sinafungu
JF-Expert Member
- Feb 13, 2010
- 1,524
- 863
anaishi na mwanamke miaka kumi sasa, wamejaaliwa kuzaa watoto 2, mume ana watoto zaidi ya 5 kabla ya kuishi na mwanamke huyo. hivi karibuni kumekuwepo kutoelewana baina yake na mwenzake, mwanamke anafanya jitihada wafunge ndoa jamaa anadai hana uwezo kwa sasa, jitihada za mwanamke zimepelekea hadi ndoa kutangazwa kanisani , jamaa baada ya kuona hivyo alimfuata padri akamfokea sana, siku mbili baadaye ndo akaja kwangu kunipa short stori na akanitaka tuende naye kwa kaka wa mkewe kwa malengo ya kuulizia mahali na utaratibu mzima .( LAKINI AKITAFUTA NJIA YA KUKWAMISHA JITIHADA ZA MKEWE) mimim nikamuuliza kwani tatizo ninini akaniambia yule mwenza wake hawapendi watoto wake hivi hajamuoa, na kishawafukuza ndg kadhaa wa jamaa pale nyumbani, hivi hajamuoa je akimuoa itakuwaje na imani yake ni ya KIKATOLIKI. nikaenda kwa shemerji yake huko tukakuta jamaa wanatusubiri ilikuwa kazi , baada ya majadiliano ilitajwa mahali tsh 600000/= yeye akasema hana kiasi alichonaco ni laki na nusu, wakamueleza anaweza kulipa hata kidogokidogo amebaki na msimamo, kwa kuwa ndg hawajui lililoko ndani yake nao wakakataa kumpunguzi, tukaondoka bila maelewano na jamaa ndivyo atakavyo, huku mwanamke ametoa tishio kama hatamuoa asije juta kwani lolote laweza kutokea, sasa mimi nageuzwa chambo ngd zangu mnisaidie ushauli ni vipi niwasaidie ama kujivua zigo hilo.