Mbepo yamba
JF-Expert Member
- Aug 5, 2012
- 1,110
- 1,475
Ndugu zangu, niko kwenye mahusiano kwa muda wa miaka miwili sasa na msichana ambaye nimempenda kweli kweli. Plan yangu ni kumfanya mke wangu wakati wowote kuanzia sasa. Tumeshirikiana mambo mengi tuu.
Tatizo lipo hapa. Ni mwanamke anayenificha mengi sana. Yaani ni mtu ambaye hata picha tuu akinitumia WhatsApp huwa anaifuta hapo hapo.
Tofauti na mimi ninayemueleza karibu kila ratiba yangu, yeye ni mara chache sana kuniambia. Naweza kumuuliza kuhusu ratiba na akawa ananipa majibu ya juu juu na ya kunikatisha tamaa tuu.
Na ndio yuko hivi kwenye mambo mengi. Hayuko wazi kabisa kwangu.
Suala hili linanipa wakati mgumu sana kuendelea mbele na mchakato wa ndoa. Je, inawezekana yeye ana plan nyingine?
Msaada wenu jamani ili ama niokoe penzi hili au nigeukie ustaarabu mwingine.
Tatizo lipo hapa. Ni mwanamke anayenificha mengi sana. Yaani ni mtu ambaye hata picha tuu akinitumia WhatsApp huwa anaifuta hapo hapo.
Tofauti na mimi ninayemueleza karibu kila ratiba yangu, yeye ni mara chache sana kuniambia. Naweza kumuuliza kuhusu ratiba na akawa ananipa majibu ya juu juu na ya kunikatisha tamaa tuu.
Na ndio yuko hivi kwenye mambo mengi. Hayuko wazi kabisa kwangu.
Suala hili linanipa wakati mgumu sana kuendelea mbele na mchakato wa ndoa. Je, inawezekana yeye ana plan nyingine?
Msaada wenu jamani ili ama niokoe penzi hili au nigeukie ustaarabu mwingine.