george aloyce
JF-Expert Member
- Aug 22, 2017
- 1,177
- 1,823
Hii ni picha iliyobeba maana kubwa kwenye jinsia zetu na matatizo mengi yaliyokosa maelewano..
Mwanaume hajui kuwa chini kuna nyoka. Na mwanamke haelewi kuwa juu kuna jiwe kubwa limemkandamiza Mwanaume wake..
Mwanamke anafikiri, naenda kuanguka na siwezi kupanda, kwasababu nyoka atanin'gata..
Lakini kwanini jamaa hanivuti kwa nguvu?
Mwanaume anafikiri, nipo kwenye maumivu makali, bado namvuta kwa kadri ya uwezo wangu,
Kwanini hajitahidi kujivuta juu na yeye?
Mwanamke anahisi mwanamme wake anatoa msaada kama hataki vile/ amelazimishwa.
Mwanaume anadhani, mwanamke wake anadeka, anajiendekeza na hataki kusaidiwa.
Somo tunalojifunza hapa, huwezi kuona presha anayopitia mwenzio, na yeye hawezi kuona maumivu yako..
Mwanamke anamlaumu mwanaume yupo bize hampi muda, kumbe anabanwa na kazi zake..
Mwanaume anamlaumu mwanamke amepoteza upendo kumbe ana madeni ya vikoba vyake..
Mwanamke asipopata kwa wakati alichokiomba anajihisi amenyimwa ama hajaliwi tena..
Bila kujua yapo maswahibu yanapita kwenye harakati za mwanaume wake asiyoweza kusema..
Kama kila mtu angekaa kwenye nafasi ya kuelewa uchungu wa mwingine, matatizo mengi yangetupa mkono wa kwaheri..
Mwanaume aelewe maumivu apitiayo mke wake..
Mwanamke atambue presha anayopitia mume wake kwenye harakati zake za kila siku..
Mwanaume hajui kuwa chini kuna nyoka. Na mwanamke haelewi kuwa juu kuna jiwe kubwa limemkandamiza Mwanaume wake..
Mwanamke anafikiri, naenda kuanguka na siwezi kupanda, kwasababu nyoka atanin'gata..
Lakini kwanini jamaa hanivuti kwa nguvu?
Mwanaume anafikiri, nipo kwenye maumivu makali, bado namvuta kwa kadri ya uwezo wangu,
Kwanini hajitahidi kujivuta juu na yeye?
Mwanamke anahisi mwanamme wake anatoa msaada kama hataki vile/ amelazimishwa.
Mwanaume anadhani, mwanamke wake anadeka, anajiendekeza na hataki kusaidiwa.
Somo tunalojifunza hapa, huwezi kuona presha anayopitia mwenzio, na yeye hawezi kuona maumivu yako..
Mwanamke anamlaumu mwanaume yupo bize hampi muda, kumbe anabanwa na kazi zake..
Mwanaume anamlaumu mwanamke amepoteza upendo kumbe ana madeni ya vikoba vyake..
Mwanamke asipopata kwa wakati alichokiomba anajihisi amenyimwa ama hajaliwi tena..
Bila kujua yapo maswahibu yanapita kwenye harakati za mwanaume wake asiyoweza kusema..
Kama kila mtu angekaa kwenye nafasi ya kuelewa uchungu wa mwingine, matatizo mengi yangetupa mkono wa kwaheri..
Mwanaume aelewe maumivu apitiayo mke wake..
Mwanamke atambue presha anayopitia mume wake kwenye harakati zake za kila siku..