Nilimaanisha nakupa heshimaSasa kwa nn unipe shikamoo jamani
HahahahahaHapo sasa Faraji ameanza kuwaza kama mwanaume. Alaaaaaah hehehe
Sawasawa
Ajiue bwana. Mambo gani ya kipumbav kuteswateswa
Kesho utasoma ya darful
ila huyo jamaa sijui faraji " ndio baadhi ya wanaume wa mkoani wanaochafua sifa yetu wanaume wa dar " jitu limetoka mkoani kasulu sijui ujiji bado linaushamba shamba kama vumbi la kwenye mihogo "... jamaa ni zoba sanaSEHEMU YA 87
Maishani mwangu nilikuwa na tabia moja. (nitaileza) tabia ambayo kimsingi siyo nzuri na ningependa mtu mwingine ajifunze kupitia mimi.
Kila nilipokuwa nikipitia wakati mgumu, nilikuwa napenda kusikiliza na kufuata ushauri ambao ulikuwa unanifurahisha nafsi, hata kama ushauri huo siyo mzuri, kwa kuwa tu umenipendeza ungekuwa swahiba wangu mkubwa kwa kunipa ushauri huo na mwisho wa maongezi ungeondoka na zawaidi kibao kutoka kwangu.
Hivyo basi, watu wote walinishauri nirudi kwa Debora nilijikuta napenda nikae nao muda wote kisha tuzungumzie namna nitakavyorudi kwenye mikono ya Debora. Na kwa kweli watu wangu walipoijua tabia hii walinipa ushauri vile nilivyopendelea mimi.
Wachache sana waliokuwa wakiniambia ukweli wa mambo ulivyo. Ndipo katika kuishi kwa mateso makubwa kwa masiku kadhaa, mwishowe nikafuata ushauri wa marafiki. Usiku mmoja wa saa nne nikampigia simu Debora.
Wakati simu ipo sikioni mapigo ya moyo yalikuwa yakinidunda kama vile simu ile ilikuwa imetegeshwa bomu kwamba itakapo pokelewa tu ingelipuka.
Simu iliita kwa muda mrefu, bila kupokelewa. Nikapiga tana. Safari hii iliita kidogo tu ikapokewa na sauti ya mwanaume.
“Hellow” sauti ya kiume ilisikika.
Nikajikutana nashindwa kuongea, fikra lukuki zikapita kichwani mwangu juu ya mtu aliyepokelea simu ya Debora. Mtu huyu ni nani? Hawara wake? Yupo na Debora kitandani usiku huu? Nilijiuliza kimoyomoyo
“Hellooow” suati ile ilinisemesha tena kwa nguvu.
“Mwenye simu yuko wapi?” hatimaye nikaunguruma.
“We ni nani?” jamaa naye akaniuliza kwa pozi. Nilihisi tumbo likifukuta joto. Nikaamini kivyovyote vile jamaa ni bwana wa Debora. “Wewe ni nani unayeniuliza mimi hivyo?” nikaunguruma tena kwa sauti yenye mamlaka.
Simu ikakatwa. Nikabaki nimeduwaa simu ikiwa bado imenata sikioni. Roho iliniuma vibaya sana, wivu wa mapenzi ukanichemka mwilini na nafsini.
Debora yupo na mwanaume mwingine wasaa huu. Kitandani! Wanafanya mapenzi au wamelala. Fikra hizi zilipita akilini mwangu, nikajikuta napatwa na donge rohoni.
Sikukoma. nikapiga tena. Safari hii nikajisemea kimoyomoyo kama akipokea tena yule jamaa mpuuzi, matusi yote ya duniani yangekuwa halali yake.
Hehee .. kapewa za usoSEHEMU YA 88
Simu iliita kisha ikapokelewa. Naam! wakati huu aliyepokea alikuwa ni Debora.
“We nani?” Debora aliongea kwa ukali mara baada tu ya kupokea. Sauti yake ilionesha kama aliyetoka usingizini. Nilihisi akili ikinizunguka. Vipi leo naulizwa mie nani na Debora.
Mwanamke huyo aliyenipenda kwa hisia kali hadi kulia machozi, ambaye alifanya kila awezalo kunitoa katika machungu na simanzi ya usaliti wa mke wangu wa mwanzo, Nasra Mfaume. Akaahidi kunipenda maisha yake yote, leo ananiuliza mimi nani?
inamaana namba yangu alikwisha ifuta kwenye simu yake? Namba hiyo aliyokuwa ameishika kichwani mwake kama kiitikio cha wimbo wa taifa. Hata ungeamshwa usiku wa manane angetaja namba yangu kwa usahihi, amekwisha isahau na kuifuta kwenye simu yake?
Mambo yote hayo niyafikiria kwa harakaharaka sana simu ikiwa sikioni huku nikitakiwa kujibu swali nililoulizwa. Mimi ni nani?
“Hunijui Debora?” na mimi nikamuliza kwa upole. “Sauti yako sio ngeni.”
“Ebwana wee!” nilimaka.
“Niambie wewe nani?” akaongea kwa amri.
“Hebu amka usingizi. Unashindwaje kunijua leo.”
“Kama hutaki kusema wewe ni nani nakata simu.” Debora akang’aka.
“Faraji.” Hatimaye nikasalimu amri, nikajibu kwa mkato huku nikihisi hasira kali rohoni.
“Unasemaje?” akaniuliza kwa kiburi.
“Ushanijua ama bado hujanikumbuka?”
“Sema shida yako.”
“Ulimpa nani simu yako Debora?”
“Hiyo ndio shida uliyonayo?”
“Tuanzie hapo kwanza kisha nitakueleza sababu ya kukupigia.”
“Wewe kama nani unaniuliza swali hilo?”
“Hujui mimi ni nani kwako?” “Hebu zungumza mambo sensitive we’ mtu, maswali gani hayo unauliza?”
“Ni wiki mbili tu zimepita tangu tutarafiane, leo mwenzangu ushapata mwanaume mwingine.”
“Kwani kuna kanuni ama utaratibu wowote katika hilo?”
“Nisikilize Debora…” nilisema. Nikaendelea.
“Usiwe kama Nasra, wewe ni mwanamke wa kipekee sana, nakutegemea kwenye maisha yangu. Tafadhali.”
“Sikia wewe!!” Debora aliongea, ni kama vile alichukulia nilikuwa mpuuzi mmoja nisiye jielewa.
“Usiwe mwanaume mpumbavu…”aliniambia. Akaendelea.
“Mrudie mkeo mlee mtoto wenu. Mimi tayari nina maisha yangu mapya, ni mwanamke wa kigogo mkubwa tu hapa nchini, kama hutaki kupata matatizo kwenye biashara zako kaa mbali na mimi.
Inasikitisha sana...SEHEMU YA 87
Maishani mwangu nilikuwa na tabia moja. (nitaileza) tabia ambayo kimsingi siyo nzuri na ningependa mtu mwingine ajifunze kupitia mimi.
Kila nilipokuwa nikipitia wakati mgumu, nilikuwa napenda kusikiliza na kufuata ushauri ambao ulikuwa unanifurahisha nafsi, hata kama ushauri huo siyo mzuri, kwa kuwa tu umenipendeza ungekuwa swahiba wangu mkubwa kwa kunipa ushauri huo na mwisho wa maongezi ungeondoka na zawaidi kibao kutoka kwangu.
Hivyo basi, watu wote walinishauri nirudi kwa Debora nilijikuta napenda nikae nao muda wote kisha tuzungumzie namna nitakavyorudi kwenye mikono ya Debora. Na kwa kweli watu wangu walipoijua tabia hii walinipa ushauri vile nilivyopendelea mimi.
Wachache sana waliokuwa wakiniambia ukweli wa mambo ulivyo. Ndipo katika kuishi kwa mateso makubwa kwa masiku kadhaa, mwishowe nikafuata ushauri wa marafiki. Usiku mmoja wa saa nne nikampigia simu Debora.
Wakati simu ipo sikioni mapigo ya moyo yalikuwa yakinidunda kama vile simu ile ilikuwa imetegeshwa bomu kwamba itakapo pokelewa tu ingelipuka.
Simu iliita kwa muda mrefu, bila kupokelewa. Nikapiga tana. Safari hii iliita kidogo tu ikapokewa na sauti ya mwanaume.
“Hellow” sauti ya kiume ilisikika.
Nikajikutana nashindwa kuongea, fikra lukuki zikapita kichwani mwangu juu ya mtu aliyepokelea simu ya Debora. Mtu huyu ni nani? Hawara wake? Yupo na Debora kitandani usiku huu? Nilijiuliza kimoyomoyo
“Hellooow” suati ile ilinisemesha tena kwa nguvu.
“Mwenye simu yuko wapi?” hatimaye nikaunguruma.
“We ni nani?” jamaa naye akaniuliza kwa pozi. Nilihisi tumbo likifukuta joto. Nikaamini kivyovyote vile jamaa ni bwana wa Debora. “Wewe ni nani unayeniuliza mimi hivyo?” nikaunguruma tena kwa sauti yenye mamlaka.
Simu ikakatwa. Nikabaki nimeduwaa simu ikiwa bado imenata sikioni. Roho iliniuma vibaya sana, wivu wa mapenzi ukanichemka mwilini na nafsini.
Debora yupo na mwanaume mwingine wasaa huu. Kitandani! Wanafanya mapenzi au wamelala. Fikra hizi zilipita akilini mwangu, nikajikuta napatwa na donge rohoni.
Sikukoma. nikapiga tena. Safari hii nikajisemea kimoyomoyo kama akipokea tena yule jamaa mpuuzi, matusi yote ya duniani yangekuwa halali yake.
Haaa haaa.mapenzi yamemvurugaHafi ila cha moto anakiona!