Ninavyofahamu mimi, kabla ya kujiingiza kwenye mahusiano na mtu, unatakiwa at least umfahamu japo kwa vitu basic kabisa kama elimu yake, anaishi wapi, kazi anazofanya, anapendelea nini nk nk. Naamini uliyajua hayo yote, lakini inawezekana kabisa kwa kujua kabasi ulimkubali na sasa ameuteka moyo wako.
Sidhani kama ni jambo la kujutia sana, maana kwa hatua, amefuzu kwenye kukuburudisha ambacho ndiyo kigezo kimojawapo cha ndoa, ingawa si kigezo pekee maana ndoa ni zaidi ya 6 x 6! Kwa hivyo, nakushauri ukae nae muulize vyema kuhusu hatma ya maisha yenu, mipango yake ya baadaye, anafikiria nini kuhusu uhusiano wenu, anapenda kufanya shughuli gani nk nk.
Kama ukimuona ana nia ya maendelea na mipango madhubuti ya kimaendeleo, unaweza kumsaidia kwa namna yoyote ile ili muweze kutimiza ndoa zenu, lakini kama unamuona kuwa ni zumbukuku baada ya mahojiano hayo, basi kazi ni kwako unaweza kuchagua kuishi naye na kumlea for the rest of your life au kufanya maamuzi magumu.
Prior na kumsaidia kwenye shughuli zake za kiuchumi ni vyema kufanya uchunguzi zaidi wa matumizi yake ya pesa, tabia zake, mwenendo wake, upendo wake kwako, commitment yake kwako, familia yake na mtazamo wake juu ya maisha yenu ya sasa na baadaye.
Kila la kheri.
HP