Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Sehemu ya 38

Pamoja na kuniona nimeingia, wala hakunijali, si salamu wala kujishughulisha na chochote. Yeye na simu, simu na yeye.

Nilipitiliza hadi chumbani, nikaoga na kubadili nguo, nikarudi sebuleni ambako niliwacha.

Nilimkuta akiendelea kucheza na simu yake, hakunisemesha chochote, mimi pia sikumsemesha lolote.

Masaa machache badaye, nilitayarishiwa chakula na dada wa kazi. Niliona yamesalia masaa machache kabla ya kukamilika kwa tukio baya na la aibu nililopanga kumtendea mwanamke yule na hawara yake.

Nilisahau kabisa methali isemayo: Jambo usilolijua ni sawa na usiku wa giza.

Wakati nakula, mke wangu aliendelea kuwa bize na simu yake, akawa anatabasamu, wakati mwingine anaachia kicheko kidogo.

Alionekana ni mwenye kufurahishwa na jambo simuni.
Roho iliniuma sana, niliamini kivyovyote mke wangu alikuwa akichati na hawara wake.

Chakula nilichokuwa nikila, hakikupita kooni. Kwa mara nyingine nikatamani nimrarue mwanamke huyu, hata hivyo malaika wa hekima walikuwa wamenizingira.

Nikaendelea kula kwa tabu, baada ya kuonja onja ule msosi, nikasimama na kuelekea zangu chumbani. Nikamwacha akiendelea kutesa na simu yake.

Nilipofika chumbani, nilijitupa kitandani nikawa nawaza hili na lile, katika kuwazawaza huko, nikakumbuka kuna kipindi mama aliwahi kuonesha hali ya kutovutiwa kwa mimi kumwoa huyu mwanamke, japokuwa fursa ya kunitafutia mke, niliwapa wao.

Je. Mama aliwahi kuijua tabia ya umalaya aliyonayo mke wangu? Na kama aliwahi kujua kwa nini alikubali nimwoe huyu mrembo?

Fikra hizi zikachochea dhamira ya kuwasiliana na mama, ili anipe majibu ya utata huu. Nilipiga namba ya mama na kuweka simu sikioni. Simu iliita, muda mfupi ikapokelewa. “Hellow!” “Asalam aleykum mama,”nilimsalimu mama simuni.

“Waleykum salam, mwajionaje huko?” “Mungu anasaidia….”nilimwitikia kinyonge kisha nikaendelea. “ Ninalo jambo ningependa nikuulize.”

“Jambo gani baba?” aliniliu za kwa shauku, nikasikia akipunguza sauti ya televisheni ili kuyapa nafasi mazungumzo yetu.

“Unakumbuka kuna siku uliwahi kunieleza kwamba Nasra alikuwa ni chaguo la baba ila wewe hukufurashishwa naye, unakumbuka?” nilisema. Nikapiga kimya kusubiri jibu.
 
Sehemu ya 39

“Endelea kueleza baba nakusikiliza…” “Unakumbuka?” nikakazia swali langu

Mama akashindwa kujibu. Nadhani alihisi huenda mimi na Nasra tunataka kumsuta, alitambua mimi kwa nasra sijiwezi.

“Sikumbuki,” akasema kwa sauti iliyooneshwa kukarahishwa na mazungumzo yale.

“Mama nina matatizo makubwa kwenye ndoa hii, niambie tafadhali, kwa nini Nasra hakuwa chaguo lako?”

“Kuna matatizo gani kwani?” badala ya kujibu, naye akaniuliza. Nilikuwa sijamweleza matatizo yanayoisibu ndoa yangu. Nilichofanya ni kumsimulia songombingo lote.

Nilipoweka kituo. Mama alishusha pumzi nyingi, akaonekana kuguswa na maswahibu yale. “Pole mwanangu ndio ukubwa huo.”

“Ahsante mama.” “Sasa umepanga kufanya nini?” “Hata sijui.” Nilimdanganya sikutaka kumwambia nimesuka mpango wa kumfumania na kumfotoa picha zitakazo pamba ukurasa wa mbele wa Gazeti la Uwazi “Hujui cha kufanya!” akauliza tena .

“Kabisa.” “Basi wewe naye una matatizo?” “Kivipi mama?” “Siku zote, tatizo lina pande mbili, upande wa chanzo na upande wa suluhu, ikitokea tatizo halafu ukabaki katikati ya chanzo na suluhu, basi na wewe ni sehemu ya tatizo.”

Kauli ya mama yangu ilinikata maini, ni kama vile alikuwa akinisuta, nawezaje kujua chanzo cha mke wangu kukengeuka na kushindwa kutatua tatizo hilo.

“Hellow” aliniita simuni baada ya kuona kimya. “Nakusikiliza mama,”nilisema kwa huzuni.

“Kesho asubuhi nitafute nikueleze kwa nini huyo mwanamke wako hakuwa chaguo langu,” mama alisema.

Tuliagana, akakata simu. Nilipogeuka nyuma, kumbe mke wangu alikuwa akinisikiliza mazungumzo yangu na mama, alikuwa akiniangalia huku amefura kama kiboko. Akachia msonyo mreefu halafu akaelekea bafuni.

Kitendo cha kusonywa na Nasra kilifanya joto la mwili liongezeke, hasira kali zilinipanda, dharau za kiwango hiki zilinielemea.

Nilimtizima kwa chati kiumbe huyu akiwa anashilizia maliwato, kimoyomoyo nikasema, dawa yako inakaribia kuiva mwarabu koko wewe.

Baada ya kutoka bafuni, hakukaa chumbani, akarudi sebuleni, huko akaendelea kuchat, sikumbuki usingizi ulinipitia baada ya muda gani, lakini kulipokucha nilijikuta niko peke yangu kitandani.

Mke wangu hakuwepo. Nikatambua atakuwa alilala sebu
 
Sehemu ya 40

Ilikuwa inaelekea kuwa saa mbili kamili, nilijiandaa ‘chapchapu’ nikapata kifungua kinywa, nikachukua funguo za gari, nikatoka kuelekea ofisini kwangu.

Nikiwa umbali kidogo na mji wangu, Issa akanipigia simu. “Mkuu tupo kwako hapa.” “Mmekwisha fika?”

“Zamani za kale” akajibu kwa kujidai. “Kwa hiyo, ndio mnaanza kufutilia nyendo zake?” “Ndio maana yake, jambo la muhimu jitahidi uwepo na wewe sehemu ya tukio.”

“Naanzaje kukosa sasa? Acha niwahi ofisini kisha niache nirudi tuungane kwenye hiyo operation.”

Baada ya kuelezana hayo, nikaongeza spidi ya gari, muda mfupi badaye nilikuwa kwenye maduka yangu, nilikuta vijana wangu wamekwisha fungua na wanaendelea na kazi, nilipitia taarifa za hapa na pale za mauzo, nikiwa katika kupitia pitia, simu ya Issa ikaingia tena.

“Mkuu” nilipokea. “nisikilize kwa makinii….”issa alisema kwa wahaka.` “Ndio, nakusikiliza” “Mkeo ndio anatoka, tena amejipodoa barabara, we jamaa una mke mrembo sana” ”

“Anakwenda wapi?” nikajikuta nimeuliza swali la kijinga. Tumbo lilipata joto. “Atakuwa ndio anakwenda gesti huyu,” kauli ya Issa ilinigusa hadi ubongoni, nikahisi kifua chote kikiwaka moto, akili ikanizunguka.

“Kweli?” “Haki ya mama tena!” “Mmefika wapi?” “Tupo Mkwajuni hapa, anachukua bodaboda, nasi tupo nyuma yake, hatuko mbali naye.” “Hakikisheni hamfanyi kosa lolote litakalopeleka kumpoteza.”

“Hilo kosa kwetu ni dhambi, na huwa halipo,” Issa aliongea kwa mbwembwe, katika namna ya kunionesha alivyo mahiri kwenye habari za kichunguzi.

Wakati simu ya Issa anakatika simu ya mama nayo ikaingia!. Nikakumbuka jana tulikubaliana kuzungumza, ili anieleze kwa nini hakufurahishwa na ndoa kati yangu na Nasra ilihali yeye na baba ndio waliohusika kuniolea mwanamke huyu.

“Hellow mama” “Asalama aleykum” alinisalimu. “Waleykum salama mama, mzima?” Kabla sijajibu nikaona Issa ananipigia, nilichofanya ni kuihold simu ya mama na kupokea ya Issa.

“Nambie Issa?” “Mkeo amefika gesti, yupo na hawara wake” “Eeeeh!!” nilihamaki
 
Sehemu ya 42

“Mkeo amefika gesti, yupo na hawara wake” “Eeeeh!!” nilihamaki “Ndio, kafika yupo na bwana wake, fika fasta basi eneo la tukio tumalize kazi,” Issa alisisitiza, nilihisi kitu ndani ya kifua changu kikilipuka kama bomu.

Kitendo cha kuambiwa mke wangu alikuwa gesti na mwanaume mwingine kilinishitua sana. “Nakuja fasta Issa,” nilimwambia na kukata simu.

Sikuwa na habari tena na simu ya mama ambayo nilikuwa nimeihold, jambo pekee lililokuwa akilini mwangu ni kufika gesti ya Madrid na kushuhudia uchafu anaofanya mke wangu Nasra.

Bila kuwaaga wafanyakazi wangu, nilikurupuka na kutoka nje ya duka, nikaona nikitumia gari langu naweza kuchelewa eneo la tukio, nilichofanya ni kuchukua bodaboda.

Dakika kumi na tano badaye, nilikuwa Kinondoni, niliwasiliana na Issa akanieleza mahali walipokuwa wamebana, walikuwa kwenye glosary moja iliyokuwa mita kama 100 kutoka kwenye gesti aliyokuwa mke wangu.

“Umechalewa sana Faraji,”Issa alinipokea na lawama. “Samahani Issa, mambo ya foleni, si unajua mji wetu huu.”

“Unajua madhala ya kuchelewa hivi, inawafanya wagoni wetu wapate wasaa wa kufanya malovee,” Issa aliniambia, maneno yale yalikuwa mkuki wa moto kifuani.

“Kwa hiyo unataka kusema, hadi wasaa huu mke wangu na hawara wake watakuwa wamekwisha vunja amri ya sita?”

“Kwa muda huu watakuwa wako katikati ya raha ya penzi, hawajamaliza bado,” Issa alisema, hakujua kabisa kama maneno yale, yalikuwa ni sawa na ncha ya sindano kwenye kidonda.

“Sasa tufanyaje?” niliuliza kwa sauti ya unyonge. “Ngoja niwastue jamaa ili tuingie” “Jamaa gani” “Polisi na mwenyekiti wa mtaa”

“Kumbe hao nao wanahusika?” “Ndio, kwenye mchakato huu inaweza kutokea jinai, polisi na mwenyekiti watasimama kama mashahidi kama ikitokea hali hiyo.”

Baada ya Issa kuwasiliana na watu hao, muda mfupi badaye mzee mmoja, aliunga nasi.

Jumla tukawa watu watatu kwa maana ya waandishi wa habari wawili, mimi na yule mzee ambaye badaye nilimtambua kama mwenyekiti wa mtaa.
 
SEHEMU YA 43


Tulizipiga hatua kuikabili gesti ile. Tulipofika mapokezi Issa na mwenyekiti wa mtaa wakajitambulisha kwa binti aliyekuwa mapokezi.

Msichana yule aliposomewa tuhuma za nyumba ile kuwa chaka la uzinzi na uasherati kwa wake za watu, hakufanya ukaidi kutoa ushirikiano.

Tuliongozana naye hadi katika chumba alichokuwa mke wangu na bwana wake. Tulipokewa na sauti za mahaba zilizotokea ndani. Miguu yangu nilihisi ikishiwa nguvu.

Mwili ukaninyong’onyea, na kadiri mambo yale yalivyozidi kunisibu, ndivyo kelele za mke wangu aliyekuwa akishughurikiwa ndani, zilivyozidi kuingia ndani ya ngoma ya masikio yangu.

Nikapepesuka kulia na kushoto na bila kutarajia nikajikuta ninaketi kitako sakafuni.

Issa na wale waandishi wengine ambao muda ule walikuwa na kamera zao tayari kwa kurekodi kila kitu, wakajikuta katika fadhaa baada ya kuniona nimekaa chini. “Jikaze bro” Issa akanihimiza, aliongea kwa sauti ya kunong’ona.

Pamoja na kujihakikishia kwamba nilikuwa nimekaa, ajabu bado nilikuwa nahamu ya kuketi, hadi leo huwa nashindwa kabisa kuelewa ile hamu ya kuketi ilikuwa imelenga kuketi wapi zaidi.

“Simamaaa!” Issa akanong’ona tena, safari hii kwa ukali, na muda huohuo mwandishi mwenziye alinifikia na kuninyanyua wima.

Nilikuwa katika mateso makubwa, kitendo cha kusikia sauti ya mke wangu akiwa anafanya mapenzi na mwanaume mwingine ilikuwa ni adhabu nzito mno maishani. “Gonga mlango” mwenyekiti wa mtaa alimwamrisha yule mhudumu wa kike.

Wakati anataka kugonga, mara akasita. “Vipi?”Issa aliyekuwa tayari kwa kufutoa picha, alimaka. “Mlango upo wazi!” mhudumu akasema. “Eeh!” tukashangaa “Upo wazi”

Baada ya mhudumu kusisitiza kwamba mlango ulikuwa wazi, tukio lililofuatia ilikuwa ni kusukuma mlango na kuingia kwa ghafla.

Lahaulaa!!....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom