Simbachewene amerogwa na nani?

Simbachewene amerogwa na nani?

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA




TAARIFA KWA UMMA
Tarehe 28/03/2016 ilisambazwa taarifa ya Uongo kwenye mitandao ya Kijamii ambayo ilikua na upotoshaji wa makusudi kwa jamii.
Taarifa hiyo imemnukuu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mheshimiwa George B. Simbachawene (Mb) kwamba ametoa tamko kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa “ Serikali haiko tayari kuajiri wasomi wenye vyeti vya baraza la Mitihani kuanzia vyeti viwili na kuendelea,watakaopata ajira yoyote ile moja kwa moja serikalini ni wasomi wenye cheti kimoja tu”. Lakini pia taarifa hiyo ambayo ilikua na maneno ya kudhalilisha iliendelea kusema kuwa “Wale waliosoma kwa kuunga unga, mara kutafuta credit, mara kurudia mitihani watafute ajira kwenye Mashirika Binafsi”
Taarifa hiyo imendelea kupotosha kuwa kwa Ajira za Walimu mwaka 2016 watakao ajiriwa ni wale ambao walisoma moja kwa moja tu.
Ofisi ya Rais – TAMISEMI imesikitishwa sana na uzushi huu ambao unalenga kuipotosha jamii, kudhalilisha taaluma za Wananchi na kupoteza muda wa Watanzania.
Serikali inawaonya wote wanaojihusisha na kutengeneza Uongo na Upotoshaji wa aina hii kuacha mara moja na serikali haitasita kuchukua hatua stahiki ili kuhakikisha jambo hili haliendelei kutokea.
Ofisi ya Rais – TAMISEMI inapenda kuwaarifu Watanzania wote kuipuuza habari hiyo kwani haina ukweli wowote.


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Ofisi ya Rais-TAMISEMI,
29 Machi, 2016.
 
Mkuu tupia clip au source yoyote inayomhusisha simbachawenye na ajira kwa watu wenye elimu ya kuunga
 
Kuna habari nilitumiwa tu online ikisema Waziri Simbachewene amesema
kuanzia sasa serikali haita ajiri 'watu wenye vyeti vya kuunga unga' akimaanisha watu waliosoma mfano certificate...na baadae kujiongeza hadi degree au wale ambao walisoma kidogo kidogo huku wameajiriwa hadi kufika chuo kikuu..

Simbachewene huyu huyu amenukuliwa akisema wapinzani hawaruhusiwi kutekeleza sera za vyama vyao iwapo wameshinda halmashauri.

Kinachoshangaza Simbachewene mwenyewe historia yake inafahamika
alisoma kwa kuunga unga na inajulikana alikuwa 'mpiga debe'
stendi ya mabasi Dodoma kabla ya kuunga kuunga hadi kufika chuo kikuu

Ukichanganya na hili la wapinzani wasirihusiwe kutumia ilani zao wakishinda uchaguzi nimebaki najiuliza tu ameshikwa na nini?

Nini kinamfanya aongee vitu kama hivi? kuna nini hasa? mbona alipokuwa kimyaa tulimuona kama kiongozi anaeonekana ana busara.Kuna nini kinamsukuma kuongea haya?

Hivi hata Magufuli hatuwezi kusema kasoma kwa kuunga unga? Au nini tafsiri ya kusoma kwa kuunga unga?

Kati ya mawaziri vilaza wenye elimu danganya toto wa kwanza ni simbachawene na wa pili ni januari makamba, records zao za shule zinaonesha dhahiri ni watu wa kuunga kuunga
 
kwa hiyo Dr John, Kasim, cha Wene mwenyewe na wengine wengi watimuliwe serikalini maana elimu zao ni za kuungaunga
 
Simbachawene ni mkurupukaji tu wa mambo
 
sasa nyie mmeshaambiwa kuwa amekana huo upuuzi, mnachoendelea kumjadili ni nini? acheni kupoteza muda, tukafanye kazi. Kama mtu aseme apewe ujumbe wa sauti unaothibitisha hlo.
 
wanasiasa wa nchi hii wajinga sana, hivi yeye ana elimu gani? ndio sababu katiba ya warioba ilipendekeza uwaziri uwe kazi ya kuajiriwa, sio ya wanasiasa wakaibaka ile katiba kwa umbumbu wao, leo tunashuhudia ujuha wa baadhi ya mawaziri ambao wameshindwa kuuficha.
 
Kuna habari nilitumiwa tu online ikisema Waziri Simbachewene amesema
kuanzia sasa serikali haita ajiri 'watu wenye vyeti vya kuunga unga' akimaanisha watu waliosoma mfano certificate...na baadae kujiongeza hadi degree au wale ambao walisoma kidogo kidogo huku wameajiriwa hadi kufika chuo kikuu..

Simbachewene huyu huyu amenukuliwa akisema wapinzani hawaruhusiwi kutekeleza sera za vyama vyao iwapo wameshinda halmashauri.

Kinachoshangaza Simbachewene mwenyewe historia yake inafahamika
alisoma kwa kuunga unga na inajulikana alikuwa 'mpiga debe'
stendi ya mabasi Dodoma kabla ya kuunga kuunga hadi kufika chuo kikuu

Ukichanganya na hili la wapinzani wasirihusiwe kutumia ilani zao wakishinda uchaguzi nimebaki najiuliza tu ameshikwa na nini?

Nini kinamfanya aongee vitu kama hivi? kuna nini hasa? mbona alipokuwa kimyaa tulimuona kama kiongozi anaeonekana ana busara.Kuna nini kinamsukuma kuongea haya?

Hivi hata Magufuli hatuwezi kusema kasoma kwa kuunga unga? Au nini tafsiri ya kusoma kwa kuunga unga?
AKIMAANISHA AU WEWE NDIO UMEMAANISHA??????????????????????
HIVI WATU MAKINI HUMU JF WAMETOKOMEA WAPI??????????????????????
 
Mbona watanzania wanastaajabisha, Mfumo ule ule alafu mnatarajia matokeo tofauti? Hayo ndio matokeo
 
Kuna habari nilitumiwa tu online ikisema Waziri Simbachewene amesema
kuanzia sasa serikali haita ajiri 'watu wenye vyeti vya kuunga unga' akimaanisha watu waliosoma mfano certificate...na baadae kujiongeza hadi degree au wale ambao walisoma kidogo kidogo huku wameajiriwa hadi kufika chuo kikuu..

Simbachewene huyu huyu amenukuliwa akisema wapinzani hawaruhusiwi kutekeleza sera za vyama vyao iwapo wameshinda halmashauri.

Kinachoshangaza Simbachewene mwenyewe historia yake inafahamika
alisoma kwa kuunga unga na inajulikana alikuwa 'mpiga debe'
stendi ya mabasi Dodoma kabla ya kuunga kuunga hadi kufika chuo kikuu

Ukichanganya na hili la wapinzani wasirihusiwe kutumia ilani zao wakishinda uchaguzi nimebaki najiuliza tu ameshikwa na nini?

Nini kinamfanya aongee vitu kama hivi? kuna nini hasa? mbona alipokuwa kimyaa tulimuona kama kiongozi anaeonekana ana busara.Kuna nini kinamsukuma kuongea haya?

Hivi hata Magufuli hatuwezi kusema kasoma kwa kuunga unga? Au nini tafsiri ya kusoma kwa kuunga unga?
Wizara aliyopewa imemzidi uwezo wa kuongoza TAMISEMI hana kabisa amebaki kuropoka huu ndio Sugu alisema mzuka wa raisi
 
Ukishaona mtu mwenye nafasi nyeti kama hiyo anaamini katika karatasi/vyeti basi ujue ndio wale wanaokazania watu kuingia ofisini saa moja na nusu na kutoka saa tisa. Hata ukimpa kazi ya kurecruit hawezi kumjua anayefaa au asiyefaa maana anaangalia vyeti tu na kwake ajira ni watu kulipwa mishahara na sio productivity. Ndio hawa hawa mwisho wa siku unasikia wanasema "sisi tumeendelea kielimu kuwazidi Uganda maana tunatoa wanafunzi milioni moja kwenda vyuoni wakati wao wanatoa wanafunzi laki sita".
 
Back
Top Bottom