisha ulinzi wa eneo hili , kwani pia licha ya kwamba eneo hili halikuwa likifahamika lakini pia kulikuwa na ulinzi wa hali ya juu sana , kwani kulikuwa na makachero wengi waliokuwa wamevalia suti nyeusi wakiwa na siraha.

Baada ya kijana huyu kushuka na kuja kupokelewa na wanaume wawili , na wanawake wawili ambao walijitambulisha kwa kijana huyo kama wafanyakazi wa sehemu hio ambao ilitumiaka kama sehemu ya siri sana duniani kwa ajili ya kutunza kumbukumbu.

Kijana huyu alishangazwa na mandhari ya hili eneo , lilikuwa ni jumba kubwa la kifahari lililokuwa limeunganishwa na maktaba kubwa ambayo ilikuwa na mavitabu na nyaraka mbalimbali za mambo ya kale na sasa.

Kijana huyu alijikuta akistaajabu mno , kwani vitu vingi viliandikwa kwa lugha asiokuwa akiielewa , wakati kijana huyu akiendelea kushangaa mara alitokea mzee mmoja wa kizungu , huyu mzee alionekana kuwa umri umeenda sana , kwani hata tembea yake na ngozi yake vilithibitisha hili.

“Karibu sana Ambrose ndani ya sehemu hii muhimu sana ndani ya dunia hii ,Niite Mr Kolfan the Great Grandfather, mimi ndio muongozaji mkuu wa makataba hii” Aliongea mzee huyu kwa sauti yake iliokuwa imenyongea sana na Ambrose alikubali utambulisho huo.

“Nafurahi sana kukufahamu Mr Kolfan”

“ Karibu sana , lakini pia hongera kwa kuteuliwa katika kuifahamu siri kuu ya ulimwengu”sifa hizi zilimfanya kijana huyu mwili kumsisimka mno na aliamini kitu ambacho anakwenda kukijua muda mfupi ni kitu kikubwa sana katika maisha yake na ni mwanzo wa yeye kuanza kuwa na nguvu duniani.

“Asante sana “ waliongea huku wakiwa wanatembea , huku mzee huyu akiwa anamuonesha mambo mbalimbali yanayopatikana kwenye maktaba hio .

“Kila kitabu na nyaraka unaziziona hapa , ni taarifa za siri sana ambazo ni watu wachache sana wanazifahamu , na wewe katika maandalizi yako ya kuifahamu siri kuu ya ulimwengu huu inakubidi upitie baadhi ya nyaraka , lakini katika miezi yako ya maandalizi unatakiwa kujua sababu kuu ya kuundwa kwa UMOJA NAMBA TISINI NA SABA .

“UMOJA NAMBA TISINI NA SABA ??”

“Ndio unaonekana kushangaa juu ya jina hilo , lakini hilo ndio jina linalotambulisha jumuiya ya siri yanye nguvu duniani, nguvu yao ndani ya jumuia hii inashikiliwa na siri kuu ya ulimwengu , siri ambayo muda si mrefu unakwenda kuijua na kukufanya mtu mwenye nguvu sana ndani ya U-97 na duniani”

Kila neno lililokuwa linatoka kwa Mr Kolfani lilikuwa ni dhahabu kwenye masikio ya kijana huyu , na kwa jinsi alivyokuwa na hali ya udadisi katika maisha yake , aliamini ndani ya miezi hio miwili ya kuwa ndani ya Maktaba ya siri duniani atakuwa amejua mambo mengi sana..

Baada ya masaa mengi kupita hatimae Mr Kolfan alimkabidhi mzee huyu kitabu kimoja cha kale sana chenye maandishi makubwa juu yaliosomeka U-97 THE REAL HISTORY –DR ROSELF J .PECKER.

“Hiko ndio kitabu ambacho kitakufanya ujue namna U-97 ilivyoanzishwa”Aliongea babu huyu na kumfanya Ambrose kupandwa na shauku ya kujua kile kilichokuwa kimeandikwa katika hiko kitabu.

Nini kimeandikwa katika hiko kitabu … see next chapter. On next seaso
ITAENDELEA IJUMAA


LIPIA 1500 NIKUTUMIE HII SIMULIZI YOTE , LIPA NAMBA 0687151346 AIRTEL/0623367345HALOTEL/0657195492TIGO JINA ISSAI SINGANO UKILIPA TUMA MESEJI WATSAPP 0687151346
UNAWEZA PIA KUJIUNGA KWENYE GRUPU LANGU LA WATSAPP KWA SHILINGI 2000 NA KUPATA OFA YA SIMULIZI YA NILIMDHANIA KAHANA KUMBE BIKRA
 

SURA YA 07.

Jambo la kwanza lililonivutia mara baada ya macho yangu kugonga juu ya mwili huu wa huyu mwanadada ,ni rangi yake , alionekana kuwa ni mwanamke kutoka bara la Afrika bila shaka , alikuwa mrefu saizi ya kati , mwenye rangi nyeupe iliofifia lakini inayovutia , sura yake ilikuwa ni ya kuchongoka , akiwa na nywele ambazo kwa kule nyumbani tunaweza kuiziita za kishombe shombe ndefu zilizomfika mabegani , jambo kubwa lililonivutia zaidi juu ya huyu mwanamke ni Shepu yake, alikuwa na umbo namba nane ambalo lilikuwa ni ugonjwa kwa wanaume wakitanzania wengi bila kunitoa kundini .

Mwanadada huyu alikuwa ametangulizana na kijana wa makamo kati ya miaa 28 hivi, alikuwa ni mzungu na ni kama kuna jambo kijana huyu alikuwa akumuelewesha huyu mwanadada mara baada ya kuingia ndani ya mgahawa huu , muda wote huu nilikuwa nikiwachora tu , huku pepo langu la kimatamanio likiwa juu .

Sura yake kwanza huyu mwanadada ilikuwa ikija na kupotea jambo ambalo niliona ni uchuro , kwani nilikuwa na njia nyingi za kumtambua mtu kwa njia ya DREAMER T.

Kwa wale msiofahamu DREAMER T ni mtandao wa kijasusi unaoendeshwa na serikali ya China wenye taarifa ya kila mtu duniani , mtandao huu uligunduliwa na rafiki yangu Luang Shu ambaye ni mtoto wa Raisi wa China.

Moja ya sababu zilizonifanya kufahamiana na Luang Shu ni koneksheni ambayo ilijengwa na Marehemu Raisi Bendera , moja ya maraisi wangu bora waliowahi kuliongoza taifa la Tanzania , raisi John bendera alikuwa ni wale maraisi ambao walikuwa wakifikiria maslahi ya taifa kulivko wanavyojifikiria yeye mwenyewe.

Na kuthibithisha hilo yeye yupo peponi mimi nipo hapa nchini Australia nikiendelea kufanya kazi ambayo hakuimaliza , kazi ambayo haimfaiidishi yoyote , Zaidi ya faida zote kwenda kwa Taifa .

Basi nilitoa miwani yangu ya kijasusi iliokuwa na teknolojia ya hali ya juu sana , miwani ambayo inavaliwa na ajenti wa Mzalendo pekee , na hio ni kwamba alieitengeneza ni mzalendo mwenzetu .

Basi baada ya kutoa miwani hii nilitoa simu yangu yenye chata la M(yaani mzalendo) ilikuwa ni simu mahususi kwa ajili ya kazi yangu na pia ilikuwa ikitumiwa na sisi wazalendo pekee , Nilivaa miwani ile na kunifaya nipendeze Zaidi na kisha baada ya kuivaa nilugusa ‘Icon’ moja kwenye simu yangu na kisha kukatokea maandishi ‘M smart device connected with AI SUPER GLASS’.

Baada ya kuona sasa simu yangu imeunganishwa na miwani nilimuacha huyu mrembo aniangalie na kisha nikampiga picha , yaani miwani ilikuwa ni kama Camera , baada ya kupiga picha ile niliipandisha(Upload) kwenye DREAMER T na kuomba kumtambua mtu huyo , na ndani ya sekunde mbili tu nilikuwa na maelezo yote .

“Bingo!!” Alikuwa ni Rania Samir mmiliki wa hii hoteli ya kifahari , sasa hapa niliona njia pekee ya kuwapata The Truth ni kupitia huyu mwanamama , ndio nimebadilisha jina kutoka mwanadada kwenda mwanamama ,kwani ana mtoto ambae ndio huyu anaemiliki kikundi hiki cha The truth , lakini si mwanamama tu hawa tunawaita kwa kimombo ‘Milf’ yaani mwanamke aliezaa lakini hajapoteza mvuto.

Sasa picha ya mpango ambao niliona utarahisisha kazi yangu , ni kuzoeana na huyu mwanamke japo niliamini ni mwanamke matawi ya juu lakini pia akionekana kuwa mkubwa kwangu kwani alikuwa amenizidi kama miaka minne lakini sikuwazia juu ya hilo kwani ni jambo ambalo pia tuna mafunzo .

Niliwaza namna ya kuanzisha ukaribu na mwanamama huyu , na hapo hapo nilipata picha la kihindi ambalo lilinifanya nitabasamu , sikuwa na haraka juu ya mpango wangu huo , basi niliendelea kula chakula changu kwa mbwembwe zote huku nikiendelea kumchora mwanamama huyu ambae kwa haraka haraka niligundua alikuwa akikagua hilo eneo , alifika mpaka upande wangu na kisha baada ya kuniona nikiwa kwenye rangi yangu ya kitanzania alitabasamu na mimi nikamrudishia tabasamu na kisha aliondoka .

Baada ya kuona ameondoka haraka haraka nilifanya mawasiliano na Janeth nikimuomba aniunganishe na simu yangu nipate kujua mwanamama huyu kila eneo atakalokuwepo na ndani ya dakika chache tu kwa kutumia ‘Face recognition system’ nilikuwa namuona mwanamama huyu akiwa bado yupo ndani ya hii hoteli.

Baada ya kuona zoezi hilo limefanikiwa niliona sina haja ya kuwa ndani ya hilo eneo la mgahawani , nilinyanyuka baada ya kulipa kwa kadi yangu ya benki na kisha nilirejea kwenye chumba changu kupumzika , nilijitupa kitandani huku nikiendelea kuangalia simu yangu kuuona ni eneo gani Rania yupo, lakini niliona bado yupo ndani ya eneo hili la hoteli,sikuona haja ya kuendelea kumfuatilia niliamua zangu kupiga usingizi kwani wakati huo ilikuwa ni saa nne hivi na madakika.

Asubuhi kulivyokucha jambo la kwanza kuangalia ni simu , kuona huyu mwanamama yuko upande gani na niliona bado yupo ndani ya hoteli hii , jambo ambalo lilinipa jibu kwamba huenda kalala ndani ya hoteli hio .

Basi nilioga vizuri baada ya kumaliza nilivuta begi langu dogo la nguo na kisha nilizimwaga nguo zote kwenye kitanda , na baada ya hapo nilitoa kitu kama kichwa cha chajio ya simu na kuchomeka kwenye swichi(switch) ya umeme , na kisha nilitupa taulo pembeni na kubakia uchi , kisha niingiza miguu ndani ya begi lile na kusimama , na ndani ya sekunde chache tu nilikua nimebadilika na kuwa Stephano Lamberk, najua wengi hawanijui ukitaka kujua vyema kuhusu hili jina uwe umesoma kitabu cha waraka wa raisi kabla ya kifo.

Nilikuwa ndani ya FBM nikiwa nimebadilika kabisa kimuonekano, na kuwa mzungu kamili yaani huwezi kujua kwamba nimevaa mask .

Stephano Lamberk ni jina nililopata ndani ya Taifa la uchina , na ndio jina ambalo nilikuwa nikitambulika nalo kama moja ya wanabodi wa kurugenzi ya kampuni ya Huwaei , kama utagoogle jina langu utaweza kunisoma nikiwa moja ya matajri wakubwa ndani ya Afrika wenye umri mdogo .

Jamani hayo sio maigizo ni kweli kabisa nina pesa ndefu ,unaweza ukanijua kama Damiani lakini pia nafahamika kama Stephano Lamberk kijana mwenye pesa kutokea Taifa la Tanzania , na mara nyingi huwa nikihudhuria mikutano yote inayohusu biashara zangu huwa natumia jina na sura ya Stephano Lamberk .

Basi baada ya kuwa kwenye muonekano mwingine , nilivaa suti yangu nadhifu kabisa ambayo ilinikaa vyema , na muonekano wangu wa kihandsome , ni Dhahiri mwanamke yoyote ambae anapenda wanaume wenye mvuto atavutiwa na mimi , usishangae kuna wanawake hawanaga

‘standard`s’ yaani hawajali mwanaume anaetoka nae ilimradi awe na pesa , hawa hawajali mvuto , sasa mimi pesa ninayo , halafu mvuto ni nao yaani ni swala la plus plus kumvutia mwanamke .

Niliangalia simu na kuona bado Milf wangu yupo ndani ya hoteli , hivyo nilitoka , huku nikiwa na nia kwanza ya kwenda kupata kifungua kinywa , swala la pili niliwaza namna ya kukutana na mrembo Rania.

Nilipata kifungua kinywa ndani ya sehemu ile ile ya jana , pasipo kumuona Rania ,lakini sikuwaza sana kwani alionekana kwenye simu , basi baada ya kumaliza nilifika mapokezi na kuulizia kuhusu kwenda eneo la peace lounge .

Ndani ya hii hoteli kulikuwa na hii huduma kwa mtu ambae anataka kutuliza mawazo , yaani kama unamistress yako huko ya maisha au mapenzi basi ukienda hili eneo akili yako inatulia tuli na kufurahia maisha , hii huduma pia inapatikana ndani ya kisiwa cha Ilbiza huko Spain.

Nyie hii sehemu kweli ilikuwa ni kwa ajili ya kutuliza mawazo , bwana bwana , ilikuwa na muonekano flani hivi wa kipekee sana yaani kuna muda ndani ya hili eneo linabadilika linakuwa kama mbuga ya wanyama , lakini pia kuna muda hili eneo linabadilika linakuwa kama upo chini ya bahari , yaani kila aina ya kitu cha kushanganza na kuchangamsha ubongo kilikuwepo , ilikuwa ni kama upo ndani ya Chupa kubwa sana ukiwa umezungukwa na vioo.

Ni sehemu ambayo haikuwa na watu wengi , nadhani ni kutokana na muda ambao niliingia ndnai ya eneo hilo , kulikuwa na baadhi ya watu kulia kwangu wasiozidi kumi , lakini pia kushoto kwangu sehemu ambayo ilikuwa na swimming pool kulikuwa na watru wasiozidi watano , lakini mbele kabisa kwenye bustani kulikuwa na mtu, sio watu, sikuweza kumuona kwa upande ambao nilikuwa nimesimama ila niliambulia kuona kofia kubwa ya mviringo rangi nyeupe(Floppy hat) ikiwa inaonekana kwa nyuma ya kiti cha kuegamia , yaani mtu huyo alikuwa amenipa kichogo , basi niliona nichague mahali pa kwenda , na nikaona ni vyema nikienda mbele yangu kwani ni eneo ambalo halikuwa na watu wengi na mimi pia nilikuwa nikipenda maua .

Baada ya kusogea karibu kabisa yaani kushoto mwa mtu ambaye alikuwa ndani ya hili eneo , upande wa kushoto , moyo ulijikuta ukipiga paah! , kwani mtu ambae nilikuwa nikitamani kuonana nae, kumuona ndio aliekuwa eneo hilo, nilijikuta nikisimama nikimwangalia mwanamke huyu kwa uzuri aliokuwa nao , lakini pia pozi ambalo alikuwa ameweka ndani ya eneo hilo , niliendelea kumsaminisha pasipo yeye mwenyewe kutambua uwepo wangu , huku akiwa ameshikilia glass ya wine .

Baada ya kuona nimeridhika na sinema hio ya bure nilisogea upande wa kushoto wake kwenye kiti cha pembeni na kukaa.

“Mambo mrembo !!”Nilisalimia kwa lugha ya Kiswahili kabisa , na nilifanya hivyo makusudi kwani nilijua mwanamama huyu alishawahi kukaa Tanzania hivyo ni lazima atakuwa anaelewa lugha ya Kiswahili vyema , lakini pia hio ndio gia yangu niliopanga kuingia nayo kwa mwanamama huyu ili kujenga ukaribu .

Basi baada ya kumpa salamu hio aligeuza shingo akiwa kama ni mtu ambae alikuwa kwenye mshangao , na mimi niliupokea mshangao huo kwa Tabasamu.

“Haaa!!!.. Stephano”Kibao jamani kilinigeukia , kwani licha ya kujua kuwa mimi ni tajiri ila sikujua kwamba naaweza kufahamika na mrembo huyu , hivyo namimi ikawa zamu yangu kushangaa , lakini sikutaka kulionyesha hilo kwani nitakuwa nimeonesha udhaifu , nilitabasamu.

“Wow! , sijatarajia kuona mwanamke kama wewe unalifahamu jina langu hususani ukiwa ndani ya nchi ya mbali kama hii”.

“I know you, na nahisi pia unanifahamu kwani kitendo cha kunisalimia kwa Kiswahili pia kimenipa maswali”.

“Naweza kusema ndio au hapana kwa wakati mmoja”

“Kwanini hapana na ndio hakuna jibu hapo”Huku akitabasamu .

“Kwa sababu nina siku moja , saa na dakika chache tokea ni kukufahamu”.Alishangaa huku akionekana kuchangamka tofauti na nilivyomkuta na huo niliona ni ushindi namba moja . “So can you tell me , umenifahamu je within that short time and how ?”Hili swali mara nyingi mtu yoyote akikuuliza , yaani pale unapoita jina lake halafu akashangaa , na akakuuliza hili swali basi jua ana ‘trust issues’ shida ya kutokuamini watu , na kama ni mwanamke jua huenda alishawahi kusalitiwa na mtu anaempenda sana na sisi majasusi mara nyingi tunaangalia na ‘Complexion’ muonekano unaombatana na hili swali .

“ Mazingira na luxuries ndani ya hii hoteli ndio ilinifanya nikufahamu , I am businessman na nimeipenda sana hii hoteli” Mpaka hapo nilikuwa nimejibu maswali yote kwa mpigo, kwa wewe ambae hujawahi kuwa mfanya biashara huwezi kuelewa , na hapa nazungumzia wafanya biashara wale wakubwa,huwa kuna lugha ambazo wafanya biashara wakubwa wanatumia pindi wanapokuwa katika mazunguzo ya kuingia mkataba au dili Fulani, mara nyingi wanakuwa na maneno ya kimikato lakini yaliobeba Zaidi ya maana.

“Karibu sana kwenye hoteli yangu Stephano , I am so happy to meet you in person”.

“Na mimi pia nimefurahi kukutana na wewe mwanamke mzuri unaemiliki hoteli nzuri, lakini nina shauku ya kujua zadi how umenifahamu”.Alipoteza tabasamu jambo ambalo lilinichanganya kidogo .

“Ni hadithi ndefu , but its all about Erick my son”Sasa sehemu ambayo niliitala ndio hapo , niliona sasa kazi yangu inaenda kuwa rahisi , na nilipanga kutumia mbinu zote za kijasusi kumchimba huyu mwanamke , yaani nikitoka katika mazungumzo hayo niwe nimepata mwanga wa misheni yangu.

“Kumbe una mtoto! , vipi kuhusu Erick?”.

“Yess one and only , but I am so sad when I think about him” ndio ninae mtoto mmoja wa kipekee , lakini najikuta nikiwa kwenye huzuni pindi ninapomuwaza”Aliongea na mpaka hapo nilijua kuna jambo kubwa kumuhusu Erick, nilijikuta nikinyamaza kwani mwanamama huyu alionekana akianza kutokwa na machozi , jambo ambalo ndio mtihani mkubwa kwangu , yaani katika maisha yangu nilikuwa ninauwezo wa kumfanya mtu afurahi lakini siwezi kumfariji mtu sasa nashindwa kuelewa maneno yangu yana mantiki lakini ndio hivyo, ndio maana mara nyingi napenda kuongea na watu wenye furaha..

“Niambie Zaidi kuhusu Erick”Niliongea na wakati huu nilikuwa nishanyanyuka nilipokuwa nimeketi na kukaa kwa kupiga magoti pembeni ya kiti chake karibu na tumbo lake ,japo mwanamama huyu kuwa katika hali ya huzuni lakini , alikuwa akinivutia mno , yaani kivazi cha kizungu alichovaa kilifanya nitamani tendo.

“Amepotea, ni mwaka mmoja sasa”Nilijikuta nikishangaa, kwani mpaka hapo niliona kabisa kazi yangu inaanza kuwa ngumu wa kupata hiki kikundi cha The Truth.

“Pole sana, but kwanini kupotea kwa mwanao kuwe ni stori ndefu ya kunifahamu?”.

“Kama unao muda nataka nikuoneshe kitu , nadhani itakuwa rahisi kwa mimi kukuhadithia”Aliongea na nilikubaliana nae.

Basi mwanamke huyu alitangulia mbele akiniacha nyuma nikijilia kwa macho , dakika tatu mbele haatukuwa upande wa hoteli hii , tulikuwa eneo hilo hilo lakini j engo tofauti la pembeni lenye goorofa tatu kwenda juu .

“Hapa ni nyumbani kwangu Stephano , karibu sana”Aliongea na hapa ndipo nilipata kufahamu kwanini wakati nikiwa namwangalia kwenye ramani alikuwa akionekana ndani ya hoteli hii , kumbe alikuwa akiishi hapo.

“Asante sana Rania”Niliongea kisha akaniangalia na kutabasamu.

Haikuwa nyumba lilikuwa ni jumba la kifahari , ni jumba ambalo lilikuwa likivutia mn ,kwanzia muundo wake , mpaka thamani na naksi zilizowekwa ndani ya hii nyumba.licha ya uzuri wa nyumba hii , hamu yangu ya kuoneshwa hiko kitu haikukauka na ilikuwa ikiongezekwa kwa kila dakika , wakati tukiwa tunapanda ngazi za kuelekea gorofa ya juu ya nyumba hii .

Tulikuja kusimama katika chumba ndani ya gorofa ya pili , na Rania alifungua mlango huo kwa kuweka kidole sehemu maalumu ya kutumia ‘fingerprint’ na ndipo tulipozama katika chumba hiki.

Kilikuwa ni chumba kikubwa mno kwa masikini lakini cha kawaida kwa watu matajiri kama mwanamke huyu , upande wa kulia wa chumba hiki ulikuwa na picha ya mchoro wa Kasuku ukiwa umetundikwa , na hapa ndipo nilipokumbuka ‘logo’ ya The truth waliokuwa wkiitumia , muda huu wote wakati tunaingia kwenye hii nyumba nilikuwa nimevalia miwani yangu , kama zile wanazotumia wagonjwa wa macho , lakini hii ikiwa na kazi maalumu kurekodi kila kona ya jumba hii na picha kuzituma katika kitengo chetu cha Mzalendo kwa tafsiri Zaidi .

Tuliweza kuingia kwenye chumba kikubwa kingine yaani ndani kwa ndani , na nilichogundua ni kwamba chumba hiki kina milango miwili , yaani kuna mlango ambao unaweza kutumia kwa kuingilia ukiwa kwenye korido na pia ukiwa ndani ya chumba hiki pia unaweza kutumia mlango wa ndani kuingilia kwenye chumba kingine , ndani ya chumba hiki kulikuwa ni kama ofisi ya Profesa flani hivi kwani kulikuwa na majivitabu mengi sana , tena yale makubwa yaliopangwa kwa mpangilio mzuri kama maktaba.

Nilikuwa nikipitisha macho yangu kwa kila kona ya chumba hiki ili nisije kosa’details’ ya aina yoyote ile , nilijikuta nikisogelea baadhi ya vitabu vile na kuviangalia , nilichogundua ni kwamba karibia vitabu vyote vilikuwa ni vya kihistoria , kuna vilivyokuwa vimeandikwa kwa lugha ya kilatin , lakini pia kuna vilivyoandikwa kwa lugha ya kigiriki na kingereza pia

“Ndio hii picha Stephano” Aliongea Rania na mimi nilijikuta nikigeuka na kuangalia hio picha na hapo ndipo nilipopigwa na mshangao , kwani picha ile ilikuwa ni ya kwangu tena zikiwa mbili ya kwanza ikiwa ni ya sura yangu halisi yaani Damiani ,ya pili ikiwa ni yakwangu halisi, jambo hili nilijikuta likinishangaza sana kwani sikuwa nimetegemea kwamba picha zangu zote mbili ile feki na ile halisi kuwa mahali hapo.

Nilijikuta nikishangaa huku nikisahau kwamba nipo kwenye chumba cha mmiliki wa kikundi cha The Truth, kikundi ambacho kilikuwa maarufu sana katika mtandao wa Deepweb , kwa kuuza taarifa mbalimbali, na kwa maana hio kuonekana kwa picha hizo hapo ilimaanisha moja kwamoja hawa The Truth walikuwa wakinifahamu nje ndani.

Niliangalia picha hii ya Stephano Lamberk kwa muda huku mwanamama huyu akiniangalia na kisha niligeukia picha yangu halisi inayonitambulisha kama Damiani.

“Kuna picha mbili hapa ya kwanagu na hii nyingine , hadithi hio inakaa vipi?”Niliongea hivyo makusudi nilikuwa nikijaribu kupima uelewa wa mwanamke huyu juu ya mimi kuwa na sura mbili, Alitabasamu…

“I know you are Damiani and even yesterday night I recognised you”Nakujua Damiani hata jana usiku nilikufahamu.





SURA YA 08

Ni siku kumi baada ya kikao kilichowakutanisha Profesa Mike Alan , na wenzake wanne wakizungumzia juu ya mafanikio ya Mpango Zero, lakini pia wakiwa wamezungumzia mpango wa kumfanya mtoto Ambrose kupenda historia ya mambo ya kale .

Mwanzo wa wiki yaani siku ya Jumatatu ,ndani ya shule ya North Broward alionekana mwanaume mmoja wa kizungu akiwa anaingia katika darasa ambalo anasomea kijana Ambrose yaani Class A.

Baada ya mwanaume huyu kuingia ndani ya darasa hili alianza kujitambulisha kwa jina la Nick Jonas mwalimu wa maswala ya saikolojia , baada ya mwalimu huyu kujitambulisha aliendelea kufundisha wanafunzi hawa ambao walionekana wachache lakini wenye kusikiliza kwa makini kile ambacho mwalimu Nick anafundisha.

Mwalimu Nick Jonasi alikuwa ni mrefu wa wastani , mwenye nywele nyeusi zilizojaza kichwwa chake na kumfanya kupendeza , alikuwa na umri kimakadirio sio chini ya miaka therathini na tano.

Staili yake ya ufundishaji iliojaa ucheshi iliwafanya wanafunzi hawa wa Class A kuvutiwa sana na mwalimu huyo akiwemo Mtoto Ambrose ,Alikuwa akifundisha mambo ya saikolojia kwa mfumo wa hadithi za zama za kale.

Baada ya nusu saaa ya mwalimu huyu kufundisha alijipatia wasaa wa kufahamiana na wanafunzi hao kwa kila mmoja na ndoto zake za baadae , alijikuta akishangazwa na mengi juu ya yale mambo ambayo watoto hao walitaka kuyakamilisha katika maisha yao ya kimasomo, licha ya kufurahishwa na mambo ambayo wanafunzi hao walikuwa wakimweleza , jambo moja tu ndio lilimshangaza lakini pia na kumfurahisha kwa wakati mmoja ni juu ya mtoto Ambrose , kwani baada ya kuulizwa ni kipi angependa kukifanikisha katika maisha yake ya baadae alijibu hakuwa na chaguo la aina yoyote kwani mpaka wakati huo alikuwa akipenda kila kitu huku akiwa hana sababu ya kuchukua kimoja na kuacha vingine .

Kwa namna ambavyo Ambrose alijibu swali hilo ,Sir Nick alikiri kweli Ambrose alikuwa na akili nyingi , lakini licha ya kukiri hivyo aliona misheni yake ambayo alikuwa amepewa na Umoja Namba Tisini Na Saba anakwenda kuifanikisha kiurahisi sana.

“This mission is going to be interesting and smooth , directing him to stick with Ancienty history is goimg to be easy as of his multiple interest”

“Kumfanya apende mambo ya zama za kale ni jambo rahisi mno kwani mpaka sasa hanakitu ambacho anamalengo nacho au alikuwa anapenda kufanya”

Hio ndio namna ambavyo mwalimu Nick akiwasiliana na mtu ambae hakujulikana kwenye simu akimpa hayo maelekezo , baada ya mwalimu huyu kumaliza kuongea na mtu huyo alitabasamu kwa muda na kisha alichukua mvinyo wake na kunywa na kuketi katika sofa ndani ya nyumba yake hio aliopewa ndani ya shule hio ya North Broward.

“Lakini kwanini ni mfundishe kupenda mambo ya kale ?”Ni moja ya swali ambalo bwana huyu alijiuliza , kwani kazi ambayo alikuwa amepewa na wakuu wake kwa mtoto Ambrose ni kumfundisha kupenda hostoria ya zama za kale ,lakini hakupewa sababu ya kufanya hivyo kwa mtoto huyo ilikuwa ni nini.

Siku iliofuata Sir Nick kama kawaida alikuwa na kipindi na Class A , siku hio aliwahi sana kufundisha na kumaliza na mara baada ya kipindi hicho alimuita Ambrose ofisini kwake kwani alikuwa na mazungumzo nae .

“Ambrose umekuwa mwanafunzi wa kipekee sana niliowahi kufundisha katika swala zima la saikolojia”.

“Kwanini unasema hivyo mwalimu , ni kipi cha kipekee ambacho umepata kuona kutoka kwangu”

“Wenzako wote wana ndoto za kukamilisha katika maisha yao , lakini wewe pekee ndio umesema unapenda kila kitu , kwangu jibu lako ndio la kwanza kupata kutoka kwa mwanafunzi wa umri wako hivyo naweza kusema ni la kipekee sana”.

“ Asante sana mwalimu , lakini kwangu ni swala la kawaida , kwani mpaka sasa sina sababu ya kupenda hiki na kuchukia kile , najiona naweza fanya kila kitu”

“Dunia inavitu vingi ambavyo vinaatakiwa kuendelezwa kila siku na kwa wewe mtu mmoja huwezi kumaliza kufanya kila kitu ,Je utajisikiaje kama kuna kitu kimoja ambacho unaweza fanya na kukupatia majibu ya vitu vyote”.

“Sijakuelewa mwalimu”.

“Utajisikiaje pale utakapo pata ufunguo wa siri ya kila kitu ndani ya dunia hii”

“Nitakuwa na furaha sana mwalimu , kwani nitakuwa nina uwezo wa kufanya kila kitu kwani napenda vyote”

“Ipo siri kubwa ndani ya hii dunia ambayo itakuwezesha kufanya kila kitu kwa ufanisi mkubwa na endapo utaweza kufanya hivyo ni Dhahiri utakuwa mtu mkubwa wa kuogopwa ndani ya dunia hii , na unaweza ukawa mfalme wa Dunia”.

“Ni kweli hayo mwalimu”Awamu hii Ambrose aliulza kwa kwa hali ya shauku kubwa , na jambo hili lilimfanya mwalimu huyu , kufurahi kwania aliona kazi yake ya kumfanya Ambrose kupenda mambo ya kale inakwenda vizuri .

Moja ya falsafa ya mwalimu Nick katika shule zote alizowahi kufanya kazi na kutatua matatizo mbalimbali ya maswala ya kisaikolojia , alikuwa akiamini kwamba kuna sababu moja kubwa ambayo inamfanya mtu kupenda kitu sana kuliko vitu vingine , na sababu hio inajengwa na tamanio lenye nguvu(Motivated desire),huku akiamini kwamba tamanio lenye nguvu mara nyingi huchipua kutokana na shauku ya mtu juu ya kitu Fulani(Curiosity).

Hivyo kitendo cha kumwambia Ambrose kwamba kuna ufunguo wa kumfanya kufanya kila kitu katika uso wa dunia na kuwa mtu mkubwa duniani , ilikuwa ni kujenga shauku yake ili hatimae kuweza kumjengea tamanio lenye nguvu.

Alikuwa ashamsoma tabia ya Ambrose tayari na kugundua ni mtu ambae anapenda vitu vikubwa , na kitendo cha kumjibu kwamba alikuwa akitaka kufanya kila jambo katika uso wa dunia , swala hilo lilimfanya amtamue Ambrose kama kijana mwenye ‘ambition’ kubwa . na hilo aliona ni jambo ambalo litamuwezesha Zaidi katika kumfanya kijana huyo kupenda historia ya mambo ya kale.

“Naongea ukweli Ambrose ,, hii ni siri ambayo nakwambia sasa , na hupaswi kumwambia mtu yoyote yule nikikueleza siri hii ,nimekuchagua wewe kwani unaonekana kuwa na akili nyingi kuzidi wenzako wote”

“Ni siri gani hio mwalimu , nahitaji kujua”.

“Sio rahisi hivyo Ambrose kukuambia siri hii kubwa , kwani ili kuielewa lazima kwanza upende kusoma mambo ya historia ya kale , ukielewa kwa ufasaha mambo ya historia ya kale ndio utakuwa umekidhi vigezo vya kujua siri hii , na nitakupeleka sehemu ambayo utakutana na mtu ambae anafahamu siri hio”.

“Nina weza kufanya hivyo mwalimu , lakini mpaka nipate uthibitisho wa jambo unalolisemea kama lina ukweli ndani yake”Aliongea Ambrose huku akionekana kumaanisha kile ambacho anaongea , na jambo hilo kwa mwalimu Nick lilimfurahisha , kwani kwanza hakutegemea kwa mtoto kama huyo ambae akili yake ilikuwa kubwa kuwashawishika bila ya kuwa na ushahidi .

Basi baada ya mwalimu Nick na Ambrose kufanya mazungumzo hayo , kazi ilibaki kwa Nick , swala la Ambrose kutaka ushahidi wa kile alichokuwa anakizungumzia lilikuwa ni kazi kwani mpaka wakati huo hakujua ni kwa namna gani anaweza kupata ushahidi ambao unaweza kumfanya Ambrose kuukubali.

Baada ya kutoka kazini alihitaji kuoanana na boss wake aliempa kazi hio , alimtafuta kwa simu na kuweka miadi ya kuonana muda wa jioni ndani ya mgahawa wa Rosela katikati ya jiji la Frolida .

Muda wa saa moja za jioni kwa saa za Kimarekani , Nick Jonasi alionekana akiwa ndani ya mgahawa huu tulivu kabisa wenye mandhari ya kuvutia , na nadhani hii ndio sababu ya watu hawa kukubaliana kukutana mwamahali hapo , kwani ndani ya hili eneo kulikuwa na utulivu wa ahali ya juu sana , japo kulikuwa na watu wa mbalimbali waliiokuwa wakipata kahawa , lakini hakukuwa na makelele.

Bwana Nick ambae tunamjua ni mwalimu wa saikolojia katika shule anayosomba Ambrose alikuwa ameketi ndani ya mgahawa huu wa kisasa upande wa kulia mbele kidogo na kaunta ya vinywaji , alionekana kupata kahawa huku akimsubiria mtu ambae alikuwa na miadi naye ya kukutana ndani ya muda hio , aliangalia saa na kuona alikuwa amewahi kuliko isivyokawaida .

Lakini mara baada ya kufika muda saa kumbi na mbili na dakika hamsini na tisa , alionekana mwanaume mfupi wa wastani alievaliaa jacketi refu jeusi ambalo limemziba miguu , bwana huyu alikuwa ni wale watu ambao washavuka daraja la ujana miaka mingi , kwani kichwa chake cha uwararaza kilichojaa mvi kilikuwa kikiongea kila kitu .

Baada ya bwana huyu kuingia moja kwa moja alinyoosha mpaka sehemu ambayo alkuwa amekaa Nick , na mara baada ya kufika aliweka begi lake aina ya Briefcase nyeusi pembeni karibu kabisa na miguu ya Nick na kisha aliketi huku wakisalimiana.

Mzee yule na yeye aliagiza kahawa yake ya kuzugia na baada ya hapo waliingia kwenye mazungumzo na hapo ndipo Nick alipomueleza bwana huyu juu ya mazungumzo yake na mtoto Ambrose , baada ya mzee huyu kuelewa hitajio la mwalimu Nick alivuta mkoba wake aliokuja nao na kuufungua na kutoa kitabu na kumpatia mwalimu Nick.

Juu kabisa ya kitabu hiki kulikuwa na nembo kubwa ya pete yenye mchoro usioeleweka ,mwalimu Nick alikiangalia kitabu hicho na kugundua kuwa kilikuwa kimeandikwa kwa lughaambayo hakuwa na uelewa nayo .

“Huo ndio uthibitisho ambao utamfanya Ambrose kukubaliana na wewe”..

“Huu unawezaje kuwa uthibitisho , naona ni kitabu ambacho kipo kwa lugha ambayo sijawahi pata kuiona”

“Mpe kijana kazi ya kutafuta maana ya hio lugha na njia pekee ambayo anaweza kupata kufahamu hio lugha ni kwa njia ya kusoma mambo ya historia ya kale , akiweza hilo misheni yako itakuwa imekwisha”Aliongea mzee huyu na kisha alinyanyuka akimuacha mwalimu Nick akiwa kwenye maswali , alikiangalia kitabu hicho na kujikuta akishangaa kile kilichoandikwa katika hiko kitabu , hakuelewa lugha iliokuwa imetumika ndani ya hiko kitabu ilikuwa ni ;iugha gani .Siku iliofuata mwalimu Nick aliingia darasani kama kawaida kwa ajili ya kipindi na wanafunzi wa Class A.

Baada ya kipindi alimwita tena Ambrose kwa ajili ya kuendeleza mazungumzo yao walioishia siku ya jana , hakutaka sana kuongea mengi , alichofanya ni kutoka kile kitabu na kumkabidhi Ambrose.

“HIko ni kitabu ambacho lugha yake mpaka sasa haifahamiki ni lugha gani , wanahistoria wa mambo ya kale wametafua namna mbalimbali ya kujua lugha hio lakini mpaka sasa hakuna ambae alipata kujua kupambanua lugha hio”.

Swala lile lilimshangaza mno kijana Ambrose , hakuamini kwamba lufha ilioandikwa katika kitabu hicho ilikuwa haifahamiki kama mwalimu wake anavyosema .

SURA YA 09.

MIAKA KUMI NA MBILI NYUMA.(kutoka kitabu cha 2HOURS OF MEMORIES kilichoandikwa na mtunzi ISSAI SINGANO)Rania anasimulia…..

Ni miaka kumi na mbili nyuma nilipoingia kwa mara ya kwanza ndani jiji la Sydney kutokea Tanzania , nchi yangu ambayo niliona ni chungu sana kwa mimi kuishi kutokana na mambo makubwa yalionitokea ya kuumiza .

Jambo lililonileta ndani ya taifa hili La Australia mbali na Nchi yangu ni kwa ajili ya kuishi , lakini pia kupata wasaa mzuri wa kupona kwa yale ambayo niliweza kuyapitia wakati nilipokuwa nchini Tanzania .

Niliingia katika nchi hii nikiwa na mwanangu Erick aliekuwa na umri wa miaka miwili tu, kwa wakati huo mwanangu Erick ndie aliekuwa faraja yangu kwa kipindi chote nilichoweza kufika ndani nya taifa hili , kwani tokea nifike sikuwa na kazi maalumu ambayo nilitaka kuanza kufanya , kwani akili yangu kwa wakati huo haikuwa sawa nilikuwa kwenye majuto makuu kwa yale ambayo yalisababishwa na familia yangu .

Ilinichukua muda wa miezi minne kwa akili yangu kukaa sawa , unaweza ukajiuliza kwa muda wote huo nilikuwa nikiishi vipi , jibu ni kwamba nilikuwa nikiishi hotelini kwa wakati wote huo kwani nilikuwa na pesa ya kutosha kuishi ndani ya jiji hili linalosifika kwa kuwa ghali Zaidi duniani.

Basi baada ya miezi minne ya kuwa ndani ya Sydney niliweza kukutana na Rasi ndani ya hoteli ya Four Season hoteli ambayo nilikuwa nikiishi kwa muda wote wa miezi hio minne , Ras ni moja wanaume wacheshi sana ambao nimewahi kukutana nao , lakini pia naweza kusema ni rafiki yangu wa kwanza kuwa nae ukiachana na Peter ambae ndie baba mzazi wa Erick ambaye na yeye pia ndie aliechangia mimi kuja ndani ya taifa hili.

Ras alikuwa ni Floor manager ndani ya hoteli hii , na floor ambayo alikuwa akisimamia ndio hio ambayo nilikuwa nimechukua chumba , na naweza kusema hilo lilichangia sana kwa mimi kufahamiana na Rasi kwani nilikuwa mteja wa pekee ambae nilikuwa nimeishi kwa miezi mingi ndani ya hoteli hio .

Mwanzo wa kufahamiana na Ras ndio mwanzo wa akili yangu kuamka kibiashara Zaidi , na hili ni kama Rasi aliliona kwangu kwamba nilikuwa nikiwaza kufanya biashara , kwani mara nyingi kila nilipoweza kukutana nae alikuwa akuzungumzia maswala ya biashara na hii yote ni pale nilipomueleza nia yangu ya kutaka kuwekeza ndani ya taifa hili.

Nakumbuka siku ambayo nilimueleza nia yangu ya kuwekeza swali moja kuitoka kwake lilikuwa ni kama ninao mtaji kiasi gani , na nilipomtajia kwamba nilikuwa na mtajji wa kiasi cha Dollar Milioni Hamsini , ndipo alipoweza kushangaa sana lakini pia kufurahishwa kwa wakati mmoja na nadhani kilichomfurahisha kwa wakati huo ni kwamba aliona fursa kupitia mimi .

Siku moja Rasi aliomba kukutana na mimi kwa ajili ya mazungumzo , na mimi nilimkubalia na tuliweza kukutana ndani ya hoteli hii kwenye mgahawa , siku hii alikuja sio kama mfanyakazi kwani alikuwa amevalia kiraia kabisa, jambo ambalo alinieleza siku hio ni juu ya hoteli ya Avani Park ilioukuwa imefilisika na ilikuwa sokoni kwa kuuzwa .

Siku hii ndipo nilipokuja kugundua kuwa Ras alikuwa ni kichwa likija swala la biashara , kwani alinipa maelezo yalioshiba ya sababu ya mimi kununua hoteli hii ambayo ilikuwa ikiuzwa kwa bei rahisi sana nusu ya pesa ambayo nilikuwa nayo .

Baada ya kurishidhishwa na maelezo ya Rasi hatimae alipanga kikao cha kunikutanisha na mmiliki wa hoteli hio kwa ajili ya mazungumzo ya bei , mmiliki alikuwa ni mmama Profesa kutoka chuo kikuu cha Monash Alikuwa akifahamika kwa jina la Victoria Lambert mwenyeji wa jiji la Mellbourne , maongezi yangu na mwanamama Victoria yalienda vyema sana kiasi cha kwamba tulijenga ukaribu kwa masaa kadhaa tu ya mazungumzo yetu.

Basi niliweza kununua hoteli hio kwa asilimia themanini huku mwanamama huyu akibakisha asilimia 20 kwahio kwanzia siku mbili mbele za kusaini makaratasi ya manunuzi nikawa mmiliki kwa asilimia thamanini za hoteli hii ambayo nilikuja kuibadilisha jina na kuita Park Hyatt Sydney.

Nilipangua utendaji mzima wa hoteli hio huku nikimuweka Ras kama Manager mkuu , na katika hili sikumpendelea kabisa kwani alikuwa akitosha kabisa katika nafasi hio na hili liilidhihirika baada ya mwaka mmoja wa kuchukua hoteli hii , kwani kwa ukarabati tuliofanya na uboreshaji wa huduma iliweza kuvutia wateja wengi sana ndani na nje ya Australia , jambo ambalo mimi mwenyewe lilinishangaza sana .

Kwani ndani ya miezi kumi na nne ya umiliki wangu matajiri wakubwa waliweza kufikia ndani nya hoteli hii ,lakini pia hoteli yangu iliweza kushinda zabuni nyingi za kimataida na za ndani ya nchi .

Mwanzo wa mafanikio makubwa niliokuwa Napata ,ndio mwanzo wa kusahau mambo yalionitokea ndani ya taifa la Tanzania, na kwa kiasi Fulani furaha yangu kurudi upya , na kwa kipindi chote hicho Ras alikuwa rafiki yangu mkubwa , japo alishawahi kunitongoza lakini nilimkatalia katakata , kwani ndani ya moyo wangu licha ya mambo ambayo Peter alinifanyia sikuwahi kumsahau hata mara moja , na nilijiapiza sitokuja kuwa na mwanume mwingine tokea pale mume wangu Hemedi alipofariki Dunia.

Upande wa Erick ukuaji wake ulikuwa ni wa kushangaza sana kuliko isivyo kawaida na hili halinikushangaza mimi tu lakini pia madaktari wengi wa hospitali ya Randwick ambayo nilikuwa nikimpeleka katika ratiba za ufuatiliaji wa ukuaji wake .

Ndani ya miaka mitano ya Erick alikuwa akiongea kama mtu mzima , na alikuwa na kichwa chepesi mno katika kukumbuka vitu, na nilipongezwa sana na walimu wa Sydney Grammer School kwa kupata bahati ya kuwa na mtoto kama Erick , jambo hilo kwangu lilikuwa la lfaraja mno , kwani ukichana na mambo ambayo yalinitokea katika maisha yangu ya nyuma , kwangu Erick ni kama bahari Mungu alionipatia.

Muda ulisonga miaka ikapita , na ukuajji wa Erick ukaendelea kushangaza wengi husani katika maendeleo ya shule.

Nilichokuja kugundua ni kwamba Erick alikuwa na akili nyingi sana na naweza kusema kwamba ni jiniasi kwani baada ya miezi kadhaa ya mwanangu kuhudhuria shule ya Grammer School , alikuwa amewaacha mbali sana wenzake ambao alikuwa akisoma nao darasa moja , lakinii pia niliweza kuletewa ripoti ya maksi alizopata mara baada ya kupimwa IQ(Intelligency Quontient ),maksi zake zilikuwa ni 140 maksi ambazo mwalimu Ashley aliniambia ni kiwango cha juu kabisa kwa binadamu wenye uwezo mkubwa wa akili .

Jambo hilo kwangu lilinifurahisha sana , lakini naweza kusema ndio mwanzo wa msururu wa matukio mbalimballi ambayoo yalikuwa yakitokea kwa mwanangu , kwani mara nyingi alikuwa akifuatwa na watu mbalimbali , wengine wakiwemo watu wakubwa wakimuhoji vitu mbalimbali , jambo ambalo lilikuwa likinitia wasiwasi juu ya usalama wa mwanangu ,, nilijaribu kuongea na walimu wa Sydney Grammer School na waliishia kunitoa hofu kwamba sina haja ya kuwa na wasiwasi kwani wanatoa ullinzi wa kutosha kwa wanafunzi wanaosoma ndani ya shule hio , na mimi niliona kama na kuwa ‘paranoid’ hivyo niliona jambo la kutoa wasiwasi wasi wangu juu ya usalama wa Erick ni kujikita katika biashara Zaidi .

Baada ya mwaka mmoja kupita yaani mwaka wa sita wa mimi kuwa ndani ya nchi hii ya Australia niliweza kumuhamisha Erick kutoka shule aliokuwa anasoma na kwenda kusoma katika shule ya vipaji maalumu , hii ni shule ambayo ilikuwa ikimilikiwa na Victoria mwanamama Profesa ambaye aliniuzia hoteli ambaye naweza kusema kwamba alikuwa ni mmiliki mwenza ,yeye ndio alioniushauri kumpeleka Erick katika shule yake iliokuwa ikifahamika Hope School of Elite Kid (HSOEK),Ilikuwa ni shule kubwa na yenye hadhi ndani ya taifa hili la Australia na ilikuwa ikifahamika sana ndani na nje ya nchi , ilikuwa na level zote mpaka High School na kilichonifurahisha na kunishawishi kumpeleka Erick katika shule hiii ni historia kubwa ya shule hio katika kutoa wanafunzi bora kitaifa ambao walikuja kufanya mageuzi katika Nyanja mbalimbali.

Biashara zangu zilikuwa zikisonga vyema jambo ambalo pia lilikuwa likinishangaza lakini pia baadhi ya wafanya biashara wenzangu kunishangaa kwa hoteli yangu kukua sana ndani ya muda mfupi huku wengi wao wakitaka kujua ni siri gani ambayo ninaitumia mpaka kufanya biashara kuniendea vizuri ,lakini sikuwa na majibu sahihi ya kuwapa , kwani kama ni ubora wa huduma hoteli nyingi ndani ya Jiji la Sdney zinakuwaga na huduma zenye ubora wa hali ya juu sana na naweza kusema hata kuzidi hoteli yangu ,japo hata hoteli yetu ilikuwa na huduma bora.

Miaka ilisogea biashara zilienda vyema , lakini pia Maendeleo ya Erick yalikuwa ni ya kufurahisha sana , kwani aliendelea kuwashangaza watu kwa uwezo wake wa kufikiria na kutatua matatizo mbalimnbali , alikuwa akipenda sana Masomo ya computer na hili naweza kusema kwamba ni kama alikuwa amerithi kutoka kwa baba yake , kwani yeye pia alikuwa akipenda sana maswala ya Computer na hata kipindi ambacho ninakutana nae kwa mara ya kwanza ni kutokana na tatizo la kitehama lilillotokea ndani ya Benki yetu , tatizo ambalo liliwashidna wafanya kazi wa ndani ya benki.

Baada ya Erick kumaliza masomo yake ndani ya HSOEK moja kwa moja alijiunga ndani ya chuo cha Monash kilichokuwepo ndani ya jiji la Melbourne akichukua kozi ya maswala ya komputa (Computer Science).

Alisoma ndani ya chuo hicho mpaka kumaliza akiwa ni kinara kati ya wanafunzi wote kwa kupata GPA kubwa , jambo ambalo liliwainua wanasayansi kutoka makampuni makubwa ndani ya nchi na nje wakitaka kumuajiri katika kampuni zao za maswala ya kiteknolojia , lakini kwa mwanangu Erick alikuwa hataki kusikia swala la ajira jambo ambalo hata kwangu halikunishangaza kwani hata mimi pia nilikuwa nikichukia sana maswala ya kuajiriwa , hivyo nilipanga kumsapoti kwa namna yoyote ile pale tu atakapo taka kujiajiri.

Siku moja wakati nikiwa nyumbani nilishangaa kumuona Erick akiwa nyumbani , jambo ambalo siio kawaida yake , kwani hakuwa mtu wa kukaa kabisa nyumbani , na nilikuwa nikimuona mara chache sana na hata mara nyingine wakati nikiwa nimemmisi kumuona huwaga nafunga safari na kwenda kumuona Mellbourne , naweza kusema japo ya kwamba alikuwa akionesha kunijari sana na kunipenda kama mama yake lakini hakuwa na ile tabia ya kuja kunisalimia mara kwa mara , na hata chumba chake kilikuwa kipweke muda mwingi , na pia nilikuja kugundua kuwa Erick alikuwa ni mtu wa wanawake sana , alikuwa akibadilisha sana wanawake , hii tabia nilijaribu kumkataza na kumuonya lakini hakuiacha ., ni kama ilikuwa starehe yake , nilipunguza hata kumpa hela nyingi lakini nalo halikusaidia kwani alizidi kunishangaza kwa namna ambavyo alikuwa akijitanua katika visiwa mbalimbali ndani ya nchi na nje ya Nchi , swala ambalo lililikuywa fikirishi kwangu pia ni kwa namna gani anapata pesa , lakini sikuweza kupata jibu kwani kila nilipokuwa namuuliza alikuwa akinipa jibu kwamba nimuache na maisha yake , na hahitaji pesa yangu kuijua dunia .

Sasa siku kumkuta nyumbani jambo hilo lilinishangaza kidogo ,, lakini pia lilinifurahisha kwani nilikuwa nimemisi uwepo wake ndani ya nyumba , baada ya kusalimiana nae , hatimae aliniambia nia yake ya kurudi nyumbani , jambo ambalo lilinifurahisha na kulipokea kwa mikono miwili , lakini hakuishia hapo tu aliweza kuniomba kiasi kikubwa cha pesa , ilikuwa ni dolla za kimarekani milioni kumi , kiasi ambacho kilikuwa kikubwa sana na nilitaka kujua sababu ya yeye kutaka kiasi hicho cha pesa na jibu alilonipa ni kwamba alikuwa akitaka kufungua kampuni yake , kwangu swala hilo lilinifurahisha mno kwani ndio jambo ambalo nilikuwa nikilisubiria sana kutoka kwake .

Sikutaka kumuhoji sana kwani mwanangu alikuwa na tabia ya kususa pale unapomuhoji sana , na mimi kwaua kipindi hicho nilikuwa na pesa nyingi na nilikuwa moja ya wawekezaji wanaochipukia wakubwa ndani ya Austraslia basi niliandaa kiasi hicho cha pesa na nikamuingizia kwenye akaunti yake.

Kama alivyo ahidi alikuwa amebadilika kabisa alikuwa akiishi nyumbani na hata ile tabia yake ya kutoka toka na wanawake maeneo mengi ya starehe aliacha, alikuwa na mwanamke mmoja tu ambae alikuja kunitambulisha kama mpenzi wake , alikuwa ni mzungu mwanadada aliekuwa akifahamika kwa jina la Sarah.

Siku moja niliingia kwenye chumba chake na hii ni mara baada ya kumgongea sana pasipo kufungua jambo lilonitia wasiwasi , sikuwa na utaratibu wa kuingia kwenye chumba chake japo ya kwamba vyumba vyetu vilikuwa mkabala .

Siku hio ndio nilishangaa mno ndani ya hiki chumba kwani nilikuta kilikuwa kimezagaa makaratasi mengi ambayo yalikuwa yametupwa chini mengine yakiiwa na michoro mbalimbali , mingine ikiwa ya ndege , mingine ikiwa ni ya kitaalamu ambayo sikuielewa , lakini pia niliweza kuona mavitabu mengi ambayo yapo juu ya meza yakiwa yametapakaa mpaka juu ya kitanda yakiwa yamefunuliwa, lakini jambo ambalo nilishangaa pia ni kwamba vitabu vingi vilikuwa ni vya lugha ya Kilatini na kigiriki ambavyo nilishindwa kusoma .

Nilisogea ndani ya chumba chake huku nikimwita , na baada ya kumkosa nilisogea kwenye chumba ambacho nilikitenga kama sehemu ya kusomea na hapo ndipo nilipo mkuta akiwa amevaa maheadphone .

“Yeeeeeessssss….!!!!!. Yes , Yes , Yes……. “ Ni maneno aliokuwa akitamka na ni kama mtu ambaye alikuwa akitafuta jambo Fulani na wakati huo alionekana kufanikiwa na alikuwa akishangilia , na hakujua kama nipo na mwangalia mpaka pale ambapo aligeuka na kuniona na alinikimbilia na kunikumbatia huku akionyesha kushindwa kuzuia furaha yake , jambo ambalo kwangu liliongeza shauku ya kutaka kujua ni kipi hicho kilicho mfanya kufurahi kwa namna hio.

“Mom ! I did it , I made it”

“You did what Erick , tell me” niliongea na kumfanya aniangalie na kisha akatabasamu na kurudi kwenye meza na kuchukua karatasi tatu na kunionyesha .

“Hii ndio alama inayowakilisha kampuni yangu (logo)” Aliongea huku akinionyesaha ndege aina ya Kasuku akiwa amesimama kwanye kijiti , karatasi ya pili alinionesha ikiwa na jina la kampuni lililosomeka kwa kama The Truth, Karatasi ya tatu ilikuwa na maandishi yaliosomeka kwa jina ONLY GIFTED KNOW THE TRUTH(akimaanisha kwamba waliozaliwa na kitu cha ziada ndio wanaoujua ukweli) ,nilishangaa lakini na kutabasamu kwa wakati mmoja huku kilichonifanya kutabasabu siku hio hata sikuwa nikijua . ni nini lakini nilichokuja kugudnua baadae ni kwamba , kwa miaka mingi sikuwahi kumuona Erick akiwa kwenye furaha ya aina hio na niliamini kwa kitu ambacho amepatia huenda kikawa kikubwa , kwani nilikuwa nikijua kuwa ana uwezo mkubwa wa akili na siku zote watu wenye akili kubwa ni mara chache sana kueleweka kwa kile ambacho wanakifanya na mimi japo ya kuonionesha makaratasi hayo nilitabasamu kuwa nina furaha kwa ajili yake kwa kila anacho kifanya , lakini ukweli ni kwamba sikuona mantiki kabisa kwa kile alichonionesha.

“Mom uneweza usielewe nilichokuonesha , lakini vitu vitatatu vinamaana kubwa sana ambazo kama unamacho ya kuona utaelewa ni kama mchoro wa Monalisa”.

“Nieleweshe nipate kuelewa maana hii hali ya hapa ndani naamini ulichofanya nikikubwa”

“Even more mom , Do you know there is only one Secret in the world that hold all the truth ?”Ni Zaidi ya hayo mama ,Je unajua kwamba dunia ina siri moja kubwa ambayo inabeba ukweli wa mambo yote”

“Ukweli upi Erick?”

“Hilo ndio jina la kampuni yangu , Kampuni yangu itakuwa ni kwa ajili ya kutambua ukweli unaoonekana na ule usio onekana ,Ukweli ni nguvu , ukweli ni madaraka , ukweli ni utajili katika dunia hii na ni wachache sana katika hii dunia wanaujua ukweli na wanatafuta namna ya kuujuha ukweli , watu watahitaji ukweli kwa namna yoyote ile iwe ni kwa kununua ama kwa njia nyinginezo.Watu ambao wanakitu cha ziada ndani yao ndio wamepewa uwezo wa kuujua ukweli ,Ukweli usionekana ndio unanguvu kubwa ndani ya dunia hii , wanaoujua ukweli ni watu wenye madaraka makubwa ndani ya dunia hii na hawa watu wanaulinda ukwei huo usionekane ili wawe ndio pekee wenye nguvu Zaidi katika dunia”.

Yalikuwa ni maneno mengi sana kutoka kwa Erick lakini mpaka wakati huo bado sikuelewa anachomaanisha , japo maneno yake yanamaana kwa kiasi chake , lakini kwa upande wa biashara sikuona namna ambavyo atatengeneza pesa na hio ngio mantiki ambayo nilikuwa nikiitafuta katika maneno yake , lakini sikuipata .

Sikuweza kuongea sana na Erick , nilimuacha aendelee na mambo yake huku nikimwambia kuwa mimi nataka mafanikio yanayoonekana sio hadithi na hilo aliniahidi kwa asilimia mia moja kwamba atanithibitishia .

Zilipita siku mbili tena nilienda kumuamsha Erick , lakini ile nafika kwenye chumba chake huku nikijua kwamba yupo ndani , nilimuona akiwa ndio anafika , huku akiwa ameshhikilia karatasi mbili , nilisalimiana nae na kisha aliniambia anakitu anataka kunionyesha na mimi sikuwa na hiyana , niliingia ndani ya chumba chake ili kuona hiko kitu .

Zilikuwa ni picha mbili alizonionesha na picha hizo zilikuwa za mwanaume ambaye aliniambia kuwa mwanaume huyo alikuwa ni Mtanzania ambae amevaa Mask , sikumwelewa , lakini aliendelea kunionyesha kwa ushahidi huku akiniambia watu wawili tofauti ambao nawaona katika picha ni mtu mmoja , na kilichhofanya watu hao kuonekana tofauti huku akiwa mtu mmoja ni teknolojia , alimalizia na kuniambia swala hilo ndio kama swala analozungumzia yaani ninachokiona ndio ukweli unaonekana na nisichokiona kwa mtu huyo kuwa mtu mwingine ndio ukweli ambao haunekani , huku akimalizia kwamba kisicho onekana ndio nguvu ya mtu huyo .

Nilimuuliza kuhusu jina la mtu huyo na hapo ndipo alipo nitajia jina la Damiani Raban na Stephano Lamberk, kwanzia siku hio sikumwelewa na kumuamini kabisa , kwani watu ambao alinionyesha walikuwa ni watu wawili tofauti ambao sikuwa nikiwajua .

Siku moja ikiwa ni Jumapili nikiwa naelekea kanisani , aliamka mapema Erick na kuniaga kwamba anaenda kutafuta ukweli , huku akiniahidi kwamba atarejea , hio ndio ikawa siku yangu kuonana na mwanangu , kwani kwanzia siku hio mpaka sasa ni miaka miwili sijawahi kuonana na Erick.

Katika haarakati za kumtafuta Erick ndio nilianza kufatilia picha ambazo alikuwa ameweka chumbani , picha ya mtu ambae aliniambia kwamba alikuwa ndio Damiani Rabani ambaye pia anafahamika kwa jina la Stephano Lamberk,dhumuni ilikuwa ni kutaka kujua kile ambacho alikuwa akimaanisha Erick kwani mpaka wakati huo sikuwahi kumuelewa na hata hela ambayo nilimpatia kwa ajili ya ufunguzi wa kampuni sikujua iko wapi kwani kwa kufaatilia akaunti za kibenki niligundua kuwa zilikwisha kutolewa , lakini pia nilijaribu kuwahusisha polisi na wanausalama wa taifa , na wao pia hawakua na majibu ya kueleweka kwa uchunguzi waliokuwa wameufanya .

Katika kufatilia habari ya Stephano Lamberk na Damiani Rabani ndipo nilikuja kupata kitabu cha WARAKA WA RAISI KABLA YA KIFO CHAKE kilicho andikwa na mwandishi ISSAI SINGANO (SINGANOJR) nilisoma kitabu hicho lakini bado sikuamini juu ya FBM mpaka siku ambayo niliweza kuonana na mtu ambaye alikuwa akizungumziwa na Erick , lakini pia na mwandishi SINGANOJR ndani ya hoteli yangu ya Hyat Park.



SURA YA 10

Kwangu simulizi hii ya huyu mwanamama ilikuwa ni ya kusisimua sana na kushangaza kwa wakati mmoja hususani kwa upande wa kijana Erick , mpaka wakati huo nilikuwa na ufahamu nusu wa kwanini Erick alianzisha kampuni aliokuwa ameiita The Truth .Licha ya kwamba nilikuwa nimejua nia yake kubwa ni kuujua ukweli lakini katika simulizi hii nijikuta nikijua mambo makuu matatu kuhusu Erick , jambo la kwanza Erick alikuwa ni mtu mwenye akili kubwa sana yaani ‘Genius’ na mimi katika maswala ya kijasusi haya mamb huwa mara nyingi yanazingatiwa sana , kwa mfano tu nchi ya Marekani wana idara za maswala ya kiusalama kwa mfan FBI , CIA ,NSA sasa katika harakati zote za maswala ya kudahili(Recruitment/Admission) kigezo kikubwa ni akili ya mtu , ukionekana una akili kubwa(IQ) , pamoja na baadhi ya vigezo vingine mfano kuwa na afya njema basi unakuwa ‘best candidate’ kwenye hizi idara .Si kwa Marekani tu , mashirika mengi ya kijasusi duniani huwa yanachukuwa watu wenye akili kubwa kwa mfano MOSSAD kutoka Israeli ,M16 kutoka

England na hata TISS kutoka Tanzania na hii yote ni kwamba hizi idara za kijasusi mara nyingi ni kama uhai wa taifa katika Nyanja zote ndio maana hata kwa sisi Mzalendo ajenti wetu ni majiniasi.

Swala la pili nililgundua kutoka katika simulizi hii yta mwanamama Rania ni ‘Ambition’ nashindwa hata kualiongelea kwa lugha yetu ya Kiswahili hili neno lakini maana yake ni kwamba ni mtu mwenye malengo makubwa yenye msukumo ndani yake , hivyo niligundua kuwa licha ya kijana huyu Erick kupewa akili kubwa ni kwamba alikuwa ni mtu mwenye malengo makubwa sana na hili linamfanya kuwa mtu hatari sana, kwani mara nyingi watu wa aina hii watafanya kitu chochote kile ilimradi kukamilisha malengo yao hata kama ni kutumia njia za giza (njia zisizohalali).

Swala la Tatu nililogundua ni kwamba licha ya kijana Erick kuwa katika umri mdogo lakini alikuwa ni mtu alietengeneza koneksheni na ni mtu ambae anaiafahamu dunia vyema na kwa simulizi ya mwanamama Raniua naungana na Erick pale aliposema kwamba Ukweli usioonekana ni Nguvu(Power) hili naliunga mkono kwa asilimia kubwa sana kwani katika uliumwengu wa kijasusi hili pia kwetu ni sehemu ya somo , Watu wanaojua ukweli au siri kubwa ndani ya hii dunia ndio watu wenye nguvu kubwa , hivi unadhani ni kwanini mashirika makubwa kama Freemasons , UMOJA NAMBA TISINI NA SABA ,Illuminat na mengineyo wanakuwa ni watu ambao hawaonekani , jibu ni kwamba kitu kisichoonekana kinakuwa na nguvu kubwa sana , na hili sitaki hata nikulazimishe kuniamini lakini unaweza ukajiuliza swali moja je ushawahi kumuona Mungu????.

Hivyo ukweli usionekana (Hidden Truth) ndio wenye nguvu kubwa na ndio unaoendesha dunia, lakini ndio unaofanya taifa na taifa kuogopana , wengi hapa ni mashahidi leo hii hakuna anaejua uwezo halisi wa kijeshi wa Marekani , au Urusi , au china hii yote ni kwamba kuna vitu ambavvo havionekani kwenye nchi hizo na hizi idara za kijasusi mara nyingi zinajikita kujua hivyo vitu visivyo onekana.

Hivyo kwa kijana Erick kuwa na malengo ya kuutafuta ukweli namuona ni kama Jasusi wa kujitegemea , kitendo cha kujua uhalisia wangu mpaka hapo ni kwamba kijana huyu kampuni yake hii ya The Truth hakuianzisha kizembe zembe, ninacho amini ni kwamba mpaka kupata wazo la kuanzisha hii kampuni au kikundi ni kwamba alianza kukutana na jambo , na hilo jambo huenda lilikuwa kubwa kwake na lilikuwa likihusiana na ukweli uliofichika na katika hilo jambo alinusa nguvu kubwa ilioambatana na kweli hio aliokumbana nayo .Kwangu hayo ni makisio tu. “Nimeguswa sana na hii simulizi ya kijana Erick”Niliongea huku nikimwangalia mwanamama huyu , na wakati huu tulikuwa tumeketi muda wote kwenye kitanda cha Erick ndani ya chumba chake huku mbele kabisa kukiwa na picha ya Kasuku pembeni kukiwa na picha zangu zilizotundikwa .

Mwanamama huyu alikuwa akionesha hali ya huzuni sana , lakini sio huzuni tu lakini pia alionyesha ishara kama zote za upweke , na jambo hili lilidhihirika ndani ya nyumba hii , kwani licha ya wafanyakazi wawili ambao niliowaona wakati wa kuingia ndani ya hiii nyumba sikuona harufu ya mtu mwingine ambaye naweza kusema ni mtu wa karibu wa mwanamama huyu.

“Nitahakikisha Erick anapatikana Rania”Niliongeea huku nikiwa nimemkazia macho usoni nikiyaangalia machozi yake yaliozidi kupendezesha uso wake ,Nilinyoosha mkono wangu na kisha nikayafuta kwa kiganja cha mkono jambo ambalo lilimfanya mwanamama huyu kupoa kiasi lakini kunikazia macho ambayo kwangu niliona ulegevu wa macho , jambo ambalo pepo la ngono lilianza kuninong`oneza nimkule huyu mwanamke.

“Vipi kuhusu Peter baba wa mtoto Erick ?”

“Long gone , nishaanza kumsahau kwasasa na sijui hata yupo hai au amekufa”

“Kwanini unasema hivyo ?”

“Ni stori ndefu sana iliotokea nchini Tanzania na hata sitaku kuikumbuka”

“Kwa hio sasa hivi umeolewa au upo kwenye mahusiano ya namna yoyote ile?” Nilijikuta nikiuliza swali hilo la kipumbavu kabisa , kwani kwa urembo wa mwanamama huyu ni Dhahiri kabisa wanaume watakuwa wamepangiliwa vyema, Aliniangalia usoni huku akionekana ni mtu ambae anavuta pumzi na kuzitoa hali ambayo niligundua alikuwa akijiandaa kwa kunijibu lakini alikuwa kwenye ‘dilemma’.

“Sijawahi kuwa kwenye mahusiano ya aina yoyote ile tokea niingie ndani ya nchi hii , japo ya kukutana na vishawishi mbalimbali kutoka kwa wanaume wengi sana wenye nazo na wasio nazo , wazungu wahindi , , arabs na hata wa Afrika walikuwa wakitaka kuwa na mahusiano na mimi lakini sijawahi kuruhusu moyo wangu kumuamini mtu , sitaku kuzungumza sana kuhusu hayo Damiani Stop making me talk about those things. they are boring enough”.

“Okey nimeacha na nakuamini kwa maneno yako japo inaweza kunigharimu”Niliongea huku nikitabasamu na yeye pia kutabasamu kwani alikuwa ashaelewa nilicho kuwa nikimaanisha .

“Nataka kukuona ukiwa kwenye ‘African Colour’ kama Damiani nachukia rangi nyeupe unajua , lakini pia nataka nione unavyobadilika”Aliongea huyu mwanaume maneno matatu ambayo ukijumlisha yote ni ombi lakini ukiyachambua unapata maneno mawili ya kawaida lakini la mwisho lenye uhatari , unaweza usijue ni uhaatari wake ila utanielewa kwa vitendo.

Sikuwa na haja ya kumbania mwanamama huyu kumuonesha kile ambacho alikuwa akitaka kuona , niliongozana nae mpaka kwenye chumba changu kwa ajili ya kuivua hii FBM m sikuwa na haja hata ya kumjali , alionekana ni mwenye kujiamini wakati tukiwa tunaingia hapa ndani kwenye hiki chumba , lakini kadri ya matendo yangu niliokuwa nikiyafanya nilimuona akiaza kupoteza kujiamini , sheria za FBM ni kwamba lazima niwe Uchi ili kuivua na hili nilidhamiria kufanya mbele yake , yeye si alitaka aone jinsi ninavyovua na kuvaa basi namimi niliona nimtimizie ombi lake .

Lakiwa akiniangalia kwa wasiwasi sana wakati huo nikiwa nimebakisha boksa tu , ni kama mtu ambae alikuwa haamini kama ninakwenda kuvua ile boksa na kufumba na kufumbua nilikuwa uchi tena nikimgeuzia upande ule bwana kalumanzira aliolala , dakika chache mbele nilikuwa Damiani Rabani, na hapa ndipo mwanamama huyu alipozidi kushangaa na kupagawa , nilijikuta nikimsogelea pale aliposimama yeye akiwa hasogei , na kuhesabu sekunde kadhaa tu nilikuwa nishamfikia na kumshika mkono , alionekana kuwa dhaifu mno , kama mtu ambae hajapata chakula kwa siku nyingi sana na mbele yake kulikuwa na chakula .

Sekunde sabini mbele Rania alikuwa chini huku mimi nikiwa juu yake tukipiga Romansi , mwanamke alikuwa na mwili laini huyu sijapata ona , kila sehemu niliokuwa nikigusa utadhani patachanika , na kwa jinsi alivyokuwa wa moto msisimko nilioupata hapo sikuwahi kuupata mahali popote pale , akili zangu zilihama kwa muda , kwa mdakika kadhaa ya kumshika shika alikuwa amelegea mno huku akipanua miguu yake Zaidi akionekana kuwa ni mwenye uhitaji wa juu sana wa uanaume wangu kumuingia , na mimi sikuwa na ajizi nilimpa kile alichokuwa anataka na hapo ndipo nilipomshuhudia mwanamama huyu kupanua mdomo huku akitoa machozi , sikujua ni ya utamu au nini lakini sikutaka kujali sana , nilipeleka chini juu mpaka pale nilipoona sauti yake inakauka kwa kilio ndipo nilipopunguza , nilimgeuza na kumgeuza huku nikijisikia utamu wa ajabu sana ambao sikuwahi kuupata , na weza kusema mtoto alikuwa mtamu huyu , nadhani hili ni kutokana na kutokukuguswa kwa muda mrefu sana kwani kitu ilikuwa mnato sana .

Dakika arobaini mbele wote tulikuwa tumechoka huku tukihema kama mbwa aliekimbia maili nyingi ,nilimwangalia mwanadada huyu na kujikuta nikipokea tabasamu ambalo liliufanya uchomvu wangu wote wa safari ndefu kuisha hapo hapo na kujikuta tukiiingia kwenye mtanange na awamu hii ulinoga sana kiasi cha kunifanya nitoe mbegu wengi sana ndani ya uanamke wa Rania .

Wakati nikimaliza ni kama Janeth alikuwa akiona kile nilichokuwa nikifanya kwani simu yangu ilitoa mlio na kuichukua.

“Damiani najua unacho kifanya lakini naomba uache , tumegundua ile picha ya Kasuku sio mchoro wa kawaida “

“Unamaanisha nini ?”

“Namaanisha unatakiwa kurudi kwenye chumba cha Erick na tutakupa maelekezo mengine “Aliongea janeth huku nikimuona kama mtu ambae anajizuia hisia zake zisiingilie kazi , lakini alikuwa amekwisha kuzoea , alikua akijua kabisa mapenzi yangu aliondoka nayo Merina.

“Hio picha ina rangi mbili ambazo hazijaungana , rangi ya juu ni rangi ambayo unaweza kuifuta kwa kuimwagia maji ya moto , naamini kuna kitu kimefichwa kwenye hio piucha “Aliongea janeth na nikampa maelekezo Rania ya kuleta maji ya moto , na dakika chache yalikuwa tayari na tuliimwagia ile picha maji baada ya kuiweka sakafuni .

“Kipi kinafuata janeth ?”

“Chukua brash ya kupakia rangi na fanya kama unaaza kuipaka rangi upya”

Nilifanya kama Janeth alivyokuwa anaelekeza na hapo ndipo mimi na Rania tulivyoweza kupigwa na mshangao kwani kila sehemu unayopitisha Brash rangi inapotea ‘Colour

Repracement’hii kitu ilinishangaza sana , nilichokuwa najua hii njia inaweza kufanyika kwenye komputa tu kumbe hata kwenye picha ya kawaida.

Ni namba kumi na mbili ambazo ziliandikwa kwa mfumo wa kirumi sikuelewa ni namba za nini , nilipiga picha na kisha nikazituma kwa Janeth ili kuzipatia maana yake na ndani ya dakika chache alikuwa na majibu .

“Ni ‘Cryptography’ namba”

“Zinamaanisha nini?”

“Hapa mpaka kuzitambua , hilo swala ili lifanikiwe nitahitaji Serial number za Kompiuta zilizopo hapo ndani” Aliongea na mimi nilimtumia na kwa mbaali nilielewa anacho maanisha , kwani kwa ninachojua kuhusu Cryptography ni kwamba huu ni mfumo wa kuficha maneno kwa muundo wa kodi , zinaweza kuwa namba au mfumo(format) wowote ule, hii njia ndio inzifanya Cryptocurrency kuwa na hali ya juu ya usalama kwani hata serikali haiwezi kujua hizi namba.

“NImefanikiwa kutambua hizo namba maana yake ni SANTORIN” “Santorin?” Niliongea na kumfanya mwanamama Rania aniangalie .

“Santorin ni kisiwa kilichopo ugiriki”.Aliongea Rania na hapo hapo nilipata kujua huenda The Truth haipo Australia kama tulivyodhania bali ipo Ugiriki.

“Erick atakuwa Ugiriki”Niliongea na mwanamama huyu alijikuta akishangaa lakini Janeth kuniunga mkono kwa kile ambacho nilikuwa nasema , na hili niliona ni swala ambalo linaleta Mantiki , kwa kazi ya hiki kikundi niliamini kabisa ni lazima wawe watu wa kujificha sana .

SURA YA 11

DAR ES SALAAM –TANZANIA

Zikiwa zimepita siku kadhaa tokea kuchaguliwa kwa waziri mkuu pamoja na mawaziri , lakini pia ikiwa imepita siku moja tokea mheshimiwa Raisi Jembe kusafiri kuelekea nchini Marekani kwa ajili ya kula kiapo cha kujiunga na umoja wa siri wenye nguvu duniani Umoja Namba Tisini Na Saba ,Ndani ya jijiji hili lenye pilikapilika za kila namna katika moja ya gorofa ndefu iliokuwa ikimilikiwa na mfanya biashara mkubwa nchini pembeni kabisa na zilipokuwepo ofisi za kampuni ya INNOVA ndani ya jengo hilo kulikuwa na kikao cha siri kilichokuwa kikiendelea .

Ndani ya hili jengo ndio zilipokuwepo ofisi za Umoja huu wa siri kwa eneo la Tanzania na ndio maana siku hio kikao hiki kilikuwa kikiafanyikia ndani ya hilo jengo.

Katika meza kubwa ndani ya chumba kikubwa ndani ya jengo hili katika floor ya kumi na tano chumba kilichokuwa na maandishi makubwa mlangoni yaliosomeka kwa lugha ya kingereza TOP LEVEL MEMBER OFFICE (TLMO) kulikuwa na mabwana wapatao kumi , watano walikuwa wakifahamika kwa majina yao kutokana na kwamba walikuwa ni viongozi wakubwa ndani ya serikali ya Tanzania, wengine hawakuwa wakitambulika kwa majina yao kwani walikuwa sio raia wa Tanzania na rangi zao zilithibitisha hilo .

Katika kikao hiki ajenda kubwa zilikuwa mbili , ajenda ya kwanza ambayo ilianza kujadiliwa ni wasiwasi wa uanachama wa mheshimiwa Jembe Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, japo ya Umoja huu kukubali ombi la raisi Jembe kujiunga na Umoja Namba Tisini na Saba lakini mabwana hawa walionekana kuwa werevu Zaidi kutokana na wasiwasi wao.

Mkuu wa majeshi , Mkuu wa kitengo cha usalama wa taifa ,Raisi mstaafu aliachia madaraka kwa Jembe ,Makamu wa raisi mteule aliengia madarakani , pamoja na mkuu wa jeshi la polisi ndio watu waliokuwa wakitambulika katika kikao hicho , lakini pia ndio viongozi wakubwa ndani ya nchi ya Tanzania walikuwa wakiunga mkono umoja huu wa siri ambao haukufahamika malengo yake kwa Taifa .

Mabwana hawa walikuwa wakijua fika mheshimiwa Jembe hakuwa na nia thabiti ya kujiunga na umoja huo , jambo ambalo mabwana hawa waliona linaweza kuufanya umoja huu kutojiimarisha vyema ndani ya nchi , walihofia juhudi walizokuwa wamefanya katika kurudisha nguvu ya umoja huu ndani ya Taifa la Tanzania zinaweza kupotea .

Jambo la kwanza liliowafanya mabwana hawa kutilia mashaka nia ya bwana Jembe ilikuwa ni siku ya kuapishwa kwake , kitendo cha Peskorov kupigwa na kuzirai siku ambayo amefanya tukio la kumpiga risasi mheshimiwa Jembe na kugundulika kwa alama ya Mzalendo iliokuwa imeachwa katika paji la uso la bwana huyo liliwafanya mabwana hawa waamini kwamba mheshimiwa jembe alikuwa na ushirikiano na kikundi hichi ambacho walikuwa wakiamini kwamba kilikuwa kimepotea ndani ya nchi hii yaani Mzalendo.

Lakini kitendo cha Jembe kupita katika uchaguzi , lakini pia kupona risasi , lakini pia kupotea mara baada ya kupigwa risasi , lakini pia kujitokeza na kutaka kujiunga na U-97 , lakini pia alama ya Peskorov katika paji la uso ilioachwa na mtu ambae alipambana nae mambo hayo yote yaliwafanya waamini kwamba Mzalendo ambayo ilikuwa imetokomezwa miaka kumi iliopita imerudi upya tena ikiwa na nguvu Zaidi kuliko awali. Kwani matukio yaliotokea hayakuwa yakufanywa na mtu mmoja , walimini matukio hayo kwa yeyote aliekuwa akihusika alikuwa na nguvu kubwa sana.

“Unatoa ushauri gani bwana Kinga juu ya rangi halishi ya bwana Jembe ?” Swali hili lilitoka kwa bwana Kent kwenda kwa mkuu wa usalama wa Taifa ,Kent ambaye alikuwa ni muwakilishi wa U-97 Afrika mashariki alikuwa akimuamini sana Kinga , katika vikao vyote alivyokuwa amefanya alikuwa akifurahishwa na michango ya kimawazo ya Kinga , kwani siku zote waliweza kufikia maaumuzi na mawazo yaliokuwa yakitolewa na bwana huyu na ndio maana kwa kila kikao alikuwa akimfanya kuwa mtu wa mwisho katika kuchangia .

“Mkuu kwanza kabisa naamini kwa asilimia mia moja kuna mpango ambao anao mheshimiwa jembe ,tena mpango huu ukiratibiwa na kikundi hiki cha Mzalendo na yeye akiwa ni moja ya jumuia ya kikundi hiki , na hata swala la yeye kutaka kujiunga ndani ya hiki kikundi nimeweza kufikiria na kuja na mambo makuu mawili kwa mheshimiwa kutaka kujiunga na umoja wetu , la kwanza ni kutaka kukalia kiri cha uraisi , kwake swala hili limekuwa ndio njia rahisi ya kupata usalama wa kufika pale ikulu kutokana na tukio lililomtokea , swala la pili , mlolongo woote wa matukio yaliotokea katika siku ile ya kupigwa risasi ni Dhahiri bwana huyu alikuwa akijua kile kilichokuwa kikiendelea , na ni jambo ambalo lilikuwa limepangwa kwa ustadi mkubwa sana na ninyi wote hapa ni mashahidi kwamba hakuna mtu duniani ambaye anaweza kupigwa risasi kwenye kifua na kupona tena bila hata ya kuwa na jeraha isipokuwa tu kama jambo hilo mtu huyo awe analifahamu na kuvaa ‘Bullet Proof’ , lakini tunaweza kusema labda mheshimiwa jembe aliweza kuvaa ‘Bullet Proof’ , lakini ni vipi kuhusu kufichwa kwake mara baada ya kupigwa risasi , tena akifichwa na wanausalama wetu ambao mpaka sasa hatujui mahali walipo,hivyo ninacho amini kwa sasa ni kwamba swala hili hatuwezi kulichukulia kwa urahisi , hili ni swala la dharura na tunapaswa kulichukulia kwa udharura wake ili kuchukua tahadhari zote , tunapambana na watu wenye maarifa na wenye nguvu , mpaka sasa mkuu wa tume ya uchaguzi hatujui aliko yeye pamoja na familia yake haya yote sio mambo ya bahati mbaya , ni maswala ya kupangwa . tena ya kupangwa kwa muda mrefu , hivyo ushauri wangu kwasasa ni kuhakikisha tunaweka nguvu zetu zote kukisaka hiki kikundi na kukitokomeza moja kwa moja na kuhakikisha tunatoa mizizi yote ili kuepusha kuchipuka tena”

Aliongea bwana kinga na kufanya watu wote waliokuwa katika kikao hicho kutafakari maneno hayo , lakini si hivyo tu kila mtu aliweza kuwaza na kuvuta picha kamili ya kikundi cha Mzalendo kwa kuunganisha matukio machache yaliotokea siku kadhaa zilizopita.

“Umeongea vyema sana bwana Kinga , lakini kwanza kabisa naomba nikutoe hofu lakini pia niwatoe hofu watu wote mliopo ndani ya hiki chumba , kwanza kabisa Mzalendo ni kakikundi kadogo sana ambako kalibahatisha kufanya matukio yaliotokea , lakini yakaleta athari kubwa , lakini kubahatisha kwao hakumaanishi kwamba kikundi hiki kinanguvu na maarifa kutuzidi sisi ,tulichokosea nikuwadharau hawa watu na kakikundi kao , lakini mpaka sasa hali imerudi kama ilivyokuwa na naweza kusema kila kitu kinaenda kama tulivyopanga na muda mfupi ujao tutawakamata wahusika wotea wa kikundi hiki”

“Swala hilo litakuwa gumu kutokana na kwamba watu hawa bado hawafahamiki na ndio maana nimeshauri kulichukulia tahadhari”Aliongea Kinga na kumfanya Bwana kent kutabasamu , moja sifa kubwa ya bwana Kent ni dharau alikuwa akiwadharau sana watu weusi , unaambiwa tokea akiwa mdogo katika historia yake ya shule zote alizopita bwana huyu alikuwa mbaguzi wa rangi wa waziwazi , sifa yake ya pili alikuwa ni ‘Sadist’ hawa ni watu ambao wanapenda kuona wenzao wakiteseka kwa kuwasababishia maumivu licha ya bwana huyu kutibiwa lakini ni kwamba hakupona kikamilifu, hata tabasamu alilokuwa akumuoneshea Kinga licha ya kwamba alikuwa akimkubali katika michango yake , tabasamu hilo lilikuwa la dharau lakini usingeweza kumjua .

“Huna haja ya kuwa na wasiwasi bwana Kinga U-97 ilijengwa na watu wenye akili na mpaka sasa tuliobaki wote tunakili , hivyo hata hawa Mzalendo hawawezi kushindana na sisi maana sisi sio nchi bali sisi ni Dunia hivyo mtu mmoja hawezi kushindana na Dunia ,Swala la Mzalendo kumtumia Jembe katika mipango yao ni makossa makubwa waliofanya na hili linadhihirisha uwezo wao mdogo wa kufikiria ,Jembe huko anakoenda anaenda kuwataja hawa panya wote na kazi itakayobaki ni sisi kuwakamata hapa Tanzania na kuhakikisha hakuna hata mmoja anaekimbia wala kukosekana”

“Itawezekana vipi kwa mheshimiwa Jembe kuwataja wafuasi wake ?”Aliulizwa Kilubwa raisi mstaafu aliechia madaraka akiwa kwenye hali ya mshangao.

“PSYOPS” Aliongea Kent na baadhi ya watu hapo ndani walielewa huku wengine wakiwa hawajaelwa na walihitaji ufafanuzi .

“Kinga atawafafanulia ninachomaanisha na mpaka sasa kikao kimekwisha na ninagharisha mpaka kikao kingine tutakapozungumzia kuhusu Mpango Zero”Aliongea Kent na kisha kuondoka huku akiwaamuru walioelewa neno aliloongea waondoke na ambao hawajaelewa wabaki , na wale wazungu wote waliweza kuondoka ikidhihirisha kwamba walikuwa wameelewa kile ambacho Kent aliongea ila viongozi wote wakubwa hawakuelewa isipokuwa kwa bwana Kinga aliekuwa amepewa jukumu la kuwafafanulia wenzie juu ya maana ya neon PSYOPS.

*****

JOHN F KENNEDY INTERNATIONAL AIRPORT –NEW YORK, USA 18:00.

JFK ni moja ya viwanja vya ndege bora kimataifa vilivyokuwa bize sana ndani ya jiji hili la New York , Zaidi ya ndege 70 huruka na kutua kwenda na kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi ya Marekani , uwanja huu upo sehemu inayoitwa Queens ndani ya New York , ni uwanja wenye jumla ya terminal sita sifa inayodhirisha ukubwa wake, huku kila terminal kiwa na huduma bora kabisa..

Lakini sifa za ukubwa wa uwanja huu unaendana na umaarufu wa Jiji la New York , ni moja ya jiji lenye watu wengi Zaidi ndani ya nchi hii ya Marekani , na moja ya sehemu ambayo ina uhuru wa kuishi na kutafuta maisha ni ndani ya jiji hili , ukuaji wa jiji hili ulikuwa ni wa haraka sana ukilinganisha na majiji mengine .New York ndio kitomvu kikubwa cha biashara ndani ya taifa hili la Marekani na nje ya nchi pia kwani wafanya biashara wengi hutembelea sana jiji hili kwa ajili ya maswala ya kibiashara , moja ya maeneo maarufu ndani ya jiji hili ni kama Wall Street hili ni eneo ambalo maswala yote ya kiuchumi na kifedha yanafanyika , ndio sehemu ambayo makampuni makubwa ya kifedha na kibenki yanapatikana , ni sehemu ambayo maswala ya masoko ya hisa yapo , sehemu nyingine ni Time Squre hili ni eneo lenye watu wengi wanaotembea kwa miguu ni sehemu inayofahamika kwa majina ya kiutani mengi na moja wapo ni kama ‘Heart of the world’, pia moja ya utambulisho mkubwa wa NYC ni uwepo wa ‘Statue of liberty’,NYC ndio mji wenye magrofa marefu na mengi Zaidi ndani ya nchi ya Marekani na ndio eneo pekee ambalo hutembelewa na watu wengi Zaidi ndani ya nchi ya Matekani. Licha ya umaarufu mkubwa wa jiji hili nje na ndani ya Marekani lakini pia yapo mambo mengi yaliokuwa yakifanyika mengine yakiwa ni halali na mengine yakiwa sio halali

Nje kabisa ya mlango wa Terminal 4 alionekana mheshimiwa Jembe akitoka ndani ya mlango uliokuwa na maandishi makubwa yaliokuwa yameandikwa ARRIVALS akiwa ameambatana na walinzi wake pamoja na wasaidizi , Ndege aliokuwa amefika nayo mheshimiwa Jembe ilikuwa ni ya shirika la Fly Emirate . ndege ambayo alikodi kwa ajili ya usafiri huo .

Mara baada ya kutoka ndani ya jengo hili la kisasa kabisa alifuatwa na mabwana wawili mmoja akiwa ni mweusi na mmoja alikuwa ni mzungu wote wakiwa wamevalia suti nyeusi na miwani za jua , hawa mabwana kabla ya kumfikia Raisi Jembe walizuiliwa na walinzi na hapo ndipo walipotoa vitambulisho vyao .

Mabwana hawa walijitambulisha kama CIA mmoja akiitwa Ben Horowtz na bwana mwingine alijitambulisha kama Sam Snowden , mabwana hawa walijieleza kama moja ya watu waliokuwa wameagizwa kwa ajili ya kumpokea mheshimiwa na kumuongoza kuelekea mahali ambako anatakiwa kufika .

Walinzi wa mheshimiwa Jembe walijiridhisha na mabwana hao na kisha waliongozana nao mpaka kwenye maegesho ya magari na walimuonyesha mheshimiwa gari ambalo lilikuwa limeandaliwa kwa ajili yake

Baada ya kuingia ndani ya gari hili pamoja na mlinzi wake wa karibu ‘Bodyguard’ huku wale walinzi wengine wakipanda kwenye gari zingine ambazo zilikuwa pia zimeandaliwa, gari hizo ziliondka ndani ya eneo hilo.

Safari ya mheshimiwa Jembe ndani ya Marekani haikua ya kikazi na wala uongozi wa Marekani hawakuwa na taarifa rasmi za raisi Jembe kudhuru ndani ya Taifa hilo na jambo hili kwa namna yake lilishangaza kidogo kwani walipokelewa na CIA. .

Jumla ya gari zilikuwa nne , zilizokuwa zikimsindikiza mheshimiwa Jembe ndani ya muda mfupi gari zile zilikuja kusimama ndani ya nje ya uzio mkubwa wa nyumba , eneo lilokuwa likifahamika kama Shirley Chishom State Park, ndani ya Broklyn.

Lilikuwa ni jumba kubwa mno la kifahari lilikuwa ndani ya uzio huu , licha ya kwamba baadhi ya ,majumb ya pembeni kutokuwa na uzio lakini hili eneo lilikuwa limezungukwa na ukuta na hii ilionesha ni mahali ambapo si pakuingia ingia tu kama sio muhusika. .

Eneo lilikuwa tulivu sana lakini lenye madhari mazuri mno , ilikuwa ni kama hoteli huku muundo wa jingo hili ukiwa ni ule wa kizamani kabisa , ni kama yale majengo ambayo mengi utayakuta Italy hususani ndani ya Vatican city , baada ya magari yale kwenda kusimama sehemu maalumu ambayo ilikuwa ikitumika kama maegesho, mheshimiwa aliamriwa kushuka na ndani ya dakika chache kulitokea wanawake wawili wakiwa wamevalie mavazi ya suti na walionekana walikuwa mahali hapo kwa ajili ya kumpokea mheshimiwa Jembe.

“Welcome Mr President wing 7 House , my name is Hellen , Iam head of house meet my Assistant Sasha we have been waiting for you eagerly”

“Karibu mheshimiwa nyumba tawi namba saba jina langu ni Hellen ndio mkuu wa nyumba kutana na Sasha msaidizi wangu, tulikuwa tukikusubiria kwa hamu” Aliongea mwanamama huyu aliejitambulisha kwa jina la Hellen huku akiweka tabasamu pana usoni mwake.

“Asante sana Hellen” Alijibu mheshimiwa na kisha mwanamama huyu alimuongoza njia mheshimiwa pamoja na walinzi wake baada ya kuwahakikishia usalama

Mandhari ya jumba hili yalikuwa yakuvutia sana kiasi kwamba hata mheshimiwa Jembe alishangaa , yalikuwa ni Mandhari ya kifalme , kwanzia wafanyakazi waliokuwa wamesimama kwa kujipanga huku kumpa mheshimiwa Jembe ishara ya heshima , lakini pia thamani zilizokuwa zimetumika kupamba eneo hilo zilikuwa ni za kiwango cha juu sana .

Hata wasaidizi wa mheshimiwa walishangaa mapokezi ya aina hio , kwani baadhi yao ambao walikuwa ni wazoefu katika kusindikiza maraisi hawakuwahi kupata mapokezi ya aina hio ya kipekee licha ya kuwa hakukua na kiongozi mkubwa aliekuwepo ndani ya eneo hilo lakini mpangilio wa matukio ya hapo ndani yalikuwa ni heshima kubwa sana kwa mheshimiwa Jembe kupata , hata ile hofu aliokuwa nayo kiasi flani ilipungua .

“Mheshimiwa hii ni nyumba maalumu kwa ajili yako kuishi kwa kipindi chote utakachokuwepo ndani ya nchi hii , kuna kila kitu utakacho kihitaji cha kiofisi na kimalazi , utaweza kutimiza majukumu yako ya kiuongozi ukiwa hapa mpaka pale utakapokamilisha hatua tano za kula kiapo”Aliongea huyu mwanamama ambae alionekana umri umemtupa mkono na maneno yale kidogo yalimshangaza mheshimiwa Jembe lakini hakutaka kutia neno .

Basi aliweza kuonyeshwa maeneo mbalimbali ndani ya jumba hilo la kifahari kabisa , lilikuwa ni jumba kubwa lenye eneo kubwa ambalo lilikuwa na kila kitu kuanzia bwawa la kuogelea , uwanja wa Gofu pamoja na wa Tennisi .

“Uzuri wa hili eneo ni Zaidi ya Ikulu ya nchi yangu”Aliongea mheshimiwa mara baada ya kuoneshwa chumba ambacho takuwa akilala na kumfanya mwanamama Hellen kutabasamu . .



SURA YA 12

Ni siku nyingine ndani ya nchi ya Marekani ndani ya jumba la kifahari ambapo mheshimiwa Jembe alikuwa ameandaliwa na U-97 kwa ajili ya kuishi .

Asubuhi hii mara baada ya taratibu zote kuisha kama kupata kifungua kinywa na mengineyo , mwanamama Hellen alimtaarifu mheshimiwa Jembe kujiandaa kuingia ofisini kwani kuna mgeni ambae anatarajiwa kufika kwa ajili ya hatua ya kwanza.

Na ndani ya nusu saa tu ya mheshimiwa Jembe kuingia ofisini hatimae bwana mmoja wa makamo mwenye rangi mchanganyiko yaani ya kizungu na kiafrika alitinga ofisini hapo, alikuwa ni bwana mmoja kwa makadirio ya umri wake si chini ya miaka therathini , alikuwa amevalia suti nyeusi na kipepeo shingoni huku nywele zake akiwa amezichana kuelekea nyuma.

.

“Naitwa Dave Hamton afisa levo 32 ndani ya U-97 mimi ni mtaalamu wa maswala ya kiuchambuzi Duniani”utambulisho huo ulimfanya mheshimiwa Jembe kushangaa , kwani alaichotegemea ni hatua ya kwanza ya kula kiapo lakini anachokutana nacho ni mtu ambae amejitambulisha kama moja ya wachambuzi wa maswala ya kiuchumi duniani jambo ambalo kwake lilimshangaza kidogo .

“Karibu sana Dave”

“Asante sana mheshimiwa , Naamini umeshangazwa na utambulisho wangu”Aliitikia kwa kichwa

“Dhumuni la kikao chetu mheshimiwa ni juu ye kukuelezea juu ya malengo ya U-97 kwa Afiraka nzima kwa upande wa kiuchumi”Aliongea na kisha alitoa tablet yake na kumkabidhi mheshimiwa .

Mheshimiwa raisi alishangazwa na mambo mengi ambayo bwana Dave aliweza kumwambia , alikiri yeye mwenyewe katika kikao hicho kilichochukua masaa mawili kwamba umoja huu wa siri licha ya kwamba hakuwa akijua madhumuni yao makuu kwa mataifa ya kiafrika lakini kwa upande mwingine walikuwa wamesaidia ukuaji wa maendeleo kwa kiasi kikubwa sana , hususani katika swala zima la miundombinu na kuboresha maisha ya wananchi wengi , licha ya hivyo Dave aliweza kumuonesha nguvu ya umoja huu ndani ya mashirika makuu duniani kama vile IMF ,WB,UNICEF,WHO,ILO na mengineyo mengi makubwa .

Jambo hili kwa mara ya kwanza hakulielewa vyema mpaka pale alipoweza kufafanuliwa nguvu ya umoja huu ndani ya haya mashirika katika kuisadia Afrika ,bwana Dave alimwambia mheshimiwa kuwa U-97 ndio mara nyingi wanaohimiza mataifa mengi ya Afrika kupara misaada ya kufanya maendeleo na hii ni kwa zile nchi tu ambazo zitakuwa chini ya umoja huo .

Siku hio ilikuwa ni ya Vikao tu kwa mheshimiwa na watu hawa waliojitambulisha kwake kama wafuasi wa umoja NAMBA TISINI NA SABA ,

Mpaka inafika muda wa jioni wa vikao mheshimiwa alikuwa amepata uelewa mkubwa sana juu ya U-97 licha ya kutojua yandani ya umoja huo yaliokuwa yakitendeka lakini alipata kuweza kufahamu kuwa umoja huo kwa namna moja ama nyingine ulikuwa na faida kwa watanzania na alikiri kwamba watu aliokutana nao walikuwa na ushawishi mkubwa sana kwake.

Hatua za mwanzo za kula kiapo zilikuwa ni za kawaida na katika hatua zote hizo zilikuwa ni kwa ajili ya kuandaliwa kisaikolojia tu , hatua ya mwisho ndio ilikuwa ni ya kuogopesha sana kwa mheshimiwa Jembe , kwani katika hatua hii alikuwa akitakiwa kutubu dhambi zake zote , na ili uweze kupata nafasi ya kuweza kutubu dhambi anatakiwa kuweka siri zake zote wazi.

Siku iliofuata ilikuwa ni ya mheshimiwa Jembe kuingia kwenye chumba cha utakaso , hiki ni chumba ambacho sheria yake kubwa ni kwamba ili uweze kutakaswa na kula kiapo hutakiwi kuwa na jambo ambalo unalifich ndani ya moyo wako (Siri) , sheria za hiki chumba ni kwamba kama utaingia basi kunauwezekano mkubwa wa mtu kutoa siri zake zote kwa kile umoja huu ulichokuwa unakiita kuungama , yaani unaweka siri zako zote wazi ili uweze kupata nafasi ya kuungama na hatimae kuwa mwanaumoja kamili ambae huna makando makando , na kupitia hiki chumba cha utakaso siri nyingi ziliweza kupatikana juu ya mataifa mbali mbali . na si hivyo tu lakini pia kwa kila mwanachama ambae aliingizwa katika chumba hiko akitoka anakuwa mtu mpya na mtiifu kwa umoja, yaani kwa mnaneno marahisi ni kwamba kama ulikuwa na lengo baya dhidi ya umoja basi ukishaingia humo ndani , ukitoka utakuwa na malengo mazuri kwa umoja na utatii kila maelekezo utakayopewa na viongozi wa juu wa U-97.

Basi baada ya mheshimiwa Jembe kumaliza kujiandaa na kupata kifungua kinywa , walinzi wake walitaarifiwa kwamba mheshimiwa ataondoka ndani ya hio nyumba na kwenda katika kikao cha siri ambacho kitachukuwa takribani masaa kumi na mbili .

Hawa walinzi wake pamoja na wasaidizi kwanza kabisa hawakuwa wakijua kile kilichokuwa kikiendelea juu ya raisi wao kiula kiapo cha kujiunga na Umoja namba Tisini na saba , walichokuwa wakijua ni kwamba mheshimiwa alikuwa ndani ya taifa hilo kwa ajili ya maswala ya kitaifa, mtu mmoja pekee aliekuwa akijua kile kilichokuwa kikiendelea ni mlinzi wa karibu wa raisi (Bodyguard) na huyu katika safari hio ya kwenda kwenye kikao alikuwa amepewa nafasi ya kutangulizana nae , huku walinzi wengine wakiwa wamebakia ndani ya jumba la Wing 8.

Saa tatu kamili ndio saa ambayo mheshimiwa Jembe aliweza kutoka ndani ya nyumba aliokuwa amefikia kuelekea katika hekalu la Utakaso sehemu ambayo atakula kiapo rasmi cha kujiunga na umoja namba tisini na saba. Lakini pia sehemu ambayo alitakiwa kutakaswa na kuwa mpya .

Usafiri uliokuwa umetumika kumchukua mheshimiwa ndani ya Wng 8 house ulikuwa ni wa njia ya anga kwa kutumia chopa , huku ndani ya ndege hio akiongozana na mlinzi wake wa karibu na bwana mmoja ambae alijitambulisha kwa jina la Henlsink , bwana huyu alikuwa ni raia kutoka Mexico , alikuwa amevalia suti ya rangi nyeusi.

Ndani ya nusu saa tu walikuwa wapo ndani ya eneo ambalo mheshimiwa raisi na mimi mwenyewe sikueza kulitambua , lakini ndani ya eneo hilo lililokuwa limezungukwa na miti mingi kulikuwa likionekana jengo kama hekalu .

Chopa iliweza kukanyaga veyema eneo husika lenye alama kubwa ya H na baada ya hapo mheshimiwa alitoka na kuja kupokelewa na wanadada wawili , waliokuwa wamevalia kama masista , baada ya kupokelewa na hawa wadada ambao walijitambulisha kama wahudumu wa jumba hilo liliokuwa na maandishi makubwa mlangoni U-97 LODGE X .

Mheshimiwa Jembe alionekana kuwa na wasiwasi mkubwa kila alipokuwa akikumbuka maneno ya mwanamama Hellen juu ya jambo ambalo linafanyika ndani ya hekalu hilo kwa ajili ya utakaso, alikuwa na hofu ya kutoa siri zake na siri kubwa aliokuwa akihofia kuitoa ilikuwa ni juu ya mpango wa Mzalendo .

Aliamini kama kweli alichoambiwa na mwanamama huyo juu ya uwezekano wa kuweka siri zake hadharani , swala hilo lilimuongopesha sana , kwani aliamini kwa kufanya hivyo ni kwamba anakwenda kuharibu kila kitu na ile mipango ambayo alikuwa amejiwekea na kitengo cha Mzalendo inakwenda kukwama.

Baada ya utaratibu wa awali kukamilika wa mheshimiwa Jembe kupewa mavazi mengine kama yale ya wagnjwa wa hospitalini , aliweza kuingizwa kwenye chumba kimoja kilichokuwa kina maandishi makubwa mlangoni kama PSYOPS ROOM , maneno ambayo kwa mheshimiwa hakuweza kuyaelewa kabisa .

Ndani ya hili jumba ni kwamba muonekano wake ulikuwa ni kama wa hospitali , kwa nje lilionekana kama hekalu ila kwa ndani ni jEngo ambalo lilikuwa limejengwa kwa ustadi wa kutenganisha vyumba , na ilionekana hio ni sehemu maaliumu kabisa kwa ajili nya U-97 , ukutani kulikuwa na michoro mingi ambayo ilikuwa imechorwa na haikueleweka maana yake ni nini kwa mara moja .

Mlinzi wa mheshimiwa raisi bwana Tomasi Kibwe alikuwa kwenye wasiwasi mwingi , kwani ni takribani masaa nane tokea mheshimiwa aingie ndani ya chumba ambacho hakuelewa ndani ya ke ni kitu gani kilikuwa kikifanyika , ubaya ni kwamba hakuweza kutoka mahali alipo kwani alikiuwa amewekewa ulinzi , wasiwasi wake ulikuwa juu japo ya wahusika wa jumba hilo kumhakikishia usalama wa mheshimiwa Jembe ,, lakini yeye kama mwanausalama hakuweza kuwa katika hali ya utulivu , aliamini kama kuna jambo baya lolote likamtokea Raisi basi yeye moja kwa moja angewajibika na hakuelewa angewaeleza nini watanzania.

Lakini wasiwasi wake ulikuja kukoma mara baada ya kusubiri lisaa limoja mbeleni na hapo ndipo alipoweza kumuona mheshimiwa Jembe akitoka ndani ya chumba alichoingizwa akiwa na mavazi yake ya suti , lakini kwa bwana Tomasi aligundua jambo ambalo si la kawaida kutoka kwa mheshimiwa Jembe , hali ya furaha iliokuwa imetanda kwenye uso wake.

“kila kitu kipo sawa Tomasi huna haja ya kuwa na wasiwasi Zaidi” Aliongea mheshimiwa na Tomasi alipiga Saluti kuonyesha kwamba anakubali kile mheshimiwa alichokuwa anasema .

Basi kwa kutumia njia ile ile mheshimiwa aliweza kurudi Wing 8 House lakini akionekana kuwaza jambo .

“Sikuwa na jinsi ilinibidi kueleza kila kitu juu ya Mzalendo , hatuwezi kushindana na hawa watu kamwe njia moja ya mimi kuliongoza taifa la Tanzania ni kula sahani moja na hawa watu ” Aliongea mheshimiwa wakati akiwa anaingia ndani ya Wing 8 na kupokelewa na kikosi chake cha usalama ambacho muda wote kilikuwa kipo katika hali ya wasiwasi juu ya usalama wa Mheshimiwa.

“Hongera sana mheshimiwa kwa hatua yako ya mwisho”

“Nashukuru sana Hellen”

“Kesho ni siku yako ya mwisho ya ukaribisho ndani ya U-97 lakini pia ndio siku utapata fursa ya kuzungumza na wafanyabiashara wakubwa ambao kama mazungumzo yako yataenda vyema ni fursa kwa watanzania wote” Aliongea Hellen na Jembe alikubaliana nae na baada ya hapo aliaga na kuondoka

*****

Upande mwingine nchini Tanzania masaa machache mara baada ya kukamilika kwa hatua ya mwisho ya Raisi jembe ndani ya Tanzania , ndani ya ofisi ya mkuu wa kitengo cha usalama wa Taifa bwana Nassoro Kinga alipokea ujumbe wa maandishi kutoka kwa namba ambayo hakuweza kuifahamu ujumbe huo ulikuwa ukisomeka ‘MZALENDO BASE AT KURASINI

NLT TOWER GROUND FLOOR ,Damiani Rabani , Janeth Bendera , Linda ….’

Meseji hii ilimsisimua sana mheshimiwa na hakutaka kusubiri , dakika hio hio aliinua simu na kumpigia Kent na kumueleza ujumbe huo , lakini jibu kutoka kwa Kent lilimfanya atabasamu kwani hisia zake zilikuwa ni kweli na hii ni mara baada ya Kent kumwambia Nasoro kuwa andae operesheni ya dharula ya kuvamia jingo la NLT sehemu ambayo walikuwa wakijua kuwa ndio makao makuu ya kambi ya Mzalendo .

Baada ya Kinga kuweka simu yake chini hakutaka kuchelewa hata kwa dakika , kwani alinyanyua simu yake na kutoa maagizo na ndani ya dakika moja tu bwana mmoja aliejazia mwili aliingia ndani ya jengo hilo , huyu hakuwa mwingine bali alikuwa ni Mr White .

“kuna operesheni ya dharula inatakiwa kufanyika usiku wa leo”

“Misheni gsani hio mheshimiwa ?”

“Tumepata eneo la maficho ya kambi ya Mzalendo hivyo nataka usiku wa leo tukavamie hio kambi , lakini kabla ya hilo kufanyika nataka watu hawa wafuatao tujue mahali walipo”Aliongea Kinga na kutoa kumtajia majina Mr White , yalikuwa ni jumla ya majina kumi na mbili ya ajenti wote wa Mzalendo.

“Mishenni hii inatakiwa kufanyika kwa weledi wa hali ya juu sana , sitaki makossa , watu tunaoenda kupambana nao ni watu makini hivyo lazima na sisi tuwe makini , watu hawa sitaki akosekane mtu hata mmoja , unda timu ambayo itavamia usiku Kurasini na unda timu nyingine itakayowafatilia mahali walipo hawa wanaojiiita wazalendo wa nchi hii “ Aliongea mheshimiwa Kinga na kisha Mr white aliondoka kwa ajili ya kupanga timu yake kuipeleka kwenye mapambano..

Ndani ya masaa kadhaa tu tokea Mr white apewe jukumu la kuunda timu kwa ajili ya kufatilia wanamzalendo , alikuwa akitoa taarifa kwa mheshimiwa Kinga juu ya hatua ambayo wamepiga .

“Tumeweza kujua jumla ya ajenti saba walipo kwa muda huu na vijana wapo wanawafatilia kwa kila hatua, walioweza kupatikana ni Janeth bendera , Linda ,Zakayo ,Kassimu ,Sabi Mboneche………”Aliongea ajenti Nyuu au Mister White.

“Hawa wengine wako wapi ?”

“Mkuu kuna uwezakano hawa kuwa katika kambi yao”

“Huo ni uwezekano tu Bakari ninachotaka ni uhakika kama kweli wapo kwenye kambi yao , hususani huyu Damiani Rabani , ndio mtu muhimu sana kwenye hiki kitengo na ni lazima tujue ni wapi alipo kwani kossa la kumpoteza huyu ni kwamba misheni yetu imefeli”.

“Ndio mheshimiwa ngoja tuendelee kufalitilia mahali walipo kabla ya muda wa operesheni kufika “ aliongea ajenti nyuu au Mr White na kisha aliondoka , akimuacha bwana Kinga katika mawazo mawazo ya hapa na pale , lakini muda mfupi baada ya kutoka kwa Mister White Kinga alipokea simu kutoka kwa Kent .

“Operesheni imefikia wapi ?” ilisikika upande wa pili .

“Ajenti saba wapo katika macbo yetu , wengine watano hatujui walipo akiwemo Damiani Rabani , tunakisia wanaweza wakawa ndani ya kambi yao”Aliongea Kinga .

“Piga bomu hio kambi , sambaratisha kila kitu na kuhusu hao wengine waliopatikana hakikisha mnawakama wakiwa hai”Aliongea Kent na kisha simu ilikatwa .

Jambo hili kidogo lilimuacha Kinga katika mshangao lakini hakuwa na jinsi , alikuwa yupo tayari kufata maelekezo ya Kent ya kupiga bomu kiwanda cha NLT Kurasini , baada ya kufikiria kwa dakika kama mbili , alitoka na moja kwa moja alienda mpaka chumba cha ufatiliaji wa operesheni hio .

“wapi mmefikia ?”

“Janeth bendera anaonekana kuelekea upande wa Kurasini , vijana wapo kazini wanaendelea kumfatilia , nadhani hili litakuwa jambo jema tukivamia akiwa ndani ya kambi “ aliongea Bakari”

“Vipi kuhusu wengine sita ?”

“Tupo nao macho na wanaonekana kutoondoka katika maeneo ambayo wameonekena “ “Operesheni ya leo usiku ni kupiga bomu katika kambi yao , haitajarisha ni nani yupo ndani ya kambi ninachotaka kambi hio ndani ya masaa sita yajayo pawe vumbi tu ndio linaloonekana”Aliongea mheshimiwa Kinga na kufanya watu wote washangae . “Uko siriasi mheshimiwa, hilo jambo ni hatari sana kwani wengine ambao hawahusiki wanaweza kupata madhara , na isitoshe tunawezo wa kuingia ndani ya kambi hio na kuwakamata wahusika bila kufanya uharibifu mkubwa”

“Bakari maamuzi yangu ni hayo na yanatoka moja kwa moja kutoka kwa mheshimiwa Raisi , hivyo saa tatu kamili ya usiku nataka kiwanda cha NLT kiwe vumbi , andaa vijana kwa hio misheni” Ajenti nyuu alijikuta akishangazwa sana na maamuzi hayo , lakini hakuwa na kupinga kwani mkuu wake wa kazi alikuwa ashaafanya maamuzi na ni moja ya jukumu lake kufata maamuzi ya mkuu wake .

“Ni shambuilio la bomu la aina gani linapaswa kutumika?”

“Tutatumia shambulio la Anga”

******

Captain Juma hizza alikuwa ndio kwanza anaingia nyumbani kwake Tegeta muda wa saa kumi na mbili za jioni , kwake hiio ndio muda wake wa siku zote wa kufika nyumbani akitokea kazini , na bwana huyu alikuwa ni moja ya watu ambao walikuwa wakipenda sana kurudi nyumbani mapema na kuiona familia yake , hii ni tabia ambayo alikuwa amejijengea lakini pia ni tabia ambayo ilimpa heshima kubwa sana kwa majirani zake .

Kwani ni tabia ya kawaida sana na iliozoeleka kwa baadhi ya wababa wafamilia kuchelewa kurudi nyumbani baada ya kazi , kwani wao mara baada ya kazi walipitia sehemu mbali mbali wanazozijua wao kwa ajili tu ya kupoteza muda ili wasirudi nyumbani mapema .

Jambo hili lilikuwa tofauti kwa Juma kwani yeye alikuwa akiwahi sana kurudi nyumbani , basi baada ya kulakiwa na watoto wake wawili Salma na Hamisa aliingia chumbani na kujimwagia maji ili kuondoa uchomvu , lakini wakati anaendelea kuoga mara mke wake aliita akimtaarifu kwamba simu yake ilikuwa ikiita na jina la mpigaji lilikuwa ni bossi .

Baada ya kusikia jina hilo alitoka na kuchukua simu hio na kupokea kwani aliamini sio kawaida kwa bossi wake kumpiigia kwa wakati huo tena mara baada ya kurudi kazini .

Baada ya kuweka simu sikioni ndani dakika chache aliweza kupata maelekezo ya kurudi kazini kuna opetesheni ya dharula ambayo alikuwa akipaswa kuifanya usiku huo , huku akielekezwa na mkuu wake huyo wa kazi kwamba eneo husika atapewa akiwa angani.

Juma hizza alikuwa ni moja ya marubani wa ndege za kijeshi waliokuwa wakiaminiwa sana na kitengo cha dharula cha jeshi cha maswala ya makombora ya kurushwa kwa Anga , licha ya kufanya kwake kazi miaka mingi hakuweza kuutumia usomi wake katika kurusha ndege na kwenda kushambulia eneo , kwani ndani ya taifa letu kulikuwa na Amani kubwa sana kiasi kwamba ni mara chache sana ndege za kivita zilikuwa zikitumika .

Sasa siku hio mara baada ya kupokea taarifa hio ya kutumia ndege yake kwa ajili ya kwenda kushambulia ni kama walimpa mzuka kabisa , kwani jambo alilokuwa akilitaka siku zote ni hilo litokee ili aweze kuonyesha manjonjo yake .

Lisaa limoja mara baada ya kupewa maelekezo alikuwa ndani ya ndege yake kubwa ya kivita iliokuwa ikifahamika kwa jina la Bird killer ndege iliokuwa imetengenezwa nchini Urusi , ndege hio iilikuwa na uwezo wa kubeba mabomu yasiooungua mia moja na kushambulia kwa umbali mrefu kutoka angali bila kukosa Target.

Saa mbili na nusu za usiku Captain juma hiza alikuwa akielea angani akiwa na shauku kama zote za kufanya shambulio katika eneo ambalo wakubwa wake walimuelekeza kumtumia ‘cordinates’

“Ndani ya dakika kumi na tano tu za kuwa angani hatimae aliweza kupokea uelekeo husika wa Terget yake anayopaswa kwenda kufanya shambulio .

“Target locked . need permission to engage” aliongea Juma akiomba ruhusa ya kuachia kombora kwani tageti alikuwa ashaipata .

“ umeruhusiwa” mIlikuwa ni neno dogo lakini lililoleta madhara makubwa sana , kwani ndani ya sekunde kadhaa ndani ya eneo lote la Kurasini lilikuwa halitamaniki , lakini si hivyo tu , wakazi waliokuwa kuwa maeneo ya karibu na eneo hilo walikuwa katika taharuki kubwa kwani ni jambo ambalo hawakuwahi kulishuhudia kwenye maisha yao ukilinganisha na historia ya taifa la Tanzania kutokuwa na matukio ya ajabu kama hayo ..

SURA YA 13

Linda mara baada ya Damiani kuelekea nchini Australia alijikuta akipendana na kijana wa kipemba aliekuwa akijulikana kwa jila la Hamadi , kwa mara ya kwanza ya Linda kukutana na Hamadi ilikuwa ni siku aliokuwa mapumzikoni ndani ya kisiwa cha Unguja ndipo alipoweza kuonana na mfanya biashara Hamadi na kwanzia siku hio ya kukutana waltokea kupendana sana kwa muda wa siku chache walizodumu pamoja .

Siku ambayo mheshimiwa Jembe anaelekea nchini Marekani ni siku ambayo Linda akiwa ndani ya kambi ya Mzalendo aliweza kuwekeana ahadi na Hamadi kuonana siku mbili mbele kwani Hamadi alikuwa akija bara akitokea Dubai alipokuwa bize kibiashara , jambo hili kwa Linda lilimpa munkari sana ukijumlisha na namna ambavyo alikuwa amemmiss Hamadi , alijua fika kazi yake haikuwa ikimruhusu kupenda , lakini kwa kijana Hamadi alikuwa ameloea kwani kijana huyo alikuwa akijua kumdekeza mno Linda kiasi cha kumchanganya sana .

Siku mbili mbele kama walivyo ahidiana , hatimae Hamadi alifika nchini na kumtaarifu Linda kwamba yupo hoteli ya Golden Tulip katikati ya jiji la Dar es salaam , Muda ambao Linda anawasiliana na Hamadi alikuwa ndani ya kambi ya Mzalendo na ilikuwa ni muda wa saa saba na nusu kwenda nane wakati wakiwa wanawasiliana na walipanga saa kumi na moja za jioni Linda atafika hotelini hapo .

Siku hii ndani ya kambi hii walikuwemo jumla ya watu watatu waliokuwa zamu katika kuhakikisha kila mipango inaenda sawa , yaani Linda alikuwa na wenzake wawili ambao wote kwa ujumla wao walikuwa wakihusika na maswala ya kitehama ndani ya kambi hii ya Mzalendo.

Ilipotimu muda wa saa kumi na robo Liuda aliwaacha wenzake wakiendelea na majukumu na yeye alitoka kwa ajili ya kwenda kuonana na mpenzi wake Hamadi, mwanadada Linda alikuwa akiendesha gari aina ya Toyota Crown nyeupe na ni gari ambayo alikuwa akiipenda sana kutembelea nayo licha ya kwamba alikuwa na gari nyingine aina ya BMW lakini gari hio ya kijapani ndio moja ya gari alizokuwa akipendelea sana kutembelea .

Kuna jambo ambalo lilimtia wasiwasi , na hio ni mara baada ya kuingia ndani ya maegesho ya magari ndani ya hoeli ya Golden Tulip , kwani kuna gari aliitilia mashaka , kwani tokea anatoka Kurasini gari hio ni kama ilikuwa nyuma yake , japo mwanzoni hakuwa akiitilia mashaka , lakini kitendo cha kuegesha gari yake ndani ya hoteli hio na kuiona lile gari swala hilo lilimpa mashaka kidogo lakini hakuwa akitaka kulifatilia sana , kiufupi alipotezea swala hilo na kuendelea na mambo yake na hilo kwake lilikuwa ni kosa kubwa sana ambalo amelifanya.

Baada ya kuingia mapokezi aliweza kuwasiliana na chumba ambacho alikuwepo mwanaume wake aliekuwa akimpenda na baada ya kuruhusiwa moja kwa moja alielekea huko , na kitendo cha kutoka tu mapokezi , waliingia wanaume wawili waliovalia kikawaida na moja kwa moja walielekea mapokezi na walitoa vitambulisho vyao vya kazi na kumuonesha mwanadada wa mapokezi na yeye baada ya kuwatambua watu hao ni wakina nani alitoa ushirikiano wa kutosha

Baada ya swala lile kuisha pale mapokezi mwanaume mmoja aliekuwa amevalia tisheri nyekundu ya Form six alibakia eneo la mapokezi na yule mwingine aliingia kwenye Lift .

Huku upande wa linda baada tu ya kuingia chumba alichokuwa Hamadi walirukiana na kupeana mabusu na kunyonyaka mfululizo jambo ambalo liliwapandisha sana hisia zao za kufanya mapenzi na ndani ya dakika chache tu walikuwa wote wapo kama walivyozaliwa na kijana Hamadi alionekana vyema katika kuumiliki mwili wa mpenzi wake Linda .

Hata pale simu ya Linda ivyotoa mlio wa kuashiria kuna ujumbe wa meseji umeingia hakushughulika nayo.

Nusu saa za purukushani mlango wao uligongwa na aliekwenda kufungua alikuwa ni Hamadi , lakini ile anafungua alijikuta akikutana na mwanaume ambae alikuwa katika uso wa kazi huku akiwa amemnyooshea bastora kitendo kile kilimfanya Hamadi atetemeke sana na hilo kwa Linda lilionekana mara moja lakini ni kama alichelewa kwani mwanaume yule alikuwa ashamtumia Hamadi kama kinga yake huku akimwamuru Linda asilete ubishi kwani akifanya jambo lolote la kijinga mwanaume huyo atapasuliwa ubongo .

Linda aliekuwa amejifunika na Shuka alijifikiria kwa muda na kisha aliinuka alipokuwa amekaa na kumsogelea mwanaume yule huku akipewa tahadhari za kutosegea hata hatua moja , lakini ni kama Linda hakujali hilo kwani alizidi kusogea licha ya mwanuaume yule kutishia kumpiga lisasi Hamadi .

Ilikuwa ni kitendo cha dakika chache , Hamadi alikuwa chini akiwa amepigwa risasi na mwanaume yule , lakini upande wa yule mwanaume alikuwa akiangalia bastora yake iliokuwa imedodokea mbali mara baada ya kupigwa teke na Linda .

Mwanaume yule alionekana kuwa akijiamini sana kwa mapigano , lakini kwa Lnda pia alichokuwa akiamini katika maisha yake ni kwamba katika taifa la Tanzania ukimtoa Damiani hakuna mtu mwingine ambae anaweza kumpiga na kumuangusha, hivyo hakuwa na presha hata kidogo , kwani ile mwanume yule analeta pigo za haraka za ngumi upande wa Linda alizipangua kama hana adabu nzuri huku akiendelea kumsoma adui yake , na alipoona adui yake kimafunzo alikuwa ni wa kawaida sana , alimpatia kile alichokuwa anataka , kwani kwa s spidi ya hali ya juu alirusha teke moja na mguu wa kushoto lisilo na nguvu lakini lililoonekana na adui yake na adui yake akataka kulipangua na hilo ndio likawa kosa kwani kama panya alimrukia na kwenda kutua shingoni mwa mwanaume yule huku papuchi yake ikigusana na macho ya yule mwanaume , lakini hakupewa hata mwanya wa kuangalia madini yaliokuwa ndani ya mgodi kwani aligongwa utosini na kisha alilegea na kushuka na Linda mpaka chini.

Linda alichukua simu yake na kisha aliangalia ujumbe uliokuwa humo na kujikuta akitoa tusi ni kama mtu aliekuwa akijitukana kwa kutoangalia huo ujumbe na baada ya kuona hivyo alivaa haraka haraka, alimwangalia Hamadi aliekuwa amelala sakafuni damu zikiwa zimetapakaa , alijilaumu kwa kujiingiza katika mapenzi nae kwani yote hayo yasingemtokea ,, aliinamna huku akionekana mwenye huzuni na kumfumba macho yake na kisha alitoka ndani ya chumba hicho na kutokomea .

Yule bwana aliekuwa ameachwa Mapokezi alijikuta akishaangaa kumuona Linda akitokezea na hapo hapo alitoa simu yake kumtafuta mwenzake , na hakupata majibu na hakutaka kuendelea kubaki pale alidhamiria kupanda juu kumtafuta mwenzake.

Lakini alichoweza kukutana nacho mara baada ya kufika ndani ya chumba alichokuwa Linda kilikuwa ni cha kuogopesha .

Alitoka mbio mbio ili kumuwahi Linda lakini alikuwa amekwisha kuchelewa kwani ajenti linda alikuwa ashatokomea kusiko julikana .

****

Saa kumi kamili za jioni wakati Linda akifikiria kwenda kuonana na mpenzi wake , upande wa huku Makongo juu mwanadada Janeth alikuwa amekaa amejipunzisha huku akifikiria hili na lile katika swala zima la kazi aliokuwa anaifanya , jambo moja ambalo lilikuwa likimuumiza kwa wakati huo ni juu ya Damiani , kwani alijua kwa namna yoyoe ile ni lazima mwanaume huyo alikuwa ashazini na mwanamama Rania , na kwake hilo lilimchanganya sana kila akikumbuka nyakati tofauti alizokiwa akipewa mapenzi na Damiani na kulinganisha na muda huo mwanamke mwenzake akipewa tamu aliokuwa akililia kila siku alijikuta roho ikimuuma kwani alikuwa akimpenda sana Damiani. .

Wakati akiendelea kuwaza juu ya hatima ya mapenzi yake simu yake iliingia ujumbe wa maandishi , na alifungua simu yake ili kuusoma huo ujumbe na hapo ndipo alipokutana na neno kidogo lililomchanganya , lakini neno hili lililokuwa katika ujumbe wa meseji ulitokea kwa jina lililokuwa limeseviwa kama SHUSHU. Yalikuwa ni maneno mawili tu yaliosomea PSYOPS to Jembe

Kwanza alishangazwa na nenp hilo , na alitumia dakika kadhaa kung`amua maana ya neno hilo kwanini litumwe kwenye simu yake , na mara baada ya kukumbuka kuwa mheshimiwa Jembe yupo nje ya nchi kwa ajili ya kula kiapo,alijikuka akitoa tusi baada ya kukumbuka kuwa neno hilo linamaana ya psychologival Operations , na ni mbinu ambayo jeshini hutumika mara nyingi kwa adui ambae wahusika wanataka kupata taatifa kutoka kwake ,na mara kama mbinu hii itatumika kwa mtu basi ni Dhahiri kwamba atamwaga siri zotemkama tu hautakuwa na mafunzo maalumu ..

Kitendo cha kudaka maana ya hilo neno aliamini kwamba kama mheshimiwa Jemebe ataweza kufanyiwa hilo jambo basi ni Dhahiri kwamba amekwisha kutoa siri ya juu ya mahali kambi yao ilipo na si hilo tu lakini pia atakuwa amewataja ajenti wote wa Mzalando na hilo lingewaweka katika hali ya hatari.

Baada ya kugundua uhatari wa swala hilo mara moja alituma ujumbe wa maandishi kwa ajenti wote kukutana mahali ambapo aliwaelekeza haraka sana hususani wale ambao mheshimiwa Jembe alikuwa akiwajua , huku akisisitiza wote walio katika kambi kutoka haraka..

Hivyo Janeth hakutaka kubakia hapo ndani alitaka kuhakikisha ajenti wote wa Mzalando hakuna hata mmoja anaekutwa na madhira ya kuingia kwenye mikono nya U-97 , alitoka haraka na kuingia kwenye gari yake kuelekea kurasini , wakati akiwa yupo bagamayo road kuna hisia zilizokuwz ikimwambia kuwa alikuwa akifatiliwa na jambo hilo alikuja kulithibirisha alivyokuwa Mwenge , lakini swala hilo halikumpa shida. Aliendelea kuendesha gari mpaka alivyokuja kuwachenga wale waliokuwa wakimfatilia na ndani ya muda mfupi alikuwa ndani ya jingo la NLT .

Baada tu ya kuingia ndani ya ‘basement’ aliwatoa wataalamu wawili ambao walikuwa wakihangaika na tarakishi zao kwamba waondoke kwani mahali hapo si salama tena .

Ndani ya dakika kadhaa kila kitu kilikuwa kwenye mkao na Janeth alikuwa ashachukua tahadhari zote na kutoka ndani ya ‘basement’ hio na kwenda kwa Rebeca ambaye alikuwa ndio mkuu wa usimamizi wa maswala ya kiwanda na kumpa maelekezo kwamba kiwanda hiko kifungwe mapema kabla ya saa kumi na mbili.

Baada ya Janeth kutoa maelekezo hayo aliingia kwenye ofisi yake na kisha alivuta begi lililokuwa lipo kwenye kabati na akavua nguo zake zote na kisha alisimama kwenye begi hilo na ndani nya sekunde chache tu alikuwa si Janeth tena , alikuwa ni mwanamke mweupe wa taifa la Korea , alijiangalia kwenye kiooo na kisha alitabasamu na kutoka na kuingia kwenye gari nyinginie tofauti na ile aliokuja nayo.

Baada ya kuingia kwenye gari alitoka hapo ndani huku akipishana na gari ile iliokuwa ikimfatilia , alitabasamu na kisha aliondoka .eneo hilo na ndani ya nusu saa alikuwa akipita Bunju kuelekea upande wa bagamoyo .

Dakika aribaini na tano mbele alikuwa eneo la Kiwangwa kwa mbele kabisa kulikuwa na shamba la katani , alikunja na kuchukua njia ya vumbi na kutembea umbali wa mita kadhaa na kufikia kwenye jumba moja la gorofa tatu lililokuwa limezungushiwa ukuta na mahali hapo kukiwa na baadhi ya nyumba kadhaa za watu waliokuwa wakiishi pembezoni , baada ya kuingiza gari alipaki na mtu aliekutana nae alikuwa ni Sabi mboneche .

"Vipi mmeweza kufika wote sabi?”

“ Hapana miss Janeth tupo wanne ambao tumefika hapa , shukrani kwa ujumbe wako tumeweza kutokukamatwa” aliongea Sabi huku wakiingia ndani na ndani ya dakika chache na Linda nae aliweza kufika ndani ya eneo hilo huku akifatiwa na wengine waliokuja kwa kupishana kwa muda kidogo.

Dakika kama kumi na tano ajenti wote kumi na mbili wa kambi ya mzalaneo walikuwandani ya kambi yao nyingine ndani ya eneo la Kiwangwa , hii sehemu hakuna ajenti aliekuwa akifahamu uwepo wake Zaidi ya Damiani na Janeth. .

Kwa nje ilionekana kama nyumba ya kawaida ya kuishi watu wenye maisha ya juu lakini chini ya nyumba hio kulikuwa na kila kitu tena Zaidi ya vitu vilivyokuwa ndani ya ‘basement’ ya Mzalendo kurasini lakini hii ikiwa ni ya kisasa Zaidi. .

Kila mmoja alishangaa baada ya kuoneshwa eneo hilo .

“Mimi na Damiani tulikuwa tukijua kuna siku jambo kama hili litatokea na ndio maana kambi hii iliweza kujengwa na kuanzia leo tunahamishia makao yetu yote mahali hapa ” Aliongea Janeth na kumfanya linda aliekuwa katika hali ya hudhuni kutabasamu , jambo ambalo hata Janeth lilimshangaza kwani hakumzoea Linda kwa hali aliokuwa nayo .

Baaada ya masaa kadhaa yaani saa mbili kamili za usiku , ajenti hawa walikuwa wapo bize kuangalia kama ni kweli kambi yao ilikuwa imegundulika , kwanni licha ya kwamba waliweza kufika mahali hapo , lakini walikuwa hawana uhakika asilimia mia moja kwamba eneo lao la mwanzo limegundulika , katika kufatilia ndipo muda wa saa tatu walipoweza kushuhudia kitu ambacho kiliwafanya kila mmoja azibe mdomo , kwani eneo lote la kiwanda chao lilibakia wingi zito mara baada ya kushuhudia ndege ikiachia bomu .

Hakuna alieweza kuamini kwamba watu hao wangeweza kuchukua hatua ya namna hio , walijikuta wakiongopa kwa wakati mmoja kwa tukio hilo .

“Shit , hii ni lazima tulipe” Aliongea Janeth kwa hasira huku akipiga ngumi kwenye meza .
TUTAENDELEA , RATIBA NI VIPANDE VIWILI KWA SIKU
MAWASILIANO NI WHATSAPP TU TUMA MESEJI 0687151346
Hatar sana
 

SURA YA 07.

Jambo la kwanza lililonivutia mara baada ya macho yangu kugonga juu ya mwili huu wa huyu mwanadada ,ni rangi yake , alionekana kuwa ni mwanamke kutoka bara la Afrika bila shaka , alikuwa mrefu saizi ya kati , mwenye rangi nyeupe iliofifia lakini inayovutia , sura yake ilikuwa ni ya kuchongoka , akiwa na nywele ambazo kwa kule nyumbani tunaweza kuiziita za kishombe shombe ndefu zilizomfika mabegani , jambo kubwa lililonivutia zaidi juu ya huyu mwanamke ni Shepu yake, alikuwa na umbo namba nane ambalo lilikuwa ni ugonjwa kwa wanaume wakitanzania wengi bila kunitoa kundini .

Mwanadada huyu alikuwa ametangulizana na kijana wa makamo kati ya miaa 28 hivi, alikuwa ni mzungu na ni kama kuna jambo kijana huyu alikuwa akumuelewesha huyu mwanadada mara baada ya kuingia ndani ya mgahawa huu , muda wote huu nilikuwa nikiwachora tu , huku pepo langu la kimatamanio likiwa juu .

Sura yake kwanza huyu mwanadada ilikuwa ikija na kupotea jambo ambalo niliona ni uchuro , kwani nilikuwa na njia nyingi za kumtambua mtu kwa njia ya DREAMER T.

Kwa wale msiofahamu DREAMER T ni mtandao wa kijasusi unaoendeshwa na serikali ya China wenye taarifa ya kila mtu duniani , mtandao huu uligunduliwa na rafiki yangu Luang Shu ambaye ni mtoto wa Raisi wa China.

Moja ya sababu zilizonifanya kufahamiana na Luang Shu ni koneksheni ambayo ilijengwa na Marehemu Raisi Bendera , moja ya maraisi wangu bora waliowahi kuliongoza taifa la Tanzania , raisi John bendera alikuwa ni wale maraisi ambao walikuwa wakifikiria maslahi ya taifa kulivko wanavyojifikiria yeye mwenyewe.

Na kuthibithisha hilo yeye yupo peponi mimi nipo hapa nchini Australia nikiendelea kufanya kazi ambayo hakuimaliza , kazi ambayo haimfaiidishi yoyote , Zaidi ya faida zote kwenda kwa Taifa .

Basi nilitoa miwani yangu ya kijasusi iliokuwa na teknolojia ya hali ya juu sana , miwani ambayo inavaliwa na ajenti wa Mzalendo pekee , na hio ni kwamba alieitengeneza ni mzalendo mwenzetu .

Basi baada ya kutoa miwani hii nilitoa simu yangu yenye chata la M(yaani mzalendo) ilikuwa ni simu mahususi kwa ajili ya kazi yangu na pia ilikuwa ikitumiwa na sisi wazalendo pekee , Nilivaa miwani ile na kunifaya nipendeze Zaidi na kisha baada ya kuivaa nilugusa ‘Icon’ moja kwenye simu yangu na kisha kukatokea maandishi ‘M smart device connected with AI SUPER GLASS’.

Baada ya kuona sasa simu yangu imeunganishwa na miwani nilimuacha huyu mrembo aniangalie na kisha nikampiga picha , yaani miwani ilikuwa ni kama Camera , baada ya kupiga picha ile niliipandisha(Upload) kwenye DREAMER T na kuomba kumtambua mtu huyo , na ndani ya sekunde mbili tu nilikuwa na maelezo yote .

“Bingo!!” Alikuwa ni Rania Samir mmiliki wa hii hoteli ya kifahari , sasa hapa niliona njia pekee ya kuwapata The Truth ni kupitia huyu mwanamama , ndio nimebadilisha jina kutoka mwanadada kwenda mwanamama ,kwani ana mtoto ambae ndio huyu anaemiliki kikundi hiki cha The truth , lakini si mwanamama tu hawa tunawaita kwa kimombo ‘Milf’ yaani mwanamke aliezaa lakini hajapoteza mvuto.

Sasa picha ya mpango ambao niliona utarahisisha kazi yangu , ni kuzoeana na huyu mwanamke japo niliamini ni mwanamke matawi ya juu lakini pia akionekana kuwa mkubwa kwangu kwani alikuwa amenizidi kama miaka minne lakini sikuwazia juu ya hilo kwani ni jambo ambalo pia tuna mafunzo .

Niliwaza namna ya kuanzisha ukaribu na mwanamama huyu , na hapo hapo nilipata picha la kihindi ambalo lilinifanya nitabasamu , sikuwa na haraka juu ya mpango wangu huo , basi niliendelea kula chakula changu kwa mbwembwe zote huku nikiendelea kumchora mwanamama huyu ambae kwa haraka haraka niligundua alikuwa akikagua hilo eneo , alifika mpaka upande wangu na kisha baada ya kuniona nikiwa kwenye rangi yangu ya kitanzania alitabasamu na mimi nikamrudishia tabasamu na kisha aliondoka .

Baada ya kuona ameondoka haraka haraka nilifanya mawasiliano na Janeth nikimuomba aniunganishe na simu yangu nipate kujua mwanamama huyu kila eneo atakalokuwepo na ndani ya dakika chache tu kwa kutumia ‘Face recognition system’ nilikuwa namuona mwanamama huyu akiwa bado yupo ndani ya hii hoteli.

Baada ya kuona zoezi hilo limefanikiwa niliona sina haja ya kuwa ndani ya hilo eneo la mgahawani , nilinyanyuka baada ya kulipa kwa kadi yangu ya benki na kisha nilirejea kwenye chumba changu kupumzika , nilijitupa kitandani huku nikiendelea kuangalia simu yangu kuuona ni eneo gani Rania yupo, lakini niliona bado yupo ndani ya eneo hili la hoteli,sikuona haja ya kuendelea kumfuatilia niliamua zangu kupiga usingizi kwani wakati huo ilikuwa ni saa nne hivi na madakika.

Asubuhi kulivyokucha jambo la kwanza kuangalia ni simu , kuona huyu mwanamama yuko upande gani na niliona bado yupo ndani ya hoteli hii , jambo ambalo lilinipa jibu kwamba huenda kalala ndani ya hoteli hio .

Basi nilioga vizuri baada ya kumaliza nilivuta begi langu dogo la nguo na kisha nilizimwaga nguo zote kwenye kitanda , na baada ya hapo nilitoa kitu kama kichwa cha chajio ya simu na kuchomeka kwenye swichi(switch) ya umeme , na kisha nilitupa taulo pembeni na kubakia uchi , kisha niingiza miguu ndani ya begi lile na kusimama , na ndani ya sekunde chache tu nilikua nimebadilika na kuwa Stephano Lamberk, najua wengi hawanijui ukitaka kujua vyema kuhusu hili jina uwe umesoma kitabu cha waraka wa raisi kabla ya kifo.

Nilikuwa ndani ya FBM nikiwa nimebadilika kabisa kimuonekano, na kuwa mzungu kamili yaani huwezi kujua kwamba nimevaa mask .

Stephano Lamberk ni jina nililopata ndani ya Taifa la uchina , na ndio jina ambalo nilikuwa nikitambulika nalo kama moja ya wanabodi wa kurugenzi ya kampuni ya Huwaei , kama utagoogle jina langu utaweza kunisoma nikiwa moja ya matajri wakubwa ndani ya Afrika wenye umri mdogo .

Jamani hayo sio maigizo ni kweli kabisa nina pesa ndefu ,unaweza ukanijua kama Damiani lakini pia nafahamika kama Stephano Lamberk kijana mwenye pesa kutokea Taifa la Tanzania , na mara nyingi huwa nikihudhuria mikutano yote inayohusu biashara zangu huwa natumia jina na sura ya Stephano Lamberk .

Basi baada ya kuwa kwenye muonekano mwingine , nilivaa suti yangu nadhifu kabisa ambayo ilinikaa vyema , na muonekano wangu wa kihandsome , ni Dhahiri mwanamke yoyote ambae anapenda wanaume wenye mvuto atavutiwa na mimi , usishangae kuna wanawake hawanaga

‘standard`s’ yaani hawajali mwanaume anaetoka nae ilimradi awe na pesa , hawa hawajali mvuto , sasa mimi pesa ninayo , halafu mvuto ni nao yaani ni swala la plus plus kumvutia mwanamke .

Niliangalia simu na kuona bado Milf wangu yupo ndani ya hoteli , hivyo nilitoka , huku nikiwa na nia kwanza ya kwenda kupata kifungua kinywa , swala la pili niliwaza namna ya kukutana na mrembo Rania.

Nilipata kifungua kinywa ndani ya sehemu ile ile ya jana , pasipo kumuona Rania ,lakini sikuwaza sana kwani alionekana kwenye simu , basi baada ya kumaliza nilifika mapokezi na kuulizia kuhusu kwenda eneo la peace lounge .

Ndani ya hii hoteli kulikuwa na hii huduma kwa mtu ambae anataka kutuliza mawazo , yaani kama unamistress yako huko ya maisha au mapenzi basi ukienda hili eneo akili yako inatulia tuli na kufurahia maisha , hii huduma pia inapatikana ndani ya kisiwa cha Ilbiza huko Spain.

Nyie hii sehemu kweli ilikuwa ni kwa ajili ya kutuliza mawazo , bwana bwana , ilikuwa na muonekano flani hivi wa kipekee sana yaani kuna muda ndani ya hili eneo linabadilika linakuwa kama mbuga ya wanyama , lakini pia kuna muda hili eneo linabadilika linakuwa kama upo chini ya bahari , yaani kila aina ya kitu cha kushanganza na kuchangamsha ubongo kilikuwepo , ilikuwa ni kama upo ndani ya Chupa kubwa sana ukiwa umezungukwa na vioo.

Ni sehemu ambayo haikuwa na watu wengi , nadhani ni kutokana na muda ambao niliingia ndnai ya eneo hilo , kulikuwa na baadhi ya watu kulia kwangu wasiozidi kumi , lakini pia kushoto kwangu sehemu ambayo ilikuwa na swimming pool kulikuwa na watru wasiozidi watano , lakini mbele kabisa kwenye bustani kulikuwa na mtu, sio watu, sikuweza kumuona kwa upande ambao nilikuwa nimesimama ila niliambulia kuona kofia kubwa ya mviringo rangi nyeupe(Floppy hat) ikiwa inaonekana kwa nyuma ya kiti cha kuegamia , yaani mtu huyo alikuwa amenipa kichogo , basi niliona nichague mahali pa kwenda , na nikaona ni vyema nikienda mbele yangu kwani ni eneo ambalo halikuwa na watu wengi na mimi pia nilikuwa nikipenda maua .

Baada ya kusogea karibu kabisa yaani kushoto mwa mtu ambaye alikuwa ndani ya hili eneo , upande wa kushoto , moyo ulijikuta ukipiga paah! , kwani mtu ambae nilikuwa nikitamani kuonana nae, kumuona ndio aliekuwa eneo hilo, nilijikuta nikisimama nikimwangalia mwanamke huyu kwa uzuri aliokuwa nao , lakini pia pozi ambalo alikuwa ameweka ndani ya eneo hilo , niliendelea kumsaminisha pasipo yeye mwenyewe kutambua uwepo wangu , huku akiwa ameshikilia glass ya wine .

Baada ya kuona nimeridhika na sinema hio ya bure nilisogea upande wa kushoto wake kwenye kiti cha pembeni na kukaa.

“Mambo mrembo !!”Nilisalimia kwa lugha ya Kiswahili kabisa , na nilifanya hivyo makusudi kwani nilijua mwanamama huyu alishawahi kukaa Tanzania hivyo ni lazima atakuwa anaelewa lugha ya Kiswahili vyema , lakini pia hio ndio gia yangu niliopanga kuingia nayo kwa mwanamama huyu ili kujenga ukaribu .

Basi baada ya kumpa salamu hio aligeuza shingo akiwa kama ni mtu ambae alikuwa kwenye mshangao , na mimi niliupokea mshangao huo kwa Tabasamu.

“Haaa!!!.. Stephano”Kibao jamani kilinigeukia , kwani licha ya kujua kuwa mimi ni tajiri ila sikujua kwamba naaweza kufahamika na mrembo huyu , hivyo namimi ikawa zamu yangu kushangaa , lakini sikutaka kulionyesha hilo kwani nitakuwa nimeonesha udhaifu , nilitabasamu.

“Wow! , sijatarajia kuona mwanamke kama wewe unalifahamu jina langu hususani ukiwa ndani ya nchi ya mbali kama hii”.

“I know you, na nahisi pia unanifahamu kwani kitendo cha kunisalimia kwa Kiswahili pia kimenipa maswali”.

“Naweza kusema ndio au hapana kwa wakati mmoja”

“Kwanini hapana na ndio hakuna jibu hapo”Huku akitabasamu .

“Kwa sababu nina siku moja , saa na dakika chache tokea ni kukufahamu”.Alishangaa huku akionekana kuchangamka tofauti na nilivyomkuta na huo niliona ni ushindi namba moja . “So can you tell me , umenifahamu je within that short time and how ?”Hili swali mara nyingi mtu yoyote akikuuliza , yaani pale unapoita jina lake halafu akashangaa , na akakuuliza hili swali basi jua ana ‘trust issues’ shida ya kutokuamini watu , na kama ni mwanamke jua huenda alishawahi kusalitiwa na mtu anaempenda sana na sisi majasusi mara nyingi tunaangalia na ‘Complexion’ muonekano unaombatana na hili swali .

“ Mazingira na luxuries ndani ya hii hoteli ndio ilinifanya nikufahamu , I am businessman na nimeipenda sana hii hoteli” Mpaka hapo nilikuwa nimejibu maswali yote kwa mpigo, kwa wewe ambae hujawahi kuwa mfanya biashara huwezi kuelewa , na hapa nazungumzia wafanya biashara wale wakubwa,huwa kuna lugha ambazo wafanya biashara wakubwa wanatumia pindi wanapokuwa katika mazunguzo ya kuingia mkataba au dili Fulani, mara nyingi wanakuwa na maneno ya kimikato lakini yaliobeba Zaidi ya maana.

“Karibu sana kwenye hoteli yangu Stephano , I am so happy to meet you in person”.

“Na mimi pia nimefurahi kukutana na wewe mwanamke mzuri unaemiliki hoteli nzuri, lakini nina shauku ya kujua zadi how umenifahamu”.Alipoteza tabasamu jambo ambalo lilinichanganya kidogo .

“Ni hadithi ndefu , but its all about Erick my son”Sasa sehemu ambayo niliitala ndio hapo , niliona sasa kazi yangu inaenda kuwa rahisi , na nilipanga kutumia mbinu zote za kijasusi kumchimba huyu mwanamke , yaani nikitoka katika mazungumzo hayo niwe nimepata mwanga wa misheni yangu.

“Kumbe una mtoto! , vipi kuhusu Erick?”.

“Yess one and only , but I am so sad when I think about him” ndio ninae mtoto mmoja wa kipekee , lakini najikuta nikiwa kwenye huzuni pindi ninapomuwaza”Aliongea na mpaka hapo nilijua kuna jambo kubwa kumuhusu Erick, nilijikuta nikinyamaza kwani mwanamama huyu alionekana akianza kutokwa na machozi , jambo ambalo ndio mtihani mkubwa kwangu , yaani katika maisha yangu nilikuwa ninauwezo wa kumfanya mtu afurahi lakini siwezi kumfariji mtu sasa nashindwa kuelewa maneno yangu yana mantiki lakini ndio hivyo, ndio maana mara nyingi napenda kuongea na watu wenye furaha..

“Niambie Zaidi kuhusu Erick”Niliongea na wakati huu nilikuwa nishanyanyuka nilipokuwa nimeketi na kukaa kwa kupiga magoti pembeni ya kiti chake karibu na tumbo lake ,japo mwanamama huyu kuwa katika hali ya huzuni lakini , alikuwa akinivutia mno , yaani kivazi cha kizungu alichovaa kilifanya nitamani tendo.

“Amepotea, ni mwaka mmoja sasa”Nilijikuta nikishangaa, kwani mpaka hapo niliona kabisa kazi yangu inaanza kuwa ngumu wa kupata hiki kikundi cha The Truth.

“Pole sana, but kwanini kupotea kwa mwanao kuwe ni stori ndefu ya kunifahamu?”.

“Kama unao muda nataka nikuoneshe kitu , nadhani itakuwa rahisi kwa mimi kukuhadithia”Aliongea na nilikubaliana nae.

Basi mwanamke huyu alitangulia mbele akiniacha nyuma nikijilia kwa macho , dakika tatu mbele haatukuwa upande wa hoteli hii , tulikuwa eneo hilo hilo lakini j engo tofauti la pembeni lenye goorofa tatu kwenda juu .

“Hapa ni nyumbani kwangu Stephano , karibu sana”Aliongea na hapa ndipo nilipata kufahamu kwanini wakati nikiwa namwangalia kwenye ramani alikuwa akionekana ndani ya hoteli hii , kumbe alikuwa akiishi hapo.

“Asante sana Rania”Niliongea kisha akaniangalia na kutabasamu.

Haikuwa nyumba lilikuwa ni jumba la kifahari , ni jumba ambalo lilikuwa likivutia mn ,kwanzia muundo wake , mpaka thamani na naksi zilizowekwa ndani ya hii nyumba.licha ya uzuri wa nyumba hii , hamu yangu ya kuoneshwa hiko kitu haikukauka na ilikuwa ikiongezekwa kwa kila dakika , wakati tukiwa tunapanda ngazi za kuelekea gorofa ya juu ya nyumba hii .

Tulikuja kusimama katika chumba ndani ya gorofa ya pili , na Rania alifungua mlango huo kwa kuweka kidole sehemu maalumu ya kutumia ‘fingerprint’ na ndipo tulipozama katika chumba hiki.

Kilikuwa ni chumba kikubwa mno kwa masikini lakini cha kawaida kwa watu matajiri kama mwanamke huyu , upande wa kulia wa chumba hiki ulikuwa na picha ya mchoro wa Kasuku ukiwa umetundikwa , na hapa ndipo nilipokumbuka ‘logo’ ya The truth waliokuwa wkiitumia , muda huu wote wakati tunaingia kwenye hii nyumba nilikuwa nimevalia miwani yangu , kama zile wanazotumia wagonjwa wa macho , lakini hii ikiwa na kazi maalumu kurekodi kila kona ya jumba hii na picha kuzituma katika kitengo chetu cha Mzalendo kwa tafsiri Zaidi .

Tuliweza kuingia kwenye chumba kikubwa kingine yaani ndani kwa ndani , na nilichogundua ni kwamba chumba hiki kina milango miwili , yaani kuna mlango ambao unaweza kutumia kwa kuingilia ukiwa kwenye korido na pia ukiwa ndani ya chumba hiki pia unaweza kutumia mlango wa ndani kuingilia kwenye chumba kingine , ndani ya chumba hiki kulikuwa ni kama ofisi ya Profesa flani hivi kwani kulikuwa na majivitabu mengi sana , tena yale makubwa yaliopangwa kwa mpangilio mzuri kama maktaba.

Nilikuwa nikipitisha macho yangu kwa kila kona ya chumba hiki ili nisije kosa’details’ ya aina yoyote ile , nilijikuta nikisogelea baadhi ya vitabu vile na kuviangalia , nilichogundua ni kwamba karibia vitabu vyote vilikuwa ni vya kihistoria , kuna vilivyokuwa vimeandikwa kwa lugha ya kilatin , lakini pia kuna vilivyoandikwa kwa lugha ya kigiriki na kingereza pia

“Ndio hii picha Stephano” Aliongea Rania na mimi nilijikuta nikigeuka na kuangalia hio picha na hapo ndipo nilipopigwa na mshangao , kwani picha ile ilikuwa ni ya kwangu tena zikiwa mbili ya kwanza ikiwa ni ya sura yangu halisi yaani Damiani ,ya pili ikiwa ni yakwangu halisi, jambo hili nilijikuta likinishangaza sana kwani sikuwa nimetegemea kwamba picha zangu zote mbili ile feki na ile halisi kuwa mahali hapo.

Nilijikuta nikishangaa huku nikisahau kwamba nipo kwenye chumba cha mmiliki wa kikundi cha The Truth, kikundi ambacho kilikuwa maarufu sana katika mtandao wa Deepweb , kwa kuuza taarifa mbalimbali, na kwa maana hio kuonekana kwa picha hizo hapo ilimaanisha moja kwamoja hawa The Truth walikuwa wakinifahamu nje ndani.

Niliangalia picha hii ya Stephano Lamberk kwa muda huku mwanamama huyu akiniangalia na kisha niligeukia picha yangu halisi inayonitambulisha kama Damiani.

“Kuna picha mbili hapa ya kwanagu na hii nyingine , hadithi hio inakaa vipi?”Niliongea hivyo makusudi nilikuwa nikijaribu kupima uelewa wa mwanamke huyu juu ya mimi kuwa na sura mbili, Alitabasamu…

“I know you are Damiani and even yesterday night I recognised you”Nakujua Damiani hata jana usiku nilikufahamu.





SURA YA 08

Ni siku kumi baada ya kikao kilichowakutanisha Profesa Mike Alan , na wenzake wanne wakizungumzia juu ya mafanikio ya Mpango Zero, lakini pia wakiwa wamezungumzia mpango wa kumfanya mtoto Ambrose kupenda historia ya mambo ya kale .

Mwanzo wa wiki yaani siku ya Jumatatu ,ndani ya shule ya North Broward alionekana mwanaume mmoja wa kizungu akiwa anaingia katika darasa ambalo anasomea kijana Ambrose yaani Class A.

Baada ya mwanaume huyu kuingia ndani ya darasa hili alianza kujitambulisha kwa jina la Nick Jonas mwalimu wa maswala ya saikolojia , baada ya mwalimu huyu kujitambulisha aliendelea kufundisha wanafunzi hawa ambao walionekana wachache lakini wenye kusikiliza kwa makini kile ambacho mwalimu Nick anafundisha.

Mwalimu Nick Jonasi alikuwa ni mrefu wa wastani , mwenye nywele nyeusi zilizojaza kichwwa chake na kumfanya kupendeza , alikuwa na umri kimakadirio sio chini ya miaka therathini na tano.

Staili yake ya ufundishaji iliojaa ucheshi iliwafanya wanafunzi hawa wa Class A kuvutiwa sana na mwalimu huyo akiwemo Mtoto Ambrose ,Alikuwa akifundisha mambo ya saikolojia kwa mfumo wa hadithi za zama za kale.

Baada ya nusu saaa ya mwalimu huyu kufundisha alijipatia wasaa wa kufahamiana na wanafunzi hao kwa kila mmoja na ndoto zake za baadae , alijikuta akishangazwa na mengi juu ya yale mambo ambayo watoto hao walitaka kuyakamilisha katika maisha yao ya kimasomo, licha ya kufurahishwa na mambo ambayo wanafunzi hao walikuwa wakimweleza , jambo moja tu ndio lilimshangaza lakini pia na kumfurahisha kwa wakati mmoja ni juu ya mtoto Ambrose , kwani baada ya kuulizwa ni kipi angependa kukifanikisha katika maisha yake ya baadae alijibu hakuwa na chaguo la aina yoyote kwani mpaka wakati huo alikuwa akipenda kila kitu huku akiwa hana sababu ya kuchukua kimoja na kuacha vingine .

Kwa namna ambavyo Ambrose alijibu swali hilo ,Sir Nick alikiri kweli Ambrose alikuwa na akili nyingi , lakini licha ya kukiri hivyo aliona misheni yake ambayo alikuwa amepewa na Umoja Namba Tisini Na Saba anakwenda kuifanikisha kiurahisi sana.

“This mission is going to be interesting and smooth , directing him to stick with Ancienty history is goimg to be easy as of his multiple interest”

“Kumfanya apende mambo ya zama za kale ni jambo rahisi mno kwani mpaka sasa hanakitu ambacho anamalengo nacho au alikuwa anapenda kufanya”

Hio ndio namna ambavyo mwalimu Nick akiwasiliana na mtu ambae hakujulikana kwenye simu akimpa hayo maelekezo , baada ya mwalimu huyu kumaliza kuongea na mtu huyo alitabasamu kwa muda na kisha alichukua mvinyo wake na kunywa na kuketi katika sofa ndani ya nyumba yake hio aliopewa ndani ya shule hio ya North Broward.

“Lakini kwanini ni mfundishe kupenda mambo ya kale ?”Ni moja ya swali ambalo bwana huyu alijiuliza , kwani kazi ambayo alikuwa amepewa na wakuu wake kwa mtoto Ambrose ni kumfundisha kupenda hostoria ya zama za kale ,lakini hakupewa sababu ya kufanya hivyo kwa mtoto huyo ilikuwa ni nini.

Siku iliofuata Sir Nick kama kawaida alikuwa na kipindi na Class A , siku hio aliwahi sana kufundisha na kumaliza na mara baada ya kipindi hicho alimuita Ambrose ofisini kwake kwani alikuwa na mazungumzo nae .

“Ambrose umekuwa mwanafunzi wa kipekee sana niliowahi kufundisha katika swala zima la saikolojia”.

“Kwanini unasema hivyo mwalimu , ni kipi cha kipekee ambacho umepata kuona kutoka kwangu”

“Wenzako wote wana ndoto za kukamilisha katika maisha yao , lakini wewe pekee ndio umesema unapenda kila kitu , kwangu jibu lako ndio la kwanza kupata kutoka kwa mwanafunzi wa umri wako hivyo naweza kusema ni la kipekee sana”.

“ Asante sana mwalimu , lakini kwangu ni swala la kawaida , kwani mpaka sasa sina sababu ya kupenda hiki na kuchukia kile , najiona naweza fanya kila kitu”

“Dunia inavitu vingi ambavyo vinaatakiwa kuendelezwa kila siku na kwa wewe mtu mmoja huwezi kumaliza kufanya kila kitu ,Je utajisikiaje kama kuna kitu kimoja ambacho unaweza fanya na kukupatia majibu ya vitu vyote”.

“Sijakuelewa mwalimu”.

“Utajisikiaje pale utakapo pata ufunguo wa siri ya kila kitu ndani ya dunia hii”

“Nitakuwa na furaha sana mwalimu , kwani nitakuwa nina uwezo wa kufanya kila kitu kwani napenda vyote”

“Ipo siri kubwa ndani ya hii dunia ambayo itakuwezesha kufanya kila kitu kwa ufanisi mkubwa na endapo utaweza kufanya hivyo ni Dhahiri utakuwa mtu mkubwa wa kuogopwa ndani ya dunia hii , na unaweza ukawa mfalme wa Dunia”.

“Ni kweli hayo mwalimu”Awamu hii Ambrose aliulza kwa kwa hali ya shauku kubwa , na jambo hili lilimfanya mwalimu huyu , kufurahi kwania aliona kazi yake ya kumfanya Ambrose kupenda mambo ya kale inakwenda vizuri .

Moja ya falsafa ya mwalimu Nick katika shule zote alizowahi kufanya kazi na kutatua matatizo mbalimbali ya maswala ya kisaikolojia , alikuwa akiamini kwamba kuna sababu moja kubwa ambayo inamfanya mtu kupenda kitu sana kuliko vitu vingine , na sababu hio inajengwa na tamanio lenye nguvu(Motivated desire),huku akiamini kwamba tamanio lenye nguvu mara nyingi huchipua kutokana na shauku ya mtu juu ya kitu Fulani(Curiosity).

Hivyo kitendo cha kumwambia Ambrose kwamba kuna ufunguo wa kumfanya kufanya kila kitu katika uso wa dunia na kuwa mtu mkubwa duniani , ilikuwa ni kujenga shauku yake ili hatimae kuweza kumjengea tamanio lenye nguvu.

Alikuwa ashamsoma tabia ya Ambrose tayari na kugundua ni mtu ambae anapenda vitu vikubwa , na kitendo cha kumjibu kwamba alikuwa akitaka kufanya kila jambo katika uso wa dunia , swala hilo lilimfanya amtamue Ambrose kama kijana mwenye ‘ambition’ kubwa . na hilo aliona ni jambo ambalo litamuwezesha Zaidi katika kumfanya kijana huyo kupenda historia ya mambo ya kale.

“Naongea ukweli Ambrose ,, hii ni siri ambayo nakwambia sasa , na hupaswi kumwambia mtu yoyote yule nikikueleza siri hii ,nimekuchagua wewe kwani unaonekana kuwa na akili nyingi kuzidi wenzako wote”

“Ni siri gani hio mwalimu , nahitaji kujua”.

“Sio rahisi hivyo Ambrose kukuambia siri hii kubwa , kwani ili kuielewa lazima kwanza upende kusoma mambo ya historia ya kale , ukielewa kwa ufasaha mambo ya historia ya kale ndio utakuwa umekidhi vigezo vya kujua siri hii , na nitakupeleka sehemu ambayo utakutana na mtu ambae anafahamu siri hio”.

“Nina weza kufanya hivyo mwalimu , lakini mpaka nipate uthibitisho wa jambo unalolisemea kama lina ukweli ndani yake”Aliongea Ambrose huku akionekana kumaanisha kile ambacho anaongea , na jambo hilo kwa mwalimu Nick lilimfurahisha , kwani kwanza hakutegemea kwa mtoto kama huyo ambae akili yake ilikuwa kubwa kuwashawishika bila ya kuwa na ushahidi .

Basi baada ya mwalimu Nick na Ambrose kufanya mazungumzo hayo , kazi ilibaki kwa Nick , swala la Ambrose kutaka ushahidi wa kile alichokuwa anakizungumzia lilikuwa ni kazi kwani mpaka wakati huo hakujua ni kwa namna gani anaweza kupata ushahidi ambao unaweza kumfanya Ambrose kuukubali.

Baada ya kutoka kazini alihitaji kuoanana na boss wake aliempa kazi hio , alimtafuta kwa simu na kuweka miadi ya kuonana muda wa jioni ndani ya mgahawa wa Rosela katikati ya jiji la Frolida .

Muda wa saa moja za jioni kwa saa za Kimarekani , Nick Jonasi alionekana akiwa ndani ya mgahawa huu tulivu kabisa wenye mandhari ya kuvutia , na nadhani hii ndio sababu ya watu hawa kukubaliana kukutana mwamahali hapo , kwani ndani ya hili eneo kulikuwa na utulivu wa ahali ya juu sana , japo kulikuwa na watu wa mbalimbali waliiokuwa wakipata kahawa , lakini hakukuwa na makelele.

Bwana Nick ambae tunamjua ni mwalimu wa saikolojia katika shule anayosomba Ambrose alikuwa ameketi ndani ya mgahawa huu wa kisasa upande wa kulia mbele kidogo na kaunta ya vinywaji , alionekana kupata kahawa huku akimsubiria mtu ambae alikuwa na miadi naye ya kukutana ndani ya muda hio , aliangalia saa na kuona alikuwa amewahi kuliko isivyokawaida .

Lakini mara baada ya kufika muda saa kumbi na mbili na dakika hamsini na tisa , alionekana mwanaume mfupi wa wastani alievaliaa jacketi refu jeusi ambalo limemziba miguu , bwana huyu alikuwa ni wale watu ambao washavuka daraja la ujana miaka mingi , kwani kichwa chake cha uwararaza kilichojaa mvi kilikuwa kikiongea kila kitu .

Baada ya bwana huyu kuingia moja kwa moja alinyoosha mpaka sehemu ambayo alkuwa amekaa Nick , na mara baada ya kufika aliweka begi lake aina ya Briefcase nyeusi pembeni karibu kabisa na miguu ya Nick na kisha aliketi huku wakisalimiana.

Mzee yule na yeye aliagiza kahawa yake ya kuzugia na baada ya hapo waliingia kwenye mazungumzo na hapo ndipo Nick alipomueleza bwana huyu juu ya mazungumzo yake na mtoto Ambrose , baada ya mzee huyu kuelewa hitajio la mwalimu Nick alivuta mkoba wake aliokuja nao na kuufungua na kutoa kitabu na kumpatia mwalimu Nick.

Juu kabisa ya kitabu hiki kulikuwa na nembo kubwa ya pete yenye mchoro usioeleweka ,mwalimu Nick alikiangalia kitabu hicho na kugundua kuwa kilikuwa kimeandikwa kwa lughaambayo hakuwa na uelewa nayo .

“Huo ndio uthibitisho ambao utamfanya Ambrose kukubaliana na wewe”..

“Huu unawezaje kuwa uthibitisho , naona ni kitabu ambacho kipo kwa lugha ambayo sijawahi pata kuiona”

“Mpe kijana kazi ya kutafuta maana ya hio lugha na njia pekee ambayo anaweza kupata kufahamu hio lugha ni kwa njia ya kusoma mambo ya historia ya kale , akiweza hilo misheni yako itakuwa imekwisha”Aliongea mzee huyu na kisha alinyanyuka akimuacha mwalimu Nick akiwa kwenye maswali , alikiangalia kitabu hicho na kujikuta akishangaa kile kilichoandikwa katika hiko kitabu , hakuelewa lugha iliokuwa imetumika ndani ya hiko kitabu ilikuwa ni ;iugha gani .Siku iliofuata mwalimu Nick aliingia darasani kama kawaida kwa ajili ya kipindi na wanafunzi wa Class A.

Baada ya kipindi alimwita tena Ambrose kwa ajili ya kuendeleza mazungumzo yao walioishia siku ya jana , hakutaka sana kuongea mengi , alichofanya ni kutoka kile kitabu na kumkabidhi Ambrose.

“HIko ni kitabu ambacho lugha yake mpaka sasa haifahamiki ni lugha gani , wanahistoria wa mambo ya kale wametafua namna mbalimbali ya kujua lugha hio lakini mpaka sasa hakuna ambae alipata kujua kupambanua lugha hio”.

Swala lile lilimshangaza mno kijana Ambrose , hakuamini kwamba lufha ilioandikwa katika kitabu hicho ilikuwa haifahamiki kama mwalimu wake anavyosema .

SURA YA 09.

MIAKA KUMI NA MBILI NYUMA.(kutoka kitabu cha 2HOURS OF MEMORIES kilichoandikwa na mtunzi ISSAI SINGANO)Rania anasimulia…..

Ni miaka kumi na mbili nyuma nilipoingia kwa mara ya kwanza ndani jiji la Sydney kutokea Tanzania , nchi yangu ambayo niliona ni chungu sana kwa mimi kuishi kutokana na mambo makubwa yalionitokea ya kuumiza .

Jambo lililonileta ndani ya taifa hili La Australia mbali na Nchi yangu ni kwa ajili ya kuishi , lakini pia kupata wasaa mzuri wa kupona kwa yale ambayo niliweza kuyapitia wakati nilipokuwa nchini Tanzania .

Niliingia katika nchi hii nikiwa na mwanangu Erick aliekuwa na umri wa miaka miwili tu, kwa wakati huo mwanangu Erick ndie aliekuwa faraja yangu kwa kipindi chote nilichoweza kufika ndani nya taifa hili , kwani tokea nifike sikuwa na kazi maalumu ambayo nilitaka kuanza kufanya , kwani akili yangu kwa wakati huo haikuwa sawa nilikuwa kwenye majuto makuu kwa yale ambayo yalisababishwa na familia yangu .

Ilinichukua muda wa miezi minne kwa akili yangu kukaa sawa , unaweza ukajiuliza kwa muda wote huo nilikuwa nikiishi vipi , jibu ni kwamba nilikuwa nikiishi hotelini kwa wakati wote huo kwani nilikuwa na pesa ya kutosha kuishi ndani ya jiji hili linalosifika kwa kuwa ghali Zaidi duniani.

Basi baada ya miezi minne ya kuwa ndani ya Sydney niliweza kukutana na Rasi ndani ya hoteli ya Four Season hoteli ambayo nilikuwa nikiishi kwa muda wote wa miezi hio minne , Ras ni moja wanaume wacheshi sana ambao nimewahi kukutana nao , lakini pia naweza kusema ni rafiki yangu wa kwanza kuwa nae ukiachana na Peter ambae ndie baba mzazi wa Erick ambaye na yeye pia ndie aliechangia mimi kuja ndani ya taifa hili.

Ras alikuwa ni Floor manager ndani ya hoteli hii , na floor ambayo alikuwa akisimamia ndio hio ambayo nilikuwa nimechukua chumba , na naweza kusema hilo lilichangia sana kwa mimi kufahamiana na Rasi kwani nilikuwa mteja wa pekee ambae nilikuwa nimeishi kwa miezi mingi ndani ya hoteli hio .

Mwanzo wa kufahamiana na Ras ndio mwanzo wa akili yangu kuamka kibiashara Zaidi , na hili ni kama Rasi aliliona kwangu kwamba nilikuwa nikiwaza kufanya biashara , kwani mara nyingi kila nilipoweza kukutana nae alikuwa akuzungumzia maswala ya biashara na hii yote ni pale nilipomueleza nia yangu ya kutaka kuwekeza ndani ya taifa hili.

Nakumbuka siku ambayo nilimueleza nia yangu ya kuwekeza swali moja kuitoka kwake lilikuwa ni kama ninao mtaji kiasi gani , na nilipomtajia kwamba nilikuwa na mtajji wa kiasi cha Dollar Milioni Hamsini , ndipo alipoweza kushangaa sana lakini pia kufurahishwa kwa wakati mmoja na nadhani kilichomfurahisha kwa wakati huo ni kwamba aliona fursa kupitia mimi .

Siku moja Rasi aliomba kukutana na mimi kwa ajili ya mazungumzo , na mimi nilimkubalia na tuliweza kukutana ndani ya hoteli hii kwenye mgahawa , siku hii alikuja sio kama mfanyakazi kwani alikuwa amevalia kiraia kabisa, jambo ambalo alinieleza siku hio ni juu ya hoteli ya Avani Park ilioukuwa imefilisika na ilikuwa sokoni kwa kuuzwa .

Siku hii ndipo nilipokuja kugundua kuwa Ras alikuwa ni kichwa likija swala la biashara , kwani alinipa maelezo yalioshiba ya sababu ya mimi kununua hoteli hii ambayo ilikuwa ikiuzwa kwa bei rahisi sana nusu ya pesa ambayo nilikuwa nayo .

Baada ya kurishidhishwa na maelezo ya Rasi hatimae alipanga kikao cha kunikutanisha na mmiliki wa hoteli hio kwa ajili ya mazungumzo ya bei , mmiliki alikuwa ni mmama Profesa kutoka chuo kikuu cha Monash Alikuwa akifahamika kwa jina la Victoria Lambert mwenyeji wa jiji la Mellbourne , maongezi yangu na mwanamama Victoria yalienda vyema sana kiasi cha kwamba tulijenga ukaribu kwa masaa kadhaa tu ya mazungumzo yetu.

Basi niliweza kununua hoteli hio kwa asilimia themanini huku mwanamama huyu akibakisha asilimia 20 kwahio kwanzia siku mbili mbele za kusaini makaratasi ya manunuzi nikawa mmiliki kwa asilimia thamanini za hoteli hii ambayo nilikuja kuibadilisha jina na kuita Park Hyatt Sydney.

Nilipangua utendaji mzima wa hoteli hio huku nikimuweka Ras kama Manager mkuu , na katika hili sikumpendelea kabisa kwani alikuwa akitosha kabisa katika nafasi hio na hili liilidhihirika baada ya mwaka mmoja wa kuchukua hoteli hii , kwani kwa ukarabati tuliofanya na uboreshaji wa huduma iliweza kuvutia wateja wengi sana ndani na nje ya Australia , jambo ambalo mimi mwenyewe lilinishangaza sana .

Kwani ndani ya miezi kumi na nne ya umiliki wangu matajiri wakubwa waliweza kufikia ndani nya hoteli hii ,lakini pia hoteli yangu iliweza kushinda zabuni nyingi za kimataida na za ndani ya nchi .

Mwanzo wa mafanikio makubwa niliokuwa Napata ,ndio mwanzo wa kusahau mambo yalionitokea ndani ya taifa la Tanzania, na kwa kiasi Fulani furaha yangu kurudi upya , na kwa kipindi chote hicho Ras alikuwa rafiki yangu mkubwa , japo alishawahi kunitongoza lakini nilimkatalia katakata , kwani ndani ya moyo wangu licha ya mambo ambayo Peter alinifanyia sikuwahi kumsahau hata mara moja , na nilijiapiza sitokuja kuwa na mwanume mwingine tokea pale mume wangu Hemedi alipofariki Dunia.

Upande wa Erick ukuaji wake ulikuwa ni wa kushangaza sana kuliko isivyo kawaida na hili halinikushangaza mimi tu lakini pia madaktari wengi wa hospitali ya Randwick ambayo nilikuwa nikimpeleka katika ratiba za ufuatiliaji wa ukuaji wake .

Ndani ya miaka mitano ya Erick alikuwa akiongea kama mtu mzima , na alikuwa na kichwa chepesi mno katika kukumbuka vitu, na nilipongezwa sana na walimu wa Sydney Grammer School kwa kupata bahati ya kuwa na mtoto kama Erick , jambo hilo kwangu lilikuwa la lfaraja mno , kwani ukichana na mambo ambayo yalinitokea katika maisha yangu ya nyuma , kwangu Erick ni kama bahari Mungu alionipatia.

Muda ulisonga miaka ikapita , na ukuajji wa Erick ukaendelea kushangaza wengi husani katika maendeleo ya shule.

Nilichokuja kugundua ni kwamba Erick alikuwa na akili nyingi sana na naweza kusema kwamba ni jiniasi kwani baada ya miezi kadhaa ya mwanangu kuhudhuria shule ya Grammer School , alikuwa amewaacha mbali sana wenzake ambao alikuwa akisoma nao darasa moja , lakinii pia niliweza kuletewa ripoti ya maksi alizopata mara baada ya kupimwa IQ(Intelligency Quontient ),maksi zake zilikuwa ni 140 maksi ambazo mwalimu Ashley aliniambia ni kiwango cha juu kabisa kwa binadamu wenye uwezo mkubwa wa akili .

Jambo hilo kwangu lilinifurahisha sana , lakini naweza kusema ndio mwanzo wa msururu wa matukio mbalimballi ambayoo yalikuwa yakitokea kwa mwanangu , kwani mara nyingi alikuwa akifuatwa na watu mbalimbali , wengine wakiwemo watu wakubwa wakimuhoji vitu mbalimbali , jambo ambalo lilikuwa likinitia wasiwasi juu ya usalama wa mwanangu ,, nilijaribu kuongea na walimu wa Sydney Grammer School na waliishia kunitoa hofu kwamba sina haja ya kuwa na wasiwasi kwani wanatoa ullinzi wa kutosha kwa wanafunzi wanaosoma ndani ya shule hio , na mimi niliona kama na kuwa ‘paranoid’ hivyo niliona jambo la kutoa wasiwasi wasi wangu juu ya usalama wa Erick ni kujikita katika biashara Zaidi .

Baada ya mwaka mmoja kupita yaani mwaka wa sita wa mimi kuwa ndani ya nchi hii ya Australia niliweza kumuhamisha Erick kutoka shule aliokuwa anasoma na kwenda kusoma katika shule ya vipaji maalumu , hii ni shule ambayo ilikuwa ikimilikiwa na Victoria mwanamama Profesa ambaye aliniuzia hoteli ambaye naweza kusema kwamba alikuwa ni mmiliki mwenza ,yeye ndio alioniushauri kumpeleka Erick katika shule yake iliokuwa ikifahamika Hope School of Elite Kid (HSOEK),Ilikuwa ni shule kubwa na yenye hadhi ndani ya taifa hili la Australia na ilikuwa ikifahamika sana ndani na nje ya nchi , ilikuwa na level zote mpaka High School na kilichonifurahisha na kunishawishi kumpeleka Erick katika shule hiii ni historia kubwa ya shule hio katika kutoa wanafunzi bora kitaifa ambao walikuja kufanya mageuzi katika Nyanja mbalimbali.

Biashara zangu zilikuwa zikisonga vyema jambo ambalo pia lilikuwa likinishangaza lakini pia baadhi ya wafanya biashara wenzangu kunishangaa kwa hoteli yangu kukua sana ndani ya muda mfupi huku wengi wao wakitaka kujua ni siri gani ambayo ninaitumia mpaka kufanya biashara kuniendea vizuri ,lakini sikuwa na majibu sahihi ya kuwapa , kwani kama ni ubora wa huduma hoteli nyingi ndani ya Jiji la Sdney zinakuwaga na huduma zenye ubora wa hali ya juu sana na naweza kusema hata kuzidi hoteli yangu ,japo hata hoteli yetu ilikuwa na huduma bora.

Miaka ilisogea biashara zilienda vyema , lakini pia Maendeleo ya Erick yalikuwa ni ya kufurahisha sana , kwani aliendelea kuwashangaza watu kwa uwezo wake wa kufikiria na kutatua matatizo mbalimnbali , alikuwa akipenda sana Masomo ya computer na hili naweza kusema kwamba ni kama alikuwa amerithi kutoka kwa baba yake , kwani yeye pia alikuwa akipenda sana maswala ya Computer na hata kipindi ambacho ninakutana nae kwa mara ya kwanza ni kutokana na tatizo la kitehama lilillotokea ndani ya Benki yetu , tatizo ambalo liliwashidna wafanya kazi wa ndani ya benki.

Baada ya Erick kumaliza masomo yake ndani ya HSOEK moja kwa moja alijiunga ndani ya chuo cha Monash kilichokuwepo ndani ya jiji la Melbourne akichukua kozi ya maswala ya komputa (Computer Science).

Alisoma ndani ya chuo hicho mpaka kumaliza akiwa ni kinara kati ya wanafunzi wote kwa kupata GPA kubwa , jambo ambalo liliwainua wanasayansi kutoka makampuni makubwa ndani ya nchi na nje wakitaka kumuajiri katika kampuni zao za maswala ya kiteknolojia , lakini kwa mwanangu Erick alikuwa hataki kusikia swala la ajira jambo ambalo hata kwangu halikunishangaza kwani hata mimi pia nilikuwa nikichukia sana maswala ya kuajiriwa , hivyo nilipanga kumsapoti kwa namna yoyote ile pale tu atakapo taka kujiajiri.

Siku moja wakati nikiwa nyumbani nilishangaa kumuona Erick akiwa nyumbani , jambo ambalo siio kawaida yake , kwani hakuwa mtu wa kukaa kabisa nyumbani , na nilikuwa nikimuona mara chache sana na hata mara nyingine wakati nikiwa nimemmisi kumuona huwaga nafunga safari na kwenda kumuona Mellbourne , naweza kusema japo ya kwamba alikuwa akionesha kunijari sana na kunipenda kama mama yake lakini hakuwa na ile tabia ya kuja kunisalimia mara kwa mara , na hata chumba chake kilikuwa kipweke muda mwingi , na pia nilikuja kugundua kuwa Erick alikuwa ni mtu wa wanawake sana , alikuwa akibadilisha sana wanawake , hii tabia nilijaribu kumkataza na kumuonya lakini hakuiacha ., ni kama ilikuwa starehe yake , nilipunguza hata kumpa hela nyingi lakini nalo halikusaidia kwani alizidi kunishangaza kwa namna ambavyo alikuwa akijitanua katika visiwa mbalimbali ndani ya nchi na nje ya Nchi , swala ambalo lililikuywa fikirishi kwangu pia ni kwa namna gani anapata pesa , lakini sikuweza kupata jibu kwani kila nilipokuwa namuuliza alikuwa akinipa jibu kwamba nimuache na maisha yake , na hahitaji pesa yangu kuijua dunia .

Sasa siku kumkuta nyumbani jambo hilo lilinishangaza kidogo ,, lakini pia lilinifurahisha kwani nilikuwa nimemisi uwepo wake ndani ya nyumba , baada ya kusalimiana nae , hatimae aliniambia nia yake ya kurudi nyumbani , jambo ambalo lilinifurahisha na kulipokea kwa mikono miwili , lakini hakuishia hapo tu aliweza kuniomba kiasi kikubwa cha pesa , ilikuwa ni dolla za kimarekani milioni kumi , kiasi ambacho kilikuwa kikubwa sana na nilitaka kujua sababu ya yeye kutaka kiasi hicho cha pesa na jibu alilonipa ni kwamba alikuwa akitaka kufungua kampuni yake , kwangu swala hilo lilinifurahisha mno kwani ndio jambo ambalo nilikuwa nikilisubiria sana kutoka kwake .

Sikutaka kumuhoji sana kwani mwanangu alikuwa na tabia ya kususa pale unapomuhoji sana , na mimi kwaua kipindi hicho nilikuwa na pesa nyingi na nilikuwa moja ya wawekezaji wanaochipukia wakubwa ndani ya Austraslia basi niliandaa kiasi hicho cha pesa na nikamuingizia kwenye akaunti yake.

Kama alivyo ahidi alikuwa amebadilika kabisa alikuwa akiishi nyumbani na hata ile tabia yake ya kutoka toka na wanawake maeneo mengi ya starehe aliacha, alikuwa na mwanamke mmoja tu ambae alikuja kunitambulisha kama mpenzi wake , alikuwa ni mzungu mwanadada aliekuwa akifahamika kwa jina la Sarah.

Siku moja niliingia kwenye chumba chake na hii ni mara baada ya kumgongea sana pasipo kufungua jambo lilonitia wasiwasi , sikuwa na utaratibu wa kuingia kwenye chumba chake japo ya kwamba vyumba vyetu vilikuwa mkabala .

Siku hio ndio nilishangaa mno ndani ya hiki chumba kwani nilikuta kilikuwa kimezagaa makaratasi mengi ambayo yalikuwa yametupwa chini mengine yakiiwa na michoro mbalimbali , mingine ikiwa ya ndege , mingine ikiwa ni ya kitaalamu ambayo sikuielewa , lakini pia niliweza kuona mavitabu mengi ambayo yapo juu ya meza yakiwa yametapakaa mpaka juu ya kitanda yakiwa yamefunuliwa, lakini jambo ambalo nilishangaa pia ni kwamba vitabu vingi vilikuwa ni vya lugha ya Kilatini na kigiriki ambavyo nilishindwa kusoma .

Nilisogea ndani ya chumba chake huku nikimwita , na baada ya kumkosa nilisogea kwenye chumba ambacho nilikitenga kama sehemu ya kusomea na hapo ndipo nilipo mkuta akiwa amevaa maheadphone .

“Yeeeeeessssss….!!!!!. Yes , Yes , Yes……. “ Ni maneno aliokuwa akitamka na ni kama mtu ambaye alikuwa akitafuta jambo Fulani na wakati huo alionekana kufanikiwa na alikuwa akishangilia , na hakujua kama nipo na mwangalia mpaka pale ambapo aligeuka na kuniona na alinikimbilia na kunikumbatia huku akionyesha kushindwa kuzuia furaha yake , jambo ambalo kwangu liliongeza shauku ya kutaka kujua ni kipi hicho kilicho mfanya kufurahi kwa namna hio.

“Mom ! I did it , I made it”

“You did what Erick , tell me” niliongea na kumfanya aniangalie na kisha akatabasamu na kurudi kwenye meza na kuchukua karatasi tatu na kunionyesha .

“Hii ndio alama inayowakilisha kampuni yangu (logo)” Aliongea huku akinionyesaha ndege aina ya Kasuku akiwa amesimama kwanye kijiti , karatasi ya pili alinionesha ikiwa na jina la kampuni lililosomeka kwa kama The Truth, Karatasi ya tatu ilikuwa na maandishi yaliosomeka kwa jina ONLY GIFTED KNOW THE TRUTH(akimaanisha kwamba waliozaliwa na kitu cha ziada ndio wanaoujua ukweli) ,nilishangaa lakini na kutabasamu kwa wakati mmoja huku kilichonifanya kutabasabu siku hio hata sikuwa nikijua . ni nini lakini nilichokuja kugudnua baadae ni kwamba , kwa miaka mingi sikuwahi kumuona Erick akiwa kwenye furaha ya aina hio na niliamini kwa kitu ambacho amepatia huenda kikawa kikubwa , kwani nilikuwa nikijua kuwa ana uwezo mkubwa wa akili na siku zote watu wenye akili kubwa ni mara chache sana kueleweka kwa kile ambacho wanakifanya na mimi japo ya kuonionesha makaratasi hayo nilitabasamu kuwa nina furaha kwa ajili yake kwa kila anacho kifanya , lakini ukweli ni kwamba sikuona mantiki kabisa kwa kile alichonionesha.

“Mom uneweza usielewe nilichokuonesha , lakini vitu vitatatu vinamaana kubwa sana ambazo kama unamacho ya kuona utaelewa ni kama mchoro wa Monalisa”.

“Nieleweshe nipate kuelewa maana hii hali ya hapa ndani naamini ulichofanya nikikubwa”

“Even more mom , Do you know there is only one Secret in the world that hold all the truth ?”Ni Zaidi ya hayo mama ,Je unajua kwamba dunia ina siri moja kubwa ambayo inabeba ukweli wa mambo yote”

“Ukweli upi Erick?”

“Hilo ndio jina la kampuni yangu , Kampuni yangu itakuwa ni kwa ajili ya kutambua ukweli unaoonekana na ule usio onekana ,Ukweli ni nguvu , ukweli ni madaraka , ukweli ni utajili katika dunia hii na ni wachache sana katika hii dunia wanaujua ukweli na wanatafuta namna ya kuujuha ukweli , watu watahitaji ukweli kwa namna yoyote ile iwe ni kwa kununua ama kwa njia nyinginezo.Watu ambao wanakitu cha ziada ndani yao ndio wamepewa uwezo wa kuujua ukweli ,Ukweli usionekana ndio unanguvu kubwa ndani ya dunia hii , wanaoujua ukweli ni watu wenye madaraka makubwa ndani ya dunia hii na hawa watu wanaulinda ukwei huo usionekane ili wawe ndio pekee wenye nguvu Zaidi katika dunia”.

Yalikuwa ni maneno mengi sana kutoka kwa Erick lakini mpaka wakati huo bado sikuelewa anachomaanisha , japo maneno yake yanamaana kwa kiasi chake , lakini kwa upande wa biashara sikuona namna ambavyo atatengeneza pesa na hio ngio mantiki ambayo nilikuwa nikiitafuta katika maneno yake , lakini sikuipata .

Sikuweza kuongea sana na Erick , nilimuacha aendelee na mambo yake huku nikimwambia kuwa mimi nataka mafanikio yanayoonekana sio hadithi na hilo aliniahidi kwa asilimia mia moja kwamba atanithibitishia .

Zilipita siku mbili tena nilienda kumuamsha Erick , lakini ile nafika kwenye chumba chake huku nikijua kwamba yupo ndani , nilimuona akiwa ndio anafika , huku akiwa ameshhikilia karatasi mbili , nilisalimiana nae na kisha aliniambia anakitu anataka kunionyesha na mimi sikuwa na hiyana , niliingia ndani ya chumba chake ili kuona hiko kitu .

Zilikuwa ni picha mbili alizonionesha na picha hizo zilikuwa za mwanaume ambaye aliniambia kuwa mwanaume huyo alikuwa ni Mtanzania ambae amevaa Mask , sikumwelewa , lakini aliendelea kunionyesha kwa ushahidi huku akiniambia watu wawili tofauti ambao nawaona katika picha ni mtu mmoja , na kilichhofanya watu hao kuonekana tofauti huku akiwa mtu mmoja ni teknolojia , alimalizia na kuniambia swala hilo ndio kama swala analozungumzia yaani ninachokiona ndio ukweli unaonekana na nisichokiona kwa mtu huyo kuwa mtu mwingine ndio ukweli ambao haunekani , huku akimalizia kwamba kisicho onekana ndio nguvu ya mtu huyo .

Nilimuuliza kuhusu jina la mtu huyo na hapo ndipo alipo nitajia jina la Damiani Raban na Stephano Lamberk, kwanzia siku hio sikumwelewa na kumuamini kabisa , kwani watu ambao alinionyesha walikuwa ni watu wawili tofauti ambao sikuwa nikiwajua .

Siku moja ikiwa ni Jumapili nikiwa naelekea kanisani , aliamka mapema Erick na kuniaga kwamba anaenda kutafuta ukweli , huku akiniahidi kwamba atarejea , hio ndio ikawa siku yangu kuonana na mwanangu , kwani kwanzia siku hio mpaka sasa ni miaka miwili sijawahi kuonana na Erick.

Katika haarakati za kumtafuta Erick ndio nilianza kufatilia picha ambazo alikuwa ameweka chumbani , picha ya mtu ambae aliniambia kwamba alikuwa ndio Damiani Rabani ambaye pia anafahamika kwa jina la Stephano Lamberk,dhumuni ilikuwa ni kutaka kujua kile ambacho alikuwa akimaanisha Erick kwani mpaka wakati huo sikuwahi kumuelewa na hata hela ambayo nilimpatia kwa ajili ya ufunguzi wa kampuni sikujua iko wapi kwani kwa kufaatilia akaunti za kibenki niligundua kuwa zilikwisha kutolewa , lakini pia nilijaribu kuwahusisha polisi na wanausalama wa taifa , na wao pia hawakua na majibu ya kueleweka kwa uchunguzi waliokuwa wameufanya .

Katika kufatilia habari ya Stephano Lamberk na Damiani Rabani ndipo nilikuja kupata kitabu cha WARAKA WA RAISI KABLA YA KIFO CHAKE kilicho andikwa na mwandishi ISSAI SINGANO (SINGANOJR) nilisoma kitabu hicho lakini bado sikuamini juu ya FBM mpaka siku ambayo niliweza kuonana na mtu ambaye alikuwa akizungumziwa na Erick , lakini pia na mwandishi SINGANOJR ndani ya hoteli yangu ya Hyat Park.



SURA YA 10

Kwangu simulizi hii ya huyu mwanamama ilikuwa ni ya kusisimua sana na kushangaza kwa wakati mmoja hususani kwa upande wa kijana Erick , mpaka wakati huo nilikuwa na ufahamu nusu wa kwanini Erick alianzisha kampuni aliokuwa ameiita The Truth .Licha ya kwamba nilikuwa nimejua nia yake kubwa ni kuujua ukweli lakini katika simulizi hii nijikuta nikijua mambo makuu matatu kuhusu Erick , jambo la kwanza Erick alikuwa ni mtu mwenye akili kubwa sana yaani ‘Genius’ na mimi katika maswala ya kijasusi haya mamb huwa mara nyingi yanazingatiwa sana , kwa mfano tu nchi ya Marekani wana idara za maswala ya kiusalama kwa mfan FBI , CIA ,NSA sasa katika harakati zote za maswala ya kudahili(Recruitment/Admission) kigezo kikubwa ni akili ya mtu , ukionekana una akili kubwa(IQ) , pamoja na baadhi ya vigezo vingine mfano kuwa na afya njema basi unakuwa ‘best candidate’ kwenye hizi idara .Si kwa Marekani tu , mashirika mengi ya kijasusi duniani huwa yanachukuwa watu wenye akili kubwa kwa mfano MOSSAD kutoka Israeli ,M16 kutoka

England na hata TISS kutoka Tanzania na hii yote ni kwamba hizi idara za kijasusi mara nyingi ni kama uhai wa taifa katika Nyanja zote ndio maana hata kwa sisi Mzalendo ajenti wetu ni majiniasi.

Swala la pili nililgundua kutoka katika simulizi hii yta mwanamama Rania ni ‘Ambition’ nashindwa hata kualiongelea kwa lugha yetu ya Kiswahili hili neno lakini maana yake ni kwamba ni mtu mwenye malengo makubwa yenye msukumo ndani yake , hivyo niligundua kuwa licha ya kijana huyu Erick kupewa akili kubwa ni kwamba alikuwa ni mtu mwenye malengo makubwa sana na hili linamfanya kuwa mtu hatari sana, kwani mara nyingi watu wa aina hii watafanya kitu chochote kile ilimradi kukamilisha malengo yao hata kama ni kutumia njia za giza (njia zisizohalali).

Swala la Tatu nililogundua ni kwamba licha ya kijana Erick kuwa katika umri mdogo lakini alikuwa ni mtu alietengeneza koneksheni na ni mtu ambae anaiafahamu dunia vyema na kwa simulizi ya mwanamama Raniua naungana na Erick pale aliposema kwamba Ukweli usioonekana ni Nguvu(Power) hili naliunga mkono kwa asilimia kubwa sana kwani katika uliumwengu wa kijasusi hili pia kwetu ni sehemu ya somo , Watu wanaojua ukweli au siri kubwa ndani ya hii dunia ndio watu wenye nguvu kubwa , hivi unadhani ni kwanini mashirika makubwa kama Freemasons , UMOJA NAMBA TISINI NA SABA ,Illuminat na mengineyo wanakuwa ni watu ambao hawaonekani , jibu ni kwamba kitu kisichoonekana kinakuwa na nguvu kubwa sana , na hili sitaki hata nikulazimishe kuniamini lakini unaweza ukajiuliza swali moja je ushawahi kumuona Mungu????.

Hivyo ukweli usionekana (Hidden Truth) ndio wenye nguvu kubwa na ndio unaoendesha dunia, lakini ndio unaofanya taifa na taifa kuogopana , wengi hapa ni mashahidi leo hii hakuna anaejua uwezo halisi wa kijeshi wa Marekani , au Urusi , au china hii yote ni kwamba kuna vitu ambavvo havionekani kwenye nchi hizo na hizi idara za kijasusi mara nyingi zinajikita kujua hivyo vitu visivyo onekana.

Hivyo kwa kijana Erick kuwa na malengo ya kuutafuta ukweli namuona ni kama Jasusi wa kujitegemea , kitendo cha kujua uhalisia wangu mpaka hapo ni kwamba kijana huyu kampuni yake hii ya The Truth hakuianzisha kizembe zembe, ninacho amini ni kwamba mpaka kupata wazo la kuanzisha hii kampuni au kikundi ni kwamba alianza kukutana na jambo , na hilo jambo huenda lilikuwa kubwa kwake na lilikuwa likihusiana na ukweli uliofichika na katika hilo jambo alinusa nguvu kubwa ilioambatana na kweli hio aliokumbana nayo .Kwangu hayo ni makisio tu. “Nimeguswa sana na hii simulizi ya kijana Erick”Niliongea huku nikimwangalia mwanamama huyu , na wakati huu tulikuwa tumeketi muda wote kwenye kitanda cha Erick ndani ya chumba chake huku mbele kabisa kukiwa na picha ya Kasuku pembeni kukiwa na picha zangu zilizotundikwa .

Mwanamama huyu alikuwa akionesha hali ya huzuni sana , lakini sio huzuni tu lakini pia alionyesha ishara kama zote za upweke , na jambo hili lilidhihirika ndani ya nyumba hii , kwani licha ya wafanyakazi wawili ambao niliowaona wakati wa kuingia ndani ya hiii nyumba sikuona harufu ya mtu mwingine ambaye naweza kusema ni mtu wa karibu wa mwanamama huyu.

“Nitahakikisha Erick anapatikana Rania”Niliongeea huku nikiwa nimemkazia macho usoni nikiyaangalia machozi yake yaliozidi kupendezesha uso wake ,Nilinyoosha mkono wangu na kisha nikayafuta kwa kiganja cha mkono jambo ambalo lilimfanya mwanamama huyu kupoa kiasi lakini kunikazia macho ambayo kwangu niliona ulegevu wa macho , jambo ambalo pepo la ngono lilianza kuninong`oneza nimkule huyu mwanamke.

“Vipi kuhusu Peter baba wa mtoto Erick ?”

“Long gone , nishaanza kumsahau kwasasa na sijui hata yupo hai au amekufa”

“Kwanini unasema hivyo ?”

“Ni stori ndefu sana iliotokea nchini Tanzania na hata sitaku kuikumbuka”

“Kwa hio sasa hivi umeolewa au upo kwenye mahusiano ya namna yoyote ile?” Nilijikuta nikiuliza swali hilo la kipumbavu kabisa , kwani kwa urembo wa mwanamama huyu ni Dhahiri kabisa wanaume watakuwa wamepangiliwa vyema, Aliniangalia usoni huku akionekana ni mtu ambae anavuta pumzi na kuzitoa hali ambayo niligundua alikuwa akijiandaa kwa kunijibu lakini alikuwa kwenye ‘dilemma’.

“Sijawahi kuwa kwenye mahusiano ya aina yoyote ile tokea niingie ndani ya nchi hii , japo ya kukutana na vishawishi mbalimbali kutoka kwa wanaume wengi sana wenye nazo na wasio nazo , wazungu wahindi , , arabs na hata wa Afrika walikuwa wakitaka kuwa na mahusiano na mimi lakini sijawahi kuruhusu moyo wangu kumuamini mtu , sitaku kuzungumza sana kuhusu hayo Damiani Stop making me talk about those things. they are boring enough”.

“Okey nimeacha na nakuamini kwa maneno yako japo inaweza kunigharimu”Niliongea huku nikitabasamu na yeye pia kutabasamu kwani alikuwa ashaelewa nilicho kuwa nikimaanisha .

“Nataka kukuona ukiwa kwenye ‘African Colour’ kama Damiani nachukia rangi nyeupe unajua , lakini pia nataka nione unavyobadilika”Aliongea huyu mwanaume maneno matatu ambayo ukijumlisha yote ni ombi lakini ukiyachambua unapata maneno mawili ya kawaida lakini la mwisho lenye uhatari , unaweza usijue ni uhaatari wake ila utanielewa kwa vitendo.

Sikuwa na haja ya kumbania mwanamama huyu kumuonesha kile ambacho alikuwa akitaka kuona , niliongozana nae mpaka kwenye chumba changu kwa ajili ya kuivua hii FBM m sikuwa na haja hata ya kumjali , alionekana ni mwenye kujiamini wakati tukiwa tunaingia hapa ndani kwenye hiki chumba , lakini kadri ya matendo yangu niliokuwa nikiyafanya nilimuona akiaza kupoteza kujiamini , sheria za FBM ni kwamba lazima niwe Uchi ili kuivua na hili nilidhamiria kufanya mbele yake , yeye si alitaka aone jinsi ninavyovua na kuvaa basi namimi niliona nimtimizie ombi lake .

Lakiwa akiniangalia kwa wasiwasi sana wakati huo nikiwa nimebakisha boksa tu , ni kama mtu ambae alikuwa haamini kama ninakwenda kuvua ile boksa na kufumba na kufumbua nilikuwa uchi tena nikimgeuzia upande ule bwana kalumanzira aliolala , dakika chache mbele nilikuwa Damiani Rabani, na hapa ndipo mwanamama huyu alipozidi kushangaa na kupagawa , nilijikuta nikimsogelea pale aliposimama yeye akiwa hasogei , na kuhesabu sekunde kadhaa tu nilikuwa nishamfikia na kumshika mkono , alionekana kuwa dhaifu mno , kama mtu ambae hajapata chakula kwa siku nyingi sana na mbele yake kulikuwa na chakula .

Sekunde sabini mbele Rania alikuwa chini huku mimi nikiwa juu yake tukipiga Romansi , mwanamke alikuwa na mwili laini huyu sijapata ona , kila sehemu niliokuwa nikigusa utadhani patachanika , na kwa jinsi alivyokuwa wa moto msisimko nilioupata hapo sikuwahi kuupata mahali popote pale , akili zangu zilihama kwa muda , kwa mdakika kadhaa ya kumshika shika alikuwa amelegea mno huku akipanua miguu yake Zaidi akionekana kuwa ni mwenye uhitaji wa juu sana wa uanaume wangu kumuingia , na mimi sikuwa na ajizi nilimpa kile alichokuwa anataka na hapo ndipo nilipomshuhudia mwanamama huyu kupanua mdomo huku akitoa machozi , sikujua ni ya utamu au nini lakini sikutaka kujali sana , nilipeleka chini juu mpaka pale nilipoona sauti yake inakauka kwa kilio ndipo nilipopunguza , nilimgeuza na kumgeuza huku nikijisikia utamu wa ajabu sana ambao sikuwahi kuupata , na weza kusema mtoto alikuwa mtamu huyu , nadhani hili ni kutokana na kutokukuguswa kwa muda mrefu sana kwani kitu ilikuwa mnato sana .

Dakika arobaini mbele wote tulikuwa tumechoka huku tukihema kama mbwa aliekimbia maili nyingi ,nilimwangalia mwanadada huyu na kujikuta nikipokea tabasamu ambalo liliufanya uchomvu wangu wote wa safari ndefu kuisha hapo hapo na kujikuta tukiiingia kwenye mtanange na awamu hii ulinoga sana kiasi cha kunifanya nitoe mbegu wengi sana ndani ya uanamke wa Rania .

Wakati nikimaliza ni kama Janeth alikuwa akiona kile nilichokuwa nikifanya kwani simu yangu ilitoa mlio na kuichukua.

“Damiani najua unacho kifanya lakini naomba uache , tumegundua ile picha ya Kasuku sio mchoro wa kawaida “

“Unamaanisha nini ?”

“Namaanisha unatakiwa kurudi kwenye chumba cha Erick na tutakupa maelekezo mengine “Aliongea janeth huku nikimuona kama mtu ambae anajizuia hisia zake zisiingilie kazi , lakini alikuwa amekwisha kuzoea , alikua akijua kabisa mapenzi yangu aliondoka nayo Merina.

“Hio picha ina rangi mbili ambazo hazijaungana , rangi ya juu ni rangi ambayo unaweza kuifuta kwa kuimwagia maji ya moto , naamini kuna kitu kimefichwa kwenye hio piucha “Aliongea janeth na nikampa maelekezo Rania ya kuleta maji ya moto , na dakika chache yalikuwa tayari na tuliimwagia ile picha maji baada ya kuiweka sakafuni .

“Kipi kinafuata janeth ?”

“Chukua brash ya kupakia rangi na fanya kama unaaza kuipaka rangi upya”

Nilifanya kama Janeth alivyokuwa anaelekeza na hapo ndipo mimi na Rania tulivyoweza kupigwa na mshangao kwani kila sehemu unayopitisha Brash rangi inapotea ‘Colour

Repracement’hii kitu ilinishangaza sana , nilichokuwa najua hii njia inaweza kufanyika kwenye komputa tu kumbe hata kwenye picha ya kawaida.

Ni namba kumi na mbili ambazo ziliandikwa kwa mfumo wa kirumi sikuelewa ni namba za nini , nilipiga picha na kisha nikazituma kwa Janeth ili kuzipatia maana yake na ndani ya dakika chache alikuwa na majibu .

“Ni ‘Cryptography’ namba”

“Zinamaanisha nini?”

“Hapa mpaka kuzitambua , hilo swala ili lifanikiwe nitahitaji Serial number za Kompiuta zilizopo hapo ndani” Aliongea na mimi nilimtumia na kwa mbaali nilielewa anacho maanisha , kwani kwa ninachojua kuhusu Cryptography ni kwamba huu ni mfumo wa kuficha maneno kwa muundo wa kodi , zinaweza kuwa namba au mfumo(format) wowote ule, hii njia ndio inzifanya Cryptocurrency kuwa na hali ya juu ya usalama kwani hata serikali haiwezi kujua hizi namba.

“NImefanikiwa kutambua hizo namba maana yake ni SANTORIN” “Santorin?” Niliongea na kumfanya mwanamama Rania aniangalie .

“Santorin ni kisiwa kilichopo ugiriki”.Aliongea Rania na hapo hapo nilipata kujua huenda The Truth haipo Australia kama tulivyodhania bali ipo Ugiriki.

“Erick atakuwa Ugiriki”Niliongea na mwanamama huyu alijikuta akishangaa lakini Janeth kuniunga mkono kwa kile ambacho nilikuwa nasema , na hili niliona ni swala ambalo linaleta Mantiki , kwa kazi ya hiki kikundi niliamini kabisa ni lazima wawe watu wa kujificha sana .

SURA YA 11

DAR ES SALAAM –TANZANIA

Zikiwa zimepita siku kadhaa tokea kuchaguliwa kwa waziri mkuu pamoja na mawaziri , lakini pia ikiwa imepita siku moja tokea mheshimiwa Raisi Jembe kusafiri kuelekea nchini Marekani kwa ajili ya kula kiapo cha kujiunga na umoja wa siri wenye nguvu duniani Umoja Namba Tisini Na Saba ,Ndani ya jijiji hili lenye pilikapilika za kila namna katika moja ya gorofa ndefu iliokuwa ikimilikiwa na mfanya biashara mkubwa nchini pembeni kabisa na zilipokuwepo ofisi za kampuni ya INNOVA ndani ya jengo hilo kulikuwa na kikao cha siri kilichokuwa kikiendelea .

Ndani ya hili jengo ndio zilipokuwepo ofisi za Umoja huu wa siri kwa eneo la Tanzania na ndio maana siku hio kikao hiki kilikuwa kikiafanyikia ndani ya hilo jengo.

Katika meza kubwa ndani ya chumba kikubwa ndani ya jengo hili katika floor ya kumi na tano chumba kilichokuwa na maandishi makubwa mlangoni yaliosomeka kwa lugha ya kingereza TOP LEVEL MEMBER OFFICE (TLMO) kulikuwa na mabwana wapatao kumi , watano walikuwa wakifahamika kwa majina yao kutokana na kwamba walikuwa ni viongozi wakubwa ndani ya serikali ya Tanzania, wengine hawakuwa wakitambulika kwa majina yao kwani walikuwa sio raia wa Tanzania na rangi zao zilithibitisha hilo .

Katika kikao hiki ajenda kubwa zilikuwa mbili , ajenda ya kwanza ambayo ilianza kujadiliwa ni wasiwasi wa uanachama wa mheshimiwa Jembe Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, japo ya Umoja huu kukubali ombi la raisi Jembe kujiunga na Umoja Namba Tisini na Saba lakini mabwana hawa walionekana kuwa werevu Zaidi kutokana na wasiwasi wao.

Mkuu wa majeshi , Mkuu wa kitengo cha usalama wa taifa ,Raisi mstaafu aliachia madaraka kwa Jembe ,Makamu wa raisi mteule aliengia madarakani , pamoja na mkuu wa jeshi la polisi ndio watu waliokuwa wakitambulika katika kikao hicho , lakini pia ndio viongozi wakubwa ndani ya nchi ya Tanzania walikuwa wakiunga mkono umoja huu wa siri ambao haukufahamika malengo yake kwa Taifa .

Mabwana hawa walikuwa wakijua fika mheshimiwa Jembe hakuwa na nia thabiti ya kujiunga na umoja huo , jambo ambalo mabwana hawa waliona linaweza kuufanya umoja huu kutojiimarisha vyema ndani ya nchi , walihofia juhudi walizokuwa wamefanya katika kurudisha nguvu ya umoja huu ndani ya Taifa la Tanzania zinaweza kupotea .

Jambo la kwanza liliowafanya mabwana hawa kutilia mashaka nia ya bwana Jembe ilikuwa ni siku ya kuapishwa kwake , kitendo cha Peskorov kupigwa na kuzirai siku ambayo amefanya tukio la kumpiga risasi mheshimiwa Jembe na kugundulika kwa alama ya Mzalendo iliokuwa imeachwa katika paji la uso la bwana huyo liliwafanya mabwana hawa waamini kwamba mheshimiwa jembe alikuwa na ushirikiano na kikundi hichi ambacho walikuwa wakiamini kwamba kilikuwa kimepotea ndani ya nchi hii yaani Mzalendo.

Lakini kitendo cha Jembe kupita katika uchaguzi , lakini pia kupona risasi , lakini pia kupotea mara baada ya kupigwa risasi , lakini pia kujitokeza na kutaka kujiunga na U-97 , lakini pia alama ya Peskorov katika paji la uso ilioachwa na mtu ambae alipambana nae mambo hayo yote yaliwafanya waamini kwamba Mzalendo ambayo ilikuwa imetokomezwa miaka kumi iliopita imerudi upya tena ikiwa na nguvu Zaidi kuliko awali. Kwani matukio yaliotokea hayakuwa yakufanywa na mtu mmoja , walimini matukio hayo kwa yeyote aliekuwa akihusika alikuwa na nguvu kubwa sana.

“Unatoa ushauri gani bwana Kinga juu ya rangi halishi ya bwana Jembe ?” Swali hili lilitoka kwa bwana Kent kwenda kwa mkuu wa usalama wa Taifa ,Kent ambaye alikuwa ni muwakilishi wa U-97 Afrika mashariki alikuwa akimuamini sana Kinga , katika vikao vyote alivyokuwa amefanya alikuwa akifurahishwa na michango ya kimawazo ya Kinga , kwani siku zote waliweza kufikia maaumuzi na mawazo yaliokuwa yakitolewa na bwana huyu na ndio maana kwa kila kikao alikuwa akimfanya kuwa mtu wa mwisho katika kuchangia .

“Mkuu kwanza kabisa naamini kwa asilimia mia moja kuna mpango ambao anao mheshimiwa jembe ,tena mpango huu ukiratibiwa na kikundi hiki cha Mzalendo na yeye akiwa ni moja ya jumuia ya kikundi hiki , na hata swala la yeye kutaka kujiunga ndani ya hiki kikundi nimeweza kufikiria na kuja na mambo makuu mawili kwa mheshimiwa kutaka kujiunga na umoja wetu , la kwanza ni kutaka kukalia kiri cha uraisi , kwake swala hili limekuwa ndio njia rahisi ya kupata usalama wa kufika pale ikulu kutokana na tukio lililomtokea , swala la pili , mlolongo woote wa matukio yaliotokea katika siku ile ya kupigwa risasi ni Dhahiri bwana huyu alikuwa akijua kile kilichokuwa kikiendelea , na ni jambo ambalo lilikuwa limepangwa kwa ustadi mkubwa sana na ninyi wote hapa ni mashahidi kwamba hakuna mtu duniani ambaye anaweza kupigwa risasi kwenye kifua na kupona tena bila hata ya kuwa na jeraha isipokuwa tu kama jambo hilo mtu huyo awe analifahamu na kuvaa ‘Bullet Proof’ , lakini tunaweza kusema labda mheshimiwa jembe aliweza kuvaa ‘Bullet Proof’ , lakini ni vipi kuhusu kufichwa kwake mara baada ya kupigwa risasi , tena akifichwa na wanausalama wetu ambao mpaka sasa hatujui mahali walipo,hivyo ninacho amini kwa sasa ni kwamba swala hili hatuwezi kulichukulia kwa urahisi , hili ni swala la dharura na tunapaswa kulichukulia kwa udharura wake ili kuchukua tahadhari zote , tunapambana na watu wenye maarifa na wenye nguvu , mpaka sasa mkuu wa tume ya uchaguzi hatujui aliko yeye pamoja na familia yake haya yote sio mambo ya bahati mbaya , ni maswala ya kupangwa . tena ya kupangwa kwa muda mrefu , hivyo ushauri wangu kwasasa ni kuhakikisha tunaweka nguvu zetu zote kukisaka hiki kikundi na kukitokomeza moja kwa moja na kuhakikisha tunatoa mizizi yote ili kuepusha kuchipuka tena”

Aliongea bwana kinga na kufanya watu wote waliokuwa katika kikao hicho kutafakari maneno hayo , lakini si hivyo tu kila mtu aliweza kuwaza na kuvuta picha kamili ya kikundi cha Mzalendo kwa kuunganisha matukio machache yaliotokea siku kadhaa zilizopita.

“Umeongea vyema sana bwana Kinga , lakini kwanza kabisa naomba nikutoe hofu lakini pia niwatoe hofu watu wote mliopo ndani ya hiki chumba , kwanza kabisa Mzalendo ni kakikundi kadogo sana ambako kalibahatisha kufanya matukio yaliotokea , lakini yakaleta athari kubwa , lakini kubahatisha kwao hakumaanishi kwamba kikundi hiki kinanguvu na maarifa kutuzidi sisi ,tulichokosea nikuwadharau hawa watu na kakikundi kao , lakini mpaka sasa hali imerudi kama ilivyokuwa na naweza kusema kila kitu kinaenda kama tulivyopanga na muda mfupi ujao tutawakamata wahusika wotea wa kikundi hiki”

“Swala hilo litakuwa gumu kutokana na kwamba watu hawa bado hawafahamiki na ndio maana nimeshauri kulichukulia tahadhari”Aliongea Kinga na kumfanya Bwana kent kutabasamu , moja sifa kubwa ya bwana Kent ni dharau alikuwa akiwadharau sana watu weusi , unaambiwa tokea akiwa mdogo katika historia yake ya shule zote alizopita bwana huyu alikuwa mbaguzi wa rangi wa waziwazi , sifa yake ya pili alikuwa ni ‘Sadist’ hawa ni watu ambao wanapenda kuona wenzao wakiteseka kwa kuwasababishia maumivu licha ya bwana huyu kutibiwa lakini ni kwamba hakupona kikamilifu, hata tabasamu alilokuwa akumuoneshea Kinga licha ya kwamba alikuwa akimkubali katika michango yake , tabasamu hilo lilikuwa la dharau lakini usingeweza kumjua .

“Huna haja ya kuwa na wasiwasi bwana Kinga U-97 ilijengwa na watu wenye akili na mpaka sasa tuliobaki wote tunakili , hivyo hata hawa Mzalendo hawawezi kushindana na sisi maana sisi sio nchi bali sisi ni Dunia hivyo mtu mmoja hawezi kushindana na Dunia ,Swala la Mzalendo kumtumia Jembe katika mipango yao ni makossa makubwa waliofanya na hili linadhihirisha uwezo wao mdogo wa kufikiria ,Jembe huko anakoenda anaenda kuwataja hawa panya wote na kazi itakayobaki ni sisi kuwakamata hapa Tanzania na kuhakikisha hakuna hata mmoja anaekimbia wala kukosekana”

“Itawezekana vipi kwa mheshimiwa Jembe kuwataja wafuasi wake ?”Aliulizwa Kilubwa raisi mstaafu aliechia madaraka akiwa kwenye hali ya mshangao.

“PSYOPS” Aliongea Kent na baadhi ya watu hapo ndani walielewa huku wengine wakiwa hawajaelwa na walihitaji ufafanuzi .

“Kinga atawafafanulia ninachomaanisha na mpaka sasa kikao kimekwisha na ninagharisha mpaka kikao kingine tutakapozungumzia kuhusu Mpango Zero”Aliongea Kent na kisha kuondoka huku akiwaamuru walioelewa neno aliloongea waondoke na ambao hawajaelewa wabaki , na wale wazungu wote waliweza kuondoka ikidhihirisha kwamba walikuwa wameelewa kile ambacho Kent aliongea ila viongozi wote wakubwa hawakuelewa isipokuwa kwa bwana Kinga aliekuwa amepewa jukumu la kuwafafanulia wenzie juu ya maana ya neon PSYOPS.

*****

JOHN F KENNEDY INTERNATIONAL AIRPORT –NEW YORK, USA 18:00.

JFK ni moja ya viwanja vya ndege bora kimataifa vilivyokuwa bize sana ndani ya jiji hili la New York , Zaidi ya ndege 70 huruka na kutua kwenda na kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi ya Marekani , uwanja huu upo sehemu inayoitwa Queens ndani ya New York , ni uwanja wenye jumla ya terminal sita sifa inayodhirisha ukubwa wake, huku kila terminal kiwa na huduma bora kabisa..

Lakini sifa za ukubwa wa uwanja huu unaendana na umaarufu wa Jiji la New York , ni moja ya jiji lenye watu wengi Zaidi ndani ya nchi hii ya Marekani , na moja ya sehemu ambayo ina uhuru wa kuishi na kutafuta maisha ni ndani ya jiji hili , ukuaji wa jiji hili ulikuwa ni wa haraka sana ukilinganisha na majiji mengine .New York ndio kitomvu kikubwa cha biashara ndani ya taifa hili la Marekani na nje ya nchi pia kwani wafanya biashara wengi hutembelea sana jiji hili kwa ajili ya maswala ya kibiashara , moja ya maeneo maarufu ndani ya jiji hili ni kama Wall Street hili ni eneo ambalo maswala yote ya kiuchumi na kifedha yanafanyika , ndio sehemu ambayo makampuni makubwa ya kifedha na kibenki yanapatikana , ni sehemu ambayo maswala ya masoko ya hisa yapo , sehemu nyingine ni Time Squre hili ni eneo lenye watu wengi wanaotembea kwa miguu ni sehemu inayofahamika kwa majina ya kiutani mengi na moja wapo ni kama ‘Heart of the world’, pia moja ya utambulisho mkubwa wa NYC ni uwepo wa ‘Statue of liberty’,NYC ndio mji wenye magrofa marefu na mengi Zaidi ndani ya nchi ya Marekani na ndio eneo pekee ambalo hutembelewa na watu wengi Zaidi ndani ya nchi ya Matekani. Licha ya umaarufu mkubwa wa jiji hili nje na ndani ya Marekani lakini pia yapo mambo mengi yaliokuwa yakifanyika mengine yakiwa ni halali na mengine yakiwa sio halali

Nje kabisa ya mlango wa Terminal 4 alionekana mheshimiwa Jembe akitoka ndani ya mlango uliokuwa na maandishi makubwa yaliokuwa yameandikwa ARRIVALS akiwa ameambatana na walinzi wake pamoja na wasaidizi , Ndege aliokuwa amefika nayo mheshimiwa Jembe ilikuwa ni ya shirika la Fly Emirate . ndege ambayo alikodi kwa ajili ya usafiri huo .

Mara baada ya kutoka ndani ya jengo hili la kisasa kabisa alifuatwa na mabwana wawili mmoja akiwa ni mweusi na mmoja alikuwa ni mzungu wote wakiwa wamevalia suti nyeusi na miwani za jua , hawa mabwana kabla ya kumfikia Raisi Jembe walizuiliwa na walinzi na hapo ndipo walipotoa vitambulisho vyao .

Mabwana hawa walijitambulisha kama CIA mmoja akiitwa Ben Horowtz na bwana mwingine alijitambulisha kama Sam Snowden , mabwana hawa walijieleza kama moja ya watu waliokuwa wameagizwa kwa ajili ya kumpokea mheshimiwa na kumuongoza kuelekea mahali ambako anatakiwa kufika .

Walinzi wa mheshimiwa Jembe walijiridhisha na mabwana hao na kisha waliongozana nao mpaka kwenye maegesho ya magari na walimuonyesha mheshimiwa gari ambalo lilikuwa limeandaliwa kwa ajili yake

Baada ya kuingia ndani ya gari hili pamoja na mlinzi wake wa karibu ‘Bodyguard’ huku wale walinzi wengine wakipanda kwenye gari zingine ambazo zilikuwa pia zimeandaliwa, gari hizo ziliondka ndani ya eneo hilo.

Safari ya mheshimiwa Jembe ndani ya Marekani haikua ya kikazi na wala uongozi wa Marekani hawakuwa na taarifa rasmi za raisi Jembe kudhuru ndani ya Taifa hilo na jambo hili kwa namna yake lilishangaza kidogo kwani walipokelewa na CIA. .

Jumla ya gari zilikuwa nne , zilizokuwa zikimsindikiza mheshimiwa Jembe ndani ya muda mfupi gari zile zilikuja kusimama ndani ya nje ya uzio mkubwa wa nyumba , eneo lilokuwa likifahamika kama Shirley Chishom State Park, ndani ya Broklyn.

Lilikuwa ni jumba kubwa mno la kifahari lilikuwa ndani ya uzio huu , licha ya kwamba baadhi ya ,majumb ya pembeni kutokuwa na uzio lakini hili eneo lilikuwa limezungukwa na ukuta na hii ilionesha ni mahali ambapo si pakuingia ingia tu kama sio muhusika. .

Eneo lilikuwa tulivu sana lakini lenye madhari mazuri mno , ilikuwa ni kama hoteli huku muundo wa jingo hili ukiwa ni ule wa kizamani kabisa , ni kama yale majengo ambayo mengi utayakuta Italy hususani ndani ya Vatican city , baada ya magari yale kwenda kusimama sehemu maalumu ambayo ilikuwa ikitumika kama maegesho, mheshimiwa aliamriwa kushuka na ndani ya dakika chache kulitokea wanawake wawili wakiwa wamevalie mavazi ya suti na walionekana walikuwa mahali hapo kwa ajili ya kumpokea mheshimiwa Jembe.

“Welcome Mr President wing 7 House , my name is Hellen , Iam head of house meet my Assistant Sasha we have been waiting for you eagerly”

“Karibu mheshimiwa nyumba tawi namba saba jina langu ni Hellen ndio mkuu wa nyumba kutana na Sasha msaidizi wangu, tulikuwa tukikusubiria kwa hamu” Aliongea mwanamama huyu aliejitambulisha kwa jina la Hellen huku akiweka tabasamu pana usoni mwake.

“Asante sana Hellen” Alijibu mheshimiwa na kisha mwanamama huyu alimuongoza njia mheshimiwa pamoja na walinzi wake baada ya kuwahakikishia usalama

Mandhari ya jumba hili yalikuwa yakuvutia sana kiasi kwamba hata mheshimiwa Jembe alishangaa , yalikuwa ni Mandhari ya kifalme , kwanzia wafanyakazi waliokuwa wamesimama kwa kujipanga huku kumpa mheshimiwa Jembe ishara ya heshima , lakini pia thamani zilizokuwa zimetumika kupamba eneo hilo zilikuwa ni za kiwango cha juu sana .

Hata wasaidizi wa mheshimiwa walishangaa mapokezi ya aina hio , kwani baadhi yao ambao walikuwa ni wazoefu katika kusindikiza maraisi hawakuwahi kupata mapokezi ya aina hio ya kipekee licha ya kuwa hakukua na kiongozi mkubwa aliekuwepo ndani ya eneo hilo lakini mpangilio wa matukio ya hapo ndani yalikuwa ni heshima kubwa sana kwa mheshimiwa Jembe kupata , hata ile hofu aliokuwa nayo kiasi flani ilipungua .

“Mheshimiwa hii ni nyumba maalumu kwa ajili yako kuishi kwa kipindi chote utakachokuwepo ndani ya nchi hii , kuna kila kitu utakacho kihitaji cha kiofisi na kimalazi , utaweza kutimiza majukumu yako ya kiuongozi ukiwa hapa mpaka pale utakapokamilisha hatua tano za kula kiapo”Aliongea huyu mwanamama ambae alionekana umri umemtupa mkono na maneno yale kidogo yalimshangaza mheshimiwa Jembe lakini hakutaka kutia neno .

Basi aliweza kuonyeshwa maeneo mbalimbali ndani ya jumba hilo la kifahari kabisa , lilikuwa ni jumba kubwa lenye eneo kubwa ambalo lilikuwa na kila kitu kuanzia bwawa la kuogelea , uwanja wa Gofu pamoja na wa Tennisi .

“Uzuri wa hili eneo ni Zaidi ya Ikulu ya nchi yangu”Aliongea mheshimiwa mara baada ya kuoneshwa chumba ambacho takuwa akilala na kumfanya mwanamama Hellen kutabasamu . .



SURA YA 12

Ni siku nyingine ndani ya nchi ya Marekani ndani ya jumba la kifahari ambapo mheshimiwa Jembe alikuwa ameandaliwa na U-97 kwa ajili ya kuishi .

Asubuhi hii mara baada ya taratibu zote kuisha kama kupata kifungua kinywa na mengineyo , mwanamama Hellen alimtaarifu mheshimiwa Jembe kujiandaa kuingia ofisini kwani kuna mgeni ambae anatarajiwa kufika kwa ajili ya hatua ya kwanza.

Na ndani ya nusu saa tu ya mheshimiwa Jembe kuingia ofisini hatimae bwana mmoja wa makamo mwenye rangi mchanganyiko yaani ya kizungu na kiafrika alitinga ofisini hapo, alikuwa ni bwana mmoja kwa makadirio ya umri wake si chini ya miaka therathini , alikuwa amevalia suti nyeusi na kipepeo shingoni huku nywele zake akiwa amezichana kuelekea nyuma.

.

“Naitwa Dave Hamton afisa levo 32 ndani ya U-97 mimi ni mtaalamu wa maswala ya kiuchambuzi Duniani”utambulisho huo ulimfanya mheshimiwa Jembe kushangaa , kwani alaichotegemea ni hatua ya kwanza ya kula kiapo lakini anachokutana nacho ni mtu ambae amejitambulisha kama moja ya wachambuzi wa maswala ya kiuchumi duniani jambo ambalo kwake lilimshangaza kidogo .

“Karibu sana Dave”

“Asante sana mheshimiwa , Naamini umeshangazwa na utambulisho wangu”Aliitikia kwa kichwa

“Dhumuni la kikao chetu mheshimiwa ni juu ye kukuelezea juu ya malengo ya U-97 kwa Afiraka nzima kwa upande wa kiuchumi”Aliongea na kisha alitoa tablet yake na kumkabidhi mheshimiwa .

Mheshimiwa raisi alishangazwa na mambo mengi ambayo bwana Dave aliweza kumwambia , alikiri yeye mwenyewe katika kikao hicho kilichochukua masaa mawili kwamba umoja huu wa siri licha ya kwamba hakuwa akijua madhumuni yao makuu kwa mataifa ya kiafrika lakini kwa upande mwingine walikuwa wamesaidia ukuaji wa maendeleo kwa kiasi kikubwa sana , hususani katika swala zima la miundombinu na kuboresha maisha ya wananchi wengi , licha ya hivyo Dave aliweza kumuonesha nguvu ya umoja huu ndani ya mashirika makuu duniani kama vile IMF ,WB,UNICEF,WHO,ILO na mengineyo mengi makubwa .

Jambo hili kwa mara ya kwanza hakulielewa vyema mpaka pale alipoweza kufafanuliwa nguvu ya umoja huu ndani ya haya mashirika katika kuisadia Afrika ,bwana Dave alimwambia mheshimiwa kuwa U-97 ndio mara nyingi wanaohimiza mataifa mengi ya Afrika kupara misaada ya kufanya maendeleo na hii ni kwa zile nchi tu ambazo zitakuwa chini ya umoja huo .

Siku hio ilikuwa ni ya Vikao tu kwa mheshimiwa na watu hawa waliojitambulisha kwake kama wafuasi wa umoja NAMBA TISINI NA SABA ,

Mpaka inafika muda wa jioni wa vikao mheshimiwa alikuwa amepata uelewa mkubwa sana juu ya U-97 licha ya kutojua yandani ya umoja huo yaliokuwa yakitendeka lakini alipata kuweza kufahamu kuwa umoja huo kwa namna moja ama nyingine ulikuwa na faida kwa watanzania na alikiri kwamba watu aliokutana nao walikuwa na ushawishi mkubwa sana kwake.

Hatua za mwanzo za kula kiapo zilikuwa ni za kawaida na katika hatua zote hizo zilikuwa ni kwa ajili ya kuandaliwa kisaikolojia tu , hatua ya mwisho ndio ilikuwa ni ya kuogopesha sana kwa mheshimiwa Jembe , kwani katika hatua hii alikuwa akitakiwa kutubu dhambi zake zote , na ili uweze kupata nafasi ya kuweza kutubu dhambi anatakiwa kuweka siri zake zote wazi.

Siku iliofuata ilikuwa ni ya mheshimiwa Jembe kuingia kwenye chumba cha utakaso , hiki ni chumba ambacho sheria yake kubwa ni kwamba ili uweze kutakaswa na kula kiapo hutakiwi kuwa na jambo ambalo unalifich ndani ya moyo wako (Siri) , sheria za hiki chumba ni kwamba kama utaingia basi kunauwezekano mkubwa wa mtu kutoa siri zake zote kwa kile umoja huu ulichokuwa unakiita kuungama , yaani unaweka siri zako zote wazi ili uweze kupata nafasi ya kuungama na hatimae kuwa mwanaumoja kamili ambae huna makando makando , na kupitia hiki chumba cha utakaso siri nyingi ziliweza kupatikana juu ya mataifa mbali mbali . na si hivyo tu lakini pia kwa kila mwanachama ambae aliingizwa katika chumba hiko akitoka anakuwa mtu mpya na mtiifu kwa umoja, yaani kwa mnaneno marahisi ni kwamba kama ulikuwa na lengo baya dhidi ya umoja basi ukishaingia humo ndani , ukitoka utakuwa na malengo mazuri kwa umoja na utatii kila maelekezo utakayopewa na viongozi wa juu wa U-97.

Basi baada ya mheshimiwa Jembe kumaliza kujiandaa na kupata kifungua kinywa , walinzi wake walitaarifiwa kwamba mheshimiwa ataondoka ndani ya hio nyumba na kwenda katika kikao cha siri ambacho kitachukuwa takribani masaa kumi na mbili .

Hawa walinzi wake pamoja na wasaidizi kwanza kabisa hawakuwa wakijua kile kilichokuwa kikiendelea juu ya raisi wao kiula kiapo cha kujiunga na Umoja namba Tisini na saba , walichokuwa wakijua ni kwamba mheshimiwa alikuwa ndani ya taifa hilo kwa ajili ya maswala ya kitaifa, mtu mmoja pekee aliekuwa akijua kile kilichokuwa kikiendelea ni mlinzi wa karibu wa raisi (Bodyguard) na huyu katika safari hio ya kwenda kwenye kikao alikuwa amepewa nafasi ya kutangulizana nae , huku walinzi wengine wakiwa wamebakia ndani ya jumba la Wing 8.

Saa tatu kamili ndio saa ambayo mheshimiwa Jembe aliweza kutoka ndani ya nyumba aliokuwa amefikia kuelekea katika hekalu la Utakaso sehemu ambayo atakula kiapo rasmi cha kujiunga na umoja namba tisini na saba. Lakini pia sehemu ambayo alitakiwa kutakaswa na kuwa mpya .

Usafiri uliokuwa umetumika kumchukua mheshimiwa ndani ya Wng 8 house ulikuwa ni wa njia ya anga kwa kutumia chopa , huku ndani ya ndege hio akiongozana na mlinzi wake wa karibu na bwana mmoja ambae alijitambulisha kwa jina la Henlsink , bwana huyu alikuwa ni raia kutoka Mexico , alikuwa amevalia suti ya rangi nyeusi.

Ndani ya nusu saa tu walikuwa wapo ndani ya eneo ambalo mheshimiwa raisi na mimi mwenyewe sikueza kulitambua , lakini ndani ya eneo hilo lililokuwa limezungukwa na miti mingi kulikuwa likionekana jengo kama hekalu .

Chopa iliweza kukanyaga veyema eneo husika lenye alama kubwa ya H na baada ya hapo mheshimiwa alitoka na kuja kupokelewa na wanadada wawili , waliokuwa wamevalia kama masista , baada ya kupokelewa na hawa wadada ambao walijitambulisha kama wahudumu wa jumba hilo liliokuwa na maandishi makubwa mlangoni U-97 LODGE X .

Mheshimiwa Jembe alionekana kuwa na wasiwasi mkubwa kila alipokuwa akikumbuka maneno ya mwanamama Hellen juu ya jambo ambalo linafanyika ndani ya hekalu hilo kwa ajili ya utakaso, alikuwa na hofu ya kutoa siri zake na siri kubwa aliokuwa akihofia kuitoa ilikuwa ni juu ya mpango wa Mzalendo .

Aliamini kama kweli alichoambiwa na mwanamama huyo juu ya uwezekano wa kuweka siri zake hadharani , swala hilo lilimuongopesha sana , kwani aliamini kwa kufanya hivyo ni kwamba anakwenda kuharibu kila kitu na ile mipango ambayo alikuwa amejiwekea na kitengo cha Mzalendo inakwenda kukwama.

Baada ya utaratibu wa awali kukamilika wa mheshimiwa Jembe kupewa mavazi mengine kama yale ya wagnjwa wa hospitalini , aliweza kuingizwa kwenye chumba kimoja kilichokuwa kina maandishi makubwa mlangoni kama PSYOPS ROOM , maneno ambayo kwa mheshimiwa hakuweza kuyaelewa kabisa .

Ndani ya hili jumba ni kwamba muonekano wake ulikuwa ni kama wa hospitali , kwa nje lilionekana kama hekalu ila kwa ndani ni jEngo ambalo lilikuwa limejengwa kwa ustadi wa kutenganisha vyumba , na ilionekana hio ni sehemu maaliumu kabisa kwa ajili nya U-97 , ukutani kulikuwa na michoro mingi ambayo ilikuwa imechorwa na haikueleweka maana yake ni nini kwa mara moja .

Mlinzi wa mheshimiwa raisi bwana Tomasi Kibwe alikuwa kwenye wasiwasi mwingi , kwani ni takribani masaa nane tokea mheshimiwa aingie ndani ya chumba ambacho hakuelewa ndani ya ke ni kitu gani kilikuwa kikifanyika , ubaya ni kwamba hakuweza kutoka mahali alipo kwani alikiuwa amewekewa ulinzi , wasiwasi wake ulikuwa juu japo ya wahusika wa jumba hilo kumhakikishia usalama wa mheshimiwa Jembe ,, lakini yeye kama mwanausalama hakuweza kuwa katika hali ya utulivu , aliamini kama kuna jambo baya lolote likamtokea Raisi basi yeye moja kwa moja angewajibika na hakuelewa angewaeleza nini watanzania.

Lakini wasiwasi wake ulikuja kukoma mara baada ya kusubiri lisaa limoja mbeleni na hapo ndipo alipoweza kumuona mheshimiwa Jembe akitoka ndani ya chumba alichoingizwa akiwa na mavazi yake ya suti , lakini kwa bwana Tomasi aligundua jambo ambalo si la kawaida kutoka kwa mheshimiwa Jembe , hali ya furaha iliokuwa imetanda kwenye uso wake.

“kila kitu kipo sawa Tomasi huna haja ya kuwa na wasiwasi Zaidi” Aliongea mheshimiwa na Tomasi alipiga Saluti kuonyesha kwamba anakubali kile mheshimiwa alichokuwa anasema .

Basi kwa kutumia njia ile ile mheshimiwa aliweza kurudi Wing 8 House lakini akionekana kuwaza jambo .

“Sikuwa na jinsi ilinibidi kueleza kila kitu juu ya Mzalendo , hatuwezi kushindana na hawa watu kamwe njia moja ya mimi kuliongoza taifa la Tanzania ni kula sahani moja na hawa watu ” Aliongea mheshimiwa wakati akiwa anaingia ndani ya Wing 8 na kupokelewa na kikosi chake cha usalama ambacho muda wote kilikuwa kipo katika hali ya wasiwasi juu ya usalama wa Mheshimiwa.

“Hongera sana mheshimiwa kwa hatua yako ya mwisho”

“Nashukuru sana Hellen”

“Kesho ni siku yako ya mwisho ya ukaribisho ndani ya U-97 lakini pia ndio siku utapata fursa ya kuzungumza na wafanyabiashara wakubwa ambao kama mazungumzo yako yataenda vyema ni fursa kwa watanzania wote” Aliongea Hellen na Jembe alikubaliana nae na baada ya hapo aliaga na kuondoka

*****

Upande mwingine nchini Tanzania masaa machache mara baada ya kukamilika kwa hatua ya mwisho ya Raisi jembe ndani ya Tanzania , ndani ya ofisi ya mkuu wa kitengo cha usalama wa Taifa bwana Nassoro Kinga alipokea ujumbe wa maandishi kutoka kwa namba ambayo hakuweza kuifahamu ujumbe huo ulikuwa ukisomeka ‘MZALENDO BASE AT KURASINI

NLT TOWER GROUND FLOOR ,Damiani Rabani , Janeth Bendera , Linda ….’

Meseji hii ilimsisimua sana mheshimiwa na hakutaka kusubiri , dakika hio hio aliinua simu na kumpigia Kent na kumueleza ujumbe huo , lakini jibu kutoka kwa Kent lilimfanya atabasamu kwani hisia zake zilikuwa ni kweli na hii ni mara baada ya Kent kumwambia Nasoro kuwa andae operesheni ya dharula ya kuvamia jingo la NLT sehemu ambayo walikuwa wakijua kuwa ndio makao makuu ya kambi ya Mzalendo .

Baada ya Kinga kuweka simu yake chini hakutaka kuchelewa hata kwa dakika , kwani alinyanyua simu yake na kutoa maagizo na ndani ya dakika moja tu bwana mmoja aliejazia mwili aliingia ndani ya jengo hilo , huyu hakuwa mwingine bali alikuwa ni Mr White .

“kuna operesheni ya dharula inatakiwa kufanyika usiku wa leo”

“Misheni gsani hio mheshimiwa ?”

“Tumepata eneo la maficho ya kambi ya Mzalendo hivyo nataka usiku wa leo tukavamie hio kambi , lakini kabla ya hilo kufanyika nataka watu hawa wafuatao tujue mahali walipo”Aliongea Kinga na kutoa kumtajia majina Mr White , yalikuwa ni jumla ya majina kumi na mbili ya ajenti wote wa Mzalendo.

“Mishenni hii inatakiwa kufanyika kwa weledi wa hali ya juu sana , sitaki makossa , watu tunaoenda kupambana nao ni watu makini hivyo lazima na sisi tuwe makini , watu hawa sitaki akosekane mtu hata mmoja , unda timu ambayo itavamia usiku Kurasini na unda timu nyingine itakayowafatilia mahali walipo hawa wanaojiiita wazalendo wa nchi hii “ Aliongea mheshimiwa Kinga na kisha Mr white aliondoka kwa ajili ya kupanga timu yake kuipeleka kwenye mapambano..

Ndani ya masaa kadhaa tu tokea Mr white apewe jukumu la kuunda timu kwa ajili ya kufatilia wanamzalendo , alikuwa akitoa taarifa kwa mheshimiwa Kinga juu ya hatua ambayo wamepiga .

“Tumeweza kujua jumla ya ajenti saba walipo kwa muda huu na vijana wapo wanawafatilia kwa kila hatua, walioweza kupatikana ni Janeth bendera , Linda ,Zakayo ,Kassimu ,Sabi Mboneche………”Aliongea ajenti Nyuu au Mister White.

“Hawa wengine wako wapi ?”

“Mkuu kuna uwezakano hawa kuwa katika kambi yao”

“Huo ni uwezekano tu Bakari ninachotaka ni uhakika kama kweli wapo kwenye kambi yao , hususani huyu Damiani Rabani , ndio mtu muhimu sana kwenye hiki kitengo na ni lazima tujue ni wapi alipo kwani kossa la kumpoteza huyu ni kwamba misheni yetu imefeli”.

“Ndio mheshimiwa ngoja tuendelee kufalitilia mahali walipo kabla ya muda wa operesheni kufika “ aliongea ajenti nyuu au Mr White na kisha aliondoka , akimuacha bwana Kinga katika mawazo mawazo ya hapa na pale , lakini muda mfupi baada ya kutoka kwa Mister White Kinga alipokea simu kutoka kwa Kent .

“Operesheni imefikia wapi ?” ilisikika upande wa pili .

“Ajenti saba wapo katika macbo yetu , wengine watano hatujui walipo akiwemo Damiani Rabani , tunakisia wanaweza wakawa ndani ya kambi yao”Aliongea Kinga .

“Piga bomu hio kambi , sambaratisha kila kitu na kuhusu hao wengine waliopatikana hakikisha mnawakama wakiwa hai”Aliongea Kent na kisha simu ilikatwa .

Jambo hili kidogo lilimuacha Kinga katika mshangao lakini hakuwa na jinsi , alikuwa yupo tayari kufata maelekezo ya Kent ya kupiga bomu kiwanda cha NLT Kurasini , baada ya kufikiria kwa dakika kama mbili , alitoka na moja kwa moja alienda mpaka chumba cha ufatiliaji wa operesheni hio .

“wapi mmefikia ?”

“Janeth bendera anaonekana kuelekea upande wa Kurasini , vijana wapo kazini wanaendelea kumfatilia , nadhani hili litakuwa jambo jema tukivamia akiwa ndani ya kambi “ aliongea Bakari”

“Vipi kuhusu wengine sita ?”

“Tupo nao macho na wanaonekana kutoondoka katika maeneo ambayo wameonekena “ “Operesheni ya leo usiku ni kupiga bomu katika kambi yao , haitajarisha ni nani yupo ndani ya kambi ninachotaka kambi hio ndani ya masaa sita yajayo pawe vumbi tu ndio linaloonekana”Aliongea mheshimiwa Kinga na kufanya watu wote washangae . “Uko siriasi mheshimiwa, hilo jambo ni hatari sana kwani wengine ambao hawahusiki wanaweza kupata madhara , na isitoshe tunawezo wa kuingia ndani ya kambi hio na kuwakamata wahusika bila kufanya uharibifu mkubwa”

“Bakari maamuzi yangu ni hayo na yanatoka moja kwa moja kutoka kwa mheshimiwa Raisi , hivyo saa tatu kamili ya usiku nataka kiwanda cha NLT kiwe vumbi , andaa vijana kwa hio misheni” Ajenti nyuu alijikuta akishangazwa sana na maamuzi hayo , lakini hakuwa na kupinga kwani mkuu wake wa kazi alikuwa ashaafanya maamuzi na ni moja ya jukumu lake kufata maamuzi ya mkuu wake .

“Ni shambuilio la bomu la aina gani linapaswa kutumika?”

“Tutatumia shambulio la Anga”

******

Captain Juma hizza alikuwa ndio kwanza anaingia nyumbani kwake Tegeta muda wa saa kumi na mbili za jioni , kwake hiio ndio muda wake wa siku zote wa kufika nyumbani akitokea kazini , na bwana huyu alikuwa ni moja ya watu ambao walikuwa wakipenda sana kurudi nyumbani mapema na kuiona familia yake , hii ni tabia ambayo alikuwa amejijengea lakini pia ni tabia ambayo ilimpa heshima kubwa sana kwa majirani zake .

Kwani ni tabia ya kawaida sana na iliozoeleka kwa baadhi ya wababa wafamilia kuchelewa kurudi nyumbani baada ya kazi , kwani wao mara baada ya kazi walipitia sehemu mbali mbali wanazozijua wao kwa ajili tu ya kupoteza muda ili wasirudi nyumbani mapema .

Jambo hili lilikuwa tofauti kwa Juma kwani yeye alikuwa akiwahi sana kurudi nyumbani , basi baada ya kulakiwa na watoto wake wawili Salma na Hamisa aliingia chumbani na kujimwagia maji ili kuondoa uchomvu , lakini wakati anaendelea kuoga mara mke wake aliita akimtaarifu kwamba simu yake ilikuwa ikiita na jina la mpigaji lilikuwa ni bossi .

Baada ya kusikia jina hilo alitoka na kuchukua simu hio na kupokea kwani aliamini sio kawaida kwa bossi wake kumpiigia kwa wakati huo tena mara baada ya kurudi kazini .

Baada ya kuweka simu sikioni ndani dakika chache aliweza kupata maelekezo ya kurudi kazini kuna opetesheni ya dharula ambayo alikuwa akipaswa kuifanya usiku huo , huku akielekezwa na mkuu wake huyo wa kazi kwamba eneo husika atapewa akiwa angani.

Juma hizza alikuwa ni moja ya marubani wa ndege za kijeshi waliokuwa wakiaminiwa sana na kitengo cha dharula cha jeshi cha maswala ya makombora ya kurushwa kwa Anga , licha ya kufanya kwake kazi miaka mingi hakuweza kuutumia usomi wake katika kurusha ndege na kwenda kushambulia eneo , kwani ndani ya taifa letu kulikuwa na Amani kubwa sana kiasi kwamba ni mara chache sana ndege za kivita zilikuwa zikitumika .

Sasa siku hio mara baada ya kupokea taarifa hio ya kutumia ndege yake kwa ajili ya kwenda kushambulia ni kama walimpa mzuka kabisa , kwani jambo alilokuwa akilitaka siku zote ni hilo litokee ili aweze kuonyesha manjonjo yake .

Lisaa limoja mara baada ya kupewa maelekezo alikuwa ndani ya ndege yake kubwa ya kivita iliokuwa ikifahamika kwa jina la Bird killer ndege iliokuwa imetengenezwa nchini Urusi , ndege hio iilikuwa na uwezo wa kubeba mabomu yasiooungua mia moja na kushambulia kwa umbali mrefu kutoka angali bila kukosa Target.

Saa mbili na nusu za usiku Captain juma hiza alikuwa akielea angani akiwa na shauku kama zote za kufanya shambulio katika eneo ambalo wakubwa wake walimuelekeza kumtumia ‘cordinates’

“Ndani ya dakika kumi na tano tu za kuwa angani hatimae aliweza kupokea uelekeo husika wa Terget yake anayopaswa kwenda kufanya shambulio .

“Target locked . need permission to engage” aliongea Juma akiomba ruhusa ya kuachia kombora kwani tageti alikuwa ashaipata .

“ umeruhusiwa” mIlikuwa ni neno dogo lakini lililoleta madhara makubwa sana , kwani ndani ya sekunde kadhaa ndani ya eneo lote la Kurasini lilikuwa halitamaniki , lakini si hivyo tu , wakazi waliokuwa kuwa maeneo ya karibu na eneo hilo walikuwa katika taharuki kubwa kwani ni jambo ambalo hawakuwahi kulishuhudia kwenye maisha yao ukilinganisha na historia ya taifa la Tanzania kutokuwa na matukio ya ajabu kama hayo ..

SURA YA 13

Linda mara baada ya Damiani kuelekea nchini Australia alijikuta akipendana na kijana wa kipemba aliekuwa akijulikana kwa jila la Hamadi , kwa mara ya kwanza ya Linda kukutana na Hamadi ilikuwa ni siku aliokuwa mapumzikoni ndani ya kisiwa cha Unguja ndipo alipoweza kuonana na mfanya biashara Hamadi na kwanzia siku hio ya kukutana waltokea kupendana sana kwa muda wa siku chache walizodumu pamoja .

Siku ambayo mheshimiwa Jembe anaelekea nchini Marekani ni siku ambayo Linda akiwa ndani ya kambi ya Mzalendo aliweza kuwekeana ahadi na Hamadi kuonana siku mbili mbele kwani Hamadi alikuwa akija bara akitokea Dubai alipokuwa bize kibiashara , jambo hili kwa Linda lilimpa munkari sana ukijumlisha na namna ambavyo alikuwa amemmiss Hamadi , alijua fika kazi yake haikuwa ikimruhusu kupenda , lakini kwa kijana Hamadi alikuwa ameloea kwani kijana huyo alikuwa akijua kumdekeza mno Linda kiasi cha kumchanganya sana .

Siku mbili mbele kama walivyo ahidiana , hatimae Hamadi alifika nchini na kumtaarifu Linda kwamba yupo hoteli ya Golden Tulip katikati ya jiji la Dar es salaam , Muda ambao Linda anawasiliana na Hamadi alikuwa ndani ya kambi ya Mzalendo na ilikuwa ni muda wa saa saba na nusu kwenda nane wakati wakiwa wanawasiliana na walipanga saa kumi na moja za jioni Linda atafika hotelini hapo .

Siku hii ndani ya kambi hii walikuwemo jumla ya watu watatu waliokuwa zamu katika kuhakikisha kila mipango inaenda sawa , yaani Linda alikuwa na wenzake wawili ambao wote kwa ujumla wao walikuwa wakihusika na maswala ya kitehama ndani ya kambi hii ya Mzalendo.

Ilipotimu muda wa saa kumi na robo Liuda aliwaacha wenzake wakiendelea na majukumu na yeye alitoka kwa ajili ya kwenda kuonana na mpenzi wake Hamadi, mwanadada Linda alikuwa akiendesha gari aina ya Toyota Crown nyeupe na ni gari ambayo alikuwa akiipenda sana kutembelea nayo licha ya kwamba alikuwa na gari nyingine aina ya BMW lakini gari hio ya kijapani ndio moja ya gari alizokuwa akipendelea sana kutembelea .

Kuna jambo ambalo lilimtia wasiwasi , na hio ni mara baada ya kuingia ndani ya maegesho ya magari ndani ya hoeli ya Golden Tulip , kwani kuna gari aliitilia mashaka , kwani tokea anatoka Kurasini gari hio ni kama ilikuwa nyuma yake , japo mwanzoni hakuwa akiitilia mashaka , lakini kitendo cha kuegesha gari yake ndani ya hoteli hio na kuiona lile gari swala hilo lilimpa mashaka kidogo lakini hakuwa akitaka kulifatilia sana , kiufupi alipotezea swala hilo na kuendelea na mambo yake na hilo kwake lilikuwa ni kosa kubwa sana ambalo amelifanya.

Baada ya kuingia mapokezi aliweza kuwasiliana na chumba ambacho alikuwepo mwanaume wake aliekuwa akimpenda na baada ya kuruhusiwa moja kwa moja alielekea huko , na kitendo cha kutoka tu mapokezi , waliingia wanaume wawili waliovalia kikawaida na moja kwa moja walielekea mapokezi na walitoa vitambulisho vyao vya kazi na kumuonesha mwanadada wa mapokezi na yeye baada ya kuwatambua watu hao ni wakina nani alitoa ushirikiano wa kutosha

Baada ya swala lile kuisha pale mapokezi mwanaume mmoja aliekuwa amevalia tisheri nyekundu ya Form six alibakia eneo la mapokezi na yule mwingine aliingia kwenye Lift .

Huku upande wa linda baada tu ya kuingia chumba alichokuwa Hamadi walirukiana na kupeana mabusu na kunyonyaka mfululizo jambo ambalo liliwapandisha sana hisia zao za kufanya mapenzi na ndani ya dakika chache tu walikuwa wote wapo kama walivyozaliwa na kijana Hamadi alionekana vyema katika kuumiliki mwili wa mpenzi wake Linda .

Hata pale simu ya Linda ivyotoa mlio wa kuashiria kuna ujumbe wa meseji umeingia hakushughulika nayo.

Nusu saa za purukushani mlango wao uligongwa na aliekwenda kufungua alikuwa ni Hamadi , lakini ile anafungua alijikuta akikutana na mwanaume ambae alikuwa katika uso wa kazi huku akiwa amemnyooshea bastora kitendo kile kilimfanya Hamadi atetemeke sana na hilo kwa Linda lilionekana mara moja lakini ni kama alichelewa kwani mwanaume yule alikuwa ashamtumia Hamadi kama kinga yake huku akimwamuru Linda asilete ubishi kwani akifanya jambo lolote la kijinga mwanaume huyo atapasuliwa ubongo .

Linda aliekuwa amejifunika na Shuka alijifikiria kwa muda na kisha aliinuka alipokuwa amekaa na kumsogelea mwanaume yule huku akipewa tahadhari za kutosegea hata hatua moja , lakini ni kama Linda hakujali hilo kwani alizidi kusogea licha ya mwanuaume yule kutishia kumpiga lisasi Hamadi .

Ilikuwa ni kitendo cha dakika chache , Hamadi alikuwa chini akiwa amepigwa risasi na mwanaume yule , lakini upande wa yule mwanaume alikuwa akiangalia bastora yake iliokuwa imedodokea mbali mara baada ya kupigwa teke na Linda .

Mwanaume yule alionekana kuwa akijiamini sana kwa mapigano , lakini kwa Lnda pia alichokuwa akiamini katika maisha yake ni kwamba katika taifa la Tanzania ukimtoa Damiani hakuna mtu mwingine ambae anaweza kumpiga na kumuangusha, hivyo hakuwa na presha hata kidogo , kwani ile mwanume yule analeta pigo za haraka za ngumi upande wa Linda alizipangua kama hana adabu nzuri huku akiendelea kumsoma adui yake , na alipoona adui yake kimafunzo alikuwa ni wa kawaida sana , alimpatia kile alichokuwa anataka , kwani kwa s spidi ya hali ya juu alirusha teke moja na mguu wa kushoto lisilo na nguvu lakini lililoonekana na adui yake na adui yake akataka kulipangua na hilo ndio likawa kosa kwani kama panya alimrukia na kwenda kutua shingoni mwa mwanaume yule huku papuchi yake ikigusana na macho ya yule mwanaume , lakini hakupewa hata mwanya wa kuangalia madini yaliokuwa ndani ya mgodi kwani aligongwa utosini na kisha alilegea na kushuka na Linda mpaka chini.

Linda alichukua simu yake na kisha aliangalia ujumbe uliokuwa humo na kujikuta akitoa tusi ni kama mtu aliekuwa akijitukana kwa kutoangalia huo ujumbe na baada ya kuona hivyo alivaa haraka haraka, alimwangalia Hamadi aliekuwa amelala sakafuni damu zikiwa zimetapakaa , alijilaumu kwa kujiingiza katika mapenzi nae kwani yote hayo yasingemtokea ,, aliinamna huku akionekana mwenye huzuni na kumfumba macho yake na kisha alitoka ndani ya chumba hicho na kutokomea .

Yule bwana aliekuwa ameachwa Mapokezi alijikuta akishaangaa kumuona Linda akitokezea na hapo hapo alitoa simu yake kumtafuta mwenzake , na hakupata majibu na hakutaka kuendelea kubaki pale alidhamiria kupanda juu kumtafuta mwenzake.

Lakini alichoweza kukutana nacho mara baada ya kufika ndani ya chumba alichokuwa Linda kilikuwa ni cha kuogopesha .

Alitoka mbio mbio ili kumuwahi Linda lakini alikuwa amekwisha kuchelewa kwani ajenti linda alikuwa ashatokomea kusiko julikana .

****

Saa kumi kamili za jioni wakati Linda akifikiria kwenda kuonana na mpenzi wake , upande wa huku Makongo juu mwanadada Janeth alikuwa amekaa amejipunzisha huku akifikiria hili na lile katika swala zima la kazi aliokuwa anaifanya , jambo moja ambalo lilikuwa likimuumiza kwa wakati huo ni juu ya Damiani , kwani alijua kwa namna yoyoe ile ni lazima mwanaume huyo alikuwa ashazini na mwanamama Rania , na kwake hilo lilimchanganya sana kila akikumbuka nyakati tofauti alizokiwa akipewa mapenzi na Damiani na kulinganisha na muda huo mwanamke mwenzake akipewa tamu aliokuwa akililia kila siku alijikuta roho ikimuuma kwani alikuwa akimpenda sana Damiani. .

Wakati akiendelea kuwaza juu ya hatima ya mapenzi yake simu yake iliingia ujumbe wa maandishi , na alifungua simu yake ili kuusoma huo ujumbe na hapo ndipo alipokutana na neno kidogo lililomchanganya , lakini neno hili lililokuwa katika ujumbe wa meseji ulitokea kwa jina lililokuwa limeseviwa kama SHUSHU. Yalikuwa ni maneno mawili tu yaliosomea PSYOPS to Jembe

Kwanza alishangazwa na nenp hilo , na alitumia dakika kadhaa kung`amua maana ya neno hilo kwanini litumwe kwenye simu yake , na mara baada ya kukumbuka kuwa mheshimiwa Jembe yupo nje ya nchi kwa ajili ya kula kiapo,alijikuka akitoa tusi baada ya kukumbuka kuwa neno hilo linamaana ya psychologival Operations , na ni mbinu ambayo jeshini hutumika mara nyingi kwa adui ambae wahusika wanataka kupata taatifa kutoka kwake ,na mara kama mbinu hii itatumika kwa mtu basi ni Dhahiri kwamba atamwaga siri zotemkama tu hautakuwa na mafunzo maalumu ..

Kitendo cha kudaka maana ya hilo neno aliamini kwamba kama mheshimiwa Jemebe ataweza kufanyiwa hilo jambo basi ni Dhahiri kwamba amekwisha kutoa siri ya juu ya mahali kambi yao ilipo na si hilo tu lakini pia atakuwa amewataja ajenti wote wa Mzalando na hilo lingewaweka katika hali ya hatari.

Baada ya kugundua uhatari wa swala hilo mara moja alituma ujumbe wa maandishi kwa ajenti wote kukutana mahali ambapo aliwaelekeza haraka sana hususani wale ambao mheshimiwa Jembe alikuwa akiwajua , huku akisisitiza wote walio katika kambi kutoka haraka..

Hivyo Janeth hakutaka kubakia hapo ndani alitaka kuhakikisha ajenti wote wa Mzalando hakuna hata mmoja anaekutwa na madhira ya kuingia kwenye mikono nya U-97 , alitoka haraka na kuingia kwenye gari yake kuelekea kurasini , wakati akiwa yupo bagamayo road kuna hisia zilizokuwz ikimwambia kuwa alikuwa akifatiliwa na jambo hilo alikuja kulithibirisha alivyokuwa Mwenge , lakini swala hilo halikumpa shida. Aliendelea kuendesha gari mpaka alivyokuja kuwachenga wale waliokuwa wakimfatilia na ndani ya muda mfupi alikuwa ndani ya jingo la NLT .

Baada tu ya kuingia ndani ya ‘basement’ aliwatoa wataalamu wawili ambao walikuwa wakihangaika na tarakishi zao kwamba waondoke kwani mahali hapo si salama tena .

Ndani ya dakika kadhaa kila kitu kilikuwa kwenye mkao na Janeth alikuwa ashachukua tahadhari zote na kutoka ndani ya ‘basement’ hio na kwenda kwa Rebeca ambaye alikuwa ndio mkuu wa usimamizi wa maswala ya kiwanda na kumpa maelekezo kwamba kiwanda hiko kifungwe mapema kabla ya saa kumi na mbili.

Baada ya Janeth kutoa maelekezo hayo aliingia kwenye ofisi yake na kisha alivuta begi lililokuwa lipo kwenye kabati na akavua nguo zake zote na kisha alisimama kwenye begi hilo na ndani nya sekunde chache tu alikuwa si Janeth tena , alikuwa ni mwanamke mweupe wa taifa la Korea , alijiangalia kwenye kiooo na kisha alitabasamu na kutoka na kuingia kwenye gari nyinginie tofauti na ile aliokuja nayo.

Baada ya kuingia kwenye gari alitoka hapo ndani huku akipishana na gari ile iliokuwa ikimfatilia , alitabasamu na kisha aliondoka .eneo hilo na ndani ya nusu saa alikuwa akipita Bunju kuelekea upande wa bagamoyo .

Dakika aribaini na tano mbele alikuwa eneo la Kiwangwa kwa mbele kabisa kulikuwa na shamba la katani , alikunja na kuchukua njia ya vumbi na kutembea umbali wa mita kadhaa na kufikia kwenye jumba moja la gorofa tatu lililokuwa limezungushiwa ukuta na mahali hapo kukiwa na baadhi ya nyumba kadhaa za watu waliokuwa wakiishi pembezoni , baada ya kuingiza gari alipaki na mtu aliekutana nae alikuwa ni Sabi mboneche .

"Vipi mmeweza kufika wote sabi?”

“ Hapana miss Janeth tupo wanne ambao tumefika hapa , shukrani kwa ujumbe wako tumeweza kutokukamatwa” aliongea Sabi huku wakiingia ndani na ndani ya dakika chache na Linda nae aliweza kufika ndani ya eneo hilo huku akifatiwa na wengine waliokuja kwa kupishana kwa muda kidogo.

Dakika kama kumi na tano ajenti wote kumi na mbili wa kambi ya mzalaneo walikuwandani ya kambi yao nyingine ndani ya eneo la Kiwangwa , hii sehemu hakuna ajenti aliekuwa akifahamu uwepo wake Zaidi ya Damiani na Janeth. .

Kwa nje ilionekana kama nyumba ya kawaida ya kuishi watu wenye maisha ya juu lakini chini ya nyumba hio kulikuwa na kila kitu tena Zaidi ya vitu vilivyokuwa ndani ya ‘basement’ ya Mzalendo kurasini lakini hii ikiwa ni ya kisasa Zaidi. .

Kila mmoja alishangaa baada ya kuoneshwa eneo hilo .

“Mimi na Damiani tulikuwa tukijua kuna siku jambo kama hili litatokea na ndio maana kambi hii iliweza kujengwa na kuanzia leo tunahamishia makao yetu yote mahali hapa ” Aliongea Janeth na kumfanya linda aliekuwa katika hali ya hudhuni kutabasamu , jambo ambalo hata Janeth lilimshangaza kwani hakumzoea Linda kwa hali aliokuwa nayo .

Baaada ya masaa kadhaa yaani saa mbili kamili za usiku , ajenti hawa walikuwa wapo bize kuangalia kama ni kweli kambi yao ilikuwa imegundulika , kwanni licha ya kwamba waliweza kufika mahali hapo , lakini walikuwa hawana uhakika asilimia mia moja kwamba eneo lao la mwanzo limegundulika , katika kufatilia ndipo muda wa saa tatu walipoweza kushuhudia kitu ambacho kiliwafanya kila mmoja azibe mdomo , kwani eneo lote la kiwanda chao lilibakia wingi zito mara baada ya kushuhudia ndege ikiachia bomu .

Hakuna alieweza kuamini kwamba watu hao wangeweza kuchukua hatua ya namna hio , walijikuta wakiongopa kwa wakati mmoja kwa tukio hilo .

“Shit , hii ni lazima tulipe” Aliongea Janeth kwa hasira huku akipiga ngumi kwenye meza .
TUTAENDELEA , RATIBA NI VIPANDE VIWILI KWA SIKU
MAWASILIANO NI WHATSAPP TU TUMA MESEJI 0687151346
Hatar sana
 

SURA YA 21​

Upande wa huku hospitalini yule baba aiekuja na kijana huyu hospitalini , alikuwa katika hali ya wasiwasi sana na hii ni baada ya kumtafuta Hassani kila kona pasipo kumuona , alijikuta akichanganyikiwa na kuogopa kwa wakati mmoja , alihofia Hassani asije akafanya kitendo hatarishi , kwani alikuwa kwenye majonzi.

Mwanadada Lisa alionekana ni mwenye kuguswa sana na tukio lile . hali ile ilimfanya kukosa amani na kujikuta akiomba wenzake ruhusa kwamba anarudi nyumbani walikokuwa wamepanga , kwani walikuwa ndani ya hospitali hii ya Bombo kwa ajili ya mafunzo ya vitendo .

Baada ya kurudi nyumbani alijikuta akikosa raha kabisa , ni kama mtu ambaye alikuwa akikukumbuka matukio ya nyuma ambayo yalimkosesha Amani , baada ya kuona mawazo bado yanamwandama , alitoka ndani na kisha alisogea upande wa barabarani na kuita bodaboda iliompeleka mpaka mtaa wa Raskazoni sehemu ambayo alikuwa akipendelea sana kukaa pindi anapokuwa na mawazo .

Baada ya kushushwa alijikuta akitembea taratibu sana kutafuta sehemu ya kukaa na ile anageuza upande wa kulia alijikuta akimuona yule kijana aliekuwa hospiutalini akilia , Lisa alijikuta akisogelea na kukaa kwenye kile kimbweta alichokuwa amekaa huyu kijana.

“Pole sana”Ni sauti iliosikika kwa mara ya pili kwenye masikio ya kijana Hassani na kujikuta akigeuza macho yake na kumwangalia mtu anaempa pole , maana hakuwa akijua kuwa pembeni yake kulikuwa na mtu aliekuwa amekaa .

Kijana huyu ambae alionekana kuwa na maisha Duni kutokana na maazi yake aliokuwa amevaa , alijikuta akimwangalia mwanadada huyu mwenye uzuri wa ajabu .

Lakini Lissa ni kama alikuwa amefungulia kilio kwa wakati mwingine kwa kijana huyu , kwani alianza kulia tena kwa kwikwi akionyesha alikuwa kwenye machungu makubwa sana.

“Nimemuua baba , sistahili kuonewa huruma”Aliongea kijana huyu jambo ambalo lilimfanya mwanadada huyu kushangaa ni kwanini kijana huyu anatamka neno kama hilo .

“Sio kweli hupaswi kujilaumu , kila kitu hutokea kwasababu ni mipango ya Mungu”Aliongea mwanadada Lisa huku akionekana kumuonea huruma kijana huyu .

“Kifo cha baba nimekisababisha mimi , na wala sio mpango wa Mungu”

“Sio kweli ni mipango ya Mungu usiseme hivyo”

“Kama Mungu amenionyesha hili jambo kabla ya kutokea , huu sio mpango wa Mungu hata kidogo , mimi ndio wa kupaswa kulaumiwa”Aliongea na kisha alinyanyuka na kuondoka .

Hakika maneno haya yalimchanganya sana mwanadada huyu Lisa , hakuelewa ni kwanini kijana huyu anaongea maneno hayo , alitamani sana kujua ni kwasababu ipi kijana huyu alikuwa akisema amemuua baba yake ,jambo ambalo ni mara chache sana kulisikia ,na hata kama ni kweli kwannini kijana huyo alikuwa akili ilihali alimuua baba yake , na hata kama ilikuwa ni nahati mbaya je ilikuwaje , hayo yote yalikuwa ni maswali aliojiuliza Lisa huku akiendelea kuangalia maji ya bahari .

*****

Naam Ndani ya kijiji cha Nkumba wilayani Muheza ndani ya nyumba moja ndogo sana iliokuwa imeezekwa kwa nyasi tofauti na nyumba zote zilizokuwepo ndani ya kijiji hiki , walionekana baadhi ya wanakijiji waliokuwa na hali ya simanzi kwenye nyuso zao , na hii ni mara baada ya kupokea mwili wa Mzee Nyangwe aliekuwa amefariki ndani ya hospitali ya Bombo Tanga .

Licha ya mazingira kuwa finyu ndani ya eneo hilo , lakini watu walionekana kujaa kwelikweli,huku kijana Hassani aliekuwa amejibanza pembeni ya nyumba yao alionekana ni mwenye huzuni kweli , mrafiki zake kutoka shule ya sekondari Nkumba walikuwa wakimpa pole lakini badi hawakuweza kutoa hali ya huzuni aliokuwa nayo kijana huyu .

Baada ya kama masaa manne kupita ndipo mwili wa marehemu ulitolewa nje na Shekhe alianza kuswali dua kwa ajili ya kuombea mwili huo , kitendo ambacho kilifanyika kwa lisaa na baada ya hapo safari ya kuupeleka kwenye nyumba yake ya milele ilianza , vijana walipokezana kubeba mwili huo kwa kujipanga njiani kuelekea lilipo shamba la Mzee Nyangwe sehemu ambayo ndio kaburi lake lilikuwa limechimbwa.

Ni ndani ya masaa kadhaa baada ya kuupeleka mwili wa mzee Nyangwe katika nyumba yake ya ,milele , muda wa saa sita kamili ndani ya nyumba hii ya mzee Nyangwe kulionekana kumepoa kutokana na kwamba maziko yalikuwa yamekwisha kufanyika na hakukuwa na lingine la kufanyika hapo nyumbani , kwani familia mzee nyangwe maisha yake ya hapo kijijini yalikuwa ni ya kimasiikini sana , kiasi kwamba hata kwenye huo msiba hakuna chochote kilichokuwa kimepikwa.

Ni karibu watu watano tu ndio waliiokuwa wamebakia hapo nyumbani mmoja akiwani rafiki yake wa karibu wa Hassani na wengine walikuwa ni family ya mzee Kitasa ambae ni yule aliemsindikiza Hassani Hospitalini.

Wakati hayo yakiendelea mara baada ya dakika chache walionekana vijana kadha wakiingia ndani ya eneo hilo huku wakiwa wameongozana na mwanadada Lisa ambae haikueleweka amefikaje ndani ya kijiji hicho , , watu wengi wa kijiji hicho walimshangaa sana mwanadada huyo , hasa pale alipoeleza kwamba amekuja kwenye msiba wa Mzee Nyangwe Jambo ambalo liliwashangaza wanakijiji hawa , kwani walikuwa wakimjua mzee ?nyangwe hakuwa na ndugu mjini na juu ya yote ni mwanadada huyu kuja akiwa na gari la kifahari . .

Hassani alijikuta akishangaa sana ujio wa mwanadada huyu , kwani katika kumbukumbu zake ni kwamba mara walipoonana kule Raskazoni hawakuongea chochote Zaidi ya Hassani kunyanyuka na kuondoka .

“Pole sana”

Ni neon ambalo kwa mara ya tatu mwanadada huyu analitamka akimwambia Hassani.

“Asante”Aliongea Hassani huku akimwangalia kwa Mshangao wanadada huyu .

“Karibu sana Dokta kiti”Aliongea Mzee Kitasa kwani alikuwa akimkumbuka mwanadada huyu kama moja ya madaktari waliokuwa wamemfanyia mzee Nyangwe upasuaji jambo ambalo lilimshangaza kidogo Hassani.

Lisa alieleza kwamba amekuja kwa ajili ya msiba , lakini pia alieleza kuwa alikuwa amegunswa na maneno ambayo kijana Hassani alikuwa akiyatamka , alitaka kujua ni kwanini kijana huyo alikuwa akisema kwamba yeye ndie aliemuaa baba yake

Na hapo ndipo alipoweza kusimuliwa kisa ambacho kilimsisimua na kumsahangaza sana mwanadada huyu .

*****

Kwa majina yangu halisi naitwa Hassani Hamisi Nyangwe nimezaliwa hapa hapa kijijini kwetu na kukulia hapa hapa , mpaka kufikia umri huu wa miaka kumi na sita nikiishi na baba yangu Nyangwe , kwani mama yangu alifariki punde tu baada ya kunileta duniani.

Maisha yetu kwa ujumla sio mazuri sana na naweza kusema kwamba kwa hapa kijijini ni familia yetu pekee ambayo ilikuwa ni ya umasikini uliokithiri , lakini licha ya hivyo sikuwahi hata mara moja kujilaumu kuzaliwa katika aina hii ya familia , kwani nilichokuwa nikiamini katika maisha yangu ni kwamba Mungu ndio mpaji wa yote.

Licha ya umasikini wetu nilikuwa nikimpenda sana baba yangu mzee Nyangwe na hata yeye ia alikuwa akinipenda sana , naweza kusema kwamba tokea nifikie umri wa kujielewa Mzee Nyangwe kwangu ndio baba ndio mama kwangu na kwangu nilimchukulia kama zawaidi ambayo Mungu amenipa

Maisha yetu hapa kijijini kwa ujumla wake licha ya kuwa masikini , yalikuwa ni ya furaha sana , kwani mimi na baba tuliishi maisha kama washikaji , na tulikuwa tumezoeana sana kiasi kwamba hata baadhi ya wanakijiji walikuwa wakishangaa namna ambavyo nilikuwa nimemzoea mzee .

Lakini licha ya furaha niliokuwa nayo katika maisha yangu , kuna jambo moja tu ambalo lilikuwa likinisumbua sana katika maisha yangu na hili ni jambo ambalo nilizaliwa nalo , sikuwahi kujua uwezo huu ambao nilizaliwa nao ulikuwa ukimaanisha nini katika maisha yangu na siku niliokuja kuanza kujua nina uwezo huu ni kipindi nikiwana miaka kumi.

Ilikuwa ni siku ya ijumaa jioni baada ya kumaliza kujisomea kwani kipindi hicho nilikuwa darasa la pili, kama ilivyokuwa kawaida baada ya kusoma nilipanda kitandani na kuutafuta usingizi , kitanda ambacho nilikuwa nikilala na baba , kwani nyumba yetu ilikuw ani ya vyumba viwili tu yaani jiko na sehemu ya kupikia .

Basi wakati nikiwa kwenye usingizi ilinijia ndoto nikiwa naenda shule asubuhi siku ya jumatatu , siku ambayo kwenye ndoto niliona ni siku ambayo ilikuwa na mvua, na hata mwendo ambao nilikuwa nikitembea ni wa kukimbia ili kuepuka kuloanisha nguo na madaftari , basi wakati nafika shule ya sekondari Nkumba , shule ambayo ilikuwa imepaka na shule ya msingi Nkumba , nilijikuta nikiteleza na kutumbukia kwenye mtaro ambao ulikuwa ndio kama mpaka kati ya shule ya sekondari na ya msingi Nkumba , na kutokana na kwamba siku hio mvua ilikuwa imenyesha sana na ule mtalo ulikuwa umejaa maji machafu , yalinichafua mwili mzima na kufanya wanafunzi wenzangu ambao walikuwa wamesimama kwenye korido za madarasa kunicheka .

Kabla ya ndoto kuisha nilijikuta nikiamshwa na baba .

“Wewe hassani Amka kumekucha tujiandae twende shambani”

Basi niliamka baada ya baba kuniamsha na niliwasha moto na kuchemsha mihogo ambayo kwa kipindi hicho ndio kilikuwa chakula chetu kikubwa , kwani ni zadi ya miezi tisa mvua hazijawahi kunyesha na hata msimu wa kulima mahindi ulikuwa unakaribia kupita , lakini mvua bado haikuwa hata na dalili.

Basi hatimae tulienda shambani na kulima na kurudi nyumbani muda wa jioni huku tukiwa tumechoka sana .

“Hivi Hassani mvua isponyesha sijui maisha yatakuwaje miezi ijayo , maana sio kwa hili jua”Aliongea mzee huku akirusha Jembe chini .

“Nimeota mvua itanyesha Jumatatu”

“Hio ni ndoto tu , sidhani kama itanyesha” Aliongea baba na mimi nikacheka na kupotezea na hata siku hio ilipita na siku pia ya jumapili ilipita na siku ya jumatatu ikafika , siku ambayo nilichelewa sana kuamka kiasi kwamba baba ndie alieniamsha .

“Wewe Hassani amka mvua imepungua uwahi shuleni utachelewa”Aliongea baba ambae alinifanya nikurupuke na kuanza kujiandaa kuelekea shuleni , huku nikiwa nimechelewa kweli halafu wiki hio iliokuwa inaanza ilikuwa ni zamu ya mwalimu Bony , mwalimu ambae alikuwa akiogopeka sana kwa kuchapa , alikuwa ni mkurya na alikuwa na kajimsemo kake akitaka kukuchapa anakwambia “Okoa muda” na hata kwenye meza yake ofisini alikuwa ameandika hilo neno la “Okoa Muda” sasa shuleni ndio tulikuwa tunamuita kwa jina hilo la Mzee wa kuokoa Muda , na siku ukiona mwalimu huyu anakwambia okoa Muda basi jua tu anamaanisha lala ule zako ambapo ukiamka baada ya kichapo wiki nzima utakuwa unakaa kwa maumivu mengi sana darasani na pengine usije kabisa shuleni.

Basi nilijiandaa harakaharaka na kunywa chai isiokuwa na sukari na kisha ninakimbia kuelekea shuleni huku mvua ikiwa inayesha japo sio sana , niliungana na wanafunzi wenzangu na kuendelea na safari , huku nikiwa nimesahau kabisa ndoto niliokuwa nimeota usiku wa kuamkia jumamosi , basi ile nilivyofika katika mtalo nilijikuta nikteleza na kutumbukia mtaloni na kuchafuka mwili mzima , huku wanafunzi wenzangu wakiwa wanazomea na kucheka , hakika ilikuwa ni aibu sana kwangu , nilijiangalia na kujiona sifai kuendelea kubaki hapo shuleni na kugeuza taratibu kurudi nyumbani kwani nisingeweza kuendelea na masomo kwa namna ambavyo nilikuwa nimechafuka na nilikuwa nikitoa harufu.

Sasa wakati narudi ndio nikaanza kukumbuka ile ndoto niliokuwa nimeota , hakika nilishangaa kabisa , kwani kila kitu kilichokuwa kwenye ile ndoto ndio kilichokuwa kimenitokea nilishangaa lakini mwisho wa siku niliipotezea japo pia nilimwambia baba , lakini hata yeye hakuizingatia sana.

Basi siku zilipita na baada ya wiki nilijikuta nikiota ndoto nyingine na hii ilikuwa ni ndoto ambayo nilimuona baba aking`atwa na nyoka , ndoto hii wakati naona ilikuwa ni siku ya jumaanne kuelekea Jumatano na jambo la kushangaza ni kwamba siku hio hio ya Jumatano wakati narudi shuleni nilipokea taarifa kutoka kwa mke wa mzee Kitasa kwamba baba ameng`atwa na nyoka na amepelekwa hospitali ya Teule , taarifa hio ilinishitia mno na kunishangaza kwa wakati mmoja , kwani nilichokuwa nimeota ndio hiko hiko kilichokuwa kimetokea na nilichokuwa nikitaka kuhakikisha ni sehemu ambayo baba alikutwa na janga hilo , na baada ya siku mbili za kutoka hospitali ya Teule ndio nikamwambia baba anionyeshe mahali ambapo alikutwa na mkasa huo wa kung`atwa na nyoka na sehemu alionipeleka ni pale pale ambapo nilipashuhudia ndotoni na hili swala niliamua kumsimulia na baba akaniambia kwamba .

“Hizo ni ndoto tu Hassani hazina maana yoyote “

“Lakini baba hii ni mara ya pili naota kitu kinatokea kweli bahati mbaya haitokeagi mara mbili”

“Basi tufanye hivi kama itatokea umeota mara ya tatu na ikawa kweli nitakupeka kwa mzee Kigo asome nyota yako huenda ukawa Nabii”Aliongea mzee na mimi nikakubaliana nae.

Basi ilipita mwezi namini nilisahau kabisa lile swala na tulikuwa kwenye mfungo wa Ramadhani mwezi wa tano , kipindi ambacho tulikuwa tukielekea kumaliza muhula wa kwanza shuleni ili tufunge shule .

Basi siku moja niliota nyumba ya Mzee Kesi ikiungua na moto huku yeye na familia yake yote wakiwa ndani , na tena ilikuwa ni muda wa usiku kabisa , Mzee kesi alikuwa ni moja ya watu waliokuwa na pesa hapo kijijini , kwani alikuwa akimiliki ‘Chain Saw’(mashine ya kukatia miti na mbao) na kupitia mashine yake hio alikuwa akijipatia pesa nyingi sana kwa kuuza mbao lakini pia kukodisha , mzee huyu alikuwa na familia ya watu saba , mke wake, yeye mwenyewe , Ratifa ambae alikuwa Sekondari Nkumba , Abasi ambaye alikuwa ni mkubwa kabisa ashamaliza shule ila alikuwa akiishi na wazee wake oamoja na wajukuu zake watatu mmoja akiwa ni mtoto wa Abasi aliezaa na mwanamke ambaye alimkimbia na wengine wawili walikuwa ni watoto wa mtoto mkubwa wa mzee Kesi aliekuwa akifahamika kwa jina la Mwantumu ambae alikuwa jijini Dar es salaam.

Basi siku ile kwangu nilikuwa na wasiwasi sana juu ya ile ndoto na mbaya Zaidi sikuwa nyumbani Nkumba siku hii , kwani tulikuwa tumeenda Magila kupasua mawe mimi na baba na Mzee Kitasa , wakati tupo njiani nilimweleza mzee huyu juu ya ndoto hio lakini hakuwa ni mtu wa kuzingatia namimi nikapotezea .

Nakumbuka siku hii tuliweza kurudi muda wa saa moja kasoro hivi na wakati tunafika Nkumba bahati nzuri niliweza kukutana na Ratifa ambae alikuwa amebeba ndoo ya maji akiwa ametangulizana na mtoto wa Abasi aliekuwa akifahamika kwa jina la Adam aliekuwa anasoma Chekechea akiwa na yeye amebeba maji kwenye kigaloni cha lita tatu .

“Dada Rat nimeota ndoto nyumba yenu inaungua”

“Wewe mtoto hebu acha kutuwangia bhna” Aliongea Ratifa kwa dharau na mimi sikumjali sana nikasepa zangu kwani kipindi hiki nilikuwa mtoto na hata ningemwambia mtu asingeniamini. .

Basi nilikuja kuamshwa na vilio vya watu muda huo ilikuwa ni saa Sita za usiku na hata nilipoangalia pembeni baba sikumuona , nilijikuta nikitoka nje na ile natoka tu niliona wingu la moshi likiwa limetanda uelekeo wa nyumba ya Mzee kesi , lakini ile nashangaa sauti za vilio huku nikisia wamam wanaongea kwa sauti ‘Nyumba ya mzee kesi jamani inaungua na wenyewe wapo ndani”

Kusikia hivyo tu nilijikuta nikipatwa kama mshituko wa moyo huku mapigo ya moyo yakienda kwa kasi sana , nilitoka na kuelekea upande huo , sehemu ambayo ulikuwa ukivuka nyumba nne tu unakuwa umefika na ile nafika ni kama vile nipo ndotoni , kwani vile vile moto ulivyokuwa unawaka ndio nilicyo ota , huku watu wakihangaika kuokoa watu waliondani , na maji kumwagwa , lakini ni kama moto ulikuwa ukizidi .

“Bahati nzuri ni kwamba wazee wa kijiji walifanikiwa kutoboa tundu na kuanza kuitia jina la Mzee Kesi wakimwambia atoke lakini tulichoweza kusikia ni neno moja tu kwa mzee Kesi , kwamba hawezi kutoka ilihali familia yake yote imeshateketea kwa moto , wanakijiji walijaribu kumbembeleza mzee Kesi atoke , lakini halikusaidia kwani hakutoka.

Mpaka inafika saa tisa za usiku moto ulikuwa umezima , lakini vilio vilikuwa vya aina yake , sio watoto sio wazee watu walishindwa kujizuia ,kila aliekuwa akiangalia miili iliokuwa imetolewa na kupangwa nje ikiwa imeungua vibaya alijikuta akilia sana , Siku hii pia nililia mno , yaani sana huku nikijiona mkosaji sana .

Tukio hili liliniathiri vibaya sana kisaikolojia kiasi kwamba hata usiku nilikuwa nikiogopa kulala kwa kuhofia kuota jambo baya , na ukiachilia kwamba hiki kipindi bado nilikuwa mtoto ,,Baba nae alijaribu kuniweka sawa , lakini bado niliogopa sana kwa wakati mmoja .

Basi baada ya wiki kupita mzee alinichukua na kunipelka kwa mzee kigo kwa ajili ya nyota yangu kuangaliwa

Mzee kigo alikuwa ni mganga aliekuwa akifahamika sana pale kijijini na kuogopeka sana , alikuwa akifichua wachawi wengi lakini pia kutibu watu wengi wenye shida mbali mbali , na wengi walikuwa wakitoka mpaka mikoani kwa ajili ya kuja kupata huduma kwa mzee Kigo.

Basi nilipokelewa na kuanza kufanyiwa tiba pale , akachukua kioo chake flani hivi alikuwa akikipaka unga flani ambao sikuwa nikiujua halafu anakirusha juu kinatua chini huku anaongea maneno anayoyajua yeye halafu anaangalia tena , na anakirusha tena juu na kinatua chini , , alivyomaliza , alikichukua akaitumbukiza kwenye maji yaliokuwa yamejaa kwenye chungu kikubwa na kisha aliweka unga flani hivi kama majivu na kisha akakitoa kile kioo na kukifuta na kisha akanisogelea na kukiweka kwenye uso wangu , yaani mimi nikiangalia nyuma ya kioo na kisha yeye akiangalia mbele ya kioo.

Baada ya dakika mbili alijikuta akishituka sana na kukidondosha kile kioo na kisha akanza kuniangalia kwa umakini huku akiokota kile kioo na wakati huo baba alikuwa anaangalia tu kinachoendelea .

Baada ya kama dakika kumi hivyo alionekana kumaliza kile alichokuwa anakifanya na kisha alinipa kisu na kuniambia nichukue Jogoo ambae tumekuja nae , maana kwa huyu mzee sheria zake kama unataka kusomewa nyota yako , basi unatakiwa kuja na jogoo mweupe na mchanga wa mlangoni , yaani pale kwenye mlango wa kutokea unachimba chini na unachukua mchanga..

“Tayariii ….. Tayariii …. Hassaniii …” aliongea kwa sauti yake ya kutisha pale na tulikuwa tayari kwa kupokea majibu

SURA YA 22​

“Kijana umezaliwa na bahati kubwa sana kwenye maisha yako , Mababu wa ukoo wako wamekupatia uwezo wa kutambua mambo yatakayokuja”

“Unamaanisha nini Mzee Kigo?”Aliuliza baba

“Hassani ni Mlinzi mkuu wa kijiji hiki , mababu wa koo zote hapa Nkumba wamemchagua kama mlinzi , ilikuwa kosa kubwa sana kuruhusu familia ya mzee Kise kuungua na moto , ulitakiwa kuwaokoa, maana ni jukumu la mababu wa koo waliokupatia na hivi sasa wamekasirika na wanapaswa kutulizwa” aliongea Mzee Kigo na kumfanya Mzee wangu kushituka na kujawa na wasiwasi , kwangu mimi sikuwa na imani sana na mambo ya kiganga tofauti na Mzee ambae yeye alikuwa ni muuminni mzuri tu.

“Kwa hio tunafanyaje mzee Kigo”.

“Kafara ya Mbuzi kwa kila koo inatakiwa kufanyika kwa ajili ya kuwatuliza mababu wa koo”.

Basi kama alivyolekeza tuliweza kutoa kafara ya Mbuzi ambayo tunachinja huko juu milimani kabisa kwenye pango moja , pembeni kabisa na kilipo chanzo cha maji ambayo ndio hutumiwa na watu wa kijijini kwetu kwani kulikuwa kumeunganishwa mabomba .

Basi baada ya hapo niliendelea kuota ndoto za kweli tu na katika kuota ndoto hizo , hakuna siku ambayo hata moja niliweza kuzuia ndoto mbaya kutokutokea , yaani nilichoweza mimi ni kuota tu lakini sikuweza kuzuia kile nilichokuwa nikiota kutokutokean kama ni kibaya , licha ya maneno ya Mzee Kigo kwamba ninatakiwa kuzuia.

Basi baada ya miaka kupita , siku ya ijumaa kuelekea jumamosi , mzee wangu muda wa usiku aliweza kuniambia kuwa siku ya kesho wanaelekea Muheza mjini kwa ajili ya kuuza vitunguu na Mzee Kitasa, huku akiniachia kazi ya kwenda kumwagilia pilipili asubuhi na mimi nilikubali na kisha tukala tukalala , basi usiku niliweza kuota ndoto mzee anagongwa na pikipiki Muheza mjini.,ndoto ambayo nilivyokuja kushituka ilikuwa ni saa kumi na moja kama na nusu hivi asubuhi na nilipoangalia pembeni sikumuona mzee ,nilijikuta nikikurupuka na kutoka nje kumwangalia kama mzee yupo lakini sikumuona , nilichokifanya ni kutulia na kusubiria , kwani mzee aliniambia ni asubuhi na huwaga hana ile tabia ya kuondoka pasipo kuniamsha , nilirudi ndani na kusubiri mpaka saa moja na robo ndipo hofu ilipo nijaa na kujua lazima mzee atakuwa amekwisha kwenda Muheza , niliinuka mbio na kwenda nyumbani kwa Mzee kitasa na nilimkuta mke wake akiwa nje anafagia nilimsalimia na kisha kumuuliza kama mzee alikuwa ashaenda mjini na jibu lake ndio liliniacha hoi kwani aliniambia kuwa walikwisha kwenda toka saa kumi na moja .

Nilijihisi kuchangayikiwa na hilo hata kwa mama Jabu aliliona hilo .

“kwani kuna nini Hassani?”

“Baba atakufa , nimeota anakufa” Niliongea na mama Jabu alijikuta akishituka mno kwani pia hata yeye alikuwa akijua uwezo wangu huo wa kuota vitu vinatokea .

“jamani jamani sasa tunafanyaje ?”

“naenda ,mjini mama Jabu niazime hela kidogo”

Basi mama Jabu alinipatia elfu moja na miatano ya nauli na kisha nikapanda bodaboda kuwahi mjini kumuokoa baba , safari ambayo kama ningejua nisingeenda , kwani ile nafika uwanja wa jitegemee , sijui ilikuwaje , kuna mtoto alikuwa barabarani na sisi tukawa tupo kwenye spidi kali halafu mbele yetu kulikuwa na gari ya Tanesko inakuja , sasa katika harakari za kumkwepa mtoto yule bodaboda alijikuta akichukua uelekeo wa kwenda hopitali ya Teule na hapo ndipo nipokuja kushitukia baba yupo mbele yetu na pikipiki ilikuwa kwenye spidi kali ,na kilichotokea ni kwamba baba tulimgonga na kumrusha upande mwingine na akaenda kuvaa chuma cha mashine ya kupasulia mbao upande wa kushoto na kujigonga kisha akatumbukia mtaloni huku damu zikiwa zimetapakaa .

****

“Pole sana Hassani , sasa hukujiona kwenye hio ndoto ukiwa kwenye pikipiki?”

“Hapana sikujiona nilchoota ni baba kugongwa na pikipiki tu ila sikujua pikipiki hio ndio itakuwa nitakayopanda” Alijibu Hassani huku mwanadada Lisa akiguswa mno na simulizi hio , licha ya kushangaa uwezo aliokuwa nao Hassani wa kuota mambo yanayotokea kweli , lakini swala la ajali ya baba yake kusababishwa na yeye mwenyewe katika harakati za kumuokoa lilimgusa mno , na aliona ni kweli kijana huyu alikuwa na haki ya kutamka yale maneno ya kwamba amemuua baba yake .

“Mimi naamini kuna kitu cha ziada juu yako , labda hujakitambua bado”

“:Sidhani kama kuna kitu kama hicho ,, hii ni laana kwangu , haiwezekani niote vitu ambavyo ni vya kweli ila nishindwe kuzuia matukio mabaya ninayoota”

“Ushawahi kutoa tukio lolote ambalo sio la kutisha ?”

“Sijawahi kuota “

“Basi kunasababu ya kuwa hivyo Hassani , naamini ni uwezo ambao Mungu kakupatia akiwa na sababu zake”

“Siamini hivyo Sister”

Basi mwandda huyu alitoa rambirambi yake na kisha kuaga huku akiahidi kurudi Nkumba akiwa na jibu juu ya uwezo wa Hassani.

Je simulizi hii inauhusiano gani na Book of all names tuendelea tulipoishia

*****

MIEZI MIWILI BAADA YA MAANDALIZI. ,SIKU MOJA KABLA YA SIKU AMBROSE AKISIMULIWA SIMULIZI YA BOOK OF ALL NAMES

WACO –TEXAS


Ni ndani ya shamba moja kubwa lililokuwa likimilikuwa na bwana mmoja aliekuwa akifahamika kwa jina la Hudson , shamba hili lilionekana kujaa mahindi mengi ambayo yalikuwa akikaribia kuvunwa , kwani yalikuwa kwenye hatua za mwisho , ilikuwa ni muda wa mchana , muda ambao bwana Hudsoni akiwa kwenye banda lake kubwa la Ng`ombe alipokea wageni , mmoja akiwa ni mwanamke rangi ya kiafrika mrembo alievalia suruali ya jeans na tisheti ya Puma , na mwingine alikuwa ni mwanaume pia akiwa ni rangi ya kiafrika alievalia jeans na tisheti nyeupe huku akiwa na koti la suti rangi ya ugoro . .

Mabwana hawa walijitambulisha mmoja akiitwa Linda na huyu mwanaume alijitambulisha kama Zakayo , ujio wa watu hawa ndani ya nyumba ya bwana Hudsoni ilikuwa ni kwa ajili ya kukodi Ghala lake moja la kuhifadhia mahindi kwa muda wa wiki moja , jambo ambalo lilimshangaza bwana Hudson kwa watu hao kuomba Ghala lake ambalo ni mwezi uliopita tu alitoka kulisafisha kwa ajili ya kuweka mahindi mapya na kutoa yale ya zamani .

“Mnahitaji ghala langu kwa madhumbuni yapi?”

“Hilo hatuwezi kuliweka wazi Mr Hudson ila tatalipa pesa nyingi sana Zaidi ya mara mbili ya bei utakayotutajia kukodi eneo hilo kwa wiki moja”

Mzee Hudsoni mwenye umri wa miaka 61 alijikuta akishawishika kwa utayari wa watu hawa kutaka kumlipa mara mbili ya pesa ambayo atawatajia , lakini licha ya kushawishika huko hakuwa tayari kutoa Ghala lake , kwani alikuwa na wasiwasi wa kile watu hao watakifanya pale tu atakapo toa hilo Ghala lake ,na maamuzi alioyafanya ni kutaja bei kubwa Zaidi kuliko s thamani ya Ghala lake na hapo watu wale yaani Zakayo na Linda walitabasamu na kuzidisha mara tatu ya hela aliotaja mzee huyu na kisha wakamwambia watampatiakiasi hicho , jambo ambalo liliibua mshangao na matamanio ya kiasi hicho cha pesa kwa mzee Hudson na moja kwa moja alikubali na kuwapeleka watu hawa kwenye Ghala kwa ajili ya kuangalia lakini pia na kuwaachia mlango .

Lakini licha ya hivyo mzee Hudsoni alitaka malipo yake hapo hapo na ilichukua dakika moja tu malipo yaliweza kufanyika na kuingia kwenye akaunti yake ya benki , kitendo ambacho mzee huyu alitoa macho , kwani hakuwahi kuzania kama anaweza kupata kiasi hiko cha pesa kwa muda mfupi na aliona kwa hela hizo zinamtosha kabisa katika uzee wake na hata asipolima tena .

Basi baada ya Linda na Zakayo kukabidhiwa ufunguo wa ghala hili ambalo lilikuwa na umeme , muda wa saa moja kamili iliingia gari nyingine na hii ilikuwa ikiendeshwa na Erick Peter.

“Kazi nzuri sana mmefanya , lakini ninawasiwasi na mzee Hudsoni asije kuta taarifa”.

“Halafu hilo tumeshau ila nitayaweka sawa na mzee huyu na kutokana na pesa tuliompatia nadhani hatafanya jambo kama hilo”Aliongea Zakayo huku wakisaidiana kutoa baadhi ya vitu kama vile tarakishi , mikoba na mazaga mengine na kuyaingiza kwenye hili Ghala , uzuri ni kwamba hili Ghala lilikuwa limejitenga kwa umbali wa mita kadhaa na nyumba aliokuwa akiishhi Mzee Hudsoni na hata kilichokuwa kinaendelea huku hakuwa ni mwenye kuona .

Ndani ya dakika kadhaa tu , ghala hili liligeuka kama ofisi ya kitehama , kwani kulikuwa na tarakishi moja kubwa na baadhi ya vifaa vingine ambavyo sikujua maana yake , lakini pia kulikuwa na meza na viti , lakini pia kulikuwa na kiti kimoja ambacho kilikuwa wazi , lakini kiti hiki pia kikiwa kimeunganishwa na umeme .

Ilikuwa ni muda wa saa nne kamili za jioni gari nyingine aina ya Range iliingia na kwenda kupaki mbele kabisa ya Ghala hilo . na ndani ya dakika kadhaa tu alionekana Janeth akiwa na mzee mmoja wa kizungu ambae alikuwa amezibwa zura yake huku akiwa na pingu kwenye mikono yake iliofungwa kwa nyuma .

Baada ya madakika sekunde kadhaa mzee alikuwa amekarishwa kwenye kile kiti ambacho kilikuwa wazi lakini kilikuwa kimefungwa na kwa kuunganishiwa umeme .

“Bruno lamberk hatimae upo kwenye mikono yangu”Aliongea mwanadada Janeth na kumvua mzee huyu lile kofia walilokuwa wamemvalisha na hapo mzee huyu aliangalia watu waliokuwa mbele yake kwa mshangao huku akichunguza mandhari ya eneo hilo.

“Janeth unachokitaka kukifanya hutofanikiwa , baba yako alijitahidi sana lakini naamini unajua kilichomkuta watu mnaocheza nao ni watu wa hatari sana na huenda wako njiani kuja eneo hili”Aliongea huyu mzee kwa ujasiri amao ulimpandisha hasira sana Janeth , lakini alijizuia na kutabasamu.

“Tutaona kama utakuwa na ujasiri wa kuongea baada ya kuona kinachoendelea ISLAND X” Aliongea janeth na kisha walifunga karatasi nyeupe mbele ya Bruno na kisha walielekeza Projecta kwenye lile karatasi , huku Linda akimpiga gundi ya mdomo mzee huyu .

Wakati huo hayo nayaendelea Erick Upande wa nje alikuwa akirusha Drones ambazo zilikuwa ni kwa ajili ya kuangalia usalama wa eneo hilo .

Baada tu ya kurudi alisogelea tarakishi ile kubwa na kisha alianza kubonyeza batani kwa spidi na ndani ya dakika chache ule upande kulikokuwa na projecta , projecta mbalimbali kulionekana Picha mbalimbali zikionyesha eneo kubwa la kisiwa.

Na ndani ya madakika kadhaa tu , tu picha ilibadilika na kuonesha eneo la nje la Jumba moja kubwa lililokuwa katikati ya Mikoko likiwa limejengwa kwa ustadi mkubwa sana huku mbele kabisa ya jengoo hilo kukiwa na maandishi makubwa yaliosomeka ISLAND X –U-97 ECLUSIVE HEADQURTER .

Ni kitendo kilichokuwa kikionesha kama Movie kwani ndani ya madakika kadhaa tu , picha zilionekana zikionesha ndani kabisa ya jumba hili , huku watu eneo hili likiwa na makachero waliokuwa wakilinda kuanzia juu ya paa , pembezoni mwa ukuta ,getini na ndani ya eneo hili .

Baada ya madakika kadhaa tu video ile ilionesha eneo la nje ya kisiwa hiki mita kadhaa kutoka kwenye hili jumba , eneo hili lilikuwa ni sehemu ya Ndege kutua yaani kulikuwa na kiwanja kikubwa cha ndege ambacho kwa haraka haraka kilionekana kutosha ndege kubwa ya abiria kutua kwenye hili eneo .

Zilipita dakika chache tu chopa moja ilifika ndani ya hili eneo huku ikiwa na wanajeshi ambao walishuka na Kamba na kuimarisha ulinzi wa hili eneo , hakika ilikuwa ni jambo la kushangaza na ilikuwa ni kama kwenye Muvi .

Yote haya wakati yanaendelea , Janeth ,Linda , Erick pamoja na Zakayo walikuwa wakifatilia kwa ukaribu kabisa , lakini hilo pia kwa upande wa Bruno pia alikuwa akiangalia kile kilichokuwa kinaendelea huku akionekana ni mwenye kuwa na wasiwasi mkubwa.

Baada ya dakika kadhaa za ulinzi kuimarishwa hatimae ndege moja kubwa ya saizi ya kati ilionekana kutua eneo hili na baada ya kama nusu saa hivi , walionekana wanaume na wanawake waliotoka katika hili ndege wakiwa na mavazi yaliokuwa kama yale ya Majaji wanayovaa , na baada ya watu hawa kutoka , walifuatia watu wanne waliovalia nguo nyeusi wakiwa wamebeba kitu kama jeneza , lakini hili halikuwa jeneza ,ni mfano wake tu lakini likiwa la kioo huku watu wale wakiwa wanabeba kwa umakini mkubwa sana .

Baada ya jeneza hilo kushushwa hatimae alionekana , kijana Ambrose alietoka akiwa amevalia Suti akiwa ndani ya hili eneo na wakati haya yote yanafanyika ilikuwa ni mchana kweupe na jambo hili lilidhihirisha kwamba eneo walilokuwepo hao watu ni bara linguine kutokana na utofauti wa muda..

Basi baada ya ya kijana Ambrose kutoka na kuelekea kwenye Gari hatimae alitoka mtu ambae alimfanya Janeth ageuze Macho na kumwangalia Bruno kwa hasira .

Huyu hakuwa mwingine bali alikuwa ni mwanaume ambae alikuwa anafanana kwa kila kitu na mwanaume aliekuwa amefungwa kwenye kiti alichokuwa amekalia Bruno , jambo hili lilimfanya mzee huyu afurukute kwenye kiti chake , jambo ambalo lilimfanya Janeth kutabasamu.

“huu ndio mwisho wa U-97 kuwa na nguvu duniani , tunakwenda kusambaratisha kila kitu mlichokiandaa karne na karne wewe pamoja na hao mashetani wenzako”Aliongea janeth akimwagnalia Bruno na kumfanya mwanaume huyu azidi kufurukuta kwani hakuwa na uwezo wa kuongea neno lolote kwani alikuwa amefungwa na gundi mdomoni.

“Operesheni Island X inaanza kuanzia sasa na nataka wote muwe makini , kwani hili ndio jambo ambalo tulikuwa tukilisubiria kwa muda mrefu na hakutakiwa kuwa na makossa ya aina yoyote ile” Aliongea kijana huyu kwa kujiamini huku akiendelea kuchezesha cidole vyake kwenye komputa .

Naam nini kilitokea mpaka kufikia hatua hii ???????.....

SURA YA 23​

BAADA YA MIEZI MIWILI YA DAMIANI KUINGIA NCHINI MAREKANI , LAKINI PIA KUANZIA SIKU AMBAYO PROFESA MIKE ALAN ANAPOKEA MAAGIZO YA KUMUANDAA AMBROSE

FRORIDA –MAREKANI

Ni siku kadhaa tokea Rania kurudi nchi Australia akitokea Tanzania , sehemu ambayo alienda kwa ajili ya kumtambulisha Erick kwa baba yake , zoezi ambalo halikufanikiwa kutokana na hali ya Peter kupoteza kumbukumbu na kutomkumbuka kabisa Rania .

Siku hii ya Jumatano saa tisa za alasiri ndani ya shule ya North Broward ndani kabisa ya eneo la mgahawa wa shule hii sehemu ambayo wazazi wa watoto mara nyingi hufikia ,wanapokuja kuwatembelea watoto wao walionekana wanaume wawili , mmoja akiwa ni kijana wa makamo alkekuwa amevaa nguo zilizompendezesha na mwingine alikuwa ni mwanaume wa miaka kati ya therathi na tano kwenda juu aliekuwa amevalia suti ya rangi ya zambarau , hawa hawakuwa wengine bali walikuwa ni Erick akiwa pamoja na Joseph...

“Mzee hakikisha akili yako inakuwa na utulivu kama unataka kumuokoa mwanao katika hatari ambayo ipo mbele yake”Aliongea kijana Erick akiwa katika hali ya kirafiki kabisa akimweleza mzee huyu ambae alionekana kuwa katika hali ya wasiwasi mno.

“Nimekuelewa”Aliongea Peter au Joseph akionekana ni mwenye kuvuta pumzi akijiweka sawa , kwani alionekana kutokuwa sawa kabisa.

Baada kama nusu saa hivi ya kukaa pale huku wakiwa wanapata kahawa mara alikuja mwanamama wa kizungu aliekuwa amevalia tisheti yenye nembo ya shule hio.

“Nipo hapa kwa ajili ya kuonana na mwanangu , anafahamika kwa jina la Ambrose Joseph”Aliongea mzee huyu mara baada ya mwanamama kujitambulisha kama Matron.,.

“Okey na huyu mwingine ni nani kwa Ambrose?”

“Huyu ni kaka yake” aliongea mzee huyu na kumfanya Erick kutabasabu .

“Okey ngoja nifanye mawasiliano na uongozi ili mpate utaratibu maalumu wa kuonana nae” Aliongea huyu mzungu kwa Lugha ya kingereza na kisha aliondoka na hazikupita dakika tano alirudi akiwa ameongozana na mwalimu mwingine , huyu hakuwa mwingine bali alikuwa ni mwalimu Nick Jonas , mwalimu aliekuw andani ya shule hio kwa ajili ya kazi maalumu , kazi ya kumfanya Ambrose kupenda mambo ya kale.

Baada ya mwalimu huyu kufika mbele ya meza hii ya mzee Peter alimwamuru yule mama kumuacha sasa aendeelee kuanzia hapo jambo ambalo kidogo lilimshangaza Peter kwani aliekuwa akitarajia kuonana nae hakua huyo kijana bali alikuwa ni mtoto wake Ambrose .

“Naitwa Nick Jonas ni mwalimu na mlezi wa Ambrose “

“Naitwa joseph ni baba wa mtoto Ambrose , nipo hapa kwa ajili ya kuonana na mwanangu”

“Nafurahi sana kuonana na wew Mr Joseph” Aliongea mwalimu Nick huku akiweka tabasamu ambalo kwa Erick aliona taasamu hilo ni la kinafiki huku akiwa amenyoosha mkono kumpatia Joseph.

“Nafurahi pia , lakini sipo hapa kwa ajili ya kuonana na wewe Mr Nick nipo kwa ajili ya kuonana na mwanangu”Jibu hili ni kama lilimfikirisha kidogo Mwalimu Nick na kisha akatabasamu.

“Ambrose hayupo hapa bali yupo katika safari ya kimasomo itakayo chukua muda wa miezi miwili , nipo hapa kw ajili ya kukufahamisha hilo lakini pia kukutoa wasiwasi kuwa mtoto wako yupo kwenye mikono salama”.

Mzee huyu alimwangalia Erick kwanza na kisha Erick alimwangalia Peter na kisha na kumpa ishara ya kukubali.

“Basi sawa mwalimu , nitafika hapa baada ya miezi miwili kwa ajili ya kuonana na Ambrose”..

Basi wawili hawa baada ya kupata jibu hilo kutoka kwa Mwalimu Nick walitoka na kuingia kwenye gari yao huku Joseph akionesha waswasi wa waziwazi .

“Mr Erick kipi kinafuata mpaka hapa naamini mtoto wangu hayupo salama kabisa”

“Punguza wasiwasi mzee , kila kitu kitakuwa katika mpangilio wake kama tu utafata kile ninachokuambia , mwanao yupo kwenye mikono hatarishi na hakuna serikali yoyote duniani itakayokusaidia Zaidi yangu , unachotakiwa ni kufata kile ninachokuambia”

“Kwa hayo nishakubali , ninachotaka ni kujua mpango wako kama unamafanikio yoyote ya kumpata mwanangu”.

Aliongea mzee huyu akiwa ni mwenye wasiwasi , lakini kwa Erick hakuonekana mwenye wasiwasi /tena alichukua simu yake na kisha aliangalia ujumbe ulioingia ambao juu kabisa ya kioo hiko cha simu kuna jina lililokuwa likisomeka STUPID BOSS.

“UNA MIEZI MIWILI TU KULIJUA SOMO LA SIRI”yalikuwa ni maandishi yaliokuwa yameandikwa kwa maneno ya kodi lakini yalioeleweka kwenye kichwa cha Erick , kwani alijua kuwa yalikuwa yakimaanisha kuwa alikuwa na ana miezi miwili tu iliobaki kukamilisha misheni ya kujua simulizi ya Book of all names

Baada ya Erick kusoma ujumbe huu aliweka simu yake mfukoni na kisha akamgeukia mzee Joseph .

“Sikia mpango uliopo hapa ni kuonana na Ambrose na kumshawishi juu ya hatari iliopo mbele yake, lakini ili niweze kumshawishi nitahitaji msaada wako katika hilo”

Aliongea kijana huyu pasipo wasiwasi huku akitoa simu yake na kupiga jina ambalo limesomeka kwene kioo chake kama Damiani.

“Nataka kwenda kuonana na Ambrose kwani kwasasa haifahamiki sehemu alipo na ili kufanikisha hilo nataka kwenda kama Profesa Mike nataka kutumia Advanced full body mask technology(A-FBM).

****


Hakuna kitu ambacho kilimpagawisha kijana Ambrose kama pale alipopata taarifa kutoka kwa mwalimu Nick kwamba anakwenda kuambiwa siri juu ya ufunguo ambao utamfanya kuwa na uwezo wa kufanya kila kitu ndani ya ya dunia , hakika hili lilikuwa ni jambo kubwa nyuma ya juhudi zake za kujituma katika kuijua historia ya kale , kwani aliaminni njia moja tu ya kutimiza malengo yake ni kuhakikisha anashikilia ufunguo uliokuwa unafungua kila mlango wa mafanikio ndani ya dunia hii , na ili kutimiza ile ndoto yake ya kuweka kumbukumbu ambayo itakuja kukumbukwa na vizazi na vizazi.

Ilikuwa ni siku ya Ijumaa siku ambayo kijana /ambrose alikuja kutolewa ndani ya shule hii ya North Broward na maafisa usalama wa UMOJA NAMBA TISINI NA SABA , Ambrose baada ya kuambiwa na mwalimu Nick kwamba watu hao watamfikisha kwa mtu ambae anasiri juu ya ufunguo unaoweza kushikilia kila kitu katika dunia hii hakuwa na wasiwasi Zaidi ya kufatishana na wanasalama hao.

Ni ndani ya dakika chache tu kijana huyu alikuwa ndani ya uwanja wa ndegea wa Frorida International Ariport , sehemu ambayo alipitishwa na wanausalama hawa pasipo hata kufata sheria za hapo uwanjani kwani alikuwa amepitishwa kupitia mlango wa VIP , yaani mlango ambao ulikuwa ukitumiwa na viongozi kupita kama vile maraisi .

Ilikuwa ni ndege moja kubwa ya wastani ya kampuni ya Boeng iliokuwa ndani ya eneo hili la uwanja wa ndege ambayo ilikuwa ni Dhahiri kabisa , kijana Ambrose ndio aliokuwa akitarajia kupanda kuelekea mahali ambapo alikuwa anamamini anakwenda kuonana na mtu ambaye atampatia siri ya namna ya kupata ufunguo utakao fungua kila mlango ndani ya dunia hii.

Naam baada ya madakika kadhaa ndege aliokuwa amepanda kijana Ambrose ilikuja kusimama ndani ya kisiwa kimoja kilichokuwa kinamaandishi yaliokuwa yanasomeka kwa jina la ISLAND Y WORLD TOP SECRET ARCHIVES

Hiki ni kisiwa ambacho hakikueleweka uelekeo wake , japo ni kisiwa ambacho kilikuwa ndani ya nchi ya Marekani , lakini jimbo halikufahamika , na hio yote ilikuwa ni kuhakikisha ulinzi wa eneo hili , kwani pia licha ya kwamba eneo hili halikuwa likifahamika lakini pia kulikuwa na ulinzi wa hali ya juu sana , kwani kulikuwa na makachero wengi waliokuwa wamevalia suti nyeusi wakiwa na siraha.

Baada ya kijana huyu kushuka na kuja kupokelewa na wanaume wawili , na wanawake wawili ambao walijitambulisha kwa kijana huyo kama wafanyakazi wa sehemu hio ambao ilitumiaka kama sehemu ya siri sana duniani kwa ajili ya kutunza kumbukumbu.

Kijana huyu alishangazwa na mandhari ya hili eneo , lilikuwa ni jumba kubwa la kifahari lililokuwa limeunganishwa na maktaba kubwa ambayo ilikuwa na mavitabu na nyaraka mbalimbali za mambo ya kale na sasa.

Kijana huyu alijikuta akistaajabu mno , kwani vitu vingi viliandikwa kwa lugha asiokuwa akiielewa , wakati kijana huyu akiendelea kushangaa mara alitokea mzee mmoja wa kizungu , huyu mzee alionekana kuwa umri umeenda sana , kwani hata tembea yake na ngozi yake vilithibitisha hili.

“Karibu sana Ambrose ndani ya sehemu hii muhimu sana ndani ya dunia hii ,Niite Mr Kolfan the Great Grandfather, mimi ndio muongozaji mkuu wa makataba hii” Aliongea mzee huyu kwa sauti yake iliokuwa imenyongea sana na Ambrose alikubali utambulisho huo.

“Nafurahi sana kukufahamu Mr Kolfan”

“ Karibu sana , lakini pia hongera kwa kuteuliwa katika kuifahamu siri kuu ya ulimwengu”sifa hizi zilimfanya kijana huyu mwili kumsisimka mno na aliamini kitu ambacho anakwenda kukijua muda mfupi ni kitu kikubwa sana katika maisha yake na ni mwanzo wa yeye kuanza kuwa na nguvu duniani.

“Asante sana “ waliongea huku wakiwa wanatembea , huku mzee huyu akiwa anamuonesha mambo mbalimbali yanayopatikana kwenye maktaba hio .

“Kila kitabu na nyaraka unaziziona hapa , ni taarifa za siri sana ambazo ni watu wachache sana wanazifahamu , na wewe katika maandalizi yako ya kuifahamu siri kuu ya ulimwengu huu inakubidi upitie baadhi ya nyaraka , lakini katika miezi yako ya maandalizi unatakiwa kujua sababu kuu ya kuundwa kwa UMOJA NAMBA TISINI NA SABA .

“UMOJA NAMBA TISINI NA SABA ??”

“Ndio unaonekana kushangaa juu ya jina hilo , lakini hilo ndio jina linalotambulisha jumuiya ya siri yanye nguvu duniani, nguvu yao ndani ya jumuia hii inashikiliwa na siri kuu ya ulimwengu , siri ambayo muda si mrefu unakwenda kuijua na kukufanya mtu mwenye nguvu sana ndani ya U-97 na duniani”

Kila neno lililokuwa linatoka kwa Mr Kolfani lilikuwa ni dhahabu kwenye masikio ya kijana huyu , na kwa jinsi alivyokuwa na hali ya udadisi katika maisha yake , aliamini ndani ya miezi hio miwili ya kuwa ndani ya Maktaba ya siri duniani atakuwa amejua mambo mengi sana..

Baada ya masaa mengi kupita hatimae Mr Kolfan alimkabidhi mzee huyu kitabu kimoja cha kale sana chenye maandishi makubwa juu yaliosomeka U-97 THE REAL HISTORY –DR ROSELF J .PECKER.

“Hiko ndio kitabu ambacho kitakufanya ujue namna U-97 ilivyoanzishwa”Aliongea babu huyu na kumfanya Ambrose kupandwa na shauku ya kujua kile kilichokuwa kimeandikwa katika hiko kitabu.

Nini kimeandikwa katika hiko kitabu … see next chapter. On next seaso
ITAENDELEA IJUMAA


LIPIA 1500 NIKUTUMIE HII SIMULIZI YOTE , LIPA NAMBA 0687151346 AIRTEL/0623367345HALOTEL/0657195492TIGO JINA ISSAI SINGANO UKILIPA TUMA MESEJI WATSAPP 0687151346
UNAWEZA PIA KUJIUNGA KWENYE GRUPU LANGU LA WATSAPP KWA SHILINGI 2000 NA KUPATA OFA YA SIMULIZI YA NILIMDHANIA KAHANA KUMBE BIKRA
Mkuu leo ni jumapili
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom