Simuelewi wifi yangu

Simuelewi wifi yangu

I wish ni mimi. Full kukarangiza kudaadeki. Full ku care aisee.

Mi sioni shida iko wapi. Muache ajinafasi kwa raha zake.

Mi singemuacha aguse chochote. Hamna kinachoharibika hapo eti labda uwe lazy bones.

Na nishakuhisi wewe ni lazy bones. :smile-big::smile-big:
 
Mi kwa kweli jikoni kwangu ndiko ufalme Wang ulipo.naamini hivyo hats nikienda kwa mtu.
Unless uniambie njoo tupike.
Kila nyumba na kila mwanamke ana namna yake ya upishi.
Sitegemei mdada analilia mtu kuingia jikoni kwake.
Naona kama intrusion of privacy aisee.

Naanzaje kuingia kwa wenyewe jikoni naanza kupika. Ndio kujionyesha fundi au?

Wakiniomba sawa tena nitafurahia but azawais I keep off.
 
haaa haaaa mapema mno inawezekana hata kaja anaumwa au anastress za huko atokako labda nae anahisi utamuuliza ww unakimbilia jf na hapo n kwako jaman jitahidi tu kutimiza majukumu yako sie kwetu wifi nae mume hvyo lazma ahudumiwe ipasavyoo. Kaa nae chini muwe marafiki unaweza ukagundua mengi sana
 
Wifi yangu amekuja juzi. Ni dada wa mume wangu. Alipofika sikuwepo nilikua kazini. Nilipofika toka kazini nikamkuta amelala. Nikamsubiri alipoamka akaja tukatambulishana tukaendelea na maongezi. Jana siku ya pili kaamka kaoga kawasha tv, akitoka anaenda kulala. Anaamka anakula anarudi kulala. Leo siku ya tatu ameamka mapema tu ameoga karudi tena kulala. Mwenzenu Simuelewi huyu mwanamke mwenzangu hata mlango wa jikoni haujui. Nimekua kama nina waume wawili. Kuolewa kuna shida wenzangu.

Ningekuwa mimi mmeo ningesha kufukuza aidha urudi kwenu ukafundishwe adabu.
 
Shukuru tu ndugu yangu maana anaonejana mkimya. Mawifi wakimya ni wazuri kwa afya ya ndoa yako
 
mtoa mada pia anatatizo but msimponde sana ila fuata ushauri hapo juu. Mkaribishe akikataa hilo jingine
 
Mbona huyo ndio bonge la wifi? Wanawake hatuna jema, angekuja akapita kila mahali huko jikoni ungesema anaharibu bajeti. Mie wifi zangu tunapendana kweli. Manake nikienda kwa kakangu nachangia stori na kuangalia tv! Na mgeni anaekaa tu hanipunguzii wala kuniongezea. Unaingia kwa watu unajipeleka jikoni unapika kuku, kumbe kuku wao kwenye friza anapikwa jumapili tu! Si ugomvi huo!

cha kufanya bi shosti asubuhi muulize wifi unajiskia kula nini? Kama hakipo muombe mumeo, muambie wifi ana hamu na kuku, naomba hela. Mbona utapendwa kote kote? Mnashindwa ndoa wenyewe!
 
Huyo ni mtu mstaarabu sana sababu hapo ni kwako sasa akikurupuka mpaka jikoni wakati hajakaribishwa ungesema anakuingilia!!!!!!!
Either ways wewe siku ya tatu tu ushaanza mpaka ku post huku, je angekuja mgonjwa kukaa hapo mwezi mzima!!!????
Kwanza wewe mtu wa kazini so hushindi hapo kazi anafanya dada labda sasa wewe nini taabu yako!!!!???
Leo wkend kesho sikukuu muamshe mwambie mwende sokoni mkanunue vya kununua na mkija fikia naye jikoni mpe nyanya muombe akusaidie wakati wewe unafanya mengine then anzisha story kuwa uko happy kwa ujio wake sababu sikukuu mtapika vyakula mbalimbali kwa kushirikiana, mtamaliza mapema na ku enjoy.................


Sikuhukumu ila ni kama hupendi ndugu wa mume au una ghubu flani kama sio mvivu..........ungekuwa mke wangu ningekuchana live!!!!!

Asipoelewa basi tena........
 
Heh!
Angefikia kujitanua kama kwake sebuleni unamkuta,jikoni ndio anaagiza kipikwe nini ungefungua thread ngapi?
 
Heh!
Angefikia kujitanua kama kwake sebuleni unamkuta,jikoni ndio anaagiza kipikwe nini ungefungua thread ngapi?

Yaani angekuwa na tabia kama yako au!!!?????
Matusi hayaruhusiwi...................................😛hoto:😛hoto:
 
Khaa we nawe unatuaibisha,mwanamke mwenye ndoa yafaa awe mvumilivu kiasi ,wewe siku tatu tu ushaanza kuona kero ,alaf kwa staili hii unaonekana ushapandikizwa mbegu ya kuwa 'mawifi ni wakorofi' wakati pengine ukorofi tunauanzshaga wenyewe!.... Wewe hapo ni nyumbani kwako yanini uanze kusemezana na mtu mambo ya jikonii?? Muache wakupita huyoo usitafute visababu vya kuona eti ndoa ama mawifi wabaya fanya shughuli zako kama ulivyozoea!! Huwezi jua labda ana matatzo je!......Binafsi sipendi kupikiwa na nafurahia uwepo wa watu kama hao nachakalika mwanzo mwisho asipate la kusema!!...... VUMILIA!! !!
 
Back
Top Bottom