Sasa ili kujua kama simu camera yake ina quality tuangalie kitu gani?
Cha muhimu zaidi ni sensor. Simu yenye sensor kubwa na megapixel chache itakuwa na mapixel makubwa ambayo yataruhusu mwanga mwingi na kuifanya picha itokee vizuri.
Hii sensor inapimwa kwa inch, kwa simu camera zake sensor haifiki inch 1 hivyo inavyokaribia inch 1 ndio jinsi sensor ilivyo nzuri
Kitu chengine kinachofanya camera itoe vizuri ni flash, simu yenye xenon flash inapiga picha nzuri sana hasa usiku na inaweza pia kupiga picha kitu kilicho kwenye motion kama vile mtu anaepiga mbizi kwenye maji, simu yenye flash za kawaida yaani led flash inakuwa inatoa picha vibaya kuna wakati picha zinatoka vizuri zaidi kama utaweka led flash off.
Chengine kinachofanya camera iwe nzuri ni optical image stabilization (ois) ambayo husaidia camera isitingishike pale mikono inapotingishika hivyo kuruhusu mwanga mwingi pamoja na kuondoa blur kwenye picha. Simu zenye ois hutoa result nzuri za picha kwenye mwanga mdogo.
Chengine ni software optimization za kampuni, mfano apple, lg na samsung wanatumia sensor za sony kwenye simu zao lakini wote hao hapo juu wana camera nzuri kuliko sony, hii inaionesha sony ana software mbaya ya camera kuliko hao hapo juu.
Kuna mambo mengine madogo madogo pia yanaweza ongeza quality ila hayo hapo juu ni makuu