Binafsi najua FC Barcelona,Real Madrid na Atletico Bilbao ndizo hazijashuka daraja,sidhani kuna nchi nyingine ulaya zaidi ya Spain,ambazo timu hazijawahi kushuka daraja ukiachilia mabara mengine sina habari nazo(unofficially).
Tuwaulize kina Ndolanga,sidhani kama Yanga ilishashuka,tumuulize Gang Chomba,ila nakumbuka Simba ilinusurika miaka 3 mfululizo 1987,1988 na 1989 kina John Makelele ZigZag alimuambia Sahau Kambi hatosahau marehemu kwa sasa(RIP Sahau Kambi)Kwahiyo hata bara la Africa hulijui kuwa lina timu ambazo hazijawahi kushuka au kushuswa DARAJA? Simba au Yanga? ila mimi Nahisi Yanga kama ilishawahi shuka daraja kama sikumbuk kisawa sawa lol
Mavi ya kale hayanuki mtakufa na kijiba cha roho na timu zenu za kufanyia daeit
Mkuu inaonekana wewe uko kwenye muono wa "the best day in the history of football"(Gooners'/Scoucers' point of view?). Kumbuka kwamba 1964 Man utd ilimaliza ya pili kwenye ligi na ilishinda ligi mwaka 1965 na 1967. Mwaka 1968 ilichukua European cup ikiwafunga Benfica 4-1 kumbuka Eusebio alikuwa anachezea Benfica muda huo. Kwa mafanikio haya inabidi uangalie tena maana yako ya kusuasua kwenye ligi kulikosababishwa na Munich accident na relegation ya 1974.
Sababu za Man utd kuwa relegated ni pamoja na kuwepo kwa wachezaji wenye umri mkubwa baada ya Matt Busby kuacha kazi na McGuiness kuchukua nafasi yake, na baadaye Busby kurudi na baada ya hapo akaja meneja mwingine O'Farell ambaye alishindwa kumudu tabia ya baadhi ya wachezaji kama Best. Kisha Charlton, Faulkes na Best walistaafu. Pia muda huu(1970-74) kulikuwa na kikundi wachezaji wakongwe(old guard clique) ambao walikuwa hawaongei na wachezaji wapya wala kuwapa ushirikiano wa kutosha na hili lilikuwa tatizo kubwa.
Alipokuja meneja mwingine Docherty december 1972 akaanza kujenga timu mpya ikiwa na vijana wengi mpaka kufikia muda timu inashushwa daraja mchezaji wa kikosi kilichochukua kombe la ulaya alikuwa ni kipa peke yake Alex Stepney
Pia kuuzwa kwa Law ni sababu nyingine iliyozidi kuivuruga timu
Hata hivyo licha ya timu kushushwa daraja mashabiki waliendelea kuwa kuishangilia timu yao na ilikuwa nafasi kwa timu kujijenga upya.
Asante sana EMT umewafunza wengi wenye roho mbaya kwa Man UTD kwamba kuteleza si kuanguka na kila kitu kina mwanzo na mwisho.Hiyo ndio raha ya mpira huwezi kuzungumzia historia ya EPL bila MAN UTD na mahasimu Looserfool.Mashabiki matonge wamepata cha kuongea kijiweni...............Shukhurani EMT. :cheer2:
Heshima kwako chifu.
Hiyo ndiyo dawa za wale kama akina EMT wanaosimulia historia nusunusu kukidhi matakwa na mitazamo yao.
Yaani amesahau kwamba baada ya baada ya ajali ya Munchen, miaka 10 baadaye Man United ikaja kuwa timu ya KWANZA UINGEREZA kubeba kombe la klabu bingwa Ulaya.
Mwanahistoria anaruka matukio hapo katika na kushukia 1974?!? Jibu ni kuwa, ili kukidhi mtazamo wake.
Historia ikiandikwa kwa mlengo wa kukidhi matakwa, mapenzi, matazamio na mitazamo ya mwandishi, hakika historia hiyo lazima iwe potofu.
Thread haihusu siku Manchester United ilipokuwa timu ya kwanza Uingereza kubeba kombe la Klabu Bingwa Ulaya.
Thread inahusu siku Manchester United iliposhushwa daraja.
Kwa vile umeongelea suala la historia ya Man United, ulipaswa kuelezea kwa kina kilichotokea.
Huwezi kuelezea Muungano wa Tanganyika na Zanzibar wa mwaka 1964, bila kuzungumzia uhuru wa Tanganyika wa mwaka 1961.
Kubali tu unatoa historia ya Man United kwa hisia na matamanio yako.
Itakumbukwa pia kuwa Manchester United ilikuwa ikisuasua kwenye ligi baada ya timu kupata ajali ya ndege Munich Ujerumani mwaka 1958 ambapo abiria 20 kati ya 44 walipoteza maisha.......Kwa hiyo, baada ya ajali hiyo, Manchester United ilikuwa wanapambana mara nyingi kuepuka kushuka daraja.
Hata hivyo licha ya timu kushushwa daraja mashabiki waliendelea kuwa kuishangilia timu yao na ilikuwa nafasi kwa timu kujijenga upya.
I hope wataendelea kufanya hivyo baada ya Fergie kutangaza rasmi kustaafu mwishoni mwa msimu huu.
I hope watakuwa wavumilivu na huyo kocha mpya mtarajiwa hasa pale timu inaposhindwa kufanya vizuri kama Arsenal.
I hope baada ya Fergie kuondoka Man Utd haitakuwa kama Liverpool.
I really hope all of the above.
I really do.
Hahahahahahaaaa!