tukiwa tunakaribia mwisho wa mwaka na manunuzi ya simu yanazidi kuongezeka makampuni mbalimbali yameanza kutangaza list ya simu zao zitakazopata hii update ya pipi ya kijiti. nimeamua kueka list ya simu zitakazopata hii update kwa pamoja ili ukienda kununua simu ujue unanunua simu gani ili baadae ipate hii update na kuondoa kero ya kununua simu kila siku.
sony xperia
sony wao wametangaza simu zao zote zinazoanziwa na heru Z basi zitapata update ya lolipop hii inainclude hadi simu kama xperia z, z ultra, zr na zl ambazo ni za toka mwaka 2013. hivyo kama una plan ya kununua xperia inayoanziwa na herufi z au unamiliki simu kama hiyo usiwe na wasiwasi utapata update yako muda ukifika.
motorola
motorola amefurahisha wengi kwa kutoa update hii kwa karibia simu zake zote, hii ni list ya simu zake zitakazopata hii update
1.moto x zote ya mwaka jana na huu
2.moto g zote za mwaka jana na huu
3.moto e
4.droid ultra
5.droid maxx
6.droid mini
inafurahisha kuona simu kama moto E inapata hii update kulingana na bei yake ilivyo rahisi.
htc
htc yeye ameconfirm simu nne tu ndio zitapata lolipop ambazo ni
1.htc one m7
2.htc one m8
3.htc one mini
4.htc one mini 2
lg
1.lg g3
2.lg g2
asus
1.zenfone zote
2.padfone infinity
3.padfone s
htc one m7 na m8 zitapata update hii ndani ya siku 90 toka ilipotangazwa hii update.
hao ni manufacture watatu wameshatangaza, wengine wakiongezeka nitaupdate list.