Siku ya Chakula Duniani: Kila baada ya sekunde 5 mtoto mmoja anafariki kutokana na njaa

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,500
9,279
Tarehe 16 Oktoba ni Siku ya Chakula Duniani na pia ni maadhimisho ya miaka 75 tangu kuanzishwa kwa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO). Maadhimisho haya yanafanyika wakati dunia ikikabiliwa na janga la virusi vya Corona, ambavyo vimevuruga kwa kiasi kikubwa mnyororo wa uzalishaji wa chakula.

Siku ya Chakula Duniani inapaswa kuchukuliwa kama fursa ya kuleta ushirikiano na mshikamano wa kimataifa ili kuhakikisha tishio linalotokana na virusi vya Corona katika usalama wa chakula na kilimo linakabiliwa ipasavyo, na watu walio hatarini zaidi wanaweza kujiendeleza tena baada ya janga hilo kumalizika.

Wakati dunia ikiadhimisha Siku ya Chakula yenye kaulimbiu “Kesho Njema Inajengwa na Lishe Bora Endelevu”, karibu watu milioni 690 duniani wanakabiliwa na njaa, ikiwa ni ongezeko la watu milioni 10 zaidi tangu mwaka 2019. Janga la virusi vya Corona linaweza kuongeza tatizo hilo zaidi, kwani shughuli za kijamii na kibiashara katika nchi nyingi zimefungwa ili kudhibiti kuenea kwa virusi hivyo.

Takwimu zinaonesha kuwa kila mwaka chakula kilichoharibiwa kote duniani kinaweza kuwalisha watu bilioni 2, na kila baada ya sekunde 5 mtoto mmoja anafariki kutokana na njaa ama ukosefu wa virutubisho.

Ili kujenga mfumo wa nafaka wenye afya na uendelevu, wanatakiwa kushirikiana na serikali, kampuni za chakula, idara za umma, taasisi na wateja kufanya juhudi kutimiza lengo la kutokomeza njaa na ukosefu wa virutubisho duiniani hadi kufikia mwaka 2030.

Siku ya chakula duniani: kila baada ya sekunde 5 mtoto mmoja anafariki kutokana na njaa
 
Marcus Rashford anapambana sana na hii issue ya food poverty kwa watoto. Sio ajabu juzi hapa amekuwa recognized na kutunukiwa MBE.
 
Dkka 1= 60 sec

So. 60/5 = 12
Apo kwa dk 1 wanakufa watoto 12

Kwa masaa je, saa 1 = dakika 60
So. Watoto 12× 60 = 720
Apo kwa saa 1 wanakufa watoto 720

Kwa siku je, sku 1 = saa 24
So. Watoto 720 × 24 = 17,280
Apo kwa sku wanakufa watoto 17,280

Namba haiongopi.....hivi inaingia akilini kweli..?
 
Dkka 1= 60 sec

So. 60/5 = 12
Apo kwa dk 1 wanakufa watoto 12

Kwa masaa je, saa 1 = dakika 60
So. Watoto 12× 60 = 720
Apo kwa saa 1 wanakufa watoto 720

Kwa siku je, sku 1 = saa 24
So. Watoto 720 × 24 = 17,280
Apo kwa sku wanakufa watoto 17,280

Namba haiongopi.....hivi inaingia akilini kweli..?
Hii haiingii akilini kabisa
 
Gawanya kwa idadi ya nchi duniani upate wastani wa vifo kwa kila nchi
Dkka 1= 60 sec

So. 60/5 = 12
Apo kwa dk 1 wanakufa watoto 12

Kwa masaa je, saa 1 = dakika 60
So. Watoto 12× 60 = 720
Apo kwa saa 1 wanakufa watoto 720

Kwa siku je, sku 1 = saa 24
So. Watoto 720 × 24 = 17,280
Apo kwa sku wanakufa watoto 17,280

Namba haiongopi.....hivi inaingia akilini kweli..?
 
Itakuwa sio vibaya, nifundishe
Wanaposema anakufa mtoto kila baada ya sekunde tano haimaanishi literally kuwa kila baada ya sekunde tano anakufa mtoto. Inaweza kupita hata siku hajafa hata mmoja lakini takwimu huwa zinatolewa kwa wastani (averages).

Mfano kwa mwaka kuna siku 365 ambazo ni sawa na sekunde 31,536,000 sasa mfano ndani ya huo mwaka pametokea vifo 6,307,200 vilivosababishwa na njaa tukitaka kupata ratio ya kila kifo kwa muda maana yake tutachukua muda husika (mwaka katika sekunde) kisha tutagawanya kwa idadi ya vifo vyote na hapo ukitumia hizo namba hapo juu ni utapata jibu kuwa kwa wastani alifariki mtoto mmoja kila baada ya sekunde tano. (hata kama kuna wakati katika mwaka husika ilipita week bila mtoto kufariki, kumbuka hapo hizo takwimu ni wastani)
 
Dkka 1= 60 sec

So. 60/5 = 12
Apo kwa dk 1 wanakufa watoto 12

Kwa masaa je, saa 1 = dakika 60
So. Watoto 12× 60 = 720
Apo kwa saa 1 wanakufa watoto 720

Kwa siku je, sku 1 = saa 24
So. Watoto 720 × 24 = 17,280
Apo kwa sku wanakufa watoto 17,280

Namba haiongopi.....hivi inaingia akilini kweli..?
Kwanini isiingie akilini mzee? Au unafikiri kwakuwa humfahamu mtoto aliekufa kutokana na njaa basi hawapo?
 
Back
Top Bottom