1. SAMSUNG GALAXY S23 ULTRA
Hii ina kamera poa na kama haitoshi imetimia kila Kona kuliko flagship nyingine yoyote ile. Kama utaipata kwa milioni 2 na nusu kwenda juu sio mbaya. Ila rangi zake haziendani na reality according to some reviewers lakini general colour science ni nzuri pia, zoom iko poa, portrait ziko poa kila kitu kiko poa hapa. Ukishindwa hii chukua hata Samsung Galaxy S23, Galaxy S23+ au hata S22 Ultra
2. APPLE IPHONE 14 PRO MAX
Hii ni level moja na huyo Samsung S23 Ultra ila picha zake zina very high contrast kuliko kawaida, nadhani ni image processing ya iOS ndio inapelekea hii hali, ila colour accuracy iko poa sana. Kwa Bongo hili ni chaguo zuri coz inapatikana madukani kiurahisi.
Ukishindwa bei ya hii chukua hata iPhone 14 Pro, iPhone 14 Plus au hata iPhone 13 Pro Max
3. GOOGLE PIXEL 7 PRO
Hii ndio ninarecommend zaidi kuliko simu nyingine yoyote ile kwa sababu ya bei yake. Ali Express inauzwa TSh 1,800,000/=
Honestly kwa bei hii huwezi kupata simu yenye kamera bora kushinda hii
Ukishindwa bei ya hii chukua hata Google Pixel 7
4. XIAOMI 13 ULTRA
Hii inakuja na two colour modes, Leica Authentic na Leica Vibrant na kuna uwezekano picha zake ni more natural kuliko hizo nyingine zote hapo juu. Global version ni very expensive so ni heri uagize kutoka China.
Kwa ajili ya biashara tumia mode ya Leica Authentic kwa sababu picha zake zina rangi za uhalisia kuliko Leica Vibrant.
Ukinunua Xiaomi 13 Ultra unapata advantage ya kuwa na vitu kama variable aperture na Leica colour science hivyo inakuruhusu kutumia photographic style unayoipenda, it's like a camera with a phone in it
Ukishindwa bei ya hii unaweza kupata Xiaomi 13 Pro au hata Xiaomi 12S Ultra.
5. OPPO FIND X6 PRO
Hii ni simu iliyo suprise phone reviewers wengi kwenye kamera mwaka huu kwa sababu ilikuwa ni beyond expectations kwa kampuni kama Oppo kuja na simu yenye kamera bomba kama hii. Ikiwa unataka kwa ajili ya biashara basi itakufaa kwa sababu bei yake ni rafiki sana na kamera yake iko poa kuliko flagship nyingi sana. Ukishindwa hii chukua Vivo X90 Pro Plus
Nimekutajia simu tano ila
Chief-Mkwawa amesema kila flagship inatoa picha nzuri. Kwa hiyo tofauti na hizi tano kuna flagship nyingine nyingi tu zinazoweza kukufaa kwa picha.
Nilichofanya mimi ni kukupa mifano tu ya hizo flagship zenye kamera nzuri
Unaweza kuangalia flagship nyingine mtandaoni, Google iko open ikiwa unataka kutafuta knowledge