Danny Jully
JF-Expert Member
- Jul 29, 2013
- 4,416
- 3,867
Kumbe China ndo walitushtua kwamba kuna kondena lipo bandarini Darisalama limejaa pembe za ndovu? Asante sana Membe. Maafisa wetu wa jeshi la polisi walikuwa bize kupiga picha pembeni ya kontena hilo, as if intelijensia yao ndio iliyofanya kazi
Kama china intelejensia yao iko makini hivyo kwa nini Profesa hakuomba msaada wao ili tembo wasiuawe kabisa?? Kwa sababu kugundua shehena ya pembe ambazo tembo wameshauawa inasaidia nini? Ni jambo la aibu waziri kueleza ujinga kama huo bungeni. Watz wanachotaka kusikia sio idadi ya pembe zilizokamatwa, bali ni hatua gani zinachukuliwa kuzuia tembo wasiuawe. Unapokamata pembe maana yake tembo wameuawa, sasa hizo pembe zitawafufua hao tembo!?
Kuna mwandishi wa Uingereza aliyeishutumu serikali ya Tz kwamba haifanyi jitihada za kuzuia tembo wasiuawe, alichofanya Nyalandu ni kumwalika kuja kuona shehena ya pembe za tembo zilizoifadhiwa na serikali. Hakujua kwamba alimsaidia huyo mwandishi kuthibitisha alichoandika kwamba ni kweli. Kwa hiyo mawaziri wetu wao wanaona kukamata pembe ndio kulinda tembo.!!