Simshangai Leticia Nyerere

Simshangai Leticia Nyerere

Leo Leticia anaonekana msaliti. maneno ya kashfa. Mlipomteua kuwa mbunge viti maalum hamkujua kuwa alitalikiwa na Madaraka Nyerere?
Amewahi kugombea ubunge wa Sadc kwa baraka za chadema, leo anaitwa majina mengi.
Demokrasia gani hiyo?
demokrasia ina mipaka! je, bado unaweza kwenda kulala chumbani kwa wazazi wako mpaka leo?
 
Acha pumba wewe ipogolo,ulitaka watu na wanacha CDM wampongeze kwa kufanya dharau na kuwasaliti au huko Lumumba ndo mnafanyaga hivyo,mchukueni basi aje atee magamba,huku CDM awatetei watanzania kwa kuja BMK ila ni msakatonge alietoka kwake kuja kwenda kuchumia tumbo lake kama yalivyo malumumba tu.
 
haa, mi nilifikiri ni mtoto wa hayati baba wa taifa. kumbe ni hayawani aliyemsaliti mtoto wa baba wa taifa madaraka nyerere, sasa anatakiwa hata hilo jina anyang'anywe analinajisi jina lilotukuka, bila mleta uzi huu nilikuwa najua ni mtoto wa hayati baba nyerere
 
Huyu mwanamke ndo maana ananangania jina wa watu
Tulijikwaa! Tusongembele tuteue wabunge wa viti maalumu kwa kuangalia sifa ya mtu na mchango wake ktk chama, vilevile waroho wa nyama kama Shibuda wafukuzwe CDM wanafanya usaliti shahiri dhahiri tunawaangalia tu kwanini?
 
Chadema ilipofikia isiwe kokoro tena ..... kuwe na utaratibu wa kupata makada waliofunzwa vizuri sana.Kuokota tu watu kisa nao wanaimba chorus ya chama itakuja kuicost chama zaidi ya tulivyowahi kushuhudia.Kuna makada wachache waliotengenezwa kwa muda mrefu kiasi unaweza kuwaona hata damu zao zinatiririka Chadema na si kuokota watu tu kama huyu bibi msaliti na very soon anakwenda ACT.
 
Uchu wa laki 3 kwa siku mara siku 90 ambayo ni sh million 27! Leticia Nyerere aibu kubwa sana kwako
 
Chadema bwana ni kweli ina wafuasi na wanachama wa ajabu..natabiri siku si nyingi zijazo kibabu Tindu lissu nae ataitwa msaliti...(si chalii yetu)
 
Hivi ule uzi kuhusu kuishi nchi gani sijui na sababu za kupewa ubunge mlijibu nini tena????!!!!
Mbona yaliandikwa mengi tu lakini "mlishupaa"????!!

Vumilieni tu next time mtakuwa makini zaid
 
CDM walipoteza jimbo la Kwimba 2010 kwa ajili yake,hakubaliki, maana ccm kumpiga zengwe Sakila wanakwimba walichukia mno
 
nafikiri hata matatizo yake na makongoro yatakuwa yamejikita kwenye tama ya hela

Huyo dada ni mtalaka wa Madaraka Nyerere ambaye ni mdogo wake Makongoro Nyerere ambaye kwa sasa ni mbunge wa bunge la jumuiya ya Afrika Mashariki.
 
Ana njaa ya pesa yeye na cc mabaka wake alowafata.
 
Aliyeleta pesa, alileta mfarakano,
Mioyo ya watu imeteka, inaleta utengano,
Mwenye kumiliki nyingi pesa, aweza fanya lolote agano,
USALITI HUU WA UKOMBOZI, SIMSHANGAI LETICIA NYERERE.


Yesu aliuzwa kwa wayahudi, sababu ilikua pesa,
Hata John aweza jiita "Iddi", kama ukimuahidi pesa,
Leticia mwana wa Mageni Musoni, shilingi inamtesa,
USALITI HUU WA UKOMBOZI, SIMSHANGAI LETICIA NYERERE.


Laki tatu na nusu kwa siku, nani asiyezitaka?
Wakulima wa tumbaku, wazipata mwisho wa mwaka,
Waalimu wenye uzoefu, mwezi mzima wazisaka,
USALITI HUU WA UKOMBOZI, SIMSHANGAI LETICIA NYERERE.


Leticia Madaraka Nyerere, pesa imempofusha,
Hawezi tena kuona mbele, kisa posho za Katiba,
Hata akila matembele, macho yake keshaziba,
USALITI HUU WA UKOMBOZI, SIMSHANGAI LETICIA NYERERE.


Mwizi huanza kama kibaka, akizoea haogopi tena kelele,
Leticia alimsaliti Madaraka, kitindamimba cha Mwal.Nyerere,
Mahakamani akadai talaka, lakini akaendelea kujiita "Nyerere"
USALITI HUU WA UKOMBOZI, SIMSHANGAI LETICIA NYERERE.


Mahakama ingempa mipaka, asitumie tena jina Nyerere,
Hakuna Nyerere kibaka, wala mwenye kiherehere,
Apendaye pesa za "mbaka", na kuweka tamaa mbele,
USALITI HUU WA UKOMBOZI, SIMSHANGAI LETICIA NYERERE.

Utashangaa sana ukisikia na Wengine wamehudhuria. Usizimie. Tanzania kwanza mengine baadaye
 
Mbona hata wewe umeachika tena mara mbili kwa aibu sana tu,mwambie mbowe na watu wake kama kweli wao wazalendo warudishe pesa walizojua ndipo wakazurule mitaani waliko.

Arudishe wap wakat walimpa?? Hakuna kurudsha lakn hii ya pili wameona haiko poa thats y hawajaenda.tumia sense than kuendesha na u....u. u cc majambazi
 
Chadema ilipofikia isiwe kokoro tena ..... kuwe na utaratibu wa kupata makada waliofunzwa vizuri sana.Kuokota tu watu kisa nao wanaimba chorus ya chama itakuja kuicost chama zaidi ya tulivyowahi kushuhudia.Kuna makada wachache waliotengenezwa kwa muda mrefu kiasi unaweza kuwaona hata damu zao zinatiririka Chadema na si kuokota watu tu kama huyu bibi msaliti na very soon anakwenda ACT.

Na kweli jamaa yangu inabidi CHADEMA sasa ijipange upya. Ni heri na vema kabisa kuwapa kipaumbele makada wapambanaji ndani ndani ya Chama wagombeapo nafasi kama Ubunge.

Habari ya kusubiria makapi yaliyomwagwa kwenye kura za maoni kutoka vyama vingine huko kisa wana majina makubwa na kumwambia kada mfia chama (die hard members) akae pembeni apishe mgeni kwenye kinyang'anyiro eti kisa hana jina kubwa matokeo yake ndio kupata wasaliti watu dezaini ya akina Shubuda type.

Chama kibadilishe staili sasa kijikite zaidi kwenye 'Quality' badala ya 'Quantity' .
 
Leo Leticia anaonekana msaliti. maneno ya kashfa. Mlipomteua kuwa mbunge viti maalum hamkujua kuwa alitalikiwa na Madaraka Nyerere?
Amewahi kugombea ubunge wa Sadc kwa baraka za chadema, leo anaitwa majina mengi.
Demokrasia gani hiyo?
Hata Mansour Yusuph Hamid alikuwa kwanachama mtiifu wa CCM leo hii yupo wapi?
 
Back
Top Bottom