Nina miezi 8 tu kwenye ndoa lakini nimemkinai huyu mwanaume hatari. Akiingia chumbani harufu ya mwili wake (body scent) ikinijia tu mimi naingiwa na hasira na hapo hapo moyo unajikunja kabisa.
Usiku nakosa usingizi kabisa na kuanza kujuta kwanini niliamua kuolewa na huyu kaka.
Namfanyia visa anichokoze nipate sababu ya kumuacha lakini busara, upole na hekima yake vinanipa wakati mgumu sana.
Kuna wakati naamka usiku naingia chooni na simu nampigia video call boyfriend wangu ili tu nimuone au tuzungumze (japo kwa kunong'ona). Basi tutaangaliana kwa muda hata wa dakika kumi halafu narudi kitandani.
Nampenda toka moyoni boyfriend wangu huyu. Sikutaka kuolewa naye kwasababu hela hana, nikaamua niolewe na huyu mwenye hela.
Sasa moyo wangu haumtaki kabisa. Najilazimisha lakini nimeshindwa.
Naombeni ushauri nifanyeje?
Usiku nakosa usingizi kabisa na kuanza kujuta kwanini niliamua kuolewa na huyu kaka.
Namfanyia visa anichokoze nipate sababu ya kumuacha lakini busara, upole na hekima yake vinanipa wakati mgumu sana.
Kuna wakati naamka usiku naingia chooni na simu nampigia video call boyfriend wangu ili tu nimuone au tuzungumze (japo kwa kunong'ona). Basi tutaangaliana kwa muda hata wa dakika kumi halafu narudi kitandani.
Nampenda toka moyoni boyfriend wangu huyu. Sikutaka kuolewa naye kwasababu hela hana, nikaamua niolewe na huyu mwenye hela.
Sasa moyo wangu haumtaki kabisa. Najilazimisha lakini nimeshindwa.
Naombeni ushauri nifanyeje?