Simu za Mikopo Scheme Mpya za Utapeli

Damaso

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2018
Posts
6,132
Reaction score
10,514
Katika miaka ya karibuni, mfumo wa kununua simu kwa mkopo maarufu kama “Lipa Mdogo Mdogo” umeenea sana Afrika Mashariki. Kampuni kama Watu Credit zimejijengea jina kwa kuahidi wananchi kupata simu haraka bila kuwa na fedha zote mkononi. Ndani ya saa chache unaweza kuondoka na simu mpya uipendayo kama Samsung Galaxy A06, huku malipo yakigawanywa kidogo kidogo kila siku au kila wiki.


Nitoe angalizo, kwa namna yoyote sina nia wala dhumuni lolote la kuharibu biashara ya mtu/ watu wala kampuni yoyote ile.

Kwa mtazamo wa kwanza, mpango huu unaonekana kuwa suluhisho kwa watu wenye kipato kidogo. Lakini nyuma ya urahisi huo kuna simulizi nyingi za maumivu ya kifedha ambazo watu huzipitia.

Katika soko la kawaida la nchi za Afrika Mashariki, simu aina ya Samsung Galaxy A06 siyo simu ya gharama kubwa sana. Nchini Tanzania, bei yake inapatikana kati ya takribani shilingi 245,000 hadi 350,000 mtanirekebisha wauza simu kama nimekosea tarakimu.

Kwa nchini Kenya, bei yake huanzia takribani KSh 11,500 hadi 14,800, sawa na takribani shilingi 230,000 hadi 350,000 za Tanzania.

Lakini hadithi ni tofauti pale ambapo unapoinunua kwa mkopo, taratibu usipaniki utaelewa.

Baadhi ya watumiaji hudai baada ya miezi kadhaa ya kulipa kila siku, jumla ya fedha walizolipa huzidi hata shilingi 500,000, huku bado wakibakiwa na deni kubwa la kurejesha. Mfumo wa malipo ya kila siku—kwa mfano karibu shilingi 2,900 kwa siku—unaweza kuonekana mdogo mwanzoni, lakini unapojumlishwa kwa miezi mingi hugeuka mzigo mkubwa.

Ukisoma matangazo yao mara kadhaa utaona wakitoa mchanganuo wa gharama kwa siku, wiki pamoja na mwezi ila hawatoi hesabu kamili ya jumla ya pesa ambazo unatakiwa kulipa kukamilisha malipo. Kwa kwa mtu masikini au wenye kipato cha chini kusikia malipo ya 2500 kwa siku ataona ni kitu rahisi ila piga hesabu 2500 kila siku kwa mwaka ni shilingi ngapi?

Wengine wanasema presha huongezeka zaidi kwa sababu simu inaweza kufungwa moja kwa moja endapo malipo hayatafanyika kwa wakati. Ndani ya mfumo, mteja anaweza kuonywa kuwa ana masaa chache tu kabla kifaa chake hakijazimwa.

Ni kweli kabsa, kuwa mipango ya mkopo imewasaidia watu wengi kumiliki simu za kisasa maarufu kama Smartphones, hasa wale ambao wasingeweza kulipa pesa yote kwa mkupuo ama kwa pamoja. Simu leo siyo anasa tu; ni chombo cha kazi, biashara na mawasiliano na hitaji la lazma.

Lakini kuna wakati kama watanzania tunapaswa kukubaliana kuwa baadhi yetu tunawaumiza sana watanzania wa kipato cha chini. Kwa watu wenye kipato kidogo, mpango huu unaweza kugeuka kuwa kama mtego wa madeni.

Mtu anachukua simu akiamini kuwa analipa kidogo kidogo, lakini mwishowe wanajikuta wamelipa 2X au hata zaidi ya thamani halisi ya simu.

Ndipo swali la msingi linapoibuka: Je, hizi ni huduma za kifedha zinazowasaidia wananchi, au ni mfumo unaowalazimisha maskini kulipa gharama kubwa kuliko thamani ya bidhaa?
 
Ungekuja na takwimu halisi, Bei ya Samsung A06 kwa kukopa ni......, ili tujue watu wanapigwaje.

Mfano: down-payment ya A06 ni Tsh. 60,000
Malipo daily ni Tsh.2,376/- ambayo weekly ni Tsh.16,632/-
Monthly ni Tsh.66,528/-

Ukilipa kwa miezi sita Tsh.399,168/-

Jumlisha na ile down-payment Tsh.60,000/- + Tsh.399,168/- = 460,000.

Huyu masikini ambaye hana uwezo wa 350,000 ya pamoja, akitoa 460,000 kuna shida gani?

Watanzania wengi tunaweza kutoa 2,000 daily lakini 500,000 ya pamoja hatuna.
 
Simu used zipo nyingi tu Kariakoo, second hand kutoka Dubai, Korea kusini, China na Amerika.

Kwa nini mtu usinunue hiyo wakati unasikilizia michongo mingine! Anyways, hakuna kupangiana maisha. Wacha wapigwe tu
 
Hata ukikopa hela ujenge au ununue gari utalipa zaidi ya ulichochukua. Ila inaonekana kwa mikopo ya simu unalipa mara mbili au zaidi ya ulichokopa. Kuna namna wakopaji hawapati elimu sahihi na kujua kiwango atakacholipa mwishoni. Wanabaki kuona 2 500/- kwa mwezi ni kidogo.
 
Sio kazi ya mtoa huduma ya mkopo kukokotoa utalipa kiasi gani mpaka umalize mkopo, elimu ni bure kabisa siku hizi ila mmeamua kuwashabikia akina Dotto Magari. Umeambiwa malipo kwa siku, ukaambiwa kianzio, ukaambiwa muda wa malipo ni miezi mingapi bado tu unataka umezewe na jumla ya malipo.

Pia kampuni ya Watu Credit sio ya Mtanzania bali mzungu ambaye sina hakika nadhani ni Mgiriki. Kwahiyo hakuna Mtanzania anamnyonya mwenzake hapo.

Mwisho, mtu badala ya kukopa nunua cash. Hakuna excuses hapo.

Ningekuwa nashauri labda ningeiomba serikali ifanye regulations na urasimishaji mkubwa kwa wanaokopesha na wanaokopa ili wote wawe wawajibikaji na gharama ya mkopo ipungue. Tanzania hii riba ni kubwa kwa kila mkopo sababu ya defaulters kuwa wengi, matapeli, wadanganyifu, wasio na address sahihi kwahiyo mkopeshaji anaweka riba kubwa kufidia hasara chache humo kwenye biashara. Ila kuna nchi ukikopa huna pa kwenda popote utafuatwa na isitoshe raia sio wendawazimu kama sisi wabongo. Taifa kukosa ustaarabu ni hasara kubwa.
 
Good point. Ila kama simu ya 200,000/- unaishia kulipa 500,000/- kidoogo ni mtihani. Na wakopaji wengi wanachemka.
 
Same applies kwa pikipiki zao, unaanza na down-payment ya Tsh.400,000 then unalipa Tsh.86,000 weekly.

Tsh.86,000×4×12 = Tsh.4,128,000 + down-payment ya Tsh.400,000 ni kama Tsh.4,528,000

Wakati huo, ungeenda na Tsh.3,350,000(?) ungenunua HLX125 bila kusumbuka.
 
Good point. Ila kama simu ya 200,000/- unaishia kulipa 500,000/- kidoogo ni mtihani. Na wakopaji wengi wanachemka.
Mkuu,
Ukishaitwa mkopo, lazima mkopeshaji aangalie faida, kuna risks factors nyingi hapo. Ikiharibika kabla ya mkopo kuisha kuna namna wanafanya hapo. Tusiangalie tu upande wa mkopaji, hata mkopeshaji anakuwa kwenye risks nyingi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…