Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,484
- 30,160
Wajibu mkubwa wa Jeshi la Polisi nchini ni kuwalinda Raia na mali zao.
Ingawa Jeshi la Polisi huwa linajidai kuwa na intelejensia ya hali ya juu kiasi ambacho kila mkutano wa kisiasa wa chama cha upinzani ukitaka kufanyika huwa wamepata taarifa za kiintelejesia kuwa mkutano huo utavamiwa na watu wasioutakia mema mkutano huo na hivyo kuufuta mkutano huo!
Lakini katika tukio hili la kuvamiwa kwa Tundu Lissu katika mji mdogo wa Dodoma, tena mchana kweupe Jeshi la Polisi limeshindwa kazi yao na hivyo viongozi wa juu wote wa Jeshi letu la Polisi wanapaswa kufutwa kazi!
Kwa kuwa kwa mtu kama Tundu Lissu, licha ya kuwa ni mbunge wa kuchaguliwa na wananchi wake wa Singida Mashariki kuwa ni mbunge wake, yeye pia ni mwanasheria mkuu wa Chama kikuu cha upinzani nchini cha Chadema, yeye pia ndiye Rais wa wanasheria wote wa Tanganyika.
Sasa ikiwa mtu kama Tundu Lissu anamiminiwa risasi 28 kwenye bunduki ya kivita na watu wasiojulikana, sembuse mimi na wewe?
Kama wajibu mkubwa wa Jeshi la Polisi ni kulinda Raia na Mali zao na Jeshi letu la Polisi limeshindwa kulinda uhai wa uhai wa Tundu Lissu na kuuweka mashakani, sembuse uhai wangu Mimi mlala hoi?
Tunatarajia Rais wetu alivyo mwepesi wa kuwatumbua viongozi wake pale wanapokosa kutimiza wajibu wao, tunatarajia kwa hili pia atafanya hivyo "faster" kwa kumuondoa kwenye nafasi yake IGP na Waziri wa Mambo ya ndani kwa kuwa wameshindwa kutuhakikishia usalama wetu na mali zetu!
Ingawa Jeshi la Polisi huwa linajidai kuwa na intelejensia ya hali ya juu kiasi ambacho kila mkutano wa kisiasa wa chama cha upinzani ukitaka kufanyika huwa wamepata taarifa za kiintelejesia kuwa mkutano huo utavamiwa na watu wasioutakia mema mkutano huo na hivyo kuufuta mkutano huo!
Lakini katika tukio hili la kuvamiwa kwa Tundu Lissu katika mji mdogo wa Dodoma, tena mchana kweupe Jeshi la Polisi limeshindwa kazi yao na hivyo viongozi wa juu wote wa Jeshi letu la Polisi wanapaswa kufutwa kazi!
Kwa kuwa kwa mtu kama Tundu Lissu, licha ya kuwa ni mbunge wa kuchaguliwa na wananchi wake wa Singida Mashariki kuwa ni mbunge wake, yeye pia ni mwanasheria mkuu wa Chama kikuu cha upinzani nchini cha Chadema, yeye pia ndiye Rais wa wanasheria wote wa Tanganyika.
Sasa ikiwa mtu kama Tundu Lissu anamiminiwa risasi 28 kwenye bunduki ya kivita na watu wasiojulikana, sembuse mimi na wewe?
Kama wajibu mkubwa wa Jeshi la Polisi ni kulinda Raia na Mali zao na Jeshi letu la Polisi limeshindwa kulinda uhai wa uhai wa Tundu Lissu na kuuweka mashakani, sembuse uhai wangu Mimi mlala hoi?
Tunatarajia Rais wetu alivyo mwepesi wa kuwatumbua viongozi wake pale wanapokosa kutimiza wajibu wao, tunatarajia kwa hili pia atafanya hivyo "faster" kwa kumuondoa kwenye nafasi yake IGP na Waziri wa Mambo ya ndani kwa kuwa wameshindwa kutuhakikishia usalama wetu na mali zetu!