SEHEMU YA 63
Na muda huo huo, akaingiza mkono wake kifuani mwangu na kunichezea viyweleo. Ingawa nilikuwa nimelewa lakini kauli ile iliniingia, na mwili wangu ukapatwa na misisimko ya mapenzi kutokana na alivyokuwa akinipapasa.
Nikasahau kabisa uvumi nilowahi kuusikia. Ni kuhusu mwanamke huyo kuishi na maambukizi ya virusi vya Ukimwi, hisia za mapenzi zikanivaa, nikawa tayari kumpa penzi.
Mwanamke yule akaendelea kunipapasa kifuani huku pumzi za huba zikimtoka. Viganja vyake vikashuka hadi ndani ya suruali yangu, akawa anamchezea mzee wa kazi aliyekuwa wima kama msumari.
Tendo lile likanifanya nitamani kumalizana naye palepale gizani, si nikaanza kufungua zipu ya sketi yake…. “No, no, nenda kachukue room,”alininong’oneza kwa sauti laini ya mahaba.
Nikaona isiwe tabu, wacha nikachukue chumba. Kwa kuwa palepale La charse pub huwa kuna huduma ya vyumba vya kulala wageni, nilimweka pembeni Debora, nikaenda kaunta kuulizia kama bado kuna nafasi ya vyumba.
Bahati ilikuwa upande wangu, nilipata chumba, nikalipia kisha nikamrudia Debora. Nilimshika mkono nikamwongoza chumbani kama kondoo aongozwaye machinjioni.
Baada ya kuingia ndani, nilisaula nguo zangu zote, Debora naye akafanya hivyo, kila mtu alikuwa na haraka ya kukata kiu ya penzi kwa mwenziye. Baada ya kuwa saresare maua, tukaanzishiana tena michezo ya kupashana joto.
Kwa kuwa mchezo wa kupashana joto ulikwishaanza tangu tukiwa nje, mule ndani haukudumu japo kwa dakika tatu, tukajikuta tumezama kwenye ulimwengu mwingine wa raha.
Asubuhi kulipokucha, mimi ndiye nilikuwa wa kwanza kuamka, Debora alikuwa bado anakoroma, akili ilipokaa sawa, nikajikuta napatwa na hofu kwa kitendo cha kuteembea na Debora.
Kama nilivyosema mwanzo, mwanamke yule amewahi kuhusishwa kuishi na maambukizi ya virusi vya Ukimwi.
Nikiwa pale kitandani, nilikosa raha, nikajilaumu kwa kuzidisha ulevi kiasi cha kushindwa kuzidhibiti hisia zangu.
Nikajiambia kimoyomoyo, kama nitakuwa nimeambukizwa Ukimwi, mke wangu Nasra hawezi kukwepa lawama maana bila yeye, nisingefikia kuishi maisha yale. Nikiwa kwenye hali ile Debora aliamka.
“Mambo sweet,”akanisalimia. “Poa tu, umeamkaje?” “Niko fresh, yaani najisikia mwepesi!...Ugwadu nili