Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

SEHEMU YA 98

“Mwanaume kujiua kwa sababu ya mpenzi ni udhaifu mkubwa sana Faraji.”

Afande Mirumbe alizidi kunipasha, kauli yake ilizidi kunifanya nijione mpuuzi. “Siwezi tena kufanya huo ujinga afaande”nilimjibu uso wangu ukionesha kujutia sana.

Alinifungulia pingu akanitaka niwe naripoti kila siku kituo cha polisi hadi pale atakaporidhishwa na mienendo yangu. Jioni ya siku hiyohiyo, niliruhusiwa, nikarudi nyumbani.

Suala langu likawa gumzo mtaani na kwa marafiki. Mama yangu pamoja na dada za zangu walipopata habari zile, kwa kweli walihuzinika sana. Ilikuwa ni aibu kubwa kwa upande wangu. Kutaka kujiua kisa kutoswa na mwanamke. Ilikuwa ni fedheha.

Siku zilikwenda, miezi ikayoyoma. Sikuwahi kumwona wala kuwasiliana tena na Debora, nilikuwa nikiugulia ndani kwa ndani, safari hii nilikuwa tayari kufa kijerumani, lakini sio kutwaa uhai wangu mwenyewe.

Katika hicho hicho kipindi, nikajikuta napata hasara kubwa kwenye miradi yangu ya biashara, nilifunga maduka yangu mawili ya nguo yaliyokuwa pale Kinondni studio, pia saluni zote za sinza nikafanga kutokana na hasaea kubwa.

Nikabakia na duka moja tu la vipodozi ambalo lilikuwa Posta mtaa wa Azikiwe. Mapenzi yalikuwa yamevuruga mno maisha yangu, hata haiba yangu nayo ilinyauka.

Katika kipindi hicho hicho mke wangu wa zamani Nasra, naye alikuwa akijaribu kunioneshea upendo mkubwa kila alipokuwa akija kumwona mwanawe pale kwangu.

Ajabu ni kwamba, moyo wangu kwakwe ulikuwa wa baridi mno, kila nilipofikiria kuwa chanzo cha matatizo yale kilitokana na yeye, sio tu sikumpenda bali nilimchukia!. “Siwezi kuwa na wewe Nasra, sina hisia tena juu yako.” Siku moja nilimwambia, baada ya kujaribu kunishawishi.

“Lakini mwanetu anahitaji malezi ya baba na mama.” “Hilo ulitakiwa ulifahamu tangu mwanzo.” “Usifikirie mabaya yangu tu Faraji, kumbuka mimi naye ni binadamu.” “Hata kama Nasra, lakini dhambi ya usaliti haivumiliki.” “Tafadhali niko chini yako.”

Kila wakati Nasra alisema neno nisamehe, ikafikia hatua nikahisi huenda Nasra anakazana kuniomba msamaha katika kipindi kile kigumu kwangu akiamini inaweza kuwa faida kwakwe kwa kuwa nilikuwa napitia nyakati ninazo hitaji faraja.
 
Usicheke Shunie, hearly anataka kutupakazia tabia za ajabu ajabu za wanaume wa daslama...
hahaha huyo ni mwanaume wa mkoani ".. bwana " wanaume wa dar hatuko hivyo aisee .. pauchi zote zinazouzwa mjini hapa ..so twaanzaje kujiua kisa papuchi !!?
 
Faraji ni mwanaume wa Dar tena mitaa ya Kinondoni Studio..

Wanaume wa mkoani hatumtambui...
hahaa wapii mtoto wa kino hawezi kuwa bwege kiasi hicho ".. huyo faraji ni wakuja hapa mjini " ... yaani mtu wa kinondoni azuzuliwe na papuchi kutoka nguruka huko " umewahi kuona wapi wakati Mk pale pichu kibao tu zimejaa
 
hahaa wapii mtoto wa kino hawezi kuwa bwege kiasi hicho ".. huyo faraji ni wakuja hapa mjini " ... yaani mtu wa kinondoni azuzuliwe na papuchi kutoka nguruka huko " umewahi kuona wapi wakati Mk pale pichu kibao tu zimejaa

Hahahahaha!! Faraji anadhalilisha uanaume..
 
hahaha huyo ni mwanaume wa mkoani ".. bwana " wanaume wa dar hatuko hivyo aisee .. pauchi zote zinazouzwa mjini hapa ..so twaanzaje kujiua kisa papuchi !!?

Halafu eti ana hela na miradi kibao ila anajitia kitanzi kisa uchi wa Debora.. Huyu atakua ana mapenzi ya Kikorea au Kihindi..
 
Halafu eti ana hela na miradi kibao ila anajitia kitanzi kisa uchi wa Debora.. Huyu atakua ana mapenzi ya Kikorea au Kihindi..
Yaani mimi mwenyew nimestaajabu kwakweli mtu ana maduka ya NICU zaidi ya matano mjini ana nyumba .gari .lakini bado anateswa na mwanamke wanawake " huyu sio bure anahitaji kupimwa na mkemia mkuu huyu
 
Hahahahaha!! Faraji anadhalilisha uanaume..
huyu jamaa anaumama " sasa sijui uso wake anauweka wapi " pindi anapokutana na ndugu zake " ... wanamuonaje " baba zee zima eti limetaka kujiua kwa sababu ya utelezi
 
hahaa wapii mtoto wa kino hawezi kuwa bwege kiasi hicho ".. huyo faraji ni wakuja hapa mjini " ... yaani mtu wa kinondoni azuzuliwe na papuchi kutoka nguruka huko " umewahi kuona wapi wakati Mk pale pichu kibao tu zimejaa
 
Yaani mimi mwenyew nimestaajabu kwakweli mtu ana maduka ya NICU zaidi ya matano mjini ana nyumba .gari .lakini bado anateswa na mwanamke wanawake " huyu sio bure anahitaji kupimwa na mkemia mkuu huyu
Hivi mnajua alichokuwa anapewa na deborah ooh mapenzi ni siri ya wawili jamani
 
Hivi mnajua alichokuwa anapewa na deborah ooh mapenzi ni siri ya wawili jamani
hakuna kitu kama hicho .. ukisha kuwa fisi " hata upewe nini !? waona nikama marudio tu ya nacte "... wakati hii simulizi inaanza sialijitapa Kuwait ameshatafuna watoto kibao " wakila namna"... sasa mtu mwenye sifa hizo za ufisi anaanzaje kuwa boya kiasi hicho !!?
 
hakuna kitu kama hicho .. ukisha kuwa fisi " hata upewe nini !? waona nikama marudio tu ya nacte "... wakati hii simulizi inaanza sialijitapa Kuwait ameshatafuna watoto kibao " wakila namna"... sasa mtu mwenye sifa hizo za ufisi anaanzaje kuwa boya kiasi hicho !!?
Hahhaha eti ukishakuwa fisi woiiii
 
Hivi mnajua alichokuwa anapewa na deborah ooh mapenzi ni siri ya wawili jamani

Hata kama alikua anafinyiwa kwa ndani, anasingwa na mafuta ya zaituni au kiuno kinazungushwa kama mapanga ya bombadia, kujiua kisa mwanamke huo ni ufala...

Hadi mtoto kashangaa, kaona dingi fwala tuu...
 
hahaa ukishakuwa fisi utaumizwa na nini sasa !? wakati mifupa yote umeshaitafuna .. hivi itokee mtu kama diamond ajinyonge kisa demu utamuelewa kweli .. jinsi anavyo litembeza !!?
Hahahaa hawezi kukuelewa
 
Hata kama alikua anafinyiwa kwa ndani, anasingwa na mafuta ya zaituni au kiuno kinazungushwa kama mapanga ya bombadia, kujiua kisa mwanamke huo ni ufala...

Hadi mtoto kashangaa, kaona dingi fwala tuu...
Ni zaidi ya ufwala jitu mmekutana ukubwani
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom