Siku Muungano Ukivunjika

Sirikali

Member
Dec 16, 2010
89
36
Tutahakikisha A.H.Mwinyi & family yake wanaongoza msafara wa wazeNj wote kurudi kwao mchambawima.

J.K vunja muungano , hauna faida kwa Watanganyika.
 
hahhah hivo hujui kama AH Mwinyi kwao ni mrima?.
Uhakikishe kuwa wale waliopo huku wamrima ni wengi sana na wamestaarabika kwa hivo hata kurudi bara hawataki na sisi tutawaweka huku kwa sabau ni waqzaznibri wa hakika. Hapa kuna wakuria, wahaya na sasa pia wamasai wanajinasibu kuwa wazanzibari kwa hivo musiwe na wasiwasi hizo chuki zenu ndio asili ya wazanzibari kudai nchi yao hahahhahaah. "UCHOMAKO NDIKO UTOKAKO".
 
Muungano hauna dawa. Tupende tusipende utavunjika tu. There is no way this UNION will survive.
 
Muungano hauna dawa. Tupende tusipende utavunjika tu. There is no way this UNION will survive.

Falconer,

..muungano hautavunjika.

..wale wasioutaka muungano hawapo ktk nafasi za maamuzi ya kuweza kuuvunja.

..viongozi wengi wa CCM na CUF toka ZNZ wametajirika kupitia mgongo wa Tanganyika kwa hiyo hawawezi kuvunja muungano na ku-risk kupoteza mali zao.
 
hizo chuki zenu ndio asili ya wazanzibari kudai nchi yao
jitengeni mapema nani kawazueni ninyi kujitenga? huku Bungeni Dodoma mnakuja kufanya nini? Tanganyika mnatafuta nini? kaeni hukohuko mchambawima ili mjitenge vizuri. haka kababu kenu na familia yake kachukue mapema, hatukataki hapa Tanganyika.
 
Siku Muungano ukivunjika mi ntakuwa wa Kwanza kumfukuza Rajao na Rtz warudi kwao PEMBA!
 
Siamin kama hapo ndo mwisho wenu waa kufikir kuvunjika kwa muungano haaina maana kila mtu arud kwao mbona tuna watu wa east africa tunaishi nao au na wao tumeungana
 
LAZIMA UTAVUNJIKA TU! VIASHIRIA NI VINGI MNO!
1. Malalamiko ya wazenji ni mengi mno - mara ooh tunaonewa!, mafuta yakigunduliwa yetu (kelele nyiingiii kabla ya ugunduzi, yakigunduliwa itakuwaje?
2. Wameshakamilisha hatua zote za kujitenga - wana Rais, wana katiba yao, wana wimbo wao wa Taifa, wana serikali yao, wana bendera yao, wana timu yao ya taifa, wana mashirika yao, wana majeshi yao, Zanzibar ni nchi kwa mujibu wa katiba yao, n.k. Je, kimebaki nini? Tanganyika ina nini cha kipekee? Vyote vya Muungano. Yaani Zanzibar ina CHANGU na CHETU, lakini Tanganyika imemezwa na kusikika kwa mbali kwenye CHETU!.
 
Mimi naona MUUNGANO ni mzigo kwa watanganyika, tena usio na sababu!. Najua wapo watakaokereka lakini POTELEA MBALI!. Acha niseme ukweli. Idadi ya watu Zanzibar iko around 1.2 milioni ina wabunge zaidi ya 80 katika bunge la jamhuri ya muungano, Dar es Salaam yenye watu wapatao millioni 5 kwa sasa wanawakilishwa na wabunge 8! Hii ni akili au matope?. LAZIMA MUUNGANO UFE hauna Tija. Ukubwa wa Zanzibar ni sawa na wilaya ya SENGEREMA, je sengerema ina wabunge wangapi? Jiulize, Iwapo kila mbunge jumla ya malipo yake kwa mwezi in milioni 12, je tunapoteza sh. ngapi ambazo zingesaidia kusomesha watanganyika na
 
Natamani MUUNGANO uvunjike kwani upo kwa maslahi ya wanasiasa tu! WANAFIKI wengi wanasema wanaupenda saana muungano lakini ukweli ni kwamba ukivunjika tutakuwa nao mtaani kushangilia.
(i) muungano unadumu kwa nguvu ya dola;
(ii) katiba mbovu - isiyoruhusu demokrasia ya kweli. NDIYO maana CCM inatumia nguvu za dola kushinda pande zote. UTAKUWAJE IMARA imara wakati si matakwa ya wananchi wote? Tena cha ajabu mfumo wa muungano ni sera ya vyama, CCM serikali 2 na vyama vingine 3 na wananchi wengine wanataka moja. KERO!
Hebu jiulize muungano huu una faida gani? Leteni hoja. Ni muda muafaka wa kuujadili muungano bila woga wala kificho anayeutaka Aseme na kuutetea kwa hoja, siyo kudanganyana kwa hadithi za kizee!. Anayeupinga kama mimi naye aseme na kutoa hoja.
(iii) Ni miaka mingi sasa watanganyika wengi tumenyamaza kimya wakati kila leo wanaoufaidi muungano (WAZANZIBARI) wakitanua na kuubeza. Tena BILA kificho wanajiondoa kwa spidi kubwa na ya AJABU!. Kwa kifupi MUUNGANO walishaudhoofisha na sasa kilichobaki ni kuuvunja.
 
Muungano utavunjika hivi mtakuwa mashahidi wangu siku utavyovujika, cuf ni chama cha wana harakati kimeona udhaifu wote wa muungano na kuweza kuufanyia kazi katika katiba yao mpya. meanwhile chadema pia kwa upande wa bara kimeyaona madhaifu yote kuhusu muungano na katiba yao mpya na kuieleza ccm bara lakini hawasikii kwa sababu moja licha ya ukweli kuuona kuwa kwa katibayao mpya wazanzibari tayari wameshavunja muungano lakini CCM bara inafumba macho kwa sababu ya kura za urais za kutoka zanzibar tu wakati wa kuteuana wenyewe kwa wenyewe nani agombee urais.

nini kitatokea,
CCM BARA itafika mahala watu wabara wataanza kuishitumu waziwazi CCM kwa kukubali kutumiwa na wanzazibari na hapo ndipo CCM BARA itapolazimika ku fight back na kuungana na CDM kuukubali ukweli kama ambavyo CCM-VISIWANI ilivyofanya na hapo ndipo muungao utakapovunjika kwa maana hakuna pande itayokubali kuridhia mabadiliko na ndipo muungano utakapovunjika.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom