Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,817
- 4,566
Maandalizi ya timu zote mbili yameenda vyema, kinachosubiriwa ni mchezo rasmi leo 29/03/2024 saa tatu usiku.
Ungana nami katika uzi huu ili kupata matukio mbalimbali yatakayojiri kabla na wakati wa mchezo huo.
Karibu.
==============
Timu ya Simba inatarajia kucheza dhidi ya Al Ahly ya Misri katika Robo Fainali ya Kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam, leo Machi 29, 2024
Takwimu zinaonesha hakuna mbabe mpaka sasa, kila upande umeshinda mechi Tatu, hizi ni mechi zilizopita baina ya timu hizo:
24/10/2023 Al-Ahly 1-1 Simba
20/10/2023 Simba 2-2 Egypt
09/04/2021 Al-Ahly 1-0 Simba
23/02/2021 Simba 1-0 Al-Ahly
12/02/2019 Simba 1-0 Al-Ahly
02/02/2019 Al-Ahly 5-0 Simba
29/08/1985 Al-Ahly 2-0 Simba
22/08/1985 Simba 2-1 Al-Ahly
---
Kikosi cha Simba kilichoanza
Kikosi cha Al Ahly kinachoanza
3' Simba wameanza wakiwa na presha ya kushambulia, wamepata kona
5' Gooooooo Al Ahly wanapata goli baada ya safi ya ulinzi ya Simba kujichanganya
11' Kasi ya Mchezo imepungua, AlAhly wanalinda lango lao muda mwingi
13' Simba Wana Kona tatu, wageni Wana Moja
16' Al Ahly wanapata Kona ya pili na ya tatu ndani ya dakika moja
21' Al Ahly wanafanya mashambulizi ya kushtukiza na yanakuwa hatari
30' Mapumziko ya dakika moja
32' Mchezo unaendelea
40' Saido anakosa nafasi ya wazi
45 ' Mapumziko, Simba wapo nyuma kwa goli 1-0.
MAPUMZIKO
Kipindi cha pili kimeanza
49' Babacar anapata kadi ya njiano kwa kucheza faulo
55' Inonga anapata kadi ya njano kwa kucheza faulo
60' Mchezo bado ni mgumu kwa Simba wanatengenesa nafasi lakini haizitumiki vizuri
70' Simba wanaendelea kumiliki mpira lakini nafasi ya kufunga bado ni ngumu
75' Mapumziko ya dakika moja kwa timu zote.
77' Saido anapat nafasi kadhaa za wazi lakini hazitumii vizuri
80' Simba wanaendelea kutengeneza nafasi lakini wanashindwa kuweka mpira wavuni
90' Zinaongezwa dakika 5
Full Time