"Sikutegemea" Nimeamini kila jambo lina sababu

"Sikutegemea" Nimeamini kila jambo lina sababu

Kwa ufupi,ukiona manyoya ujue amekwishaliwa,logically upande wa pili kuna mtu ametendwa kama ulivyotendwa wewe 2011.Ila atarudi kama alivyorudi kwak😵NYO:Usiamini benki ya chini ya Godoro maana aliyepigwa 1M atapelekewa 5 M.!
 
Wasalamu wana MMU natumaini mu wazima wa afya, nawatakia weekend njema na maandalizi ya X-mass pamoja na mwaka mpya.
*************
Kipindi nko chuoni nilikuwa na GF wangu ambaye tulipendana sana.. na malengo yetu ilikuwa ni kuja kuoana baada ya kumaliza chuo. mapenzi yetu yakaenda hivyo hvyo kwa upendo wa juu kabisa... siunajua tena mapenzi ya kiscul scul jinsi yalivyo, yani ni full maigizo na mbwembwe nyingi.. huku tukiwa tunaongozana ongozana ovyo kama kumbikumbi vile. ilikuwa ni GOOD COUPLE Kwa kwel.

Sasa wakati tumemaliza chuo mwaka 2011 huku tukiwa tunaishi pamoja gheto na tukiendelea kutafuta kazi huku na kule. Siku mojo narudi home kutokea kwenye mishe zangu za kutafuta kazi, nkashangaa gheto liko ovyo kinoma alaf na mwenyewe hayupo.

nikiangalia begi lake la nguo na viatu vyake havipo.. Ndo nkapigwa na butwaa!! na kukumbuka kuna hela zangu 750000 zilikuwa chini ya godoro nimeziweka tokea kitambo. kwenda kuangalia sizioni, nikatafuta huku na kule wapi.. sikuziona. Nikajua tayari huyu demu kashaniibia.. ikabidi nmpigie simu lakini hakawa hapatikani, nkapiga kila mara sikumpata pamoja na kumtumia txt.

ikapita siku mbili tatu, nkamcheki hewani simu ikaita.. alafa akapokea nkamwambia "vip, inakwaje umeondoka na mkwanja wangu alafu hukuniaga? akanijibu "amepata dili la kwenda Canada hvyo pesa zangu atanirudishia soon" basi nkamwambia Poa.

nikamisikilizia dakika,saa mwezi, miaka na miaka lakini wapi... No kunorudishia mkwanja No nini!!!..

*****BACK TO POINT******
sasa leo wakati niko church ukafika muda wa kutoa sadaka, nikaingiza mkono mfukoni nkachambua chambua nikatoa pesa bila kuiangalia nmetoa sh. ngapi nikaitumbukiza kwenye kapu la sadaka.

Heeee!!! ile tumetoka naangalia pesa zilizopo mfukoni nakuta nna buku mbili tuuu, huku wakati natoka home kuja church nilikuwa ma 12000, nijlkajua yesss kwenye sadaka nmetoa 10000 badala ya 2000 na huku salio kweny account liko empty nkajiuliza leo nitaishi vipi wakati hii 10000 nilikuwa nmeipangia nikitoka church nipitie shop nnunue mazagazaga ya msosi.

akili ikanituma niende ofisi ya kanisa nkawaeleze labda wanaweza kunisaidia. nilipomweleza mzee wa kanisa akasema "sasa nitaamini vipi kama ulitoa 10000?

ila akasema kama ni kwel basi acha tuu, huwezi jua Mungu anakusudio gani juu yako. nikaona isiwe noma.. nikasepa zangu.
nilipofika home nikafunga mlango nikaenda kwa mshikaji wangu ili niangalie uwezekano wa kuimaliza siku ya leo. nikafika home kwangu nikamkosa, nikampigia cm akasema "ametoka kidogo na atachelewa kurudi" nikabidi nirudi zangu home.

ile nafika tuu namkita yule EX wangu aliyeniibiaga kipindi kile amekaa kwenye kiti ananisubiri. hapo sa hiyo hasira zimeshanipanda najiuliza kichwani "hivi nimfanye ninu huyu" kufika akanisakimu kwa furaha huku akinikumbatia lakini mimi sikuonyesha kujali.. nkamuuliza nani amekuelekeza hapa ninapoishi? akajibu "kwa mtu umpendaye lazima ajue tuu. Ok nikamkaribisha ndani tulupofika akanipa bahasha akasema nmekuletea fedha zako, mimi nikajifanya kama vile haikuwa na haja kwani nilikwisha msamehe tokea kitambo.. akaning'ang'aniza nikabidi nizipokee ile kuhesabu nikakuta ni 1000000 nkamwambia mimi nakudai laki 7 tuu hvyo hizi laki 3 chukua akasema " hizo ni riba" nikaona poa nikachukua..

akasema "nmekumiss sana hivyo leo nitalala hapa.. nkamwambia poa..
yani mpaka muda huu ninavyiandika hapa niko naye.. na tayari nmeshapasha kiporo tayari.
SASA NDO NIKAKUMBUKA MANENO YA YULE MZEE WA KANISA ALIPONIAMBIA "KILA JAMBO LINA SABABU.

ona sasa elfu 10 imezaa milioni 1.

Ninafuraha ajabu na nmeshasahau kitu alichonifanyia kipindi cha nyuma. YANI LEO NI MWENDO WA KUPASHA KIPORO KWA SANAAAA, NA WEEKEND YA LEO TUNAIMALIZIA KWA MAUTAMUZI KWA KWENDA MBELEEEEE.

nawasilisha jamani na nitakuwa nawapa Updates

Tuma picha
 
Hv ww unasomaga hadithi za KUFIKIRIKA.. ZA SHIGONGO.. au unaandika udaku tu huku... huu ni uongo mkubwa..!! 😨👎👌

Na kama amerudi kakuletea ukimwi ndio ukome... Hv you been to University with this FOOLISH mind..? Nasty...!!

👉🚶🚶🚶
 
Hv ww unasomaga hadithi za KUFIKIRIKA.. ZA SHIGONGO.. au unaandika udaku tu huku... huu ni uongo mkubwa..!! 😨👎👌

Na kama amerudi kakuletea ukimwi ndio ukome... Hv you been to University with this FOOLISH mind..? Nasty...!!

👉🚶🚶🚶

huwa mimi siyo muanzisha thread, sasa ni mchangiaji tuu.. mpaka ifikie kuandika hivi ujue sijakurupuka
 
Tunapeana updates za ngono. Miafrika bana!!
 
2011 alipo maliza chuo na bila ajira alikuwa na saving ya 750,000

2015- miaka 4 imepita saving yake 12,000
!!!!

Aisee Bei Mbaya ongeza mwaka m1 tuone angebaki na nini huyu?
 
nahisi kiporo kimechacha ila umelazimisha sio mbaya tahadhari usijekuharisha?
 
Hii story haina connection nzuri, huku juu unasema 750k huku unasema 700k na riba ya 300k? Which is which? Taratibu kaka katumwa kichwa chako leo na mganga kwa ajili ya business zake. Kama sio kichwa cha juu basi ni cha chini. Utupe updates pi
 
Back
Top Bottom