Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Sehemu ya 53

Nilikumbuka mzozo mkubwa uliobuka dhidi yangu na dokta huyo, nikimuhakikishia kuwa sijawahi kujihusisha na michezo hiyo.

“Kumbe mwanamke yule ni mchafu kiasi hiki!” “Hafai hafai, hakufai,”mama alitia msisitizo. “Na unasema yeye ndio alimuua baba?” “Ndio” mama akaitikia huku machozi yakimlenga.

“Kivipi? Ilikuwaje?” nikauliza na kujiweka sawa kusubiri majibu. Mama alipiga kimya kidogo kama vile alikuwa akiwaza jambo fulani, kisha akaniambia. “Unajua nini mwanangu?”

“Eeh!” “Ni kweli baba yako alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya presha, tena ile presha ya kupanda, hata hivyo kwa muda mrefu ilikuwa ni aghalabu kukuta presha hiyo imepanda,” alisema. Akaendelea.

Baada tu ya kipindi kile kurudi Kigoma na kumweleza juu ya vituko vya mkeo, hapo ndipo kama nilikuwa nimeyamsha maradhi yake ya moyo.”

“Ilikuwaje?” “Unajua marehemu baba yako alikuwa anakupenda sana. Nakumbuka nilipomuhadithia habari za mkeo alipatwa na simanzi kubwa, muda wote akawa ni mtu wa kujutia kitendo cha kukuolea mke mwenye tabia chafu, tangu siku hiyo baba yako akawa mtu asiye na raha.

Aliona ni kama alikutia kwenye tanuri la moto. Hali ile ikachoche presha yake. Hatimaye siku moja akaanguka bafuni na kufariki,” mama alihitimisha.

Nilibakia kimya, nikahisi kizunguzungu, donge kubwa lilinikaba kooni. Jambo lile lilinifanya nimwone Nasra kuwa muuaji wa baba yangu.

“Lakini, lakini…” nilishia kubabaika, maneno yakiwa hayatamkiki kinywani. “Ndio maana nasema huyu binti anahusika na kifo cha mume wangu.” “Lakini mama!! Dah!.... Nasra!” nilighafirikia mno.

Mama hakuwa na kuongeza akaishia kutikisa kichwa kwa masikitiko. “Unasema ulizifahamu vema tabia za Nasra, tena kabla hata ya ndoa yangu, sasa…”

“Sikiliza Faraji…” mama alinikatisha, alikwisha tambua nilikuwa nataka kusema nini. “Mimi ningefanya nini na baba yako alikuwa king’anga’nizi?” alisema, akaendelea.

“Kila kitu kuhusu tabia za mwanamke huyo nilimwambia, lakini mume wangu ubishi ulimjaa, nilimshauri angalau tukakuolee kijiji cha Usinge, kidogo kule wanawake wamejituliza ukilinganisha na wale wa kijiji cha Nguruka.

Baba yako hakunisikiliza, akamkazania huyu mtoto wa Kipemba, sijui alizuzuka na nini
 
Sehemu ya 54

“Ndio.” Akajibu. Uso wake ukionekana kuwa na hamaniko kubwa. “Kwa nini sasa? Baba alikuwa na maslahi gani na binti huyu,”niliendelea kuhoji.

“Sijui hata niseme nini. Nadhani asili ya tabia za watu wa Kigoma sasa inatuhukumu.” “Unamaana gani?” “Ni kuhusu tabia ya ubishi.

Ubishi wa mume wangu sasa hii ndio matokeo yake. Liati kama Marehemu mzee Hussein angenisikiliza, haya yote yasingekuwepo.” Mama alisema.

“Kwa kweli mmeniangusha wazazi wangu,” nilisema, uchungu mkubwa ukiwa kifuni. “Dunia ya leo ni mtoto gani atawapa heshima wazee wake wamtafutie mke ama mume?

Mimi nilifanya hivyo. Badala ya kumpata mke, mmeniletea kahaba.” Kauli ile ilimumiza sana mama yangu, machozi yakambubujika, akayapangusa kwa kutumia ukingo wa kanga yake huku kwikwi za kilio zikimtoka.

“Uko sahihi Faraji. Hakuna hata moja lisilo la kweli baba, tunastahili lawama, tunastahili kuzodolewa, hata hivyo nahitaji msamaha wako mwanangu.”

“Maji yamekwisha mwagika mama, hakuna jinsi tena,” nilimwambia kumtuliza, sikupenda kumwona anavyolia kwa majuto, ukizingatia makosa yalifanywa na marehemu baba.

Siku hiyo, tulizungumza mambo mengi sana, miongoni mwa tuliyoazungumza ni kuhusu mama kumchukua mtoto wangu na kwenda naye kijijini kwa ajili ya malezi.

Siku ya pili, nilifanya taratibu za kupata tiketi ya ndege ya Fast Jet, jioni ilipotimu mama na mwanangu Mwanda, wakaondoka na ndege.

Angalau roho yangu ilitulia, sikupenda kabisa mtoto yule alelewe na mama yake, mwanamke ambaye hadi wakati ule mama anaondoka na ndege, sikusikia habari zozote kumuhusu.

Pale nyumbani, nikabakia na Doreen, msichana wangu wa kazi,naye nikafikiria nimlipe pesa zake za mshara kisha arudi kwao Iringa.

Hata hivyo, nilipofikiria ukubwa wa jumba lile, nikaona sio vizuri likiwa linabakia pweke, ingawa sikuona pia uzuri wa kuishi na mtoto yule wa kike tukiwa wawili tu ndani ya nyumba.

Sasa nifanye nini? Nimrudishe Doreen nyumbani kwao ama nimwache tuendelee kuishi wawili ndani ya nyumba, akiwa kama mwangalizi na mlinzi wa mji wangu? Nilijiuliza kimoyomoyo. Mwishowe nikaamua Doreen abaki awe mwangalizi wa mji.
 
Sehemu ya 55

Niliendelea na shughuli zangu kama kawaida, ingawa kazi sikuzifanya kwa ufanisi mkubwa. Kila wakati picha ya mke wangu akifanya mapenzi na mwanaume mwingine ilijitengeneza akilini mwangu.

Na kila jambo hilo lilivyokuwa likipita kichwani mwangu, ndivyo chuki dhidi yake ilivyoongezeka. Chuki ikanifanya nimkumbuke Issa, mwandishi wa gazeti la Uwazi. Nikampigia simu.

Kujua juu ya uchapaji wa habari ya fumanizi ya mke wangu kwenye gazeti lao. “Mkuu,” Issa aliongea baada ya kupokea simu yangu. “Habari yako kaka?”

“Safi mkuu, nilikuwa nakufikiria muda huu huu” “Haya nambie.” “Jioni tunaweza kuonana?” “Jioni ya leo?”

“Ndio” “Tunaweza, kuna nini kwani? Habari itatoka kwenye gazeti?” nilimuuliza kwa kiherehere. “Njoo tukutane La_Charse pub.” Badala ya kujibu maswali, akaishia kunipa miadi.

Kiodogo kidogo nikawa na mashaka kwa kuhisi huenda mpango wangu wa kumkomesha Nasra pamoja na hawara wake umeingia dosari.

Baada ya shughuli za mchana kutwa, jioni niliendesha gari hadi La_Charse nikagiza mishikaki na pilipili, nikawa natafuna zile nyama nikimngoja Issa awasili.

Muda mfupi badaye, Issa akafika, baada ya salamu, akaagiza bia ya baridi, ilipoletwa akapiga tarumbeta, chupa ilipotua chini akaanzisha mazungumzo: “Mkuu leo mkeo alikuja ofisini kwentu.” “Alikuja kufanya nini?” nikahoji kwa wahaka.

“Alileta pingamizi kuhusu kuchapwa kwa habari inayohusu skendo ya kufaminiwa kwakwe.”

“Kwa nini?” “Anasema ameingiliwa kwenye uhuru wake wa faragha kwa kuwa wewe si mume wake na mlikwisha achana miaka mingi kwa talaka isipokuwa wewe ndio umekuwa ukimng’ang’nia” “Shubamit!!!. Kumbe huyu mwanamke fedhuli hivi?”

nilibweka hadi cheche za mate zilizochanganyikana na vinyama vikanitoka “Si kweli kaka, si kweli kabisa. Huyu mwanamke anatafuta pakujifichia, toeni hiyo habari, tena iwe kwa ukubwa ukurasa wa mbele,”

“Ishapigwa pini kaka, habari za namna hiyo huwa hazitoki ili kuto-risk kampuni, kama muhusika akiamua kwenda mahakamani” Issa alisema.

Roho iliniuma, mwili ulinitetemeka kwa hasira, Nasra alikuwa amenizidi kete, vipande vya nyama nilivyokuwa natafuna niliviona vichungu kama shubiri.

Je nini kitatoke?
 
Sehemu ya 54

“Ndio.” Akajibu. Uso wake ukionekana kuwa na hamaniko kubwa. “Kwa nini sasa? Baba alikuwa na maslahi gani na binti huyu,”niliendelea kuhoji.

“Sijui hata niseme nini. Nadhani asili ya tabia za watu wa Kigoma sasa inatuhukumu.” “Unamaana gani?” “Ni kuhusu tabia ya ubishi.

Ubishi wa mume wangu sasa hii ndio matokeo yake. Liati kama Marehemu mzee Hussein angenisikiliza, haya yote yasingekuwepo.” Mama alisema.

“Kwa kweli mmeniangusha wazazi wangu,” nilisema, uchungu mkubwa ukiwa kifuni. “Dunia ya leo ni mtoto gani atawapa heshima wazee wake wamtafutie mke ama mume?

Mimi nilifanya hivyo. Badala ya kumpata mke, mmeniletea kahaba.” Kauli ile ilimumiza sana mama yangu, machozi yakambubujika, akayapangusa kwa kutumia ukingo wa kanga yake huku kwikwi za kilio zikimtoka.

“Uko sahihi Faraji. Hakuna hata moja lisilo la kweli baba, tunastahili lawama, tunastahili kuzodolewa, hata hivyo nahitaji msamaha wako mwanangu.”

“Maji yamekwisha mwagika mama, hakuna jinsi tena,” nilimwambia kumtuliza, sikupenda kumwona anavyolia kwa majuto, ukizingatia makosa yalifanywa na marehemu baba.

Siku hiyo, tulizungumza mambo mengi sana, miongoni mwa tuliyoazungumza ni kuhusu mama kumchukua mtoto wangu na kwenda naye kijijini kwa ajili ya malezi.

Siku ya pili, nilifanya taratibu za kupata tiketi ya ndege ya Fast Jet, jioni ilipotimu mama na mwanangu Mwanda, wakaondoka na ndege.

Angalau roho yangu ilitulia, sikupenda kabisa mtoto yule alelewe na mama yake, mwanamke ambaye hadi wakati ule mama anaondoka na ndege, sikusikia habari zozote kumuhusu.

Pale nyumbani, nikabakia na Doreen, msichana wangu wa kazi,naye nikafikiria nimlipe pesa zake za mshara kisha arudi kwao Iringa.

Hata hivyo, nilipofikiria ukubwa wa jumba lile, nikaona sio vizuri likiwa linabakia pweke, ingawa sikuona pia uzuri wa kuishi na mtoto yule wa kike tukiwa wawili tu ndani ya nyumba.

Sasa nifanye nini? Nimrudishe Doreen nyumbani kwao ama nimwache tuendelee kuishi wawili ndani ya nyumba, akiwa kama mwangalizi na mlinzi wa mji wangu? Nilijiuliza kimoyomoyo. Mwishowe nikaamua Doreen abaki awe mwangalizi wa mji.
Doreen anaweza panda cheo ghafla...


Cc: mahondaw
 
Sehemu ya 55

Niliendelea na shughuli zangu kama kawaida, ingawa kazi sikuzifanya kwa ufanisi mkubwa. Kila wakati picha ya mke wangu akifanya mapenzi na mwanaume mwingine ilijitengeneza akilini mwangu.

Na kila jambo hilo lilivyokuwa likipita kichwani mwangu, ndivyo chuki dhidi yake ilivyoongezeka. Chuki ikanifanya nimkumbuke Issa, mwandishi wa gazeti la Uwazi. Nikampigia simu.

Kujua juu ya uchapaji wa habari ya fumanizi ya mke wangu kwenye gazeti lao. “Mkuu,” Issa aliongea baada ya kupokea simu yangu. “Habari yako kaka?”

“Safi mkuu, nilikuwa nakufikiria muda huu huu” “Haya nambie.” “Jioni tunaweza kuonana?” “Jioni ya leo?”

“Ndio” “Tunaweza, kuna nini kwani? Habari itatoka kwenye gazeti?” nilimuuliza kwa kiherehere. “Njoo tukutane La_Charse pub.” Badala ya kujibu maswali, akaishia kunipa miadi.

Kiodogo kidogo nikawa na mashaka kwa kuhisi huenda mpango wangu wa kumkomesha Nasra pamoja na hawara wake umeingia dosari.

Baada ya shughuli za mchana kutwa, jioni niliendesha gari hadi La_Charse nikagiza mishikaki na pilipili, nikawa natafuna zile nyama nikimngoja Issa awasili.

Muda mfupi badaye, Issa akafika, baada ya salamu, akaagiza bia ya baridi, ilipoletwa akapiga tarumbeta, chupa ilipotua chini akaanzisha mazungumzo: “Mkuu leo mkeo alikuja ofisini kwentu.” “Alikuja kufanya nini?” nikahoji kwa wahaka.

“Alileta pingamizi kuhusu kuchapwa kwa habari inayohusu skendo ya kufaminiwa kwakwe.”

“Kwa nini?” “Anasema ameingiliwa kwenye uhuru wake wa faragha kwa kuwa wewe si mume wake na mlikwisha achana miaka mingi kwa talaka isipokuwa wewe ndio umekuwa ukimng’ang’nia” “Shubamit!!!. Kumbe huyu mwanamke fedhuli hivi?”

nilibweka hadi cheche za mate zilizochanganyikana na vinyama vikanitoka “Si kweli kaka, si kweli kabisa. Huyu mwanamke anatafuta pakujifichia, toeni hiyo habari, tena iwe kwa ukubwa ukurasa wa mbele,”

“Ishapigwa pini kaka, habari za namna hiyo huwa hazitoki ili kuto-risk kampuni, kama muhusika akiamua kwenda mahakamani” Issa alisema.

Roho iliniuma, mwili ulinitetemeka kwa hasira, Nasra alikuwa amenizidi kete, vipande vya nyama nilivyokuwa natafuna niliviona vichungu kama shubiri.

Je nini kitatoke?
Jamaa nae bwege sana... kwani hana vyeti vya ndoa, kuthibitisha kwamba huyo ni mke wake na hajamuacha...


Cc: mahondaw
 
SEHEMU YA 56

Macho yaliniiva, yakawa mekundu utadhani yalitiwa pilipili. “Issa,” nilimwita kwa sauti kavu. “Naam kaka.”

“Nitakupa laki tatu, fanya kila uwezalo habari hii itoke kwenye gazeti.” “Tatizo sio pesa kaka, tatizo ni utata wa hiyo habari yenyewe,”

Issa aliendelea kunikatalia katakata. Nikambembeleza kwa ahadi lukuki, mwandishi yule aligoma.

Nilibakia na donge kavu rohoni, wakati huo jua la jioni lilikuwa linaishilizia, kichwa changu kilikuwa kimevurugwa vibaya sana.Nilikuwa nimezodoka kama teja aliyekosa kidonge cha methadone.

Wakati huo, tayari Issa alikuwa amekwisha ondoka. Niliyazungusha macho kulia na kushoto, meza za pembeni yangu, waliketi wanaume mbalimbali.

Nyuso za baadhi ya wanaume wengi zilionyesha ni watu wenye kuyafurahia maisha, walikuwa wakinywa pombe wengine wakicheza muziki, baadhi walikuwa wakicheka na kugonga glasi kwa furaha.

Kimwonekano walikuwa ni watu wenye familia, nilijikuta nikiwaonea wivu kila mtu niliyemwona akitabasamu, nikaitamani furaha yao ingekuwa yangu.

Katikati ya tamaa, nikawa najiuliza: Je watu wale nao walikuwa wakikutana na changamoto kama zangu kwenye ndoa zao? Wake zao waliwapa furaha? Ama walikuwa washenzi kama alivyo mke wangu? Nini siri ya tabasamu lao? Nikajiuliza:

kweli kuna mwanaume anayefurahia ndoa yake akiwa na mwanamke mrembo kama ilivyokuwa kwangu? Je walevi wale walikuwa na wanawake wenye mvuto wakiwa wamewacha majumbani mwao, huku wao wakiendelea kufurahia pombe kirabuni?

Sauti moja akilini ikanambia, walevi wale, walikuwa wakipitia changamoto mbalimbali maishani, lakini siri pekee ya wao kuwa wenye furaha ni pombe wanazokunywa.

Ibirisi wa ulevi akazidi kunisukuma katika mtaro wa ulevi, akili yangu ikaamini msongo wa mawazo mwarobaini wake ni ‘gambe’

Nikaagiza chupa mbili za waini, mhudumu aliponiuliza waini gani, nikamwambia yoyote kali. Sikuwahi kunywa pombe maishani mwangu. Hata majina ya pombe sikuwa nayajua. Siku ile ilikuwa ni mara yangu ya kwanza.

Nakumbuka nilipoletewa chumba mbili za waini, Pombe ambayo hata jina lake siikumbuki vizuri ilikuwa inaiitwaje. Nilipiga mafunda ya haraka haraka kama soda.

Ndani ya dakika 20 nikaanza kuhisi kizunguzungu, kufumba na kufumbua
 
SEHEMU YA 57


Tukawa tunaendelea kupata kinywaji huku tukizama kwenye mijadala ya mambo mbalimbali kama ya siasa na mpira.

Kwa kuwa eneo hilo nilikuwa vizuri wale jamaa walijikuta wakinisikiliza nikidadavua kwa weledi mkubwa mijadala ya siasa na soka.

Pombe ikazidi kunyweka, nikaendelea kupata marafiki, tukala nyama, tukacheza muziki, ilipotimu saa sita usiku, nikajitoma kwenye gari langu na kurudi nyumbani.

Nilipofika, Doreen akanifungulia geti, nikiwa nayumba, naongea mambo yasiyoelewa kutokana na ulevi, mara nikajitupa sofani, chakula alichokipika Doreen, kikakosa mlaji. Sikuamka hadi siku ya pili asubuhi.

Asubuhi niliamshwa na Doreen. Nilipofumbua macho kivivu, Doreen alisimama mbele yangu. “Shiikamoo shemeji,”

“Marhabaa. Hujambo Doreen.” “Sijambo. Kuna mgeni wako yupo getini anakuhitaji.”

“Ni nani?” “Simjui.” Nilijinyanyua sofani, pombe ikiwa bado kichwani, nikazipia gatua kutoka nje.

Nikajizoazoa hadi getini. Nikamkuta mwanaume aliyechomekea shati la mikono mirefu, tai ikiwa inaning’inia shingoni.

“Habari yako,”nikamsalimia “Salama tu, naitwa Joseph John, ni mjumbe kutoka dawati la ustawi wa jamii, wilaya ya Kinondoni, ninabarua yako ya wito siku ya Jumatatu saa mbili asubuhi,” aliniambia huku akitoa bahasha yenye barua ya wito na kunipa.

Kumekucha!. Nilinong’ona kimoyomoyo, nilitambua Nasra alikuwa amekwenda kunishitaki kwenye Ofisi za Ustawi wa jamii, nikaamini madai yake makubwa ni kutaka kumchukua mtoto.

Nilinyakua barua ile na kufunga geti kwa hasira, nikarudi ndani nikiapa moyoni kutofanya kosa lolote litakalopelekea mwanangu kuishi na mwanamke yule.

Tukio hilo la asubuhi, likanifanya nirudi kwenye msongo wa mawazo, mkandamizo wa kufikiria mabaya aliyonifanyia mwanamke yule ukawa mkubwa.

Nilioga, nikabdili nguo, niliporudi mezani, nikakuta Doreen ameniandalia supu nzuri ya nyama ya mbuzi. Moyoni nikajiuliza: “Haka katoto kamejuaje supu itanifaa asubuhi hii, ukizingatia niliamka na ‘hangover’ “

Nilishambualia supu ile, nilipomaliza kidogo kichwa changu kikawa vizuri, nikaondoka na kwenda kwenye mihangaiko yangu.

Nilifanya kazi zangu kutwa nzima. Jioni ilipotimu niliendesha gari hadi La Cherse, huko nikakutana na marafiki,
 
SEHEMU YA 58

Doreen. Msichana mweusi, mwenye chuchu zilizosimama wima alionesha kunijali.

Siku ya jumatatu ilipotimu, nilitikia wito, nilikwenda ofisi za halmashauri ya kinondoni, niliingia kwenye ofisi ndogo ya maofisa ustawi, mke wangu Nasra naye alikuwepo.

Hakuwa peke yake, aliongozana na hawara wake,Ally, roho yangu iliniuma sana kadiri nilikuwa nikiowana watu wale wako pamoja, kitendo cha kuwaona ilikuwa ni kutonesha kidonda kibichi.

Zamu ya kuhudumiwa ilipofika, tuliingizwa kwenye ofisi ndogo, kabla ya kuanza kuzungumza kinaganaga juu ya nani anastahili kumlea mtoto, maofisa ustawi walitutaka radhi tuwe na subira kidogo tumngojee kiongozi wao.

Tulingoja kwa muda kidogo, punde mtu aliyesemwa ni mkuu wao akaingia. Sikuamini macho yangu baada ya kumwoana bosi huyo.

Alikuwa ni Debora, mwanamke ambaye alikuwa katibu muhtasi wangu, wakati nikiwa mratibu wa elimu wilaya ya Temeke, hata yeye aliponiona alishituka. Lakini alificha mshituko wake, watu wengine hawakugundua chochote.

Aliketi. Kesi ikaanza kusikilizwa. Alianza mke wangu kujieleza, akawaeleza ameachana na mimi kutokana na manyanyaso yatokanayo na kipigo nilichokuwa nikimpa baada ya kulewa pombe, lakini kama haitoshi, akasema nimemnyang’anya mtoto mdogo ambaye kisheria ilibidi alelewe na yeye hivyo madia yake ya msingi ni kumtaka mtoto wake.

Wakati mke wangu anaeleza mambo yale nilihisi kifua changu kikijaa hewa, nikawa sihemi vizuri, hasira zilinilipanda vibaya sana. Nasra alikuwa akizungumza uongo mwingi sana huku akinipaka matope mbele za watu.

Zamu yangu ya kujieleza ilifika, nilieleza kwa ufupi sababu ya kumwacha mwanamke yule, nikawambia nimetengana na Nasra kutokana na umalaya wake , tabia ambayo nimeona inaweza kuleta matatizo kwa mwanangu.

“Tumewasikiliza…” Hatimaye Debora kiongozi wa wale maofisa alisema. “Pamoja na mambo yote hayo, bado sheria inampa haki mama wa mtoto kuishi na mtoto huyo.

Na si hilo tu, sheria inampa haki mwanamke huyu ya kupata sehemu ya mali mlizochuma pamoja katika maisha yenu ya ndoa.” Debora alisema, tena bila kuniangalia usoni.

JE? NINI KITATOKEA.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom