Simuamini tena mke wangu!

Simuamini tena mke wangu!

sm tym wanawake tuna matatizo sana! inashangaza kuona unashindwa kumlipia mwanao wa kumzaa ada ya shule, eti km vipi mtoto akae nyumbani! dah! we mwanamke! pole sana bro. swala la kufanya biashara na dadaake its ok, but kubwa ni mtt kumpa haki yake, na isitoshe mume mambo yameyumba na ukweli mke kaambiwa, dah! aisee hii dunia inamazito sana! binadamu tuna roho za ajabu sana! km kuna ugomvi kati yenu, hizo tofauti zisipelekee kumweka mtoto kwny mazingira magumu na akakosa haki yake ya msingi tena ELIMU! jamani!!

...kweli kabisa, hapa mwanamke amekosea,basi tu!...na cc muda mwingine wanawake tunamatizo
 
Haya ndiyo matatizo ya wanaume wa cku hizi wanaoa wanawake wenye kazi ili kupunguziwa majukumu yao! Aaaagh! Kwani kutuma pesa home ni tatizo? Labda kama hajakushriksha! Je,mlikubalianaje kuhusu matumizi yenu ya pesa?au umemkurupusha tu?afterall mwanaume ndiye mwenye jukumu la kutunza familia zakwangu nitatoa nikiamua tena penye ulazima eboo! usilalamike kakope! ndo uanaume huo!

Ukiwa na msimamo kama huu kwa maisha ya sasa, sitashangaa kusikia nyumba yenu ikiporomoka kila uchwao.
Mlipokula kiapo cha ndoa mlikubaliana kuishi wawili kama mke na mume. Maisha ya ndoa ni ya kusaidiana as much as a man has to make ends meet in his family. Siku hazilingani na sio kila siku mwanaume atakuwa analeta fedha kukidhi mahitaji ya familia. Kama mwanamke amebarikiwa vijisenti si mbaya kusukuma gurudumu la familia pia. Inaitwa kusaidiana na hapo ndipo ndoa msingi wake ulipo. Watoto ni wenu wote. Usidhani baba akishindwa kuwalipia ada anafedheheka peke yake. You are their mother too. It would be too embarassing to know that you had means to help your children and you decided to step aside and leave responsibility to your husband.
Mwanamke mwema
biblia imemtaja kwenye Mithali 31: 26, 28
Mke mwema anawafundisha watoto wake njia za Mungu na pia anawatunza kwa upendo. Huwafundisha kwa hekima na kuwaelekeza njia iwapasayo kuiendea. Mithali 22:6

Mithali 31:14, 16, 18
Mke mwema anatafuta kwanza ushauri wa mumewe kabla ya kutumia fedha na pia anafanya manunuzi kwa hekima. Ni muangalifu kununua bidhaa zenye ubora kulingana na mahitaji ya familia yake.Efeso 5:23

Mithali 31:13, 19, 27
Hutumia muda wake vizuri na kuhakikisha anakamilisha kazi zake za kila siku. Kamwe hapotezi muda katika kufanya mambo ambayo hayampendezi Mungu na yasiyo na faida.


 
me nilifikiri labda iile dhana yenu ya haki sawa mnaamaanisha itekelezwe kwa vitendo,kumbe nayo mnataka muipate kwa kupewa...hakika MKIWEZESHWA MNAWEZA
Haya ndiyo matatizo ya wanaume wa cku hizi wanaoa wanawake wenye kazi ili kupunguziwa majukumu yao! Aaaagh! Kwani kutuma pesa home ni tatizo? Labda kama hajakushriksha! Je,mlikubalianaje kuhusu matumizi yenu ya pesa?au umemkurupusha tu?afterall mwanaume ndiye mwenye jukumu la kutunza familia zakwangu nitatoa nikiamua tena penye ulazima eboo! usilalamike kakope! ndo uanaume huo!
 
Kimtokacho mtu ndo huwa kimeujaza moyo wake! Wapo waliotoa mawazo ya maana na pia wapo waliotoa ushauri usiofaa! Nawashukuru wote kwa mitizamo yenu kazi imebaki kwangu kufanya maamuzi sahihi na kwa muda muafaka!
 
MKUU inatakiwa wyf aamini kwamba wakati unapeleka mahari kwao ulimaanisha kwamba Unauwezo wakumtunza pamoja na watt wako Ikibidi fanya km nilivyofanya mm unamtemesha KZ anakaa hom anakula nakulala pamoja na watt wake 5yrs! baadae unamtafutia miradi ya Familia km ataweza kuiicmamia hiyo ni kwa faida yake! Ila mbinu hii nikwa wa2 waco waoga waMAISHA! bila hivyo ndg utalialia kila cku! Inatakiwa wanaume 2jue ukiona mwanamke anakupa PESA awe MKE or Gfriend Twink twice niwaGUMU sn hata akikupenda namna gan!!
 
Majukumu makubwa kama elimu ya watoto wako, matumizi yote ya nyumbani, kujenga nyumba, kununua vitu muhimu vya ndani pamoja na gari...... usitegemee pesa ya mke. Fanya majukumu hayo, acha pesa za mke kwa matumizi yake. Angalizo: Endapo kama mke wako ana kipato kikubwa zaidi kuliko wewe, hapo inabidi mpange na kuamua ili kupeana majukumu ya kifamilia.
 
Mimi na wife tumebahatika kupata watoto 2 wa kiume! Mm nafanya kazi dsm yy anafanyia mara. Kijana wetu yupo grade 1 kwenye hizi academy!

Takriban wiki kadhaa nilienda kumsabahi! Niligundua amekuwa akiwatumia ndg zake pesa nyingi paspo kunijulisha nahisi kuna business wanafanya yy na dadake! Niligundua baada ya kumwambia kwamba mm kulingana na ujio wangu siko fresh kiuchumi hivo jitahidi ada ya mtoto make ndo wanafungua mwezi wa tisa kwa kifupi alinipa majibu ya kunikatisha tamaa akadai hana hela na isitoshe kwenye ubini wa mtoto anaandikwa yy au mm? Km sitaki kumsomesha akae nyumbani! Nikamuuliza km waweza tumia ndg zako malaki ya pesa unashimdwa nn kumlipia mwanao? Akakanusha wakati mm nilicheki kwenye mpesa ametuma pesa two times tena last month! Tukazinguana sana mm nikapanda basi nikasepa kwa ufupi hana mpango wa kusaidiana na mm ktk kusukuma gurudumu!

Nimfanyaje mke wa namna hii?

Hakuna ndoa hapo
 
na wewe acha ubahili kutoka dar es salaam hadi mara unaenda kwa bus??mafast jet yote hayooo ukomeeeeee
 
Mie naona kafanya jambo jema sana.
Maana ninyi wanaume huwa hamuaminiki hata kidogo.
Madame B!
Hata wewe washabikia mfumojike/dume.
Haki gani mnazodai sasa!
A wanawake, wanawake ndio wanawake
Hawajui wanataka au kudai nini
Ni majanga tu.

Bazazi!
 
Last edited by a moderator:
pole yako
mkeo ni mchaga???? maana wachaga ndio wana hiyo kasumba mbovu ,yakusema mume sio ndugu yako jenga kwenu upate pakufikia akishajenga wanakaa wao!!!kama ni mchagga umeliwa mbe!
 
pole jamani ila hela ya mwanamke ni ya saluni na pamba nyepesi, jitahidi majukumu ya familia ujibebe mwenyewe na sahau kipato cha mkeo.
 
pole yako
mkeo ni mchaga???? maana wachaga ndio wana hiyo kasumba mbovu ,yakusema mume sio ndugu yako jenga kwenu upate pakufikia akishajenga wanakaa wao!!!kama ni mchagga umeliwa mbe!

Ooh!thanx ngoja niwatahadharishe kaka zangu
 
Madame B!
Hata wewe washabikia mfumojike/dume.
Haki gani mnazodai sasa!
A wanawake, wanawake ndio wanawake
Hawajui wanataka au kudai nini
Ni majanga tu.

Bazazi!

Kwa hiyo mwataka mfanye jema nyie tu?
Tupisheni huko Bazazi.
 
Last edited by a moderator:
Edson vaa viatu vya baba wa familia na hudumia familia yako. Pesa za kina mama zinawatosha kwa saloon na kucheza kibati si vinginevyo

labda mkeo ambaye anapata pesa ndogo hivyo haoni cha kufanyia zaidi ya hayo uliyoyataja, lkn sisi wengine pesa zetu zinafanya mambo makubwa sana hadi wanaume wanatuheshimu kwa hayo tunasomesha tunajenga tunaendesha maisha na familia zetu tunanunua magari kwa pesa tulizozifanyia kazi, acha dhana potofu kuh wanawake.
 
Tunza familia baba, hupaswi kuangalia sms za hela afu ndo uombe hela ya ada. Je kama usingekuta hizo sms za mpesa ina maana usiongeomba.
 
Well said....tatizo pia wanaume hamuaminiki mkilegezewa na wake zenu ndo mmejipatia ruhusa za kuhonga....gangamala hudumia familia..
 
ndoa....!
..ss mkuu hata hatuujui makubaliano yenu kwny masuala ya pesa!
..km mwanaume ni jukumu lako hilo bt ukisaidiana na mama,.hapa wanawake lazima tukubali kusaidiana kupo! Ila sio mwanaume ss ndo ujiachie kila kitu afanye hyo mkeo
..najua sio muda wote mtu unakuwa na hela, ila hapo mwanamke nae hajafanya fresh,ss akiacha mtt akae nyumbani atakuwa amemkomoa nani!?
...big up my Mom aisee!

Thumb up!
 
Ukimuuliza huyo mwanaume kama alishawahi kutuma hela kwa wakwe zake utashangaa majibu. Utashangaa zaidi ukimuuliza na yeye ameshatuma hela ngapi kwao ndo utakoma. Hukawii kukuta anamjengea dadake!
mara ya mwisho kumtumia pesa mama mkwe ilikua janauary mwaka huu! Huwa nawatumia mara kwa mara tena kabla wife hajapata kazi!
 
Back
Top Bottom