Habarini wanajukwaa,
Naombeni kujuzwa maana ya hii kitu kwani na amini kuna watu wenye ufahamu zaidi,. Katika harakati zangu za kutafuta green pasture nilikutana na wahindi watatu tukakubaliana kuanzisha kiwanda hapa nchini, basi wiki iliyopita siku ya jumatatu wahindi wakaja kutoka India kwani walikua safarini, na mimi nilikua Arusha.
Ilinipasa kusafiri kutoka Arusha kuelekea Dar es salaam na kushukia katika hoteli moja, ambapo pia na muhindi mmoja alikua akilala apo. tulikubaliana kuwa gharama zote ni juu yao nilikaa daresalaam kwa takribani siku 6 tukiwa tunaendelea na mambo mbalimbali ikiwemo kuandaa brandy name na mambo mengine ya usajili.
KISA CHENYEWE!!!
Ilikua siku ya jumamosi ambapo muhindi mmoja alinipigia simu na kuniuliza nipo wapi nikamjibu nipo maeneo ya Kimara matembezi akaniuliza Je funguo za rum kwangu niko nazo nikamjibu nimeziwacha reception basi akasema sawa, Kichwani nikajiuliza maswali mengi kwa nini aliniuliza kuhusu funguo za chumbani kwangu??? Au amehisi nmeamua kutembea nazo?? Au anataka kuniibia vyeti vyangu au passport yangu ya kusafiria?? Kwa nini aulizie kuhusu funguo?? Niliwaza sana.
Sikukawiaa sana nikarudi hotelini na kwenda kukagua chumbani kwangu sikukuta kitu chochote kimeibiwa lakini baada ya kuzidi kukagua uvunguni nikakutana na kitambaa chekundu pamoja na uzi wa kushonea pia mashuka yalikuwa kama kuna mtu aligusa kwani nilipoondoka niliacha baadhi ya document kwenye angle ya kitanda na hivo kukuta zimesogezwa mpaka katikati ya kitanda.
Niliamua kwenda kumfuata muhudumu wa mapokezi na kumuuliza ni nani ameingia chumbani kwangu alishtuka sana na kuniuliza kwani kuna kitu kimeibiwa?? sikumjibu nikamuuliza tena kwa ukali nani ameingia chumbani kwangu?? basi akanijibu kuwa boss wako alikuja akaniambia nimpe funguo aliingia dakika chache na kutoka. Nikamuuliza tena umejuaje kuwa yeye ndiye boss wangu?? Akajibu kwa kuwa ndiye anayekuja kulipia garama zako za hoteli na chakula.
Nikamwambia siku ingine kwa mteja mwingine nakuomba usirudie hiki kitendo mpaka upate ruhusa kutoka kwa muhusika Je ningekuta vitu vyangu havipo ungefanyaje?? Baada ya kumdodosa sana aliniambia kuwa yule mhindi anapenda kuchoma udi chumbani kwake na kufanya sala kwa namna fulani lakini kwa jinsi alivo nielezea nikatambua kuwa huwa atakuwa anafanya Meditation ila muhudumu alishindwa kutambua.
sikumuuliza yule muhindi kuhusiana na yeye kuingia chumba changu bila mimi kuwepo wala kupata ruhusa yangu, nilimwambia mhudumu anibadilishie chumba kingine na kuendelea na kazi yangu, ila bado najiuliza alikuja kufanya nini chumbani kwangu?? Je niendelee naye katika biashara au niachane nao???