Simu iliyobadilisha maisha yangu

Simu iliyobadilisha maisha yangu

Kwahiyo ulichapiwaaa jiangalie tenaaa ukija kwangu nako watakuchapi maana wewe si mbunifu kuwa kama chupa ya chai utakufa kwa pressure
 
Jiulize utaacha wangapi?uvumilivu na moyo wa msamaha ni vitu muhimu sana katika maisha ya ndoa Dada and no one is perfect
 
Nashawishika kuamini kwamba mmama hajapata penzi la kijana.
Isipokuwa ni mbinu zake tu chafu za kuharibu kupitia upande wa pili ili uhusiano ufe ili ajichukulie dogo dogo yake kiulaini.
Kwa maana nyingine angekua kwenye uhusiano angeelewa kwanini mkataba unaisha. Na hivyo kama kuna wa kumlaumu basi angebaki kujilaumu yeye mwenyewe. Alishindwa nini kum-maintain!!
 
Nawasabahi wanaMMU.


Ni Jumapili kama hii wiki moja imepita nilipokea simu ambayo imebadilisha maisha yangu na mtazamo wangu kuhusu mahusiano. Well, nilipokea simu na upande wa pili nikasikia sauti ya mwanamke, na kwa sauti ni mtu mzima.

Aliongea mengi na mwisho akaniambia kama unataka kujua zaidi kuhusu mume wako nitafute. Basi Jumatatu, akanipigia tena na nilikuwa nasita kuonana naye, basi akaanza kuniambia wewe hauko serious.

Basi kama wazungu wanavyosema - Curiosity killed the cat, but satisfaction brought it back.

Imagine kumeet na mtu haumfahamu then mawazo ya tindikali na mambo mengi yakanijia kichwani, nikaanza safari kuonana naye huku nasali novena takatifu.

Well sikuamini nilipokutana naye - ni mama mtu mzima na age diff kama 18 - 20 years. Basi nikampa heshima na kukaa, nikamuuliza mama ishu ni nini na ana mahusiano gani na mume wangu (nikidhania ni biashara) Aisee, mapigo ya moyo yalisimama sekunde kadhaa aliponiambia wanamahusiano ya kimapenzi.

Na aliponiona kama nashangaa as in seriously, akaniambia nijuwe na yeye pia ana hamu na hajakuwa na mwanamume 4 years baada ya ndoa yake ya miaka 28 kuvunjika.

Akanitolea na picha kabisa na roho inamuuma kweli kuhusu mume wangu na anajitetea hakumwambia ana mke na watoto.


To cut a long story short, wamekuwa na mahusiano miezi 3 na anavyoongea alikuwa ameambiwa mahusiano yaishe lakini she was not happy na inamuuma sana. Mwisho akaniambia mi ndoa ya 28 years imevunjika sembuse ww wa miaka michache.

Basi angesubiri na mimi nifikishe hiyo 28 na ndo amshambulie huyu kiumbe dhaifu. I am so angry, not for me only but for all those men who cheat on good women na wanawake ambao wanavunja ndoa za watu kwa ajili hawana self control au basi watafute wa rika yao.


There are some battles worth fighting but this one am throwing in my towel. Hivi mtu akikuambia ni shetani - seriously miezi 3 ni yeye tu shetani anamwandama?

Kuna mambo magumu napitia wakati huu, everything is looking down but this put the last nail on my coffin.


Swali - Why would a man take the risk of losing a diamond to pick stones?

Pole sana
Seen that, hao majimama washenzi sana kama ndo angekuwa mpenzi tu angeenda mpaka kwa wazazi wako kuwaambia unatembea na bwana ake ndo walivyo na atavuruga mahusiano yenu na kama ana maradhi atawaambukiza. Wanaume nyakati za sasa hawachagui naona maana wanalala na wazee vijana mpaka vitoto vya shule.
 
Just because your marriage is in shatters doesnt mean you have to go wrecking homes!
shame on that old cunt!
 
Maridhiano muhimu, kaeni chini mzungumze....,
Last week maridhiano yaliiokoa nchi...,
Mkiwa na imani ya pamoja maridhiano yataijenga ndoa, mkishindwa bahati mbaya nalo pia ni kuja kumshukuru mungu mmeimaliza ndoa yenu salama na amani...,
Maisha yanaendelea, na binadamu muhimu kuishi kw furaha na amani!
 
Pole sana kwa yaliyokukuta lakini hakuna sababu yoyote ya kufanya maamuzi ya haraka ili kuivunja ndoa. Huyu mama anataka kuvunja ndoa yako kwa mategemeo kwamba mumeo atabaki naye yeye vinginevyo sioni sababu ya yeye kukutafuta ili akwambie mapungufu ya mume wako. Mume wako baada ya kumwambia penzi lao la miezi mitatu limefikia ukingoni akaamua amkomoe ili aharibu ndoa yenu.

Kuwa na subira na uwe na tayari kumsamehe mumeo hasa kama anaona amekukosea kwa aliyoyafanya katika hiyo miezi mitatu. Huyo mama asingeambiwa penzi la miezi mitatu limefikia ukingoni wala asingehangaika kukutafuta hata kwa sekunde moja. Pole sana.
Kabisaaaaaa

Huyo mtumzima anataka wakose wote au aopoe kirahisi.....

Tena angempiga marufuku kumuita na kumueleza ujinga
 
Ndoa ikishaingia mdudu wa kukosa uaminifu, kwangu imekufa. Sihitaji mshauri nasaha kuniambia ndoa iende vipi, naomba huyo mdudu aende mbali kabisa coz for me it will mean divorce. Sitavumilia kuishi na mzinzi, naithamini sana afya yangu.
 
Pole mdada, Mungu akupe macho ya kiroho kuweza kulikabili hili
 
leaving a man bcoz of cheating is like leaving a country or town because it is raining...
 
huyo mama lengolake akuharibie ndoa yako tu ili achukue nafasi yako vizuri....wakati mwingine tumia akili ya ziada we achana na mumeo uone mbaya wako vema......hata kama mumeo kaanguka we unatakiwa ulinde ndoa yako.......hapo ni kazi kwako jaribu hilo....utalimudu...?tupe mrejesho tuu
 
Ndoa ikishaingia mdudu wa kukosa uaminifu, kwangu imekufa. Sihitaji mshauri nasaha kuniambia ndoa iende vipi, naomba huyo mdudu aende mbali kabisa coz for me it will mean divorce. Sitavumilia kuishi na mzinzi, naithamini sana afya yangu.
Hujambo my Eliiii
Japo thread nimeisoma jujuu nimevutiwa na majibu yako. It seems mwanamke ndo amecheat. Suppose ingekuwa wewe ndo umepunguza uaminifu ndani ya ndoa kwa so called uzinzii will you let her go?

Ila nimekumiss

Sent from my SM-J110H using JamiiForums mobile app
 
Ndoa ikishaingia mdudu wa kukosa uaminifu, kwangu imekufa. Sihitaji mshauri nasaha kuniambia ndoa iende vipi, naomba huyo mdudu aende mbali kabisa coz for me it will mean divorce. Sitavumilia kuishi na mzinzi, naithamini sana afya yangu.
Nimependa msimamo wako na inatakiwa iwe hivyo
 
Hujambo my Eliiii
Japo thread nimeisoma jujuu nimevutiwa na majibu yako. It seems mwanamke ndo amecheat. Suppose ingekuwa wewe ndo umepunguza uaminifu ndani ya ndoa kwa so called uzinzii will you let her go?

Ila nimekumiss

Sent from my SM-J110H using JamiiForums mobile app
KOKUTONA long time sana, umepotelea wapi kipenzi?
Suppose mimi ndio nimecheat(which is very unlikely), mke ana uhuru wa kuniacha. Nitaomba anisamehe, lakini uhuru wa kunipiga chini anao coz kuvumilia uzinzi inahitaji moyo wa chuma, na ujuwe mtu akianza huo upumbavu kuacha ni ngumu sana.
 
Back
Top Bottom