Heshima zenu?
Kwanza kabisa mara nyingi HR Department za ibongo huwa wanaweka malengo na ni ngumu au hayana uhalisia ktk utekelezzaji na ndio ujanja ujanja unapoanzia, nina uzoefu mkubwa wanakuambia tareh 20 usaili wakati hata kufupisha orodha (shortlisting) hawajafanya/hawajamaliza.
Na kama ikitokea sehemu ya kuajiriwa halafu mnaambiwa wote mliomba muende kwenye usaili hiyo sehemu ni ya kuogopa kama ukoma. Huwezi kuita watu wote waliotuma maombi kwenye usaili kama kweli uko makini.
Kama ningelikuwa mimi ningesubiria tu simu wasipopiga basi, RIZKI HAIVUTWI KWA KAMBA!!