Simba akila majani kazidiwa si asili yake

Simba akila majani kazidiwa si asili yake

Naona kama DAWA za mganga wake zimeisha nguvu au kakosea masharti vinginevyo usingeleta uzi huu. Kama kweli unataka kudeka kwenye mapenzi jitahidi kuwa nyumba dogo.


ha ha haaaa inawezekana eee maana sijielewi elewi..... mmmh ngoja nijitoe fasta
 
Mbona hujawahi kuhoji kwanini wanaume tu ndiyo wanahonga baada ya mtanange?


Sio lazima mwanamume kuhonga baada ya mtanange, huo ni udhaifu wa mtu tu. Nachozungumzia mimi ni mwanamke kumhudumia kidume (kumlea mpenzi wake).
 
mapepo ya ngono haya jamani...mnatuvuruga tume concentrate na katiba mpya jamani

Ka mimi leo sijatia mguu kwenye katiba mpa kabisa. Leo nimeshinda huku huku! Ntalipa sita tukifungua si eti?
 
Bible yangu imeandikwa hivyo, yako inasemaje?
Na ni Bible hiyo hiyo iliandika mwanamume ni kichwa cha nyumba, kama mnaifuata Biblia nini kiliwafanya muende Bejing kutaka usawa?

Biblia hiyo hiyo unayoiamini inasema enzi za Yesu mwanamke alikuwa hata kuhesabiwa hahesabiwi na hata kanisani hakutakiwa kusema lolote wala kusimama mbele ya mimbari. Kama ikitokea ana neno lolote la kuuliza sinagogi alitakiwa kumsubiri mumewe nyumbani na kumuuliza swali hilo. AU Biblia yako tayari ime-editiwa na Wabeijing?
 
Ninahisi unafuta mtu wa kukuhonga!
Hivi mimi ni wa kumhonga mwanamume? Loh hivi nimepatwa na nini? Mwenzenu najishangaa sijawahi honga kidume chochote na si utaratibu wangu hata siku moja! Cha ajabu nimeangukia eti kwenye penzi, kidume hakina kazi, nakipa nauli, pesa ya kula, ya dawa na nguo nakinunulia! loh najishangaa nimekuwaje mie???? Najua vidume vitapiga kelele lakini ukweli utabaki pale pale, nimezaliwa mwanamke nastahili kupata huduma zote kutoka kwa mwanamume, nastahili kulelewa na sio kulea kidume chochote! Ndio je, ... mnataka kubisha, nyie bisheni tu ila nahitaji kukiondoa hiki kilichoniingilia na kupelekea mimi kuhonga kidume! eti penzi; loooo penzi gani la kulea dume zima lenye nguvu zake.

Kama kupenda ndio huku sitaki tena, nahitaji kuwa freee, nahitaji kupenda atakayenitunza na kunirusha rusha kwenye bahari ya maraha niufurahie uanamke wangu. Potelea mbali acha niliue hili penzi ingawa limenikaba koo maana kidume kiroho changu kimeridhika ila akili yangu haikubali kabisa... nitajitahidi niliepuke nipumue mtoto wa kike loH! nisaidieni jamani ili hiki kiroho changu kiache kupenda janga, yes, hili ni janga kwangu maana bajeti zangu zinaharibika kisa kuhudumia kidume... uwiiiiiiiiiiii
 
Ni kweli Biblia imeandika yote hayo uliyoyasema grafani11; na ukiisoma Biblia vizuri utaona kuna mambo yanagongana nadhani ndio maana majoto anaingia mitini kwa kuwa umembana katika hilo. Cha kuangalia hapa ni kwamba Mkutano wa Beijing ulilenga haki sawa kwa jinsia zote, kumbuka wana Beijing hawafati yaliyoandikwa kwenye Biblia ila lengo lao ni kumpa haki sawa mwanamke katika njanja zote ikiwemo elimu, kufanya kazi, kumiliki ardhi na mengine.

Sasa hapo msijichanganye maana hata hao wana Beijing walijichanganya ndio maana wengine walipoteza ndoa zao kwa kutokuwa na busara ya kupambanua mambo na kujua nini wanadai. Back to the topic Majoto anaona si halali kumlea mwanamume kisa mapenzi.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom