Ilibidi awe hivyo kutokana na!
Kwanza ndilo lilikuwa hitaji kamili la nchi wakati huo, lakini pia lilikuwa hitaji la Upinzani Kwa kuwa walitaka apatikane kiongozi sio dhaifu, ni mwenye chembe ya udicteta, na wakati nchi ikingia ktk Hali ya kuombea, watu waliomba apatikane kuiongozi atakayezuia wizi na ufisadi uliokuwa umekithili
Kukithili Kwa uwizi, ufisadi, huduma mbovu, uuzaji madawa ya kulevya, ukwepaji Kodi, Uonevu na kila Aina ya ufisadi, ilikuwa ni cheni iliyokuwa imechukua watu weeengi mpaka ktk ngazi za juuu kabisa za viongozi wetu,
Kuondoa huo uozo, ilitakiwa awepo Mtu kama huyo, na ilimbidi awe mithili ya Dicteta Kwa sababu bila hivyo, isingewezekana kuondoa huo mfumo
Kipindi cha nyuma, watu wengi Sana walikuwa walipoteza Maisha Yao Kwa kukosa huduma nzuri mahospitalini, kwani dawa zoote za Serikali zilikuwa zikigawanwa ju Kwa ju, huku Masikini na wasiojiweza kabisa wakiathirika na mfumo huo mbovu
Kipindi cha nyuma, vijana wengi wa Kitanzania walikosa mwelekeo Kwa sababu ya kujiingiza katika mihadarati ambapo huduma hiyo ilikuwa IPO kila eneo na hakuna kizuizi, ilifikia mtu akitaka kutaja wauza madawa, anapewa masaa 24 apotee au apotezwe, Kwa sababu tu ya nguvu ya wauza madawa, na walikuwa hatari kuishinda hata serikali yenyewe
Nahitimisha kusema, JPM ambaye ni Hayati, udicteta wake tunaousema leo, tuliutengeneza Sisi, ama mazingira yaliyokuwepo ndio yaliyomtengeneza kuwa Dicteta!