Wapendwa Shalom, Ninaorodhesha machache ninayoyafahamu kuhusu Pool of Siloam Church ambalo lilianza mwaka 2003. (Kwa maoni yangu walianza vizuri hadi ilipofika mwaka 2008 – ndipo U-Turn ilipotokea). Pia unaweza kusoma juuya wanachokiaminikuhusiana naMWENENDO WA KANISAkwenye link hii;
http://The Pool of Siloam Church - Shika neno, tenda neno MAMBO MACHACHE YA KANISA LA KIZAZI CHA NNE HAYA HAPA.
1. Pool of Siloam ilianzishwa rasmi 2003, na Mtumishi N. Munuo
2. Mafunuo ya Nabii Eliya anatambulika kuwa ni sahihi hutakiwi kuyahoji wala kuyaoanisha na Maandiko Matakatifu unapaswa kuyatii. Mojawapo ya ufunuo /maelezo ya ajabu ni hili Shetani aliuwawa naNabii Eliya Novemba2008. Hapa ndipo kwenyevile vitisho ya kuwabubu, tasa kufa n.k.
3. Imani yao imejengwana kuongozwa katikaufunuo wa majira nanyakati na jambo hili nimuhimu sana. Hivi sasawapo katika kizazi channe. Kizazi cha kwanzaAdamu mpaka gharika,kizazi cha pili Nuhu hadi Yesu, kizazi cha tatu kutoka Yesu hadi Februari 2012.
Kizazi channe kutoka Machi 2012 na kuendelea. Kwamba kwa kutumia Kalenda inayotumika sasa (Mwasisi wake akiwa ni Gregory – mwaka 1582) kanisa ilikuwa chini yautumwa kwa miaka 430 kama Israel utumwani Misri. Kuanzia 2008 watuwa kizazi cha nne wanakalenda yao.
4. Kanisa hivi sasa lipokatika kipindi cha miaka1000 iliyoanza mweziMachi 2012 (hii ni baadaya kupita kwa miaka6000. Hesabu yao ni kuwamiezi yote (12) ina siku28 na mwaka una siku336). Yaani wenzetutayari wamesha-spentmwaka mmoja katika ilemiaka 1000 ya utawalawa Yesu hapa duniani,kama iliyoandikwa katikaUFUNUO 20:1-5.
5. Kwa kuwa Kristo anaishi na Kanisa hapa duniani hivyo hakuna magonjwa, dhiki,kudharauliwa na maonevu yote. Ni siku ya saba yaani miaka 1000 ya kustarehe na kutawala. Huenda hapa ndipo ile concept ya kutokufa inapokuja / ingia / attach.
6. Waumini waohutakiwa kubadilishahadi majina yao ya ukoo.Kwa sababu majina hayoyanabeba laana, kishamuumini hupewa familianyingine (miongoni mwa washirika) na hutengwana wazazi na ndugu wa kimwili.
7. Maombi yao huombakwa kushikamanisha namadhabahu ya Siloam /Mungu wa nabii Eliya.
8. Wanapomfanyia Deliverance mtu (mmoja wa wahudumu –huingiwa na pepo/mzimu ambao unamsumbua anayeombewa na kumweleza kilichokuwa kinamfunga). Biblically,mtu mwenye pepo/mizimu yeye ndiye hupagawa na kuongea, kisha huamuriwa kutoka ndani ya mtu. Kila nilichokieleza hapo juu ina tafasiri yake ya ziada ambayo yeyote akipenda na akifunguka anaweza kutufafanulia. source:
https://strictlygospel.wordpress.com/2013/04/08/kanisa-la-siloamu/