Simba leo tumebebwa penati ,duh

nzagambadume

JF-Expert Member
Apr 9, 2018
2,430
5,769
Jamani ile penalty ya pili hapana aiseee,hata sijashangilia,najua wachezaji wanachoka kwa ratiba iliyobanana ila waongeze umakini kwenye chances wana zo create,maana kama kipindi cha kwanza walipoteza chances nyingi sana
Tushukuru tu refa kwa ile controversial penalty ya pili.
 
Simba akishinda anabebwa/ananunua

Simba akifungwa timu mbovu/hakuna kitu.

Wachezaji waliofungwa hawajalalamika ila wewe.

Bado mtaelewa tu.
 
ili awe mwana simba anatakiwa aweje? Au kwakusema kwake ukweli kunamuondolea sifa ya kuwa mwanasimba? Kwa staili hiyo bora Simba na Yanga zife tu ndipo soka letu lipige hatua.
Mzee ni klabu gani inamafanikio kwenye soka la bongo kama hiyo.
Basi tuseme msimu ujao tupeleke Azam na KMC kwenye mashindano ya CAF uone wapi tutaishia.

Mwana Simba hawezi kuitakia mabaya klabu yake, mwana simba hutaka mafanikio tu huyu ni Mbute
 
tafuta threads zangu utaona mimi ni shabiki wa simba,hatukuhitaji penalty ile ya kijinga ku win game ile, tulikuwa na uwezo wa kufunga 3 clean goals kabisa
Sikatai ila wana Simba hatuna mawazo kama yako jinasibu kama mwana Tasaf fc ieleweke
 
Mzee ni klabu gani inamafanikio kwenye soka la bongo kama hiyo.
Basi tuseme msimu ujao tupeleke Azam na KMC kwenye mashindano ya CAF uone wapi tutaishia.

Mwana Simba hawezi kuitakia mabaya klabu yake, mwana simba hutaka mafanikio tu huyu ni Mbute
ule ujinga wako wa ubishani wa kina Ray vanny naona umeuleta huku?mechi umeangalia kweli au aunadhani huu ni ubishani wa ali kiba na diamond?
 
ule ujinga wako wa ubishani wa kina Ray vanny naona umeuleta huku?mechi umeangalia kweli au aunadhani huu ni ubishani wa ali kiba na diamond?
Mimi si mjinga nitake radhi naweza kuchafua hali ya hewa na usiamini.

Mpira nimetizama kulikuwa na maamuzi mabovu kwenye pande zote mbili loop lile goal ni clear kabisa pengine hujui hata nini kilisababisha penati a pili ifunikwe mzee mimi ni zaidi ya uzaniavyo kuhusu Entertainment and sports huniwezi hata robo.
 
tatizo la Azam Tv huwa hawaonyeshi vitu kwa slow motion ile penati ilikuwa sahihi sema wachezaji wengi wa simba kiwango ni kibovu kuanzia kapteni wao Boko, Mkude, Zaha na Mpilipili wameonyesha kiwango kibovu sana
 
hizo ni baadhi ya threads zangu nikiikandia yanga na Papaa zahera,yaani kusema ukweli kwamba tumebebwa leo ndiyo nimekuwa siyo simba?vipi kuhusu lile boko la nyoni alilorudisha nyuma refa akasema offside Kmc wakiwa wanenda kusawazisha?

Endeleeni kulialia. Zahera kagomewa kule







 
Jamani ile penalty ya pili hapana aiseee,hata sijashangilia,najua wachezaji wanachoka kwa ratiba iliyobanana ila waongeze umakini kwenye chances wana zo create,maana kama kipindi cha kwanza walipoteza chances nyingi sana
Tushukuru tu refa kwa ile controversial penalty ya pili.
mi mwenyewe ni simba damu ila kiuchambuzi madogo walitubana sana
 
mi mwenyewe ni simba damu ila kiuchambuzi madogo walitubana sana
ukisema unaambiwa ni TASAF,penalty ya kwanza sawa ila ya pili hapana aisee ni ball to hand na siyo kwamba kuna movement iliyozuiwa ni beki aliokoa ukagonga mwenzake,vipi ile ya nyoni dakika ya mwisho kurudisha nyuma refa akasema ni offside kwa kmc?
 
Mzee ni klabu gani inamafanikio kwenye soka la bongo kama hiyo.
Basi tuseme msimu ujao tupeleke Azam na KMC kwenye mashindano ya CAF uone wapi tutaishia.

Mwana Simba hawezi kuitakia mabaya klabu yake, mwana simba hutaka mafanikio tu huyu ni Mbute
Swala sio kulazimisha timu iende kilazima kwavile tu ndio ina mwelekeo bali timu iende kwa kuonesha uwezo wake halali. Hata KMC au Biashara united wakiwa na uwezo wa kuchukua kombe la ligi waende tu wakawakilishe nchi kimataifa hata wakifungwa magoli 20+ ni sawa tu kwasababu watakuwa ndio timu bora kuliko zingine kwa Tz na ndio maana wakachukua kombe. Sio kulazimisha timu ikawakishe timu hata kwa kubebwa
 
tatizo la Azam Tv huwa hawaonyeshi vitu kwa slow motion ile penati ilikuwa sahihi sema wachezaji wengi wa simba kiwango ni kibovu kuanzia kapteni wao Boko, Mkude, Zaha na Mpilipili wameonyesha kiwango kibovu sana
Penati ilikuwa sahihi kivipi? Embu tupe ufafanuzi kwanini unaona ni sahihi?
 
Swala sio kulazimisha timu iende kilazima kwavile tu ndio ina mwelekeo bali timu iende kwa kuonesha uwezo wake halali. Hata KMC au Biashara united wakiwa na uwezo wa kuchukua kombe la ligi waende tu wakawakilishe nchi kimataifa hata wakifungwa magoli 20+ ni sawa tu kwasababu watakuwa ndio timu bora kuliko zingine kwa Tz na ndio maana wakachukua kombe. Sio kulazimisha timu ikawakishe timu hata kwa kubebwa
Yanga mnateseka sana kwa nini lakini? Au kwa vile mlibebwa sana kipindi cha malinzi miaka minne hamkuweza kufikia ilipo simba? Roho zinawaumaaa subrini dawa iwakolee kwanza. Sa hivi tunaifata nafas yetu ya kuongoza tulieni ivo ivo kama mnanyolewa. Shubamitiii
 
Back
Top Bottom