Ndugu zangu, niko kwenye mahusiano kwa muda wa miaka miwili sasa na msichana ambaye nimempenda kweli kweli. Plan yangu ni kumfanya mke wangu wakati wowote kuanzia sasa. Tumeshirikiana mambo mengi tuu.
Tatizo lipo hapa. Ni mwanamke anayenificha mengi sana. Yaani ni mtu ambaye hata picha tuu akinitumia WhatsApp huwa anaifuta hapo hapo.
Tofauti na mimi ninayemueleza karibu kila ratiba yangu, yeye ni mara chache sana kuniambia. Naweza kumuuliza kuhusu ratiba na akawa ananipa majibu ya juu juu na ya kunikatisha tamaa tuu.
Na ndo yuko hivi kwenye mambo mengi. Hayuko wazi kabisa kwangu.
Suala hili linanipa wakati mgumu sana kuendelea mbele na mchakato wa ndoa. Je, inawezekana yeye ana plan nyingine?
Msaada wenu jamani ili ama niokoe penzi hili au nigeukie ustaarabu mwingine.
Asante mkuu. Bahati nzuri kwa kweli tumefungua joint saving account. Hili la posa ngoja nijitahidi kulifanya ila kwa akili maana neno nakupenda limekuwa wimbo kwakeHuyo ana two competitive bonds zina fighting kuwa muwazi mtashtukia.
Unaweza fanya yafuatayo
1. Mtolee hata posa tu ili ndugu wajue
2. Weka msimamo wa maamuzi yako
3. Wekeni mipango ya pamoja kwaajili ya maandalizi ya kujenga familia. Mfano fungueni joint account mnaanza kutunza hela for future
4. Mfanye kila hatua ya maendeleo yenu ashiriki.
6. Msisitize uwazi ndo msingi wa mahusiano na ndoa.
Ukiona anagomea hayo ujue huyo hana nia na wewe kuna mtu kamshika mapembe. Ila siku atakuja kumwagwa na atakukumbuka.
Mwambie kabisa unampenda sana ila siku kuirudisha moyo nyuma asije laumu.
Tafuta mwanamke anayeweza kukidhi matarajio yako, usimlazimishe huyo huenda sio wako ama mko wengi mmpangwa foleni, kuna vitu sio vya kulazimisha,Ananiuma maana nampenda sana mkuu
Mimi natamani wanawake ndio wachangie zaidi hapa ili watuambie huwa hawataki nini na ama huwa wanataka nini, wanaume mkichangia hapa itaonekana kama tunachochora, mtoa mada amesema haelewi afanye nini, sasa bidadas ndio waweza kusema ukweli kwani naamini tatizo hilo sio lake peke yake linawasumbua wengi na wanaweza kusaidiwa hapa.Niliambiwa na mtu kuwa "asiyekushirikisha matarajio yake bhasi uwezekano mkubwa ni hakuoni katika future yake, asiyekushirikisha maumivu yake bhasi haupo moyoni mwake"..
Mkuu nimesoma between lines na inaonesha umeshaelewa mchezo mzima ila unasubiri watu wakupe ujasiri tu. Jiamini
🤔🤔🤔🤔🤔🤔🤔🤔Kuna watu wengine hua sio wa kujielezea elezea na sio wawazi..mfano mimi ninaweza kua naongea vitu lakini asilimia kubwa unajikuta unajielezea wewe mwenyewe lakini mimi sijielezi..nakumbuka wasichana kadhaa wameshawahi niambie "sasa mbona wewe hauniambii vitu kuhusu wewe na familia yako" maana sijui kitu chochote kile enh? Nawauliza unataka kujua nini...?
Sasa unakaa na mwanamke miaka miwili bado hata mwelekeo wa kumuoa hamna unategemea nini sasaNdugu zangu, niko kwenye mahusiano kwa muda wa miaka miwili sasa na msichana ambaye nimempenda kweli kweli. Plan yangu ni kumfanya mke wangu wakati wowote kuanzia sasa. Tumeshirikiana mambo mengi tuu.
Tatizo lipo hapa. Ni mwanamke anayenificha mengi sana. Yaani ni mtu ambaye hata picha tuu akinitumia WhatsApp huwa anaifuta hapo hapo.
Tofauti na mimi ninayemueleza karibu kila ratiba yangu, yeye ni mara chache sana kuniambia. Naweza kumuuliza kuhusu ratiba na akawa ananipa majibu ya juu juu na ya kunikatisha tamaa tuu.
Na ndio yuko hivi kwenye mambo mengi. Hayuko wazi kabisa kwangu.
Suala hili linanipa wakati mgumu sana kuendelea mbele na mchakato wa ndoa. Je, inawezekana yeye ana plan nyingine?
Msaada wenu jamani ili ama niokoe penzi hili au nigeukie ustaarabu mwingine.
Ukamilifu wake wala siuhitaji. Hana sura ta kuvutia kwamba ni mrembo kiviile, ila moyo wangu umemridhia yeye pekee. Ukamilifu siyo kigezo kwangu mkuuHakuna aliye mkamilifu isipokua muumba tu!