domokaya
JF-Expert Member
- Apr 22, 2010
- 3,588
- 1,758
Yaani mbunge mzima anahoji habari aliyosoma kwenye mitandao na magazeti? Hivi ina maana hakwenda na hoja za wananchi wake toka jimboni mwake waliomtuma bungeni? Kuna wabunge si wawakilishi wa watu waliowapigia kura.Shilinde ni mmoja wao kaamua kuwa mwakilishi wa mitandao ya kijamii na magazeti.
Naomba Shilinde akinyoosha mkono kutaka kuongea spika awe anamwambia haya sasa ni zamu ya mwakilishi wa mitandao ya kijamii na magazeti ongea!
Ama! nchi hii tatizo la ufisadi ni dogo wala si kubwa kama wengi tunavyodhani ukilinganisha na tatizo letu la aidha kushindwa kufikiri ama kufikiri hovyohovyo kusikoweza kuleta tija. kushindwa kufikiri ni kansa yetu watanzania inatumaliza jamani mpaka huruma