Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Angeshake vipi ilhali huu mzigo ali order on line??
Nauona mwisho mbaya wa Nasra.. Mwanamke mpumbavu huivunja ndoa yake kwa mikono yake mwenyewe...

Ila jamaa alizingua sana aliruka kanuni muhimu sana 'shake well before use'....

Shake well before use woiiii
 
SEHEMU YA 50

MAUMIVU ya ndani kwa ndani yalifukuta kifuani mwangu, taswira ya mke wangu akifanya mapenzi na hawara wake, ikajitengeneza akilini mwangu. Donge zito likanikaba kooni.

Pumzi zilinitoka kwa shida. Nikataka kusema kitu, nikashindwa, sauti ikagoma ndio usiulize, iligoma kabisa kutoka. “Yanii!..Yaniii…Khaaa!” nilibwabwaja. Kigugumizi kikinizonga, bila kutarajia, machozi yakanibubujika.

Shemeji Aisha alitaka kunipa pole, akasita. Akataka kusema kitu, akaghairi, mwishowe akazipiga hatua kinyonge akiniacha nikipambana na hali yangu. “Baba unalia!” mwangu niliyekuwa nimempakata miguuni, akasema, ni baada ya kuyaona machozi yakinibubujika mashavuni na kutengeneza mifereji.

Jambo lile lilinighafirisha sana, sikupenda kabisa kulia mbele ya mtoto yule mdogo. Nilimwacha sebuleni, nikaingia chumbani na kufungulia sauti kubwa ya redio, kisha nikalia mno.

Dakika 15 badaye nikahisi kuna kitu nimepunguza baada ya kilio kile. Nikaingia bafuni, nikanawa uso, nikwanywa maji, nikajiweka vizuri ili Doreen na mtoto wangu Faraji wasione mabadiliko yoyote.

Baada ya kurudi sebuleni, nikakuta Doreen amekwisha aanda chakula cha usiku na wamekaa ‘dining Room’ wananingoja.

Tukiwa tunakula, kutokuwepo kwa mke wangu na shemeji Aisha kuliifanya nyumba yangu ipooze sana. Hata kwenye meza ya chakula kulipwaya. Pamoja na maumivu niliyokuwa nayapitia muda ule, sitaki kuficha kusema ukweli huu. Upweke wa nyumba yangu, ulinifanya nimisi uwepo wa watu wale wawili.

Hata hamu ya kula sikuwa nayo. Nikaonja onja kama kuwapa hamasa ya kula wale watu wawili kisha nilijiondoa pale ‘dining room’ nikarudi sebuleni, ile naketi kitini nikamkumbuka Issa Mnally, mwandishi aliyefotoa picha za mke wangu na hawara wake wakiwa wanafanya mapenzi.

Sikuwa nimewasilina naye tangu tulipoachana kwenye fumanizi la gesti, nilimpigia simu, nikamuuliza kama picha za mke wangu na hawara wake zipo, akanijibu zipo zote, na wahariri wa gazeti lao wamefurahia upatikanaji wa habari ile.

“Kwa hiyo, habari hiyo mtaitoa kwenye Gazeti gani?”nikamuuliza nikitambua kwenye kampuni aliyokuwa akihudumu kulikuwa na magazeti mengi.
 
SEHEMU YA 51

“Hii stori itatoka kwenye gazeti la Risasi toleo la Jumatano.” “Sawa Issa, nimekuelewa.”

“Lakini kabla ya yote, itabidi niipate maelezo kutoka upande wa mkeo na hawara wake, kwa maana ya ‘balance’ Kwa hiyo kama unazo namba zao hebu nitumie ili kesho asubuhi niwasiliane nao.”

Hilo halikuwa tatizo, baada ya mazungumzo, nikamtumia namba za watesi wangu.

Nilikaa pale sebuleni muda mrefu, mwananangu akiwa miguuni mwangu, wakati wote swali lake lilikuwa ni moja tu. Mama atarudi saa ngapi.

Nilitumia uongo mwingi kumtuliza kiumbe yule hadi alipopitiwa na usingizi.Dooren akambeba na kwenda naye chumbani mwao.

Wakati mambo hayo yakifanyika, kadhalika, wakati ule niliutumia kuwaleza baadhi ya ndugu kama dada zangu kinagaubaga juu ya tukio la fumanizi.

Dada zangu walichukizwa mno na taarifa hiyo, kila mtu alilaani vikali kitendo alichonifanyia mke wangu. “Umekwisha andika talaka?” niliulizwa na dada Khadija, ambaye ni mdogo wangu wa pili kuzaliwa baada ya mimi.

“Kesho nitaandika.” “Umechelewa sana kaka, huyo mwanamke ni muuaji, achana naye kabisa.”

“Nitafanya hivyo mdogo wangu.” “Na vipi kuhusu mtoto?” “Mama amesema kesho anakuja, nadhani anampango wa kumchukua.”

Niliendelea kuwaeleza watu wangu wa karibu matatizo yangu hadi simu ikaishiwa salio!. ****
 
SEHEMU YA 52

Nikamwambia kuwa presha iliyompanda akiwa maliwato na kuanguka.

Sikujua kwa nini mama liingiza hadithi ya kiof cha baba kwenye matatizo yangu ya ndoa.

“Muhusika wa kifo cha baba yako ni huyo huyo mkeo.” “Kivipi?”nikauliza kwa wahaka wa kutaka kujua.

“Kama ulivyokwisha sikia, pamoja na kwamba ulitupa jukumu la kukutafutia mke, ukweli ni kwamba mwanamke huyu hakuwa chaguo langu, bali baba yako.”

“Kwa nini kivipi?”nikazidisha maswali. “Huyu binti ni chui aliyejivisha ngozi ya kondoo, kwa nje anaonekana ni mwanamke mstarabu sana, lakini ni mshenzi wa washezi”

“Kwa nini!!!” nikazidi kuliza, maelezo ya mama bado hayakuwa yamejibu swali la kwa nini? “Nasra alikuwa na mabwana utitiri huko Nguruka” “Eeeh!” “Ndio, tena unaambiwa wengi walikuwa wanaume za watu”

“Haiwezekani!” “Tatizo lako ndio hilo, ubishi tu!” “Sio kwamba nabisha tu, ni kwa sababu nimemkuta Nasra akiwa bado mwanamwali, bikira,” baada ya kusema hilo, mama alicheka ingawa uso wake haukuwa na japo chembe ya furaha.

“Sikia nikupashe mwanangu,” alisema, kisha akaendelea. “Yule binti alikuwa na skendo ya kutoka kimapenzi na wanaume kinyume na maumbile na ndio maana umebahatika kukumkuta mwali.” “Tobaa!” nilishituka sana.

Akili ilinizunguka, kauli ya mama japokuwa ilinishitua sana, lakini ikanikumbusha siku mke wangu alipojifungua nililaumiwa n a dokta Caharles Meleka akinishutumu kwa nini nimekuwa na tabia ya kupita malngo wa nyuma. kiasi cha kuleta lapsha wakati wa kujifungua!

Nilikumbuka mzozo mkubwa uliobuka dokta huyo, nikimuhakikishia kuwa sijawahi kujihusisha na michezo hiyo. “Kumbe mwanamke yule ni mchafu kiasi hiki!”

“Hafai hafai, hakufai,”mama alitia msisitizo. “Na unasema yeye ndio alimuua baba?” “Ndio” mama akaitikia huku machozi yakimlenga. “Kivipi? Ilikuwaje” nikauliza na kujiweka sawa kusubiri majibu.

JE? NINI KITATOKEA.
 
mmh!..

inawezekana labda...maana huyo bibie shoga/ marafiki zake ni mashoga..na tanga ndio ficho lake...

wanasema ule mchezo wa pwani ..wakati bara ndio umetamalaki!
na zile mimba zilizoingiaga, ziliingiaga kwa uwani?hawa celebrities wa kike mashoga ni kama misukule yao; kila mtu anafuga lake.
 
na zile mimba zilizoingiaga, ziliingiaga kwa uwani?hawa celebrities wa kike mashoga ni kama misukule yao; kila mtu anafuga lake.
hawafugi bure mkuu..

wennzie wale...wanapeana mautundu...

ukiona mwanamke ako karibu sana na wale ujuwe na yeye ni mwenzao!

Sasa huyo bibie ..tuhuma hizo zipo zamani.... ....

Maseleb wengi wanadhalilika sana kwa kutaka good time@
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom