Sikubaliani na utumiaji nguvu

emalau

JF-Expert Member
Apr 25, 2009
2,775
3,100
Siku za hivi karibuni kumekuwa na vitendo vya utumiaji nguvu watu wakishindwa hoja, na kwa bahati mbaya midomo ya wanasiasa imekuwa haina breki matokeo yake wananchi wameanza kujichukulia sheria mikononi.

Mara ya kwanza nilimsikia mheshimiwa Kitwanga akiwa bungeni akitishia kuhamasisha wananchi wa jimbo lake kuvamia miundo mbinu ya maji kisa wananchi wake hawana maji, ile kauli ilikuwa ya uchochezi lakini hakuna hata aliyemkemea ndani ya bunge wala nje ya bunge.
Mara ya pili nilimsikia Hussein Bashe naye akitishia wananchi wa jimbo lake la Nzega kuvamia mgodi (jina silikumbuki), ingawa huyu kijana namkubali kwa umakini wake lakini hapa alikosa umakini wa kulinda mdomo wake, kauli ile ilikuwa ya uchochezi lakini hakuna aliyemkemea nje ya bunge wala ndani ya bunge.

Juzi nimemsikia mbunge John Heche akitishia kuvamia mgodi, kwa bahati mbaya akasahau kwamba watu wa kule subira yao ni kidogo wameitikia wito wake na wamevamia mgodi.

Jeshi la polisi linavamia mikutano ya vijana wa Chadema vyuoni na kuwapiga bila sababu za msingi huku wa ccm wakifanyia mikutano yao ndani ya vyuo bila kupigwa.

Hii trend ya utumiaji nguvu badala ya maarifa si nzuri na haipaswi kuungwa mkono. Kama mwekezaji anawaibia ni kwa sababu mliingia mikataba mibovu, kwa ustaarabu inatakiwa tukae chini tufanya negotiation tufikie muafaka. Utumiaji nguvu unawatisha potential investors tunaonekana hatuna sheria zinazoaminika na kwa mwekezaji awe wa nje au ndani anahitaji a credible legal framework.

Nawasilisha
 
Siku za hivi karibuni kumekuwa na vitendo vya utumiaji nguvu watu wakishindwa hoja, na kwa bahati mbaya midomo ya wanasiasa imekuwa haina breki matokeo yake wananchi wameanza kujichukulia sheria mikononi.

Mara ya kwanza nilimsikia mheshimiwa Kitwanga akiwa bungeni akitishia kuhamasisha wananchi wa jimbo lake kuvamia miundo mbinu ya maji kisa wananchi wake hawana maji, ile kauli ilikuwa ya uchochezi lakini hakuna hata aliyemkemea ndani ya bunge wala nje ya bunge.
Mara ya pili nilimsikia Hussein Bashe naye akitishia wananchi wa jimbo lake la Nzega kuvamia mgodi (jina silikumbuki), ingawa huyu kijana namkubali kwa umakini wake lakini hapa alikosa umakini wa kulinda mdomo wake, kauli ile ilikuwa ya uchochezi lakini hakuna aliyemkemea nje ya bunge wala ndani ya bunge.

Juzi nimemsikia mbunge John Heche akitishia kuvamia mgodi, kwa bahati mbaya akasahau kwamba watu wa kule subira yao ni kidogo wameitikia wito wake na wamevamia mgodi.

Jeshi la polisi linavamia mikutano ya vijana wa Chadema vyuoni na kuwapiga bila sababu za msingi huku wa ccm wakifanyia mikutano yao ndani ya vyuo bila kupigwa.

Hii trend ya utumiaji nguvu badala ya maarifa si nzuri na haipaswi kuungwa mkono. Kama mwekezaji anawaibia ni kwa sababu mliingia mikataba mibovu, kwa ustaarabu inatakiwa tukae chini tufanya negotiation tufikie muafaka. Utumiaji nguvu unawatisha potential investors tunaonekana hatuna sheria zinazoaminika na kwa mwekezaji awe wa nje au ndani anahitaji a credible legal framework.

Nawasilisha
We are creating an altitude of lawlessness among our people, and this is dangerous, very dangerous
 
Back
Top Bottom