Siku ya nne bila maji Kibamba, Dar (Juni 9, 2019)

Siku ya nne bila maji Kibamba, Dar (Juni 9, 2019)

Hii ni fursa iliyo uchi kwa vijana sasa hasa graduate ambao ndio wamejaa kitaa, kama mkokoteni wako kama huna azima, jaza madumu ata matano kwenye visima yanakopatikana, ingia nayo kitaa kwa hali ya maji ilivyo ngumu utayauza buku buku kwa kila dumu kirahisi kabisa, ukianza saa 12 asubui kuyasambaza kwa wateja mpk jion saa kumi na mbili utakuwa umetengeneza mkwanja mrefu tu, ukifanya hvyo mpk yatakaporudi utakuwa umetengeneza mtaji wa kutosha kuanza kabiashara kako ka kishkaji kakuanzia maisha. Kamateni fursa vijana,.
Kwa sababu huyo utakayemuazima ye hataki hela atakuazima wewe si ndio?
 
.
IMG-20190608-WA0001.jpeg
 
Eeeh chadema
MBUNGE wa Kibamba katika Jiji la Dar es Salaam John Mnyika (CHADEMA) ametakiwa kufanya ziara ndani ya jimbo lake ili kuona utekelezaji wa miradi mbalimbali inayofanywa na Serikali ikiwemo ya miradi ya maji.

Mnyika ameelezwa hayo leo Bungeni Mjini Dodoma baada ya Naibu Waziri wa Maji Jumaa Aweso kuelezea hatua ambazo zinachukuliwa na Serikali kutatua changamoto ya uhaba wa maji.

Wakati Aweso anazungumzia miradi ya maji alizungumzia jimbo la Kibamba na miradi ya maji ambayo imefanyika lakini baada ya maelezo hayo Mnyika alisimama bungeni na kumtaka aombe radhi kwa madai Naibu Waziri anasema uongo bungeni.

Mnyika alisema "Nimemsikia Naibu Waziri wa Maji anavyoelezea miradi ya maji na ametaja jimbo la Kibamba lakini ukweli hayo anayoyasema hayana ukweli wowote na ni vema akaomba radhi kwa kusema uongo bungeni."

Baada ya kauli hiyo ya Mnyika, Naibu Waziri wa Maji alitakiwa kutoa ufafanuzi na hapo ndipo alipoamua kumpa makavu mbunge huyo kwa kuelezea hatua ambazo zimefanywa na Serikali katika kutatua changamoto ya maji katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Kibamba jijini Dar es Salaam.

"Naomba nitumie nafasi hii kumshauri ndugu yangu Mnyika, tatizo lake hafanyi ziara katika jimbo lake na hivyo hata miradi ya maendeleo inavyotekelezwa na Serikali haoni.Ukitoka Bungeni nenda kafanye ziara ya kutembelea jimbo.

"Kote ambako nimetaja uwepo wa miradi ya maji iliyokamilika utaikuta.Wizara ya Maji kwa niaba ya Serikali inafanya kazi kubwa ya kuhakikisha maji safi na salama yanapatikana,"amesema Aweso.

Naibu Waziri huyo pia ametumia nafasi hiyo kueleza wazi Serikali imedhamiria kutatua changamoto ya uhaba wa maji nchini na ndio maana imeanzisha Wakala wa Maji Vijijini ambayo itakwenda kumaliza tatizo lililoko sasa na kwamba Wizara ya Maji iko makini.

"Kupitia Wakala wa Maji Vijijini tunakwenda kumaliza tatizo la uhaba wa maji, na hata wale wakandarasi uchwara katika maji nao wanakwenda kuondoka kwa namna ambavyo Wizara ya Maji tumejipanga,"amesema Aweso.
 
Ndugu zangu wanaJF nawasalimia.

Ninasikitika kusema kuwa leo Jumapili, Juni 09, 2019 ni siku ya nne maji hayatoki maeneo yote ya Kibamba.

Na cha kusikitisha zaidi ni kuwa mamlaka husika zipo kimya na hakuna taarifa zozote kuhusiana na tatizo hili.

Naomba tueleweshwe nini hatma ya tatizo hili toka kwa mamlaka husika..

=======

UPDATES: 10 Juni 2019

Huduma ya maji imerejea
IMG_20190610_212423_536.jpg
 
Visiga na viunga vyake pia hayapo maji kwa namba ya siku hizo!
 
Dooh poleni sana maji ni uhai kwa ustawi wa jamii.
 
MBUNGE wa Kibamba katika Jiji la Dar es Salaam John Mnyika (CHADEMA) ametakiwa kufanya ziara ndani ya jimbo lake ili kuona utekelezaji wa miradi mbalimbali inayofanywa na Serikali ikiwemo ya miradi ya maji.

Mnyika ameelezwa hayo leo Bungeni Mjini Dodoma baada ya Naibu Waziri wa Maji Jumaa Aweso kuelezea hatua ambazo zinachukuliwa na Serikali kutatua changamoto ya uhaba wa maji.

Wakati Aweso anazungumzia miradi ya maji alizungumzia jimbo la Kibamba na miradi ya maji ambayo imefanyika lakini baada ya maelezo hayo Mnyika alisimama bungeni na kumtaka aombe radhi kwa madai Naibu Waziri anasema uongo bungeni.

Mnyika alisema "Nimemsikia Naibu Waziri wa Maji anavyoelezea miradi ya maji na ametaja jimbo la Kibamba lakini ukweli hayo anayoyasema hayana ukweli wowote na ni vema akaomba radhi kwa kusema uongo bungeni."

Baada ya kauli hiyo ya Mnyika, Naibu Waziri wa Maji alitakiwa kutoa ufafanuzi na hapo ndipo alipoamua kumpa makavu mbunge huyo kwa kuelezea hatua ambazo zimefanywa na Serikali katika kutatua changamoto ya maji katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Kibamba jijini Dar es Salaam.

"Naomba nitumie nafasi hii kumshauri ndugu yangu Mnyika, tatizo lake hafanyi ziara katika jimbo lake na hivyo hata miradi ya maendeleo inavyotekelezwa na Serikali haoni.Ukitoka Bungeni nenda kafanye ziara ya kutembelea jimbo.

"Kote ambako nimetaja uwepo wa miradi ya maji iliyokamilika utaikuta.Wizara ya Maji kwa niaba ya Serikali inafanya kazi kubwa ya kuhakikisha maji safi na salama yanapatikana,"amesema Aweso.

Naibu Waziri huyo pia ametumia nafasi hiyo kueleza wazi Serikali imedhamiria kutatua changamoto ya uhaba wa maji nchini na ndio maana imeanzisha Wakala wa Maji Vijijini ambayo itakwenda kumaliza tatizo lililoko sasa na kwamba Wizara ya Maji iko makini.

"Kupitia Wakala wa Maji Vijijini tunakwenda kumaliza tatizo la uhaba wa maji, na hata wale wakandarasi uchwara katika maji nao wanakwenda kuondoka kwa namna ambavyo Wizara ya Maji tumejipanga,"amesema Aweso.
Waziri yuko sahihi,malamba 2,king'azi,kifuru,kwembe shida ya maji tunaisikia kwenye bomba
 
Hakuna maji Kibaha yoteee toka mlandizi mpaka kiluvya ni kujuta tu hakuna Kuku wala njiwa wanaokunywa maada maji
 
Nipo hapa mtaa mmoja Kimara Mwisho nako maji hakuna kwa siku hizo hizo tajwa.. Sijui hawa Dawasco wanataka tupikie mkojo
 
Back
Top Bottom