Simshangai Leticia Nyerere

Simshangai Leticia Nyerere

Congratulations Mr malisa, LETISIA NYERERE atasaidiwa na mahakama tu ndo pona yake iyo. Toka Acha kuchafua cv ya baba wa taifa Mwlm, Julius kambarage nyerere
 
duh..sikua najua unyerere wake unatokea wapi, ..kumbe kwa sasa ni bandia? ila muwacheni mdada wa watu.., si nyie mlikua mnaimba katiba sio ya chama sasa kwa nini mnamwekea bifu.
 
NJAA KALI SANA YENYE rangi ya kijani imemuondoa dada wa watu kwenye ulingo wa siasa , nawasikitia waliomlea !
 
Nafarijika sana kuwaona vijana mahiri kama wewe uko kwenye njia sahihi kwa maslahi mapana ya Taifa letu... Intensity ni muhimu sana, always pambana kuwaelimisha na kuwa tayari kuwaokoa vijana wenzio waliodumbukia kwenye mitego ya kijinga! Always inspires them, waambie kuwa nchi hii ni tajiri tena kuliko nchi nyingi za ulaya na kuwa Maisha bora yanawezekana iwapo tu CCM watatolewa madarakani... kwa mbali Napata faraja kuwa 2015 kuna mambo mazuri kwa Watanzania ... Kudos Malisa ...keep it up...
Aliyeleta pesa, alileta mfarakano,
Mioyo ya watu imeteka, inaleta utengano,
Mwenye kumiliki nyingi pesa, aweza fanya lolote agano,
USALITI HUU WA UKOMBOZI, SIMSHANGAI LETICIA NYERERE.


Yesu aliuzwa kwa wayahudi, sababu ilikua pesa,
Hata John aweza jiita "Iddi", kama ukimuahidi pesa,
Leticia mwana wa Mageni Musoni, shilingi inamtesa,
USALITI HUU WA UKOMBOZI, SIMSHANGAI LETICIA NYERERE.


Laki tatu na nusu kwa siku, nani asiyezitaka?
Wakulima wa tumbaku, wazipata mwisho wa mwaka,
Waalimu wenye uzoefu, mwezi mzima wazisaka,
USALITI HUU WA UKOMBOZI, SIMSHANGAI LETICIA NYERERE.


Leticia Madaraka Nyerere, pesa imempofusha,
Hawezi tena kuona mbele, kisa posho za Katiba,
Hata akila matembele, macho yake keshaziba,
USALITI HUU WA UKOMBOZI, SIMSHANGAI LETICIA NYERERE.


Mwizi huanza kama kibaka, akizoea haogopi tena kelele,
Leticia alimsaliti Madaraka, kitindamimba cha Mwal.Nyerere,
Mahakamani akadai talaka, lakini akaendelea kujiita "Nyerere"
USALITI HUU WA UKOMBOZI, SIMSHANGAI LETICIA NYERERE.


Mahakama ingempa mipaka, asitumie tena jina Nyerere,
Hakuna Nyerere kibaka, wala mwenye kiherehere,
Apendaye pesa za "mbaka", na kuweka tamaa mbele,
USALITI HUU WA UKOMBOZI, SIMSHANGAI LETICIA NYERERE.
 
leticia ananjaa kuliko hata darfuu , yaani kama wewe una buku 10 u.n.a.m.t.i.a kilaini tu bila shida
 
Back
Top Bottom