LwandaMagere
JF-Expert Member
- Mar 15, 2020
- 264
- 2,489
Hello,habari za majukumu wadau,bila shaka mtakuwa mko vyema na mnaendelea kuchukua hatua na tahadhari dhidi ya hili gonjwa dharimu la Covid-19 linalosababishwa na virus hatari wa corona,Mungu awabariki sana!.
Niende moja kwa moja kwenye mada.
Kuna mjadala mahali fulani nimekutana nao kuhusu mnyama SIMBA na TIGER (Chui milia).
Kiukweli kama mnavyofahamu mijadala mizito mara nyingi huwa ina vuta nkuvute,kulingana na tafiti mbalimbali pamoja na Historia kadha wa kadha!,sasa kuna wengine waliosema ya kwamba SIMBA ni hatari zaidi ya Tiger na kuna wengine waliosema Tiger ni hatari zaidi ya Simba,na huo uhatari wao ni pale wanapokutana wao kwa wao.
Wapo waliosema SIMBA kwa uwezo wa nguvu,uwindaji,mapigano basi akikutana na Tiger atapokea kipondo kikali,lakini pia wapo vilevile waliosema kwamba Tiger kwa uwezo,minguvu,uwindaji na mapigano basi akikutana na Simba atampiga mpaka achakae kabisa,na si kuchakaa tu bali pia kuua kabisa.
Mtazamo wako wewe ni upi hapa,hebu lete facts za uhalisia,kiroho na kimwili pia unaweza kuhusisha!!
Tulia hivyo hivyo dawa ikuingie..
Niende moja kwa moja kwenye mada.
Kuna mjadala mahali fulani nimekutana nao kuhusu mnyama SIMBA na TIGER (Chui milia).
Kiukweli kama mnavyofahamu mijadala mizito mara nyingi huwa ina vuta nkuvute,kulingana na tafiti mbalimbali pamoja na Historia kadha wa kadha!,sasa kuna wengine waliosema ya kwamba SIMBA ni hatari zaidi ya Tiger na kuna wengine waliosema Tiger ni hatari zaidi ya Simba,na huo uhatari wao ni pale wanapokutana wao kwa wao.
Wapo waliosema SIMBA kwa uwezo wa nguvu,uwindaji,mapigano basi akikutana na Tiger atapokea kipondo kikali,lakini pia wapo vilevile waliosema kwamba Tiger kwa uwezo,minguvu,uwindaji na mapigano basi akikutana na Simba atampiga mpaka achakae kabisa,na si kuchakaa tu bali pia kuua kabisa.
Mtazamo wako wewe ni upi hapa,hebu lete facts za uhalisia,kiroho na kimwili pia unaweza kuhusisha!!
Tulia hivyo hivyo dawa ikuingie..

anapatikana marekani ya kusini huyo unaemuita mamba ni alligator
... tiger kwa asili anapatikana Asia ... na kwa taarifa tu hakuna mnyama anaeweza kufanya huo upumbavu wa kuwinda mamba mtoni ( the strongest bite on earth
) Hakuna mnyama anaeweza kuwinda hawa jamaa nile crocodile au salt crocodile labda alligator they’re more like lizards than mazafaka crocs