Siku Manchester United iliposhushwa daraja

Siku Manchester United iliposhushwa daraja

huo mwaka 1974 hakuna memba wa JF aliyekuwa ana akili yeyote ya kujua mpira tena kuwa na ushabiki na timu za ulaya wapi na kwa vipi katika mazingira gani zaidi kusikiliza redio tanzania wakitangaza mpira ule wa alalalala lalalalal goooooo halafu mtangazaji ana sema ni golkiki
 
Mhhh kuna mambo sitaki hata kuyakumbuka,na hili moja wapo.
 
Sawa mkuu,
Kwa Hitoria inayoendelea sasa aseno haijachukua ubigwa wowote kwa zaidi ya miaka10, chesi timu ya kwanza bigwa mtetezi kutolewa kwenye makundi champions legue, liverpool haija chukua EPL tangu ianzishwe 1992, Man u ni timu iliyochukua ubigwa wa ligi kuu mara nyingi kuliko timu yoyote,
 
We dogo acha ututo wako........

Kucheza na Chelsea na Historia hii tamu kuna uhusiano gani?....Wewe kila siku unataka kusikia mazuri tu ya Man Utd.........Jamvini humu kuna mabandiko mengi tu, kama unaona hili halikufai si usee tu uende kwenye bandiko la 'Man Utd Hamshikiki'..........

Ukweli utabaki pale kwamba Man Utd walishawahi kushuka daraja....Period.

sawa man utd wameshuka daraja na arsenal hawajawahi kushuka daraja...si ndio...sasa niambie man utd na arsenal which is the most successful club!! piga mstari mwenyewe
 
Hivi wewe bila kuomgelea Arsenal huwa hujisikii vizuri eti eeh!!

arsenal wao si hawajashuka daraja? so nataka nijue kwa wao kukaa kwenye ligi kuu toka kuanzishwa kwao wameshashinda makombe mangapi...
 
arsenal wao si hawajashuka daraja? so nataka nijue kwa wao kukaa kwenye ligi kuu toka kuanzishwa kwao wameshashinda makombe mangapi...

Team ambayo imekaa kwenye top flight kwa muda mrefu bila kushushwa ni Everton ikifuatiwa na Aston Villa the rest including Arsenal zishalambishwa mchanga sana tu!
 
sawa man utd wameshuka daraja na arsenal hawajawahi kushuka daraja...si ndio...sasa niambie man utd na arsenal which is the most successful club!! piga mstari mwenyewe

arsenal wao si hawajashuka daraja? so nataka nijue kwa wao kukaa kwenye ligi kuu toka kuanzishwa kwao wameshashinda makombe mangapi...




Arsenal walishuka daraja 1913. Wakapandishwa kihunihuni (hongo ilitembea) mwaka 1919 baada ya kumaliza nafasi ya tano kwenye ligi daraja la pili. Ukisikia mafundi wa rushwa kwenye soka la England basi Arsenal ni namba moja, wanaijua vizuri sana hiyo art, from stone age.
 
Kwa timu kubwa kama Man U kushuka daraja ni aibu sana, ni sawa na mwanamme anayejisifu ana mademu kibao huku na yeye aliishawahi kuliwa 0713..!
 
Nimeamini ukweli unauma, yaani Mashabiki wa MAN U wanatamani kudelete mada ila "Tusiache mbachao kwa msala upitao"....Historia inajenga leo nzuri
 
nafikiri wengi ya wapenzi wa Man united wa hapa JF hawaijui historia hiyo wakati huo timu yangu ilikuwa Everton

Nasikia timu pekee ambayo haijawahi kushuka daraja ni Everton.

Nyingine zoto zikiwepo Liverpool, Man City, Arsenal na Chelsea nilishashushwa.
 
Arsenal walishuka daraja 1913. Wakapandishwa kihunihuni (hongo ilitembea) mwaka 1919 baada ya kumaliza nafasi ya tano kwenye ligi daraja la pili. Ukisikia mafundi wa rushwa kwenye soka la England basi Arsenal ni namba moja, wanaijua vizuri sana hiyo art, from stone age.

:biggrin1::biggrin1:
 
Nimeamini ukweli unauma, yaani Mashabiki wa MAN U wanatamani kudelete mada ila "Tusiache mbachao kwa msala upitao"....Historia inajenga leo nzuri

unavosema ukweli unauma uumaje sasa...kwani man u ndio team kubwa pekee iliyowahi kushuka daraja? mimi hata msimu huu man utd ikishuka daraja bado nitaendelea kua a lifelong fan...ONCE A DEVIL ALWAYS A DEVIL :biggrin1:
 
unavosema ukweli unauma uumaje sasa...kwani man u ndio team kubwa pekee iliyowahi kushuka daraja? mimi hata msimu huu man utd ikishuka daraja bado nitaendelea kua a lifelong fan...ONCE A DEVIL ALWAYS A DEVIL :biggrin1:

Looh! I wish ningeweza kupata hizo nguvu, mie kila mwaka nadrop na kusajili timu mpya za kushabikia kwa nyakati 2 hadi X-mass ikiboronga nachagua nyingine hadi may na maisha full starehe, sitaki mipresure
 
Simply History it does not affect anything in taking the title this season, as well as beating Tottenham today

I see. Totenham ilifungwa bao ngapi? Usije uka :behindsofa: lakini.
 
Mkuu inaonekana wewe uko kwenye muono wa "the best day in the history of football"(Gooners'/Scoucers' point of view?). Kumbuka kwamba 1964 Man utd ilimaliza ya pili kwenye ligi na ilishinda ligi mwaka 1965 na 1967. Mwaka 1968 ilichukua European cup ikiwafunga Benfica 4-1 kumbuka Eusebio alikuwa anachezea Benfica muda huo. Kwa mafanikio haya inabidi uangalie tena maana yako ya kusuasua kwenye ligi kulikosababishwa na Munich accident na relegation ya 1974.

Sababu za Man utd kuwa relegated ni pamoja na kuwepo kwa wachezaji wenye umri mkubwa baada ya Matt Busby kuacha kazi na McGuiness kuchukua nafasi yake, na baadaye Busby kurudi na baada ya hapo akaja meneja mwingine O'Farell ambaye alishindwa kumudu tabia ya baadhi ya wachezaji kama Best. Kisha Charlton, Faulkes na Best walistaafu. Pia muda huu(1970-74) kulikuwa na kikundi wachezaji wakongwe(old guard clique) ambao walikuwa hawaongei na wachezaji wapya wala kuwapa ushirikiano wa kutosha na hili lilikuwa tatizo kubwa.

Alipokuja meneja mwingine Docherty december 1972 akaanza kujenga timu mpya ikiwa na vijana wengi mpaka kufikia muda timu inashushwa daraja mchezaji wa kikosi kilichochukua kombe la ulaya alikuwa ni kipa peke yake Alex Stepney

Pia kuuzwa kwa Law ni sababu nyingine iliyozidi kuivuruga timu

Hata hivyo licha ya timu kushushwa daraja mashabiki waliendelea kuwa kuishangilia timu yao na ilikuwa nafasi kwa timu kujijenga upya.

Kama vile umesoma nusu nusu. Nimesema wazi kuwa "Itakumbukwa pia kuwa Manchester United ilikuwa ikisuasua kwenye ligi baada ya timu kupata ajali ya ndege Munich Ujerumani mwaka 1958 ambapo abiria 20 kati ya 44 walipoteza maisha."

Sasa sijui unachopinga hapo ni nini? Au unataka some hairdryer?

 
Last edited by a moderator:
Kama vile umesoma nusu nusu. Nimesema wazi kuwa "Itakumbukwa pia kuwa Manchester United ilikuwa ikisuasua kwenye ligi baada ya timu kupata ajali ya ndege Munich Ujerumani mwaka 1958 ambapo abiria 20 kati ya 44 walipoteza maisha."

Sasa sijui unachopinga hapo ni nini? Au unataka some hairdryer?


Sijasoma nusunusu, wewe umeandika hivi

Kwa hiyo, baada ya ajali hiyo, Manchester United ilikuwa wanapambana mara nyingi kuepuka kushuka daraja.



ManUtd ilishuka daraja 1974 ajali ya Munich ilitokea 1958, kwa hiyo timu ilishuka daraja miaka 16 baada ya ajali. ManUtd iliweza kuwa na timu nzuri kiasi cha kuwa runner up 1964 na kuchukua ligi 1965 na 1967 na kombe la ulaya 1968, hii na maana kuwa timu ilikuwa imefanya 'recovery' kutokana na maafa ya ajali. Sababu za kushuka daraja nimeshaziandika.
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Binafsi najua FC Barcelona,Real Madrid na Atletico Bilbao ndizo hazijashuka daraja,sidhani kuna nchi nyingine ulaya zaidi ya Spain,ambazo timu hazijawahi kushuka daraja ukiachilia mabara mengine sina habari nazo(unofficially).
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Kuna watu wana wivu kama kobe.Hiyo historia inasadia nini ?.
 
Kuna watu wana wivu kama kobe.Hiyo historia inasadia nini ?.

Mkuu umenifurahisha kweli. Kwenye ile thread yangu ya historia ya Mtwara miaka 10 kabla ya uhuru umeipenda kweli kweli.

Lakini kwenye hii thread ya historia ya Manchester United umeiponda. Kuhusu hii historia inasaidia nini, hapo itabidi tena kurudi darasani kujua ni kwa nini tunajifunza historia. You ready for a supp?
 
Back
Top Bottom