Ushimen
JF-Expert Member
- Oct 24, 2012
- 42,417
- 104,853
Nicholas,
Ndugu yangu Umezungumza maneno mazito sana!..na kila kitu umekichambua kiutaalam na pia umeweza kuzama ndani ya mioyo ya watu wote - Waathirika na hao warithi wanaofaidika. Swala kubwa tu ambalo ningekuomba labda utufunulie ama kutupatia ufumbuzihapa...
Tuanzie wapi... wapi panatakiwa kweli serikali yetu iwekee mkazo zaidi kwa sababu mimi binafsi kinachonishinda kuelewa na hata kupata ufumbuzi ni kwamba haohao viongozi wetu - wanasiasa ndi haohao wasomi wetu wa uchumi na watoa maamuzi ya sehemu zote mbili. Siamini kabisa kwamba tuachie dunia iwe fundisho la utandawazi na dira ya maendeleo yetu. Lazima ipo njia ya kutupa hata mwanga wapi wananchi wanatakiwa waelekee! hata kwa jina kama waislaam wanavyoamini KIBLA ni MECCA.. kokote uliko maelekeo yako yatalenga malengo ya hilo neno Kibla.
Mwisho kuna kipengele umezungumzia kuwa wananchi bado hawapo tayari kuhimili mabadaliko ya kuleta usawa na haki. Ebu nipe dawa kidogo hapo maanake nimekwama.
Please Google