shamsi shabani
Member
- Dec 25, 2017
- 13
- 2
Nilijikuta sina la kufanya katika wakati ule mgumu nikiwa mpweke
Kitandani macho yangu yakiangalia mwanga wa jua ulio penya katika tundu la paa lililochoka na kurusu mwanga kupita kila sehemu ya chumba kile kutokana na paa hilo kuwa na vidirisha vidogo ambavyo viliifanya chumba kuwa na Giza ata wakati wa mchana,,, na ndivyo pia ilivokuwa wakati wa masika maji yaliingia ndani kirahisi,,,,
Nakujikuta nikifanya kazi yakuhamisha hamisha kitanda angalau kupata sehemu ambayo inauwafadhali....kutokana na chumba kile kuwa na mwanga mdogo basi nilijua bado ni mapema sana kunyanyuka kitandani....Mara nilipitiwa na usingizi mzito ulionifanya nilale nakusahau kibarua changu kilichonipa angalau pesa ya kula........
Uuuuuh!!!!!!! Nimechelewa kazini ni sauti ya mbwa waliokuwa wakibweka ndio walionitoa usingizini nilitoka nje haraka haraka huku nikifunga vifungo vya shati langu la kazi.....ilikuwa ni sa nne na nusu nilijisemea peke angu "ooh masikini kazi yenyewe niliipata kwa tundu la sindano......Mungu nisaidie sitorudia kitendo hiki"
Kwakuwa nilikuwa ni kijana wa maji ya moto basi nilianza kutroti kama wasemavyo yani kamchakamchaka kadogo ili angalau nisiendele kuchelewa zaidi......
Haikuchukuwa muda mrefu nikawa nimefika kazini kwangu nikiwa na jibu la kumjibu boss ili kutuliza hasira zake ile kufika tu kabla sijafanya lolote niliwauliza wafanyakazi wenzangu kama boss amekuja ama bado
Ilikuwa ni saa tano sasa wakiwa bize kidogo na kazi woote waliniangalia na kucheka sana,,,,,...
Nanisijue sababu iliowafanya wacheke vile kwa utofauti wake Njoza yeye hakucheka ila alinionesha tu kwa vitendo niangalie shati langu........Loooh!!!!!¡yani ndo nimetembea Hivi kutoka.......sikumalizia kuongea baada yakukatishwa nasauti zakicheko hii sasa ata Njoze aliachia kicheko......lakini wazee nambieni basi boss yupo ama!!!???
Kodraki alijibu akimwigilizia boss anavoongeaga "wee kijana unapenda kazi ama hupendii huu ndo muda wakuja kaziniii".... Basi nilishusha pumzi zangu maana nilijua kama boss angekuwa maeneo Ya kazi basi Kodraki asingeigilizia vile.......
Nilivua shati nakuliweka pembeni tayari kwakuanza kazi
Tukiwa tunaendelea na kazi utani haukukosa maana ndo ulitufanya tuwe na hamasa na tusijihisi
Kumechoka..
Hii siku ikawa yangu kwa sababu tayari nimeonekana katika kila kichwa cha habari cha magazeti ya Leo apa kazini......
Baada ya ukimia wa kama dakika tatu Njoze aliuanzisha tena mjadala wakunihusu mimi.....
Akiniuliza sababu iliyonifanya Leo nikachelewa kazini ila katika kuuliza swali hilo hakuniacha hivihivi bali aliwafanya watu wote wanguke kicheko baada yakusema " au ndo Jana umezindua mwali nini Pastor".......swali hili lilinibadilisha kimawazo japo sikutaka kuonesha wazi kwamba limeniumiza.....
"Oyaa leta mchanga huo"...aliniita Kodraki huku akimalizia kwakusema au ndo utaki utani Leo..!??
Nilimjibu kwaharaka hapana Kodraki nilikuwa najipangusa jicho nilitoswa apa,.......
Hatimae siku hii ilimalika vizuri japo ilionekana kuanza vibaya
Tuliagana pale kila mmoja akapita njia yake na hapo ndipo hali yangu ya mawazo ikarudi nikiwa njiani naelekea pangoni kwangu nilikutana na msichana mmoja akionekana aliyepoteza matumaini kabisa.......
Alikuwa ni msichana mrembo sana ila tu kutokana na ile hali niliyomkuta nayo usingeweza kulitambua hilo basi kwakuwa nilijua nimpita njia tu kama Mimi niliendelea kupiga hatua nikisogea lakini kabla sijapiga hatua nyingi nilisikia sauti ikiniita " Kaka...kakaa samahani kaka angu"........
Nini kitaendelea.......usikose sehemu ya pili
Imeandikwa na shamsi shabani,
0759 859030:WhatsApp
Kitandani macho yangu yakiangalia mwanga wa jua ulio penya katika tundu la paa lililochoka na kurusu mwanga kupita kila sehemu ya chumba kile kutokana na paa hilo kuwa na vidirisha vidogo ambavyo viliifanya chumba kuwa na Giza ata wakati wa mchana,,, na ndivyo pia ilivokuwa wakati wa masika maji yaliingia ndani kirahisi,,,,
Nakujikuta nikifanya kazi yakuhamisha hamisha kitanda angalau kupata sehemu ambayo inauwafadhali....kutokana na chumba kile kuwa na mwanga mdogo basi nilijua bado ni mapema sana kunyanyuka kitandani....Mara nilipitiwa na usingizi mzito ulionifanya nilale nakusahau kibarua changu kilichonipa angalau pesa ya kula........
Uuuuuh!!!!!!! Nimechelewa kazini ni sauti ya mbwa waliokuwa wakibweka ndio walionitoa usingizini nilitoka nje haraka haraka huku nikifunga vifungo vya shati langu la kazi.....ilikuwa ni sa nne na nusu nilijisemea peke angu "ooh masikini kazi yenyewe niliipata kwa tundu la sindano......Mungu nisaidie sitorudia kitendo hiki"
Kwakuwa nilikuwa ni kijana wa maji ya moto basi nilianza kutroti kama wasemavyo yani kamchakamchaka kadogo ili angalau nisiendele kuchelewa zaidi......
Haikuchukuwa muda mrefu nikawa nimefika kazini kwangu nikiwa na jibu la kumjibu boss ili kutuliza hasira zake ile kufika tu kabla sijafanya lolote niliwauliza wafanyakazi wenzangu kama boss amekuja ama bado
Ilikuwa ni saa tano sasa wakiwa bize kidogo na kazi woote waliniangalia na kucheka sana,,,,,...
Nanisijue sababu iliowafanya wacheke vile kwa utofauti wake Njoza yeye hakucheka ila alinionesha tu kwa vitendo niangalie shati langu........Loooh!!!!!¡yani ndo nimetembea Hivi kutoka.......sikumalizia kuongea baada yakukatishwa nasauti zakicheko hii sasa ata Njoze aliachia kicheko......lakini wazee nambieni basi boss yupo ama!!!???
Kodraki alijibu akimwigilizia boss anavoongeaga "wee kijana unapenda kazi ama hupendii huu ndo muda wakuja kaziniii".... Basi nilishusha pumzi zangu maana nilijua kama boss angekuwa maeneo Ya kazi basi Kodraki asingeigilizia vile.......
Nilivua shati nakuliweka pembeni tayari kwakuanza kazi
Tukiwa tunaendelea na kazi utani haukukosa maana ndo ulitufanya tuwe na hamasa na tusijihisi
Kumechoka..
Hii siku ikawa yangu kwa sababu tayari nimeonekana katika kila kichwa cha habari cha magazeti ya Leo apa kazini......
Baada ya ukimia wa kama dakika tatu Njoze aliuanzisha tena mjadala wakunihusu mimi.....
Akiniuliza sababu iliyonifanya Leo nikachelewa kazini ila katika kuuliza swali hilo hakuniacha hivihivi bali aliwafanya watu wote wanguke kicheko baada yakusema " au ndo Jana umezindua mwali nini Pastor".......swali hili lilinibadilisha kimawazo japo sikutaka kuonesha wazi kwamba limeniumiza.....
"Oyaa leta mchanga huo"...aliniita Kodraki huku akimalizia kwakusema au ndo utaki utani Leo..!??
Nilimjibu kwaharaka hapana Kodraki nilikuwa najipangusa jicho nilitoswa apa,.......
Hatimae siku hii ilimalika vizuri japo ilionekana kuanza vibaya
Tuliagana pale kila mmoja akapita njia yake na hapo ndipo hali yangu ya mawazo ikarudi nikiwa njiani naelekea pangoni kwangu nilikutana na msichana mmoja akionekana aliyepoteza matumaini kabisa.......
Alikuwa ni msichana mrembo sana ila tu kutokana na ile hali niliyomkuta nayo usingeweza kulitambua hilo basi kwakuwa nilijua nimpita njia tu kama Mimi niliendelea kupiga hatua nikisogea lakini kabla sijapiga hatua nyingi nilisikia sauti ikiniita " Kaka...kakaa samahani kaka angu"........
Nini kitaendelea.......usikose sehemu ya pili
Imeandikwa na shamsi shabani,
0759 859030:WhatsApp