Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

SEHEMU YA 93

Katika anguko lile, nikabaini kwamba nilikuwa natumbukia kwenye shimo lenye giza zito.

Kuzimu. Kumbe ndio hivi mtu akiwa anataka kufa inavyokuwa. Niliwaza. Wakati nikiwa natembea kwenye njozi ile, bila kutarajia nikajikuta najibamiza chini.

‘Paaa! na muda huohuo maumivu makali yakanitambaa kichwani mwangu. hapo sikujua tena kilichoendelea.

Na hata kabla sijajua kilichoendelea nafsi yangu ilikwishakiri kwamba mimi ni MAITI. **** Nilifumbua macho kivivu, nuru yenye ukungu ndiyo iliyoanza kuonekana kwenye mboni zangu.

Wakati nuru hiyo ikizidi kung’aa na ule ukungu kuyeyuka kwa kasi ya kinyonga, ndivyo picha ya mwanamke mzuri ilivyokuwa ikijidhihilisha mbele yangu.

Niliyakaza macho kwake na ukungu ukiyeyuka mithili ya kioo cha gari kisafishwacho na ‘wiper’ katika mvua, ndivyo tabasamu lake lilivyozidi kunawiri usoni kwake na kuburudisha nafsi yangu. Mrembo huyo hakuwa mwingine bali Debora. “Nimekufa na mungu ameningiza peponi.

Kumbe kwa Mungu Debora yupo!” nilinong’ona kihaywani. Tabasamu la Debora likapanda cheo na kuwa kicheko kidogo kilichomfanya azidi kuwa mrembo kwenye macho yangu.

“Umeamka.” Sikujua kama ananiuliza ama ananiambia. “Umekuja saa ngapi hapa?” na mimi nikasema. “Tangu nilipopata taarifa zako za kujiua.”

“Sasa mbona sijafa?” “Hujafa wakati unasema Mungu amekuingiza pepeoni! Labda kweli umekufa.” “Nini kilitokea!” “Hayo maswali atakuja kuyajibu mwanamke wako” alisema.

Uso wake haukuonesha kama alikuwa na pendo lilisalia juu yangu. Debora hakuwa na hisia yoyote japo ya huruma tu kwangu, macho yake yalionesha ni kama aliyekuwa akipoteza muda wake kuwa kando ya kitanda changu, hata lile tabasamu lake lilitokana na kichekesho alichokiona kwangu. “Mwanamke wangu!!!....” nilishangaa.

Nikaendelea kuongea “Yupi mwingine zaidi yako Debora, nilikuwa radhi nife kuliko kukukosa, moyo wangu bila wewe si kitu.”

“Usiwe mjinga Faraji, unajua ni kwa kiasi gani umenipiotezea muda wangu kutoka Mwanza hadi huku? na unajua kama…” alisema, kabla hajamaliza, mlango wa wodi ulisukumwa.

Muda huohuo aliingia mke wangu wa zamani, Nasra Mfaume. Naye alipoona nimefumbua macho alinikimbilia na kunikumbatia kwa furaha. “Umeamka mpenzi, ahsante Mungu!
 
SEHEMU YA 94

Hakuna hisia zozote nilizozipata kwa kumbato na hisia za mke wangu yule wa zamani, moyo wangu kwake ulikwisha poa na kuwa wa baridi tangu siku ile aliponiliza machozi kwa kumfumania na mwanaume mwingine wakifanya mapenzi katika nyumba ya kulala wageni.

Alipojitoa kifuani alinitizama usoni machozi yakimlenga lenga.

“Kwa nini ulitaka kijua Faraji, kwa nini?” aliniuliza kwa hisia kali. Sikuwa na hamu ya kuzungumza na mwanamke yule.

Mtu pekee niliyekuwa namwitaji kwa wakati huo ni Debora. Nikageuza shingo kuangalia pale alipokuwa amesimama. Sikumwona. Yayari Debora alikwisha ondoka.

Kuondoka kwa kwakwe kukanikumbusha ile kauli yake ya ‘mwanamke wako’ nikabaini kivyovyote vile atakuwa amendoka kwa kuona nikikumbatiwa na Nasra Mfaume.

Sasa amekasirika! Anadhani nasra ni mwanamke wangu. “Kwa nini umenikumbatia?

Nani amekuruhusu uniguse?” nilimkalipia kwa ukali Nasra kwa kuamini yeye ndiye amesababisha Debora aondoke.

“Umesababisha Debora amendoka hebu nipishe.” Nilizidiku kucharuka. Nikataka kusimama nimfute. Lakini nikajikuta narudi kitandani, mkono wangu mmoja ulikuwa umefungwa pingu.

Sasa akili yangu ikakaa sawa bin sawia nikatambua pamoja na kwamba nilikuwa kitandani pia kumbe nilikuwa chini ya ulinzi wa jeshi la polisi kwa kosa la kujaribu kujiua.

NILIKUWA nimeghafirika. Mke wangu wa zamani Nasra alibaki akiniangalia kwa masikitiko makubwa.

“Wewe ndiye chanzo cha haya yote, kama ungejituliza kwenye ndoa yako, nisingepitia mateso yote kiasi hiki,” niliongea kwa uchungu sana. Nilikuwa nimelala chali.

Machozi mepesi yalinichuruzika na kumwagikia masikioni kisha kitandani. Nasra mfaume alibaki kimya, lakini uso wake ukajawa na majuto.

“Debora ndio sababu ya wewe kutaka kujiua?” Nasra aliongea kwa sauti ya kunong’ona lakini iliyojaa simanzi.

Sikupenda kabisa kuendelea kuzungumza na mwanamke yule, roho yangu ilikuwa na kinyongo kwakwe, niliona uwepo wake pale ni kama kejeli tu dhidi yangu.

Mzizi wa matatizo yote yale, ilitokana na yeye. “Kama ungejituliza kwenye ndoa yetu, leo nisingekuwa hapa,” nilimwambia kwa ghadhabu.
 
SEHEMUYA 95

Mara, muda huo huo, mlango wa wodi ukafunguliwa, wakaingia watu wanne.

Miongoni mwao alikuwa ni dada wa kazi wa kazi, yeye alikuwa amemshika mkono mwanangu Mwanda, mwingine alikuwa ni daktari pamoja na jamaa mmoja ambaye alivaa suruali na shati zuri lililochomekewa mkanda nje. Kwa kumwangalia mara moja nikabaini alikuwa ni askari kanzu.

Mtoto wangu Mwanda alinifuata na kunikumbatia kifuani. Watu wengine wakasimama kando ya kitanda changu. “Baba ulitaka kujiua?” mtoto akaniuliza.

Watu wote walikuwa kimya, wakiniangalia mimi na mwanangu. Nilijisikia aibu kubwa. “Baba unataka ufe, kisha mimi nibakie na nani?” mtoto alizidi kuhoji.

Ingawa alikuwa mtoto mdogo wa miaka mitano tu. Lakini maswali yake yalikuwa mwimba mkali kifuani mwangu. Kwa kweli nilizidi kujiona punguani mbele ya kundi lile la watu waliokizunguka kitanda changu.

Mwanangu alikuwa akizungumza kwa hisia kali huku machozi yakijikusanya machoni kwakwe. Sikuwa na jibu hata moja la kumpa mtoto wangu, nilikuwa baba mjinga nisiyetakiwa kuigwa katika jamii.

“Pole sana Faraji, unajionaje sasa?” baada ya ukimya, hatimaye dokta aliyekuwa amevaa koti jeupe na miwani ndogo ya macho aliniuliza. “Niko vizuri.”

“Mshukuru sana msichana wako wa kazi Faraji, kama siye yeye, pengine muda huu, mwili wako ungekuwa chumba cha kuhifadhia maiti, ukisubiri kuzikwa.” Alisema. Ilikuwa ni kauli nzito, iliyoniingia ndani kabisa ya mshipa wa damu. Kadhalika ilikuwa ni kauli iliyozindua fikra zangu.

Fikra za kwa nini niko hai? Tangu niliporejewa na fahamu sikuwa nimewaza, ilikuwaje hadi nikawa sijafa ilihali katika hatua za mwisho nilijiona katika shimo la kuzimu. Penzi la Debora lilinifanya kipofu na kiziwi. Penzi la mwanamke yule lilinifanya nipoteze sifa za uanaume.

Penzi lake lilinifanya nionekane wa hovyo kutokana na utashi wa kijinga ulitokea zaidi moyoni. Ila sasa, angalau kauli ya doktari ilinipa mwangaza wa kufahamu hadithi ntingine ya uzima wangu, kumbe kuna uhusiano wa moja kwa moja na Tatu.
 
SEHEMU YA 92

Roho ya mauti ilikuwa imenivaa, sikuona ubaya wa jambo lile, sikuipa nafasi akali yangu kufikiria mara mbili ama mara tatu na zaidi.

Kila kitu nilichofanya kilisukumwa kwa utashi wa hisia.

Kabla sijajiua sauti ya kimalaika ikanikumbusha “Sasa ukijua nani mwenye hasara? unamkomesha nani. Unajiua Debora anabaki duniani anaponda raha. Ujinga huo.”

Bahati mbaya ibirisi alikwisha nizingira pande zote za dunia, nilichofanya ni kuanza kuhesabu moja hadi tatu kabla ya kujiachia na kujinyongelea mbali: “Moja, mbili, tatuuuu!” nikajiachia!!. Kamba ikanibana shingoni kwa nguvu.

Nikaanza kutapatapa kwa kukosa hewa, kadiri sekunde zilivyojongea ndivyo nafsi yangu ilivyohitaji kuhema, niliishika ile kamba ili nijinasue. lakini wapi. Sikuwa na nafasi nzuri ya kujiondosha.

Uzito wa mwili ukazidi kuikaza zaidi ile kamba shingoni, nikauhisi mkojo ukinitoka na kulowanisha suruali yangu. Kila sekunde zilivyozidi kupotea ndivyo nilivyoona nguvu zikiniishia.

Hamu ya kuishi ikanirejea. Nikajitahidi kwa nguvu zangu zote ili nipige kelele za kuomba msaada, bahati mbaya sauti haikutoka.

Na hata kama sauti ingetoka, bado nisingeweza kupata msaada kwa wakati sahihi. Kamba ilikuwa imebana shingo yangu.

Muda ule ilikuwa ni usiku mkubwa, msichana wangu wa kazi na mwanangu Faraji walikuwa wakikoroma huko vyumbani mwao. “Nilikwambia usijiue, unaona sasa unakufa!!”ile sauti ya pili ilinilaumu fikirani nikiwa naipambania roho yangu.

Nikataka kusema neno ‘nisaidie’ nikajikutana nalitamka kimoyomoyo. “Jitahidi kuizua kamba usife, piga kelele.” Sauti ilinisihi. Wakati huu nikaitii sauti ile ya kimalaika.

Nikaing’ang’ania kamba kwa nguvu ili isizidi kunikaba shingoni, kadhalika nikijitahidi kupiga kelele. Bahati mbaya sauti haikutoka zaidi ya kuishia kukoroma kama chura au gari lililoishiwa mafuta.

Muda huohuo, giza la ajabu likazikumba mboni zangu, na wakati giza linagubika mbele ya ngu nikajiona naelea katika anga maili nyingi kutoka ardhini.

Halafu muda huohuo nikajiona naanguka kwa kasi kuelekea chini, ajabu nikawa sifiki. Katika anguko lile, nikabaini kwamba nilikuwa natumbukia kwenye shimo lenye giza zito. Kuzimu.

JARIBU KUTABIRI KITU GANI KITATOKEA.... . TUKUTANE KESHO HAPAHAPA
duh !!, huyo nyau anataka kujiua kwaajili ya papuchi .. wanaume wa mikoani bwana shida kweli aisee
 
duh !!, huyo nyau anataka kujiua kwaajili ya papuchi .. wanaume wa mikoani bwana shida kweli aisee

Faraji ni mwanaume wa Dar tena mitaa ya Kinondoni Studio..

Wanaume wa mkoani hatumtambui...
 
sehemu ya 95

NILIKUWA nimeghafirika. Mke wangu wa zamani Nasra alibaki akiniangalia kwa masikitiko makubwa.

“Wewe ndiye chanzo cha haya yote, kama ungejituliza kwenye ndoa yako, nisingepitia mateso yote kiasi hiki,” niliongea kwa uchungu sana. Nilikuwa nimelala chali.

Machozi mepesi yalinichuruzika na kumwagikia masikioni kisha kitandani. Nasra mfaume alibaki kimya, lakini uso wake ukajawa na majuto. “Debora ndio sababu ya wewe kutaka kujiua?”

Nasra aliongea kwa sauti ya kunong’ona lakini iliyojaa simanzi. Sikupenda kabisa kuendelea kuzungumza na mwanamke yule, roho yangu ilikuwa na kinyongo kwakwe, niliona uwepo wake pale ni kama kejeli tu dhidi yangu.

Mzizi wa matatizo yote yale, ilitokana na yeye. “Kama ungejituliza kwenye ndoa yetu, leo nisingekuwa hapa,” nilimwambia kwa ghadhabu. Mara, muda huo huo, mlango wa wodi ukafunguliwa, wakaingia watu wanne.

Miongoni mwao alikuwa ni dada wa kazi wa kazi, yeye alikuwa amemshika mkono mwanangu Mwanda, mwingine alikuwa ni daktari pamoja na jamaa mmoja ambaye alivaa suruali na shati zuri lililochomekewa mkanda nje. Kwa kumwangalia mara moja nikabaini alikuwa ni askari kanzu.

Mtoto wangu Mwanda alinifuata na kunikumbatia kifuani. Watu wengine wakasimama kando ya kitanda changu. “Baba ulitaka kujiua?” mtoto akaniuliza. Watu wote walikuwa kimya, wakiniangalia mimi na mwanangu.

Nilijisikia aibu kubwa. “Baba unataka ufe, kisha mimi nibakie na nani?” mtoto alizidi kuhoji. Ingawa alikuwa mtoto mdogo wa miaka mitano tu.

Lakini maswali yake yalikuwa mwimba mkali kifuani mwangu. Kwa kweli nilizidi kujiona punguani mbele ya kundi lile la watu waliokizunguka kitanda changu. Mwanangu alikuwa akizungumza kwa hisia kali huku machozi yakijikusanya machoni kwakwe.

Sikuwa na jibu hata moja la kumpa mtoto wangu, nilikuwa baba mjinga nisiyetakiwa kuigwa katika jamii. “Pole sana Faraji, unajionaje sasa?” baada ya ukimya, hatimaye dokta aliyekuwa amevaa koti jeupe na miwani ndogo ya macho aliniuliza. “Niko vizuri.”

“Mshukuru sana msichana wako wa kazi Faraji, kama siye yeye, pengine muda huu, mwili wako ungekuwa chumba cha kuhifadhia maiti, ukisubiri kuzikwa.” Alisema.
 
SEHEMU YA 96

Ilikuwa ni kauli nzito, iliyoniingia ndani kabisa ya mshipa wa damu. Kadhalika ilikuwa ni kauli iliyozindua fikra zangu. Fikra za kwa nini niko hai?

Tangu niliporejewa na fahamu sikuwa nimewaza, ilikuwaje hadi nikawa sijafa ilihali katika hatua za mwisho nilijiona katika shimo la kuzimu. Penzi la Debora lilinifanya kipofu na kiziwi. Penzi la mwanamke yule lilinifanya nipoteze sifa za uanaume.

Penzi lake lilinifanya nionekane wa hovyo kutokana na utashi wa kijinga ulitokea zaidi moyoni. Ila sasa, angalau kauli ya doktari ilinipa mwangaza wa kufahamu hadithi ntingine ya uzima wangu, kumbe kuna uhusiano wa moja kwa moja na Tatu, dada wa kazi za ndani.

Nilimwangalia Tatu aliyekuwa kando, alionionesha tabasamu la faraja, Mwanangu Mwanda yeye alitokwa na machozi kabisa, mama yake naye alikuwa akizivuta kamasi kwa ndani, huku akiwa na kilio cha ndani kwa ndani.

“Naombeni mtupishe kidogo tuzungumze,” yule jamaa, ambaye ni askari kanzu naye akaongea.

Watu wote wakaondoka, tukabakia wawili tu, mimi na yule jamaa. “Naitwa sajent Geofrey Mirumbe, natoka mkoa wa kipolisi Kinondoni,” alijitambulisha.

Nikatikisa kichwa kuashiria nimemwelewa. Akaendelea. “Pole kwa maswahibu Faraji.” “Nimekwisha poa.” “Tatizo ni nini hasa?” “Maisha tu afande.” “Yamekufanya nini maisha hadi ufikie hatua ya kutaka kujiua?”

“Ni hali ya kushindwa kustahimili msongo.” “Msongo huo umetokana na nini hasa?” “mambo binafsi tu.” “Nahitaji kujua.” Jamaa alisema kwa amri.

“Ni mambo ya kiuchumi” nilimdanganya. “Kivipi, umefilisika?” “Ndio,” nilizidi kudanganya. Askari yule alitoa pumzi nyingi nje, kisha akaniambia huku akiwa amenikazia macho makali ya kipolisi:

“Kadiri utakavyoendelea kunidanganya, sintakuwa na simile zaidi ya kukuburuza mahakamani Faraji.” Alisema akaendelea. “Na Usisahau kujaribu kujiua ni kosa la jinai. Na kwa kukukumbusha tu.Kwa mujibu kifungu cha 217 cha kanuni za adhabu.

kujaribu kujiua adhabu yake ni kifungo cha miaka miwili jela. Je uko tayari ukapoteze muda wako jela ukiacha familia yako uraiani huku wewe ukitumikia adhabu ya kosa la kijinga kama hilo?”
 
Sehemu ya 97

Yule kamanda alinihoji. Nilitikisa kichwa kumkatalia, sikuwa tayari kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma zile. “Nikikwambia ukweli utanisaidia afande ili hili suala lisifike huko?”

“Usinipe masharti ya jambo ambalo ni wajibu wako…” kamanda Mirembe aliunguruma kwa ukali. Ukimya wa kama dakika zinama ukapita. Kisha akaniambia.

Ni wajibu wako kuwa mkweli na ni haki yangu pia kukusaidia kama mwanaume mwenzangu ambaye ninafamilia kama yako… ”

Akaendelea “Hata hivyo…Nitakuwa tayari kulimalimiza hili suala endapo nitaridhishwa na mienendo yako ya kimaisha, sijui umenielewa?”

“Nimekuelewa afande.” “Haya nieleze kinaganaga cha wewe kutaka kujiua” alisema.

Tofauti na polisi wengi yule jamaa uso wake ulionesha hali fulani ya utu. Kwa kweli alikuwa ni moja kati ya polisi wazuri sana miongoni mwa wengi niliowahi kukutana nao.

Sikuwa na jinsi ilibidi nimsumulie kila kitu bila kuficha. “Pole sana, nilijua tu, lazima sababu iwe ni mapenzi, wanawake sio watu wa kuamini sana maishani.

Ni vigeugeu mno hao viumbe, mnaweza kukubaliana kuimba wimbo wa iana moja, kesho akiamka usishangae anaimba kibwagizo cha wimbo mwingine kabisa.

Hata hivyo huna budi kumshukuru Tatu, kama sio ujasiri wake labda sasa hivi jina lako lingeanza na neno Marehemu” “Hivi ilikuwaje hadi akanisaidia?” nikamuuliza.

“Kwa mujibu wa maelezo yake, anasema akiwa chumbani, majira kama ya saa saba kasoro, mwanao alimka na kulalamika tumbo linaumuma. Akamua kuja kugonga mlango chumbani kwako ili akujilishe hali ya mwanao.

“Anasema, aligonga sana mlango bila majibu, akaamua kusukuma na kuingia ndani na hakukuona, ndipo akataka kurudi tena chumbani kwake. Lakini kabla hajapiga hatua, akasikia mkoromo mbaya na vitu vikijigonga gonga ndani ya maliwato.

Alipochungulia ndipo alikuona ukining’inia katika kamba huku ukirusha rusha miguu.” Alichofanya ni kukimbilia stuli sebuleni na kukata kamba, ukajipigiza chini kama furushi, hiyo ndio ilikuwa slama yako.”

Maelezo yale yalinisisimua sana, ilikuwa ni mithili ya hadithi ya kusadikia, lakini ndio ukweli ulikuwa hivyo, nafsi yangu ilikiri Mungu alikuwa bado na makusudi na mimi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom